Bank Loan Propasal
W
Description
Bank Loan Propasal document sample
Document Sample


TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA AHADI ZA
SERIKALI BUNGENI KWA KIPINDI CHA MWAKA
2006 - 2007
1
OFISI YA WAZIRI MKUU
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa Tathmini ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 imetolewa
kushirikiana na wadau wake na kusambazwa kwa wadau kupitia Taarifa ya Tume ya
itakamilisha tathmini ya Uchaguzi Taifa ya Uchaguzi kuhusu Uchaguzi wa Rais, Wabunge
Mkuu wa mwaka 2005 ili itumike na Madiwani, 2005 ya tarehe 9 Juni, 2006. Taarifa
kuboresha zaidi uendeshaji wa chaguzi imeainisha mafanikio na upungufu uliojitokeza kwenye
zijazo. hatua mbalimbali za mchakato wa uchaguzi. Hatua hizo
ni pamoja na:
(i) Uhakikishwaji wa wapiga kura kwenye Daftari la
Kudumu la Wapiga Kura,
(ii) Uteuzi wa wagombea na kampeni za uchaguzi,
(iii) Upigaji na uhesabuji wa kura,
(iv) Utangazaji wa matokeo,
(v) Elimu ya mpiga kura na ya wasimamizi wa
uchaguzi, na
(vi) Menejimenti na uendeshaji wa uchaguzi kwa ujumla
ikiwemo ushirikishwaji wa wadau pamoja na
upatikanaji wa fedha na vifaa kwa wakati
uliopangwa. Aidha, upungufu wote uliojitokeza
utatumika kuboresha zaidi sheria, kanuni na taratibu
za uendeshaji wa chaguzi zijazo.
2. Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Dhana na mfumo wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la
litaboreshwa kwa kuwaondoa wapiga Kura vimekubalika. Taratibu za uboreshaji wa
wasiostahili na kuingiza wenye sifa za Daftari la Kudumu la Wapiga Kura zitafanywa kikanda
kujiandikisha na ambao kwa sababu na uboreshaji huo utafanyika mara mbili katika kipindi
mbalimbali hawakujiandikisha katika cha miaka mitano kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka
kipindi kilichopita. 2010.
Awamu ya kwanza inatarajiwa kutekelezwa katika
mwaka wa fedha 2007/2008, na ile ya pili itatekelezwa
miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Uboreshaji huo unalenga:-
(i) Kuandikisha wapiga kura wapya watakaokuwa
wamefikia umri wa miaka 18 na waliokuwa
hawakujiandikisha katika kipindi kilichopita iwapo
2
watahitaji kujiandikisha.
(ii) Kurekebisha taarifa zilizokosewa awali au za
waliohama kutoka Kata/Jimbo moja la uchaguzi
kwenda Kata/ Jimbo jingine.
(iii) Kuondoa majina ya waliofariki au kupoteza sifa
za Wapiga kura kwa mujibu wa Sheria ya
Uchaguzi.
3. Kuhakikisha vikao vya SMT na SMZ Uchambuzi wa Taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya
kuhusu masuala ya Muungano Kikao cha pili kati ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi
vinafanyika kama ilivyoelekezwa na kilichofanyika tarehe 21 Novemba, 2006 Ikulu ya
Mhe. Rais. Zanzibar umekamilika. Maandalizi ya Kikao kingine
yanaendelea ili kukiwezesha kufanyika baada ya
Mkutano wa Bunge la Bajeti kwa mwaka 2007/2008.
4. Kuboresha menejimenti na mazingira Wakala wa Majengo (TBA) ambaye ni Msimamizi wa
ya ukumbi mpya wa Bunge na majengo yote ya Serikali amepewa jukumu na Ofisi ya
kuwapatia Wabunge Ofisi majimboni Bunge kusimamia ukumbi mpya wa Bunge. Huduma za
mwao kwa awamu kadri uwezo kutunza na kuhifadhi jengo hilo zinaratibiwa na Wakala
utakavyoruhusu. hiyo kuanzia Juni, 2007. Serikali imetenga shilingi
bilioni moja katika mwaka fedha 2007/08 kwa ajili ya
ujenzi wa ofisi 40 za awali za Wabunge katika majimbo
yao ya uchaguzi. Ujenzi utasimamiwa na
Halmashauri/Mamlaka za Serikali za Mitaa.
5. Kwa kushirikiana na wadau Tume Rasimu ya Sera ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya
itaandaa Sera ya Udhibiti wa Dawa za imejadiliwa na Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri.
Kulevya kama mbinu mojawapo ya Marekebisho yaliyopendekezwa yanaendelea kufanyiwa
kupambana na tatizo hilo. Aidha, kazi. Mchakato wa Marekebisho ya Sheria ya Kuzuia
Sheria ya Dawa za Kulevya Na.9 ya na Kupambana na Biashara Haramu ya Dawa za
mwaka 1995 itafanyiwa marekebisho. Kulevya Na.9 ya Mwaka 1995 yapo katika hatua za
mwisho kwenye ngazi za juu serikalini ili kuidhinishwa.
6. Elimu kwa umma itaendelea kutolewa Tume imeendelea kuyatumia matukio ya kitaifa katika
kuhusu matatizo yatokanayo na kuelimisha umma. Kwa mfano:-
matumizi pamoja na biashara ya dawa (i) Maonyesho ya Wakulima ya Nane Nane mkoani
za kulevya na uhusiano wa dawa hizo Arusha.
na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Kadhalika, mafunzo na vitendea kazi (ii) Wiki ya Usalama Barabarani mkoani Kigoma.
vitaendelea kutolewa kwa Vyombo vya
Dola kama Polisi, Uhamiaji na Forodha (iii) Wiki ya Vijana na Kilele cha Mbio za Mwenge
ili kuimarisha udhibiti na mapambano mkoani Ruvuma.
dhidi ya uhalifu unaotokana na dawa
za kulevya. (iv) Siku ya UKIMWI Duniani mkoani Mara.
(v) Maonyesho ya Saba Saba (Dar es Salaam).
3
Serikali ilitumia fursa ya Mbio za Mwenge wa Uhuru
kufikisha ujumbe maalum kwa jamii juu ya athari za
biashara na matumizi ya dawa za kulevya. Vilevile Tume
imewaelimisha wanafunzi 300 wa shule za msingi na 45
wa sekondari za Dar es salaam kuhusu athari
zitokanazo na matumizi ya dawa za kulevya.
Tume ilitumia pia fursa ya Maadhimisho ya Siku ya
Kimataifa ya Kupiga Vita Biashara Haramu na Matumizi
ya Dawa za Kulevya, Juni 26, 2007 yaliyofanyika kitaifa
jijini Tanga kuuelimisha umma. Mgeni rasmi katika
maadhimisho hayo alikuwa Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tume imeendelea kutoa machapisho mbalimbali
ikiwemo vipeperushi na fulana na kutumia vyombo vya
habari kama redio, magazeti, na televisheni
kuwaelimisha wananchi. Aidha, mwongozo kuhusu
udhibiti wa UKIMWI miongoni mwa watumiaji wa dawa
za kulevya nchini, umetayarishwa.
Tume ilishirikiana na vyombo vya dola katika
operesheni za kuwakamata wafanyabiashara wa dawa
za kulevya (watuhumiwa 121) na kati yao 86
wamewekwa chini ya uangalizi wa Mahakama.
Operesheni ya kitaifa ya uteketezaji wa zao la Bangi
kuanzia Januari, 2006 mpaka Juni 2007, ilifanyika vizuri
na ekari 1,603 za bangi ziliteketezwa. Tume ya Madawa
ya Kulevya imechangia gharama za kuteketeza bangi
katika mikoa ya Morogoro na Arusha.
Kiasi cha dawa za kulevya kilichokamatwa katika kipindi
husika ni:
Bangi- kilo 296,997; Mirungi- kilo 7391; Heroine- kilo 99;
Morphine- kilo 37; Mandrax- kilo 11 na Cocaine- kilo 5.9.
7. Utoaji wa huduma za matibabu na Tathmini ya uwezo imefanywa kwenye Hospitali za
ushauri nasaha kwa waathirika Lutindi na Mirembe ambazo hutoa huduma ya matibabu
vitaendelea kutolewa na kuratibiwa na kwa waathirika wa dawa za kulevya na kuonyesha kuwa
Tume ikishirikisha wadau wake. uwezo wa kutoa tiba wa vituo hivyo haukidhi mahitaji ya
idadi ya waathirika waliopo. Kwa kutambua hali hiyo,
Tume ya Madawa ya Kulevya ilisaidia kulipia gharama
za kiwanja kitakachojengwa kituo cha matibabu kwa
waathirika wa dawa za kulevya eneo la Mirembe,
Dodoma. Kituo hicho kinajengwa chini ya usimamizi wa
4
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
8. Serikali itakamilisha upimaji wa hekta Upimaji wa eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma
4,000 katika eneo la Chimwaga kwa umekamilika na ramani yake imeidhinishwa na
ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu kipya Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani. Uthamini wa mali za
cha Serikali. wananchi pia umekamilika. Thamani halisi ya mali ni
shilingi bilioni 3.5 na imeidhinishwa na Mthamini Mkuu
wa Serikali. Ramani na jedwali lenye viwango vya fidia
itakayolipwa kwa wananchi vimekabidhiwa Wizara ya
Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia.
9. Muswada wa Sheria wa Marekebisho Rasimu ya Mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya
ya msingi katika Sheria Na. 9 ya Menejimenti ya Maafa imekamilika na kupitiwa na
mwaka 1990 utaandaliwa na Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri. Maoni ya
kuwasilishwa Bungeni ili kukidhi Sekretarieti (BLM) yanafanyiwa kazi kwa hatua na
mahitaji ya Sera ya Taifa ya idhini ya Baraza la Mawaziri na hatimaye kuwasilishwa
Menejimenti ya Maafa ya Mwaka 2004. Bungeni. Marekebisho yatakidhi mahitaji ya Sera ya
Taifa ya Maafa ya mwaka 2004.
10. Elimu kwa umma, miongozo, nyenzo Mwongozo umetolewa kwa Halmashauri zote kuweka
na huduma kwa yatima zitatolewa zaidi bajeti na huduma kwa yatima katika mipango yao. Hadi
mijini na vijijini. Aidha, itahakikishwa Juni, 2007, jumla ya Shilingi bilioni 9 zilitolewa na
kuwa kila Halmashauri inakuwa na “Global Fund” kwa Halmashauri kwa ajili ya mpango wa
mipango ya kukabiliana na UKIMWI. kudhibiti UKIMWI ikiwa ni pamoja na huduma kwa
yatima. Mwongozo wa uundaji wa Kamati za Kudhibiti
UKIMWI umerekebishwa ili kuimarisha utaratibu,
usimamizi na uwajibikaji katika ngazi ya Mkoa na
Mamlaka ya Serikali za Mitaa.
11. Kila Halmashauri itatengewa ikama ya Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Fedha na
wahasibu 8 na Wakaguzi wa ndani 3 ili Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
kuziwezesha kufanya kazi kwa ufanisi. imekubali Ikama hiyo. Serikali imeajiri na kutuma
Watumishi Wahasibu 478 Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani kwenye
watapangiwa kwenye Halmashauri Halmashauri. Wahasibu 269 na Wakaguzi wa Ndani 89
mbalimbali ili kupunguza uhaba wa waliripoti katika Halmashauri zote.
watumishi waliopo.
12. OWM – TAMISEMI itashirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI imeainisha mahitaji ya
Wizara ya Afya ili kujaza nafasi wazi watumishi katika Hospitali ya Bombo na kuyawasilisha
Katika Hospitali ya Bombo. Wizara ya Afya kwa hatua zaidi.
13. OWM – TAMISEMI itaandaa mkutano Baada ya warsha ya Wakurugenzi wa Sera na Mipango
wa pamoja kati ya Makatibu Wakuu wa iliyofanyika tarehe 4 na 5 Desemba 2006, OWM
Wizara za kisekta ili kuelimishana TAMISEMI sasa inawasiliana na Wizara za Kisekta ili
kuhusu mahusiano na majukumu ya kupanga tarehe ya Mkutano wa pamoja wa Makatibu
kila Wizara. Wakuu wa Kisekta ili pamoja na kuelimishwa kuhusu
mahusiano na majukumu ya kila Wizara, pia waweze
kujadili na kuyatolea maamuzi mapendekezo
yaliyotolewa ya namna ya kuwatumia vilivyo Maafisa
Mipango katika Sekretariati za Mikoa na wale wa
Halmashauri.
5
14. Kufanya warsha za Wakurugenzi ili OWM - TAMISEMI iliandaa warsha ya Wakurugenzi wa
wajue majukumu ya kila Wizara na Sera na Mipango iliyofanyika tarehe 4-5 Desemba, 2006
baadaye wawaelimishe Watendaji katika Hoteli ya Kunduchi. Madhumuni makubwa ya
wengine katika Wizara zao. warsha hii yalikuwa ni kujadili njia nzuri ya kuhakikisha
kuwa Sera za Kisekta zinaendana na lengo la upelekaji
madaraka kwa wananchi; kujadili matatizo ya kiutendaji
kati ya OWM - TAMISEMI na Wizara za Kisekta kwa
upande mmoja na kati ya Wizara za Kisekta na Mikoa
na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa upande mwingine;
kujadili matatizo yanayoathiri utendaji kazi wa Maafisa
Mipango wa Sekretarieti za Mikoa na wale wa Wilaya,
kutoa mapendekezo ya ufumbuzi wake na
kufahamishwa juu ya maendeleo ya utayarishaji wa
Mkakati wa Uratibu wa Sekta kutoka kwa Wataalam
Washauri kutoka ESAMI. Warsha hii ilipendekeza kuwa:
Kiundwe chombo cha Wataalam wa kuishauri
Serikali juu ya matumizi muafaka ya Maafisa
Mipango/Wachumi hapa nchini.
Majukumu ya Maafisa Mipango yafanyiwe
mapitio kuona kama yanaendana na kazi zao
kikamilifu.
Kuwe na fursa (forum) ambapo OWM
TAMISEMI, Wizara za Kisekta na Serikali za
Mitaa watakaa na kuainisha shughuli
zitakazogatuliwa (devolved), zitakazokaimishwa
(delegated) na zile za kufanyika kwa pamoja
(shared) kwa kufahamu kuwa zoezi la dhana ya
kupeleka madaraka kwa wananchi (D by D) ni la
hatua kwa hatua (gradual process).
OWM - TAMISEMI itoe mapema mwongozo wa
utayarishaji/uandaaji wa mipango na bajeti.
Pawepo na Mkakati wa ugatuaji wa madaraka
kwa wananchi utakaotekelezwa kwa awamu na
kwa kipaumbele.
15. Serikali itatoa Sh. Bilioni 1 kwa kila Serikali imetenga sh. bilioni 21 katika bajeti ya mwaka
Mkoa kupitia benki zilizopo kwa ajili ya 2006/2007 kwa ajili ya kuwezesha wananchi
uwezeshaji wa Wananchi kiuchumi na kujikwamua kiuchumi. Fedha hizo zitatolewa kama
kuongeza ajira nchini. mikopo kupitia benki na Vyama Vya Kukopa na Kulipa.
6
Baraza la Taifa la Uwezeshaji wa Wananchi lililopo
chini ya Wizara ya Mipango Uchumi na Uwezeshaji
limeandaa miongozo na taratibu za ukopeshaji fedha
hizi. T.Shs.10.5 Billioni zimetolewa kupitia Benki ya
NMB na CRDB chini ya Masharti ya Ukopeshaji (Credit
Guarantee). Fedha hizo zitakopeshwa mtu mmoja
mmoja, vikundi na vyama vya kuweka na kukopa
(SACCOS). Aidha, Serikali imeshatoa mafunzo kwa
maofisa watatu wa kila Halmashauri kuhusu ujasiriamali
ili waweze kuwafundisha wananchi watakaokopa fedha
hizo katika Wilaya zao. Maafisa hao ni Afisa Mipango 1,
Afisa Ushirika 1 na Afisa Maendeleo ya Jamii 1.
Mafunzo hayo yamefanyika kikanda katika Kanda za
Mwanza, Mbeya, Arusha, Dar es Salaam na Dodoma na
yalisimamiwa na Benki Kuu ya Tanzania.
16. Serikali itatoa maelekezo kwa Wakuu Watendaji wanaolipwa mishahara ni wale walioingia
wa Mikoa kufuatilia kwa karibu suala la kwenye Kompyuta ambao ni Watendaji wa Vijiji 9,786
ulipaji wa mishahara ya VEO na MEO kati ya 10,344 ya Vijiji vilivyopo ambayo ni asilimia 95 na
kwa wakati. Watendaji wa Mitaa 1,597 kati ya Mitaa 1,755 iliyopo
ambayo ni asilimia 91. Watendaji wa Mitaa na Watendaji
wa Vijijji ambao hawajalipwa ni wale ambao taratibu zao
za ajira hazijakamilika kwa mujibu wa Mwongozo
uliotolewa.
17. Serikali itaelekeza Wakurugenzi wa Pamoja na kutokamilika kwa taarifa za baadhi ya
Halmashauri kutoa uzito Katika suala Watendaji wa Vijiji, kwa wale ambao wapo kwenye
la kulipa mishahara ya VEO na MEO orodha ya malipo mishahara yao italipwa tarehe 25 ya
ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi. kila mwezi kama ilivyo kwa watumishi wengine wa
Serikali. Serikali imezielekeza Halmashauri kuchukua
orodha ya mishahara kila tarehe 16 na mishahara iwe
imeshalipwa ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi kama
watumishi wengine wa Serikali. Aidha, Benki
zimeshaelekezwa kuhusu uamuzi huo na kuridhia
kuanzia Desemba, 2006.
18. Kwa kuwa Serikali inatoa fidia ya Kwa sasa Serikali Kuu haina utaratibu wa kulipa posho
mapato kwa Halmashauri, Serikali Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji. Katika tangazo la
itatoa maelekezo kwa Halmashauri ili Serikali namba tatu (3) la tarehe 7 Januari, 1994
ziwalipe posho Wenyeviti wa Vijijji na Halmashauri zote nchini zilielekezwa kuwalipa Wenyeviti
Vitongoji. wa Mitaa na Vijiji si chini ya asilimia tatu (3%) ya
makusanyo ya vyanzo vya mapato alivyohamasisha
hasa kodi ya maendeleo. Baada ya Serikali kufuta kodi
zenye kero bado Halmashauri zimebaki na vyanzo vya
mapato ambavyo Halmashauri zinawajibika kukusanya.
Hivyo Halmashauri zina uwezo wa kulipa asilimia (3%)
ya posho ya Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa.
Aidha, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI mwaka 2003
7
ilipeleka Mwongozo wa jinsi Halmashauri zinavyoweza
kutumia ruzuku ya fidia ya mapato ili kugharimia
matumizi mbalimbali katika Halmashauri. Mwongozo
huo utapitiwa upya ili kuuboresha.
19. Ofisi itafuatilia kuona ni sababu zipi Barua Kumb. Na. HB.114/200/02/18 ya tarehe
zinazofanya Halmashauri ya Wilaya ya 20/10/2006 ilitumwa Halmashauri na kupata majibu
Same ishindwe kukusanya mapato kama ifuatavyo: Katika mwaka wa fedha 2004/05
ipasavyo. mapato ya vyanzo vya Halmashauri ya Same yalishuka
kutokana na mgogoro wa wafanyabiashara wa madini
ya jasi kudai kuwa ushuru wa madini umefutwa kama
walivyoelekezwa na viongozi wao. Hivyo, ushuru
haukulipwa. Wafanyabiashara walielimishwa na
Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.
Hivi sasa ushuru unalipwa na wanunuzi wa madini ya
jasi na makusanyo kwa mwaka yameongezeka kwa
zaidi ya asilimia 50 kuanzia mwaka 2005/2006 kama
ifuatavyo:-
MWAKA MAKISIO MAKUSANYO
HALISI
2003 247,700,000/= 110,800,000/=
2004 Jan-Juni 34,700/= 31,000,000/=
2004/05 120,000,000/= 59,000,000/=
2005/06 133,600,000/= 131,800,000/=
2006/07 158,800,000/= 69,000,000/=
Makusanyo ya mwaka 2006/2007 ni hadi mwezi
Novemba, 2006.
20. Serikali itaanza zoezi la kufanya OWM-TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi,
mapitio ya maelezo ya mipaka ya Nyumba na Maendeleo ya Makazi, imepeleka maelezo
Wilaya za nchi nzima ili kufanya ya Mipaka (GN) kwenye Mikoa yote nchini ambayo
marekebisho yanayohitajika. nakala pia zimepelekwa Wilayani. Maoni juu ya utata wa
maelezo yanaratibiwa na kuchambuliwa ili zoezi la
kuhakiki mipaka yenye matatizo lifanyike.
21. Serikali itaanzisha Mabaraza ya Ardhi Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji yalikwishaanzishwa na
ya Vijijji na yatashughulikia migogoro kuanza kushughulikia migogoro ya ardhi. Halmashauri
ya Ardhi. zimeelekezwa kuyaimarisha na kuyawezesha ili yaweze
kushughulikia migogoro kikamilifu.
22. Serikali kwa kushirikana na Shule ya Msingi Mitindo iliyopo katika Halmashauri ya
Halmashauri ya Misungwi Wilaya ya Misungwi ina wanafunzi 822. Kati ya hao
itaishughulikia shule ya Msingi Mtindo wanafunzi wasioona ni 52 wanaotoka katika maeneo
katika Wilaya ya Misungwi yenye mbalimbali ya nchi. Kutokana na hali ya wanafunzi hao,
wanafunzi wasioona ili wapate huduma Serikali huwapatia fedha kupitia Halmashauri ya Wilaya
muhimu. ya Misungwi kwa ajili ya kupata chakula, usafiri wakati
wa kwenda na kurudi likizoni na fedha za uendeshaji wa
8
shule (Capitation grant). Halmashauri huwapatia fedha
kwa ajili ya kununulia vifaa vya usafi kama sabuni na
mafuta ya taa. Katika kipindi cha Julai hadi Desemba
2006, shule ilipelekewa shilingi 3,240,000/= kwa ajili ya
chakula, 1,000,000/= usafiri na 1,500,000/= kwa ajili ya
kununua vifaa vya usafi. Jumla ya shilingi 2,430,654/=
zilipelekwa shuleni hadi Septemba kama “capitation
grant”. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeipatia
shule walimu wanne (4), Mashine za kuchapa tatu,
shilingi 11,000,000/= kurekebisha miundombinu na
karatasi za kuchapishia (Braille) ream 53 kwa wanafunzi
hao.
23. OWM – TAMISEMI itawasilisha suala Barabara ya Usagara - Fela - Kisesa; kwa mwaka wa
la matengenezo ya barabara ya fedha 2006/07 hakuna fedha zilizotengwa kwa ajili ya
Usagara – Fela – Kisesa na barabara barabara hii.
ya Sikonge – Ipole – Rungwa katika Barabara ya Sikonge – Ipole – Rungwa; Barabara hii
Wizara ya Miundombinu ili imefanyiwa matengenezo na TANROADS kama
mawasiliano ya barabara yawepo. ifuatavyo:- “Bairley bridge” moja (1), “Culvert” nne (4),
matengenezo ya culvert moja la zamani na kuziba
mashimo katika eneo la Fela. Hivyo barabara hii
inapitika.
24. Serikali itaanza zoezi la kufanya Wilaya ya Kilindi imewasilisha maelezo ya mgogoro wa
mapitio ya maelezo ya mipaka ya mpaka na yanafanyiwa kazi. Tatizo ni kati ya Mkoa wa
Wilaya ya nchi nzima ili kufanya Tanga na Mkoa wa Manyara (Kilindi na Kiteto) ambapo
marekebisho yanayohitajika hususani maelezo katika GN. yanatofautiana na hali halisi ya
Wilaya ya Kilindi. mipaka ilivyo ardhini.
25. Serikali itaimarisha Mabaraza ya kata Mwezi Agosti, 2006 OWM – TAMISEMI iliendesha
ili yaweze kutekeleza majukumu yake mafunzo kwa wanasheria wa Serikali za Mitaa kuhusu
ipasavyo. uendeshaji wa mabaraza ya kata ili nao wakaendeshe
mafunzo hayo katika maeneo yao. Aidha Ofisi inaandaa
mwongozo (Guideline) wa uendeshaji wa mabaraza
hayo. Mwongozo utakamilishwa baada ya marekebisho
ya Sheria za Serikali za Mitaa kuwekewa saini na
Mheshimiwa Rais na utasambazwa katika Halmashauri
zote.
26. OWM – TAMISEMI kwa kushirikana na Serikali inatambua umiliki wa maeneo kimila.
Wizara ya Ardhi na Makazi na Halmashauri inayohusika inatoa Hati Miliki za Kimila
MKURABITA zitaangalia namna ya ambazo zinaweza kutumika kupata mikopo na
kuharakisha zoezi la umilikishaji ardhi dhamana. Aidha, MKURABITA kwa kushirikiana na
kwa Wakulima na Wafugaji ili waweze Mamlaka za Serikali za Mitaa katika Wilaya ya Mbozi
kupata mikopo. imepima Ardhi kwa Wakulima na Wafugaji. Jumla ya
Vijiji 164 vimepimwa mipaka yake mwaka 2002 mpaka
2003 kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi. Mwaka 2004 Halmashauri
imetoa Hati miliki za kimila kwa wananchi 1,451. Hati
9
miliki zinaendelea kuandaliwa kwa wananchi wengine.
27. OWM – TAMISEMI kwa kushirikiana Katika mwaka wa fedha 2006/07 Halmashauri ya
na Halmashauri ya Manispaa ya Manispaa ya Temeke imetenga jumla ya
Temeke itaangalia jinsi ya kutatua T.Shs.16,000,000/= kwa ajili ya kuchimba visima viwili
tatizo la huduma ya maji safi na virefu. Kimoja kitachimbwa Mtaa wa Mponda Kata ya
salama katika kata ya Charambe. Charambe na kingine katika Sekondari ya Charambe.
Halmashauri ya Temeke imeingia mkataba na wakala
wa uchimbaji wa visima mwezi Aprili 2007 kwa ajili ya
kuchimba visima katika eneo hilo.
28. Serikali itaangalia uwezekano wa Serikali imetoa kiasi cha Tshs. 178,010,000 kwa ajili ya
kutenga fedha za ujenzi wa Makao Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Longido, na Tshs
Makuu ya Wilaya ya Longido kwa 90,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Nyumba ya Mkuu wa
kushirikiana na Wilaya ya Monduli. Wilaya ya Longido. Zabuni ya kumpata Mkandarasi kwa
ajili ya Ujenzi imetangazwa na tarehe 27/12/06 Bodi ya
Tenda ya Mkoa ilimchagua Mkandarasi. Kazi ya
kuandaa Mchoro wa Mipango Miji na kupima eneo la
Makao Makuu ya Wilaya imekamilika. Ujenzi ulianza
rasmi Januari, 2007.
29. Halmashauri ambazo mto Bubu Mto Bubu umeanzia katika Wilaya za Mbulu na Babati
(Kondoa) umepita zitaelekezwa ambako ndio chanzo kikuu cha maji. Mto huu unapitia
kufanya utafiti wa awali kuhusu katika Halmashauri ya Kondoa na kuishia Wilaya ya
uanzishaji wa kilimo cha umwagiliaji. Bahi. Mto Bubu ni mto wa msimu, hivyo kilimo cha
umwagiliaji hufanyika katika kipindi cha mvua
(supplementary irrigation) na hii ni katika maeneo ya
Wilaya ya Bahi. Kulingana na mwinuko (topography)
kilimo katika Wilaya za Mbulu, Babati na Kondoa
hufanyika katika maeneo oevu (wetland) yanayopata
maji kutoka Mto Bubu. Hivyo umwagiliaji katika mto
Bubu hufanyika zaidi katika Wilaya ya Bahi. Katika
miaka ya 1990, IFAD kupitia mradi wa ”Smallholder
Development Programme in Marginal Areas ((SDPMA)”
walijenga Miundombinu ya umwagiliaji, lakini bado
uzalishaji ni mdogo usio na tija. Wizara ya Kilimo,
Chakula na Ushirika kwa kushirikiana na OWM –
TAMISEMI ilifanya semina elekezi tarehe 3 – 4 Januari,
2007, mjini Babati iliyowahusisha Wakurugenzi
Watendaji wa Halmashauri, Maafisa Kilimo wa Wilaya
na Maafisa Kilimo umwagiliaji. Mada kuu zilizojadiliwa
ni kama ifuatavyo:-
Kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika
programu ya ASDP.
Kuibua miradi ya umwagiliaji kwa kutumia
“National Irrigation Master Plan”.
Kuainisha upatikanaji wa fedha kutoka katika
Mfuko wa Kitaifa na Kiwilaya wa Uendelezaji
10
wa Umwagiliaji.
Baada ya semina hii Halmashauri zimeweza kuibua
miradi na kuwasilisha OWM – TAMISEMI na kisha
kuombewa fedha za kuendeleza kilimo cha umwagiliaji.
Katika ngazi ya Kitaifa, Wizara ya Kilimo Chakula na
Ushirika ilipanga kutoa semina elekezi katika vituo vya
kanda zote za umwagiliaji ambazo zitawajumuisha
wajumbe watatu kutoka katika kila Wilaya. Wajumbe
waliohusishwa ni Wakurugenzi Watendaji wa
Halmashauri, Maafisa Kilimo wa Wilaya husika na
Maafisa Kilimo Umwagiliaji. Semina hizo zilifanyika
kuanzia tarehe 18/12/2006.
30. Katika Bunge la Bajeti 2006/07 Serikali Muswada wa marekebisho ya Sheria ya kuwaingiza
itawasilisha Muswada wa marekebisho Wabunge wa Viti Maalum kama Wajumbe wa Mabaraza
ya Sheria ya Serikali za Mitaa ya ya Halmashauri za Miji umepitishwa kwenye Bunge la
mwaka 1982 ili kuwaingiza Wabunge Novemba, 2006. Wabunge Viti Maalum ni Wajumbe wa
wa Viti Maalumu kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Halmashauri za Miji.
Mabaraza ya Halmashauri za Miji.
31. OWM –TAMISEMI itawasiliana na Biashara ya Mabenki kwa sasa ni biashara huria na
Wizara ya Fedha ili kuona uwezekano hasa baada ya kubinafsisha NMB. Wilaya ya Simanjiro
wa kuwapatia wananchi wa Simanjiro haina huduma ya benki kwenye Makao Makuu yake -
huduma ya Benki. Orkesmet. Mpaka sasa inapata huduma hizo kutoka
benki ya NMB Clock Tower Mkoani Arusha. Benki ya
CRDB inaanzisha kituo kwa ajili ya SACCOS kwa lengo
la kuhudumia mikopo ya sh. bilioni moja kwa wananchi.
Aidha SACCOS hiyo itaanzishwa mara baada ya
kukamilika kwa Kituo cha Polisi ambacho ujenzi wake
upo katika hatua za mwisho.
Hata hivyo, OWM-TAMISEMI imewasiliana na Wizara
ya Fedha kwa barua Kumb.Na. CA.29/307/03 ya tarehe
18/12/06 ili iweze kutoa mwongozo na masharti ya
uanzishwaji wa huduma za kibenki. Mwongozo huo
utasaidia hata wawekezaji katika sekta ya fedha kuona
uwezekano wa kufungua Benki Simanjiro katika mji wa
Orkesmet. Aidha wananchi wa mji wa Orkesmet
wanashauriwa kutumia huduma za benki katika Wilaya
ya Kibaya badala ya kwenda mjini Arusha ambako ni
mbali.
32. OWM – TAMISEMI itashirikiana na Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko kwa
Wizara ya Viwanda, Biashara na kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani (ILO) iliandaa
Masoko na Bodi ya Biashara ya Nje ili mafunzo ya kuwajengea uwezo wajasiriamali wenye
kuona uwezekano wa Wanawake ulemavu na wanawake mwishoni mwa mwezi Novemba,
kushiriki Katika maonyesho ya 2006 jijini Dar es Salaam na Morogoro. Lengo la
11
Kimataifa ili kupanua wigo wa masoko mafunzo hayo ilikuwa kuwaandaa watu wenye ulemavu
ya bidhaa zao. na wanawake kuzalisha bidhaa zenye ubora ili waweze
kuhimili ushindani katika maonyesho ya kimataifa.
OWM-TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto (WMJJW)
ilihimiza Halmashauri zote kuwawezesha wanawake
kushiriki katika Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara
yaliyofanyika Dar es Salaam Julai, 2006 ili waweze
kupanua soko la bidhaa zao pamoja na kujifunza kutoka
kwa washiriki wengine.
Pia OWM-TAMISEMI kwa kushirikiana na WMJJW na
Mfuko wa Fursa sawa kwa Wote, wamekuwa
wakiendesha mafunzo katika Mikoa ili kuwajengea
uwezo wanawake katika shughuli za kibiashara.
Aidha, katika kulitafutia ufumbuzi suala la wanawake
kushiriki katika maonyesho ya kimataifa, OWM-
TAMISEMI imewasiliana na Wizara ya Viwanda,
Biashara na Masoko kwa barua Kumb.Na.
HA.307/399/01 ya tarehe 18/12/06 kama Wizara
inayohusika zaidi na suala hili iweze kulipa kipaumbele.
33. Semina Elekezi itafanyika kwa Semina Elekezi ya Viongozi wa Tawala za Mikoa
Viongozi wa Mikoa na Wilaya ili ilifanyika tarehe 22-26 Agosti, 2006, Ngurdoto, Arusha.
kufanya Utumishi wa Umma Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano alitoa maelekezo
uendeshwe kwa misingi ya Utawala ya uendeshaji wa Serikali ya Awamu ya Nne na
Bora. kusisitiza ufanisi wa washiriki hao katika UONGOZI,
UTAWALA na UENDESHAJI wa Serikali. Viongozi
walitakiwa kuwa Wabunifu na kuwa Viongozi wa
mabadiliko. Aidha, walitakiwa kutumia vizuri Raslimali
zote kwenye maeneo ya Utawala na kuongoza kwa
mujibu wa Katiba, Sheria, Kanuni na Taratibu. Washiriki
walikuwa ni RCs, DCs, RASs na baadhi ya Mawaziri na
Makatibu Wakuu.
34. Katika mwaka 2006/2007 Serikali Kazi ya kuhuisha Muundo wa Sekretarieti za Mikoa
itaendelea kutekeleza programu ya imefanyika. Taarifa ya awali imewasilishwa Ikulu kwa
kukuza uwezo wa Sekretarieti za ajili ya kupitiwa na Kikao cha Kazi cha Makatibu Wakuu
Mikoa na kuhuisha muundo wa wa Wizara.
Sekretarieti za Mikoa.
35. Serikali Kuu itaingia Mkataba wa Halmashauri zote zimeingia Mkataba wa Rasilimali
Kiutendaji na Serikali za Mitaa ili Fedha na Serikali katika Mwaka wa Fedha 2006/2007.
kuhakikisha pande zote mbili Kwa kipindi cha kuanzia Septemba, 2006 hadi sasa
zinawajibika kisheria na zinatekeleza Serikali Kuu inatekeleza majukumu yake katika Mkataba
majukumu yake kwa mujibu wa Katiba, kwa kutoa Ruzuku kwa Halmashauri kwa wakati na
Sheria, Sera za Kitaifa, Kanuni na Halmashauri zinatekeleza majukumu yake kwa
Miongozo mbalimbali. kukusanya mapato yake kufuatana na Bajeti.
36. Serikali katika mwaka 2006/2007 Mwaka 2006/2007 Serikali ilitambua miliki katika
12
itaendelea kutambua milki katika maeneo yaliyojengwa kiholela katika Miji. Halmashauri
maeneo yaliyojengwa kiholela Katika zimeelekezwa kutekeleza hilo. Kwa mfano, eneo la
miji nchini na kutoa leseni za makazi. Chang‟ombe Manispaa ya Dodoma, Dar es Salaam –
Manzese na maeneo ya Mwanza. Maeneo hayo
yaliyojengwa kiholela yamehalalishwa na kutolewa
leseni za makazi ili waweze kuombea mikopo. Kati ya
nyumba 400,000 tayari nyumba 200,000 zimetambuliwa
na nyumba 45,000 zimepata leseni katika jiji la Dar es
Salaam. Kazi inaendelea.
13
OFISI YA RAIS - MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuimarisha uwajibikaji wa watumishi Ili kuimarisha uwajibikaji wa watumishi wa Umma,
wa umma. Serikali imeweka mipango madhubuti ya kuhakikisha
kwamba watumishi wa umma wanawajibika katika
kufikia malengo na matarajio yaliyowekwa na taasisi zao
kulingana na mipango waliyojiwekea na
wanavyotarajiwa na Umma kwa ujumla.
Baadhi ya mambo ambayo hadi sasa yanaendelea
kutekelezwa kwa awamu na OR-MUU katika Wizara,
Idara zinazojitegemea na Wakala za Serikali ili
kukamilisha mipango hiyo ni pamoja na kuandaa:
(i) Mikataba ya huduma kwa Wateja (CLIENT SERVICE
CHARTERS),
(ii) Kuendelea kuimarisha matumizi ya Mfumo wa
Upimaji wa wazi wa utendaji kazi (OPRAS) na
(iii) Uandaaji wa Mipango Mikakati (Strategic Plans) ya
Wizara, Idara zinazojitegemea na Wakala za
Serikali.
2. Kuongeza watumishi wa Afya hasa Ili kuongeza watumishi wa Afya, Serikali imefanya
Madaktari bingwa. yafuatayo:-
Imelegeza masharti ya ajira za watumishi wa afya
kwa kuwaajiri moja kwa moja wanapohitimu kutoka
vyuoni na kuwapanga katika vituo vya kazi mikoani
na wilayani.
Serikali imekuwa ikiboresha mishahara ya
watumishi wa afya mwaka hadi mwaka.
3. Kuboresha mishahara na maslahi ya Katika mwaka wa fedha 2006/07 Serikali imeendelea
watumishi wa Umma. kuboresha maslahi ya watumishi kwa kutekeleza Sera
ya Muda wa Kati ya Malipo ya mishahara kwa kufanya
yafuatayo:
Kufanya utafiti wa viwango vya mishahara katika
sekta mbalimbali kwa lengo la kuainisha mishahara
ya Watumishi wa umma na sekta nyingine. Taarifa
ya utafiti huu itaisaidia serikali inapofanya maamuzi
ya nyongeza za mishahara ya mwaka.
Tume ya kuboresha maslahi ya watumishi iliundwa
na imekamilisha kazi yake na mapendekezo
yameanza kufanyiwa kazi.
Serikali imeendelea kuboresha mishahara ya
watumishi wake kwa kadiri ya ukuaji wa uchumi
14
wake.
4. Kutoa elimu endelevu kwa watumishi Mafunzo kwa watumishi wa umma yanatolewa kwa
wa Umma serikalini ili kuwavutia na misingi ya kukuza vipaji, maarifa na ujuzi na
kuwabakiza watumishi wenye sifa. yanayohitajika kuboresha utendaji kazi, utaratibu
endeleveu wa kupanga, kutekeleza na kusimamia
mafunzo, umeandaliwa kupitia Sera ya Mafunzo katika
Utumishi wa Umma ambayo ipo tayari katika hatua za
mwisho kuidhinishwa kutumika.
Mafunzo kwa viongozi 84 yametolewa, katika nyanja
zifuatazo: uongozi, maadili na uwajibikaji, na huduma
kwa wateja. Mafunzo ya huduma kwa wateja
yametolewa kwa maafisa wa ngazi za juu wa jeshi la
polisi.
Udhibiti wa wahitimu Ili kudhibiti wahitimu wanaosomeshwa na Serikali
5.
wanaosomeshwa na Serikali ili wasiende kufanya kazi nchi nyingine, Serikali inafanya
wasiende kufanya kazi nchi nyingine. yafuatayo:-
Inaendelea kurekebisha mshahara wa watumishi wa
umma.
Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya kazi
ikiwa ni pamoja na vitendea kazi.
Tatizo la watumishi wengi wa sehemu Serikali kupitia TAMISEMI imeshafanya utafiti juu ya
6.
za vijijini kukataa kwenda kwenye tatizo hili.
vituo vya kazi na wengine kuacha kazi Hili ni moja ya mapendekezo ya Tume ya Rais ya
kabisa kwa sababu ya mazingira kuboresha maslahi ya watumishi wa umma.
magumu. Mapendekezo hayo yatajadiliwa na Serikali kwenye
kikao cha Baraza la Mawaziri tarehe 24/08/2007.
Upandishaji vyeo watumishi wa Katika mwaka wa fedha 2006/2007 Serikali
7.
umma. iliwapandisha vyeo watumishi 9,414 ambapo Serikali
ilitumia jumla ya Shs. 12.06 bilioni kwa ajili ya
kugharamia ongezeko la mishahara yao. Aidha katika
mwaka wa fedha 2007/2008 Serikali imetenga fedha
kwa ajili ya kupandisha vyeo jumla ya watumishi
85,267. Hii inajumuisha watumishi 25,597 toka Wizara
na Idara zinazojitegemea, 1,127 toka Sekretarieti za
mikoa na watumishi 58,544 toka Serikali za Mitaa
ambapo 38,505 ni walimu waliokuwa wamelundikana
katika cheo kimoja kwa muda mrefu.
Kuandaa mkakati wa utekelezaji wa Kazi hii imeendelea kufanywa hatua kwa hatua
8.
sera ya mawasiliano ya serikali kwa kupitia makala kwenye magazeti, vipindi vya
umma na kutoa ufafanuzi wa masuala Televisheni na Redio, semina za Wabunge na
mbalimbali ya kiserikali kwa semina kwa watendaji wote wakuu wa wilaya zote za
wananchi. mikoa ya Manyara, Kigoma, Rukwa na Ruvuma.
Lengo la kutoa elimu hii ni kujenga uelewa kwa
15
watendaji mbalimbali wa serikali ili waweze kuelewa
na kubadilika kiutendaji kuendana na mabadiliko ya
kiutendaji yanayoendelea serikalini chini ya
Programu ya Kuboresha Utumishi wa Umma. Aidha,
kujenga ufahamu kwa wananchi ili waweze kuelewa
maboresho ya kiutendaji serikalini na kuweza
kuyatumia katika kupata na kudai huduma bora toka
vyombo mbalimbali vya umma.
Mafunzo kuhusu matumizi ya Teknolojia ya Habari
na Mawasiliano yalitolewa kwa watumishi 150 kutoka
Wizara na Idara mbalimbali za Serikali.
Kwa kuanzia Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma ili iweze kuwafikia watanzania wote
kuwaelimisha kupitia Radio za Mikoani imeandaa
vipindi vya radio na Televisheni kwa ajili ya
kuelimisha watanzania wote. Vipindi hivyo ambavyo
tayari vimeanza kurushwa na Televisheni ya Taifa
(TVT) na Radio Tanzania Dar es Salaam vimelenga
kutoa elimu ya dhati kwa wananchi wote.
Ikulu:
9.
Kuandaa mkakati wa utekelezaji wa Maafisa Mawasiliano 89 kutoka Wizara na Taasisi za
Sera ya Mawasiliano ya Serikali kwa Serikali walipatiwa mafunzo juu ya kuandaa mikakati ya
Umma na kutoa ufafanuzi wa masuala kuwasiliana na umma kwa kutumia vyombo mbalimbali
mbali mbali ya kiserikali kwa wananchi. vya habari.
10. Kushughulikia rufaa za watumishi wa Rufaa 110 za watumishi wa umma zilichambuliwa na
umma zinazotolewa kwa Rais na kwa uamuzi wa Rais au Katibu Mkuu Kiongozi kutolewa.
Katibu Mkuu Kiongozi. Aidha, malalamiko 333 ya watumishi wa umma
yalichambuliwa na kutolewa uamuzi kwa maelekezo ya
Rais au Katibu Mkuu Kiongozi.
11. Ikulu-Utawala Bora: Mkakati wa Awamu ya Pili wa Kupambana na
Kuendelea kuratibu utekelezaji wa Rushwa uliandaliwa na kuzinduliwa tarehe 10
Mpango wa Awamu ya Pili wa Mkakati Desemba, 2006.
wa Kupambana na Rushwa ambao Wafanyakazi 460 kutoka Wizara na Taasisi za
katika kipindi hiki utahusisha Umma walipatiwa mafunzo kuhusu mkakati
Halmashauri za Wilaya, Manispaa na wa kuzuia rushwa na utawala bora.
Majiji yote nchini. Wajumbe 200 wa Kamati za Uadilifu za Wizara na
Taasisi za Umma walipatiwa mafunzo ya
utawala bora na majukumu wanayotakiwa kutekeleza
kama wajumbe wa kamati hizo.
12. Kuhakiki na kufuatilia utekelezaji wa Mfumo wa utoaji taarifa kila robo mwaka za rushwa
Mpango wa Awamu ya Pili wa Mkakati umeboreshwa kwa kuanzisha Kamati za Uadilifu
wa Taifa dhidi ya Rushwa ili kwenda (Integrity Committees) katika Wizara hadi ngazi ya
sambamba na utekelezaji wa Wilaya. Wajumbe wa Kamati hizi ni wa ngazi za
programu zingine za Utawala Bora ukurugenzi ambao huwajibika kwa kutoa taarifa kwa
16
kama vile Maboresho katika Sekta ya wakati.
Umma, Maboresho katika Serikali za
Mitaa na MKUKUTA. Mpango wa kuhuisha utekelezaji wa Mkakati wa Taifa
Dhidi ya Rushwa kwenda sambamba na programu
zingine za utawala bora unaendelea vyema. Kwa mfano
malengo ya Mkakati wa kupambana na rushwa
yamekwishaingizwa (Mainstreamed) katika taratibu za
utekelezaji wa MKUKUTA na programu ya Maboresho
katika Serikali za Mitaa.
13. Siasa na Uhusiano wa Jamii:
Kuendelea kuratibu masuala ya siasa Masuala ya siasa na mahusiano ya jamii yameendelea
na mahusiano ya jamii. kutafutiwa ufumbuzi na kumshauri Mh. Rais kwa kadri
yalivyowasilishwa.
14. Taasisi ya Kuzuia Rushwa:
Kuendelea na uchunguzi wa tuhuma Upelelezi wa majalada 2,304 pamoja na majalada 1,272
2,304 zilizopo na zingine yaliyofunguliwa na kupokelewa kuhusu tuhuma za
zitakazopokelewa. vitendo vya rushwa uliendelea katika maeneo
mbalimbali nchini ambapo jumla ya majalada 1,188
yalishughulikiwa na kukamilika.
15. Kuendelea na uendeshaji wa kesi 195 Jumla ya kesi za rushwa 268 ziliendeshwa mahakamani
zilizopo mahakamani na nyingine zikiwemo kesi mpya zilizofikishwa mahakamani. Kesi
zitakazofunguliwa kipindi hicho. 50 zilitolewa uamuzi, kesi 25 watuhumiwa wake
walihukumiwa vifungo, kesi 9 ziliondolewa mahakamani
na kesi 16 watuhumiwa waliachiwa huru.
16. Kuendelea kuelimisha, kufahamisha na Jumla ya vipindi vya radio 21 vya uelimishaji
kuhamasisha wananchi juu ya haki wananchi kujiepusha na vitendo vya rushwa
zao, madhara ya rushwa na jinsi ya vimerushwa kupitia Radio Tanzania. Elimu kwa umma
kupambana na kujiepusha na vitendo juu ya kujiepusha na rushwa imetolewa kwa
vya rushwa. kuhudhuria semina za mialiko 10 zilizoandaliwa na
Wizara, Idara na Wakala wa Serikali.
Nakala 20,000 za jalada “uvuvi endelevu
unawezekana tukiepuka rushwa” zilisambazwa kwa
wananchi kwa lengo la kuwaelimisha kujiepusha na
vitendo vya rushwa na hivyo kuzuia uvuvi haramu.
Taasisi imeshiriki katika maonyesho ya Sabasaba,
Nanenane, Nenda kwa Usalama barabarani, Kilele
cha Mwenge (wiki ya vijana) kwa lengo la kutoa elimu
ya kuwaelimisha washiriki madhara ya kujihusisha na
vitendo vya rushwa.
Tathmini ya usikivu wa vipindi vya Radio “Rushwa
Adui wa Haki” kwa mikoa 12 kwa ajili ya kupata maoni
ya wananchi imefanyika. Uchambuzi wa utafiti huo
unaendelea.
17. Kufanya tafiti 48 zitakazohusu sekta za Tafiti mbili (2) zinazohusu ufuatiliaji wa malalamiko ya
umma na binafsi. Lengo likiwa ni utumiaji wa vipimo vya UKIMWI visivyokuwa na ubora
17
kuongeza kasi ya kupambana na na utafiti kuhusu huduma, ununuzi na usambazaji wa
rushwa kwa kuziba mianya iliyobainika dawa MSD zimekamilika. Aidha, tafiti zingine 12
katika maeneo husika. zimekwishaanzishwa na utafiti unaendelea.
18. Kukamilisha marekebisho ya Sheria ya Sheria mpya ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
Kuzuia Rushwa Namba 16 ya mwaka ilipitishwa na Bunge mwezi Aprili, 2007. Sheria hii
1971. mpya imeainisha makosa ya rushwa 24 kutoka makosa
manne (4) katika Sheria Na. 16 ya mwaka 1971 ambayo
sasa imefutwa.
19. Mfuko wa Maendeleo ya Jamii
(TASAF)
Kushirikiana na jamii, Halmashauri na Katika Awamu ya Kwanza TASAF ilifadhili miradi 33
Ofisi ya Waziri Kiongozi kwa upande Unguja (elimu 15, maji 9, afya 9) yenye thamani ya
wa Unguja na Pemba ili kuhakikisha shilingi 897,743,057.20 na kwa Pemba TASAF ilifadhili
kuwa miradi ambayo haikukamilika miradi 28 (elimu 4, maji 17, afya 3, barabara 3) yenye
katika Awamu ya Kwanza ya TASAF thamani ya shs. 709,730,928. Miradi hii yote ilikamilika
inakamilishwa. kwa mujibu wa makubaliano baina ya TASAF na jamii
ambazo zilikuwa zimeomba miradi hiyo.
Aidha, kwa upande wa Tanzania Bara miradi 98 yenye
thamani ya Shs. 867,336,601 ambayo haikukamilika,
jamii katika maeneo husika imeshauriwa kuzingatia
utaratibu kwa kuomba fedha ili kukamilisha miradi hiyo.
20. Kujenga uwezo wa uelewa wa
TASAF kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya na
wananchi kuhusu suala zima la
Ofisi ya Waziri Kiongozi, imefanya semina kuhusu
utekelezaji wa miradi kwa lengo la
TASAF kwa vijiji, mitaa yote kwa Tanzania Bara, na vile
kuwa na miradi endelevu na
vile kwa Shehia zote Zanzibar ili kueleza kuhusu TASAF
kuimarisha dhana ya umiliki wa jamii
na taratibu zake. Elimu hii imetolewa kwa kuwahusisha
na kuifanya jamii itambue kuwa miradi
viongozi katika maeneo husika ili kupeleka ujumbe
hiyo ni mali yao na kwa ajili ya
sahihi kwa wananchi.
maendeleo yao.
Kamati ambazo zimeteuliwa na jamii kusimamia
utekelezaji wa miradi hupatiwa mafunzo ili kuweza
kuelewa taratibu zote zinazotakiwa kufuatwa zikiwemo
utoaji wa taarifa, kutunza kumbukumbu za maendeleo
ya mradi, kutunza vitabu vya fedha, vifaa, usimamizi na
ufuatiliaji.
Katika ngazi ya Halmashauri, watendaji wote ambao
wanafanya kazi moja kwa moja na jamii katika
utekelezaji wa mradi hupatiwa mafunzo kuhusiana na
majukumu yao.
21. Kufadhili jumla ya miradi 1800 nchi Jumla ya miradi 1200 imeibuliwa na wananchi na
nzima. Aina ya miradi inayotarajiwa kuwasilishwa TASAF ili kupatiwa fedha. Kati ya miradi
kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa hiyo, miradi 541 yenye thamani ya Shs 12,453,251,186
barabara, madaraja, madarasa, imekubalika na kupelekewa kiasi hicho cha fedha. Hadi
zahanati, nyumba za walimu na kufikia mwishoni mwa mwaka huu, inakadiriwa kufikia
18
waganga, visima vya maji, masoko, lengo la kufadhili miradi 1800. Utaratibu wa kuidhinisha
upandaji miti na miradi ya kuongeza hadi kupata fedha za kutekeleza miradi ya TASAF ni
kipato kwa watu wa makundi maalum. kama ifuatavyo:-
Halmashauri zinatakiwa kutuma maombi ya fedha
TASAF yaliyoambatanishwa na mchanganuo wa
gharama za mradi.
TASAF makao makuu inakagua maombi
yaliyowasilishwa kama yamekamilika na yana
viambatanisho vyote vinavyohitajika kwa mujibu wa
miongozo.
Timu ya Wataalamu wa Sekta itakagua maombi
yote kuhakiki kuwa miradi inayoombewa imekidhi
viwango na vigezo vya sekta husika.
Kamati ya uendeshaji ya TASAF Taifa (NSC)
itaidhinisha fedha ili zitumwe kwenye Halmashauri
au miradi iliyopitishwa na Timu ya Wataalam wa
Sekta na TASAF makao makuu kwa ajili ya
utekelezaji wa miradi hiyo.
22. MKURABITA
Kufanya utafiti wa kina katika wilaya 26 Utafiti umefanyika katika wilaya 34 za Tanzania Bara na
za Tanzania Bara na katika Visiwa vya wilaya 9 za Tanzania Visiwani (Zanzibar na Pemba).
Unguja na Pemba na kuandaa
mapendekezo ya awali ya maboresho Uandaaji wa maboresho ya sheria na kanuni zitumikazo
ya sheria na kanuni zitumikazo katika katika sekta isiyo rasmi unaendelea na mtaalam kutoka
sekta isiyo rasmi ili ziwe sehemu Peru ameshatoa mapendekezo ya maboresho.
muhimu za mfumo mpya
unaokusudiwa. Aidha, mawasiliano na
wadau yatafanyika ili kukamilisha
rasimu za awali za maboresho.
23. Kutoa mafunzo kwa wataalam wa Zaidi ya wataalam arobaini na mbili (42) wameshapata
Kitanzania ishirini (20) watakaohusika mafunzo juu ya mchakato wa kutengeneza sheria kwa
katika mchakato wa kutengeneza ajili kuhakikisha umiliki na ushiriki wa Tanzania katika
sheria ili kuhakikisha umiliki wa ushiriki zoezi zima la mapendekezo ya maboresho.
wa Tanzania katika kutengeneza
sheria husika. Aidha, MKURABITA Wafanyabiashara wadogo 388 kutoka vikundi
itatoa mapendekezo ya marekebisho mbalimbali wamepewa mafunzo ya ujasiriamali na
yanayohitajika katika sheria za sasa za utayarishaji wa vitabu vya mahesabu. Kutokana na
umiliki mali ili ziunganishwe na kanuni mafunzo haya vikundi 8 tayari vimeshasajiliwa na msajili
za jamii zilizoboreshwa kupata mfumo wa makampuni ili kuwa rasmi.
mpya unaokusudiwa.
Mafunzo elekezi juu ya mchakato wa urasilimishaji mali
na biashara yalitolewa kwa wataalamu wazalendo 42
ambao kwa kushirikiana na INSTITUTE OF LIBERTY
19
AND DEMOCRACY wamefanya utafiti na uchambuzi
wa nyaraka na taarifa mbalimbali zilizotumika
kutayarisha mapendekezo ya maboresho ya awali.
24. Kukamilisha mipango ya utekelezaji wa
shughuli ambazo zinaweza kwenda
sambamba na maandalizi ya
maboresho kwa nia ya kuendeleza
nguvu na msukumo wa watanzania
uliotokana na Taarifa ya Utafiti kama
ifuatavyo:-
a) Kuandaa na kutekeleza mkakati Maandalizi ya mkakati mahsusi wa mawasiliano na
wa mawasiliano ili kuhakikisha mpango wa utekelezaji yameanza na yanategemewa
kuwa maboresho yaliyochaguliwa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Oktoba, 2007.
yanamfikia mlengwa.
b) Kukamilisha utaratibu wa mkataba Mkataba umeshatengenezwa na kutiwa saini na pande
na Taasisi ya Takwimu ya Taifa ili zote mbili. Kazi imeshaanza rasmi na kwamba mshauri
kufanya utafiti wa msingi wa sekta mwelekezi yuko katika hatua ya kutengeneza hojaji
isiyo rasmi kwa Zanzibar na Dar (questionnaires).
es Salaam. Aidha, utafiti huu
unalenga kusaidia katika kuratibu
ukuaji wa sekta isiyo rasmi.
25. Kukamilisha dhana ya MKURABITA Kabrasha limeshasambazwa kwa walengwa kwa ajili ya
(Program Concept Document) ili kupata maoni yao. Maoni hayo yatajadiliwa kwenye
litumike kwa ajili ya kuandaa warsha maalum itakayoshirikisha wadau wa
utekelezaji wa awamu zinazofuatia. MKURABITA kabla haijapelekwa serikalini kwa
kuidhinishwa. Mchakato wote ulikamilika mwezi Machi,
2007.
26. Kutengeneza miongozo na taratibu Taratibu za kutengeneza kitabu cha rejea cha watoa
ambazo zitawapa uwezo walengwa na huduma (service providers directory) zimeshaanza ili
watekelezaji kwa kushiriki kikamilifu kuwezesha walengwa kupata huduma kwa wakati
katika suala zima la urasimishaji. unaofaa na kwa bei inayofaa.
(a) Kuwawezesha walengwa ambao Upimaji wa ardhi ya vijiji na utoaji wa hati kwa kulingana
kwa sasa wameshaanza na mahitaji ya sheria ya ardhi ya vijiji ya mwaka 1995
mchakato wa kurasimisha unaendelea katika vijiji 7 vya wilaya ya Handeni. Hati za
rasilimali na biashara zao vijiji hivyo saba zimeshatolewa na sasa ugawaji wa ardhi
kukamilisha urasimishaji na kwa wanakijiji (land parceling) unaendelea. Vijiji hivyo ni;
kuanza kutumia rasilimali na Kweisasu; Mzeri; Bongi; Kwamkono; Mbuyuni; Nkale;
biashara zao kupata mikopo na Sindeni.
fursa nyingine katika soko rasmi.
(b) Kushirikiana na Wizara ya Ardhi Upimaji wa mashamba ya “Lungufu Farmers Group”
na Maendeleo ya Makazi kuandaa mkoani Kigoma umekamilika na hati za umiliki kwa ajili
utaratibu wa muda (Temporary ya watu 25 zinasubiri sahihi ya Kamishna wa Ardhi. Kazi
20
arrangements) za kutoa hati za hii imefanywa kwa kuwashirikisha Wizara ya Ardhi na
kumiliki ardhi kimila kwa kasi zaidi Maendeleo ya Makazi.
kuliko ilivyo sasa.
Kwa kushirikiana na “WAT Human Settlement” upimaji
wa makazi ya Hananasifu katika Manispaa ya Kinondoni
unaendelea vyema. Kazi hii imeanza tarehe 27
Septemba, 2006.
Uandaaji wa miongozo na taratibu ambazo zitawapa
walengwa na watekelezaji uwezo wa kushiriki kikamilifu
katika suala zima la Urasimishaji umeanza. Miongozo hii
ni pamoja na kitabu cha Rejea cha watoa Huduma za
Kibiashara na kitabu cha Kiongozi cha Urasimishaji
Ardhi kwa mujibu wa Sheria.
Mawasiliano na mabenki yanaendelea ili kuona
uwezekano wa benki kupunguza masharti hasa kwa
wafanyabiashara wadogo na wa kati. Benki
zinazohusika ni; Benki ya Akiba, CRDB, NBC na
Eurafrican. Vile vile, Benki Kuu inahusishwa katika
majadiliano haya.
Jumla ya hati za vijiji saba wilayani Handeni zimetolewa.
Tunaendelea na taratibu za kupima kwa ajili ya
wanakijiji. Zoezi hili litahamia Bagamoyo.
Kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, TAMISEMI, MKURABITA
imefanya upimaji wa ardhi ya vijiji na utoaji wa hati
kulingana na mahitaji ya Sheria ya Ardhi ya Vijiji, Na. 5
ya mwaka 1999, katika vijiji saba (7) vya Wilaya ya
Handeni. Hati za vijiji hivyo saba (7) zimeshatolewa na
kazi inayoendelea ni upimaji wa mashamba katika vijiji
hivyo. Aidha, upimaji wa mashamba ya “Lungufu
Farmers Group” mkoani Kigoma na makazi ya
Hananasif Wilayani Kinondoni kwa utaratibu huo huo wa
kushirikisha mamlaka nyingine umekamilika na hati za
umiliki zinaandaliwa.
27. Taasisi ya Kuzuia Rushwa
Kuimarisha Ofisi sita za Kanda kwa
kuziongezea watumishi na vitendea Kibali cha kuajiri watumishi wapya kimeshatolewa na
kazi ili kuboresha huduma zake kwa watumishi hao wanapatiwa mafunzo kabla ya
Viongozi na wananchi kwa ujumla. kupangiwa vituo vya kazi katika kanda hizo.
21
28. Kuhakiki mali za baadhi ya viongozi Jumla ya viongozi 3,317 walikuwa wametoa Tamko la
walizozitaja katika tamko la Rasilimali Mali na Madeni yao kati ya 6,415 ambao walikuwa
na madeni kwa madhumuni ya wametumiwa fomu.Utaratibu wa kufuatilia fomu
kuhakikisha kuwa mali zilizotajwa zilizobaki unaendelea. Aidha, uhakiki wa kina wa mali au
katika tamko ndizo walizonazo. Aidha, rasilimali za Viongozi wa Umma 195 wa kada mbali
ulinganisho utafanywa kati ya mali mbali nchini kote umefanywa.
zilizotajwa kwenye tamko na maelezo
ya kipato ya viongozi husika.
29. Kuandaa mfumo wa Benki ya Takwimu Hadidu za rejea kwa ajili ya kuandaa mfumo wa Benki
(Data Bank) ya mali za Viongozi wa ya Takwimu (Data Bank) ya Viongozi wa Umma na mali
Umma kwa ajili ya kurahisisha rejea zao ili kurahisisha rejea na uwekaji kumbukumbu sahihi
na uwekaji kumbukumbu wa mali hizo ya viongozi na mali zimeandaliwa. Kazi hii imekamilika.
na taratibu za viongozi kwa usahihi.
30. Kuandaa, kuchapisha na kusambaza Rasimu ya awali ya kanuni za Maadili ya Viongozi wa
kanuni za Maadili ya Viongozi wa Umma kwa lugha nyepesi imeandaliwa na Sekretarieti
Umma kwa lugha nyepesi ili viongozi ya Maadili ya Viongozi wa Umma. Aidha, machapisho
wa wananchi waweze kuelewa kanuni mbali mbali kama vile Kalenda kwa mwaka 2007 na
hizo kwa urahisi. vipeperushi yamechapishwa na kusambazwa kwa
wadau mbali mbali. Vile vile Sekretarieti ya Maadili ya
Viongozi wa Umma imeshiriki kwenye maonyesho ya
Nane Nane, Wiki ya Utumishi wa Umma na Uandaaji wa
Awamu ya Pili ya Utekelezaji wa Mkakati wa Taifa dhidi
ya Rushwa.
31. Kupitia Sheria ya Maadili ya Viongozi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeandaa
wa Umma ya mwaka 1995 na Sheria Hadidu za Rejea kwa lengo la kupitia upya vipengere
ndogo zilizotungwa chini ya sheria hiyo katika Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba
na kupendekeza marekebisho 13 ya 1995 pamoja na Kanuni/Sheria Ndogo
yanayohitajika. zilizotungwa chini ya Sheria hiyo. Lengo ni kupata
mtaalam wa nje au ndani kufanya mapitio hayo na kutoa
mapendekezo yanayohitajika. Aidha, Sekretarieti ya
Maadili ya Viongozi wa Umma inawasiliana na
Menejimenti ya Utumishi wa Umma ili kupata msaada
wa fedha kutoka "Performance Improvement Fund
(PIF)" kulipia gharama ya mtaalam atakayefanya kazi
hiyo.
32. Kuchunguza kwa haraka malalamiko Utaratibu umeboreshwa katika kufanya uchunguzi kwa
ya ukiukaji wa maadili ya viongozi haraka na kwa ufanisi mkubwa dhidi ya malalamiko ya
yatakayowasilishwa na wananchi ukiukaji wa maadili ya viongozi. Uchunguzi wa awali wa
kwenye Sekretarieti ya Maadili ya malalamiko 156 yaliyowasilishwa na wananchi dhidi ya
Viongozi wa Umma. viongozi wa umma waliotuhumiwa kukiuka maadili ya
viongozi ulifanywa.
33. Kutoa elimu ya Maadili kwa Viongozi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma
wa wananchi kwa njia ya Redio, imekamilisha taratibu za kurusha matangazo kwa njia ya
Semina na machapisho mbalimbali redio kupitia Redio Tanzania kwa mikoa ya Lindi,
kwa lengo la kukuza maadili mema na Mtwara na Ruvuma. Jumla ya vipindi vya redio 52
22
utawala bora nchini. vimeandaliwa na kulipiwa kwa ajili ya kurushwa hewani.
Aidha, Sekretarieti inakamilisha uandaaji wa vipindi vya
redio 44 kupitia Radio Free Afrika na Radio Maria. Vile
vile ratiba ya kuendesha semina/warsha imeandaliwa
kwa Viongozi wa Umma hususan Madiwani, Watendaji
Wakuu wa Halmashauri za Wilaya, Miji, Manispaa,
Wilaya na Mikoa. Vivyo hivyo, maandalizi ya
machapisho mbalimbali kwa lengo la kukuza maadili
mema na utawala bora miongoni mwa viongozi wa
umma yamefanywa.
34. Kuwapatia watumishi 25 wa Mpango na ratiba ya mafunzo kwa watumishi 25 wa
Sekretarieti mafunzo mbalimbali kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa lengo
lengo la kuboresha utendaji wao wa la kuboresha utendaji kazi imeandaliwa na utekelezaji
kazi. wake unaendelea. Aidha Sekretarieti ya Maadili ya
Viongozi wa Umma imepata nyongeza ya fedha kutoka
"Perfomance Improvement Fund" kwa ajili ya mafunzo
ya watumishi wake.
35. Kusimamia uendeshaji wa Mfuko Kuhusu uendeshaji wa Mfuko (Facility for Ethics,
(Facility) utakaoanzishwa chini ya Accountability and Transparency – FEAT) Sekretarieti
mradi wa kuimarisha uwajibikaji, uwazi ya Maadili ya Viongozi wa Umma imeshakamilisha
na uadilifu katika utendaji wa umma ufunguaji wa Akaunti Maalum kwa ajili ya Mfuko,
(Accountability Transparency and imeandaa na kutangaza ajira ya Meneja wa Mfuko.
Integrity Program – ATIP). (Component Manager), Tenda ya ujenzi wa Ofisi ya
Muda kwa ajili ya Mfuko. Aidha Sekretarieti ya Maadili
ya Viongozi wa Umma kwa kushirikiana na Maafisa wa
Benki ya Dunia hapa nchini inakamilisha kanuni na
taratibu za kuzindua na kuendesha Mfuko huu.
23
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuanzisha mfumo wa mawasiliano Mawasiliano mbalimbali na wadau wa Muungano
ambao utatumika katika tafiti yamefanyika ili kukusanya taarifa mbalimbali ambazo
mbalimbali zitakazohusu Mambo ya zitatumika katika tafiti zitakazohusu mambo ya
Muungano na kutoa mapendekezo Muungano. Aidha, taarifa hizo zimejumuishwa katika
kwa Serikali zetu mbili kwa lengo la Rasimu ya Mkakati wa Kuondoa Kero za Muungano na
kuondoa matatizo mbalimbali ya Kudumisha Ushirikiano Kati ya Serikali ya Jamhuri ya
Muungano yaliyopo na Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi
yatakayojitokeza. Zanzibar.
2. Kuhifadhi taarifa na kumbukumbu Taarifa mbalimbali za Muungano zimekusanywa,
mbalimbali za Muungano katika kuchambuliwa na kuingizwa katika mfumo wa
Maktaba ya Kielektroniki (Electronic kielektroniki. Aidha, kazi ya kutengeneza „‟Electronic
Library) ambapo wadau wa Muungano Library‟‟ haijakamilika kutokana na ukosefu wa vifaa,
watakuwa na haki ya kupata taarifa ufinyu wa Ofisi na ukosefu wa wataalamu.
sahihi za Muungano wetu. Inategemewa kuwa kazi hii itakamilika baada ya
kuhamia katika jengo jipya pamoja na kupata vifaa na
wataalamu.
3. Kuboresha utoaji huduma na kuongeza Watumishi 6 wameongezewa uwezo wa utendaji kazi
tija kwa Watumishi kwa kutoa mafunzo kwa kupata mafunzo ya muda mfupi nje na ndani ya
kwa Watumishi wa Idara ya Muungano nchi . Aidha, ziara zilifanyika katika nchi za Uingereza,
ikiwa ni pamoja na kufanya ziara za Ujerumani, Canada na Norway ili kupata Uzoefu wa
mafunzo katika Nchi zenye Muungano. namna bora ya kushughulikia masuala ya Muungano na
kuongeza ushirikiano kati ya Serikali zetu.
4. Kuandaa na kuhudhuria vikao angalau Vikao 14 vya ushirikiano vilivyoshirikisha wadau
viwili kwa mwaka vya uratibu wa mbalimbali wa Wizara, Idara, Taasisi na Asasi za SMT
mambo ya Muunagano kwa kila na SMZ vilifanyika Zanzibar na Tanzania Bara. Taarifa
Wizara, Idara na Asasi za Muungano za vikao hivi zimekusanywa na zimesaidia katika
na zile ambazo si za Muunagano ili kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kuondoa Kero za
kuongeza ufanisi zaidi kwa Serikali Muungano na Kudumisha Ushirikiano Kati ya Serikali ya
zetu mbili. Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar na kufuatilia utekelezaji wake. Aidha, vikao
hivyo vimesaidia pia kuongeza ushirikiano wa kisekta
baina ya pande mbili za Muungano.
5. Kuchukua hatua za makusudi za Ofisi iliandaa nakala 12,000 za vipeperushi na
kuielimisha jamii kuhusu Muungano kuvisambaza kwa wadau wa Muungano Tanzania Bara
wetu kupitia Vijarida, Redio, Luninga, na Tanzania Zanzibar.
Tovuti, Semina na Makongamano.
Vipindi 18 vya masuala ya Muungano vilirushwa hewani
kupitia Redio Tumaini, Redio Mlimani, Redio Uhuru na
Redio Tanzania pamoja na Sauti ya Tanzania Zanzibar.
Shirika la Habari la Uingereza na Sauti ya Ujerumani
walirusha hewani mahojiano na Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Makamu wa Rais - Muungano. Aidha,kulifanyika
24
mahojiano ya moja kwa moja na Waziri wa Nchi Ofisi ya
Makamu wa Rais – Muungano kupitia TVT na TVZ.
Ukusanyaji wa taarifa za Masuala ya Muungano kwa ajili
ya kuanzisha ukurasa wa masuala ya Muungano katika
tovuti ya Ofisi umekamilika. Hivi sasa wataalamu wa
Ofisi wanaendelea na kazi ya kuunganisha taarifa hizo
katika tovuti ya Taifa. Aidha, baadhi ya taarifa hizo
zimetolewa kama makala katika magazeti.
Ofisi iliandaa kongamano la Wanafunzi wa vyuo vikuu
Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar likiwa na lengo la
kuelimisha jamii juu ya masuala ya Muungano na
umuhimu wake. Ofisi pia ilishiriki katika maonyesho ya
wiki ya Utumishi wa Umma kuanzia tarehe 17-23 Juni,
2007 ambapo wananchi walipata fursa ya kuelimishwa
juu ya majukumu ya Ofisi ya Makamu wa Rais
Muungano ikiwa ni pamoja na masuala ya Muungano na
yasiyo ya Muungano. Katika maonyesho hayo, Ofisi
ilitoa Elimu kwa wananchi kuhusu Historia ya Muungano
hususan kuelezea matukio mbalimbali yaliyojiri katika
wiki ya Muungano. Aidha masuala ya kodi za Muungano
yalitolewa ufafanuzi kwa wananchi kwa undani katika
wiki hiyo.
6. Kuadhimisha siku ya kuanzishwa kwa
Muungano wetu kwa kushiriki Ofisi imeshiriki katika kutafuta wafadhili wa mashindano
kikamilifu katika maandalizi na ya Kombe la Muungano la Mufindi ambayo yalikutanisha
kuhudhuria sherehe za Muungano timu mbalimbali za Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar
ikiwa ni pamoja na kufuatilia matukio yaliyofanyika mwezi Machi – Aprili 2007. Aidha, ushiriki
mbalimbali yatokanayo na sherehe ulifanywa katika maandalizi na maadhimisho ya siku ya
hizo. Muungano iliyoadhimishwa tarehe 26 Aprili, 2007 katika
uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikiwa ni pamoja
kufuatilia matukio mbalimbali.
7. Kuratibu, kufuatilia na kutathimini Taarifa za utekelezaji wa masuala ya Muungano na
utekelezaji wa mambo ya Muungano yasiyo ya Muungano za kila robo mwaka ziliandaliwa na
ikiwa ni pamoja na miradi ya kuwasilishwa katika Vikao vya Menejimenti ya Ofisi ya
Muungano na kutoa mapendekezo Makamu wa Rais.
kwa Serikali zetu mbili.
Utekelezaji wa miradi kwa pande zote za Muungano. Hii
ni miradi mbalimbali ya maendeleo yenye sura ya Kitaifa
kama vile Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF),
SELF, MACEMP n.k ili kuweza kuweka uwiano mzuri wa
maendeleo ya kiuchumi.
8. Kuondoa kero za Muungano kwa Ofisi ya Makamu wa Rais imeandaa na kushiriki vikao
kuandaa na kushiriki vikao vya Waziri vya; Mhe. Waziri Mkuu na Mhe. Waziri Kiongozi
Mkuu na Waziri Kiongozi angalau mara Novemba, 2006; Vikao vitano vya Mawaziri wa sekta
tatu (3) kwa mwaka wa fedha za Muungano SMT na Mhe. Waziri Mkuu; na Vikao
25
2006/2007 ambavyo vitatanguliwa na vitatu vya Makatibu Wakuu wa Sekta za Muungano
vikao vya Wataalam na Mawaziri wa SMT. Maamuzi yaliyofikiwa na kutekelezwa:-
Sekta husika.
(i) Kwamba suala la Haki za Binadamu ni la Kikatiba
na ni la Kimataifa. Sheria ya Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora,Na. 7 ya mwaka 2001
imeshafanyiwa marekebisho na inatumika pande
zote za Muungano.
(ii) Marekebisho ya Sheria ya Mamlaka ya Kusimamia
Uvuvi katika Ukanda wa Bahari Kuu, ya mwaka
1998, yamepitishwa na Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania mwanzoni mwa Februari,
2007.
Aidha, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Kiongozi na
Katibu Mkuu, Wizara inayoshughulikia masuala ya
Kikosi Maaalumu cha Kuzuia Magendo (KMKM)
wamejumuishwa katika Kamati ya Utendaji ya
Mamlaka ya Uvuvi Katika Ukanda wa Bahari Kuu.
(iii) Ofisi imeratibu ujumuishwaji wa Zanzibar katika
Miradi ya Kikanda inayotekelezwa katika Jumuiya
ya Afrika ya Mashariki kama vile:-
(a) Mradi wa „East Africa Power Master Plan‟
ambapo Zanzibar imeunganishwa katika
Gridi ya Taifa ambayo itaunganishwa na
Gridi za wanachama wengine;
(b) Mradi wa kuimarisha Bandari ya Zanzibar;
(c) Mkakati wa Maendeleo wa Afrika Mashariki
kwa kipindi cha mwaka 2006/2010;
(d) Mpango endelevu wa kuendeleza Bandari
za Afrika Mashariki.
(iv) Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi:
Wizara husika kwa kushirikiana na TPDC
zimeandaa hadidu za rejea ambazo zitatumiwa na
Mshauri Mwelekezi atakayezishauri Serikali zetu
juu ya njia bora ya kugawana mapato
yatakayotokana na mafuta. Kwa hivi sasa hatua za
kumpata Mshauri Mwelekezi zinaendelea kwa
kufuata taratibu za manunuzi za Serikali.
(v) Utekelezaji wa Sheria ya „Merchant Shipping Act‟ ya
2003 katika Jamhuri ya Muungano na uwezo wa
Zanzibar kujiunga na „IMO‟ imeonekana bayana
26
kwamba,
Uanachama wa IMO ni wa Kitaifa ambapo
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndio
mwanachama. Wizara husika ziliunda Kamati
iliyojumuisha wajumbe toka pande zote za
Muungano kuchambua maeneo ambayo Zanzibar
itafaidika na ushauri uliotolewa na kamati hiyo
umeanza kutekelezwa kama ifuatavyo:-
Kanuni nane(8) za „Merchant Shipping Act‟,
2003 tayari zimeshapelekwa Wizara ya
Mawasiliano na Uchukuzi ya Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar ili zioanishwe na kanuni za
„Zanzibar Maritime Transport Act, 2006‟ kwa
lengo la kuleta usimamizi usiokinzana katika
masuala ya uchukuzi majini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano na
Uchukuzi, SMZ amepatiwa „access code‟ ili
aweze kuona nyaraka mbalimbali katika
mtandao wa IMO. Masuala mengine
yaliyopendekezwa yanaendelea kufanyiwa
kazi.
(v) Katika kuboresha shughuli za kifedha za Muungano,
Serikali imeandaa Mkakati wa Pamoja wa Misaada
Tanzania (JAST) ambao umejumuisha wajumbe wa
pande mbili za Muungano kwa lengo la kuhakikisha
kwamba miradi ya Tanzania Zanzibar inajumuishwa.
(vi) Upatikanaji na ugawaji wa misaada na mikopo
toka nje: Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
imeendelea kupata gawio la asilimia 4.5 kutokana
na misaada na misamaha ya madeni isiyokuwa na
masharti pamoja na faida ya Benki Kuu ya
Tanzania. Mwaka wa fedha 2006/07 Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar imepata kiasi cha TShs.
23,020,440,000/=. Gawio hilo huongezeka au
kupungua kulingana na misaada, misamaha ya
madeni na faida ya Benki kuu ya Tanzania.
(vii) Suala la wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa
kodi mara mbili: Mtandao wa ASYCUDA++
umeshaanzishwa na kufanya kazi Zanzibar kuanzia
mwezi Juni, 2006 ambao utaondosha ulipishwaji wa
27
kodi mara mbili. Mtandao huu unamtaka muingizaji
bidhaa kutoa tamko la gharama za bidhaa
anazoingiza nchini.
(viii) Tume ya Pamoja ya Fedha imefanya tathmini na
kukamilisha taarifa ya mapendekezo juu ya vigezo
vya kugawana mapato na kuchangia gharama za
Muungano. Aidha, tayari Serikali imeandaa Waraka
wa Baraza la Mawaziri kwa utekelezaji zaidi.
9. MAZINGIRA Maandalizi ya Kanuni, Miongozo, Viwango vya
Kuandaa kanuni, miongozo, viwango Mazingira na Taratibu mbalimbali yameendelea
vya mazingira na taratibu zilizobaki ili kufanywa.
kuiwezesha Sheria ya Usimamizi wa Kanuni kuhusu kupiga marufuku matumizi ya baadhi
Mazingira ya mwaka 2004 kutekelezwa ya mifuko ya plastiki “The Environmental
kikamilifu. Management (Prohibition of Manufacturing,
Importation, Selling, Buying and Use of Plastic Bags)
Regulations, 2006” imeandaliwa na kuanza kutumika.
Maandalizi ya Kanuni nyingine nne yanaendelea
ambazo ni:
(i) „Strategic Environmental Assessment (SEA)‟;
(ii) „Ozone Depleting Substances‟ (ODS);
(iii) „Environmental Quality Standards‟ (EQS);
(iv) „Fees and Charges Payable under the Atc‟.
10. Kukamilisha Programu ya kujenga Rasimu ya Programu ya utekelezaji iko katika hatua za
uwezo wa wadau kuielewa na mwisho kukamilika. Ripoti ya awali ya utekelezaji wa
kuitekeleza kikamilifu Sheria ya Programu hii imeandaliwa.
Usimamizi wa Mazingira.
11. Kukamilisha zoezi la uteuzi wa Wizara nne zimeteua Waratibu wa Mazingira wa Sekta.
Waratibu wa Mazingira wa Sekta na Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana; Wizara
Maafisa Mazingira katika ngazi ya Mambo ya Ndani; Wizara ya Kilimo, Chakula na
mbalimbali za Serikali za Mitaa. Ushirika; na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii. Juhudi
zinaendelea kuzihamasisha sekta nyingine ziweze
kufanya hivyo.
12. Kufuatilia utekelezaji wa uzalishaji bora Viwanda 12 vinaendelea kutekeleza mbinu mbalimbali
viwandani (Cleaner Production) katika za uzalishaji bora zilizobuniwa na viwanda hivyo wakati
viwanda vinavyotekeleza Programu ya wa utekelezaji wa Awamu ya kwanza ya Programu ya
Hifadhi ya Mazingira ya Ziwa Victoria. Hifadhi ya Ziwa Victoria.
13. Kuanza utekelezaji wa Programu ya Maandalizi ya utekelezaji programu hii ikiwemo
Bonde la Ziwa Tanganyika. upatikanaji wa ofisi, na uajiri wa wataalamu
yamekamilika. Kikao cha kwanza cha Mawaziri wa
Mazingira wa nchi husika na programu kimefanyika.
14. Kuendelea na utekelezaji wa Programu Programu ya Usimamizi wa Hifadhi ya Mazingira na
ya Hifadhi ya Mazingira na Maliasili Maliasili inatekelezwa kwa kushirikiana na Serikali ya
(Environmental and Natural Resources Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la USAID.
28
Progamme) Awamu ya Kwanza iliyoanza 1997 ilimalizika 30
Septemba, 2005. Kabla ya kuanza awamu ya pili,
palikuwepo na mwaka mmoja wa „No cost extension‟ ili
kumalizia shughuli zilizokuwa hazijamalizika. Awamu ya
pili ilianza rasmi tarehe 1 Novemba, 2006; na itamalizika
mwaka 2014. Ofisi ya Makamu wa Rais inaendelea
kuratibu programu hiyo.
15. Kuendesha warsha za mafunzo kwa Warsha ya mafunzo kwa wataalamu wa sekta
wataalamu wa Sekta mbalimbali, mbalimbali, Mahakama na Serikali za Mitaa kuhusu
Mahakama na Serikali za Mitaa Sera na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira katika
kuhusu Sera na Sheria ya Usimamizi kutekeleza programu ya Usimamizi wa Hifadhi ya
wa Mazingira katika kutekeleza Mazingira na Maliasili ilifanyika Juni, 2007.
Programu ya Usimamizi wa Mazingira
na Maliasili.
16. Kufanya maboresho na maandalizi ya Maandalizi ya programu ya pamoja kwa ajili ya hifadhi
utekelezaji wa Programu ya Hifadhi ya ya Nyanda za juu Kusini yameanza chini ya ufadhili wa
Mazingira ya Bonde la Ziwa Nyasa. Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF) kupitia UNDP.
17. Kuendelea kuratibu kitaifa Programu Kazi ya kuratibu inaendelea chini ya Ofisi ya Makamu
ya Hifadhi ya Mazingira ya Bonde la wa Rais.
Mto Nile.
18. Kuendesha warsha itakayojadili athari Warsha ilifanyika tarehe 17-18 Oktoba, 2006 kwa
za sera za maendeleo kwa mazingira, kushirikisha walimu 20 kutoka katika shule 10, za
mafunzo kwa walimu wa shule kumi za sekondari za Bwiru, Lake, Nganza, Karagwe, Bukoba,
sekondari katika mikoa ya kanda ya Rugambwa, St. Pius, Nansio, Maswa, na Shinyanga.
ziwa kuhusu teknolojia ya habari na
mawasiliano kwenye elimu ya
mazingira chini ya Programu ya Hifadhi
ya Bonde la Mto Nile.
19. Kuendesha warsha kwa Wabunge Warsha ilifanyika huko Entebbe Nchini Uganda tarehe
kuhusu programu na changamoto 17 – 20 Julai, 2006. Bunge liliwakilishwa na Mhe. J. M.
zinazolikabili Bonde la Mto Nile. Shibuda (Mb) na Mhe. Kidawa Salehe (Mb).
20. Kubuni miradi zaidi kutoka 9 ya sasa Miradi 20 inatekelezwa kwa gharama ya dola za
hadi 22 na kutekeleza miradi 10 ya Kimarekani 452,233. Hadi sasa kiasi cha dola za
sekondari. Kimarekani 238,669 zimetumika.
21. Kuendesha mashindano ya insha, Tangazo la shindano la mwaka 2006/07 limetolewa na
uchoraji na upigaji picha kuhusu kusambazwa kwenye shule mbalimbali kanda ya ziwa.
hifadhi ya mazingira.
22 Kuendesha mafunzo na mikutano ya Mikutano na warsha katika ngazi mbalimbali
wadau kuhusu Programu ya Hifadhi ya zimefanyika.
Mazingira ya Bonde la Mto Nile.
23. Kutekeleza awamu ya pili ya mradi Maandalizi ya awamu ya pili ya mradi yamekamilika na
kuhusu matumizi salama ya utekelezaji wake umeanza.
biotekinolojia ya kisasa katika
kutekeleza Itifaki ya Cartagena.
29
24. Kuendesha mafunzo kwa sekta Mafunzo juu ya upashanaji habari kuhusu matumizi
mbalimbali na kutoa vifaa vya maabara salama ya biotekinolojia ya kisasa yaliyoshirikisha
kwa ajili ya utafiti. Kutambua bidhaa, washiriki 21 kutoka Wizara mbalimbali yalifanyika kati ya
mazao na viumbe ambavyo vilifanyiwa tarehe 12 – 16 Septemba, 2006.
mabadiliko ya kijenetiki na kufuatilia
athari zinazoweza kusababishwa na
matumizi ya biotekinolojia ya kisasa.
25. Kuandaa kanuni kuhusu matumizi Kanuni zitaandaliwa wakati wa utekelezaji wa awamu ya
salama ya biotekinolojia ya kisasa na pili ya mradi kuhusu matumizi salama ya biotekinolijia ya
kuendelea kutoa elimu, kukuza weledi kisasa. Utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi huu
kwa sekta mbalimbali na umma unatarajiwa kuanza katika mwaka wa faedha 2007/08.
kuhusu muundo na mwongozo.
26. Kukamilsiha ukarabati wa Jengo la Ukarabati wa jengo umefikia asilimia 95.
Kituo cha Uzalishaji Bora na Hifadhi ya
Mazingira Tanzania (CPCT).
27. Kuanda na kuendesha semina ya Kazi hii haikufanyika kutokana na kukosekana kwa
kitaifa kuhusu mafanikio ya utekelezaji fedha.
wa mbinu ya za ulishaji bora.
28. Kufanya tathmini ya uzalishaji bora na Tathmini ya uzalishaji bora ilifanyika katika viwanda
matumizi ya nishati kwenye viwanda viwili (Karibu Textile Mills (KTM) cha Dar es salaam na
mbalimbali vinavyohitaji huduma hiyo. China Paper Cooperation cha mjini Moshi. Aidha
Mpango wa ustaarifu wa mazingira kwa ajili ya Kiwanda
cha KTM ulitayarishwa na kuridhiwa na Baraza la
Mazingira kwa ajili ya kutekelezwa na KTM.
29. Kuendesha semina na warsha za Semina kuhusu uzalishaji bora kwa wadau mbalimbali
kukuza ufahamu wa dhana ya wa Manispaa ya Tanga ilifanyika na kuhudhuriwa na
uzalisahji bora na matumizi endelevu wenye viwanda na sekta isiyo rasmi. Aidha Semina ya
kwa wadau mbalimbali. kukuza uelewa juu ya dhana ya uzalishaji bora ilifanyika
Dodoma, walengwa wakiwa; Wakurugenzi wa
Manispaa, Waratibu wa programu za Miji endelevu,
Waratibu wa vikundi kazi na Maafisa Mipango Miji katika
Manispaa zote nchini.
30. Kuandaa mkutano wa kimataifa Semina ilifanyika Arusha ikijumuisha washiriki kutoka
kuhusu uzalishaji wa matumizi nchi zaidi ya 30 za mabara ya Afrika, Asia, Marekani,
endelevu, utakaofanyika mwezi Mashariki ya kati, Ulaya na Urusi. Washiriki walikuwa
Desemba 2006 Jijini Arusha. 130 wa ngazi za juu za uongozi Serikalini, Bunge,
Taasisi zisizo za kiserikali, waandishi wa habari na
Asasi za kiraia.
31. Kukuza weledi kwa umma kuhusu Semina ya wadau kuhusu ukanda wa Ozoni ilifanyika
ukanda wa Ozoni na mbinu za kudhibiti siku ya ozoni duniani tarehe 16 Septemba, 2006.
madhara yake kwa kuhusisha vyombo
vya habari kama redio, runinga na
magazeti.
32. Kutoa mafunzo kwa mafundi mchundo Mafundi mchundo 43 kutoka Tanga, Arusha, Zanzibar,
wa majokofu na viyoyozi kuhusu aina Tabora, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza na Dar es
30
ya gesi mbadala zinazoweza kutumika salaam walihudhuria mafunzo.
nchini na njia bora za kuhudumia
viyoyozi na majokofu.
33. Kutoa mafunzo kwa maofisa forodha Mafunzo yamefanyika mwezi Machi, 2007.
kuhusu mbinu za kutambua gesi
zinazoingizwa nchini kwa ajili ya
matumizi ya majokofu na viyoyozi na
udhibiti wa uingizaji wa gesi
zinazoharibu ukanda wa hewa ya
Ozoni.
34. Kukamilisha kanuni za kusimamia Kanuni za kusimamia uingizaji na matumizi ya gesi
uingizaji na matumizi ya gesi zinazoharibu ukanda wa Ozoni zinaendelea
zinazoharibu ukanda wa Ozoni. kuandaliwa.
35. Kuandaa miradi na kutafuta wafadhili Pendekezo la mradi kuhusu “Capacity Building For
kuhusu maeneo ya kipaumbele ya Environmentally Sound Management of Polychlorinated
usimamizi wa kemikali zinazodumu Biphenyls (Pcbs) And Equipment Containing Pcbs”
katika mazingira. limeandaliwa.
36. Kukamilisha taratibu za kuridhia Kikao cha sita cha Bunge Januari /Februari 2007
Mkataba wa kuundwa Kituo cha Afrika kiliridhia Mkataba wa kuundwa kwa Kituo cha Kanda
cha Usimamizi wa Taka za sumu na cha Afrika cha kutolea mafunzo na kusambaza
nyinginezo. teknolojia juu ya usimamizi wa taka za sumu.
37. Kuandaa mkakati wa upatikanaji wa Mkakati wa upatikanaji wa fedha unaendelea
fedha kwa ajili ya shughuli za kuandaliwa ili kuwasilishwa ngazi za juu Serikalini kwa
usimamizi wa taka za sumu. maamuzi.
38. Kuandaa mapendekezo ya miradi na Mapendekezo ya miradi yameandaliwa kuhusu Mpango
kuiwasilisha kwa wahisani. wa Taifa wa Usimamizi wa Kemikali zinazodumu katika
Mazingira.
39. Kuendesha warsha ya mafunzo Kazi hii haikufanyika kutokana na ukosefu wa fedha
kuhusu usimamizi wa taka zenye sumu katika kipindi husika.
kwa maofisa wa Idara na taasisi za
Serikali.
40. Kuendesha semina ya kuhamasisha Kazi hii haikufanyika kutokana na ukosefu wa fedha
viongozi wa juu serikalini kuhusiana na katika kipindi husika.
majukumu yao katika usimamizi wa
taka zenye sumu.
41. Kupiga marufuku uingizaji, uuzaji, Kanuni za kupiga marufuku mifuko ya plastiki
ununuzi na matumizi ya mifuko ya zimetolewa kwenye Gazeti la Serikali (Government
plastiki laini yenye unene chini ya Notice No. 137) la tarehe 6/ 10/ 2006. Aidha, Ofisi
microns 30 (au milimita 0.03) na ile ya iliweza kutoa taarifa kwa vyombo vya habari “Press
kufungia maji ya matunda, ya unene Release” mwezi Septemba, 2006.
wa microns 65 (au milimita 0.065)
ifikapo Oktoba 2006. Katika usimamizi wa utekelezaji wa kanuni hii, Baraza la
Taifa la Hifadhi ya Mazingira limefanya yafuatayo:-
Limetoa Matangazo mbalimbali katika magazeti
31
pamoja na kuendesha vipindi maalum vya
mahojiano katika redio na televisheni vikiwa na nia
ya kuelimisha wananchi juu ya athari za kiafya na
mazingira zinazotokana na taka za plastiki na
sababu zilizosababisha aina ya bidhaa za plastiki
zilizotajwa kupigwa marufuku.
Kuainisha aina zipi za plastiki laini zilizopigwa
marufuku.
Kuchukua hatua za sampuli za mifuko mbali mbali
ya plastiki inayozalishwa hapa nchini na
inayoingizwa toka nje ya nchi na kuipeleka Shirika la
Viwango la Taifa (TBS) ili kubaini unene wake ili
kujua ni ipi inayokidhi matakwa ya sheria na ni ipi
isiyokidhi matakwa hayo na hivyo kupigwa
marufuku.
Umefanyika utafiti katika jiji la Dar es Salaam
kubaini athari za kiuchumi na kijamii zinazotokana
na hatua hiyo ya serikali ya kupiga marufuku bidhaa
ya aina hizi za plastiki, na ripoti yake imewasilishwa
serikalini.
Ukaguzi wa kushitukiza kwa wazalishaji,
wasambazaji na wauzaji wadogo wadogo ulifanywa
katika jiji la Dar es Salaam. Baraza liligundua
kwamba baadhi ya wazalishaji walikuwa bado
wanaendelea na uzalishaji wa mifuko iliyopigwa
marufuku na katika maduka na sehemu za masoko
mifuko hiyo ilikuwa bado ikitumika. Kufuatia hali hiyo
Baraza lilitoa siku saba (7) kusitisha uzalishaji na
matumizi ya mifuko hiyo.
Baraza liliitisha mkutano wa wadau wote uliofanyika
tarehe 10 – 11 Mei, 2007 kujadili hatima ya zoezi hili
na kupata maoni ya wadau.
42. Kuongeza kodi kwa zaidi ya asilimia Serikali imeongeza kodi (Excise Duty) ya asilimia 120
mia moja kwenye mifuko ya plastiki katika mifuko ya aina hii ya plastiki.
aina nyingine ya Rambo yenye
microns 30 (milimita 0.003) na zaidi ili
kuhamasisha uingizaji wa mifuko
mbadala kama vile vikapu vya asili na
mifuko ya nguo na karatasi.
32
43. Kukamilisha utekelezaji wa Mradi wa Mafunzo ya kuimarisha uwezo katika masuala ya kupiga
Kuimarisha Uwezo wa Serikali katika vita kuenea kwa Hali ya Jangwa na Ukame kwenye
Kupambana na Kuenea kwa Hali ya miradi mbalimbali katika ngazi za wilaya yaliendeshwa.
Jangwa na Ukame kwa kuendesha Mafunzo haya yaliwahusisha Maafisa Mipango (W) na
mafunzo kwa wadau mbalimbali kwa Maafisa Maliasili (W) pamoja na vyama visivyokuwa vya
kushirikiana na JET. kiserikali vya JET, EPMS na TANGO. Maafisa Mipango
walipewa pia mafunzo ya ukusanyaji na utunzaji wa
kumbukumbu zinazohusu hali ya kuenea kwa jangwa na
ukame. Wilaya zilizohusika katika mafunzo na kupewa
msaada wa kompyuta ni: Singida, Manyoni, Iramba,
Magu, Kwimba, Misungwi, Kishapu na Meatu. Aidha,
JET wameandaa Mwongozo wa Mtandao wa Wadau
wanaoshughulika na kupiga vita kuenea kwa hali ya
jangwa na ukame.
44. Kusaidia miradi midogo midogo ya Miradi 12 imefadhiliwa chini ya mfuko wa msaada kwa
vikundi vya jamii inayolenga kuhifadhi ajili ya miradi ya Mazingira na Kuondoa Umasikini.
mazingira na kupambana na umaskini Mfuko huu uko chini ya mradi wa kujenga uwezo na
kupitia utekelezaji wa Mikataba ya kupunguza umasikini kupitia utekelezaji wa mikataba ya
Kimataifa ya Mazingira. mazingira (UNCCD, UNFCCC na CBD).
Awali katika awamu ya kwanza miradi 2 ilifadhiliwa na
katika awamu ya pili ya mwisho, miradi 10 imefadhiliwa.
Miradi yote 12 inagharimu jumla ya dola za Kimarekani
150,000.
45. Kufuatilia upatikanaji wa fedha kutoka Tanzania imetengewa jumla ya dola za Marekani milioni
GEF kwa ajili ya kufadhili miradi 12.8 katika kutekeleza miradi mbalimbali ya kuhifadhi
iliyokwisha wasilishwa na mipya Bioanuai kwa kipindi cha miaka minne ijayo (2007 –
itakayoandaliwa. 2010) na US$ 4.8 milioni zimetengwa kwa Tanzania
katika kutekeleza miradi ya Mabadiliko ya Tabianchi kwa
kipindi cha miaka minne ijayo (2007 – 2010).
46. Kuandaa taarifa ya mwaka ya Taarifa ya mwaka ya utekelezaji wa shughuli za “Global
utekelezaji wa shughuli za Mfuko wa Enviromental Fund (GEF)” imeandaliwa.
Mazingira wa Dunia (GEF) nchini.
47. Kuratibu utekezaji wa masuala ya Programu ya kujenga uwezo wa wadau wa mazingira
mazingira katika MKUKUTA pamoja na kutekeleza Sheria ya Mazingira imeandaliwa. Programu
programu ya kujenga uwezo wa wadau hii ni ya miaka 5. Tayari DANIDA wamekubali kufadhili
wa mazingira, na kutekeleza Sheria ya na utekelezaji utaanza 2007/2008.
Usimamizi wa Mazingira.
48. Kuratibu mashindano ya Tuzo za Rais Rasimu ya Mwongozo wa Tuzo ya Rais Kuhifadhi
kuhusu ubora wa Uhifadhi wa Vyanzo vya Maji, Kupanda na Kutunza Miti imendaliwa
Mazingira, Tuzo ya Rais ya Kupanda na iko katika mchakato wa kuwasilishwa ngazi za juu
na Kutunza Miti, na Kuhifadhi Vyanzo Serikalini kwa hatua za maamuzi.
vya Maji.
49. Kuelimisha wananchi umuhimu wa Uelimishaji umeendelea kupitia Mkakati wa Kuhifadhi
Kampeni ya upandaji miti inayokidhi Mazingira ya Ardhi na Vyanzo vya Maji, ambapo kila
33
mahitaji ya wananchi katika maeneo Wilaya inatakiwa ipande na kutunza miti isiyopungua
mbalimbali. milioni moja na laki tano kwa mwaka.
50. Kufuatilia utekelezaji wa Mkakati wa Kazi zifuatazo zimefanyika:-
Kuhifadhi Mazingira ya Ardhi na Kuchapisha na kusambaza vijitabu vya Mkakati;
Vyanzo vya Maji kwenye sekta Kutembelea na kuhamasisha utekelezaji wa Mkakati
mbalimbali. katika sekta na mikoa 9; Kuandaa na kuwasilisha Hati
ya Taarifa ya utekelezaji wa Mkakati kwa ajili ya Baraza
la Mawaziri.
51. Kuboresha Mpango wa Taifa wa Utafiti Baraza limetembelea Wilaya kumi za Tanzania Bara ili
wa Masuala ya Mazingira (National kukusanya maoni ya wadau kuhusu matatizo ya
Environmental Research Agenda) kwa Mazingira. Wilaya hizo ni Ilala na Kinondoni (Dar-es
kupata maoni ya wadau katika ngazi Salaam), Mikindani (Mtwara), Kondoa (Dodoma),
ya wilaya na vijiji kuhusu mikataba ya Sumbawanga vijijini (Rukwa), Uyui (Tabora), Makete
mazingira, ambayo serikali imeridhia (Iringa), Mwanza mjini (Mwanza), Ngara (Kagera) na
na matatizo sugu ya mazingira nchini. Simanjiro (Manyara).
Watafiti wa Baraza kwa kushirikiana na watendaji wa
Wilaya walitembelea vijiji 3 kila Wilaya na kujadili
matatizo yanayohusiana na mazingira na ambayo
yanahitaji kupewa kipaumbele katika utafiti. Taarifa za
ziara hizo pamoja na maoni yaliyopatikana kufuatia
Mkutano na wadau uliofanyika Januari 2007, vilitumika
kuboresha rasimu ya mpango wa utafiti wa mazingira.
Rasimu hiyo iko katika hatua za mwisho za marekebisho
tayari kwa kuchapishwa na kusambazwa kwa wadau
kwa ajili ya utekelezaji.
52. Kufanya utafiti wa kina wa ikolojia Watafiti wa Baraza wametembelea Wilaya ya Mbinga,
katika safu za milima ya Livingstone, ambayo imo katika safu ya Milima ya Livingstone na
mikoa ya Mbeya, Iringa na Ruvuma. kukusanya maoni ya awali. Mbinga iliteuliwa kwa vile
idadi kubwa ya wananchi wake wanafaidika na mfumo
wa kiikolojia wa Milima hiyo. Katika ziara hii Baraza
lilifanya tathmini ya awali (recoinnaisance survey) na
kuzungumza na watendaji wa Wilaya na Vijiji ambavyo
vitahusishwa kwenye tathmini hiyo.
Tathmini kamilifu ilitarajiwa kuanza mwezi Desemba
2006, ila kutokana na fedha kuchelewa kupatikana utafiti
umeanza Juni, 2007 (kipindi cha mvua) na awamu ya
pili itafanyika mwezi Oktoba (kipindi cha kiangazi).
Tathmini hii itatumia mfumo unaojulikana kama
“Millenium Ecosystems Assessment Framework”.
Mfumo huo umejaribiwa kidunia na kupendekezwa
utumike kote duniani kwa kuwa umedhihirisha uhusiano
baina ya binaadamu na mazingira yake.
34
53. Kufanya mapitio ya taarifa 55 za Mapitio ya taarifa 15 za Tathmini ya Athari kwa
Tathmini ya Athari kwa Mazingira na Mazingira na kutoa ushauri wa kuziboresha
kutoa ushauri. yamefanyika. Taarifa 30 zimepokelewa na zinafanyiwa
kazi katika hatua mbalimbali.
54. Kupitia taarifa za ukaguzi wa mazingira Taarifa 5 za Ukaguzi (Environmental Audit Reports)
(Environmental Audit Reports) na zimepitiwa na ushauri wa kuboresha mazingira
kutoa ushauri wa kuboresha mazingira umetolewa. Miradi hiyo ni ile ya IPTL na Placer Dome –
wakati wa utekelezaji wa miradi. North Mara Gold Mine.
55. Kupitia fomu za usajili wa miradi, Fomu za usajili wa awali wa miradi kwa ajili ya TAM
taarifa za awali na hadidu za rejea (Preliminary EIA Registration Forms) za miradi 20
(Registration, Preliminary Impact zimepitiwa. Ripoti za awali za TAM (Scoping Reports)
Assessement Reports and Terms of na Hadidu za Rejea za kufanya TAM (Terms of
Reference) na taarifa za Mipango ya Reference for conducting EIA) za miradi 10 zilipitiwa na
Usimamizi wa Mazingira na maswala kuboreshwa.
ya jamii (Environmental and Social
Management Plans) Taarifa 2 za Mipango ya Usimamizi wa Mazingira na
masuala ya Jamii (Environmental and Social
Management Plans) zilipitiwa na ushauri wa
kuboreshwa kutolewa. Taarifa hizo ni “TANESCO
Emergency Power Project” na “Sumaria Consumer
Products”.
56. Kuandaa kwa kushirikiana na sekta Baraza lilishirikiana na sekta 2 ili kutoa miongozo ya
mbali mbali na Serikali za Mitaa TAM. Sekta za Maji (Wizara ya Maji) na Nishati
Miongozo ya Tathmini ya Athari (TANESCO Emergency Power Projects). Mafunzo ya
kwenye Mazingira (TAM) ya kisekta na Tathmini ya Athari kwenye Mazingira (TAM) yalitolewa
ile ya kutumika wakati wa kufanya kwa watendaji wa Wilaya ya Mbarali mwezi wa
uchambuzi wa maswala ya Novemba 2006.
kuzingatiwa wakati wa kutekeleza
miradi ya jamii.
57. Kuhamasisha Wilaya za Magu, Kazi imeanza kwa hatua mbalimbali kwa fedha za
Musoma, Geita na Bunda kuendelea ufadhili kupitia mradi wa LVEMP. Magu (Simiyu)
kutekeleza mikakati ya kuhifadhi makabrasha yameandaliwa, lakini utekelezaji
maeneo ya ardhi oevu. haujaanza, Musoma (Bwawa la Kitaji), Bunda (Mto
Rubana) na Geita (Mto Mabubi), zote zimekamilisha
maandalizi zinasubiri kupata fedha ili utekelezaji
uendelee.
58. Kuendelea kutekeleza mipango ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira
uwiano ya kuhifadhi maeneo ya pwani kwa kupitia programu yake ya hifadhi na usimamizi
katika wilaya za Kilwa, Lindi, Mtwara kamilifu wa mazingira ya pwani (TCMP), limeweza
na Tanga kuwasaidia wakazi wa pwani katika kuyalinda na
kuyahifadhi maeneo tete ya pwani na kuboresha
shughuli za kiuchumi katika wilaya za Pangani (Tanga),
Bagamoyo, Mkuranga, Mafia na Rufiji (Pwani) na Kilwa
(Lindi).
35
59. Kutoa Tuzo za hifadhi ya mazingira na Maandalizi kwa ajili ya utoaji Tuzo ya Rais kuhusu ubora
ushiriki katika Siku ya Mazingira wa uhifadhi mazingira katika uchimbaji madini
Duniani. yameanza. Ofisi ya Makamu wa Rais imeshiriki katika
maadhimisho ya Siku ya Mazingira kitaifa yaliyofanyika
Singida.
60. Kukamilisha miongozo itakayotumika Maandalizi ya kutengeneza kitini (Manual) yameanza
katika kutambua maeneo tete (special kwa kuendesha warsha ya kitaifa ya wadau ili
or critical sites) na kukusanya taarifa kutambua, kujadili na kuunda miongozo itakayotumika
za awali kwa lengo la kuandaa katika usimamizi wa maeneo tete nchini (special or
viashiria kwa ajili ya uperembaji. critical sites).
61. Kufanya ukaguzi wa miji na viwanda ili Baraza liliendelea kufanya ukaguzi wa viwanda mbali
kudhibiti uchafuzi wa Mazingira. mbali hapa nchini hasa katika jiji la Dar es Salaam
kubaini hali halisi ya uchafuzi wa mazingira unaotokana
na viwanda hivyo na kutoa ushauri wa kitaalam jinsi ya
kuondokana na uchafuzi huo. Pia viwanda kadhaa
katika miji ya Mwanza, Bukoba, Tanga, Morogoro na
Arusha vilikaguliwa na kupewa maagizo ya kufanya ili
kuondosha uchafuzi unaolalamikiwa, kuwaathiri wakazi
wa maeneo ya viwanda.
Aidha, Baraza limeandaa miongozo ya ukaguzi wa
mazingira (Environmental Monitoring Tools) na
mwongozo wa ukaguzi wa maeneo mbalimbali (Site
Specific Inspection Procedures) itakayotumika kama
nyenzo kwa Maafisa Wakaguzi wa Mazingira
(Environmental Inspectors) watakapokuwa wakifanya
kazi zao kote nchini.
Vile vile Baraza limeandaa Mwongozo wa Kitaifa wa
Uchunguzi wa Mazingira (National Investigation Manual
and National Prosecution Procedure) ili kuweza kufanya
ukaguzi inavyostahili na kuwafikisha mahakamani wale
watakaobainika wanavunja vipengele mbalimbali
vilivyomo katika sheria ya usimamizi wa Mazingira ya
mwaka 2004.
Pia Baraza linafanya utafiti wa kutengeneza modeli ya
utekelezaji (Compliance and Enforcement Model)
itakayotumiwa katika kudhibiti utupaji wa maji taka toka
viwandani na wadau wengine wanaozalisha maji taka
kwa wingi hapa nchini. Modeli hii itakapokamilika
itasaidia sana katika kuwafanya wenye viwanda na
wakaguzi wa Mazingira kusisitiza utupaji wa maji taka
katika njia inayofaa na isiyochafua mazingira.
36
62. Kuandaa miongozo ya namna ya Baraza lilitoa elimu kwa umma kupitia Radio na
kuendeleza elimu ya mazingira kwenye Televisheni, vipeperushi na vijarida. Aidha, Baraza
taasisi za elimu na wanahabari kwa limetoa elimu ya mazingira kwa wadau mbalimbali
kuimarisha huduma ya mawasiliano, kupitia maktaba na makala katika vyombo vya habari,
maktaba na tovuti. warsha, mtandao wa tovuti, makongamano na mikutano.
Baraza pia lilishirikiana na Wizara ya Elimu katika
kuandaa vitini vitakavyotumika kuendeleza elimu ya
mazingira kwenye shule za msingi.
63. Kuendesha warsha, semina, Makala mbalimbali zimechapishwa vikiwemo
kushindanisha shule na vikundi vipeperushi 8,000, vijarida 5,000, Kalenda 3,000, Fulana
mbalimbali, kuchapisha makala, 2,000, Kofia 1000 na kuvisambaza kwa wadau
vipeperushi, majarida na kalenda ili mbalimbali. Baraza linaandaa mtandao wa upashanaji
kukuza uelewa juu ya hifadhi ya habari za mazingira (Central Environment Information
mazingira na maendeleo endelevu. Systems).
64. Kujenga uwezo wa kupanua ajira ili Ofisi ya Makamu wa Rais ilipeleka mapendekezo Ofisi
kuweza kukabiliana na majukumu ya ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma ya
utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa kuongeza sehemu za Idara ya Mazingira ili kuweza
Mazingira. kukabiliana na majukumu ya utekelezaji wa Sheria ya
Mazingira. Aidha, ofisi imeandaa ikama, sambamba na
mapendekezo hayo ili kukidhi hoja hiyo.
65. Kukamilisha ujenzi wa jengo la Ofisi ya Ujenzi wa jengo la Ofisi ya Makamu wa Rais Mtaa wa
Makamu wa Rais lililopo Mtaa wa Lithuli Plot No.10, Dar es Salaam unaendelea na
Luthuli Plot No.10 ifikapo September umefikia asilimia 85. Jengo halitakamilika kama
2006 ilivyotarajiwa kutokana na mabadiliko ya gharama
zilizosababishwa na kuanza ujenzi wa jengo lingine la
mbele. Ujenzi unatarajiwa kukamilika 2008.
66. Kuanza ujenzi wa jengo la Makazi ya Hati miliki ya kiwanja imepatikana, Michoro na utafiti wa
Makamu wa Rais huko Tunguu- Udongo tayari umefanyiwa kazi. Ujenzi unatarajiwa
Zanzibar. kuanza katika mwaka wa fedha, 2007/2008.
67. Kuratibu, kusimamia na kushughulikia Jumla ya watumishi 30 wameajiriwa, 25
masuala yote ya watumishi kuhusu wamepandishwa vyeo na 43 wamehudhuria mafunzo.
ajira, maslahi, nidhamu, upandishwaji Aidha vikao 2 vya Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya
vyeo na haki za wafanyakazi. Makamu wa Rais viliandaliwa na kujadili masuala
mbalimbali yahusuyo watumishi na utendaji kazi.
68. Kuendeleza mapambano dhidi ya Warsha tatu za mapambano dhidi ya UKIMWI
ugonjwa hatari wa UKIMWI. zimefanyika katika vipindi tofauti vya mwaka 2006/2007.
69. Kuhakikisha utunzaji mzuri wa Vifaa vyote vya Ofisi vimeorodheshwa katika vitabu vya
rasilimali na nyaraka za Serikali na kumbukumbu na kuwekewa namba. Lengo ni kuvitunza
kuhakikisha malengo yaliyopangwa na na kuvihifadhi kwa mujibu wa kanuni na sheria za nchi.
Ofisi katika vipindi vya mwaka
yanazingatiwa.
70. Kuhakikisha kuwa wafanyakazi wa Ofisi imewawezesha Watumishi 54 kushiriki
Ofisi ya Makamu wa Rais wanakuwa mazoezi/Michezo na ilikuwa kati ya timu zilizoshiriki
na afya bora na ushirikiano mzuri kati mashindano ya Mwezi Septemba, 2006 Tanga.
yao na Wizara nyingine kupitia
37
michezo. Aidha, watumishi wameshiriki kikamilifu katika
mabonanza ya kila mwisho wa mwezi yaliyoandaliwa na
SHIMIWI Taifa.
71. Kushirikiana na Ofisi ya Rais Kitengo Watumishi wamepata mafunzo ya Maadili katika
cha utawala, uratibu wa Utawala Bora, Utumishi wa Umma na pia namna ya kuzuia na kuziba
katika vita dhidi ya rushwa na mianya ya rushwa sehemu za kazi.
kudumisha utawala bora.
38
WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kukamilisha ukarabati wa majengo ya Ukarabati wa majengo ya wodi ya wazazi, Mwaisela na
Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili "Renal Dialysis" umefikia kiwango cha asilimia 95 ya
hususani jengo la wazazi, wodi ya kukamilika. Kazi hiyo ilitarajiwa kukamilishwa mwezi
Mwaisela, upanuzi wa majengo ya Julai, 2007. Ujenzi wa wodi ya watoto utakamilishwa
hospitali za Jiji la Dar es Salaam na katika mwaka wa fedha wa 2007/2008. Aidha, majengo
kuboresha utoaji wa huduma za wenye ya hospitali za Jiji yamekamilika na yalikwisha
matatizo ya figo kutofanya kazi (renal kabidhiwa; ikiwa ni pamoja na kituo cha Afya cha
dialysis) katika hospitali ya Taifa ya Vijibweni – Kigamboni, Wilaya ya Temeke.
Muhimbili.
2. Ukarabati wa wodi 5, chumba cha Ujenzi wa hosteli na ukarabati wa maabara umefikia
upasuaji, chumba cha kumbukumbu za asilimia 70. Ununuzi wa vifaa tiba umefanyika kupitia
tiba, ukamilishaji wa upanuzi wa Bohari ya Madawa (MSD). Aidha ukarabati wa wodi tano
maabara, ujenzi wa Interns Hostel, haujafanyika kutokana na uhaba wa fedha. Fedha
upanuzi wa Idara ya mionzi na uwekaji zilizotengwa zitatumika kukamilisha ujenzi wa "Interns
wa vifaa na vifaa tiba katika hospitali Hostel".
ya Rufaa Mbeya.
3. Kukamilisha upanuzi wa zahanati ya Ujenzi wa majengo mapya ya upanuzi wa zahanati ya
Lupaso kuwa Kituo cha Afya. Lupaso umekamilika. Kazi ya kuunganisha umeme wa
“3 phase” imekamilika na mkandarasi ameagiza vifaa
vya “mortuary”.
4. Kuanzisha kituo cha upasuaji wa moyo Serikali imepeleka timu ya wataalamu wa upasuaji wa
katika hospitali ya Taifa Muhimbili. moyo katika hospitali ya “CARE“ nchini India. Baadhi
ya wataalamu wamekwisharudi kutoka masomoni na
kuna baadhi ya madaktari ambao bado wako India na
Israel. Wanatarajiwa kumaliza mafunzo hayo baada ya
mwaka mmoja. Aidha taratibu za ununuzi wa vifaa
zimekamilika, huduma zinatarajiwa kuanza kutolewa
mwezi Novemba, 2007.
5. Kukarabati majengo yatakayotumika Ukarabati wa majengo ya hosteli za Wataalam wahitimu
kama hosteli ya wataalamu wahitimu (Interns) katika hospitali za St. Gaspar (Itigi) na
(interns) katika hospitali za St. Gaspar Peramiho Songea haukutekelezeka kuchelewa kwa
(Itigi), Peramiho (Songea) na Seliani mkataba wa makubaliano ya ukarabati na upanuzi wa
(Arusha). majengo kati ya Wizara na hospitali husika pamoja na
taratibu za tenda. Hata hivyo, hospitali zimefanikiwa
kufanya ukarabati kwa kutumia fedha zao. Aidha,
mradi wa ukarabati katika hospitali ya Selian – Arusha
ulihamishiwa hospitali ya Mkoa (Mount Meru) na tayari
umekwishakamilika.
39
6. Kujenga kituo cha tiba cha waathirika Ujenzi wa kituo cha tiba cha Waathirika wa madawa ya
wa dawa za kulevya na pombe; ujenzi kulevya umeanza na unaendelea. Ujenzi wa uzio
wa uzio na jengo la mapokezi na pamoja na ukarabati wa mfumo wa umeme
ukarabati wa majengo katika hospitali umekamilika. Kituo kinajengwa kwa kushirikiana na
maalum ya Mirembe na Taasisi ya Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya na pia Wizara ya
Isanga. Afya na Ustawi wa Jamii.
7. Kujenga jiko jipya, wodi ya watoto, Kazi ya kujenga majengo hayo pamoja na uzio imeanza
nyumba 3 za watumishi na uzio wa kufanyika na inaendelea. Lengo ni kukamilika mwaka
hospitali maalum ya Kifua Kikuu ya wa fedha 2006/07 kutegemeana na kupatikana kwa
Kibong‟oto. fedha.
8. Ununuzi na ufungaji wa vifaa na vifaa Vifaa mbali mbali kwa ajili ya hospitali za rufaa na
tiba katika hospitali ya Taifa ya maalum tayari vimenunuliwa.
Muhimbili, Hospitali za rufaa za
Bugando, KCMC na Mbeya pamoja na
hospitali maalum za MOI, “Ocean
Road”, Kibong‟oto na Mirembe.
9. Kuanza matayarisho ya ujenzi wa Gharama za ununuzi na upimaji wa uwanja
hospitali mpya ya Rufaa Mtwara, zimekwishalipwa. Kwa wakati huu hadidu za rejea na
kanda ya Kusini. nyaraka za kumpata mshauri mwelekezi wa kuandaa
mapendekezo (Propasal) zimekamilika. Kazi ya
kutayarisha michoro itaendelea mwaka 2007/2008.
10. Ununuzi wa gari la wagonjwa na Serikali tayari imeagiza gari kwa ajili ya Hospitali ya
uboreshaji wa wodi ya watoto hospitali “Ocean Road”. Aidha, uboreshaji wa wodi ya watoto
ya Saratani “Ocean Road”. “Ocean Road” umeanza kufanyika na unaendelea vizuri.
11. Kukamilisha ujenzi wa maabara ya Hatua ya umaliziaji inaendelea ambapo kwa sasa
Mkemia Mkuu wa Serikali makao mkandarasi anaweka vioo katika jengo hilo. Ujenzi wa
makuu pamoja na ununuzi wa vifaa na Maabara hiyo umekamilika kwa asilimia 90. Ujenzi huu
kemikali kwa ajili ya maabara mpya ya utakamilika mwaka 2007/2008.
Mwanza. Taratibu za ununuzi wa vifaa na kemikali kwa ajili ya
Maabara ya Mwanza zimekamilika na mikataba mitatu
imewekewa saini.
12. Ujenzi wa maabara ya dawa za asili Ujenzi wa maabara ya dawa za Asili Mabibo inaendelea
Mabibo, maabara Tabora, utoaji wa ambapo kwa sasa jengo limefikia hatua ya kuezekwa.
mchango kwa mfuko wa utafiti na Ujenzi wa maabara ya Tabora uko katika hatua za awali.
ukamilishaji wa awamu ya mwisho ya Ukarabati wa majengo ya Kituo cha Gonja umekamilika.
ukarabati wa kituo cha Gonja.
13. Kukamilisha wa ujenzi wa ofisi na Ujenzi wa maabara unaendelea na mkandarasi
upanuzi wa maabara ya Makao Makuu anamalizia kuweka “fittings” katika jengo hilo.
ya Mamlaka ya Chakula na Dawa.
14. Ukarabati wa jengo la Ofisi ya Makao Ukarabati wa Jengo la ofisi za makao makuu ya NHIF
Makuu ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya umefika asilimia 95.
Afya.
15. Ukarabati wa vyuo vya uuguzi 14, chuo Ukarabati wa majengo ya chuo cha Ifakara (COTC)
cha „Vector Control‟ Muheza na ujenzi umekamilika. Ukarabati wa majengo ya vyuo 14 vya
40
wa nyumba za walimu na hosteli ya uuguzi na cha “Vector Control” kule Muheza
wanafunzi katika chuo cha Waganga unaendelea.
Wasaidizi Ifakara.
16. Kujengea uwezo ofisi nane (8) za Serikali imetoa mafunzo kwa waalimu wa waalimu kwa
kanda za mafunzo kwa kununua Kanda zote na wanaendelea kuwafundisha Watendaji
kompyuta, Magari na vifaa vya wa Halmashauri.
kufundishia.
Mafunzo ya uwezeshaji katika kutumia „Tools‟ za
utekelezaji wa mipango ya wizara yamefanyika kwa
wasimamizi wa Kanda na Timu za usimamizi ngazi ya
mkoa katika mikoa yote na sasa yanaelekezwa katika
ngazi ya Wilaya. Magari 7 yameagizwa kwa ajili ya
kuimarisha Kanda, pamoja na magari 3 ambayo tayari
yamewasili kwa ajili ya Makao Makuu.
Uchambuzi wa awali kuhusu „Internet connectivity‟ kati
ya Kanda na Kanda na Kanda na Makao Makuu ya
Wizara umekamilika.
Maafisa Afya wenye sifa ya “Sanitary Engineers” ( BSc -
holders ) wanne (4) na Madaktari 4 wamepangiwa kazi
ili kuimarisha Kanda. Vile vile, Mtaalamu
atakayeziwezesha Kanda kutengeneza Mpango Kitita
(Bussiness Plans) ameteuliwa na ameanza kazi.
17. Kuwajengea nyumba, kuwalipia ada na Maandalizi ya kuwajengea na kuwapa vifaa vya shule
mahitaji mengine watoto yatima na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi katika
wanaoishi katika mazingira magumu Halmashauri 5 yamekamilika na kazi ya ujenzi
waliotambuliwa na jamii. inaendelea vizuri.
18. Kukarabati mahabusi 5 za watoto, Maandalizi ya kutangaza zabuni kwa ajili ya ukarabati
makazi 2 ya wazee, kituo cha ustawi wa shule ya maadilisho Irambo, makazi ya wazee
wa akina mama na watoto Ilonga, Kolandoto na Nunge na mahabusu ya watoto Mtwara
shule ya maadilisho Irambo na ujenzi yamekamilika. Wazabuni tayari wameteuliwa na ujenzi
wa maktaba ya wanafunzi Taasisi ya unaendelea.
Ustawi wa Jamii.
19. Upembuzi yakinifu utafanyika kwa Kamati kwa ajili ya kufanya tathmini iliteuliwa. Kwa
kushirikiana na OWM - TAMISEMI ili kushirikiana na TAMISEMI wizara imefanya mapitio ya
kuainisha vijiji vinavyohitaji vituo vya kazi zilizofanyika ambapo “Geographical information” ya
huduma za afya na kuboresha mfumo NHIF na GIS ya TAMISEMI itatumika kuangalia vijiji
wa utoaji huduma na kuweka visivyo na huduma. Kwa sasa Wizara
vipaumbele kwa ajili ya utekelezaji imekwishawasiliana na wilaya kama hatua ya awali
kutegemea na raslimali zilizopo, kupata idadi ya vituo ukilinganisha na vijiji. Mpango wa
hususan raslimali watu. Maendeleo ya Afya ya Msingi umeandaliwa na tayari
umepitishwa na Serikali.
20. Kuendelea kuelimisha na kuhamasisha Maandalizi ya vipindi na matangazo mapya, na
Halmashauri, vituo vya kutolea kubadilisha yale ya muda mrefu katika TV kuhusu
huduma za afya, na jamii kuhusu haki mabadiliko katika Sekta ya Afya yamefanyika.
41
na wajibu wao katika mabadiliko
yanayoendelea katika sekta ya afya
kwa kutumia vipindi na matangazo
katika redio na televiseni.
21. Kupitia, kutengeneza na kusambaza Maandalizi ya awali ya utengenezaji wa “Advocacy Kit”
vipeperushi, vijitabu, mabango, na (vipeperushi na vijitabu) yamefanyika na kumalizika,
majarida yenye ujumbe wa kuelimisha yanasubiri majaribio (pre-testing) ya matumizi kwa
watoa huduma za afya na jamii kuhusu walengwa ambapo yatafanyika mwaka wa fedha wa
mabadiliko ya sekta ya afya. 2007/2008 kabla ya kuchapishwa na kusambazwa kwa
wadau.
22. Kufanya mapitio ya Sera ya Afya ili Sera ya mwaka 1990 imefanyiwa mapitio. Rasimu ya
kujumuisha mabadiliko yanayoendelea mwisho iliwasilishwa Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri
katika sekta ya afya. tarehe 13/06/2007 Dodoma, ambapo ilijadiliwa na
kupitishwa. Wizara inaendelea kuyafanyia kazi
maelekezo yaliyotolewa na baada ya hapo
itakamilishwa, kuchapishwa na kusambazwa kwa wadau
mbalimbali kwa ajili ya utekelezaji.
23. Kupitia mwongozo wa uchangiaji Mwongozo umepitiwa. Rasimu ya kwanza iliyopitiwa ya
gharama wa huduma za afya mwongozo wa uchangiaji gharama za Huduma za Afya
unaojumuisha misamaha kwa makundi imetolewa. Wizara inaendelea kukamilisha Mwongozo
na magonjwa maalum kwa lengo la huo, ili upelekwe kwa watumiaji baada ya kupitishwa na
kuwaondolea kero wanaostahili serikali.
misamaha hiyo.
24. Kutoa mchango wa Tele kwa Tele kwa Halmashauri zimeendelea kuwasilisha madai yao ya tele
Halmashauri zilizokwisha anzisha kwa tele na wizara imelipa. Halmashauri saba ambazo
Mfuko wa Afya ya Jamii pia ni Geita, Sumbawanga, Kigoma, Rungwe, Iringa, Igunga
kuhamasisha jamii kuhusu Mfuko wa na Kasulu zimewasilisha madai yao ya jumla ya shilingi
Afya ya Jamii na kutoa mafunzo milioni 259. Kazi ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mfuko
yanayohusu utunzaji na matumizi bora wa Afya ya Jamii nchi nzima imefanyika na mafunzo
ya fedha za mfuko kwa kufuata kwa ajili ya kuanzisha Tiba kwa Kadi hadi kufikia 30
miongozo na kushirikiana na mikoa Juni, 2007 yamefanyika katika miji ya Tanga,
kukamilisha uteuzi wa waratibu wa Kigoma/Ujiji, Mtwara/ Mikindani, Singida, Dodoma Mjini,
Mfuko wa Afya ya Jamii kwa Mbeya Mjini, Iringa, Songea Vijijini na Mtwara vijijini.
Halmashauri 24 ili wawe kiungo katika
Mikoa na Halmashauri.
25. Kuziwezesha Halmashauri zote za Miji, Maandalizi ya mafunzo ya kuziwezesha Halmashauri za
Manispaa na Majiji kuanzisha mpango Jiji, Manispaa na Miji kuandaa sheria ya TIKA
wa Tiba kwa Kadi (TIKA). unaendelea. Manispaa za Kigoma/Ujiji, Tabora, Tanga,
Moshi, Mtwara/Mikindani, Dodoma, Singida, na Mbeya
zimehamasishwa na kuweza kuandaa sheria ndogo na
kuidhinishwa na Manispaa ili ziweze kutumika.
26. Kuhakikisha watumishi wastaafu Mfuko uko katika hatua za mwisho za kukamilisha kutoa
wanachama wa Bima ya Afya mafao kwa wastaafu. Tayari serikali imekwishaidhinisha
wanaendelea kupata huduma za mpango huo. Kazi ya kupitia sheria imeanza na
matibabu kwa maisha yao yaliyobakia inaendelea.
42
baada ya utumishi wa umma.
27. Kuongeza wigo wa wanufaika na Bima Muswada wa Sheria uko katika hatua za kuwasilishwa
ya Afya ikiwemo vyombo vya Usalama Bungeni kwa ajili ya marekebisho ya sheria kuwezesha
wa Raia na Magereza. kundi hili lianze kunufaika katika mwaka wa fedha
2007/2008.
28. Kutoa mafunzo ya sensa ya jamii kwa Maandalizi ya kutoa mafunzo ya sensa ya Jamii tayari
wilaya zilizoteuliwa za Hai, Morogoro, yamekwishafanyika. Sensa hiyo imeanza kufanyika
Temeke, Ilala, Igunga na Kigoma kwa katika robo ya nne ya mwaka wa fedha 2006/07 na
ajili ya kutoa mwelekeo wa hali ya itaendelea katika mwaka wa fedha 2007/2008.
takwimu za huduma za jamii na
kufanya ufuatiliaji katika wilaya hizo.
29. Kuchapisha na kusambaza nyezo za Nyezo za kukusanyia takwimu za Mfumo wa Taarifa za
kukusanya takwimu za Jamii na za Uendeshaji Huduma za Afya, (MTUHA) zimesambazwa
Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji nchi nzima na zinatumika katika vituo vyote vya kutolea
Huduma za Afya (MTUHA). huduma za afya.
30. Kuendelea kuboresha Tovuti ya Tovuti imeboreshwa na kuwa ya kisasa zaidi kwa
Wizara (www.moh.go.tz) ili iwe na kutumia “database” kuhifadhi habari mbalimbali. Baadhi
taarifa muhimu zinazohusu sekta ya ya vitu vilivyoongezwa ni majina ya watu waliochaguliwa
afya. kujiunga na vyuo mbali mbali vilivyo chini ya Wizara ya
Afya kwa mwaka wa masomo 2006/07, baadhi ya
nyaraka muhimu za sekta ya afya pia zimeongezwa.
31. Kuwaelimisha wananchi juu ya Kipindupindu:
kukabiliana na magonjwa ya Kwa kupitia Maadhimisho ya Siku ya Choo Duniani
kuambukiza kama vile kipindupindu, ambayo iliazimishwa tarehe 19/11/06 wananchi na
UKIMWI, Kifua Kikuu, Ukoma, na kusisitizwa kuzingatia mambo muhimu ya kufanyika ili
magonjwa mengine ikiwa ni pamoja na kuzuia kipindupindu kupitia Tamko la Waziri wa Afya
tahadhari ya ugonjwa wa mafua makali (17/11/06 na Maonyesho ya barabarani ya aina ya vyoo
ya ndege. – yaliyofanyika jijini Dar es Salaam). Wizara imeshiriki
katika maandalizi na ukamilishaji wa rasimu ya Mkakati
wa Taifa wa Kupambana na Kipindupindu.
Vipeperushi na majarida zaidi ya 40,000
yamesambazwa na kutoa mafunzo yametolewa kwa
watumishi wa afya ya ngazi ya wilaya ili waweze kutoa
taarifa sahihi kuhusu maambukizi na tahadhari dhidi ya
kifua kikuu na ukoma.
Wizara iliandaa tamasha la uzinduzi wa kampeni ya
kuongeza kasi ya kudhibiti magonjwa ya UKIMWI, Kifua
Kikuu na Malaria. Mgeni Rasmi katika tamasha hili
alikuwa Waziri Mkuu, Mhe. Edward Lowassa ambaye
pia alitangaza ugonjwa wa Kifua Kikuu kuwa wa dharura
hapa nchini. Aidha elimu juu ya Kifua Kikuu na Ukoma
ilitolewa kwa wanachi kupitia radio, televisheni na
magazeti.
43
Wizara imeendelea kuandaa na kutoa taarifa kwa ajili ya
kuwaelimisha wananchi juu ya kukabiliana na magonjwa
ya kuambukiza kupitia mifumo mbalimbali ya habari
kama vile magazeti, vipeperushi, mabango na
matangazo ya redio na televisheni.
Imeandaliwa na kukamilishwa filamu ijulikanayo kama
“HALI HALISI” inayoelimisha jamii kuhusu athari za
unyanyapaa kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI (VVU)
na wenye UKIMWI, umuhimu wa kutumia huduma za
ushauri nasaha na upimaji wa VVU na huduma za dawa
za kupunguza Makali ya UKIMWI. Filamu hii ilianza
kurushwa hewani na kituo cha Televisheni ya Taifa
(TVT) kuanzia tarehe 5/11/2006. Aidha, vipindi vingine
vya moja kwa moja vinaendelea kurushwa hewani na
kituo hicho. Vipindi vingine kama hivyo
vinarushwa na kituo cha Radio Tanzania.
32. Mapambano dhidi ya magonjwa Mafunzo yanayohusu njia sahihi za udhibiti wa
yanayoenezwa na wadudu wanaoruka, magonjwa yamefanyika katika Halmashauri zote 30
wasioruka pamoja na wanyama dhurifu zilizokuwa zimepangwa.
kwa kutoa mafunzo yanayohusu njia
sahihi za udhibiti wa magonjwa hayo
katika wilaya 30.
33. Kubadilisha matibabu ya malaria Waganga wa vituo vyote vya huduma vya
kutoka dawa ya safu ya kwanza ya SP serikali,mashirika yasiyo ya serikali na baadhi ya vituo
kwenda dawa ya mseto ya Artemether binafsi vya huduma ya afya, wamepewa mafunzo ya
/Lumefantrine (ALu). dawa hiyo mpya. Aidha, wafamasia wa Mikoa na Wilaya
zote wamepata mafunzo kuhusu menejimenti ya dawa
hii mpya ya (ALU).
Dawa dozi 8,000,000 (zinazotosha matumizi ya miezi 6)
zimenunuliwa na kusambazwa katika bohari zote za
kanda za MSD nchini. Wilaya zinaendelea kuagiza
kutoka katika bohari za kanda na kupeleka katika vituo
vya huduma. Uzinduzi wa dawa hiyo mpya ulifanyika
tarehe 15 Januari, 2007 Wilayani Temeke.
34. Kuanza kutumia teknolojia nyepesi na Teknolojia hii (RDT) ni ghali hivyo itaingizwa kwa
ya haraka ya utambuzi wa vimelea vya awamu katika matumizi ya utambuzi wa vimelea vya
malaria ambayo itatumika kwa malaria. Kwa kuanzia imeanza kutumika katika wilaya 1
uchunguzi wa malaria. yenye uwezekano mkubwa wa kupata milipuko ya
malaria. Wilaya hiyo ni Muleba. Ni matarajio ya serikali
kuwa ifikapo mwaka 2008 itakuwa inatumika katika
wilaya zote 25 zenye uwezekano wa kupata milipuko ya
malaria.
44
35. Kuwapatia Hati Punguzo kwa Hadi tarehe 31/05/2007 kinamama 2,044,160 walikuwa
vyandarua watoto wenye umri chini ya wamepata vyandarua kwa kupitia mpango huu wa hati
mwaka mmoja pale wanapopelekwa punguzo kote nchini. Mafunzo kwa ajili ya Hati Punguzo
kwenye chanjo ya surua. Pia kwa kwa watoto chini ya mwaka 1 yameanza kwa
wajawazito wasio na uwezo wa Wahudumu wa Afya, na mpango huu ulifanyika katika
kununua chandarua watapatiwa hati mikoa 15 hadi Juni, 2007. Mikoa 6 iliyobaki itatekeleza
maalum itakayowawezesha kupata mpango huu mwaka 2007/08 kuanzia Julai, 2007.
vyandarua bila malipo yoyote.
36. Kuanza matumizi ya DDT ndani ya Mawasiliano yanaendelea kati ya Wizara na Baraza la
nyumba kwa ajili ya kudhibiti Malaria. Mazingira nchini kuhusiana na Suala la DDT. Kimsingi
Matumizi hayo yataanza kwa awamu kabla ya DDT kuanza kutumika, utafiti wa kina lazima
kwenye maeneo yenye milipuko. ufanyike kuona kiwango cha madhara na namna ya
kupunguza madhara. Baada ya hatua hiyo, kutakuwepo
na utaratibu wa usajili wa dawa husika, kupanga
maeneo ya utekelezaji na uhamasishaji wa jamii.
37. Kupanua huduma za mpango wa Hadi Juni , 2007 Wilaya 46 zimeanzisha mipango ya
pamoja wa kudhibiti uambukizo wa pamoja ya kupambana na Kifua Kikuu na UKIMWI.
Kifua Kikuu na UKIMWI katika wilaya Wilaya hizo ni Arusha Mjini, Kisarawe, Bagamoyo,
30. Sengerema, Geita, Kinondoni (Mwananyamala), Ilala
(Amana), Ilemela, Nyamagana, Misungwi, Temeke,
Korogwe, Muheza, Jiji la Tanga, Tanga vijijini, Morogoro
Manispaa, Kilosa, Iringa Manispaa, Iringa Vijijini,
Makete, Njombe, Kahama, Mufindi, Shinyanga
Manispaa, Shinyanga Vijijini na Bariadi. Wilaya zote za
mikoa ya Mbeya na Kilimanjaro. Aidha tathmini ya awali
inafanyika ili kupanua huduma za pamoja za Kifua
Kikuu na UKIMWI katika Halmashauri zingine sita.
38. Kuendesha kampeni za kutokomeza Kampeni za kutokomeza ukoma zilifanyika katika mikoa
ukoma katika wilaya za mikoa ya ya Tanga, Mtwara, Tabora na Zanzibar. Maandalizi
Kigoma, Morogoro na Mara ili kufikia yameanza kwa wilaya za Mkoa wa Kigoma.
lengo la kimataifa la kutokomeza
ukoma ifikapo 2007.
39. Kuhakikisha kuwa viungo bandia na Serikali ilitengeneza viatu maalum jozi 3,050 kwa ajili ya
viatu vinatolewa kwa wale wote walemavu wa ukoma na miguu bandia 19 ambavyo kwa
waliopata ulemavu unaotokana na pamoja vilisambazwa mikoa yote Tanzania Bara na
ukoma. Zanzibar kwa kipindi husika. Aidha serikali ililipia
gharama za rufaa kwa walemavu 53 kwenda kupata
matibabu katika hospitali za CCBRT – Dar es Salaam ,
Dodoma, KCMC-Moshi na Mtwara. Wagonjwa hao
walitoka mikoa ya Singida wawili, Dodoma mmoja,
Tanga mmoja na Zanzibar wawili.
40. Kuandaa Mkakati Mpya wa Miaka Kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI
Mitano wa Sekta ya Afya wa Kudhibiti pamoja na Wadau wengine Wizara imeanza kuandaa
UKIMWI. mkakati wake mwingine mpya wa miaka mitano wa
kudhibiti UKIMWI (2008 – 2012). Maandalizi ya mkakati
45
huo mpya yatafanyika katika awamu mbalimbali.
Taratibu za utayarishaji wa hadidu za rejea kwa
Mtaalamu atakayefanya uchambuzi yakinifu katika
awamu ya kwanza ya maandalizi haya zimekwisha
kamilika.
Utayarishaji wa mkakati mpya wa Sekta ya Afya na
Ustawi wa Jamii utaenda sambamba na ule mkakati wa
kitaifa unaoandaliwa na Tume ya Taifa ya Kudhibiti
UKIMWI utakaoanza kutekelezwa katika kipindi cha
miaka mitano ijayo kuanzia 2008 hadi 2012 baada ya
kumalizika kwa kipindi cha mkakati uliopo hivi sasa
(2003 – 2007).
41. Mpango wa Taifa wa kusambaza dawa Serikali imepanga kuendelea kutoa huduma za
za kupunguza makali ya UKIMWI matibabu ya Ugonjwa wa UKIMWI kwa kutumia dawa za
utapanuliwa ili huduma hii ipatikane kupunguza makali ya UKIMWI (ARVs) kutoka hospitali
katika baadhi ya vituo vya afya na zilizoko katika ngazi ya wilaya na kupeleka huduma hizo
zahanati katika kila wilaya hapa nchini katika ngazi ya vituo vya Afya na zahanati ili kupeleka
na kuwapatia Watanzania 150,000 huduma hizi karibu zaidi kwa wananchi.
dawa za kupunguza makali ya
UKIMWI. Huduma za kudhibiti UKIMWI Katika mkakati huu, kila wilaya imepewa jukumu la
zitaendelea kutolewa na kufikishwa kuchagua vituo vya Afya vitatu hadi vitano ambavyo
karibu zaidi na wananchi. vitatoa huduma za kutoa dawa za kupunguza makali ya
UKIMWI.
Watoa huduma, na watendaji wa vituo vya Afya
watapatiwa mafunzo kabla ya kuanza kutoa huduma
hizi. Utekelezaji wa mpango huu unatarajiwa kuanza
mwaka 2007/08.
42. Wilaya 32 zitagawiwa dawa ya Wilaya 32 zimegawiwa dawa za Zithromax katika
Zithromax kwa ajili ya vikope katika mwaka 2006/2007.
mzunguko wa mwaka huu wa
2006/2007 ambapo jumla ya wananchi
8,800,000 wanatarajiwa kupata dawa
hiyo.
43. Kugawa dawa ya Mectizan kudhibiti Dawa hiyo imesambazwa katika wilaya za Songea,
ugonjwa wa usubi katika vijiji 695 Mbinga, Tunduru, Ludewa, Rungwe, Kyela, Muheza,
vilivyoko katika wilaya 14, ambazo ni Korogwe na Mvomero. Wilaya hizi zinajiandaa kwa
Ulanga, Kilombero, Kilosa, Morogoro, ugawaji wa dawa hiyo kwa wananchi. Wilaya za
Mvomero, Songea, Mbinga, Tunduru, Lushoto, Muheza na Korogwe wameanza kugawa dawa
Ludewa, Rungwe, Kyela, Muheza, hizo ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa mpango wa
Korogwe na Lushoto. Jumla ya mabusha na matende. Dawa kwa wilaya za Kilosa na
wananchi 1,400,000 watapewa dawa Kilombero nazo tayari zimeshaanza kusambazwa.
hiyo.
46
44. Kuandaa mitaala na kutoa mafunzo Mafunzo kwa watoa huduma kuhusu uzazi wa mpango
kwa watoa huduma kuhusu uzazi wa yalifanyika katika mikoa ya Mbeya, Shinyanga, Dar es
mpango katika mikoa ya Mbeya, Salaam na Mwanza.
Shinyanga, Dar es Salaam na
Mwanza.
45. Dawa mbalimbali za uzazi wa mpango Dawa za Uzazi wa mpango zilizonunuliwa kwa kipindi
zitasambazwa katika vituo vyote vya cha fedha 2006/07 zilisambazwa katika vituo vya
kutolea huduma. kutolea huduma ambazo ni Vidonge vya uzazi wa
mpango(Oral Contraceptives), Vipandikizi (Implants),
Kitanzi ( Copper T380), Sindano (Injectables) na mipira
ya kike na kiume (condoms).
46. Kutekeleza mkakati wa IMCI ili Mafunzo rejea ya IMCI yenye kuboresha utendaji wa
kupunguza vifo vya watoto wenye umri watoa huduma za afya kwa wafanyakazi wa wodi za
chini ya miaka mitano. watoto yamefanyika. Pia mafunzo ya namna ya
kuboresha huduma kwa watoto wagonjwa waliozidiwa
au kupewa rufaa kwa kamati za uendeshaji wa huduma
za afya katika ngazi ya Mkoa na Wilaya yalifanyika.
47. Kuendelea kutoa huduma za chanjo Huduma za mpango wa chanjo zimeendelea kutolewa
nchini na kuhakikisha viwango vya juu kwa nchi nzima kama ilivyopangwa. Aidha viwango vya
vya chanjo vilivyofikiwa vinakuwa chanjo kwa nchi nzima kwa kiashiria (indicator) DPT-
endelevu. HB3 imeendelea kuwa zaidi ya asilimia 90 na kwa
chanjo ya surua asilimia 91.
48. Kuendelea na juhudi za kutokomeza Ufuatiliaji wa magonjwa ya polio, surua na pepopunda
ugonjwa wa polio, kudhibiti surua na kwa watoto wachanga umeendelea kufanyika kwa nchi
kufuta ugonjwa wa pepopunda. nzima. Kampeni ya chanjo ya surua ilifanyika Septemba
Upembuzi yakinifu wa matumizi ya 22 - 24 kwa mkoa wa Dar es salaam ikiwa ni mojawapo
chanjo ambazo hazijaanzishwa kwa ya mkakati wa kudhibiti ugonjwa wa surua. Aidha
magonjwa mengine yanayozuilika kwa upembuzi yakinifu kwa matumizi ya chanjo ambazo
chanjo utafanyika. hazijaanzishwa unaendelea kufanyika katika “sentinel
sites” za hospitali ya Muhimbili na Hospitali teule ya
Muheza.
49. Kufanya uhamasishaji kuhusu utoaji Kazi ya uhamasishaji kuhusu utoaji wa chakula cha
wa chakula cha mchana shuleni, mchana shuleni, huduma ya kwanza na usafi wa
huduma ya kwanza na usafi wa mazingira na afya mashuleni umefanyika.
mazingira na kufuatilia shughuli za
afya mashuleni.
50. Kuendeleza mashindano ya afya na Mashindano ya afya na usafi wa mazingira umefanyika
usafi wa mazingira nchini kwa kwa kushirikisha majiji matatu, manispaa 17, miji minne,
kushirikiana na Halmashauri zote na halmashauri za wilaya 20 nchini. Utekelezaji wa
nchini. Mashindano haya yatafanyika mashindano haya ulianzia ngazi ya kijiji,mtaa, kata, na
katika ngazi za kata na vijiji na hatimaye ngazi ya Halmashauri ya Wilaya. Baadhi ya
yatachochea uwekaji mazingira katika Halmashauri zimekwisha tenga maeneo maalumu kwa
hali ya usafi na kudhibiti kuzagaa kwa ajili ya utupaji sahihi wa taka. Serikali imepiga marufuku
taka ikiwemo mifuko ya plastiki katika matumizi ya mifuko ya plastiki laini kuanzia tarehe
maeneo yao. Pia, itazishauri 1/10/06.
47
Halmashauri kutenga maeneo ya Wizara inashiriki katika utayarishaji wa Mkakati wa
kutupia, taka na kuzifukia kitaalamu. Kitaifa wa Udhibiti wa Taka ambao unazungumzia
masuala ya Utupaji wa Taka. “Concept Paper”
imeandikwa kwa kushirikiana na Mradi wa “Sustainable
Cities Program (SCP)” na Kitengo cha “Urban
Authorities Support Unit” (UASU) katika Ofisi ya Waziri
Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
51. Kutoa vitendea kazi na kuwapa Watumishi wawili wanapatiwa mafunzo ngazi ya Uzamili
mafunzo ya uzamili katika fani ya nchini Uholanzi na katika Chuo kikuu cha Tumaini, hapa
udhibiti wa uchafuzi wa mazingira, pia nchini. Utekelezaji wa Sheria ya Mazingira unafanyika
utekelezaji wa sheria ya mazingira kupitia mashindano ya Usafi wa Mazingira.
pamoja na maagizo ya Serikali ya
kudhibiti uharibifu na uchafuzi wa
mazingira.
52. Mafunzo kwa watumishi wa afya Mafunzo, yamefanyika kwa watumishi bandarini
Bandarini kuhusu sheria na mbinu kuhusiana na sheria za afya za kimataifa pamoja na
mbalimbali za udhibiti wa magonjwa mbinu mbalimbali za udhibiti wa magonjwa
ya kuambukiza ya kitaifa na kimataifa yanayotolewa taarifa kimataifa.
yatatolewa na gari moja kwa kituo cha
KIA na pipikipi 3 kwa vituo vya Gari moja kwa kituo cha KIA limeagizwa ikiwa ni pamoja
Tunduma, Kabanga na Holili na pikipiki 3 kwa ajili ya vituo vya Tunduma na Kabanga.
zitanunuliwa.
53. Mwongozo wa kufundisha juu ya Mwongozo umeandaliwa na kusainiwa na Waziri wa
UKIMWI katika maeneo mbalimbali ya Afya na Ustawi wa Jamii. Mafunzo kwa wafanyakazi wa
kazi utaandaliwa na mafunzo ya afya Afya juu ya UKIMWI na athari zitokanazo na kazi
kazini kwa wafanyakazi yatatolewa ili yametolewa katika mwaka huu 2006/07.
kujenga uwezo wa kutambua athari
zinazotokana na matumizi ya
kiteknolojia.
54. Kuendelea kuelimisha na kuhamasisha Wizara inaendelea kutumia vyombo vya habari kama
jamii kwa kushirikiana na vyombo vya vile radio na televisheni na vikundi vya sanaa
habari na kuimarisha matumizi ya kuelimisha na kuhamasisha jamii kuhusu masuala
sanaa kwa maendeleo ya afya, ili mbalimbali ya afya kama vile udhibiti wa magonjwa ya
kufikisha ujumbe wa afya kwa Malaria, UKIMWI, Kifua Kikuu, nk. Aidha, wakati wa
wananchi wengi, hususan wale maadhimisho na matamasha, vikundi vya sanaa
wanaoishi vijijini. vinatumika kufikisha ujumbe uliokusudiwa. Wizara
inaandaa mwongozo wa mafunzo maalum ya afya kwa
vikundi vya sanaa kuviwezesha kutoa ujumbe wa afya
ulio sahihi kwa umma.
55. Kuanzisha maabara ndogo sita Maabara hizo zimeshakamilika na zinafanya kazi. Vifaa
zitakazochunguza viwango vya madini zikiwemo mashine za kupimia ziitwazo „WYD‟ „Iodine
joto yanayowekwa kwenye chumvi Checker‟ na kemikali za kupimia viwango vya madini
katika wilaya za Tanga, Bagamoyo, joto katika chumvi, viliagizwa kupitia UNICEF na baadhi
Kinondoni, Kilwa, Lindi na Mtwara. ya mashine na kemikali zimekwishafika nchini. Vifaa
vyote vimepokelewa na maabara zimeshaanza kazi.
48
Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC) kwa kushirikiana
na Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi (TFDA),
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Chama Cha
Wazalishaji Chumvi Tanzania (TASPA) imetoa mafunzo
kwa wataalam 12 (wawili kila eneo) toka maeneo
yatakayoanzishwa maabara hizo za Tanga, Bagamoyo,
Kinondoni, Kilwa, Lindi na Mtwara. Aidha Chama Cha
Wazalisha Chumvi katika maeneo husika kimetayarisha
vyumba ambavyo vitatumika kama maabara ndogo
ambako mashine hizo zitafungwa. Kila eneo
limeshapata chumba cha maabara na ukarabati wake
umekamilika.
56. Kuendeleza juhudi zake katika Taasisi ilitoa mafunzo ya lishe na UKIMWI kwa watoa
kuwajengea uwezo watendaji ngazi ya huduma majumbani katika Halmashauri za Moshi (M),
wilaya ili watoe huduma na matunzo Muheza na Iringa (M). Pia kila Halmashauri iliandaa
bora ya lishe kwa watu wanaoishi na mpango endelevu. Mafunzo kwa watoa huduma kwa
VVU na wenye UKIMWI. wagonjwa wa UKIMWI majumbani yameendelea
kutolewa kuanzia ngazi ya wilaya hadi kwenye jamii ili
waweze kutoa huduma, matunzo na kuelimisha watu
wanaoishi na virusi vya UKIMWI na wenye UKIMWI,
familia na jamii yote kwa ujumla kuhusu lishe bora.
57. Kufanya utafiti wa dawa ya mmea wa Utafiti wa mmea huu ulisimama kwa muda kutokana na
TMS-2001 unaoweza kutumika kutibu tatizo la ufadhili. Aidha kwa hivi sasa fedha za utafiti
malaria na kufanya utafiti wa mimea ya huu kiasi cha Tsh 15,000,000/= zimetolewa na serikali
Abrus precatorius, Aloe sp, 5M, na na hivyo hatua za mwisho za utafiti huu kwa kutumia
Muyamba inayotibu magonjwa wanyama (panya) zinaendelea.
mbalimbali.
Aloe vera
Matokeo ya utafiti wa awali yameonyesha kuwa Aloe
vera ina uwezo mkubwa wa kuzuia kukua kwa vimelea
aina ya staphylococcus aureus na shigella flexineri
vinavyosababisha kuoza kwa meno. Hata hivyo utafiti
zaidi na wa kina utafanyika ili kupata viini vya dawa hiyo
vinavyosaidia kutibu matatizo hayo ya meno.
Mmea wa 5M
Mmea 5M umeonyesha kuwa na uwezo wa kupambana
na kuzuia kukua kwa bacteria aina ya Escherichia coli,
Bacilus anthracis, Shigella flexineri na Staphylococcus
aureus wanaosababisha magonjwa katika njia ya tumbo
la chakula (magonjwa kama vidonda vya tumbo). Aidha
utafiti wa kina utafanyika ili kuona kama mmea huo
unaweza kufaa kwa tiba ya magonjwa ya tumbo
yaletwayo na bacteria wa aina hizo tatu.
49
Abras Precatorius
Utafiti wa Abras Precatorius umeonyesha kuwa na
uwezo wa kutibu magonjwa ya tumbo pamoja na
matatizo ya kichefuchefu na kutapika
yanayosababishwa na bacteria aina ya Shigella flexineri.
Utafiti zaidi utaendelezwa ili kupata majibu sahihi.
Muyamba
Utafiti wa mmea huu umeonyesha kuwa dawa ya
Muyamba ina uwezo wa kutibu baadhi ya magonjwa
yanayosababishwa na bacteria na fangasi katika
sehemu za mdomoni, tumboni na sehemu za njia ya
haja kubwa. Majaribio ya maabara yameonyesha kuwa
dozi ya 5-10mg/disc inaweza kuzuia kukua kwa vimelea
hivyo kwa asilimia kati ya 40-70. Matarajio ni kuendelea
na utafiti ili kufahamu zaidi viini vinavyofanya kazi ya
kutibu na kutafuta kujua usalama wa dawa yenyewe.
58. Kufanya utafiti wa awali wa kuzuia Mpango wa udhibiti wa viluwiluwi wa mbu waambukizao
mazalio ya mbu kwa kutumia dawa ya magonjwa ya malaria, matende na mabusha ulifanyika
kuua viluwiluwi inayojulikana kwa jina katika wilaya mbili za Bagamoyo na Mvomero. Mpango
la GRISELESF katika wilaya tatu za huu ulifanyika kwa ushirikiano na Serikali ya Cuba ili
Mvomero, Bagamoyo, na Mafia kufanya majaribio ya dawa aina mbili za Griselesf™ na
Bactivec™ katika mazingira ya Tanzania. Nia ya serikali
ni kutathmini dawa hizi ili kuzitumia katika meneo
mengineyo ya nchi baada ya kuridhika na ufanisi wake.
Tathmini iliyofanyika baada ya kuanza majaribio
imeonesha kwamba dawa hizi zinao uwezo mkubwa wa
kudhibiti mbu kwa kupunguza idadi ya viluwiluwi katika
mazalio kwa kiwango cha asilimia kati ya 60 na 80 kwa
kipindi cha miezi miwili. Aidha dawa hizi zimeonesha
uwezo mdogo wa kudhibiti mbu katika mashamba ya
mpunga hususan yale yaliyoko wilaya ya Mvomero.
Uwekaji wa dawa ukifuatiwa na kutathmini utaendelea
kwa kipindi cha miezi sita kuanzia kipindi cha mvua za
vuli hadi Juni 30 ili kupata takwimu za kutosha
kukamilisha zoezi la kutathmini uwezo wa dawa hizo.
59. Kuendelea kutoa usimamizi wa Serikali iliendelea kutoa usimamizi wa kitaalamu kwa
kitaalamu kwa Halmashauri juu ya Halmashauri juu ya uendeshaji wa huduma za afya
uendeshaji wa huduma za afya katika katika ngazi ya wilaya ili kuboresha huduma. Pia
ngazi ya wilaya ili kuboresha huduma. ilifanya mapitio ya mwongozo wa utekelezaji wa
Mipango Kabambe ya Afya ya Halmashauri. Aidha
serikali ilianzisha mfumo wa „Indent‟ ili kuwezesha
zahanati na vituo vya afya kuagiza dawa na vifaa
muhimu kulingana na mahitaji na mgao wa fedha badala
50
ya mfumo wa makasha (drug kits). Hivi sasa, mfumo
huo unatumika katika mikoa 16 nchini.
60. Kupeleka magari mapya 10 na boti 1 Taratibu za ununuzi wa magari mapya 10 na boti 1
kwenye Halmashauri kwa ajili ya kazi zinakamilishwa, ili kuzipeleka kwenye Halmashauri kwa
za ufuatiliaji na usambazaji wa dawa ajili ya kazi za ufuatiliaji na usambazaji wa dawa na vifaa
na vifaa muhimu vya afya. muhimu vya afya.
61. Kuendelea kutoa mafunzo ya Serikali ilikamilisha uzinduzi wa Bodi za huduma za afya
uhamasishaji kwa Halmashauri mpya katika halmashauri 52 kati ya Halmashauri 113 zilizobaki
zilizoundwa ili ziunde Bodi na baada ya Hati Rasmi (Instrument) kutangazwa katika
kuanzisha Mfuko wa Afya ya Jamii. Gazeti la Serikali. Uzinduzi wa Bodi hizo ulienda
sambamba na uanzishwaji wa Mifuko ya Afya ya Jamii.
62. Ununuzi wa dawa, vifaa na vifaa tiba. Bohari Kuu ya Madawa (MSD) wananunua na
kusambaza dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi kwa
ajili ya zahanati, Vituo vya Afya na hospitali za umma.
Zahanati na vituo vya Afya katika mikoa ya Mbeya,
Rukwa, Kigoma, Tabora, Singida, Lindi, Pwani, Tanga
na Dar es Salaam vinapata makasha ya dawa kila
mwezi. Zahanati na vituo vya afya katika mikoa ya
Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Mwanza, Mara, Kagera,
Shinyanga, Dodoma, Iringa, Morogoro, Ruvuma na
Mtwara pamoja na hospitali zote zinawekewa fedha
MSD kuziwezesha kuagiza dawa na vifaa kulingana na
mahitaji.
63. Kuendelea na ujenzi wa vituo vya Kazi ya ujenzi wa vituo ilishaanza na inaendelea vizuri.
Damu salama kwa Kanda za Kusini - Vituo vya Damu Salama Kanda ya Magharibi Tabora na
Mtwara, Magharibi – Tabora na Kati – Kanda ya Kusini Mtwara ujenzi wake umekamilika. Vituo
Dodoma. Katika Kanda ya Kati hivi vimeanza kufanya kazi mwezi Januari, 2007.
kitajengwa chuo cha mafunzo juu ya
taaluma ya Damu Salama. Ujenzi wa Kituo cha Damu Salama Kanda ya Kati
Dodoma uko katika hatua za mwanzo na utaanza
kutekelezwa 2007/2008. Aidha upo mpango wa kujenga
uwezo wa kuhifadhi damu kwenye majokofu yanayokidhi
ubora kwenye mikoa yote.
64. Kufunga vifaa vya huduma za kinywa Taratibu za uagizaji wa vifaa hivyo kupitia MSD
katika kliniki za meno nchini, ununuzi zimekamilika. Fedha za ununuzi wa vifaa hivyo
wa mashine za X-ray kwa ajili ya kliniki zilishapelekwa MSD, mzabuni alishateuliwa, ununuzi
za meno za Hospitali za Mikoa ya umefanyika, kinachosubiriwa ni kuwasili kwa vifaa hivyo
Mtwara, Lindi, Ruvuma, Rukwa, viwili.
Kigoma, na Mara.
65. Kuendeleza huduma za afya ya akili na Serikali imeandaa mpango wa kufanya utafiti juu ya
kwa walioathirika na dawa za kulevya matatizo ya akili pamoja na utumiaji wa madawa ya
ngazi ya msingi katika wilaya 20 za kulevya. Aidha, mikoa mitatu (3) ya Dar es salaam,
mikoa ya Mara, Shinyanga, Lindi, Dodoma na Kilimanjaro ilifanya uchambuzi yakinifu
Morogoro na Dodoma, pia kitafanya kuhusu matumizi ya pombe katika jamii. Vile vile
utafiti ili kujua hali halisi ya afya ya akili mafunzo ya namna ya kubainisha na kutoa tiba kwa
51
nchini. wagonjwa wa akili ngazi ya msingi yalitolewa kwa
watumishi katika Mikoa ya Morogoro, Shinyanga, na
Dar es Salaam.
66. Kuhamasisha Halmashauri za Wilaya Mwongozo wa kutoa ruzuku umerekebishwa na
na wamiliki wa vituo vya huduma za kupelekwa kwa wadau ili watoe maoni yao.
afya vya mashirika ya dini kuingia
makubaliano ya kutoa huduma mahali
ambapo Serikali haina kituo lakini kuna
kituo cha Shirika la dini na kupitia
mwongozo wa kutoa ruzuku kwa ajili
ya mishahara ya watumishi wa
mashirika hayo.
67. Kuendelea kusimamia huduma za Tiba Kuundwa kwa baraza la tiba asili na tiba mbadala
Asili na Tiba Mbadala kwa manufaa ya kumeweka chombo ambacho kitatumia sheria na
wananchi pia kukamilisha na miongozo ya wizara kusimamia huduma za tiba asili na
kusambaza mwongozo kwa ajili ya tiba mbadala kama ilivyo “Medical Association of
utekelezaji wa Sheria Na. 23 ya Tanzania” (MAT). Jukumu la serikali ni kuhakikisha
mwaka 2002 inayosimamia Tiba Asili kuwa wananchi wanapata huduma iliyo bora na salama
na Tiba Mbadala, pamoja na kwa afya zao, hivyo wizara ina jukumu la kuhakikisha
kukamilisha tafsiri ya sheria hiyo kuwa waganga wa tiba asili wanafuata maadili, (ethical
kutoka lugha ya Kiingereza kuwa code of conduct). Rasimu iliyofanyiwa tafsiri
katika Kiswahili. imeandaliwa na inasubiri marekebisho mengine madogo
madogo yanayojitokeza katika tafsiri ya lugha.
68. Kuendelea kuzijengea uwezo Hospitali Wataalamu 27 wako mafunzoni nchini India na Israel
za rufaa ili ziweze kutoa huduma kwa ajili ya kuanzishwa kwa huduma za upasuaji wa
zinazopatikana nje ya nchi pia moyo. Aidha chumba cha upasuliaji na cha wagonjwa
kuendelea kufanya maandalizi ili mahututi cha hospitali ya MOI kinaendelea
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ianze kutayarishwa, kitanda cha upasuaji na taa viko tayari.
kutoa huduma za upasuaji wa moyo,
pamoja na ununuzi wa vifaa na vifaa
tiba vinavyotakiwa pia kutoa mafunzo
na ujenzi wa sehemu ya kutolea
huduma.
69. Kuanzisha huduma ya kusafisha damu Suala hili linaenda sambamba na mkakati wa serikali
kwa wagonjwa ambao figo zao katika kuboresha huduma za matibabu ya wagonjwa
hazifanyi kazi na huduma za matibabu yanayohitaji matibabu ya nje. Mpango wa seriklali ni
ya macho kwa kutumia Laser. kuziwezesha hospitali zote za rufaa kutoa huduma hii.
Kwa sasa huduma hii ipo Hospitali ya Taifa Muhimbili na
Hospitali ya Rufaa Mbeya. Mipango ya kuziwezesha
hospitali za rufaa Bugando na KCMC kutoa huduma hii,
inaandaliwa. Katika kuhakikisha huduma hii inatolewa
vizuri, wataalamu kadhaa wamepelekwa nchi za nje
kupata mafunzo.
70. Kuweka mtandao wa kompyuta katika Huduma za tiba na ushauri kwa mawasiliano
utoaji wa huduma na huduma za tiba (Telemedicine) zimekwishaanza katika hospitali ya
52
na ushauri kwa mawasiliano Bugando kwa kushirikiana na Hospitali ya Breschia
“Telemedicine”, idara ya magonjwa ya University (kwa upande wa Pathology) na Serikali kwa
Saratani na kununua mashine ya kushirikiana na shirika la AMREF inaanzisha huduma
kuchomea taka na ya kufulia nguo. hizo katika hospitali za Rubya mkoani Kagera na
Kibondo mkoani, Kigoma.
Katika Hospitali ya Kibong‟oto tanuru ya kuchomea taka
(Incinerator) imeshajengwa na inafanya kazi, Mashine
mbili za kufulia nguo zimeshanunuliwa zitaanza kazi
mara baada ya kufungwa; wakati shirika la „Axios
International‟ la Marekani lilitoa msaada wa mashine
moja ambayo imeshafungwa na inafanya kazi sasa.
71. Hospital ya KCMC kwa kushirikiana na Ujenzi umefikia 90%, kazi zinazoendelea ni “fittings”,
“Elizabeth Glaizer Foundation” itajenga yaani “Electrical works”, “water” na “painting” pamoja na
kituo cha kuimarisha huduma za afya “fixtures” (madirisha, vioo, n.k.) Kazi ya ujenzi
kwa watoto na kukamilisha upanuzi wa itakamilika Agosti, 2007 na kituo kitafunguliwa rasmi
jengo la vyumba vya upasuaji kwa wakati huo, ili kuanza kufanya kazi na kutoa huduma
wagonjwa wa macho na upanuzi wa kwa wananchi.
idara ya magonjwa ya njia za mkojo na
figo. Pia kuendelea kutoa huduma za
upasuaji wa moyo.
72. Kuendelea kutoa huduma za kusafisha Vifaa ambavyo ni mashine 10, vimetolewa na Serikali
damu kwa wagonjwa ambao figo zao ya Uholanzi kwa ajili ya hospitali ya Muhimbili. Kwa sasa
hazifanyi kazi na kuendeleza utafiti wa ukarabati wa chumba unaendelea. Hospitali ya Rufaa
ugonjwa wa UKIMWI ikiwa ni pamoja Mbeya, tayari imekwishaanza kutoa huduma hiyo ya
na majaribio ya chanjo yake. kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo. Utafiti wa
UKIMWI unaendelea kufanyika na kuna wagonjwa 2,600
Muhimbili. Lengo ni kutathmini athari ya dawa
zinazotolewa kwa wagonjwa. Kuhusu chanjo Shirika la
Afya Muhimbili linaendelea kujiandaa na liko katika
hatua za mwisho za utafiti.
73. Kuanza kutoa huduma za matibabu ya Huduma za matibabu na kuweka viungo bandia vya goti
kuweka viungo bandia vya goti na ziliaanza kutolewa mwezi Februari, 2007. Kiwanja cha
kuanzisha kituo cha kuwafanyia kujenga kituo cha kufanyia mazoezi wagonjwa
mazoezi wagonjwa waliopooza (Spinal waliopooza kimenunuliwa. Fedha za kujenga kituo
Rehabilitation Centre). hicho zimetengwa katika bajeti ya 2007/2008.
74. Kuanzisha kituo cha Mafunzo ya Mafunzo yamepangwa kufanyika katika Taasisi ya
habari na mawasiliano , ambacho Saratani ya “Ocean Road Cancer Institute (ORCI)”.
kitatoa mafunzo kwa wataalam Majengo yote na vifaa vinavyohitajika kwa ajili ya
wanaotoa huduma kwa kutumia mionzi uanzishwaji wa mafunzo hayo ya kutumia mionzi na
na wauguzi wa wagonjwa wa saratani. wauguzi wa saratani tayari yamekamilika. Mtaala wa
mafunzo hayo kwa hivi sasa uko katika hatua za mwisho
ili uweze kuidhinishwa kwa matumizi na Baraza la
Seneti la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mafunzo hayo yanategemewa kuanza katika mwaka
53
ujao wa masomo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mafunzo haya yatakuwa katika ngazi ya Stashahada ya
Juu na kuendelea.
75. Kuendelea kutoa huduma kwa Hospitali ya Kibongo‟oto imehudumia jumla ya
wagonjwa wa Kifua Kikuu kutoka kote wagonjwa wa vimelea 11 na kati yao 4 walikufa na 7
nchini na uchunguzi wa vimelea sugu walirudishwa makwao baada ya kukaa hospitali kwa
(Multi Drug Resistant – MDR). muda mrefu.
76. Kuendelea kutoa huduma kwa Kama sehemu ya kuadhimisha siku ya afya ya akili
wagonjwa wa akili na wale duniani waratibu wa Afya ya Akili mikoani na wilayani
walioathirika na dawa za kulevya pia wamehusisha shule na vyuo katika maeneo yao kutoa
elimu mashuleni na vyuo vya juu elimu ya kinga dhidi ya magonjwa ya akili na dawa za
kuhusu athari na jinsi ya kupambana kulevya. Elimu iliyotolewa ilihusu uhusiano wa
na dawa za kulevya zitatolewa. magonjwa ya akili na dawa za kulevya na matukio ya
kujiua.
77. Kuendelea kuziimarisha hospitali zote Serikali kupitia Bohari Kuu ya Madawa imekuwa
kwa kuzipatia wataalam, dawa, vifaa, ikinunua dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi pamoja
vifaa tiba na vitendanishi ili kuzipa na kuzipatia wataalamu hospitali zote za Serikali
uwezo wa kutoa huduma zinazostahili. kulingana na rasilimali zilizopo. Vituo vya kutolea
huduma za afya nchini vimepatiwa mgao wa dawa, vifaa
tiba na vitendanishi kwa wakati.
78. Kukamilisha mapitio na marekebisho Rasimu imeshawasilishwa ofisi ya Rais, Menejimenti ya
ya Miundo ya Utumishi ya Kada za Utumishi wa Umma. Aidha Menejimenti ya Utumishi wa
Afya na Ustawi wa Jamii, sanjari na Umma wameainisha sehemu za kufanyia
kuboresha mipango ya kazi kwa kada marekekebisho na Wizara inaendelea kufanya
mbalimbali za watumishi katika marekebisho hayo.
kuboresha maslahi na utendaji wao.
79. Kuajiri jumla ya watumishi 153 wa Serikali iliwapangia vituo vya Kazi, Madaktari 34,
kada mbalimbali ili kupunguza tatizo la Maafisa Tabibu 526, Maafisa Wauguzi 11, Maafisa Afya
upungufu wa watumishi katika Wizara 24, Wauguzi 237, Mafundi Sanifu 42, Wafamasia 3, na
na kuwapangia vituo vya kazi wahitimu Wazoeza Viungo 6. Jumla ya wataalamu wa Afya 983
wa mafunzo mbalimbali ya kada za walipangiwa vituo katika kipindi cha 2006/07.
afya.
80. Kusimamia utekelezaji wa Utawala Wizara imekamilisha uandaaji wa mkakati mpya wa
Bora na kuimarisha maadili ya kupambana na rushwa wa mwaka 2006-2010 na tayari
Utumishi wa Umma kwa kutoa umewasilishwa kitengo cha Utawala Bora. Aidha,
mafunzo kwa watumishi wa Wizara na Wizara imeendesha semina za maadili katika Utumishi
kudhibiti vitendo vya utoaji na upokeaji wa Umma,kudhibiti utoaji na upokeaji rushwa na taratibu
rushwa pamoja na ukiukwaji wa za ugavi kwa watumishi 113 ikijumuisha maafisa tawala
maadili kwa kuwachukulia hatua za na utumishi, wasaidizi wa masijala, maafisa ugavi na
kinidhamu na kisheria wote makatibu mahsusi.
watakaobainika kujihusisha na vitendo
hivyo. Wizara imepitia upya mkataba wake wa huduma kwa
mteja wa tarehe 1/7/2005 ambapo vijarida 4000
vilichapishwa na kusambazwa katika vyuo, Hospitali za
Rufaa, Vyuo vilivyo chini ya Wizara, Taasisi zilizo chini
54
ya Wizara na makao makuu ya Wizara.
Watumishi wameendelea kuelimishwa kuhusu umuhimu
wa kuvaa vitambulisho na kuimarisha matumizi ya
visanduku vya maoni katika Vyuo, Taasisi, Hospitali za
Rufaa na Makao Makuu ya Wizara.
81. Kuimarisha ushirikishwaji wa Wizara imewawezesha Viongozi na Wajumbe wa
wafanyakazi katika mipango na TUGHE kuhudhuria mafunzo ya Sheria za kazi na
utekelezaji wa maamuzi mbalimbali Wajibu wa Tawi mahala pa kazi. Aidha, Baraza la
kupitia Tawi la TUGHE na Baraza la Wafanyakazi limeshirikishwa katika mchakato wa
Wafanyakazi la Wizara. kuandaa mipango na bajeti ya Wizara kwa mwaka
2007/08.
82. Kuandaa mipango thabiti Mpango huu umefanyika kwa kuyafundisha makundi
itakayotumika katika kutekeleza na mbalimbali ya watumishi wa Wizara wakiwemo
kuelimisha watumishi wa Wizara wataalam wa bajeti, masjala na makatibu muhtasi.
masuala yanayohusu jinsia.
83. Kuendelea kutoa mafunzo ili Mikoa iliyokuwa imebakia ni Kigoma, Tabora, Dar es
kuimarisha utendaji wa timu za Salaam, Lindi, Mtwara na Mbeya ambayo wataalam
uendeshaji za mikoa ya Kigoma, wake walipatiwa mafunzo tarehe 16/10/2006 hadi
Mbeya, Rukwa, Ruvuma, Tabora na 4/11/2006. Kwa sasa kamati zote za mikoa Tanzania
Iringa. Jumla ya wataalamu 62 Bara zimepata mafunzo hayo.
watapatiwa mafunzo hayo.
84. Kuendesha mafunzo kwa njia ya posta Mitaala imepitiwa na moduli kwa mafunzo ya Waganga
kwa Waganga Wasaidizi Vijijini. Jumla Wasaidizi Vijijini na Wakunga Wasaidizi ( MCHA)
ya Waganga Wasaidizi Vijijini 140 kati imeandaliwa na inaendelea kutumika katika mafunzo
ya 306 wanatarajia kuhitimu mafunzo hayo. Inatarajiwa kuwa mafunzo hayo yataendelea hadi
ya Afisa Tabibu kupitia mafunzo hayo. hapo wataalamu wote wa kada hizi wakatapokuwa
Aidha, mafunzo katika fani ya Uuguzi wamepatiwa mafunzo ya “upgrading” na kuwa “Clinical
kwa njia ya posta yataanza kutolewa Officers” na “PHN - Nurses”.
kwa Wakunga Wasaidizi Vijijini
(MCHA). Wizara pia inatarajia kutoa
wataalam 2,750 katika fani ya sayansi
shiriki na uuguzi.
85. Kufanya ufuatiliaji wa wahitimu (tracer “Proposal”. iliandaliwa na Mkuu wa Chuo cha “Vector
study) wa mafunzo ya udhibiti wa Control” Muheza na aliiwasilisha wizarani. Wizara
magonjwa yanayoambukizwa na inalifanyia kazi suala hili na mafunzo hayo yanatarajiwa
wadudu kutoka Chuo cha Vector kuanza mwaka 2007/08.
Control cha Muheza.
86. Kuongeza nafasi za mabweni na Vyuo vyote 15 vilivyokuwa vya Uuguzi vinaendelea
madarasa kwa ajili ya kuongeza idadi kufanyiwa ukarabati ili viweze kuchukua wanafunzi
ya wanafunzi katika vyuo 15 vya wengi zaidi wa “upgrading” na “pre-service”. Vyuo vya
uuguzi ambavyo hapo awali vilikuwa Njombe na Tukuyu vimeanza kuingiza wanafunzi
vinatoa mafunzo ya afya ya mama na mkondo wa pili. Vyuo vya Kahama, Kondoa, Geita, na
mtoto (Maternal and Child Health – Tarime vinategemea kupokea wanafunzi mkondo wa pili
MCHA). Septemba, 2007.
55
87. Kuendelea kusimamia viwango vya Serikali imefanyia ufuatiliaji wa utoaji huduma katika
ubora wa huduma, uwiano mzuri wa mikoa ya Mtwara, Lindi, Ruvuma, Manyara, Morogoro,
idadi ya wataalam, uboreshaji wa Kigoma, Tabora na Tanga ili kuimarisha viwango vya
huduma za uuguzi, kukabiliana na afya vya wananchi, kubaini mapungufu yaliyojitokeza na
dharura na maafa, ukaguzi wa huduma namna ya kuyatatua. Ukaguzi wa huduma za afya
za afya na maadili ya taaluma ulifanyika katika mikoa ya Arusha, Iringa, Manyara na
mbalimbali kupitia mabaraza na vyama Pwani.
vya kitaaluma.
88. Kuboresha miongozo inayoelekeza Tafsiri ya mwongozo wa kuthibiti na kuzuia maambukizi
viwango vya utoaji huduma ili kwa lugha ya Kiswahili imefanyika. Mwongozo huo kwa
kuimarisha kitengo cha ukaguzi lugha ya Taifa utaweza kutumiwa na watoa huduma
kimuundo na kiutendaji ili kukipa ngazi zote za utoaji huduma kwa urahisi. Mwongozo
uwezo wa kufuatilia utoaji wa huduma utasambazwa kwenye vituo vya huduma baada ya
za afya katika ngazi mbalimbali. kupata maoni ya Wadau wengine.
89. Kuboresha mafunzo ya ufundi katika Vifaa vya kufundishia na kujifunzia vyenye thamani ya
vyuo kwa watu wenye ulemavu na Shilingi milioni14.2 vilinunuliwa kwa ajili ya vyuo vya
mafunzo ya walezi wa watoto wadogo ufundi kwa watu wenye ulemavu vya Singida, Mirongo,
katika Chuo cha Kisangara kwa Yombo na chuo cha Walezi Kisangara.
kununua vifaa vya kufundishia.
90. Kupitia mtaala wa mafunzo ya malezi Kazi ya kupitia mtaala wa mafunzo imefanyika. Mtaala
kwa vituo vya kulelea watoto wadogo wa mafunzo ya malezi kwa vituo vya kulelea watoto
mchana na kuboresha ili kuendana na umeandaliwa na kusambazwa kwa wadau wote.
wakati.
91. Kufanya ukarabati katika shule ya Katika kipindi husika uwekaji wa Umeme katika vyuo
maadilisho ya Irambo, makazi ya vya Luanzari na Kisangara ulifanyika kwa gharama ya
wazee Kolandoto, mahabusu ya Sh. 18,500,000.
watoto Dar es Salaam na Mbeya,
Chuo cha ufundi kwa watu wenye Ukarabati Irambo, Kolandoto, Dar es Salaam na Mbeya
ulemavu Luanzari na Chuo cha walezi haujafanyika kutokana na ukosefu wa fedha.
wa vituo vya kulelea watoto wadogo
mchana Kisangara.
92. Kuanza ujenzi wa mahabusi mpya ya Mkataba wa ujenzi wa mahabusu mpya ya watoto
watoto mkoani Mtwara. mkoani Mtwara ambao uliwekwa saini mwezi Juni, 2006,
ujenzi wake umeanza na unaendelea. Fedha kwa ajili
ya kazi hii zimewekwa kwenye miradi ili ziendelee
kutumika.
93. Kuendelea kutoa vifaa vya kujimudu Jumla ya watu 110 wenye ulemavu walipatiwa vifaa vya
kwa watu wenye ulemavu pamoja na kujimudu vyenye thamani ya Shilingi milioni 25. Aidha
kuwapatia mitaji ya biashara na wanafunzi 150 wenye ulemavu na waadiliwa 50
vitendea kazi wahitimu kutoka vyuo walipatiwa mitaji ya biashara na vitendea kazi vyenye
vya ufundi kwa watu wenye ulemavu, thamani ya Shilingi milioni 15.
waadiliwa na vijana kutoka katika
makazi ya wazee na makao ya watoto
yatima Kurasini.
56
94. Kuendelea na hatua za kuandaa na Kazi ya uandaaji wa Sera ya Huduma za Ustawi wa
kukamilisha Sera ya utoaji wa huduma Jamii imeanza kutekelezwa. Warsha ya uhamasishaji
za ustawi wa jamii, kuendelea wa utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Maendeleo na
kuhamasisha jamii, Mamlaka za Miji na Huduma kwa watu wenye ulemavu, Sera ya Taifa ya
Halmashauri kuhusu utekelezaji wa Wazee na Mwongozo wa huduma kwa watoto walio
Sera ya Taifa ya Maendeleo na katika mazingira magumu ilifanyika.
Huduma kwa Watu Wenye Ulemavu,
Sera ya Taifa ya Wazee na Mwongozo
wa huduma kwa watoto walio katika
mazingira magumu.
95. Kuendelea kuboresha maisha ya Katika kipindi hiki huduma za chakula malazi na
makundi maalum kwa kutoa chakula, madawa ziliendelea kutolewa. Jumla ya Shilingi milioni
malazi na huduma za afya katika 130 zilitumika kutekeleza jukumu hili.
makazi ya wazee, vyuo vya ufundi kwa
watu wenye ulemavu, mahabusu na
makao ya watoto, Kituo cha mama na
mtoto Ilonga, Chuo cha malezi
Kisangara na shule ya maadilisho
Irambo.
96. Kuendelea kutoa misaada ya dharura Katika kipindi hiki jumla ya familia zenye dhiki 127, watu
kwa familia zenye dhiki, watu wenye wenye ulemavu 225, watoto walio katika mazingira
ulemavu na wazee, watoto walio katika magumu zaidi 139 na watoto waliozaliwa zaidi ya wawili
mazingira magumu zaidi, watoto 35 walipatiwa misaada ya dharura. Jumla ya Shilingi
waliozaliwa zaidi ya wawili kwa mara milioni 26.8 zilitumika kutekeleza jukumu hili.
moja na akina mama wanaopata
ulemavu wakati wa kujifungua.
97. Kuendelea kutoa huduma za majaribio Huduma za majaribio zilitolewa kwa wajaribiwa 102.
na ujenzi wa tabia pamoja na mafunzo Aidha, mafunzo kwa wawezeshaji wa malezi ya watoto
kwa wawezeshaji ngazi ya wilaya wa walio katika mazingira magumu yalitolewa katika Wilaya
malezi ya watoto walio katika za Masasi, Kisarawe, Bagamoyo, Singida Vijijini,
mazingira magumu. Musoma Vijijini, Makete, Iringa na Ngara, ambapo jumla
ya wawezeshaji 96 walipatiwa mafunzo.
98. Kuanzisha mafunzo ya shahada na Taasisi ya Ustawi wa Jamii imeanza kutoa mafunzo ya
Stashahada ya kawaida katika fani ya Shahada na Stashahada ya kawaida katika fani ya
Mahusiano Viwandani na Menejimenti Mahusiano Viwandani na Manejimenti ya Rasilimali
ya Rasilimali Watu. Pia iliongeza idadi Watu. Aidha, Taasisi imeongeza idadi ya wanafunzi
ya wanafunzi kutoka 1,036 hadi 1,500 kutoka 1036 kufikia 1500 katika mwaka wa masomo
katika mwaka wa masomo 2006/07. 2006/07.
99. Kuanza ujenzi wa maktaba ya kisasa Kazi ya awali ya ujenzi ilianza katika robo ya kwanza na
kwenye Taasisi ya Ustawi wa Jamii, ili ya pili ikiwemo uandaaji wa michoro. Ujenzi umeanza
kukidhi mahitaji ya ongezeko la kozi, katika robo ya nne ya mwaka wa fedha 2006/07 na
idadi ya wanafunzi na wahadhiri. utaendelea katika mwaka wa 2007/2008.
100 Kuendelea kusimamia ubora na Mifumo ya usajili wa dawa, vyakula vilivyofungashwa na
usalama wa vyakula, dawa, vipodozi vipodozi inaendelea kutumika. Mfumo wa vifaa tiba
na vifaa tiba na kuimarisha mfumo wa bado unaendelea kutayarishwa. Jumla ya biashara za
57
usajili na ukaguzi wa bidhaa hizi kwa vyakula 125, dawa 434 na vipodozi 275 zilikaguliwa.
kuzingatia ushirikishwaji wa wadau Jumla ya biashara zote zilizokaguliwa ni 834. Viwanda
katika ngazi mbalimbali. vya kutengeneza dawa 14 vilikaguliwa huko nchini India.
Jumla ya mizigo 212,604 ya vyakula ilikaguliwa
mipakani na kuruhusiwa kuingia nchini. Papo hapo,
mizigo ya dawa, vifaa tiba na vipodozi 219 ilikaguliwa
mipakani na mizigo 8 kati yake ilikataliwa kuingizwa
nchini. Sambamba na ukaguzi huo jumla ya kilo 500 za
dawa na 7.08 za vyakula ziliharibiwa kwa ajili ya kutofaa
kwa matumizi ya binadamu.
101 Kukamilisha taratibu za kuifanya Mkandarasi amekwisha anza maandalizi ya upanuzi wa
maabara yake iweze kutambulika jengo la maabara. Vile vile, mtaalam kutoka WHO alitoa
kimataifa ifikapo mwaka 2008. mafunzo, mwongozo na kuainisha maeneo ya kufanyia
kazi kabla ya maabara kutambuliwa kimataifa
(Laboratory accreditation).
102 Kuimarisha huduma za maabara Maabara ndogo zilizoko katika vituo vya forodha na
ndogo zilizoko katika vituo vya forodha baadhi ya hospitali za mikoa zinaendelea kuimarishwa.
na baadhi ya hospitali za mikoa kwa Kwa hivi sasa, maabara hizo mbali na kupima dawa za
kuongeza wigo wa aina ya dawa kutibu malaria vile vile zinapima dawa za kupunguza
zinazofanyiwa uchunguzi na vile vile makali ya UKIMWI kwa waathirika wa ukimwi kama vile;
kuanza kufanya uchunguzi wa sumu Nevirapine, Stavudine, Zidovudine, Lamivudine n.k. Vile
aina ya „aflatoxin‟ kwenye vyakula vya vile, TFDA inashirikiana na Chuo Kikuu cha Tiba
aina ya nafaka. Muhimbili kufanya utafiti wa kupata njia bora ya namna
ya kupima dawa mseto mpya ya malaria. Kuhusu
upimaji wa sumu “aflatoxin” kwenye vyakula vya nafaka
na jamii ya kunde, maandalizi ya kitaalam yanaendelea
ili kuweza kubaini njia bora ya kufanya uchunguzi huo
katika mazingira ya kitropiki.
103. Kuandaa mkakati wa kuimarisha Kwa upande wa dawa, Mamlaka inafanya maandalizi ya
viwango vya uzalishaji wa vyakula na uteuzi wa kamati maalum ya wadau muhimu kutoka
dawa nchini ili kuinua ubora wa dawa katika wizara na taasisi za Serikali itakayosimamia
zinazozalishwa kwa lengo la kulinda utekelezaji wa mkakati huu. Utafiti wa awali (Baseline
afya za walaji, kuongeza ushindani wa Survey) wa viwanda vya vyakula umekwisha fanyika
dawa zinazozalishwa nchini na nchi nzima. Hatua inayofuata ni kukutana na taasisi za
kuongeza mchango wa sekta katika Serikali kama vile TBS, SIDO n.k. kabla ya kukutana na
pato la taifa. wadau wengine ambao siyo taasisi za Serikali.
104. Kuendelea kutoa mafunzo kwa Mamlaka imeendelea kuwasomesha watumishi wawili
watumishi ili waweze kufanya kazi kwa (2) hapa nchini kwa mafunzo ya muda mrefu na
ufanisi zaidi. kuwapeleka watumishi wengine wawili (2) nje ya nchi
(Uingereza). Mafunzo ya muda mfupi yataendelea
kutolewa kwa watumishi husika kwa kuzingatia mpango
wa mafunzo wa Mamlaka.
105. Kuendeleza mpango wa Maduka ya Mpango kwa Mikoa ya Lindi na Pwani haukutekelezwa
Dawa Muhimu katika mikoa ya Lindi, kutokana na ukosefu wa fedha za kuanzisha mradi
Morogoro, Pwani, Rukwa na Mtwara. husika. Mkoa wa Morogoro – Wilaya za Kilosa na
58
Kilombero; uhamasishaji, ukaguzi wa maduka ya dawa,
mafunzo kwa wakaguzi wa wilaya vimefanyika. Wilaya
za Mvomero na Morogoro Vijijini; Semina za
uhamasishaji wa ngazi ya wilaya, Kata na vijiji zilifanyika
ukaguzi wa maduka ya dawa, uhamasishaji, uboreshaji
wa mitaala na mwongozo wa uwezeshaji vimefanyika
katika mikoa ya Rukwa na Mtwara. Sambamba na
utendaji huo, Mpango mkakati wa upanuzi wa Maduka
ya Dawa Muhimu wa 2006 – 2012 umekamilika.
106. Kuimarisha uwezo wa Wakala kutoa Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali
huduma bora kwa kutumia teknolojia umenunua vitendea kazi kama kemikali, vitendanishi,
na vifaa vya kisasa na kemikali zenye “glassware, standards”, mashine, vipuri na
ubora. matengenezo ya mitambo kwa ajili ya utekelezaji wa
majukumu yake ya uchunguzi wa ubora, usalama na
utambuzi wa sampuli za Vyakula, Dawa, Maji, Majitaka,
Kemikali,Toksikolojia, Dawa za kulevya na DNA. Jumla
ya sampuli 12,860 zimechunguzwa na matokeo
kutolewa katika muda wa siku 14 kama ilivyoainishwa
katika Mkataba wa Huduma kwa Mteja.
107. Mafunzo ya muda mfupi na mrefu Mafunzo ya muda mfupi na mrefu ndani na nje ya nchi
yanayoendana na mabadiliko ya yametolewa kama ifuatavyo;
teknolojía ili kuboresha utoaji wa Muda mfupi: “Instrumental and Analytical Techniques”,
huduma kwa jamii. in Austria, (Mtu 1), Occupational Safety and Health in
Swaziland
(Mtu 1), “EPICOR Training” in DSM (Mtu 1), “Laboratory
Skills in Analysing Chemicals related to Chemical
Weapons” Finland (Mtu 1), “Customer Care” DSM
(Watu 16) na “Driving Skills”, DSM (Mtu 1). Muda mrefu:
MSc DNA Profiling UK (Mtu 1), MBA ESAMI and
Mzumbe University (Watu 2), “MSc Microbiology”
Belgium (Mtu 1) na “MSc Integrated Environmental
Management UDSM (Watu 2).
108. Kuongeza ufanisi katika usimamizi wa Kompyuta nne zimenunuliwa, tovuti (gcla@gcla.go.tz)
Sheria ya Kemikali za Viwandani na imeimarishwa na “website” ya Wakala (www.gcla.go.tz)
Majumbani kwa kuanzisha mtandao ambayo ina sheria ya kemikali imeboreshwa na
wa ndani na nje ambao utaiwezesha inasomeka ndani na nje ya nchi. Kazi inayoendelea ni
kupata taarifa zilizo bora na kwa kufunga “Local” and “Wide Area Net Work” ili taarifa
wakati. zipatikane kwa wakati.
59
109. Kuimarisha ukaguzi wa kemikali, Katika kuimarisha utekelezaji na usimamizi wa sheria ya
kuhamasisha Wadau juu ya sheria ya kemikali, Maabara imeendelea kuimarisha ukaguzi
kemikali na miongozo yake na kutoa mara kwa mara wa waingizaji wa kemikali nchini kwa
mafunzo kwa Maafisa Forodha, kuendesha warsha, mafunzo na miongozo kwa
Maafisa Afya, Polisi na wadau wengine wafanyakazi wake na wadau wanaojishughulisha na
juu ya sheria ya kemikali. biashara ya kemikali.
Utaratibu wa kutembelea sehemu za biashara ya
kemikali ili kuwahamasisha kujisajili na kutoa maelekezo
ya utendaji bora katika kutumia au kuhudumia kemikali
umeimarishwa. Aidha, mafunzo ya ukaguzi kwa maofisa
wa vituo vya mipakani ambavyo ni Sirari, Bandari ya
DSM, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. J. K.
Nyerere, Tunduma, Mbambabay, Kasumulo, Namanga,
Holili na Horohoro yamefanyika.
Jumla ya maduka, maghala na viwanda 130 vya wadau
wanaofanya biashara ya kemikali katika mikoa ya
Arusha, Tanga, Iringa, Kilimanjaro, Shinyanga na
Mwanza yalikaguliwa.
60
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kukamilisha ukarabati wa jengo Kazi zinazoendelea kukamilishwa kwa sasa ni ufungaji
litakalotumika kama ofisi ya Makao wa mtandao wa simu, kompyuta na mfumo wa viyoyozi.
Makuu ya Magereza.
2. Kukarabati Ofisi ya Mkuu wa Magereza Mshauri wa mradi (TBA) anaendelea kuandaa taratibu
Mkoa wa Dodoma. za ukarabati.
Kuendelea na ukarabati wa majengo Ukarabati wa miundo mbinu ya majengo ya Magereza
na Miundombinu ya Magereza yenye yenye ulinzi mkali unaendelea na uko katika hatua
ulinzi Mkali likiwemo Gereza la mbalimbali za utekelezaji katika Magereza ya Ukonga,
Maweni, Uyui, Ukonga, Lilungu na Isanga Maalum, Keko, Lindi, Lilungu na Uyui.
Gereza Maalum Isanga.
4. Kuendelea kukamilisha baadhi ya Ujenzi wa bweni moja lenye selo mbili yenye uwezo wa
viporo vya miradi ya mabweni ya kuhifadhi wafungwa 100 kwenye gereza la Kahama
wafungwa na Mahabusu na kuendelea umekamilika na linatumika. Bweni lingine lenye selo 2
na ujenzi wa Magereza ya Mbarali, limefikia hatua ya mtambaa wa panya.
Mbinga, Igunga, Meatu, Kahama,
Kasulu, Bangwe (Kigoma). Ujenzi wa mabweni yenye uwezo wa kuhifadhi
wafungwa 50 kila moja katika gereza la Igunga, Mbinga
na Bangwe umekamilika na yanatumika. Ujenzi wa
bweni la pili kwenye gereza la Bangwe pia umekamilika.
Ukarabati unaendelea katika Magereza ya mahabusu ya
Shinyanga, Iringa, Njombe, Maswa na Rombo. Aidha
ukamilishaji wa viporo vya mabweni ya wafungwa
haukufanyika kutokana na ukosefu wa fedha.
5. Kukamilisha ujenzi wa nyumba za Ukamilishaji wa nyumba za Askari na Maafisa zilizoanza
askari zilizoanza mwaka 2005/2006 kujengwa kwa kipindi tajwa unaendelea kwa awamu
katika Magereza ya Loliondo - Arusha, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa “Rest House” Morogoro,
Mbulu - Manyara, Mpwapwa - Mpwapwa, Muleba na Keko. Aidha ujenzi wa jengo la
Dodoma, Mwanga - Kilimanjaro, Iringa ghorofa nne kwa ajili ya kuishi familia 16 za askari
- Iringa, Sumbawanga - Rukwa, Kibiti - unaendelea ambapo mpaka sasa kazi iliyofikiwa ni
Pwani, Namajani - Mtwara na Wami kusimikwa nguzo za sakafu ya chini.
Vijana - Morogoro.
6. Kuanza ujenzi wa nyumba za askari Ujenzi wa nyumba katika Magereza tajwa haukufanyika
katika Magereza ya Igunga – Tabora, kutokana na ukosefu wa fedha.
Mkuza na Kigongoni – Pwani, Lindi,
King‟ang‟a – Dodoma, Rombo –
Kilimanjaro, Mbarali na Mbozi – Mbeya
na Kikosi Maalum – Ukonga Dar es
Salaam.
7. Kuendelea kujenga nyumba za askari Ujenzi haukufanyika kutokana na ukosefu wa fedha.
na Maafisa wa Mkoa mpya wa
61
Manyara.
8. Kuendelea kuimarisha mifumo ya maji Uimarishaji na uboreshaji wa mifumo ya maji taka na
safi na maji taka Magerezani. maji safi magerezani umefanyika katika vituo vya
K/Kimbiji- Ukonga, K/Chikuyu-Manyoni kwa kujenga
mnara wa maji, kununua mabomba kwa ajili ya
kusambaza maji, kujenga kibanda cha maji na kununua
“simtank” mbili zenye ujazo wa lita 5,000 kila moja.
Aidha mifumo ya maji taka imeimarishwa katika
Magereza ya Mahabusu Tanga, Sumbawanga, Bukoba,
Lindi, Urambo- Kilimo, Kwamngumi na gereza Tarime.
9. Kupima maeneo ya Magereza ya Upimaji wa maeneo unaendelea kufanyika katika
King‟ang‟a, Mpwapwa, Kibondo, Magereza ya King‟ang‟a, Mpwapwa, Kibondo, Mugumu,
Mugumu, Chuo Kiwira, Tandahimba – Mkuza, Meatu na Uyui.
Mtwara, Ubena, Mkuza, Meatu, Uyui
(Kambi Kakola na Kambi Kazima),
Nzega, Kizwite – Rukwa.
10. Kuanza ujenzi wa Magereza mapya ya Ujenzi wa bweni moja lenye selo mbili unaendelea
Wilaya za Karatu, Nkasi, Bukombe na katika gereza la wilaya Bukombe. Aidha ujenzi wa
Ruangwa. Magereza mapya kwa Wilaya za Ruangwa, Hanang na
Nkasi haujaanza kutokana na ukosefu wa fedha.
11. Kununua magari 82 na matrekta kwa Taratibu za ununuzi wa magari zimekamilika na
ajili ya shughuli za Magereza kama mzabuni amepatikana.
ifuatayo:-
Magari maalum 11 kwa ajili ya
kusafirisha mahabusu kwenda na
kurudi Mahakamani; Malori matatu (3)
ya tani 7 (7tons long wheel base);
Tipper mbili (2) za tani 7 (7 tons Dump
Trucks); Magari madogo 64 (4WD
P/Ups) kwa ajili ya vituo vya Magereza
ya Wilaya 64; Magari madogo mawili
(2) (2 saloon cars), matrekta matano
(5) kwa ajili ya kuimarisha kilimo.
12. Kuanzisha mradi wa kupanda ekari Mkakati wa kuhifadhi mazingira ya ardhi na vyanzo vya
3,000 za miti aina mbalimbali katika maji katika eneo la Ekari 3,000 kwa maeneo tajwa upo
Magereza ya Idete - Morogoro, Isupulo katika hatua ya uandaaji wa maeneo hayo kwa ajili ya
- Iringa na Msalato - Dodoma. kupanda miche ya miti. Kazi ya uchimbaji wa mashimo,
usombaji wa mbolea ya samadi kwa ajili ya vitalu vya
miti inaendelea.
13. Kufanya utafiti wa nishati mbadala kwa Utafiti umekamilika na gharama za ujenzi zimepatikana,
ajili ya matumizi ya kupikia chakula cha utekelezaji utafanyika katika mwaka wa fedha 2007/08.
wafungwa Magerezani na Kuondokana
na matumizi ya kuni ili kuokoa uharibifu
wa mazingira ya nchi yetu.
62
14. Kuendelea na Ujenzi na ukarabati wa Ujenzi wa nyumba tano Chuo cha Ukonga umekamilika
Vyuo Ukonga na Kiwira Mbeya. na zinatumika. Ujenzi wa bweni moja la wanafunzi wa
kike lenye uwezo wa kulaza wanafunzi 99 lipo katika
hatua za ukamilishwaji na ukarabati wa madarasa
unaendelea Chuo cha Kiwira.
15. Kuanza kwa awamu jukumu la Taratibu za ununuzi wa magari maalumu ya kusafirishia
kusafirisha mahabusu kwenda mahabusu zimekamilika na mzabuni amepatikana.
Mahakamani na kurudi Magerezani.
16. Kufanya ukarabati wa majengo katika Utaratibu wa kuwapata wakandarasi kupitia Bodi za
vituo vya Manyovu, Mabamba, Zabuni za mikoa husika uko katika hatua za mwisho.
Rusumo, Mkoa wa Pwani, Sirari, na Utekelezaji unatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha
Kilimanjaro. 2007/08.
17. Idara ya Uhamiaji Jenereta 17 zimenunuliwa na tayari zimekwisha fungwa
Ununuzi wa Magari 20, Pikipiki 30, Boti katika vituo vifuatavyo: Namanga, KIA, Holili, Tarakea,
4 na Jenereta 15. Horohoro, Uwanja wa ndege wa Mwanza, Sirari,
Mtukula, Rusumo, Kabanga, Bandari – Kigoma,
Manyovu, Kasesya, Tunduma, Kasumolu, Kilambo na
Bandarini Zanzibar.
18. Kuanza ujenzi wa Ofisi za Mikoa ya Zoezi la kumpata mkandarasi wa kujenga Ofisi za
Dar es Salaam, Manyara, Mtwara na Uhamiaji katika Mikoa ya Dar es Salaam na Manyara
Kituo cha Kagunga Mkoani Kigoma, na limekamilika na ujenzi wa ofisi hizi umekwishaanza.
kukarabati jengo la Ofisi ya Mkoa wa Aidha, ujenzi wa ofisi ya uhamiaji mkoa wa Mtwara,kituo
Dodoma. cha Kagunga Kigoma na ukarabati wa jengo la ofisi ya
Dodoma haujafanyika kutokana na ufinyu wa bajeti
uliosababishwa na kukatwa bajeti ili kugharimia mahitaji
ya Serikali nje ya bajeti.
19. Kuanza utekelezaji wa Mradi wa Mpango kazi (Action Plan) umeandaliwa ambao
Vitambulisho vya Uraia ikiwa ni pamoja umeidhinishwa na Baraza la Mawaziri kwamba ifikapo
na kupata watumishi wenye ujuzi, mwaka 2009 vitambulisho viwe vimeanza kutolewa.
kuanza ujenzi wa jengo la mradi huo
na kupata mzabuni atakayetengeneza Aidha, Mpango wa kuundwa kwa Wakala wa
vitambulisho hivyo. vitambulisho vya kitaifa (National Identity Agency)
unaendelea kufanyiwa kazi. Aidha mchakato wa uteuzi
wa Mtendaji Mkuu wa Mradi huu (Chief Executive
Officer) kwa mujibu wa ratiba unafanyiwa kazi kwa
ushirikiano baina ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Pia
Jengo kwa ajili ya mradi huo limenunuliwa.
20. Kuendeleza zoezi la „visa stickers‟ Zoezi la ufungaji wa mashine za „visa stickers‟ katika
kwenye vituo kumi na saba (17) vya vituo kumi na saba (17) na balozi zetu limekamilika.
kuingilia nchini pamoja na kuzihusisha
ofisi za Balozi zetu zote.
21. Kuanzisha Chuo cha Uhamiaji Majengo kwa ajili ya Chuo anzilishi yamenunuliwa huko
(National Immigration Training mjini Moshi na tayari ukarabati umekwishafanyika. Aidha
Institute) huko Moshi. chuo hiki kinahitaji kufungwa mtandao wa kompyuta
63
ambao bado haujafungwa, Chuo hiki kinatarajiwa
kufunguliwa rasmi mwezi Septemba, 2007.
22. Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Taarifa ya utekelezaji ni kama ifuatavyo:-
Kununua magari ya Zimamoto na
Uokoaji katika Manispaa ya Arusha, Arusha
Shinyanga, Sumbawanga, Musoma na Zabuni imefanyika Manispaa iko katika hatua ya
Halmashauri ya Miji za Babati, mwisho ya kutoa “ award” ya “Supplier.”.
Korogwe, Arumeru na Kahama. Shinyanga
Tathmini imeshafanyika. Bodi ilimwita aliyeshinda
zabuni kupunguza baadhi ya vifaa kwa sababu ya
kuongezeka gharama. Hata hivyo bado gharama
ilibakia kuwa shilingi 396,000,000. Fedha zilizotengwa
ni shilingi 380,000,000/-.
Musoma
Wamepewa gari kutoka TAMISEMI.
Babati
Zabuni imekamilika “supplier” amepewa “award” na
“Letter of Credit L/C” iko katika ufunguzi.
Arumeru
Mchakato wa “evaluation team” unaendelea kumpata
atakayenunua gari hilo la Zimamoto.
Kahama
Zabuni ilifunguliwa akapatikana muuzaji mmoja hivyo
waliongeza muda ili wapatikane zaidi kuleta ushindani.
Sumbawanga
Wametangaza na kufunga zabuni. Kinachosubiriwa ni
“Evaluation team” kufanya kazi ya uchambuzi.
23. Kuangalia upya Sera, Sheria na Rasimu ya Sera ya Taifa ya moto iko ngazi ya Wizara.
Muundo wa Jeshi la Zimamoto na Sheria ya Zimamoto na Uokoaji imejadiliwa na
Uokoaji kwa nia ya kuliimarisha ili kupitishwa na Bunge tarehe 19/04/2007. Kazi
lifanye kazi kwa ufanisi zaidi na kukidhi inayoendelea kufanywa na Jeshi la Zimamoto ni
matarajio ya wananchi. kutunga Kanuni za Kiutumishi na kiutendaji ikijumuisha
amri za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
24. Kuimarisha Chuo cha Zimamoto na Bado ufuatiliaji wa kupatikana eneo muafaka la kujenga
Uokoaji. Chuo cha Kitaifa cha Zimamoto na Uokoaji unaendelea
pamoja na kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo
hicho.
25. Kusimamia zoezi la uanzishwaji wa Mchakato wa ajira ya Askari wa Zimamoto kwa ajili ya
“Commanding Post” kwa kila Mkoa. kuanzisha “Commanding Post” Mikoani unakamilishwa.
Pia zoezi la ufuatiliaji wa kupata ofisi mikoani
linaendelea.
26. Kukamilisha zoezi la kuhuisha Sheria Marekebisho yamekwishafanyika na Rasimu iko katika
ya Wakimbizi ya mwaka 1998 ili iweze hatua ya kupelekwa kwenye Baraza la Mawaziri kwa
kulingana na Sera ya Taifa ya hatua zaidi.
64
Wakimbizi pamoja na mabadiliko
mengine.
27. Kufuatilia upatikanaji wa gati Gati limekwishajengwa na Wakimbizi wanaendelea
zitakazosaidia Wakimbizi kuingia kurejea makwao DRC kama ratiba ilivyopangwa. Kati
kwenye meli wakati kina cha maji ya Aprili na Mei, 2007 Wakimbizi 3,537 walikuwa
kitakapopungua katika Ziwa wamerejea.
Tanganyika ili kurahisisha na
kuongeza kasi ya urejeaji wa
Wakimbizi wa DRC.
28. Kupanua programu ya huduma kwa Semina elekezi zimeendeshwa kwa wadau kutoka Idara
jamii kwa kuipeleka katika Mikoa sita ya Mahakama (Mahakimu), Idara ya Magereza (Wakuu
zaidi. Mikoa hiyo ni Kagera, wa Magereza wa Mikoa na Wilaya) na Idara ya Polisi
Shinyanga, Mara, Tanga, Arusha na (Waendesha Mashataka na Maafisa Upelelezi wa Mikoa
Iringa. na Wilaya) katika mikoa ya Iringa, Tanga na Arusha.
Wadau wengine walioshirikishwa kwenye semina hizo ni
Maafisa Tawala wa Mikoa na Wilaya, Wakurugenzi
Watendaji na Maafisa Mipango wa Halmashauri za
Manispaa, Miji na Wilaya kutoka Wizara ya Tawala za
Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) katika Mikoa
husika.
Semina ziliwajumuisha pia Wasimamizi wa utekelezaji
wa Sheria ya Huduma kwa Jamii (Maafisa Huduma kwa
Jamii) ambao ni Maafisa Maendeleo ya Jamii (CDOs) na
Maafisa wa Jamii (SWOs) katika maeneo hayo.
Aidha upanuzi wa Programu ya Huduma kwa Jamii
katika Mikoa ya Kagera, Mara na Shinyanga kama
ilivyokuwa imepangwa haukuweza kufanyika kutokana
na ufinyu wa bajeti ikilinganishwa na mahitaji halisi
katika kutekeleza majukumu husika.
65
WIZARA YA USALAMA WA RAIA
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuanza mchakato wa kuandaa Sera ya Mtaalam Mwelekezi amepatikana ambaye ni “ Dean -
Usalama wa Raia. Faculty of Laws” – Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
ambaye ameanza kazi mwezi Mei, 2007.
2. Kuangalia upya muundo na mfumo wa Jeshi la Polisi lipo kwenye mchakato wa kuandaa
Jeshi la Polisi pamoja na Sheria na Programu ya Maboresho (Police Force Reform
Kanuni za Jeshi la Polisi. Programe) chini ya usimamizi wa wataalam kutoka
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mchakato upo katika
hatua nzuri ya utayarishaji. Programu hii itakapokamilika
itatoa nafasi ya kuangalia upya muundo, mfumo, sheria
na kanuni za Jeshi la Polisi.
3. Upatikanaji wa makazi na Ofisi Kanda Mipango ya upatikanaji wa maeneo ya makazi na Ofisi
Maalum ya Polisi Dar es Salaam. kwa ajili ya Kanda hiyo imefanyika kama ifuatavyo:
Temeke
Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi imeahidi
kulipatia Jeshi la Polisi eneo lenye ukubwa wa ekari 10
Kibada - Kigamboni. Bado Jeshi la Polisi
halijamilikishwa eneo hilo. Aidha, Wizara kwa
kushirikiana na Jeshi la Polisi itawasiliana na Wizara ya
Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ili kuomba kupatiwa
eneo la ekari 10 lililopo karibu na Kituo cha Polisi
Mbagala Kizuiani.
Mazungumzo ya ununuzi wa nyumba za iliyokuwa
Kampuni ya Kusafisha Mafuta ghafi (TIPER) Kigamboni
yamekamilika. Wizara ya Fedha imekubali kuliuzia Jeshi
la Polisi nyumba hizo kwa thamani ya shilingi milioni
600. Fedha hizo zimetengwa katika bajeti ya 2007/08 ya
Jeshi la Polisi.
Ilala
Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi imeahidi
kulipatia Jeshi la Polisi eneo la ekari 20 Chanika - Pugu
Kajiungeni.
Kinondoni
Maeneo ya Kimara Baruti kimepatikana kiwanja kimoja
lakini hakijamilikishwa kwa Polisi. Aidha, Jeshi la Polisi
limemilikishwa kiwanja kimoja ambacho hakiwezi kukidhi
mahitaji halisi maeneo ya Tegeta. Maombi
yaliyopelekwa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi
yalikuwa ni kubadilishwa wamiliki wa viwanja vinne
66
vilivyoko katika "Block" moja na kiwanja
kilichomilikishwa na kupatiwa Jeshi la Polisi kwa ajili ya
ujenzi wa kituo na nyumba za askari. Utekelezaji wa
Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kwa ajili ya
kupatiwa maeneo hayo unasubiriwa.
4. Kuboresha maslahi ya askari. Wizara kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi iliandaa
mapendekezo ya kuboresha maslahi ya askari Polisi na
kuyawasilisha kwenye Kamati ya Taifa ya kushughulikia
maslahi ya watumishi wa Serikali. Uamuzi wa Kamati
hiyo unasubiriwa. Mikakati ya ndani ya Jeshi la Polisi
iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa kwa lengo
la kuboresha maslahi ya askari ni pamoja na:
Kuanzishwa kwa SACCOS ya Wizara inayoitwa
“URA
SACCOS”.
Ufufuaji wa Kantini za Polisi.
Mkataba wa NSSF wa kuanza kujenga nyumba za
Polisi kwa awamu upo katika hatua ya kuwekwa
saini na Waziri wa Fedha. Awamu ya kwanza ya
mradi itakuwa ni Kambi ya Polisi Kilwa Road na
Ziwani Zanzibar. Mradi utaanza kutekelezwa mwaka
2007/08.
5. Kuwapatia askari mafunzo mbalimbali Jeshi la Polisi limeendelea kuwapatia askari mafunzo ya
ya taaluma zao pamoja na mafunzo taaluma ndani na nje ya nchi. Katika mwaka huu wa
kuhusu Haki za Binadamu na Utawala masomo 2006/07, kati ya Julai, 2006 hadi Mei, 2007
Bora. askari 967 wameruhusiwa kwenda kusoma katika vyuo
mbalimbali hapa nchini na askari 13 wamepatiwa
nafasi ya kwenda kusoma nje ya nchi.
Vile vile katika kipindi hiki askari 86 wamehudhuria
mafunzo mbalimbali yanayotolewa na nchi marafiki kwa
ufadhili wa nchi hizo kama vile Marekani, Misri, India,
Morocco, Japan, Urusi.
Mafunzo ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
Askari wamekuwa wanapatiwa mafunzo kazini (On job
training) katika vituo vyao vya kazi. Walimu wa masomo
hayo ni Maafisa, Wakaguzi na askari wa vyeo
mbalimbali ambao walihudhuria mafunzo ya Waelimisha
Kada “Training Of Trainers” yaliyofanyika Chuo cha
Polisi Moshi. Idadi ya TOT ni 192. Mitaala ya mafunzo
hayo imeandaliwa na Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na
kusambazwa kwa Makamanda wote wa Mikoa /Vikosi
nchi nzima ambapo Haki za Binadamu na Utawala Bora
67
ni miongoni mwa masomo yanayofundishwa.
Aidha, katika vyuo vyote vya Jeshi la Polisi: Chuo cha
Polisi Dar es Salaam, Chuo cha Polisi Moshi na Chuo
cha Polisi Zanzibar somo la Haki za Binadamu na
Utawala Bora hufundishwa kwa kozi za awali (Basic
Recruits ), Uongozi mdogo (NCOs course), Ukaguzi
(Inspectorate ) na Uofisa (Gazzeted ).
6. Kuimarisha Vyuo vya Polisi vya Ujenzi wa maktaba umekamilika katika Chuo cha
Moshi, Dar es Salaam na Zanzibar. Polisi Moshi.
Katika Chuo cha Polisi Dar es Salaam, ujenzi wa
bweni moja na uzio umekamilika. Ujenzi wa mtaro
wa maji machafu unaendelea na michoro ya awali
kwa ajili ya upanuzi wa Chuo kwa mafunzo ya
Senior Management imekamilika.
Katika Chuo cha Polisi Zanzibar ujenzi wa maktaba
awamu ya kwanza umekamilika na ujenzi wa
bwalo/jiko la wanafunzi unaendelea.
7. Kuanza maandalizi ya ujenzi wa Chuo Michoro ya awali na “design” imekamilika. Ufinyu wa
cha Upelelezi (CID) Dodoma. bajeti umekwamisha kuanza ujenzi wa chuo hicho kwani
mahitaji yake ni makubwa mno.
8. Kuanza ujenzi wa Kituo cha Polisi Utaratibu wa Jeshi la Polisi ni kwamba vituo vidogo vya
Mvumi Mission – Jimbo la Mtera na Polisi hujengwa kwa nguvu za wananchi. Hii ni kutokana
Kituo cha Polisi Kata ya Nshamba - na bajeti finyu inayolikabili Jeshi la Polisi. Jeshi la Polisi
Muleba Kusini. Aidha, kukamilisha huchangia nguvu za wananchi pale hali ya kifedha
ujenzi wa Kituo cha Polisi Pawaga - inaporuhusu. Hivyo wananchi katika maeneo hayo
Iringa. wahamasishwe kuhusu ujenzi wa vituo hivyo.
Kutokana na ufinyu wa bajeti ya Jeshi la Polisi,
wananchi wa eneo hilo wanahamasishwa kukamilisha
ujenzi wa Kituo hicho.
68
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kukamilisha Sera ya Malikale, na Rasimu ya Sera ya Malikale imekamilika. Sera hii
kufanya mapitio ya Sera za imejadiliwa na Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri na
Wanyamapori na Misitu na Nyuki. tayari imewasilishwa na kujadiliwa katika kikao cha
Kamati Maalum ya Makatibu Wakuu. Sera hiyo
inatarajiwa kusambazwa kwa wadau katika mwaka wa
fedha ujao.
Sera ya Wanyamapori iliyofanyiwa marekebisho
imepitishwa tarehe 27 Machi, 2007. Aidha, Mchakato
wa kupitia Sera ya Misitu ya mwaka 1998 umeanza.
2. Kukamilisha Sheria ya Utalii pamoja na Rasimu kuhusu Sheria Mpya ya Wanyamapori
Sheria mpya ya Wanyamapori. iliwasilishwa lakini haikujadiliwa kutokana na
kutokuwepo kwa Sera ya Wanyamapori. Sera ya
Wanyamapori imeshapitishwa, hivyo, Waraka wa Sheria
Mpya ya Wanyamapori inategemewa kuwasilishwa
muda mfupi ujao.
Sheria ya Utalii imewasilishwa kwenye Kamati ya Bunge
ya Sheria na Katiba. Sheria hii inategemewa kuwa
imekamilika katika kipindi cha 2007/2008.
3. Kutayarisha Kanuni za uanzishwaji wa Kulingana na Kanuni za WMA (2002 zilizopitiwa 2005)
Mashamba ya kufuga Wanyamapori na maeneo 16 yalichaguliwa kwa ajili ya majaribio. Kipindi
Biashara ya viumbe hai na Kanuni cha majaribio kimefikia kikomo, na tathmini ya mchakato
kuhusu namna ya kuwashirikisha (kwa mujibu wa Kanuni) wa kuanzisha na kusimamia
wananchi katika Uhifadhi wa maeneo haya imefanyika. Wataalamu wa Chuo Kikuu
wanyamapori (WMA Regulations). cha Dar es Salaam kupitia “Institute of Resources
Assessement” ambao wanafanya kazi hiyo,
wamewasilisha rasimu ya kwanza ya taarifa.
Mchakato kuhusu taratibu za kujumuisha maoni ya
wadau muhimu hususan wawezeshaji kama WWF,
Africare, na AWF unaendelea.
4. Kutafsiri Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 pamoja na
Mwaka 2003 pamoja na Kanuni za Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2005 hazijatafsiriwa kwa
Misitu na Uvuvi kwa lugha ya Kiswahili lugha ya Kiswahili na kusambazwa kwa wadau. Kazi
na kuzisambaza kwa wadau. ya kutafsiri itafanyika baada ya marekebisho kukamilika
katika kipindi cha mwaka 2007/2008.
69
5. Kuandaa Mpango wa Uendeshaji na Rasimu ya kwanza ya Mpango wa Uendeshaji wa Pori
Usimamizi wa Mapori ya Akiba ya la Akiba Maswa imekamilika. Aidha, mchakato wa
Maswa, Ugalla, na Lukwika Lumesule kuandaa Mpango wa Uendeshaji wa Hifadhi ya Taifa ya
pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Kitulo Kitulo unaendelea ikiwa ni pamoja na kukusanya
taarifa/takwimu za kuandaa mpango huo. Mpango huo
unatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha wa
2007/2008.
Mchakato wa kuandaa Mpango wa Uendeshaji wa
Mapori ya Akiba Ugalla na Lukwika - Lumesule
haukufanyika kutokana bajeti kuwa finyu.
6. Kuandaa mipango ya Usimamizi wa Shughuli hii itafanyika chini ya Mradi wa Usimamizi
Misitu ya Hifadhi ya Geita Ilombero Hill Misitu Shirikishi (Participatory Forest Management
na North East Mpanda. PFM) kupitia TASAF katika Wilaya husika. Mradi huu
umejikita katika usimamizi shirikishi wa misitu katika
wilaya 40 na kusimamiwa na Halmashauri za Wilaya.
7. Kuanza kutekeleza na kusimamia Mkakati wa Kitaifa wa Kuhifadhi Ardhioevu umekamilika
Mkakati wa Kitaifa wa Ardhioevu, na na kupitishwa na Kamati ya Kitaifa ya Kuratibu
kuendelea kutekeleza Mpango Ardhioevu (National Wetlands Steering Committee –
endelevu wa usimamizi wa ardhioevu NAWESCO).
katika Mikoa ya Mbeya, Iringa na
Utekelezaji wa programu ya usimamizi endelevu wa
Arusha pamoja na kusaidia Wilaya tisa
ardhioevu katika Mikoa ya Mbeya na Iringa na Mapori ya
katika Mikoa ya Mbeya na Iringa,
Akiba ya Usangu, Mpanga-Kipengere na Rukwa/Lukwati
Mapori ya Akiba ya Usangu na
na Wilaya tisa za Mikoa ya Mbeya na Iringa inaendelea.
Mpanga – Kipengele katika kutekeleza
shughuli zinazohusu Uhifadhi na
Matumizi endelevu ya Ardhioevu.
8. Wavamizi wapatao 100,000 wa Misitu Wavamizi wapatao 81,843 pamoja na mifugo ipatayo
ya Lindimaji na Mikoko wataondolewa 44,611 wameondolewa kwenye mikoa ya Tanga na
msituni katika mikoa ya Tabora, Tabora kuanzia mwezi Julai 2006.
Tanga, Pwani na Shinyanga.
9. Kuingizwa katika Hifadhi za Taifa Mchakato wa kupandisha hadhi Pori la Akiba Usangu
baadhi ya maeneo ya Mabonde ya lenye ukubwa wa kilometa za mraba 4,148 na maeneo
vyanzo vya maji, kama bonde la muhimu ya ardhioevu za Bonde la Usangu zenye
Usangu ili utunzaji madhubuti uwepo ukubwa wa kilometa za mraba 5,778 kuwa sehemu ya
na baadhi ya maeneo ya wazi Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, hivyo kufanya hifadhi hiyo
yatawekwa katika taratibu za Mapori kuwa na ukubwa wa kilometa za mraba 20,226
ya Akiba ili kutunza mazingira umekamilika. Azimio la kuridhia hoja hiyo litafikishwa
yasiharibiwe na shughuli za binadamu. Bungeni.
10. Kutangaza maeneo ya Visiwa vidogo Maeneo hayo yametangazwa rasmi kuwa maeneo
70
vya Sinda, Makatumbe, Nyororo, Tengefu na yatasimamiwa na Kitengo cha hifadhi za
Shungimbili na Mbarakuni kuwa Bahari na maeneo Tengefu (Government Notice No.52
maeneo tengefu. ya tarehe 2/3/2007).
11. Kuendelea kukarabati na kuimarisha Katika mwaka huu wa fedha serikali imetekeleza
Magofu ya majengo na maeneo ya yafuatayo katika kulinusuru eneo la Kilwa kutoka
urithi wa dunia ya Kilwa Kisiwani na katika orodha ya Urithi ulio hatarini kutoweka.
Songo Mnara kwa lengo la kuendeleza
Uoteshaji wa mikoko karibu na Gereza la Kilwa-
jitihada za kulinusuru eneo hilo kutoka
Kisiwani; Kujenga kinga maji Kilwa Kisiwani; Kujenga
katika orodha ya urithi wa ulio hatarini
birika za maji kwa ajili ya mahitaji ya ukarabati;
kutoweka kwenye kumbukumbu.
Kujenga tanuru la kuchomea chokaa; Mafunzo
yalitolewa kwa wananchi wa Kilwa Kisiwani na
kushirikishwa katika shughuli za uhifadhi; Kuweka
mabango yenye maelezo mbalimbali kwa wageni;
Uchongaji wa mawe kwa ajili ya shughuli za uhifadhi
wa Songo Mnara unaendelea; Kuandaa vipeperushi
kwa ajili ya Elimu kwa Umma.
12. Kukuza na kusambaza miche 15,000 Wakala wa Mbegu za Miti umekusanya kilo 10,557 za
ya miti aina mbalimbali na kupima mbegu bora, kuuza kilo 8,858 za mbegu bora humu
ubora wa mbegu kwa kuchunguza nchini na kilo 1,187 nchi za nje. Aidha, wakala
sampuli 1,200. umesambaza miche 31,307, imehifadhi kiasi cha kilo
15,700 na kuchunguza sampuli 337 za mbegu.
13. Kuendelea kushirikiana na Serikali za
Shughuli za ugani, kuhamasisha upandaji miti
Mitaa, Serikali za Vijiji na wadau
zinaendelea ikiwa ni sehemu ya matayarisho na
wengine kuendeleza Kampeni ya Taifa
kuhamasisha kampeni ya upandaji miti. Taarifa za
ya Upandaji miti kwa kutambua vyanzo
kisekta, kuanzia ngazi ya vijiji hadi kitaifa zitakusanywa
vya maji na kuhimiza kupanda miti kwa
na kusambazwa kwa kutumia mfumo wa kompyuta
kila Wilaya kupanda miti milioni 1.5.
(National Forestry and Beekeeping Databank –
NAFOBEDA).
Mfumo huo wa NAFOBEDA utaunganishwa na mfumo
wa kompyuta wa Serikali za Mitaa, yaani “Local
Government Management Database-LGMD”.
Muungano huu utawezesha kupatikana kwa taarifa za
upandaji miti kuanzia ngazi ya kijiji, vikundi na watu
binafsi.
Wizara kupitia mpango shirikishi wa usimamizi misitu,
yaani “Partipatory Forest Management” imehamasisha
wilaya kutenga misitu ya usimamizi shirikishi, ambayo
mpaka sasa imefikia eneo la hekta 3,672,854, ambapo
71
jumla ya vijiji 1,821 vimesimamia misitu hiyo.
Wilaya zimeelekezwa kutenga maeneo, hasa yale
yalioko katika eneo lisilohifadhi (General land) ili
yapandwe miti mingi kwa ajili ya matumizi ya nishati
(kuni na mkaa). Kwa yale maeneo yenye vyanzo vya
maji yanapandwa miti inayohifadhi vyanzo. Lengo la
Serikali ni kupanda miti milioni 1.5 kwa kila wilaya.
Mwaka 2001 miti milioni 80 ilipandwa (kitaifa), ambapo
mwaka 2006/2007 lengo liliongezeka na kufikia miti
milioni 118, sawa na ongezeko la asilimia 47.5.
14. Kutenga maeneo manne (4) ya Hifadhi
Eneo la hekta 1,700 za hifadhi za Nyuki za Taifa
za Nyuki (Bee Reserve) katika Wilaya
limetengwa katika Wilaya ya Handeni na Manyoni.
za Manyoni, Handeni, Kondoa na
Hifadhi hizo ni Hifadhi ya Nyuki Aghondi katika Wilaya
Kibondo, na wafugaji Nyuki
ya Manyoni yenye hekta 500 na ya Kang‟ata Wilayani
watawezeshwa kuanzisha na
Handeni yenye hekta 1,200. Hatua za kuzitangaza na
kuimarisha vyama vya ushirika ili
kumiliki hifadhi hizi zinaendelea baada ya vijiji husika
viweze kusimamia uzalishaji na
kuandaa muhtasari wa kukubali kutenga eneo kwa ajili
Masoko.
ya hifadhi ya Nyuki. Aidha katika kuwezesha wafugaji
nyuki kuanzisha hifadhi za nyuki Vijiji vya Kalangasi,
Lutona na Tura katika Wilaya ya Uyui; Nkonko na
Mpola katika Wilaya ya Manyoni na Kijiji cha
Kilimamzinga Wilayani Handeni viliwezeshwa kutenga
maeneo na kupima hifadhi za nyuki za Vijiji. Vile vile
shule za msingi tano Wilayani Manyoni ziliwezeshwa
kuanzisha manzuki.
Katika juhudi za kuwezesha wafugaji nyuki kuanzisha
vyama vya ushirika, wizara imewezesha wilaya za
Manyoni na Kondoa kuanzisha vyama vya msingi katika
ngazi ya Kijiji.
Wilaya ya Kondoa hadi sasa imesajili vyama vya msingi
vya wafugaji nyuki tisa ambavyo viko katika hatua ya
kuunda chama cha ushirika ngazi ya wilaya.
Wilaya ya Manyoni imesajili vyama vitatu vya msingi na
viko kwenye hatua ya kuunda chama cha ufugaji nyuki
Manyoni (Bekeepers Association).
Wilaya ya Handeni Kijiji cha Mswaki kimeunda
SACCOS na Katika Wilaya ya Uyui, Vijiji vya Kizengi na
Malongwe vimeunda SACCOS.
Africare imewezesha wafugaji nyuki katika wilaya za
72
Sikonge na Urambo kuunda SACCOS tatu kwa kila
wilaya.
15. Kabrasha jipya la Maombi kuwezesha Kabrasha la maombi la kuwezesha mji Mkongwe wa
Mji Mkongwe wa Kilwa Kivinje Kilwa-Kivinje kujumuishwa pamoja na Kilwa-Kisiwani na
kujumuishwa pamoja na Kilwa Kisiwani Songo Mnara katika urithi wa Dunia limekamilika na
na Songo Mnara litawasilishwa limewasilishwa UNESCO kwa ajili ya utekelezaji.
UNESCO.
Kuendelea kutekeleza programu ya
16. Kazi ya upimaji na uchoraji wa ramani ya Njia Kuu ya
uboreshaji wa Njia ya Kati ya Biashara
Kati ya Biashara ya Utumwa na Vipusa ambalo ni hitaji
ya Utumwa na Vipusa kutoka
muhimu kuwezesha njia hiyo kuwekwa katika orodha ya
Bagamoyo mkoa wa Pwani hadi Ujiji
Urithi wa Dunia imekamilishwa.
mkoa wa Kigoma. Kazi ya upimaji
pamoja na uchoraji wa ramani ya njia
ya kati ya Utumwa na Vipusa
vitakamilikishwa.
17. Kuhifadhi Mji Mkongwe wa Bagamoyo Kwa kushirikiana na mtaalam – mshauri Wizara
kwa kupima viwanja na kuandaa inaendelea na ukamilishaji wa zoezi la upimaji wa
mchoro wa Mpango Mji. viwanja pamoja na uandaaji wa mchoro wa Mpango Mji
– Bagamoyo.
18. Maeneo kumi (10) ya Jumuiya ya Mafunzo ya ujasiriamali kwa Jumuiya nne yalifanyika
Hifadhi ya Wanyamapori yatapatiwa kupitia kituo cha ujasiriamali cha Chuo Kikuu cha DSM.
haki ya matumizi ya rasilimali ya Jumla ya washiki 43 walipatiwa mafunzo hayo.
Wanyamapori.
Eneo la Ukutu wilayani Morogoro na eneo la Songea
wilayani Songea walipatiwa fedha kukamilisha mipango
ya matumizi bora ya ardhi. Jumla ya vijiji 29 vilipata
huduma hiyo.
Maeneo 8 kati ya 16 ya majaribio ya WMA yamepatiwa
Haki ya Kutumia raslimali ya wanyamapori. Kati ya
hayo, Jumuiya tano zilipatiwa mgawo wa mafao
yatokanayo na uwindaji wa kitalii ya jumla ya TZS
74,074,705.
Maeneo matatu (Twatwatwa, Loliondo na Tarime)
yamesitishwa kwenye majaribio kutokana na migogoro
ya matumizi ya ardhi (wakulima na wafugaji) na mipaka
(kijiji cha Mrito na Mbiso wilaya ya Tarime).
19. Kutoa elimu kwa Maofisa Ugavi 300 na Kutokana na mpango wa utekelezaji wa kazi za Idara
Wafugaji Samaki 300 juu ya ya Uvuvi, kazi hiyo imetekelezwa kuanzia mwezi Mei,
uendelezaji na usimamizi bora wa 2007.
ufugaji uwiano wa samaki katika Mikoa
73
ya Mbeya, Iringa na Kilimanjaro.
20. Elimu itatolewa kwa vikundi 60 vya Vipindi 9 vya Radio vimeandaliwa na kutangazwa
wakulima wa zao la Mwani ili kupitia Radio Tanzania Dar es Salaam ambapo kwa
kuwajengea uwezo wa kiujasiriamali mwaka mzima hutangazwa vipindi 18 kulingana na
na uundaji wa vikundi vya kuweka na ratiba. Vipindi 10 vya televisheni vimeandaliwa na
kukopa ili waweze kunufaika zaidi na vinatangazwa na Televisheni ya Taifa – TUT.
rasilimali za Uvuvi.
Vipeperushi, vijarida na makala yanayohusiana na
sheria na kanuni navyo havikutengenezwa kutokana na
ufinyu wa bajeti.
21. Vyombo vya Uvuvi baharini ikiwa ni Mfumo wa kuratibu vyombo vya uvuvi kwa njia ya
pamoja na vile vya kigeni vinavyovua satellite ujulikanao kama VMS (VESSEL MONITORING
katika Bahari Kuu vitadhibitiwa kwa SYSTEM) umefungwa kwenye Ofisi za Idara ya Uvuvi
kutumia mfumo wa Satelite Makao Makuu na unafanyakazi. Mfumo huu unatumia
(Kompyuta) ili kuratibu mienendo ya teknolojia zifuatazo:
vyombo hivyo.
INMARSAT – C mfumo ambao utatumiwa kuratibu meli
za uvuvi kutoka nchi za Umoja wa Ulaya (EU) na
ARGOS mfumo ambao utatumika kuratibu mienendo ya
meli za uvuvi za Kijapani.
22. Kuandaa na kutangaza vipindi 120 vya Kwa kushirikiana na Taasisi ya Utangazaji Tanzania
redio na televisheni, kuchapisha (TUT) Wizara ilianza rasmi kurusha kipindi cha
nakala 4,000 za majarida, vipeperushi, ZAMADAMU kuanzia tarehe 16/11/2006. Kipindi hiki
mabango pamoja na kuendesha hurushwa na TVT kila Alhamisi saa 1.30 hadi 2.00
mikutano, warsha/semina kwa usiku na kurudiwa Jumapili saa 5.30 – 6.00 mchana.
wananchi na viongozi ili kutoa elimu Hadi kufikia mwezi Mei, 2007, Idara imeweza kurusha
kwa Umma kuhusu sheria, kanuni na jumla ya vipindi 26 kuhusu masuala mbalimbali
matumizi endelevu ya rasilimali za yanayohusu malikale.
Maliasili na Malikale.
Maandalizi ya Mpango wa Uhamasishaji jamii
yamekamilika. Mpango huu utatoa fursa kwa jamii
kuifahamu historia ya nchi yetu na urithi wa utamaduni,
kukuza utalii na kuhamasisha jamii kuendelea kutunza
urithi wetu kwa faida ya vizazi vijavyo. Utekelezaji wake
utaanza katika mwaka wa fedha 2007/2008.
Vimechapishwa vipeperushi kuhusu Kilwa Kisiwani,
Mapango ya Amboni na Caravan Serai.
Vipindi 70 vya Redio vimerushwa kupitia kipindi chake
cha Misitu ni Uhai na Maliasili, kati ya Programu 5 za
televisheni ni vipindi viwili vya mahojiano ya moja kwa
moja vimeonyeshwa. Mada za vipindi hivi zilikuwa elimu
juu ya:
74
Sera ya Taifa ya Misitu ya mwaka 1998; Sera ya Taifa
ya Ufugaji Nyuki ya mwaka 1998; Mwongozo wa uvunaji
endelevu wa mazao ya misitu; Ufafanuzi wa Sheria Na.
14 ya mwaka 2002 ya Misitu; Taratibu za kuanzisha
hifadhi za nyuki nchini; Mbinu bora za Ufugaji Nyuki.
Machapisho mbalimbali, vipeperushi, vijarida na vijitabu
vifuatavyo vilitayarishwa, kuchapishwa na kusambazwa
kwa wananchi wakati wa maonesho ya Biashara ya
Kimataifa Dar es Salaam(Saba Saba) yaliyofanyika
katika viwanja wa Mwl. Julius Kambarage Nyerere,
Barabara ya Kilwa na katika maonesho ya kilimo (Nane
Nane) yaliyofanyika katika Viwanja vya Mwl. Julius
Kambarage Nyerere;
Nakala 3000 za stika ya Moto na Mazingira; Fuga
nyuki, hifadhi mazingira punguza umaskini, misitu ni
uhai.
Nakala 4000 za mabango ya Sera ya Taifa ya
Ufugaji Nyuki; Nyuki ni hazina, kilio cha mti, nishati
mbadala na usimamizi shirikishi wa misitu.
Nakala 7000 za vijarida kuhusiana na Matumizi ya
Mlonge, taratibu za serikali za kusafirisha mazao ya
misitu nje ya nchi, taratibu za uvunaji, usafirishaji na
biashara ya mazao ya misitu “Investment
opportunities in Beekeeping in Tanzania”, ubora wa
asali, njia rahisi ya kutambua asali yenye kiwango
kizuri cha maji na isiyochemshwa.
Nakala 1000 za vijitabu vya ufugaji nyuki vijijini
vilichapishwa.
Semina 14 kuhusu mbinu bora za ufugaji nyuki
zimetolewa kwa wafugaji nyuki katika Wilaya tisa
ambazo ni: Chunya, Uyui, Nachingwea, Rufiji, Kilindi,
Njombe, Simanjiro, Kiteto na Babati.
23. Ili kudhibiti kunguru weusi wajulikanao Jumla ya mitego 65 ya kukamata Kunguru weusi
kama “Indian House Crow” Wizara imetengenezwa na kusambazwa katika maeneo 36 jijini
itatumia mbinu za Kisayansi ambazo Dar es Salaam. Jumla ya Kunguru 11,427
hazitakuwa na madhara kwa wameshanaswa kwenye mitego hiyo na kuuawa.
binadamu, mifugo, viumbe wengine na
Sumu iitwayo DRC 1339 imenunuliwa kutoka nchini
mazingira.
New Zealand na kufanyiwa majaribio na wataalamu
kutoka Taasisi ya Utafiti wa Viuatilifu katika nchi za
Tropiki (Tropical Pesticides Research Institute-TPRI).
75
Majaribio ya sumu hii yameonyesha mafanikio makubwa
katika kuua Kunguru hao.
Zoezi la kuharibu mayai na makinda ya Kunguru
linatarajiwa kufanyika kuanzia mwezi Septemba, 2007
ambacho ni kipindi cha majira ya Kunguru weusi kutaga
mayai.
24. Kufanya sensa katika maeneo ya Sensa za Wanyamapori zilifanyika nchi nzima isipokuwa
Hifadhi za Taifa za Serengeti, Ruaha Pori la Akiba Mkomazi na Umba.
na Katavi pamoja na Mapori ya Akiba
ya Selous, Rungwa na Mkomazi.
25. Kuboresha Maonyesho ya Ekolojia ya Mchanganuo wa mradi wa kuboresha maonyesho ya
wanyama na matengenezo ya magari Ekolojia ya wanyama umekamilika ikiwa ni pamoja na
aina ya Rolls Royce yaliyokuwa michoro na gharama za mradi zinazofikia Sh.
yakitumiwa wakati wa Ukoloni na 77,905,340/=. Aidha, matengenezo ya masanduku ya
baada ya Ukoloni na baada ya Uhuru, maonyesho kwenye chumba kimoja yamekamilika na
yatafanyiwa matengenezo ili yaweze baadhi ya vifaa vya maonyesho vikiwemo fuvu la Faru
kutumika katika siku rasmi za Kitaifa. na fuvu la Tembo vimepatikana.
Banda la maonyesho lilitengenezwa na hivyo magari ya
kihistoria kuonwa na wananchi na watalii kwa urahisi
zaidi. Uthamini wa utafiti umefanywa kubaini gharama
za kutengeneza magari haya ili yaweze kutumika katika
siku rasmi za kitaifa. Utafiti ulihusu mawasiliano na
Kampuni ya Rolls Royce inayotengeneza magari hayo.
Matengenezo kwa gari moja yanakadiriwa kufikia
Shilingi 501,026,000 sawa na Pauni za Kiingereza
200,000 na hivyo kwa magari mawili ni Shilingi
1,002,052,000. Jitihada zinafanywa kushawishi
Makampuni na watu binafsi kuchangia gharama za
matengenezo ya magari hayo ya kihistoria.
26. Kuimarisha na kuendeleza Utalii Utalii wa kiekolojia unaendelea kuimarishwa huko
Ekologia katika Misitu ya Mazingira Amani Tanga kwa kuendelea kuboresha mazingira
Asili ya Amani, Milima ya Ukaguru, kwa kuwaondoa wavamizi wanaochimba madini, n.k.
West Kilombero na Nilo-Tanga. Kwa upande wa Misitu ya Nilo na West Kilombero
mchakato unaendelea wa kubadili matumizi ya misitu
hiyo na kuwa “Natural Reserves” kama ilivyo kwa
msitu wa Amani.
27. Ili kuharakisha utekelezaji wa Sera ya Katika kuandaa Programu hiyo Wizara ilishirikisha
Utalii ya mwaka 1999, Wizara wadau mbalimbali na kukamilisha awamu tatu za
itakamilisha Programu ya Uendelezaji programu hiyo ambazo ni; uchambuzi wa hali halisi ya
Utalii itakayobainisha dhima ya kila sekta, kupitia mipango mbalimbali inayogusa sekta ya
76
mdau wa sekta na kuanza maandalizi Utalii, kuoanisha mipango ya sekta mbalimbali na
ya Mwongozo wa Utalii Ikolojia. muelekeo wa sekta ya utalii. Rasimu ya awali ya
mpango huo inatarajia kukamilishwa katika mwaka ujao
wa fedha.
28. Katika kuendeleza na kuimarisha Kutokana na ufinyu wa bajeti, majarida hayo
utangazaji wa utalii ndani na nje ya hayakuweza kuchapishwa. Majarida husika ni yale
nchi, Wizara itachapisha nakala yanayobeba Marketing Slogan ya “Tanzania the Land of
250,000 za majarida kwa lugha za Kilimanjaro and Zanzibar” hapo nyuma lilijulikana
Kiingereza, Kiitaliano, Kijerumani, “Tanzania Authentic Africa”.
Kiarabu, Kichina, Kijapani, Kirusi na
Kihispaniola.
29. Kukamilisha ujenzi wa kituo cha taarifa Ujenzi wa kituo cha Taarifa cha Dkt. Livingstone Ujiji
katika Kituo cha Kumbukumbu cha unaendelea vizuri.
Dkt. Livingstone, Ujiji – Kigoma.
30. Kuendelea kusimamia maendeleo ya Washauri Wasanifu Majengo walikamilisha michoro ya
ujenzi wa Nyumba ya Utamaduni Dar majengo na ujenzi ulipangwa uanze Mei, 2007. Katika
es Salaam pamoja na kuboresha Kijiji bajeti ya maendeleo ya mwaka 2006/07 Wizara ilitenga
cha Makumbusho ili kiweze kuvutia Shilingi 130,000,000/- kwa ajili ya Mradi kununua magari
watalii wengi zaidi badala ya kutumika mawili (2) ambayo yatasaidia kupeleka programu za
kama eneo la burudani kama ilivyo kielimu kwa wananchi.
sasa.
Kijiji cha Makumbusho huendesha matamasha ya Siku
ya Utamaduni wa Mtanzania. Mwaka 2006 ilifanikisha
tamasha la jamii za kutoka Ukerewe lililofanyika kwa
siku mbili kuanzia tarehe 19-20/8/2006. Aidha, kuna
vikundi vya sanaa vya aina tatu ambavyo hufanya
shughuli zake katika Kijiji cha Makumbusho. Sanaa hizo
ni za ngoma, maigizo na Uchoraji. Vikundi hivyo ni
Kusini Group Sanaa – Tanzania, Jakamoyo Dancing
Group, Makumbusho Dancing Group na Nchabwende
Dancing Group. Vingine, ni Dhahabu Arts Group, Impera
Arts Group na Dira Arts Group. Vilevile kuanzia mwezi
Septemba, 2006 kikundi cha Sanaa cha Nosimo
kimekuwa kikiendesha gulio la sanaa kila Jumamosi na
Jumapili. Vipo vikundi vingine ambavyo hufanya
mazoezi kila wiki. Tarehe 1-6 Novemba Chama cha
Masoko ya Sanaa Tanzania (CHAMASATA) kilifanya
maonesho ya sanaa za Tanzania katika Kijiji cha
Makumbusho katika wiki ya mfuko wa Utamaduni
Tanzania.
Mgahawa wa vyakula vya kitanzania uliboreshwa kwa
kutoa huduma ya vyakula vya jadi na kuandaa tamasha
la “Ya Kale yanapokutana na ya sasa” lililofanyika katika
77
Kijiji cha Makumbusho tarehe 11–17 Januari, 2007.
Tamasha lilihusisha vikundi mbalimbali vya wasanii
kutoka Dar es Salaam na Bagamoyo.
Mipango ya baadaye ya Kijiji ni ujenzi wa maduka ya
Sanaa na uanzishaji wa bustani ndogo ya wanyama.
31. Kuweka Miundombinu eneo la Taratibu za kuwapata wakandarasi watakaojenga Kituo
Oldonyosambu (Tarafa ya Sale) kwa cha Polisi, Zahanati na Shule ya Msingi kwa kuzingatia
ajili ya wahamiaji wa Tarafa ya Sheria ya Manunuzi (Public Procurement Act)
Ngorongoro. zinaendelea.
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inashirikiana na
Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kutengeneza
barabara kati ya Kijiji cha Oldonyosambu na eneo
lililotengwa ili kurahisisha mawasiliano katika eneo hilo.
32. Kukarabati kilometa 400 za barabara Barabara za urefu wa km. 282 na viwanja vya ndege 8
na viwanja vya ndege vinane (8) katika vimekarabatiwa katika Mapori ya Akiba ya Selous,
Mapori ya Akiba. Rungwa, Maswa, Rukwa-Lukwati, Mpanga –Kipengele,
Liparamba na Lukwika – Lumesule - Msanjesi.
Kilometa 24 za barabara kutoka “View Point” hadi
33. Kuanza kuendelezwa kwa “Crater” ya
Lemala zimekarabatiwa ili watalii waweze kutembelea
Embakai katika kiwango cha juu sawa
eneo hilo.
na Ngorongoro ili eneo hilo liweze
kunufaisha Taifa ki-utalii.
“Request for Proposals” ya kujenga Hotel Embakai
zimeshapokelewa ili hatimaye ijengwe Hotel ya Kitalii
katika eneo hilo.
78
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuendelea kuiletea nchi yetu maslahi Serikali ilitekeleza jukumu hili kwa kufanikisha ziara za
ya kiuchumi kwa kuwavutia viongozi wa kitaifa katika nchi mbalimbali zenye lengo
wawekezaji wenye mitaji na teknolojia la kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini mwetu
ya kisasa na watalii. na kuwashawishi wawekezaji kuja kuwekeza nchini.
Ziara zilizofanywa na viongozi wa kitaifa na kuleta
mafanikio makubwa ni pamoja na ziara za Mheshimiwa
Rais nchini Marekani, Japan, China, Korea ya Kusini na
ziara za Mheshimiwa Waziri Mkuu nchini Vietnam,
Thailand na Canada. Kutokana na ziara hizi
wafanyabiashara na wawekezaji katika sekta
mbalimbali wameahidi kutembelea Tanzania ili kuja
kujionea mazingira halisi na hatimaye kuanza
kuwekeza au kuingia ubia na kufanya biashara za
pamoja na Watanzania.
Kufuatia ziara ya Mhe. Rais nchini Japan, Gavana na
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Japan (Japan Bank of
International Cooperation – JBIC) Bwana Koji Tonami
alizuru Tanzania mwezi Machi, 2007. Ziara ambayo
pamoja na mambo mengine, iliwezesha kutia saini
mikataba ya mkopo wa utekelezaji wa MKUKUTA wa
dola za kimarekani milioni 20 kila mwaka kwa miaka
mitano, mkopo wa shilingi bilioni 74.2 kwa ajili ya ujenzi
wa barabara ya Arusha-Namanga, pamoja na
uboreshwaji wa huduma za uhamiaji na forodha
mpakani Namanga. Bwana Tonami alitangaza pia
hatua ya Japan kuisamehe Tanzania deni la shilingi
bilioni 742.
Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imetia saini
makubaliano ya kujenga ukumbi wa mikutano wa
Kimataifa jijini Dar es Salaam. Pia kufuatia mwaliko
alioutoa Mhe. Rais wakati wa ziara yake katika Umoja
wa Falme za Kiarabu, Mtoto wa Mfalme na Naibu
Mtawala wa Imarati ya Ras Al Khaimah, H.H. Sheikh
Saud Bin Saqr Al Qasimi alifanya ziara nchini Tanzania
mwezi Aprili, 2007 kwa nia ya kuangalia na kutafuta
fursa za uwekezaji nchini huku akiambatana na
wawekezaji na wafanyabiashara ambao wameonyesha
nia ya kuwekeza katika utafutaji wa mafuta na gesi,
uchimbaji wa madini, ujenzi wa nyumba na makazi,
sekta ya utalii na upanuzi na uendelezaji wa bandari na
79
viwanja vya ndege. Katika juhudi za kuimarisha
mahusiano yetu ya kibiashara na kukuza utalii, Shirika
la Ndege la Qatar lilianzisha safari za ndege kati ya
Doha na Dar es Salaam mnamo mwezi Februari, 2007.
Wizara imeshiriki kikamilifu katika kuandaa na
kusimamia mkutano mkubwa wa Taasisi ya Kimataifa
ya ”Technology Entertainment and Design (TED)
Global” kati ya tarehe 4 hadi 8 Juni, 2007 huko Arusha
ambapo zaidi ya washiriki 600 wakiwemo wawekezaji,
wabunifu na wanasayansi kutoka nchi mbalimbali za
dunia walihudhuria.
Vile vile Wizara ilishiriki katika makongamano ya
uwekezaji na maonyesho ya biashara yaliyofanyika
Moscow, Urusi mwezi Oktoba, 2006 na maonyesho ya
biashara na utalii yaliyofanyika London, Novemba,
2006.
Kutokana na ziara ya Kiserikali katika nchi za Falme ya
Kiarabu, Tanzania imepata fursa ya kuuza nyama
katika nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE),
Oman na Kuwait. Aidha, ujumbe kutoka UAE
(advanced team) ulikuja nchini mwezi Oktoba, 2006
kuangalia/kutathmini maeneo ya uwekezaji.
Serikali pia iliwakilishwa katika kikao cha Mawaziri wa
Umoja wa Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi huko
Tehran, Iran tarehe 7-8 Machi, 2007. Katika kikao hicho
Mawaziri waliazimia kuanzisha Eneo la Biashara Huru
(Preferential Trade Area); kutayarisha na kutekeleza
mpango wa kubadilishana wataalam na wanafunzi wa
vyuo vikuu vya nchi wanachama; kushirikiana katika
maonyesho ya biashara kila mwaka; na kuimarisha
Sekretarieti ya Umoja huo yenye Makao Makuu yake
nchini Mauritius.
2. Kuendeleza sera ya ujirani mwema na Jukumu hili limefanikishwa kwa ufanisi mkubwa hasa
nchi jirani. kutokana na kufanyika kwa vikao vya ujirani mwema
baina ya nchi yetu na nchi za jirani. Vikao hivi
vimefanyika katika mikoa ya mipakani na nchi za jirani.
Tume za pamoja za ushirikiano wa kiuchumi na ziara
za viongozi wa kitaifa na wataalam kutoka katika sekta
mbalimbali zimekuwa chachu kubwa ya kuendeleza
sera ya ujirani mwema na nchi jirani.
Serikali imeendelea na juhudi za kuvishawishi vyama
vya CNDD-FDD na PALIPEHUTU-FNL vya Burundi
80
katika kufikia makubaliano. Kutokana na ushawishi huo
pande hizi mbili ziliweza kufikia makubaliano tarehe 7
Septemba, 2006, Jijini Dar es Salaam. Viongozi wa
PALIPEHUTU-FNL walirejea Burundi ili kuanza hatua
ya utekelezaji wa Mkataba huo mapema mwaka huu
2007. Katika hatua za mwisho wa mazungumzo baina
ya pande husika iliafikiwa kwamba askari wa chama
cha P-FNL wajumuishwe kwenye Jeshi la serikali ya
Burundi.
3. Kushiriki katika kuimarisha Jumuiya ya Serikali imeshiriki katika mikutano inayohusu Jumuiya
Afrika Mashariki (EAC), Jumuiya ya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) kama
Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ifuatavyo:
Umoja wa Nchi za Afrika (UA), Umoja
Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa SADC wenye
wa Nchi Zisizofungamana na Upande
dhamana ya Ulinzi na Usalama (ISDSC) uliofanyika
Wowote (NAM), na Umoja wa Mataifa
Windhoek, Namibia tarehe 18-21 Julai, 2006. Katika
(UNO).
mkutano huo, Tanzania ilikabidhiwa uenyekiti wa
Kamati hiyo; Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa SADC
wenye dhamana ya masuala ya Siasa, Ulinzi na
Usalama (MCO) uliofanyika Windhoek, Namibia tarehe
2-4 Agosti, 2006. Katika mkutano huo Tanzania
ilikabidhiwa uenyekiti wa Kamati hiyo ya Mawaziri;
Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC
uliofanyika Maseru, Lesotho tarehe 17-18 Agosti, 2006.
Katika mkutano huo, Tanzania ilichaguliwa kuwa
Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya kusimamia masuala
ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ on Politics,
Defence and Security Cooperation). Hivyo Mhe. Rais
Jakaya Mrisho Kikwete hivi sasa ndiye Mwenyekiti wa
”Organ” hadi Agosti 2007.
Tanzania imeongoza waangalizi wa uchaguzi wa SADC
katika nchi za Zambia, DRC, Madagascar na Ufalme
wa Lesotho. Aidha Tanzania ilisimamia Mkutano wa
Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC
uliofanyika mjini Dar es Salaam tarehe 29 Machi, 2007.
Wakuu hao walifanya tathmni ya hali ya siasa ya
Lesotho, DRC na Zimbabwe ambapo Rais Thabo
Mbeki wa Jamhuri ya Afrika Kusini alipendekezwa kuwa
msuluhishi wa mazungumzo ya kisiasa ndani ya
Zimbabwe.
Mkutano wa Mawaziri wa Troika ya Asasi ya Siasa,
Ulinzi na Usalama ya SADC (SADC Organ Troika)
ulifanyika Dar es Salaam tarehe 26 Mei, 2007 kwa
madhumuni ya kufuatilia kwa karibu maendeleo ya hali
81
ya kisiasa katika nchi za Lesotho, DRC na Zimbabwe.
Aidha, Wizara pia imeshiriki kwenye mikutano
inayohusu Jumuiya ya Afrika Mashariki kama ifuatavyo:
(i) Mkutano wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya
Afrika Mashariki uliofanyika Arusha, Tanzania
tarehe 27-28 Novemba 2006. Katika kikao hicho,
Baraza la Mawaziri lilipendekeza kwa Wakuu wa
Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakubali
maombi ya Burundi na Rwanda kujiunga na
Jumuiya ya Afrika Mashariki na mpango wa
maendeleo wa miaka minne hadi 2010 wa
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.
(ii) Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya
ya Afrika ya Mashariki uliofanyika Arusha,
Tanzania tarehe 30 Novemba, 2006. Katika
mkutano huo mapendekezo ya Baraza la
Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
yalikubaliwa na hivyo kuzifanya Burundi na
Rwanda kuwa wanachama wapya wa Jumuiya
ya Afrika Mashariki. Hivyo mnamo tarehe 18
Juni, 2007 katika kikao cha Wakuu wa nchi za
Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichofanyika jijini
Kampala, Uganda, Nchi za Rwanda na Burundi
zilisimikwa rasmi kuwa wanachama wa jumuiya
hiyo.
Serikali ilishiriki kikamilifu katika mkutano wa
Wakuu wa Nchi zisizofungamana na upande
wowote (NAM), Havana, Cuba, tarehe 11-16
Septemba, 2006. Katika mkutano huo suala la
haki za Watu wa Sahara Magharibi kujitawala
wenyewe ambalo lilishindikana kupatiwa ufumbuzi
katika Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nchi
za Nje wa Umoja huo mwezi Mei/Juni 2006 nchini
Malaysia hali iliyotishia kuugawa umoja huo
lilijadiliwa. Mchango madhubuti uliotolewa na
ujumbe wa Tanzania ulisaidia katika kuepusha
kuwepo kwa mgawanyiko wa umoja huo. Wizara
ilishiriki kikamilifu katika kuandika rasimu ya Ibara
163,194 na 165 ambazo kwa pamoja zinakubalika
na pande zote zinazohusika na mgogoro huo
ikiwemo Morocco. Ibara hizo zinasisitiza kwamba
Watu wa Sahara Magharibi wana haki ya
kujitawala wenyewe chini ya Umoja wa Mataifa
82
kwa mujibu wa maazimio mbalimbali
yaliyopitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa
Mataifa – Azimio Na. 60/144 na Azimio Na.
1514(XV). Aidha suala la haki ya Wapalestina ya
kujitawala wenyewe kama Taifa huru na kuishi
kwa amani na Taifa la Israel lilisisitizwa na
ujumbe wa nchi yetu katika mkutano huo.
Kwa kutambua juhudi na mchango wa Tanzania
katika masuala mbalimbali yanayohusu Ukanda
wa Maziwa Makuu, Wizara, katika kikao cha Nchi
Zisizofungamana na Upande wowote (NAM)
iliandika rasimu ya Ibara 162 kuhusu kutambulika
kwa juhudi za nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu
katika kuleta amani, demokrasia na maendeleo
endelevu katika eneo hilo hususan Tamko la Dar
es Salaam la mwaka 2004. Ibara hiyo ilipitishwa
kwa kauli moja.
Serikali ilishiriki kikamilifu katika kuimarisha Umoja
wa Mataifa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi
na Serikali waliohudhuria kikao cha Baraza Kuu la
Umoja wa Mataifa tarehe 17 Septemba hadi
Oktoba, 2006. Katika kikao hicho Tanzania
ilisisitiza umuhimu wa Umoja wa Mataifa
kuendelea kuwa mhimili wa kutatua masuala
mbambali ya kimataifa. Kuhusu Ukanda wa
Maziwa Makuu, Tanzania aliahidi kuendelea
kujihusisha na juhudi zake za kuleta amani,
utulivu na maendeleo katika eneo hilo. Aidha,
kuhusu Mashariki ya Kati, Tanzania ilionyesha
wasiwasi wake kuhusu kusuasua kwa
mazungumzo ya kuleta amani ya kudumu kati ya
Palestina na Israel. Iliziomba nchi wanachama
wa Umoja wa Mataifa na taasisi mbalimbali
duniani hususan Umoja wa Mataifa, Umoja wa
nchi za Ulaya, Marekani na Urusi kuendelea na
juhudi hizo za kuleta amani kati ya Mataifa hayo
mawili kwa njia ya mazungumzo.
4. Kulitangaza jina la nchi yetu na Wizara imetekeleza jukumu la kuitangaza nchi yetu kwa
kuitetea heshima yake miongoni mwa kupitia vipindi mbalimbali vilivyorushwa katika
mataifa. Televisheni ya Taifa (TVT). Vipindi hivyo vya
televisheni vilihusu ziara za Mheshimiwa Rais na
wafanyabiashara alioambatana nao nje ya nchi,
diplomasia ya uchumi na Mchakato wa Helsinki.
83
Vipindi hivi vya Televisheni vimesaidia kuitangaza Sera
yetu Mpya ya Mambo ya Nje inayoweka msisitizo wa
diplomasia ya uchumi ndani na nje ya nchi yetu.
Wizara imeshiriki katika maonyesho na makongamano
ya kimataifa kama vile ”Forum on China-Africa
Cooperation” (FOCAC) lililofanyika tarehe 1 hadi 5
Novemba, 2006 huko Beijing, China. Katika
kongamano hili Serikali ya China iliahidi kuongeza idadi
ya bidhaa za Afrika ziingizwazo kwenye soko la China
bila kulipia ushuru kutoka 187 hadi 440, kuongeza
misaada yake maradufu kwa nchi za Afrika ifikapo 2009
na kuleta wafanyakazi wa kujitolea katika sekta za
kilimo, afya, michezo, elimu, n.k. Makongamano
mengine ni pamoja na ”Economic Forum” iliyofanyika
Hanoi, Vietnam tarehe 6 Septemba, 2006 na Moscow,
Urusi Novemba, 2006. Maonyesho ya Kumi ya
Kimataifa ya China yaliyofanyika huko Xiamen, Jimbo
la Fujian kuanzia tarehe 8 hadi 11 Septemba, 2006 na
Kongamano la Biashara na Utalii lililofanyika London,
Uingereza Novemba, 2006.
Balozi zetu za Riyadh na Abu Dhabi tayari zimeanzisha
tovuti ambazo zina taarifa nyingi kuhusu Tanzania na
zimeunganishwa na anuani za tovuti za mashirika na
taasisi mbalimbali. Aidha, Ubalozi wetu wa Muscat na
Ubalozi Mdogo Dubai wako mbioni kuanzisha tovuti zao
ifikapo mwishoni mwa 2007.
Serikali imeshiriki kikamilifu katika mikutano ya Umoja
wa Afrika (AU), SADC na Umoja wa Mataifa (UNO)
ambapo mchango wa Tanzania umeendelea
kuheshimika katika jumuiya ya kimataifa.
5. Kudai mageuzi katika Umoja wa Wizara ilishiriki katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Mataifa kwa lengo la kuongeza sauti uliofanyika New York, Septemba, 2006 ambao
za nchi zinazoendelea. uliwahusisha Wakuu wa Nchi na Serikali ambapo
pamoja na mambo mengine serikali ilisisitiza dhima ya
Tanzania kuendelea kuhimiza umuhimu wa kuleta
mabadiliko ya mfumo wa muundo wa Umoja wa Mataifa
hususan Baraza la Usalama la Umoja huo ili liweze
kuwa wakilishi na sikivu kwa nchi zinazoendelea na
linalokwenda na wakati.
6. Kuitambua Jumuiya ya Watanzania Serikali imeanza kulishughulikia suala hili kwa
wanaoishi Ughaibuni "Tanzanians in kushirikiana na Balozi zetu nchi za nje. Viongozi wetu
the Diaspora" na kuweka utaratibu wa Kitaifa katika ziara zao nchi za nje, wamepata fursa
84
utakaowawezesha kuchangia ya kuzungumza na Watanzania waishio nchi za Japan,
maendeleo ya Taifa lao. China, Korea Kusini, Saudi Arabia, Falme za Kiarabu
n.k na kuwahamasisha kuwekeza vitega uchumi vyao
hapa nchini ikiwemo pia kuitangaza nchi yetu huko
ughaibuni. Aidha, Wizara inaandaa utaratibu maalum
utakaoimarisha zaidi dhima ya Serikali yetu katika suala
hili.
Wizara ilizielekeza balozi zetu kuwatambua na kujua
idadi ya Watanzania waliopo ughaibuni wakati wa zoezi
la kubadilisha pasi mpya za kusafiria.
Wizara ilishiriki katika mkutano wa "Wanataaluma wa
Afrika walio Ughaibuni – ”Intellectuals from Africa and
the Diaspora” uliofanyika Salvador, Brazil mwezi Julai,
2006 ambao ujumbe wa Serikali ya Tanzania
uliongozwa na Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Ali
Mohamed Shein. Mkutano huo ulihimiza umuhimu wa
kuwatumia wasomi wetu waliopo ughaibuni ili
kuwawezesha kuchangia maendeleo ya nchi za Afrika.
Kwa kutambua umuhimu wa habari kwa wananchi na
wadau wetu ikiwa ni pamoja na Watanzania waishio nje
ya nchi, Wizara imefungua tovuti yake mwezi Mei, 2007
inayopatikana kwa anwani ya www.mfaic.go.tz ambapo
taarifa zote muhimu kuhusu muundo wa Wizara na
idara zake, balozi au uwakilishi hapa Tanzania,
mashirika ya kimataifa yaliyopo nchini, taarifa za balozi
zetu zilizopo nje ya nchi na taarifa za uhamiaji
zitapatikana.
7. Kutekeleza kwa makini jukumu la Serikali inafuatilia kwa makini majukumu yanayotokana
uenyekiti wa kuratibu masuala ya na Tanzania kuwa mwenyekiti wa asasi ya kusimamia
siasa, ulinzi na usalama katika Kanda masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika jumuiya ya
ya SADC. SADC. Majukumu hayo ni pamoja na kuimarisha
demokrasia, utulivu wa kisiasa na hali ya usalama
katika jumuiya ya SADC, kuratibu utekelezaji wa Mradi
wa Hashim Mbita, kuanzisha chombo cha masuala ya
Polisi; maandalizi ya kituo cha masuala ya usalama na
kuratibu maandalizi ya kuunda Brigedi ya Jeshi la
kulinda amani. Waraka wa Baraza la Mawaziri
umeshaandaliwa maalum kwa kulitaarifu Baraza
kuhusu taarifa ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na
Serikali za SADC uliofanyika Maseru, Lesotho mwezi
Agosti, 2006.
85
8. Kufanya maandalizi yote Hatua iliyofikiwa katika mchakato wa uanzishwaji wa
yanayohitajika ili azma ya kuanzishwa Mahakama hiyo ni kupatikana kwa kiwanja
kwa Mahakama ya Haki za Binadamu yatakapojengwa makao makuu ya Mahakama hiyo
na Watu ya Afrika itakayokuwa na maeneo ya Tengeru, jijini Arusha. Serikali iko katika
Makao Makuu mjini Arusha itimie hatua za mwanzo za mazungumzo na mmiliki wa eneo
haraka. hilo ili kuangalia uwezekano wa kulinunua badala ya
kupangisha kwa muda. Jumla ya shilingi bilioni 19.3
zinahitajika kwa ajili ya uanzishwaji wake. Gharama
hizo zinajumuisha ununuzi wa eneo na majengo yake,
kodi za pango kwa ajili ya nyumba za kuishi Rais na
Msajili wa Mahakama, pamoja na ununuzi wa vitendea
kazi vikuu vinavyohitajika.
9. Kufuatilia kwa karibu utekelezaji wa Wizara kwa niaba ya Serikali iliendelea kupitia na
makubaliano ya Tume za Pamoja ili kufufua Tume za Kudumu za Ushirikiano katika kipindi
kufikia malengo yaliyokusudiwa. cha mwaka 2006/2007 ambapo Tanzania ilisaini
Mkataba na Msumbiji katika sekta ya afya na
ushirikiano wa pamoja na kuondoa matumizi ya viza
kwa pasi za kidiplomasia na za kiserikali. Pia Tanzania
ilisaini Mkataba wa kuondoa viza kwa pasi za
kidiplomasia na kiserikali na nchi ya Afrika ya Kusini.
Lengo ni kurahisisha muingiliano baina ya Serikali hizi
mbili na kukuza mahusiano yatakayosababisha kukua
kwa biashara.
Katika kipindi cha 2006/2007 serikali imefanya
mikutano ya Tume za Pamoja za Ushirikiano kati ya
nchi yetu na Msumbiji na Burundi, Tume ya Uchumi ya
Marais (PEC) kati ya nchi yetu na Afrika Kusini pamoja
na kusaini mkataba wa Ushirikiano na Serikali ya
Uganda. Mikutano yote ililenga kukuza ushirikiano
katika usalama wa anga; kupambana na wahalifu;
usalama mipakani; ushirikiano katika sekta ya biashara;
elimu na ufundi; kilimo na masoko;masuala ya viza na
matumizi ya bandari. Mashirikiano haya hukuza
maslahi makubwa ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na
kutupatia ushuru wa forodha, fedha za kigeni na ajira
kwa raia wetu.
Wizara imeshiriki katika mchakato utakaowezesha
kufanyika kwa vikao vya Tume ya Pamoja kati ya
Tanzania na nchi za India na Vietnam. Aidha, imeshiriki
katika kikao cha Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya
Tanzania na Cuba kilichofanyika Arusha mwezi Machi,
2006. Maeneo ambayo utekelezaji wake umefanyika
kulingana na mkataba ni katika sekta ya afya ambapo
86
madaktari 12 kutoka Cuba wapo nchini na idadi hiyo
itaongezeka zaidi katika kipindi cha muda mfupi ujao.
Aidha, Taasisi ya uchunguzi wa magonjwa ya NIMR ya
Tanzania imeshirikiana vyema na Labiofam ya Cuba
katika utafiti wa madawa ya kuangamiza panya na kuua
vimelea vya mbu wa malaria. Wataalamu 3 wa
Labiofam walikuja nchini kufanya utafiti. Kwa upande
wa elimu wanafunzi 5 wa Kitanzania wamekwenda
Cuba kati ya Septemba na Oktoba, 2006 kusomea
shahada za kwanza za ”Sports Administration”,
”Computer Science” na ”Economics”.
10. Kushirikiana na Wizara nyingine katika Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano
uendelezaji wa sera zinazolenga wa Kimataifa, Mipango, Uchumi na Uwezeshaji,
kuongeza kasi ya kukuza uchumi na Fedha, Viwanda, Biashara na Masoko, Maliasili na
kujenga mazingira ya kuliletea taifa Utalii imeweza kuandaa na kufanikisha Makongamano
letu maendeleo. ya Biashara na Uwekezaji yaliyofanyika katika nchi
mbalimbali kama vile ”Tanzania Business Forum” na
”Tanzania Tourism Seminar” zilizofanyika tarehe 1
Novemba, 2006 huko Tokyo, Japan na ”Tanzania-
Korea Business Forum” iliyofanyika huko Seoul, Korea
ya Kusini tarehe 8 Novemba, 2006 wakati wa ziara ya
Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete nchini Korea ya
Kusini.
Kwa kushirikiana na Wizara zinazohusika na sekta za
kilimo, nishati, maji, madini, afya na elimu, Wizara
imetayarisha jumla ya miradi kumi na saba na
kuwasilishwa Serikali ya China.
11. Kufuatilia kwa makini utekelezaji wa Wizara imeshirikiana vyema na Wizara ya Fedha katika
mpango wa kuondoa umaskini vituo vya ”Millennium Challenge Account” vilivyokuwa
ulioandaliwa na Serikali ya Marekani na lengo la kuandaa mazingira mazuri ya kupata
unaoitwa ”Millenium Challenge msaada kutoka Serikali ya Marekani.
Account” ambao umeihusisha
Tanzania.
12. Kufuatilia kwa umakini mkubwa tatizo Majadiliano yamefanyika kati ya serikali na maafisa wa
la upatikanaji wa viza katika baadhi ya Ubalozi wa Marekani na Uingereza ili kupata ufumbuzi
balozi mbalimbali kwa kufanya jitihada wa kudumu wa tatizo la visa katika balozi hizi. Kufuatia
zaidi za kuondoa tatizo hilo kwa majadiliano hayo Ubalozi wa Marekani ulikubali
kuzingatia taratibu za kidiplomasia. kubadilisha mwenendo wao wa kutoa visa. Aidha,
Ubalozi wa Uingereza ulikubali kubadilisha utaratibu wa
waomba visa kusimama kwa muda mrefu wakisubiri
kufikisha maombi kwa wahusika.
87
13. Kukamilisha taratibu mpya za uteuzi na Utaratibu huo umekamilishwa na Wizara na hivi sasa
utendaji kazi wa ofisi za Wawakilishi upo katika hatua za mwisho za utekelezaji.
wa Heshima wa nchi.
14. Kuajiri watumishi wapya 48 wa kada Kibali cha ajira ya nafasi mpya 40 kimeshatolewa.
mbalimbali. Hatua za kuajiri watumishi wapya 25 zinaendelea kwa
kuchambua maombi ya Ajira hizo. Kibali kinafuatiliwa
kwa ajili ya nafasi 15 ambazo ni:-
Maafisa Utumishi 7, Wahasibu 2 na Maafisa Mambo ya
Nje 5 – jumla nafasi 14. Nafasi 3 za Wakurugenzi
zimejazwa. Nafasi ya Mkurugenzi wa Sera na Mipango
(DPP) imefikishwa kwenye Mamlaka ya Ajira.
15. Kuwapatia mafunzo muhimu watumishi Mpango wa mafunzo, (Training Programme)
wa Wizara. umekamilishwa na mafunzo husika yameanza kutolewa
kwa watumishi wa kada zote kwa kuzingatia mahitaji.
Kwa kushirikiana na OR-Menejimenti ya Utumishi wa
Umma yametolewa mafunzo ya Mfumo wa Wazi wa
Mapitio ya Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS). Jumla
ya watumishi mia moja na hamsini na nne (154)
wamekwishapatiwa mafunzo hayo kati ya watumishi
mia tatu na themanini na nane (388). Zoezi hili
linaendelea na litawafikia watumishi wote.
Wizara iliendelea kutoa semina ya mafunzo elekezi kwa
Wakuu wa Utawala na Fedha katika balozi zetu zote.
Jumla ya wakuu wa utawala na Waambata Fedha sitini
na nne (64) kutoka katika balozi zetu thelathini
walishiriki mafunzo hayo.
16. Kupitia upya Kanuni za Utumishi wa Kanuni mpya zimekamilishwa katika ngazi zote na
Nje ( Foreign Service Regulations) na zimeshawasilishwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya
Posho za Utumishi wa Nje ( Foreign Utumishi wa Umma kwa ajili ya hatua za kiutawala
Service Allowance) ili zizingatie hali ikiwa ni pamoja na kuzisajili, ili ziwe na nguvu ya
halisi ya maisha katika vituo kisheria. Viwango vya posho vimeongezwa kwa
mbalimbali. aslimilia 13 kwa vituo vyote vya Ubalozi.
17. Kuendeleza mpango wa miaka 15 wa Wizara inaendelea na ujenzi/ununuzi wa majengo yake.
kununua na kujenga majengo katika Mwaka 2006/2007 imejenga majengo mapya ya kisasa
balozi zetu. kwa ajili ya Ofisi (Chancery) na makazi ya watumishi
(Apartments) huko New Delhi, India ambako Jengo la
Ubalozi lilizinduliwa na Mhe. Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa tarehe 23 Novemba, 2006.
Vile vile tumefanikiwa kupewa na wenyeji wetu kiwanja
kwa ajili ya ujenzi wa Ubalozi huko Kigali, Rwanda.
Katika kipindi hiki cha mwaka wa fedha wa 2006/2007
88
pia Wizara imeweza kununua jengo la ubalozi
(Chancery) jijini Stockholm, Sweden.
Aidha, Wizara inaendelea na mazungumzo na mfuko
wa Hifadhi ya Jamii ya Taifa (NSSF) ili kuwa na
Mkataba wa kutupatia mikopo ya kujengea nyumba au
kujenga kwa ubia kwenye vituo vyetu mbalimbali.
18. Kuhakikisha kuwa Chuo cha Wizara imeendelea kutekeleza juhudi za kukiimarisha
Diplomasia kinaandaa mkakati wa Chuo cha Diplomasia kwa kutekeleza yafuatayo:
maendeleo kwa kurekebisha mitaala,
(i) Mkakati wa maendeleo unaojumuisha uandaaji wa
kuandaa mpango mkuu wa matumizi
mitaala umeandaliwa na upo katika rasimu kwa
ya ardhi na kuimarisha miundombinu
vile hakukuwepo Baraza la Chuo la kupitisha.
ya Chuo.
Aidha, Kamati ya uongozi ya kusimamia uinuaji wa
hadhi ya Chuo imeshaundwa.
(ii) Mpango Mkuu wa matumizi ya ardhi umeandaliwa
na upo katika rasimu ukingojea Baraza la Chuo
kuupitisha.
(iii) Uimarishaji wa miundombinu unaendelea;
Madarasa yameboreshwa kwa juhudi za ndani.
Maboresho hayo yamefanyika katika awamu mbili.
19. Kuhakikisha kuwa Kituo cha Mikutano Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC)
cha Kimataifa cha Arusha kinaongeza kimeendelea na jitihada za kujitangaza zaidi ndani na
idadi ya mikutano kwa kujitangaza na nje ya nchi pamoja na kuboresha huduma na vifaa kwa
kutoa huduma bora zaidi. kadri bajeti ilivyoruhusu, ili kutoa huduma bora zaidi
kwa wateja na kuongeza pato la kituo na nchi kwa
ujumla.
Ili kuongeza idadi ya wateja wa mikutano ya ndani ya
nchi (local meetings) Kituo kimeendelea kujitangaza
katika Televisheni ya Taifa na ITV, kuweka matangazo
katika majarida yanayohusiana na utalii (Tourism
Industry related magazine) kushiriki katika salaam za
pongezi na/au matukio muhimu nchini, kuchapisha
kalenda na ‟diaries‟ za Kituo pamoja na vipeperushi
mbalimbali. Kituo pia hutumia tovuti yake kujitangaza.
Kituo kinashiriki katika maonyesho makubwa ya
mikutano na utalii kwa ajili ya kujitangaza zaidi na pia
kuuza huduma kwa wateja wa mikutano ya kimataifa,
ambao hualikwa kuhudhuria maonyesho hayo. Haya ni
pamoja na yale yaliyoratibiwa na Bodi ya Utalii ya
Tanzania (TTB) ya ”European Incentive Business
Tourism and Meetings Exhibitions (EIBTM) –
Barcelona, Spain (Novemba 27 – Desemba 01, 2006)”
89
pamoja na "Incentive Meetings and Exhibitions (IMEX)”
yanayofanyika Frankfurt, Ujerumani kila mwaka kati ya
Aprili na Mei.
20. Kushirikiana na Wizara ya Elimu na Kwa kushirikiana na Wizara husika, vimeshafanywa
Mafunzo ya Ufundi na Wizara ya vikao vya kuainisha namna ya kutekeleza ahadi ya
Habari, Utamaduni na Michezo katika Mheshimiwa Rais kuhusu kufundisha Kiswahili nje ya
kuandaa walimu wa Kiswahili mipaka ya Tanzania. Wizara kwa kushirikiana na
watakaochukua nafasi za ajira Ubalozi wetu nchini Ethiopia imepitisha bajeti ya
zinazojitokeza katika Umoja wa Afrika kuanzisha kituo cha kufundishia lugha ya Kiswahili.
na nchi nyingine za Afrika. Aidha, nchi zinazohitaji walimu wa Kiswahili
zimeombwa kuainisha azma zao kwa maandishi na
kuweka bayana kuhusu maslahi ya raia wetu katika
ajira hizo.
90
WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kutangaza fursa za masoko zilizoko Wizara kwa kushirikiana na wadau wa sekta mbalimbali
Kenya na Uganda na kwingineko kwa imewezesha utoaji wa taarifa kuhusu fursa na
kutumia vyombo mbalimbali vya habari changamoto zilizoko katika Jumuiya. Aidha, vikao vya
yakiwemo Magazeti, Radio na sekta ya biashara vya kila mkoa vimetumika kutoa
Televisheni. taarifa muhimu kwa wafanyabiashara na wajasiriamali
nchini. Serikali imetoa fursa ya kuziwezesha Taasisi na
Sekta binafsi kutoa mapendekezo ya kuendeleza sekta
muhimu za uchumi zikiwemo viwanda na kilimo.
Jitihada hizo zinaonyesha mafanikio kupitia
mashauriano rasmi yanayofanywa kila mwaka kati ya
Serikali na Sekta binafsi chini ya uenyekiti wa
Mheshimiwa Rais.
2. Kuwahamasisha Waheshimiwa Semina kwa Waheshimiwa Wabunge zilifanyika mwezi
Wabunge kutumia mikutano yao na Machi/Aprili, 2007 kwa ajili ya kutoa elimu ya masuala
wapiga kura kuwaelimisha kuhusu ya Shirikisho la Afrika Mashariki, kutoa taarifa ya
umuhimu wa kukuza uzalishaji mali uamuzi wa kuziingiza nchi za Rwanda na Burundi
nchini ili Tanzania iweze kunufaika na katika Jumuiya pamoja na masuala ya utekelezaji wa
fursa inayotolewa na Jumuiya ya Afrika Umoja wa Forodha.
Mashariki.
3. Kufanya utafiti kuhusu nyanja za Kamati za kitaifa za kuchambua na kutafuta njia za
ushirikiano kwa lengo la kubaini ufumbuzi kuhusu masuala ya umoja wa forodha
vikwazo na kubuni mikakati ya hususan masuala ya vikwazo visivyo na kodi ziliteuliwa
kukabiliana navyo. katika nchi wanachama Mwezi Juni, 2006.
4. Kutumia Balozi zetu nchini Kenya na Balozi zetu zimekuwa zikishiriki kikamilifu katika
Uganda katika kuwawezesha mikutano ya sekta mbalimbali katika vikao vya Jumuiya
Watanzania kuendeleza biashara. na zimeiwezesha Serikali kupokea taarifa sahihi na
kamili kuhusu nchi za Kenya na Uganda kulingana na
makubaliano mbalimbali na Mkataba wa Jumuiya kwa
ujumla.
5. Kuwasiliana na Wizara, sekta binafsi Wizara imeratibu vikao mbalimbali kwa kushirikisha
na wadau wengine katika kubuni sera, sekta mbalimbali kwa ajili ya kupitia masuala ya vifungu
mikakati na programu za utekelezaji vya mkataba wa Jumuiya, masuala ya kijamii na elimu.
katika kukuza na kuendeleza uzalishaji Wizara imeshiriki katika majadiliano ya Itifaki ya
mali na biashara. Kamisheni ya Sayansi na Teknolojia katika kikao
kilichofanyika mwezi Machi, 2007, Zanzibar. Itifaki hiyo
imekamilika na kuwekwa saini na nchi wanachama
mwezi Aprili, 2007.
Aidha, Wizara ilishiriki katika kukamilisha vigezo kwa
ajili ya „centres of excellence‟ ambavyo vilipitishwa na
Jumuiya. Vituo vitakavyofaidika na utaratibu huu ni
pamoja na Mweka – Moshi, Chuo cha Sanaa –
91
Bagamoyo, Utalii College – Kenya na „Sorot School of
Aviation‟ ya nchini Uganda. Aidha, katika kukuza
matumizi ya Kiswahili katika Jumuiya, Muswada wa
Sheria kuhusu Kamisheni ya Jumuiya ya Kiswahili
unatarajiwa kuwasilishwa katika mkutano wa Bajeti wa
mwaka 2007/2008.
6. Kufanya maandalizi ya Kutosha katika Kuzishirikisha sekta mbali mbali kuandaa makala
majadiliano na Nchi Wanachama. mahsusi juu ya sekta zao kuhusiana na masuala ya
Soko la Pamoja. Aidha, Mwezi Aprili, 2007 Sekretariat
iliiteua Kampuni ya „MA consultants‟ ili kuandaa taarifa
ya awali kuhusu Soko la Pamoja. Taarifa hiyo inapitiwa
na kila nchi wanachama. Tarehe 22/6/2007 ilipitiwa na
Nchi yetu kwa kuhusisha wadau wa sekta za umma,
sekta binafsi na taasisi mbali mbali Tanzania Bara na
Zanzibar.
7. Kufanya tathmini ya utekelezaji wa Serikali imeshirikiana na wadau wa Sekta ya sheria na
Mkataba wa kuanzisha Jumuiya ya wadau mbalimbali mwezi Februari, 2007 katika kupitia
Afrika Mashariki na Itifaki zake kwa mapendekezo ya marekebisho ya Kifungu cha Mkataba
lengo la kubaini mafanikio au upungufu wa kuanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kinachohusu
wa utekelezaji na kuchukua hatua masuala ya Mahakama. Aidha, Mapendekezo ya
zinazostahili. marekebisho ya baadhi ya vifungu yalisainiwa na
Wakuu wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika
Mashariki katika Mkutano Mkuu wa Kilele wa Nane
(Summit) wa Wakuu wa Nchi uliofanyika mwezi
Novemba, 2006 mjini Arusha.
Marekebisho hayo yanalenga kuunda upya Mahakama
ya Afrika Mashariki kwa kuanzisha vitengo viwili yaani
kitengo cha Mahakama ya awali na kitengo cha
Mahakama ya Rufani. Kitengo cha Mahakama ya
Rufani kitatoa fursa ya rufaa kwa mtu ambaye
hataridhika na uamuzi wa Mahakama ya awali.
8. Kujifunza kutoka Kanda au Nchi Ushiriki wetu katika mikutano ya Kikanda kama vile
nyingine jinsi ya kuimarisha ushiriki wa SADC, WTO unawezesha Nchi kujifunza mahusiano
Tanzania katika Jumuiya ya Afrika mbalimbali ya kiuchumi na kibiashara yaliyopo katika
Mashariki na ukuaji wa Jumuiya Kanda nyingine.
yenyewe.
9. Kuratibu kwa karibu utekelezaji wa Wizara imekuwa ikishiriki na kuratibu vikao, mikutano
maamuzi mbali mbali ya vyombo vya inayohusu Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Jumuiya
Jumuiya ya Afrika Mashariki ukiwemo kwa ajili ya kufuatilia kwa karibu maendeleo ya Taasisi
Mkutano wa Wakuu wa Nchi hizo kama vile Kamisheni ya Ziwa Victoria, Bunge la
Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Jumuiya, Mahakama pamoja na Sekretariati ya
Mashariki, Baraza la Mawaziri la Jumuiya.
Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bunge na
Mahakama ya Jumuiya ya Afrika Aidha, Jumuiya iliandaa semina iliyolenga kujenga
92
Mashariki. mahusiano ya ndani baina ya Mabunge ya Nchi
wanachama na Bunge la Afrika Mashariki (enhancing
functional relationship between East African legislative
Assembly – EALA and national Assemblies). Semina
ilifanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 13-16 Agosti, 2006
na kuhudhuriwa na Wajumbe 150 kutoka Nchi
wanachama wa Jumuiya. Waheshimiwa Wabunge wa
Nchi wanachama na Waheshimiwa Wabunge wa
Bunge la Jumuiya.
10. Kuendelea kushawishi Nchi Tanzania imekuwa makini katika ushiriki wake katika
wanachama kuweka mkazo katika majadiliano mbalimbali kwa kuzingatia maslahi ya nchi
masuala yahusuyo maendeleo badala na wananchi kwa ujumla. Aidha, imehakikisha ushiriki
ya biashara pekee. wake kuwa sawa na Dira ya Taifa 2025, MKUKUTA na
Mikakati ya sekta mbalimbali Nchini.
11. Kujenga uelewa kwa Wananchi katika Wizara kwa kushirikiana na wadau wa Sekta
Mikoa yote ya Tanzania Bara na mbalimbali wameshiriki miezi ya Februari na Machi,
Visiwani, Sekta binafsi, Baraza la 2007 katika kutoa elimu na mafunzo kwa wananchi
Wawakilishi la Mapinduzi Zanzibar, kuhusu fursa na changamoto zilizo katika Jumuiya.
Wabunge na viongozi wa Serikali kwa Aidha, Wizara kwa kutambua nafasi waliyo nayo
ujumla kuhusu masuala ya Ushirikiano Waheshimiwa Wabunge katika kuhamasisha na
wa Afrika Mashariki. kuelimisha wananchi juu ya masuala ya Jumuiya,
iliandaa semina kwa wabunge mwezi Novemba, 2006
kuhusu Utekelezaji wa Umoja wa Forodha, Soko la
Pamoja na Mchakato wa kukusanya maoni ya
Wananchi kuhusu Shirikisho.
12. Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Kwa kushirikiana na Wadau wa sekta mbalimbali
Itifaki ya Umoja wa Forodha. wizara imeratibu utoaji wa elimu na mafunzo kuhusu
Umoja wa Forodha kwa wajasiriamali na wananchi
waishio mipakani kwa ujumla.
13. Kuratibu na kuandaa taarifa kuhusu Zoezi la kukusanya maoni ya wananchi kuhusu
maoni ya wananchi, sekta binafsi na uharakishwaji wa Shirikisho la Afrika mashariki kwa
wadau wengine kuhusu haja ya sehemu kubwa lilitumika pia kutoa elimu kwa wananchi
kuharakisha Shirikisho la Afrika kuhusu Jumuiya. Zoezi lilifanyika katika mikoa na
Mashariki (Fast Tracking of Political Wilaya mbalimbali Tanzania Bara na Visiwani. Mikoa
Federation). iligawanywa kwa kanda ili kuwezesha kuwafikia
wananchi walio wengi kwa urahisi. Zoezi lilizinduliwa
mwezi Oktoba, 2006 katika nchi za Jumuiya ya Afrika
Mashariki na linatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2007.
Aidha, Kamati ya Kitaifa iliandaa na kukamilisha taarifa
husika.
14. Kufuatilia kwa karibu miradi na Wizara iliratibu kwa karibu sana miradi na Programu za
programu za maendeleo endelevu ya Jumuiya hususan maendeleo endelevu ya Ziwa Victoria
ziwa Victoria na Ukanda wake. na miundombinu. Tanzania ilitoa kila msaada katika
kuihamisha meli “RV” Jumuiya kutoka Ziwa Nyasa na
93
kuipeleka Ziwa Victoria.
Meli husika itatumika kufanya tafiti mbalimbali
zinazohusu usafi na usalama wa ziwa, kiwango cha
uchafuzi wa mazingira na bioanuai ya Ziwa hilo. Vile
Vile itasaidia kutafiti kiwango cha utajiri na aina ya
samaki waliopo katika Ziwa hilo. Kamisheni
inayosimamia maendeleo endelevu ya ziwa imehamia
rasmi Kisumu nchini Kenya mwezi Desemba, 2006.
Baadhi ya Miradi ya maendeleo iliyopo katika bonde
hilo ni; Mradi wa usalama na uchukuzi katika Ziwa
Victoria (The Lake Victoria Safety and Navigation
Study); Mradi wa kuendeleza makazi kwa wananchi
waishio kuzunguka Ziwa Victoria katika jumuiya. Mradi
huu unaendeshwa kwa kushirikiana na UN – Habitat.
Aidha, mradi unashughulikia masuala ya maji na
utunzaji wa mazingira na makazi ya wananchi
kuzunguka Ziwa katika miji ya Kisii, Homabay, Muleba
na Bukoba. Mpango huu unatarajiwa kuhusisha miji 22.
(Lake Victoria Regional Water and Sanitation Initiative);
na Mradi unaosimamia uvuvi.
15. Kuajri watumishi wasiopungua 40 Watumishi 30 wa kada mbalimbali wameajiriwa kwa
katika mwaka 2006/2007 ambao kati mwaka 2006/2007.
ya hao ni wataalam wa masuala ya
fedha, biashara, uchumi, sheria,
sayansi ya jamii, takwimu na
mawasiliano.
16. Kuandaa mpango wa kuwapatia Kutokana na ufinyu wa bajeti jukumu hili
mafunzo wataalam wa Wizara katika halikutekelezwa mwaka 2006/2007, hivyo linatarajiwa
stadi za majadiliano (Negotiation kutekelezwa mwaka 2007/2008.
Skills), eneo ambalo ni muhimu katika
kufanikisha ushiriki wa Tanzania katika
Jumuiya.
17. Kuimarisha uwezo wa Wizara Serikali imewezesha kupatikana ofisi kwa ajili ya
kiutendaji kwa kuboresha mazingira ya Wizara katika jengo la NSSF – Waterfront pamoja na
kazi pamoja na kutoa mafunzo kwa kununua vitendea kazi na samani za ofisi ili kujenga
wataalam wa Wizara. mazingira bora ya utendaji kazi kwa watumishi.
18. Kuratibu kwa karibu zaidi maombi ya Nchi za Rwanda na Burundi zimeingizwa katika
Rwanda na Burundi ya kutaka kujiunga Jumuiya tarehe 18/6/2007 baada ya kusainiwa kwa
na Jumuiya ya Afrika Mashariki. “Accession Treaty”. Aidha, nchi hizo zimekubaliwa
baada kukamilisha vigezo maalum vilivyowekwa na
nchi wanachama kulingana na mkataba wa uanzishwaji
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
94
Vigezo viliwekwa katika sehemu kuu mbili ambazo
zililenga kupima mambo makuu ya msingi kuhusu
makubaliano juu ya Muundo wa Taasisi na Mkakati wa
maendeleo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Aidha
sehemu ya pili ilihusu maeneo maalum ya sekta
mbalimbali. Masuala yaliyopewa kipaumbele ni pamoja
na utawala bora, demokrasia, haki za binadamu, usawa
wa kijinsia na kumaliza migogoro ya kivita baina yao
wenyewe kwa wenyewe. Nchi za Rwanda na Burundi
watakuwa wanachama kamili ifikapo tarehe 1 Julai,
2007.
95
WIZARA YA ELIMU YA JUU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. IDARA YA ELIMU YA JUU
Kuwadhamini wanafunzi shahada Wizara imeendelea kudhamini wanafunzi wa shahada
ya kwanza 1,500 katika programu ya kwanza katika fani za Udaktari kwa mwaka wa
ya udaktari (MD) katika vyuo masomo 2006/07 kama ifuatavyo:
vikuu hapa nchini.
KCM – College 125
BUCHS 110
IMTU 65
HKMU 143
MUCHS 980
JUMLA 1,423
Kudhamini wanafunzi tisini (90) Wizara imeendelea kudhamini wanafunzi 90 raia wa
raia wa Uganda ikiwa ni Uganda ikiwa ni kutekeleza utaratibu wa kubadilishana
kutekeleza utaratibu wa wanafunzi wa shahada ya kwanza kwa mwaka 2006/07
kubadilishana wanafunzi wa kama ifuatavyo:
shahada ya kwanza katika vyuo
vikuu vya Afrika Mashariki. UDSM - 52
UCLAS - 14
MUCHS - 16
SUA - 08
JUMLA - 90
Kudhamini mafunzo wanafunzi Serikali imedhamini wanafunzi 5 raia wa China
watano, raia wa China, ikiwa ni kusomea utaalamu wa Lugha ya Kiswahili Chuo Kikuu
kutekeleza mkataba wa cha Dar es Salaam kwa mwaka 2006/07 ikiwa ni
ushirikiano kati ya Tanzania na kutekeleza mkataba wa Ushirikiano kati ya Tanzania na
China. China.
Kuendelea kuelimisha umma juu Imeelimisha umma kuhusu Sera ya uchangiaji wa elimu
ya Sera ya uchangiaji gharama za ya juu.
elimu ya juu.
Kukamilisha kazi ya kuhuisha
Imepitia rasimu ya Sera ya Elimu ya Juu ya mwaka
Sera ya Elimu ya Juu ya mwaka
1999 iliyohuishwa na ambayo imejadiliwa na wadau
1999.
mwezi Juni, 2007.
Kudhamini mafunzo ya Imeendelea na udhamini wa mafunzo ya wanataaluma
wanataaluma themanini (80) themanini (80) katika vyuo vikuu vya umma.
katika idara ambazo zina
upungufu mkubwa wa wahadhiri,
katika vyuo vikuu vya umma.
96
Kuongeza ushiriki wa rika husika Kuna ongezeko la kwa rika husika kwa Elimu ya Juu
katika Elimu ya Juu kutoka kutoka 0.27 mwaka 1997 na kufikia 1.269 kwa mwaka
asilimia 1.219 mwaka 2006/2007 2005/06. Lengo la Wizara ni kuongeza ushiriki wa
na kufikia asilimia 2.0 ifikapo Tanzania kwa rika hadi kufikia 2.0 mwaka 2010. Hii
mwaka 2010. inatokanana na ongezeko la udahili katika Taasisi za
umma na binafsi. Vile vile uanzishwaji wa Chuo Kikuu
cha Dodoma utasaidia kufikia azma hii.
2. IDARA YA ELIMU YA UFUNDI
Kudhamini mafunzo kwa Ilidhamini mafunzo kwa wanafunzi 1,754 katika ngazi
wanafunzi 1,754 katika ngazi ya ya Ufundi Sanifu katika Vyuo na Taasisi za Ufundi zilizo
Ufundi Sanifu katika Vyuo na chini ya Wizara
Taasisi za Ufundi zilizo chini ya
Wizara.
Sera ya Elimu ya Ufundi inaendelea kuboreshwa na
Kukamilisha kuhuisha Sera ya utaratibu wa kupata maoni kutoka kwa wadau
Elimu ya Ufundi ya mwaka 1996. unaandaliwa.
Wizara iligharimia mafunzo ya watumishi kumi na
Kugharimia mafunzo ya watumishi
wawili 12 wa Chuo cha Ufundi Arusha na Makao Makuu
kumi na wawili (12) wa Chuo cha
katika ngazi ya udaktari wa falsafa 4 na Shahada ya
Ufundi Arusha na Makao Makuu
Uzamili 8.
katika ngazi ya udaktari wa falsafa
(4), Shahada ya Uzamili (8).
Kuratibu na kugharamia mafunzo Wizara iliratibu na kugharamia mafunzo maalumu ya
maalum ya ualimu (Pedagogical ualimu (Pedagogical Skills) kwa wahandisi 23
Skills) kwa walimu wahandisi 23 walioajiriwa katika Chuo cha Ufundi Arusha.
watakaoajiriwa.
Kuhamasisha wasichana katika Uhamasishaji umefanyika katika robo ya tatu ya mwaka
shule za sekondari ili waweze wa fedha 2006/07 katika mikoa ya Mwanza, Iringa,
kujiunga na Elimu na Mafunzo ya Tanga, Morogoro na Songea.
Ufundi kwa wingi.
3. IDARA YA SAYANSI NA
TEKNOLOJIA
Kukamilisha utungaji wa Sera ya Rasimu ya Sera ya Taifa ya Utafiti iliwasilishwa
Taifa ya Utafiti. Sekretariati ya Baraza la Mawaziri.
Kukamilisha uandaaji wa Muswada wa sheria utaandaliwa mara tu
Muswada wa Sheria ya itakapokamilishwa uhuishwaji wa Sera ya Sayansi na
Kuendeleza Sayansi na Teknolojia (1996). Uhuishaji wa Sera ulianza mwezi wa
97
Teknolojia Tanzania. Februari, 2007. Mchakato wa urejeaji wa Sera ya
Kukamilisha uhuishaji wa Sera ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia kwa madhumuni ya
Taifa ya Sayansi na Teknolojia na kutunga Sera mpya ya Taifa ya Sayansi, Teknolojia na
Sheria Na. 7 ya mwaka 1986 Ubunifu, unaendelea.
iliyoanzisha Tume ya Taifa ya
Sayansi na Teknolojia.
Taratibu za uanzishwaji wa Taasisi ya Nelson Mandela,
Kuendelea na uanzishaji wa katika eneo la kudumu lililoko Karangai katika
Taasisi ya Kujenga Uwezo wa Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru, Arusha,
Maarifa na Kuendeleza Sayansi zinaendelea.
na Teknolojia nchini
itakayojulikana kwa jina la Taasisi
ya Nelson Mandela.
Wizara ilitoa jumla ya tuzo 119 kwa wanafunzi wa kike
Kuandaa mkakati wa kutoka shule 20 zilizofanya vizuri katika masomo ya
uhamasishaji wa wanafunzi wa Sayansi na Hisabati katika mitihani ya kumaliza kidato
kike ili waweze kujiunga katika cha nne mwaka 2006 18, kidato cha sita mwaka 2006
masomo ya sayansi, teknolojia na na 2007 25 vyuo vikuu, taasisi za serikali na binafsi za
uhandisi katika ngazi mbali mbali Elimu ya Juu na Ufundi 43. Aidha wizara pia ilitoa tuzo
za elimu. 33 kwa shule za sekondari zilizowezesha wanafunzi
hao kufanya vizuri katika masomo hayo.
Kukamilisha uundaji wa Kamati ya Rasimu ya mkakati inaendelea kukamilishwa. Taarifa
Kitaifa ya Elimu ya Sayansi nchini. ya Kikao cha Task Force iliyojadili makala mbalimbali
zilizoeleza umuhimu wa kuundwa kwa Kamati
imekwishaandaliwa na itajadiliwa, na Mkutano wa
Wadau pindi fedha zitakapopatikana. Aidha, Rasimu
ya WBLM kuhusu uundaji wa Kamati ime- tayarishwa,
inasubiri kujadiliwa katika Kikao cha Menejimenti.
4. IDARA YA SERA NA MIPANGO
Kuratibu utekelezaji wa Ilani ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha
Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005-2010, na kuandaa taarifa ya
Mapinduzi ya mwaka 2005. utekelezaji, unaendelea.
kuratibu utekelezaji wa miradi ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo 21, katika Taasisi
maendeleo inayoendelea na ile na Makao Makuu unaendelea kati ya miradi hiyo, 18 ni
itakayoidhinishwa katika kipindi miradi inayogharamiwa na fedha za ndani na 3
cha mwaka 2006/2007. inagharamiwa na fedha za nje.
Uanzishwaji wa Chuo Kikuu cha Dodoma umekamilika.
Kuratibu ujenzi wa Chuo Kikuu
kipya Dodoma.
98
Kuratibu Uhuishaji wa Sera tatu Sera zote tatu zimekabidhiwa kwa washauri waelekezi,
(3) za Wizara, (Sera ya Elimu ya Rasimu za awali zimewasilishwa Wizarani. Utaratibu wa
Juu, Elimu ya Ufundi na Sera ya kupata maoni ya Wadau unaandaliwa.
Sayansi na Teknolojia).
Kuratibu shughuli za Ushirikiano Wizara imeshiriki katika mikutano mbalimbali ndani na
wa Kimataifa. nje ya nchi.
Kukamilisha zoezi la uhuishaji wa Zoezi la ‟Maping Survey‟ limeanza na ripoti imetolewa
vyuo vya elimu (Rationalization of Juni, 2007.
Post Secondary Institutions).
Kukamilisha program nane (8) za Maandalizi ya mpango maalum (Quickwin Programme)
uwekezaji katika Elimu ya Juu na kwa ajili ya kuendeleza Elimu ya Juu na Ufundi
Elimu ya Ufundi. utakaofadhiliwa na Benki ya Dunia yanaendelea.
5. IDARA YA UTAWALA NA UTUMISHI.
Kuajiri watumishi 14 kwa ajili ya Watumishi 14 waliajiriwa kati ya hao 2 Makao Makuu
makao Makuu na Chuo cha na 12 Chuo cha Ufundi Arusha. Aidha, watumishi 22
Ufundi Arusha. wamepandishwa vyeo na 3 kuthibitishwa kazini.
Mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi yalitolewa
Kugharimia mafunzo mbalimbali kwa watumishi 47 ili kuwaongezea ujuzi maarifa na
ya watumishi thelathini (30) ya ufanisi katika utendaji wao kazi.
muda mrefu na mfupi ndani na nje
ya nchi.
Utaratibu unaandaliwa ili watumishi wengine
Kuendelea kutekeleza mkakati wa wahudhurie mafunzo hayo ili kufikia lengo lililowekwa.
kuwaelimisha wananchi na
watumishi kupitia vyombo vya Vyombo vya habari kama magazeti vimetumika
habari kuhusu taratibu za kupata kuelimisha wananchi juu ya taratibu za kupata huduma
huduma zinazotolewa na wizara. zitolewazo na Wizara.
Kutekeleza mfumo wa uwazi wa Utaratibu wa mafunzo elekezi kwa watumishi
upimaji utendaji kazi wa umeandaliwa.
watumishi wa umma.
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ndicho pekee
Kushirikiana na vyuo vya Elimu ya kilichohuisha mitaala yake na kuingiza masuala ya
Juu katika kuhuisha mitaala ili UKIMWI.
kuingiza masuala ya elimu ya
UKIMWI.
Iliendelea kushirikisha sekta binafsi katika utoaji wa
huduma zisizo rasmi (non-core services) Makao Makuu
Kuendelea kushirikisha sekta
binafsi katika utoaji wa huduma pamoja na Chuo cha Ufundi Arusha, hususan huduma
99
zisizo rasmi (non-core services) za ulinzi, usafi na chakula.
za ulinzi, mapokezi, usafi na
chakula makao makuu ya wizara
na Chuo cha Ufundi Arusha.
Siku ya UKIMWI ya Wizara iliadhimishwa kwa kufanya
Kuendelea kuhamasisha shughuli mbalimbali zinazohusu upimaji UKIMWI kwa
watumishi kupima afya zao kwa hiari, matumizi ya dawa za kurefusha maisha kwa
hiari hususan virusi vya UKIMWI waishio na virusi vya UKIMWI na kupunguza
na kutoa huduma kwa wale maambukizo ya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda
watakaojitokeza kuwa kwa mtoto. Pia iliandaa mwongozo wa kushughulikia
wameathirika na VVU/UKIMWI. taratibu za kutoa lishe na matibabu kwa watumishi
waishio na virusi ya UKIMWI.
6. CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
Kudahili jumla ya wanafunzi Kilidahili jumla ya wanafunzi 6,027, kati yao wanafunzi
4,075. wa Shahada ya kwanza ni 3,890 wanafunzi wa kike ni
1,400 sawa na 36% na Shahada ya Uzamili ni 2,137
wanafunzi wa kike ni 577 sawa na 27%.
Zoezi ni la kila mwaka na linaendelea katika vitivo na
Kuendelea na utaratibu wa taasisi
kuboresha mitaala kwa kuifanyia
tathmini kila mwaka.
Kuendeleza juhudi za kutumia Kiliendeleza juhudi za kutumia teknolojia ya
teknolojia ya mawasiliano (ICT) mawasiliano (ICT) katika kufundisha na kujifunza kwa
katika ufundishaji na kujifunzia kutumia Kituo cha Elimu Endelevu (Centre for
kwa kutumia kitengo cha “Centre Continuing Education), kuwafundisha wahadhiri mbinu
of Countinuing Education” (CCE) mpya na bora za kufundishia pamoja na kuimarisha
kuwafundisha wahadhiri mbinu mtandao wa ndani (Local Area Network).
mpya na bora za kufundishia
pamoja na kuimarisha mtandao
wa ndani “Local Area Network”
(LAN).
Kuajiri na kutoa mafunzo katika Wameajiri watumishi 281 wanataaluma 185 na
ngazi mbalimbali kwa wataalamu waendeshaji 96 katika ngazi mbalimbali kwenye idara
kwenye idara zenye upungufu 17 zenye upungufu mkubwa wa wafanyakazi.
mkubwa wa wafanyakazi.
Kiliendelea kushirikiana na taasisi za ndani na nje ya
Kuendelea kushirikiana na taasisi
nchi kugharamia utafiti kulingana na sera ya utafiti ya
za ndani na nje ya nchi
chuo.
kugharamia utafiti kulingana na
100
sera ya utafiti ya Chuo. Chuo
kitaweka juhudi zake kuhakikisha
kuwa matokeo ya utafiti
yanasambazwa kwa walengwa.
Kiliendelea kutumia mikakati mbalimbali pamoja na
Kuendelea kutumia mikakati kutoa mafunzo maalum kwa wasichana wanaotaka
mbalimbali pamoja na kutoa kujiunga na programu za sayansi, uhandisi na
mafunzo maalum kwa wasichana teknolojia, uchumi na takwimu, ili kuinua uwiano wa
wanaotaka kujiunga na programu wavulana kwa wasichana.
za sayansi, uhandisi na teknolojia,
uchumi na takwimu; ili kuinua
uwiano wa wavulana na
wasichana.
Kiliendeleza ujenzi wa madarasa mawili yenye
Kukamilisha ujenzi wa madarasa uwezo wa kutumiwa na wanafunzi 1,000 kila moja
makubwa mawili yenye uwezo wa kwa wakati mmoja. Ujenzi umefikia asilimia 70.
kutumiwa na wanafunzi 1000 kila Kiliendelea na ukarabati wa Mabweni ya
moja kwa wakati mmoja. wanafunzi hususan bweni Na. 2 na Na. 5.
Kukamilisha ujenzi wa awamu ya Kilikamilisha ujenzi wa msingi wa jengo la Utawala la
kwanza ya Taasisi ya Sayansi za Taasisi ya Sayansi za Bahari iliyopo Buyu Zanzibar.
Baharini iliyopo Buyu Zanzibar.
Ujenzi umekamilika.
Kukamilisha ujenzi wa kitengo
kitakachotumiwa na kituo cha
ujasiriamali.
Ujenzi wa awamu ya kwanza ya mradi wa Mlimani City
Kuendelea na ujenzi wa awamu
umekamilika.
ya kwanza ya mradi wa “Mlimani
City”.
Kuendeleza majadiliano na Kilikabidhiwa majengo yaliyokuwa ya Kampuni ya Simu
Kampuni ya Simu Tanzania Tanzania (TTCL) yaliyoko Kijitonyama, kwa ajili ya
(TTCL) ili chuo kikabidhiwe rasmi Kitivo cha Uhandisi Umeme na Mifumo ya Kompyuta
majengo ya kilichokuwa Chuo cha cha Kampasi ya Uhandisi (COET).
Wafanyakazi wa Kampuni ya
Simu eneo la Kijitonyama.
7. CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA
KILIMO
Kudahili jumla ya wanafunzi wa Kilidahili jumla ya wanafunzi 1,089 kati ya hao Shahada
shahada ya kwanza 820 na 300 ya kwanza ni wanafunzi 820 wanafunzi wa kike wakiwa
wa shahada za juu. ni 33% na Shahada Uzamili 269 wanafunzi wa kike
101
wakiwa 30%.
Kuimarisha mafunzo ya shahada Mitaala ya shahada zote za kwanza na za juu inapitiwa
za kwanza, uzamili na shahada za upya ili ziweze kuvutia na ziendane na mahitaji ya
Juu za Falsafa. soko.
Kuimarisha miradi ya utafiti Kiliimarisha tafiti zinazolenga kuboresha kilimo, mifugo
unaoshirikisha wakulima. na maliasili mfano kilimo cha mboga na matunda katika
vijiji vya Mvomero, Mgeta, Mkuyuni, Kiroka, Matombo
na Bunduki mkoani Morogoro.
Kufanya warsha/kongamano za Kilifanya warsha/kongamano 19 za kisayansi ambazo
kisayansi ambazo wanataaluma ziliwashirikisha wanataaluma na wadau ndani na nje ya
na wadau ndani na nje ya nchi nchi.
watajadili matokeo ya utafiti na
matumizi yake.
Kuendesha kozi fupi, warsha,
mikutano na semina na kutoa Kiliendesha kozi fupi, semina na kutoa huduma za
huduma za ushauri wa kilimo, ushauri wa kilimo, utunzaji na usimamizi wa mali ya
utunzaji na usimamizi wa mali ya asili, misitu, na ufugaji kwa wakulima na wafanyakazi.
asili, misitu na ufugaji kwa
wakulima na wafanyakazi.
Kuendeleza miradi ya maendeleo
kama ifuatavyo:-
- Kukarabati majengo, Ukarabati wa mabweni 12 umeanza na mpango wa
(mabweni 5 na nyumba 20) kukarabati nyumba 20 za wafanyakazi unafanyiwa kazi.
na mtandao wa mabomba
ya maji.
- Kuanza ujenzi wa chanzo Kilikamilisha ujenzi wa maktaba iliyopo Kampasi ya
mbadala cha maji katika Solomon Mahlangu na jengo la Ujasiriamali na
Kampasi ya Solomon Biashara.
Mahlangu.
Kilikarabati madarasa 3, mabweni 12,maabara 1 na
- Kuendelea na ujezi wa nyumba za wafanyakazi 4.
vyumba viwili vya
mihadhara, vyenye uwezo
wa kukaa wanafunzi 500
kila kimoja kwa wakati
mmoja.
Utaratibu wa kununua samani hizo umekamilika.
- Kununua samani kwa ajili ya
Tayari mzabuni ameteuliwa.
102
maabara ya Zoolojia, Jengo
la Ujasiriamali na Biashara,
na Jengo la Maktaba lililopo
Kampasi ya Solomoni
Mahlangu.
8. CHUO KIKUU MZUMBE
Kudahili jumla ya wanafunzi elfu Kilidahili wanafunzi 816 wa Shahada ya kwanza, kati ya
moja (1000) hao wanafunzi wa kike ni 358 sawa na 44% na wa
kiume ni 458. Aidha Chuo kilidahili wanafunzi 282 wa
Shahada ya Uzamili kati yao wanafunzi 133 ni wa kike
sawa na 47%.
Kukamilisha ujenzi wa mabweni Taratibu za kupata michoro kwa ajili ya Mradi huu
ya wanafunzi yenye uwezo wa zinaendelea.
kuhudumia wanafunzi elfu moja
(1,000) pamoja na ofisi za
wahadhiri.
Kilikamilisha upanuzi wa maktaba ya Chuo, kampasi ya
Kujenga maktaba yenye uwezo
Mzumbe.
wa kuhudumia wanafunzi 1,000
katika Kampasi ya Mbeya.
Kujenga ukumbi wa mihadhara
wenye uwezo wa kutumiwa na Kiliendelea na ujenzi wa ukumbi wa mihadhara wenye
wanafunzi 300 katika Kampasi ya uwezo wa kutumiwa na wanafunzi 300 katika kampasi
Mbeya. ya Mbeya. Ujenzi huu utakamilika mwezi Septemba,
2007.
Kuendelea kusomesha wahadhiri Kilisomesha Wahadhiri watano (5) shahada ya uzamili
14 ngazi ya Shahada ya Udaktari na tisa (9) masomo ya Shahada ya Uzamivu.
wa Falsafa na 13 ngazi ya
Shahada ya uzamili.
Kukamilisha tafiti 5 maeneo ya Kilikamilisha tafiti ishirini na moja (21) katika maeneo ya
Sayansi ya Jamii. Sayansi ya Jamii, maeneo hayo ni;
- “Public Private Partnership”
- “Environment”
- “HIV/AIDS”
- “Financial Management”
- “Administration”
Kununua kompyuta 100 kwa ajili Kilinunua kompyuta 130 kwa ajili ya kuboresha
103
ya matumizi ya wahadhiri. ufundishaji.
9. CHUO KIKUU HURIA CHA
TANZANIA
Kudahili jumla ya wanafunzi 5000 Kilidahili wanafunzi 3,868 kati ya hao Shahada ya
kwanza ni wanafunzi 3,354 wanafunzi wa kike wakiwa
987 sawa na 29% na Shahada ya uzamili 514 kati ya
hao wanafunzi wa kike wakiwa 58 sawa na 11%.
Kilikarabati ofisi za wafanyakazi Makao makuu na
Kuendeleza kuboresha ofisi za katika mikoa ya Iringa, Dodoma na kuzindua rasmi
wafanyakazi makao makuu na majengo ya mkoa wa Singida.
katika mikoa ya Iringa, Kilimanjaro
na Ruvuma, Rukwa, Mtwara na
Manyara.
Kuongeza idadi ya wafanyakazi Kiliongeza idadi ya wanataaluma na waendeshaji ili
wanataaluma na waendeshaji kuimarisha utendaji. Idadi ya wanataaluma imefikia
mikoani. 181, waendeshaji 166 na mafundi wa TEKNOHAMA
10.
Kuongeza maabara za kompyuta Vituo vya Mikoa ya Mtwara na Kinondoni vilipatiwa
katika vituo vya mikoa na kuweka maabara za kompyuta. Vituo hivyo pia vina mtandao
mtandao wa ndani “Local Area wa ndani (LAN). Uwekaji wa LAN katika vituo vingine
Network”(LAN) katika vituo 5 vya haujafanyika kwa sababu ya kutokuwa na majengo
mikoa. ambayo yanamilikiwa na Chuo katika Mikoa husika.
Kuanzisha mafunzo ya ngazi ya
cheti, stashahada na kozi fupi za Kilianzisha vituo vipya katika wilaya tatu (3) za mkoa
ujasiriamali ili kuimarisha uwezo wa Dar es salaam, ili kukabiliana na idadi kubwa ya
wa wananchi kushiriki kikamilifu wanafunzi.
kwenye “MKUKUTA”.
Kuanza utekelezaji wa mpango Hadidu za rejea (ToRs) zimekwisha andaliwa.
wa matumizi bora ya ardhi ya Mkandarasi amekwisha teuliwa ambaye ni UCLAS.
ekari 105 eneo liliko Kibaha. Kazi inatarajiwa kuanza mwezi Desemba, 2006.
Kuendelea kuongeza idadi ya Chuo kimeunda mfuko kwa ajili ya elimu ya wanawake
wanafunzi wa kike. (Women Education Fund). Chuo huhamasisha umma
kupitia majarida yake, vipeperushi, maonyesho na
mikutano ya ufunguzi wa mwaka mpya ili wanawake
wengi zaidi wajiunge na Chuo.
Idadi ya wanafunzi wanawake iliongezeka kutoka 689
mwaka 2005 na kufikia 1035 mwaka 2006, yaani
104
ongezeko la wanafunzi 346 wa Shahada ya Kwanza au
asilimia 50.2.
Idadi ya wanafunzi wa kike wa Shahada za uzamili
iliongezeka kutoka 52 mwaka 2005 na kufikia 118,
yaani ongezeko la wanafunzi 66.
Kuimarisha ushirikiano na Wizara Idadi ya wanafunzi wa programu ngazi ya cheti cha
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stashahada iliongezeka kutoka 371 mwaka 2005 na
kwa lengo la kuongeza idadi ya kufikia 570 mwaka 2006; yaani ongezeko la wanafunzi
walimu wanafunzi. 199.
Kuendesha mafunzo maalum kwa Chuo kimeanza kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa
walimu wa masomo ya Sayansi, baadhi ya Wakufunzi wa Vyuo vya Ualimu (Teacher
Hisabati na Teknolojia katika kituo Educators). Hadi sasa kimetoa mafunzo hayo kwa
cha “Open and Distance wakufunzi 150. Chuo kikatoa mafunzo kwa walimu
Education Learning wapatao 1500 wa shule za Sekondari ambao
Centre”(ODEL Centre), kilichopo hawakuwa na vyeti vya ualimu. Mafunzo hayo
makao makuu ya Chuo Kikuu yanatarajiwa kuanza mwezi Januari, 2007.
Huria.
Programu hii inaendeshwa na Vyuo Vikuu 10 kwa
pamoja. Vyuo hivyo ni pamoja na:
- Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki (East Africa
University – Putland Somalia).
- Chuo Kikuu cha Nairobi (Kenya).
- Mandlane Pedagogical University (Msumbiji).
- Chuo Kikuu cha Kyambogo (Uganda)
- Chuo Kikuu cha Zimbabwe.
- Chuo Kikuu cha Zambia.
- Chuo Kikuu cha Addis Ababa.
- Chuo Kikuu cha Amoud (Somalia).
- Chuo Kikuu cha Hargeisa (Somalia).
- Cho Kikuu Huria cha Tanzania.
Programme hii itaendeshwa kwa njia ya
mawasiliano huria (Online taught Programme).
Programme hii inawalenga Walimu na itatolewa
kupitia AVU.
Mpaka sasa mitaala (Curricula) imekamilika.
Awamu ya kwanza ya kuandaa vifaa vya kujifunzia
(authoring of study materials) imeanza. Awamu hii
inahusu uandaaji wa vitabu vya kujifunzia vya
Hisabati na Kemia.
Awamu ya pili itaanza mwezi Januari 2007 na
105
itahusu uandaaji wa vitabu vya Fizikia na Biolojia.
Vitivo vya Elimu vya vyuo vikuu vilivyotajwa
vitatakiwa kuandaa kozi za elimu ambazo
zitafundishwa katika vyuo vyote vilivyotajwa hapo
juu.
10. CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA
SAYANSI ZA AFYA MUHIMBILI
Kudahili jumla ya wanafunzi 300. Kilidahili jumla ya wanafunzi 331 kati ya hao wanafunzi
wa kiume ni 230 na wa kike ni 101 sawa na 31%.
Kukamilisha ukarabati wa hosteli Kilikamilisha ukarabati wa Mabweni ya wanafunzi
za wanafunzi zilizopo Barabara ya yaliyopo barabara ya Chole Dar es salaam.
Chole Dar es Salaam pamoja na
kuweka samani.
Kukamilisha ujenzi wa kumbi mbili Kiliendelea na ujenzi wa kumbi mbili (2) za kufundishia
(2) za kufundishia zenye uwezo zenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 350 kila moja
wa kuchukua wanafunzi 350 kila kwa wakati mmoja na vyumba 40 vya ofisi.
moja kwa wakati mmoja na
vyumba 40 vya ofisi.
Kuanza kujenga barabara katika Kiliendelea na uendelezaji wa miundombinu ya Chuo
ardhi ya Chuo iliyopo Kisokwa na huko Mloganzila Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na
Mloganzila. TANROADS
Kilikamilisha maandalizi ya kukifanya Chuo Kikuu kamili
Kukamilisha taratibu za cha Tiba na Sayansi za Afya (Muhimbili University of
kukipandisha hadhi kuwa Chuo Health and Allied Sciences-MUHAS).
Kikuu Kamili.
Kiliendelea na utafiti wa magonjwa ya binadamu
Kuendelea na utafiti wa magonjwa hususan UKIMWI (chanjo), Kifua kikuu, Malaria na
ya binadamu hususan UKIMWI, magonjwa ya wanawake.
Kifua kikuu, Malaria na magonjwa
ya wanawake.
Kukamilisha upanuzi wa maktaba
ya chuo kuitayarisha kuwa Kilikamilisha upanuzi wa maktaba ya Chuo.
maktaba ya Taifa ya Sayansi za
Afya ya Binadamu.
11. CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ARDHI
NA USANIFU MAJENGO
Kuimarisha utawala wa Chuo Chuo kimekamilisha zoezi la uaandaji wa Charter na
ikiwa ni maandalizi ya kuwa Chuo tayari limepitishwa na Baraza la Chuo. Mapendekezo
106
Kikuu Kamili kwa kukamilisha ya Charter yamewasilishwa Serikalini.
“Charter” ya Chuo na kupata
Mkuu wa Chuo na Makamu Mkuu
wa Chuo.
Kuongeza udahili wa wanafunzi
kwa asilimia 50 baada ya Kilidahili wanafunzi 466 wa shahada ya kwanza kati ya
kuongeza idara za taaluma kutoka hao 375 ni wa kiume na 91 ni wa kike sawa na 20% .
6 na kufikia 22.
Jumla ya tafiti 13 zimekamilika na tafiti 85 zinaendelea.
Kupanua shughuli za utafiti,
ushauri wa kitaalamu na matumizi
ya Teknolojia ya Mawasiliano.
Chuo kimeendelea kushirikiana na Vyuo Vikuu vingine
Kuendelea kutafuta wahisani
pamoja na mashirika ya misaada ndani na nje ya nchi
mbalimbali kwa shughuli za utafiti
katika shughuli za utafiti. Chuo kwa sasa kinashirikiana
na maendeleo.
na vyuo vikuu na mashirika ya misaada zaidi ya 30
kutoka ndani na nje ya nchi katika shughuli za utafiti.
Kuendelea na ukarabati wa Chuo kiliendelea kupata misaada ya shughuli za
mabweni, ofisi, madarasa, maendeleo kutoka NORAD na Carnegie Corperation.
barabara, mifereji ya maji na njia Aidha Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) wamekipatia
za umeme. chuo mkopo wa milioni mia tatu (TShs 300m) kwa
madhumuni ya kuongeza kumbi za mihadhara hapa
chuoni.
Kukarabati jengo la zamani la Chuo kimetekeleza awamu ya kwanza na ya pili ya
utawala kuwa maktaba. ukarabati wa mabweni ya wanafunzi ambao
umehusisha upakaji wa rangi, uwekaji wa nyavu za
kuzuia mbu, ubadilishaji wa milango mibovu na
uboreshaji wa mfumo wa umeme chuoni. Chuo
kimeendelea kuboresha mandhari yake ya nje na usafi
wa madarasa, maabara na maofisi kupiti wakandarasi
wa nje.
Ukarabati wa jengo umekamilika na tayari huduma za
Maktaba zimehamia kwenye jengo jipya. Maktaba
mpya ina uwezo wa kuchukua wasomaji 400 kwa
wakati mmoja na eneo la kompyuta kwa watumiaji100.
maktaba ya zamani ilikuwa na uwezo wa kuchukua
wanafunzi 70 na eneo la kompyuta kwa watumiaji 30 tu
kwa wakati mmoja.
Kuimarisha vifaa vya maabara Chuo kimepanua eneo la maabara kwa kukarabati
107
jengo lililokuwa likitumika kwa ajili ya uchapishaji
ambalo kwa sasa litakuwa sehemu ya maabara ili
liweze kuchukua vifaa vingi vya maabara hususani
vifaa ambavyo Chuo kimepata kutokana na msaada wa
Mamlaka ya Elimu Tanzania. Michoro ya eneo
imeandaliwa na kazi ya ukarabati imeanza na
inatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha.
Kuboresha huduma za wanafunzi Chuo kimejenga mabenchi ya nje kwa ajili ya wanafunzi
ikiwa ni pamoja na tiba na kujisomea na kufanya mijadala.
huduma za ushauri nasaha.
Mfanyakazi mmoja wa chuo amehitimu mafunzo ya
ushauri nasaha katika ngazi ya stashahada.
Chuo kimeingia mkataba na hospitali na Phamasi mbili
kwa ajili ya kuhudumia wanafunzi wakati wa dharura.
12. CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU
DAR ES SALAAM
Kudahili wanafunzi 500 wa Kilidahili wanafunzi 1,479 kati ya hao wa kiume ni 833
masomo ya Sayansi na 1000 na wa kike 646, sawa na 44%.
masomo ya Sanaa na Sayansi ya
Jamii.
Kuajiri walimu 106 na
Kiliajiri walimu 103 kati yao 3 wana Shahada ya
wafanyakazi waendeshaji 221 kati
Udaktari wa Falsafa, 39 Shahada ya Uzamili na 61
ya hawa walimu 75 ni kwa ajili ya
Shahada ya kwanza. Pia Chuo kiliajiri wafanyakazi
shule za Awali, Msingi na
waendeshaji 191 kati yao 66 ni walimu wa Shule za
Sekondari.
Awali, Msingi na Sekondari, shule hizo zinamilikiwa na
kuendeshwa kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo kwa
walimu wanafunzi.
Kupanua maktaba na kununua Kilipanua maktaba na kununua vitabu 316 vya
vitabu vya kufundishia na kufundishia na kujifunzia.
kujifunzia.
Vifaa vya maabara vimenunuliwa pia kwa udhamini
Kununua vifaa vya maabara. mkubwa wa TEA ambao walitoa msaada wa vifaa hivyo
vyenye thamani ya shilingi milioni mia moja (100M).
Kuongeza walimu wa sayansi na Ili kupata walimu bora chuo kimeweka malengo ya
lugha, na kuweka mkazo katika kusomesha walimu kufikia kiwango cha PhD. Mpaka
uzalishaji wa walimu bora na wa sasa chuo kimedhamini walimu 18 ambao wanafanya
kutosha katika lugha za kiswahili, Shahada ya Uzamili katika Chuo Kikuu cha Dar es
kiingereza na lugha zingine za Salaam.
kigeni.
108
Walimu watatu pia wamepata udhamini wa Wizara ya
Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, mmoja wao akiwa
ni mwalimu wa lugha ya Kiswahili
Kati ya walimu 18 wanaodhaminiwa na chuo, wawili
wanachukua Masters ya Kifaransa, - 2 Literature, 1-
Kiswahili na waliobaki wanachukua Masters za
masomo mbalimbali.
Kuongeza walimu wa sayansi, Chuo kimeanzisha
programu ya Pre-entry kwa ajili ya wanafunzi wa kike ili
kuongeza idadi ya wanafunzi wanaojiunga na masomo
ya sayansi na hesabu na hatimaye kuweza kuongeza
idadi ya walimu wa sayansi na hisabati. Kwa mwaka
2006/2007 chuo kimedahili wanafunzi 53 wa kike
kutoka kwenye programu hii.
Chuo pia kinaandaa andiko kwa ajili ya kuboresha
ufundishaji wa lugha za Kifaransa na Kiingereza.
Andiko hizi zikikamilika zitawasilishwa ubalozi wa
Ufaransa na Uingereza kwa ajili ya misaada ya vifaa
vya kufundishia walimu na kusomesha walimu wa
kifaransa na kiingereza katika kiwango cha Masters na
PhD.
13. CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA
USHIRIKA NA BIASHARA – MOSHI
Kudahili wanafunzi 300. Kilidahili wanafunzi 403 kati ya hao 69 ni kwa ajili ya
Diploma ya Uzamili na 334 ni kwa ajili ya Shahada ya
kwanza.
Kuendelea na mikakati ya Kiliimarisha mtandao wa kompyuta kwenye maktaba.
kuimarisha mtandao wa kompyuta
kwenye maktaba.
Kiliendeleza mafunzo ya wafanyakazi wanataaluma
Kuendeleza mafunzo ya
kumi (10) kufikia kiwango cha Udaktari wa Falsafa.
wafanyakazi wanataaluma kumi
(10) kufikia kiwango cha Udaktari
wa Falsafa.
Kuboresha shughuli za utafiti na Machapisho 4 yametolewa.
uchapishaji.
Kuendelea kuboresha kiwango Mafunzo ya wanachama wa SACCOS yamefanyika.
cha huduma za uelekezi na
ushauri.
109
Kozi ya kujenga uwezo wa uendeshaji wa SACCOS
Kuandaa programu na mipango inatolewa kwa njia ya Masafa na Chuoni.
ya kujenga uwezo wa wanachama
wa ushirika katika kuendeleza
vyama vyao.
Wanafunzi wameelimishwa kupitia warsha kuhusu jinsi
Kupambana na maadui UKIMWI UKIMWI unavyoambukiza na njia za kujikinga. Semina
na rushwa. zaidi zitaandaliwa kuhamasisha wanachuo kujikinga na
kupima.
14. CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU
MKWAWA
Kudahili wanafunzi 130 wa Kilidahili wanafunzi 917 kati ya hao, wanafunzi wa
stashahada na 870 wa shahada kiume ni 656 na wa kike 301 sawa na 33%.
ya kwanza.
Ukarabati wa mabweni umekamilika na tayari samani
Kuendelea na ukarabati wa mbalimbali zimeshanunuliwa. Aidha ukarabati wa
mabweni, madarasa na kuweka madarasa umekamilika ambapo vyumba 8 vya
samani. mihadhara na vyumba 10 vya semina vimewekewa
samani kwa ajili ya kufundishia.
Chuo kinaendelea na ukarabati wa vyumba vya
Kuweka samani na vifaa vya maabara na kwamba vifaa vya maabara
maabara ya Kemia, Elimu Viumbe vimeshaagizwa na baadhi vimeshapokelewa chuoni.
na Fizikia.
Chuo kimemaliza ukarabati wa jengo la maktaba na
Kukarabati na kupanua jengo la kimepokea fedha kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania
maktaba. jumla ya TShs. 50,000,000/= na Dola za Kimarekani
24,000 kwa ajili ya kununua vitabu na kompyuta.
Chuo imeendelea na ukarabati wa zahanati ya chuo
Kuendelea na ukarabati wa yenye uwezo wa kutoa huduma kwa wanachuo,
zahanati. waalimu, na familia zao, pamoja na jamii inayoizunguka
chuo. Zahanati hiyo, ina uwezo wa kulaza wagonjwa
40 kwa wakati mmoja. Chuo kwa sasa kimeanza
utaratibu wa kuigeuza zahanati hii kuwa kituo cha afya.
Kuanza ukarabati wa barabara, Ukarabati wa barabara na usawazishaji wa maeneo
miundombinu ya maji safi na maji “landscaping” bado haujaanza kutokana na ukosefu wa
taka. fedha. Shughuli hizi zinatarajia kuanza katika awamu
ya pili ya mpango wa maendeleo.
Kutoa mafunzo maalum kwa Utoaji wa mafunzo maalumu kwa wanafunzi wa kike
110
wanafunzi wa kike katika masomo katika masomo ya sayansi ili kuinua uwiano wa
ya Sayansi ili kuinua uwiano wa wanafunzi wa kike na wa kiume bado haujaanza kwa
wanafunzi wa kike na wa kiume. ville chuo ndio kwanza kimeanza na kinatarajia kuanza
mafunzo haya katika mwaka ujao wa masomo.
Kuajiri wafanyakazi mia moja na Chuo kimeajiri wafanyakazi waendeshaji 70 na
ishirini na saba (127) kati ya hawa wahadhiri 18. Aidha wahadhiri 7 wamehamishwa kwa
Wahadhiri ni hamsini (50),na muda kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Vile vile
Waendeshaji sabini na saba (77). chuo kimeweka utaratibu wa kuajiri waadhiri kutoka
vyuo vikuu vingine kwa muda (Part Time Staff).
15. TAASISI YA UANDISHI WA HABARI
NA MAWASILIANO YA UMMA
Kudahili wanafunzi 120 wa Ilidahili wanafunzi 301, kati ya hao wavulana ni 187 na
shahada ya kwanza na 20 wa wasichana 114, sawa na 38%.
shahada ya uzamili, ukiwa
mkupuo wa pili ngazi ya shahada.
Kuongeza madarasa mawili (2)
Iliongeza madarasa mawili yenye uwezo wa kuhudumia
yenye uwezo wa kuhudumia
wanafunzi sitini (60) kila darasa.
wanafunzi sitini (60) kila darasa.
Kuendesha Radio Mlimani FM na Iliendesha kituo cha Radio – Radio Mlimani FM kwa
kuanza kuendesha kituo cha kutoa ushauri wa kitaalam katika masuala ya habari,
Television kiitwacho “Mlimani mawasiliano ya umma, matangazo na utangazaji.
Television”.
Kuendelea kutoa ushauri wa Taasisi imetoa huduma ya utaalamu kwa kuendesha
kitaalam katika masuala ya kozi fupi na warsha juu ya masuala ya mawasiliano kwa
habari, mawasiliano ya umma, wafanyakazi wa Taasisi ya Kuzuia Rushwa (TAKURU).
matangazo na utangazaji. Vile vile Taasisi imetoa huduma kwa Ofisi ya Rais juu
ya MKUKUTA, kwa waandishi wa habari.
16. TAASISI YA TEKNOLOJIA DAR ES
SALAAM
Kudahili wanafunzi 647. Kati ya Ilidahili jumla ya wanafunzi 793 wa mwaka wa kwanza
hao wanafunzi 25 katika fani za katika programu za Shahada ya Uhandisi 278,
Kompyuta na (25) kwa ajili ya Stashahada ya Ufundi sanifu 411 na Cheti cha Ufundi
Mawasiliano ya Anga ili sanifu 104. Aidha, kati ya wanafunzi 411 wa
kupunguza pengo kati ya mahitaji stashahada ya Ufundi Sanifu waliodahiliwa, 23 ni wa
ya soko na wataalamu wa fani fani ya Uhandisi Migodi.
hizo.
Kuanza mafunzo ya Uhandisi Matayarisho ya Program yameishakamilika bado
Migodi “Mining Engineering” tunasubiri kibali kutoka NACTE mafunzo kuanza.
katika ngazi ya Ufundi Sanifu.
111
Kukamilisha matayarisho ya Ilikamilisha mtaala wa programu ya mafunzo ya
mitaala na taratibu za programu Shahada ya Uzamili ya Ukarabati (Culture of
ya mafunzo ya Shahada ya Maintenance).
Uzamili ya Ukarabati
(Maintenance Management).
Iligharimia mafunzo ya wafanyakazi 16 wa Taasisi
Kuendelea kutoa mafunzo ya katika masomo ya muda mrefu na 5 katika masomo ya
muda mfupi na muda mrefu kwa muda mfupi
wafanyakazi 43 wa Taasisi katika
nyanja mbalimbali kwa lengo la
kuongeza ufanisi katika kutoa
elimu bora ya ufundi.
Iliendesha mafunzo maalum kwa wanafunzi wa kike na
Kutoa mafunzo maalum kwa kufanikiwa kudahili 23 baada ya kupata sifa za kujiunga
wasichana ili waweze kujiunga na na Taasisi
elimu ya ufundi katika Taasisi ya
Teknolojia Dar er Salaam kwa
lengo la kuongeza uwiano wa
kijinsia.
(i) Kutayarisha mtaala wa kozi husika kunahitaji
Kutayarisha mtaala wa kozi ya TShs. 20 mill/= lakini kwa sababu ya ufinyu wa
mafunzo ya Ufundi Sanifu katika bajeti (OC) zimetengwa Tshs. 2 mill/= ambazo
fani ya “Multimedia Graphics and hazitoshi kukamilisha kazi hii.
Animation”.
(ii) Fedha hii itatosha kufanya utafiti wa mahitaji ya
soko ya mafundi wa fani hii tu (market survey).
Kuanza ujenzi wa jengo jipya kwa (iii) Ilikamilisha utafiti wa udongo sehemu ya ujenzi
ajili ya kuongeza madarasa, (soil testing), maombi ya kibali cha ujenzi,
maabara na ofisi za wafanyakazi. michoro ya ujenzi (structural drawings) na
taratibu za kumpata Msimamizi wa Ujenzi
(Consultant), kwa ajili ya kuanza ujenzi wa
“Teaching Tower” ili kuongeza madarasa,
maabara na ofisi za wafanyakazi.
17. TAASISI YA SAYANSI NA
TEKNOLOJIA MBEYA
Kudahili wanafunzi 175. Ilidahili wanafunzi 175 wa mwaka wa kwanza katika
ngazi ya Ufundi Sanifu kati yao 18 ni wasichana sawa
na 10% na 34 wa Stashahada ya Juu ya Uhandisi.
Kukarabati mabweni 2, mfumo wa Ukarabati haujafanyika. Fedha kwa ajili ya kazi hizi
maji taka na kuufanyia hazijatolewa.
marekebisho mfumo wa umeme.
112
Kununua na kukarabati mitambo, Hakuna mitambo na mashine mpya zilizonunuliwa
mashine na vifaa mbalimbali vya katika kipindi hiki kwa ajili ya ukosefu wa fedha.
kufundishia na kujifunzia. Ukarabati mdogo unafanywa na walimu.
Kuajiri walimu tisini na mmoja (91) Iligharamia mafunzo ya walimu 10. Kati ya hao 5
na wafanyakazi hamsini na watatu wanachukua mafunzo ya uzamili, 3 mafunzo ya
(53) wengine kulingana na mfumo udaktari wa falsafa na 2 wanasoma Shahada ya
mpya wa Taasisi. kwanza. Aidha, wafanyakazi 4 wasiokuwa walimu
wanasomea mafunzo mbalimbali hapa nchini.
Kuongeza udahili wa wanafunzi Kupitia utaratibu wa “Access Programme” Taasisi
wa kike katika kozi za imeweza kudahili wanafunzi 15 wa kike. Mwanafunzi
ufundi/uhandisi kwa lengo la aliyedahiliwa kupitia utaratibu wa kawaida wa
kuongeza uwiano wa kijinsia. wanafunzi waliomaliza kidato cha nne alikuwa mmoja tu
(1).
18. CHUO CHA KUMBUKUMBU YA
MWALIMU NYERERE
Kudahili wanafunzi 120 wa Hadi Alhamisi tarehe 19 Oktoba, 2006 wanafunzi wa
shahada ya kwanza. Shahada ya kwanza waliokuwa wamedahiliwa ni kama
ifuatavyo:-
(a) Shahada ya kwanza ya Siasa na Uendeshaji
wa Maendeleo ya Jamii – 43.
(b) Shahada ya kwanza ya Uchumi kuhusu
Maendeleo – 35 Jumla – 78.
Kuanza kuendesha programu ya Udahili wa Shahada ya kwanza umechelewa kukamilika
shahada ya kwanza ya Siasa na kutokana na ucheleweshaji wa mikopo kutoka Bodi ya
Menejimenti ya Maendeleo ya Mikopo. Chuo kilipokea orodha ya wanafunzi waliopata
Kijamii na Uchumi katika mikopo tarehe 9 Oktoba, 2006 wakati udahili wa
Maendeleo. wanafunzi wa Shahada ya kwanza ulianza tarehe 25
Septemba, 2006. kwa mujibu wa orodha kutoka Bodi
ya Mikopo, wanafunzi wa MNMA waliopata mikopo ni
83 (43.23%) katika wanafunzi 192 waliochaguliwa
kujiunga na mafunzo ya Shahada ya kwanza.
Mafunzo ya Shahada ya kwanza ya siasa na
Uendeshaji wa Maendeleo ya Jamii na Uchumi kuhusu
Maendeleo yalianza rasmi Jumatatu, tarehe 02 Oktoba,
2006.
Kuajiri wanataaluma 21 na Wahadhiri 22 na watumishi wengine 20 wameajiriwa na
watumishi wengine 20 ili kumudu Chuo kuanzia tarehe 01 Septemba, 2006. kuhusu
113
majukumu ya chuo. wahadhiri, mchanganuo ni kama ifuatavyo:-
(a) Wahadhiri Daraja la Pili – 14 (wote wana
Shahada ya Uzamili).
(b) Wahadhiri Daraja la Tatu – 8 (wote wana
Shahada ya kwanza).
Ajira ya Wahadhiri 22 imekiwezesha Chuo kuanza
mafunzo ya Shahada ya kwanza katika mwaka wa
masomo 2006/2007.
Kukarabati jengo la Utawala, (1) Ukarabati wa Jengo la Utawala ulianza katika
jengo la Uhuru, Jengo la mwaka wa fedha 2005/2006. Ukarabati huo
Mihadhara na Jengo la unaendelea vizuri na unategemewa kukamilika
Utamaduni. 2006/2007.
(2) Kuhusu ukarabati wa Jengo la Uhuru, Jengo la
Mihadhara na Jengo la Utamaduni ni kwamba
Zabuni ya “Prequalification” ilitangazwa na Bodi
ya Zabuni ya Chuo na ilifunguliwa tarehe 18
Septemba, 2006. Bodi ya Zabuni ya Chuo
iliwapitisha makandarasi watano wenye uwezo
wa kufanya kazi hiyo ya ukarabati. Uteuzi wa
mwisho wa mkandarasi haujafanyika kwa kuwa
bado Chuo hakijapata fedha za ukarabati huo.
Mara baada ya fedha kupatikana, uteuzi wa
mwisho utafanyika na kazi itaanza mara moja.
Kuendeleza wahadhiri kumi (10) Hadi sasa chuo kimefanikiwa kumpeleka mfanyakazi
na watumishi wengine watano (5) mmoja kusomea Stashahada ya Juu katika Ugavi.
kitaaluma na kitaalamu. Kuhusu wahadhiri ni kwamba jitihada za kujiendeleza
kitaaluma zilikwamishwa na uhaba wa wahadhiri. Chuo
kilikuwa na wahadhiri 12 tu wa kudumu. Baada ya ajira
mpya ya wahadhiri 22, kikwazo hicho hakitakuwepo
tena.
Kuandaa mpango Mkakati wa Chuo kimeingia mkataba na “National Institute for
Chuo wa Miaka 10. Productivity” wa kuandaa mpango mkakati.
19. CHUO CHA UFUNDI ARUSHA
Kudahili wanafunzi 418. Chuo Kimedahili wanafunzi 389 ikiwa ni asilimia 93.06
ya makadirio.
114
Kununua na kufunga mashine na Ahadi hii bado kutekelezwa kwa sababu fedha bado
mitambo mbalimbali kwa lengo la kupatikana.
kuboresha mafunzo.
Kuanza ujenzi wa maktaba mpya Fedha kwa ajili ya kujenga maktaba mpya bado
ili kukidhi na kuboresha huduma kupatikana. Hata hivyo Wizara imeendelea kununua
ya maktaba. vitabu vipya vya kiada na rejea.
Kutoa mafunzo maalum kwa Chuo kwa kupitia mkondo wa “Access Course”
wasichana ili waweze kujiunga na kimefanikiwa kudahili wanafunzi wa kike 13.
matumizi ya elimu ya ufundi kwa
lengo la kuongeza uwiano wa
kijinsia.
Kukarabati majengo, mitambo na Chuo kimetekeleza yafuatayo:-
vifaa mbalimbali. - Kukamilisha ukarabati wa jengo la wasichana.
- Kupaka rangi majengo ya madarasa pamoja na
jengo la utawala.
20. TUME YA TAIFA YA UNESCO
Kuratibu utekelezaji na kufanya Mwaka 2004/05 Tanzania ilipata miradi 6 na yote
tathmini ya miradi inayoendelea imetekelezwa. Taarifa za matumizi ya fedha na
na ile itakayoidhinishwa na tathmini za miradi hiyo zimewasilishwa UNESCO.
UNESCO kwa kipindi cha
2006/2007 kama ilivyoamuliwa Mwaka 2006/07 mpaka sasa miradi 2 yenye thamani ya
katika Kikao cha 33 cha Mkutano Dola za Kimarekani $ 40,000 imepokelewa; (i) Msaada
Mkuu wa UNESCO. wa dharura kwa shule ya sekondari Solifo, Songea, $
25,000 (ii) Warsha ya kuhamasisha Wabunge kuhusu
shughuli za UNESCO nchini, $ 15,000. Mipango ya
utekelezaji wa miradi hiyo inaandaliwa.
Kulishirikisha Taifa katika Kongamano kuhusu Mwaka wa Kimataifa wa Sayari
Maadhimisho ya kuutangaza Dunia lilifanyika Dar es Salaam tarehe 28/06/2006.
mwaka 2008 kuwa “Mwaka wa
Kimataifa wa Sayari Dunia” Kamati ya wajumbe 21 ya Ki-Taifa ya Mwaka wa
(International Year for Planet Kimataifa ya Sayari Dunia imeundwa.
Earth).
Rasimu ya Waraka wa Baraza la Mawaziri iliandaliwa
Kukamilisha mchakato wa
na kuwasilishwa Sekretariati ya Baraza la Mawaziri.
kuifanya Tume ya Taifa ya
Inasubiriwa kujadiliwa na Baraza la Mawaziri.
UNESCO kuwa chombo huru cha
Serikali.
Mapendekezo ya Muundo mpya wa Tume ya UNESCO
yamewasilishwa kwa Msajili wa Hazina kutolewa
maamuzi.
115
Huu ni Mradi wa miaka miwili wa UNESCO kwa nchi
wanachama Kusini mwa Jangwa la Sahara wenye
lengo la kuimarisha mafunzo ya Waalimu umeanza
rasmi Aprili, 2005.
Kuratibu mradi wa UNESCO wa UNESCO imetoa US $ 1,000,000 kwa Tanzania kwa
kuimarisha mafunzo ya walimu. ajili ya Mradi huu.
Hadi sasa, walimu 36 toka Tanzania Bara na 30 toka
visiwani wameishapata mafunzo ya muda mfupi.
Wakufunzi 32 Tanzania Bara na 35 Tanzania Visiwani
wamepata mafunzo ya wiki mbili kuanzia Agosti, 2006.
Kuratibu utekelezaji wa mradi wa Mradi unatekelezwa kwa ushirikiano na Taasisi ya
kujenga Utamaduni wa Ukarabati Teknolojia Dar es Salaam, (DIT), Ofisi ya UNESCO
Miundombinu na Vitendea Kazi Dar es Salaam, na UNESCO Paris. Mchanganuo wa
“Culture of Maintenance.” kutafuta fedha umewasilishwa UNESCO.
Kufuatilia ombi la Kuanzishwa Ombi la kuanzisha Kiti cha UNESCO cha Historia
kwa “UNESCO Chair” katika Chuo liliandaliwa na Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar
Kikuu cha Taifa cha Zanzibar ili (SUZA) na kupelekwa UNESCO Paris.
kukiwezesha kupata kituo cha
kumbukumbu za kihistoria Ofisi ya Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika
(History Resource Centre). masuala ya UNESCO mjini Paris inafuatilia
ukamilishwaji wa ombi hilo.
Kuandaa warsha ya kuhamasisha Warsha ilifanyika tarehe 26-29 Septemba, 2006 mjini
Mtandao wa Shule Mwanza.
zilizoshirikishwa katika shughuli
za UNESCO katika Kanda ya Wajumbe walikuwa walimu wa sekondari kutoka
Ziwa Victoria (UNESCO Unguja, Pemba, mikoa ya Mara, Kagera, Shinyanga,
Associated Schools Project Mwanza na nchi za jirani Kenya na Uganda, na
Network). viongozi wa juu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Ufundi walihudhuria.
Kuratibu mradi wa kutunza na Mradi unahusisha nchi zilikuwa mstari wa mbele katika
kuhifadhi kumbukumbu za harakati za Ukombozi Kusini mwa Afrika, ambazo ni
ukombozi Barani Afrika “Africa Afrika ya Kusini, Angola, Msumbiji, Namibia, Tanzania.
Liberation Movements Project” Zambia, na Zimbabwe.
(Mradi huu uko katika hatua za
kutafutiwa fedha). Lengo ni kuanzisha kituo cha kutunza kumbukumbu ya
historia ya harakati hizo.
Kiasi cha $ 200,000 zimetolewa na UNDP kupitia
UNESCO kwa ajili ya maandalizi ya awali.
116
21. TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA
Kuratibu na kusimamia usajili na Ukaguzi (Technical Visitation) wa vyuo hivi uliohusisha
upatikanaji wa “Charter” kwa vyuo wataalam wa ndani na nje ya nchi umekamilika.
vikuu 5 na vyuo vikuu vishiriki 3 Maandalizi muhimu ya kukamilisha “Charters”
vya Serikali. yanakwenda vizuri na kazi hii inategemewa kukamilika
kabla ya tarehe 31 Desemba, 2006 kama Sheria Na. 7
ya vyuo vikuu inavyoelekeza.
Kuendelea kuboresha taratibu za Zoezi hili ni la kudumu. Tume inaandaa miongozo
udahili. mbalimbali na inapanga kuwasiliana na wadau ili kuwe
na warsha katika nusu ya pili ya mwaka kuhusu
kuboresha udahili na kuepuka matatizo yanayojitokeza
mara kwa mara.
Kuendesha warsha ya wadau wa Maandalizi ya rasimu ya mfumo na mada kwa ajili ya
ubora wa elimu ya juu, kuhusu warsha yameanza.
mfumo wa tuzo za kitaifa
(National Qualifications
Framework).
Kuandaa na kuratibu maonyesho Maonyesho ya pili ya Elimu ya Juu, Sayansi na
ya pili ya Elimu ya Juu, Sayansi Teknolojia yalifanyika kwa mafanikio makubwa kwenye
na Teknolojia. ukumbi wa Diamond Jubilee toka tarehe 31 Agosti hadi
tarehe 2 Septemba, 2006.
Kuendesha semina za maadili na Semina hizi hazijafanyika. Mategemeo ni kwamba
utendaji kwa wataalamu zitafanyika 2007/2008.
wanaoshirikishwa katika tathmini
ya vyuo, programu na vyeti.
Kuratibu uendeshaji wa semina za Juhudi za Tume za kupata fedha kwa ajili ya
uongozi wa vyuo na ufundishaji. kuendesha semina hizi bado hazijafanikiwa.
Mategemeo ni kwamba semina hizi zitafanyika
2007/2008.
Kuendelea kutoa machapisho ya Hili ni zoezi la kudumu. Tume inatoa machapisho
kuelimisha umma na mbalimbali kwa madhumuni yaliyotajwa. Tume ina
kuhamasisha wawekezaji tovuti na pia inawasiliana na wadau mbalimbali na kila
kuanzisha vyuo vikuu bora vyenye inapotakiwa inatoa ushauri na maelekezo kwa
kutoa elimu inayozingatia mahitaji wanaokusudia kuanzisha vyuo.
ya Taifa na soko la ajira.
Kazi hii imeanza kufanyika baada ya Wizara kutoa
Kuimarisha mtandao wa teknolojia
“server” moja kwa Tume na kuvipa baadhi ya vyuo
ya mawasiliano ndani ya Tume na
kompyuta moja moja. Mategemeo ni kwamba vifaa
wadau wake.
vyote pamoja na programu zinazotakiwa kukamilisha
117
mfumo wa mawasiliano vitapatikana na kwamba kazi
itakamilika 2007/2008.
Kuendeleza ushirikiano na Tume ina ushirikiano wa karibu na mabaraza ya Ithibati
mabaraza ya Ithibati ya Elimu ya ya Elimu ya Juu ya Kenya na Uganda. Tume pia
Juu duniani. inashiriki kikamilifu katika shughuli za IUCEA na
kuhudhuria mikutano mbalimbali inayoandaliwa na
UNESCO, Association of African Universities, pamoja
na Asasi nyingine zinazojishughulisha na masuala ya
ithibati ya elimu ya juu.
Kuendelea na mapambano dhidi Hili ni zoezi la kudumu. Wafanyakazi wanakumbushwa
ya UKIMWI na rushwa. kila mara kuhusu masuala haya wakati wa mikutano.
Tume imepanga kuwa na walau semina moja kwa
wafanyakazi kuhusu mapambano dhidi ya ukimwi.
kabla ya mwisho wa mwaka 2006/2007.
22. TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA
TEKNOLOJIA
1. Kuhawilisha tekinolojia mbali (a) Teknolojia ya jiko bunifu kwa ajili ya kupunguza
mbali kwa wananchi. matumizi ya kuni na mkaa na uhifadhi wa
mazingira. Sekta isiyo rasmi imepatiwa mafunzo
kwa ajili ya utengenezaji wa majiko bunifu katika
mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Singida,
Shinyanga, Morogoro na Mbeya. Wananchi
katika maeneo haya wamehamasishwa na
mpaka sasa zaidi ya majiko elfu kumi (10,000)
yamesambazwa. Kufuatia mafanikio
yaliyopatikana katika mikoa hiyo, jitihada
zinafanyika kuwasilisha teknolojia hii katika
mikoa mingine ya Tanzania kwa kushirikiana na
taasisi ya Chuo Kikuu cha Calfonia, Bekerley.
(b) Teknolojia ya Umeme wa Jua Wananchi
wamehamasishwa kutumia umeme unaotoka
katika mionzi ya jua hasa kwa ajili ya matumizi
ya majumbani hasa zile sehemu ambazo hazina
umeme wa gridi ya taifa katika mikoa ya Iringa
na Mwanza. Matumizi yanayoshauriwa ni hasa
ya mahitaji ya taa, mawasiliano, radio, kompyuta
na television. Tayari yapo makampuni kadhaa
yanayouza vifaa na vipuli vyake hapa nchini.
(c) Mashine ya Upepo (Windmill) kwa ajili ya
kusukuma maji Uboreshaji wa mashine ya
kusukuma maji (wind water pump) unaendelea.
118
Inatarajiwa kujaribiwa huko Ifakara na mradi wa
RUBADA na huko Iringa.
(d) Matumizi ya Makaa ya Mawe (Coal-Biomass
Briquettes) Majumbani Badala ya Kuni
Kuokoa Misitu. Tume ya Sayansi na Teknolojia
imejenga uwezo wa kitaalamu kwa Kampuni ya
Kiwira ya Tukuyu, Upendo Group –
Sumbawanga na SPACE Engineering ya Dar es
Salaam kwa ajili ya kuboresha makaa ya mawe
yaweze kutumika majumbani.
(e) Matumizi ya Mkaa Bora (Biomass Briquettes)
kutokanana na masalia ya nafaka
(agricultural residues). Jitihada zimefanyika
kujenga uwezo wa kiwanda cha kutengeneza
mkaa bora kutokana na masalia ya
nafaka/mimea (agricultural/forest resdues) kwa
ajili ya matumizi ya majumbani badala ya mkaa
unaotokana na ukataji misitu na kuharibu
mazingira. Kampuni ya Umbwana Engineering
ya Dar es Salaam inaendeleza teknolojia hii
ambayo inatarajiwa kupelekwa Mufindi.
(f) Kuhawilisha Teknolojia katika Taasisi za
Utafiti Nchini.
Tume ya Sayansi na Teknolojia imeandaa kitabu
cha teknolojia mbalimbali “catalogue”
zinazotengenezwa na taasisi za hapa nchini.
Teknolojia hizo zinahusu sekta mbalimbali hasa
viwanda na kilimo. Taarifa hizi zitasambwa katika
ofisi za Makatibu Tawala Mikoa (RAS) na Wilaya
(DAS) kwa ajili ya kuhamasisha na kuwaongoza
wanachi sehemu za upatikanaji wa teknolojia hizo.
(g)Teknolojia ya Samadi ya Mifugo (Biogas)
Tume ya Sayansi kwa kushirikiana na Idara ya
Mifugo ya Wilaya ya Mbozi, Mbeya imeendelea
kutoa mafunzo kwa wananchi ya ujenzi wa
mitambo ya gesi ya “biogas” kwa ajili ya matumizi
ya Majumbani hasa kupikia na kuwashia taa.
Uwezo uliojengwa katika Idara hiyo ya mifugo
itasaidi kusambaza teknolojia hiyo katika wilaya ya
Mbozi kama nishati mbadala ya matumizi ya kuni
na mkaa. Mpango upo wa kushirikisha Magereza
katika mpango huu.
119
(h) Teknolojia ya ujenzi wa nyumba za gharama
nafuu.
Kikundi kimoja cha ujenzi cha Ukonga Mwembe
Madafu walipatiwa teknolojia hiyo. Juhudi ziko
mbioni kuwapatia teknolojia hiyo watengeneza
matofali wa mkoa wa Morogoro ili kuboresha
ubora wa matofali wanayozalisha.
Kufanya tathmini ya mahitaji ya
Tathmini katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na
teknolojia katika mikoa minne (4)
Morogoro inaendelea na iko karibu kumalizika. Mikoa
nchini ikiwemo Dar es Salaam,
ya Iringa, Mbeya na Dodoma itafuatia.
Morogoro, Iringa na Mbeya.
Kutoa elimu kwa wagunduzi na Kituo kipya cha kutoa ushauri na habari kuhusu hati
watafiti kuhusu umuhimu wa haki miliki kimekamilika na elimu ya uendeshaji wa kituo hiki
miliki (Interlectual Property Rights) ilitolewa Desemba 2006 na washauri kutoka WIPO na
na jinsi ya kutumia hataza BRELA. Warsha ya matumizi ya hati miliki kwa umma
(patents) kwa manufaa ya inaandaliwa kufanyika Februari 2007. Warsha moja
maendeleo. ilifanyika wakati wa PI & Today hapo 13 Septemba
2006 Mnazi Mmoja Dar es Salaam.
Kuandaa Benki ya Takwimu Tume imekwisha kupata mtaalamu atakayetengeneza
(database) ya wanasayansi nchini muundo wa Benki ya Takwimu (database). Mtaalamu
kwa ajili ya kubaini fani zao na huyu ataanza kazi hii mnamo mwezi Januari 2007.
kiwango cha elimu walichofikia na Kazi hii inategemewa kukamilika baada ya miezi 3.
maeneo wanayofanyia utafiti kwa Baada ya muundo kutengenezwa, taasisi mbalimbali
lengo la kusukuma maendeleo ya zitakaribishwa kuingiza taarifa zao kupitia tovuti ya
nchi kiuchumi na kijamii. Tume ambako muundo huo utakuwa umewekwa.
Kuendelea kufadhili utafiti wa Kutokana na ufinyu wa bajeti katika mwaka huu wa
kisayansi katika maeneo ya fedha, Tume inaendelea kufadhili miradi iliyoanzishwa
kipaumbele ya taifa na mwaka uliopita.
kuwawezesha wanasayansi
kubadilishana mawazo juu ya Vilevile, Tume imekusudia kutumia fedha kidogo
matokeo ya utafiti wao. zilizopatikana kuandaa miradi inayolenga kuleta
matunda kwa jamii na maendeleo ya Taifa. Mradi
ambao unaandaliwa hivi sasa unahusu:
“Matumizi ya sayansi na teknolojia katika uzalishaji na
utumiaji wa mazao ya mihogo na alizeti hapa
Tanzania”.
Lengo:
- Kupatikana kwa chakula cha kutosha
120
- Kuzalisha bidhaa nyingi za Viwandani
zitokanazo na muhogo na alizeti.
- Kutumia muhogo na alizeti kuzalisha
nishati (biofuels).
Kuimarisha mtandao wa taasisi za Taasisi moja ya utafiti na maendeleo (Ifakara)
utafiti na mendeleo, kupanua imeboreshewa miundombinu ya mawasiliano ya
Masjala ya utafiti, kustawisha internet hadi kufikia “broadband connectivity”.
matumizi ya mifumo ya Ujenzi wa Kituo mama (base station) umeanzwa
mawasiliano na habari vijijini; na kujengwa.
kuhamasisha wananchi kutumia
sayansi na teknolojia katika
harakati za maendeleo.
Kuandaa mkakati wa kufikisha
Sayansi, Teknolojia na Ubunifu
kwa wananchi kwa kutumia
Mifumo ya Ubunifu (Innovation
Systems).
23. TUME YA NGUVU YA ATOMIKI
TANZANIA
Kuimarisha huduma za Mtumishi mmoja anapata mafunzo ya MSc; Technician
matengenezo ya vifaa vya mmoja ameajiriwa; na mafunzo kwa watumishi wanne
elektroniki, mashine za “X-ray”, toka Taasisi mbalimbali walipata mafunzo ya ndani
kinga na upimaji wa mionzi katika TAEC, katika ukarabati wa vifaa vya mionzi na x-rei
vyanzo mbali mbali vya mionzi. vifaa 10 vya electroniki na mashine 8 za x-rei
zilikarabatiwa. Pia semina ya kinga ya mionzi kwa
wafanyakazi wa mionzi 42, ukaguzi wa vituo 42
vilifanyika na maombi 112 ya leseni zilishughulikiwa ili
kuimarisha kinga ya mionzi.
Kuratibu utekelezaji wa miradi ya Tume iliendelea kuratibu miradi 14 ya kitaifa na 24 ya
misaada na kikanda (Afrika) kikanda ambapo URT ilipata misaada ya karibu USD
inayogharamiwa na Shirika la 800,000 kwa mwaka wa 2006 hadi 30 Septemba, 2006.
Kimataifa la Nguvu za Atomiki Misaada hii, kupitia miradi hiyo katika taasisi
“Internationa Atomic Energy mbalimbali, ilikuwa katika vifaa, mafunzo na ushauri wa
Agency” (IAEA). kitaalamu katika matumizi ya Teknolojia ya nyuklia.
Kutoa elimu ya kinga dhidi ya Zoezi hili limesogezwa mbele kwa sababu ya ukosefu
madhara ya mionzi Ayonisha na wa fedha na matayarisho muhimu kutokamilika.
isiyo Ayonisha kwa Waheshimiwa
Wabunge.
Kuimarisha na kutoa miongozo ya Mfumo wa utumishi (scheme of service) umekamilika
uendeshaji wa shughuli na na kupitishwa na Hazina. Sheria ndogo za fedha na
majukumu ya Tume. utumishi ziko katika hatua ya kujadiliwa na Bodi ya
121
Tume.
Kukamilisha uanzishaji wa ofisi Baada ya kupata usafiri, mtumishi na kumfunza; na
Zanzibar katika kutekeleza kupata pango: zoezi hili lilisitishwa kusubiri uridhiaji wa
majukumu yanayohusiana na sheria ya Nguvu za Atomiki na Baraza la Wawakilishi
Sheria ya Nguvu za Atomiki ya Zanzibar ili iweze kutumika huko. Hivyo matayarisho
mwaka 2003. ya kuanzishwa ofisi yalikamilika na inasubiriwa Baraza
la Wawakilishi waridhie kutumika kwa sheria hiyo huko
Zanzibar sawa na katiba ya Zanzibar.
24. MAMLAKA YA ELIMU TANZANIA
Kuendelea kuhamasisha na Mamlaka ya Elimu Tanzania inaendelea kuhamasisha
kuelimisha wadau kuchangia na wadau mbalimbali. Katika kipindi cha nusu mwaka
kuwekeza kwenye miradi ya elimu imeshiriki kwenye maonyesho ya Utumishi wa Umma,
na kupanua wigo wa uchangiaji maonyesho ya Mwalimu Nyerere pamoja na
katika Mfuko wa Elimu kwa maonyesho ya Elimu ya Juu kwa lengo la kuelimisha
kushirikisha wadau katika ngazi wadau; aidha Mamlaka ya Elimu iliandaa harambee
ya Wilaya. mkoani Arusha kwa lengo la kuhamasisha uchangiaji.
Kushawishi uanzishwaji na Mamlaka ya Elimu Tanzania imekamilisha makubaliano
uendelezaji wa mifuko ya Elimu na ALAT kuendeleza ushawishi wa Halmashauri
ya Halmashauri za wilaya kuingia mashirikiano na Mamlaka ya Elimu Tanzania.
mbalimbali. Aidha, mamlaka Hadi sasa Manispaa za Ilala, Kinondoni pamoja na
itaendelea kushawishi ushirikiano Halmashauri za Maswa, Karagwe, Kasulu na Musoma
na mifuko hiyo ili kuchochea Mjini zimekamilisha taratibu zote za mashirikiano na
uchangiaji na maendeleo katika Mamlaka ya Elimu Tanzania.
elimu nchini.
Mamlaka ya Elimu Tanzania ilitembelea Kisarawe,
Mkuranga, Kibaha, Kyela, Kondoa, Babati na Hanang
kwa lengo la kuwasilisha mada katika vikao vya
madiwani juu ya dhana ya Mfuko wa Elimu na taratibu
za mashirikiano.
Kuendelea kutoa ruzuku na Katika utekelezaji wa ahadi hii TEA tunakusudia kutoa
mikopo kwa vyuo na shule kwa ruzuku na misaada ipatayo Sh. 3.7 Bilioni katika kipindi
ajili ya miradi mbalimbali ya cha mwaka 2006/07. Aidha kwa sasa tumefanya
kuboresha elimu, kuongeza uchambuzi wa miradi mbalimbali iliyopokelewa na
udahili na kuongeza usawa. tunategemea ipitishwe na Bodi hivi karibuni, miradi hiyo
inajumuisha vyuo vipatavyo 15 yenye thamani ya Sh.
1.37 Bilioni na ya shule 13 yenye thamani ya Sh. 273.4
milioni. Aidha tunaendelea kutafuta ufadhili kutoka nje
ya bajeti ya TEA.
Kuendelea kufanya ukaguzi wa Kwa kushirikiana na Ofisi za Wakaguzi wa Elimu wa
miradi iliyofadhiliwa na Mfuko wa Kanda pamoja na Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
Elimu. za Serikali; Mamlaka inaendelea kufanya Ukaguzi wa
122
miradi iliyofadhiliwa na Mfuko wa Elimu. Ukaguzi huo
unafanyika katika Vyuo vya Elimu ya Juu, Vyuo vya
Ufundi na Sekondari katika mikoa ya Tanzania Bara na
Zanzibar. Jumla ya miradi 29 itakuwa
imekwishakaguliwa hadi mwishoni mwa mwezi
Desemba, 2007.
Kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Katika kufanya maandalizi ya upimaji wa matokeo ya
ili kuongeza ufanisi. uboreshaji wa elimu kupitia kwenye Mfuko wa Elimu;
Mamlaka, kwa ushirikiano na wadau wengine wa elimu
inaandaa vigezo ambavyo vitatumika katika kufanya
tathmini hiyo.
Mamlaka iliendesha Semina kwa wafanyakazi wote
kuhusu maambukizi ya UKIMWI na jinsi ya kujikinga na
Ugonjwa huo. Aidha, Masomo kuhusu upimaji wa hiari
na Lishe Bora kwa wagonjwa wa UKIMWI
yalifundishwa.
Kuimarisha Mamlaka ya Elimu Mamlaka kwa kushirikiana na Idara ya Utawala Bora na
Tanzania kwa kuajiri wafanyakazi Ofisi ya Usalama wa Serikali (Government Security
kulingana na mahitaji. Office) ilifanya Semina kwa wafanyakazi wote kuhusu
Rushwa na Maadili ya Kiutendaji kazini.
Kuendelea na mapambano dhidi
ya maadui UKIMWI na rushwa.
25. BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI
WA ELIMU YA JUU
Kuanza kutumia chombo cha Chombo kimeanza kutumika na kinafanya kazi vizuri.
elektroniki (means Testing Chombo hiki kinafanya kazi kwa kutegemea taarifa
Software) chenye uwezo wa zilizojazwa kwenye fomu za maombi ya mikopo.
kutambua wanafunzi wahitaji wa Matokeo ya awali ya utumiaji chombo hiki yanaonyesha
mikopo na kuweka kiwango kwamba wanafunzi wengi wanawekwa katika kundi “B”
maalum ambacho muhitaji ambalo stahili yao ya mkopo ni asilimia 60. matokeo
anaweza kukopeshwa. haya yanaashiria kuwa wanafunzi wengi wanashirikiana
wakati wa kujaza fomu za maombi ya mikopo. Ili
kuondoa dosari hizo chombo hicho sasa kinafanyiwa
marekebisho, pia waombaji wanaelimishwa kuhusu
umuhimu wa kujaza taarifa sahihi kwenye fomu za
kuomba mkopo.
Kuendelea kutoa mikopo kwa Wanafunzi 8,023 wa vyuo vya elimu ya juu vya umma
wanafunzi wahitaji wa elimu ya na binafsi wamekopeshwa kiasi cha Tzs
juu wanaostahili katika maeneo 3,318,969,510.00 kwa ajili ya ada ya masomo katika
yafuatayo: kipindi cha Julai-Oktoba, 2006.
123
- Ada ya masomo, Wanafunzi 44,847 wa vyuo vya elimu ya juu vya umma
- Chakula na Malazi na binafsi wamekopeshwa kiasi cha Tzs
21,223,877,125.52 kwa ajili ya chakula na malazi.
- Vitabu na viandiko Wanafunzi 24,534 wa vyuo vya elimu ya juu vya umma
na binafsi wamekopeshwa kiasi cha Tzs
4,617,000,000.00 kwa ajili ya vitabu na viandiko.
- Elimu kwa vitendo Wanafunzi 2,001 wa vyuo vya elimu ya juu vya umma
na binafsi wamekopeshwa kiasi cha Tzs
775,662,000.00 kwa ajili ya elimu kwa vitendo
- Mahitaji maalumu ya vitivo Wanafunzi 4.038 wa vyuo vya elimu ya juu vya umma
na binafsi wamekopeshwa kiasi cha Tzs
217,744,660.00 kwa ajili ya mahitaji maalumu ya vitivo
Kuanza kukusanya madeni ya Jumla ya fedha iliyotumika kukopesha wanafunzi
mikopo iliyotolewa toka mwaka mpaka tarehe 15/11/2006 ni Tzs 30,558,688,295.72
1994/95.
(i) mawasiliano ya awali na taasisi zinazoajiri
wanufaika wa mikopo yamefanyika. Taasisi 552
zimepokea barua za kuomba kutoa kwa Bodi taarifa
za waajiriwa ambao wamenufaika mkopo.
(ii) “Database” ya wakopaji waliokwisha hitimu na
mahali wanakofanyia kazi imeandaliwa na
inaendelea kuimarishwa.
(iii) Baadhi ya wahitimu walionufaika na mikopo
wameanza kurejesha mikopo yao. Hii inajumuisha
pia wahitimu ambao wameajiriwa na Bodi ya
Mikopo.
(iv) Uhamasishaji kuhusu kurejesha mikopo
umefanyika kupitia vyombo vya habari yaani „press
release‟ na redio.
Mawasiliano na uongozi wa vyuo vya elimu ya juu
umefanyika kupitia njia ya simu, barua fax na pia
maafisa wa Bodi wamevitembelea vyuo ili kujenga
uhusiano mzuri na kupata taarifa sahihi.
Kushirikiana na vyuo vya elimu ya Mwezi wa Agosti, 2006 Bodi ya Mikopo ilikutana
124
juu na taasisi zingine kwa lengo la na wakuu wa vyuo vya elimu ya juu na viongozi
kuongeza ufanisi katika utoaji wa wa wizara na kujadiliana, kuweka mikakati ya
mikopo na ukusanyaji wa madeni ushirikiano baina ya Bodi, Wizara na vyuo.
kutoka kwa waliokopeshwa.
Tarehe 7 Oktoba, 2006 Bodi ilikutana na viongozi
wa Serikali za wanafunzi kutoka vyuo vyote vya
elimu ya juu na kupeana taarifa ya utekelezaji
kuhusu utoaji kuhusu utoaji mikopo. Katika kikao
hicho mikakati ya kuboresha huduma hivyo na
kuimarisha ushirikiano baina ya Bodi, Serikali za
Wanafunzi na uongozi wa vyuo ilijadiliwa kwa kina.
Kutoa elimu kwa wadau wa Elimu imetolewa kupitia vyombo vya habari yaani
mikopo – wanafunzi na umma magazeti, radio, tovuti “press conference” na pia
kwa ujumla kuhusu dhana ya vijarida vimesambazwa kwa wateja mbalimbali.
uchangiaji gharama za elimu na
suala zima la mkopo na Bodi ilishiriki maonyesho ya taasisi za elimu ya juu
urejeshwaji wake. tarehe 31/8/2006-2/9/2006 huko Diamond Jubilee Hall.
Katika maonyesho haya, jamii ilielimishwa kwa maelezo
ya mdomo pamoja na vijarida.
Tarehe 17-23 Juni 2006 Bodi ilishiriki maonyesho ya
Utumishi wa Umma katika viwanja vya Mnazi Mmoja.
Katika maonyesho haya jamii ilielimishwa kwa maelezo
ya mdomo pamoja na vipeperushi.
Kuendelea kuajiri wafanyakazi Hivi sasa Bodi ina wafanyakazi 37 ambao wako kazini.
waendeshaji wa Bodi ya Mikopo. Taratibu za ajira zimezingatiwa, wakurugenzi wanne
wamekwishateuliwa. Taratibu za “vetting” zinaendelea.
Nafasi zingine 45 za ajira zitatangazwa kipindi cha tatu
cha robo mwaka baada ya upanuzi wa ofisi za Bodi
zilizopo katika eneo la TIRDO-Msasani.
26. BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA
UFUNDI
Kukagua na kutathmini Vyuo 8 vimekaguliwa kwa ajili ya ithibati. Kati ya hivyo,
taasisi/vyuo vya ufundi 20 kwa ajili 7 vimepata ithibati ya muda. Chuo 1 kimeelekezwa
ya ithibati. kufanya marekebisho.
Kusajili vyuo 15 vyenye uwezo wa Vyuo 23 vimekaguliwa. Kati ya hivyo, 15 vimepata
kutoa elimu na mafunzo ya ufundi. usajili kamili na 8 vimepata usajili wa muda. Vyuo 4
vimeruhusiwa kuendelea na matayarisho kwa ajili ya
usajili.
Kuandaa na kuidhinisha mitaala Mitaala ya programu za mafunzo 8 imeandaliwa na
ya programu za mafunzo 20 kuidhinishwa.
125
yenye kuzingatia mahitaji ya soko
la ajira.
Kuratibu mitihani ya ufundi ya Baraza limeratibu mitihani ya Ufundi katika mfumo
kitaifa katika mfumo mpya wa mpya wa “National Technical Awards (NTA)” katika
“National Technical Award” (NTA) Vyuo 12 vinavyotumia mitaala mipya iliyoidhinishwa na
katika vyuo 17 ambavyo Baraza
vinatumia mitaala mipya
iliyoidhinishwa na Baraza.
Kusimamia na kuhakiki ubora wa Vyuo 21 vimetembelewa ili kuelekezwa namna ya
mafunzo katika taasisi/vyuo 30 kuboresha taaluma kwa kutumia vigezo na viwango vya
vya ufundi. ubora vilivyowekwa na Baraza.
Kuandaa taratibu na kanuni za Hadidu za rejea kwa ajili ya maandalizi ya taratibu na
kuidhinisha programu za mafunzo kanuni za kuidhinisha programu za mafunzo ya ufundi
ya ufundi kwa taasisi/vyuo vya nje nchini yatolewayo na Taasisi/Vyuo vya nje zimekamilika
zinazotaka kuendesha mafunzo tayari kwa hatua ya uzabuni.
hayo nchini.
Kuimarisha ushirikiano na baadhi Baraza lina ushirikiano na “International Association for
ya taasisi/vyuo vya ndani na nje Education Assessment”. Wawakilishi wa Baraza
vilivyo na majukumu wamekuwa wakitoa mada katika mikutano ya IAEA.
yanayofanana na Baraza hili. Baraza lina ushirikiano pia na CAPA (Commonwealth
Association of Polytechnics in Africa) na wawakilishi
wake walitoa mada juu ya mageuzi katika utoaji elimu
ya ufundi ili kukidhi mahitaji ya soko la ajira. Kikao
kilifanyika Lusaka Zambia tarehe 3-9 Desemba, 2006.
126
WIZARA YA NISHATI NA MADINI
NA. AHADI UTEKELEZAJI
Sekta ya Nishati
1. Katika kukabiliana na tatizo la umeme Mitambo ya kukodi ya kampuni ya AGGREKO na
nchini Serikali itakodi mitambo ya Dowans Holdings yenye uwezo wa kuzalisha jumla ya
uzalishaji umeme ya MW 100 na megawati 145 imefungwa Dar es Salaam. Aidha,
kuifunga Ubungo. mitambo ya Alstom Power Rentals yenye uwezo wa
kuzalisha MW 40 imefungwa Mwanza.
2. Grid ya Taifa ya umeme ya kV 220 Taratibu za awali za kuajiri mshauri mwelekezi ambaye
kutoka Iringa hadi Singida kupitia atafanya tathmini ya kiufundi pamoja na kutayarisha
Dodoma itaimarishwa. hadidu za rejea ya zabuni zimekamilika.
3. Hatua za utekelezaji wa miradi ya Katika mradi wa upanuzi wa gridi ya msongo wa kV 220
upanuzi gridi ya msongo wa kV220 kutoka Bulyankulu kwenda Geita, mtaalamu mshauri
kutoka Bulyanhulu kwenda Geita, na ameshaanza kazi, na Shinyanga hadi Buzwagi tathmini
kutoka Shinyanga hadi Buzwagi na ya ya mazingira na fidia zinaendelea.
msongo wa kV 132 kutoka Musoma
hadi Tarime zitaanza. Katika mradi wa upanuzi wa gridi ya msongo wa kV 132
kutoka Musoma hadi Tarime Memorandum of
Understanding na mwendelezaji wa mradi imesainiwa.
4. Taratibu za awali za ujenzi wa gridi ya Tathmini ya kupeleka umeme Kigoma kutokea Geita
msongo wa kV132 kutoka Tabora hadi kupitia Kibondo na Kasulu inaendelea.
Kigoma na kutoka Makambako hadi Upembuzi yakinifu wa Makambako-Songea
Songea zitaanza. umekamilika. Serikali ya Sweden inaangalia
uwezekano wa kugharimia mradi huu.
5. Mifumo ya usambazaji wa umeme Majadiliano na Benki ya Dunia bado yanaendelea kwa
katika miji ya Arusha, Moshi na Dar es ajili ya kuruhusu fedha zilizobakia wakati wa kutekeleza
Salaam itaboreshwa. mradi wa Songo Songo zitumike kuimarisha mifumo ya
usambazaji ya Arusha, Moshi na Dar es Salaam.
Majadiliano ya kina kati ya TANESCO na TANROADS
kwa ajili ya kutandaza nyaya yanaendelea.
6. Ujenzi wa kituo cha MW 6 eneo la a) Ujenzi wa Kituo Kuzalishia Umeme
Somanga Funga wilayani Kilwa chini
Mkandarasi amerudisha mashine na vifaa vingine na
ya mradi wa Songo Songo
ameanza kazi mwezi Aprili, 2007.Mitambo pamoja
utakamilishwa.
na vifaa vingine vimeshafika na ufungaji wa
mitambo na waya umekaribia kukamilika.
b) Ujenzi wa nguzo na waya za Umeme wa Gesi wa
kV 33
Usimikaji wa nguzo unaendelea na kazi
imekamilika kwenye kipande kati ya Somanga
/Singino na Hospitali ya Mchukwi. Eneo la Kibiti –
Ikwiriri kazi ya kusimika nguzo imeanza baada ya
zoezi la kulipa fidia kukamilika hivi karibuni.
127
c) Kuongeza Wigo wa Gridi (Grid Extension)
Ujenzi wa laini ya kV 33 kati ya Mwanambaya na
Mipeko umekamilika. Ujenzi wa laini ya kV 11
kutoka Charambe mpaka Mbande na Chamazi
umekamilika. Transfoma 10 zimekwishafungwa
katika vijiji vyote 5.
7. Kuendeleza mradi wa soko la umeme Mradi umewezesha kuweka mitambo ya umeme nuru
nuru mkoani Mwanza kwa lengo la (Solar PV) katika shule, Zahanati na Kituo cha Afya
kuondoa vikwazo vya matumizi ya kimoja katika Wilaya zote za mkoa wa Mwanza.
umeme nuru kama Nishati Mbadala.
Kitabu cha Solar kwa ajili ya Shule za Sekondari
kimekamilika na kuchapwa tayari kwa kusambaza
katika shule za Sekondari mkoani Mwanza. Baada ya
kukamilisha kuweka solar katika maeneo husika
mkoani Mwanza, moduli (solar modules) zilizobaki
zitapelekwa katika mikoa ya jirani ya Shinyanga na
Mara.
8. Umeme utasambazwa kwenye miji Kazi za upelekaji umeme katika makao makuu ya
mikuu ya wilaya ambazo ni Mbinga, wilaya hizi ni kama ifuatavyo:
Orkesmet, Ushirombo, Kilolo, Utete, na
Ludewa. Mbinga
Kazi za ukarabati mifumo na upanuzi wa njia ya umeme
wa msongo wa kilovoti 11 zinaendelea kufanywa na
TANESCO. Zabuni ya ununuzi wa mashine mpya za
2x1250 kVA imefunguliwa tarehe 24 Novemba, 2006 na
tathmini (evaluation) imekamilika. Mkandarasi kwa ajili
ya kufanya kazi hiyo amekwishapatikana na fedha za
kazi hiyo zimeidhinishwa.
Zabuni ya kazi za ujenzi (civil works) kwa ajili ya
matanki ya mafuta, na gereji imepitishwa na Bodi ya
Zabuni ya TANESCO kwa ajili ya kutangaza na kupata
mkandarasi.
Orkesmet
Zabuni kwa ajili ya ujenzi imepitishwa na Bodi ya
Zabuni ya TANESCO na Sida imeshatoa No Objection
kwa ajili ya kuingia mkataba wa ujenzi na Kampuni ya
Power Line Africa ya Namibia. Mazungumzo kwa ajili
ya Mkataba (Contract Negotiations) yalifanyika tarehe 6
Desemba, 2006. Lengo ni mkandarasi kumaliza kazi
mapema mwaka 2008.
128
Ushirombo
Mshauri wa utayarishaji upembuzi yakinifu wa mradi
huu, yaani, Kampuni ya SWECO ya Sweden
amemaliza kazi yake na Serikali imetuma maombi
rasmi kwa Shirika la Maendeleo la Sweden (Sida) ili
kufadhili mradi huu. Sida wameonesha nia ya
kuufadhili.
Kilolo
Upimaji wa awali wa njia ya umeme ya msongo wa
kilovoti 33 toka Iringa (Tagamenda) hadi Kilolo
umekamilika. Uandaaji wa vifaa vya ujenzi wa laini
unaendelea.
Utete
Ujenzi wa njia ya msongo wa kilovoti 33 kutoka kituo
cha Somanga hadi Utete –Ikwiriri na Bungu unaendelea
chini ya mradi wa Benki ya Dunia ujulikanao kama
Wayleave Electrification Scheme (WVES). Upatikanaji
wa umeme katika mji wa Utete utategemea kukamilika
kwa ujenzi wa kituo cha Somanga na ujenzi wa njia ya
umeme wa msongo wa Kilovoti 33.
Ludewa
TANESCO imeendelea na ujenzi wa njia za umeme
zenye msongo wa kilovoti 33 mjini Ludewa. Zabuni ya
ununuzi wa mashine mpya za 2x 600 kVA imefunguliwa
tarehe 24 Novemba, 2006 na tathmini imekamilika.
Ruhusa ya kutumia fedha kutoka Multilateral Debt
Relief Initiatives (MDRI) imetolewa.
Zabuni ya kazi za ujenzi kwa ajili ya matanki ya mafuta,
na gereji imeshapitishwa na Bodi ya Zabuni ya
TANESCO kwa ajili ya kutangaza na kupata
mkandarasi.
9. Kuendeleza vyanzo mbalimbali vya Majadiliano na wawekezaji wenye nia ya kuwekeza
nishati kama vile jua, upepo, katika kuzalisha umeme huko Makambaku mkoani
tungamotaka, maporomoko ya maji, Iringa na Kititimo mkoani Singida yalifanyika. Takwimu
joto ardhi na makaa ya mawe. za kasi ya upepo kutoka vituo viwili Makambaku na
Singida zilipatikana na kuonesha uwezekano wa
kuzalisha umeme.
Kwa kushirikiana na Geological Survey ya Tanzania na
Federal Institute for Geosciences and Natural
Resources (BGR) ya Ujerumani, Wizara ya Nishati na
129
Madini imefanya utafiti wa awali (reconnaissance)
katika eneo la Songwe – Mbeya, na sampuli za maji na
vipande vya miamba tayari zimepelekwa Ujerumani
kwenye maabara kwa ajili ya uchunguzi wa kina.
Serikali kwa kushirikiana na TANESCO inafanya utafiti
wa kuzalisha umeme katika maporomoko katika mikoa
7 nchini ambayo ni Morogoro, Iringa, Mbeya, Ruvuma,
Rukwa, Kigoma na Kagera. Tayari ukaguzi wa maeneo
umefanyika katika mikoa ya Rukwa, Ruvuma na Iringa.
Mawasiliano na wadau yalifanyika ili kuona jinsi ya
kuendeleza matumizi ya vitofali vya makaa ya mawe.
Sampuli za vitofali na jiko husika vilipelekwa maabara
kuhakiki usalama wa matumizi na ubora wa jiko.
10. Mradi wa umeme nuru unaofadhiliwa Shughuli za mradi zilizinduliwa katika mikoa ya
na Serikali ya Sweden kupitia Sida Morogoro na Pwani. Wafanyabiashara wa umeme nuru
utaanza kutekelezwa katika mikoa ya 12 katika mikoa hiyo walipewa mafunzo ya ukuzaji soko
Iringa Morogoro na Kigoma. la umeme nuru.
11. Kuendelea na utafiti wa jiko linalotumia Mradi wa Programme for Biomass Energy Conservation
mkaa, kuni lijulikanalo kama rocket. (ProBEC) chini ya SADC, unaendelea kuhamasisha
matumizi ya jiko bora la rocket. Katika awamu ya pili ya
mradi Kamati ya Ushauri (National Advisory Group)
iliundwa. Kazi ya kamati hiyo ni kuishauri Serikali
kuhusu utekelezaji wa mradi kwa manufaa ya
walengwa na Taifa kwa ujumla. Awamu ya pili ya mradi
ilianza kutekeleza shughuli zake kwa kutoa kipaumbele
katika maeneo kando kando ya barabara ya Morogoro
kupitia Iringa hadi Songea (Uhuru Corridor).
12. Kuendelea kutekeleza Mradi wa Mining Mfumo mpya wa utoaji wa leseni kwa njia ya kompyuta
Cadastral Information Management (FlexiCadastre) umeshaanza kutumika katika mchakato
System (MCIMS) wenye lengo la wa utayarishaji na utoaji wa leseni za madini kuanzia
kuunganisha ofisi 22 zilizoko mikoani ili Januari, 2007. Upungufu uliojitokeza unarekebishwa
kuwa na mawasiliano ya moja kwa kwa njia ya mtandao kadri unavyojitokeza.
moja yatakayowezesha kila ofisi kujua
hatua zilizofikiwa na Masjala Kuu ya Takwimu zote zinazohusiana na leseni na vibali vya
Madini na ofisi nyingine katika utoaji utafutaji na uchimbaji wa madini; biashara ya madini na
wa leseni za madini na malipo ya kodi vibali vya kusafirisha madini nje ya nchi chini ya Sheria
zinazostahili kwa kila leseni. ya Madini ya mwaka 1998 na Sheria ya Baruti ya
mwaka 1963, zimehamishiwa kwenye mfumo wa
FlexiCadastre. Uhakiki wa taarifa hizo unaendelea
kubaki na taarifa sahihi.
Zoezi la upimaji wa mipaka ya viwanja vya madini na
leseni za uchimbaji mdogo (PMLs) kupata alama za
kijiografia (geographical coordinates) kwa kila leseni
130
kwa nchi nzima lilianza mwezi Agosti, 2006 na
kukamilika mwezi Machi, 2007. Jumla ya leseni za
uchimbaji mdogo 4,166 kati ya 5,800 sawa na asilimia
72 zilipimwa katika zoezi hilo. Kama ilivyo kwa leseni za
uchimbaji mkubwa takwimu zilizopatikana zinaingizwa
kwenye Mfumo Mpya wa Utoaji wa Leseni
(FlexiCadastre) ili kurahisisha ufuatialiaji wa leseni hizo
katika kutimiza masharti mbalimbali ya leseni kwa
mujibu wa sheria. Masharti ya leseni za madini ni
pamoja na: kutoa ripoti za utendaji, taarifa za matumizi
ya fedha na gharama nyingine, taarifa za uzalishaji
madini yanayochimbwa, taarifa za mapato na malipo ya
maduhuli na kodi mbalimbali inavyohitajika kisheria.
Ujenzi wa mtandao (Wide Area Network) wa
mawasiliano utakaounganisha ofisi za madini kwa
kutumia njia ya satelaiti (VSAT) umekamilika. Mtandao
huu unaolenga kuwezesha mawasiliano ya papo kwa
papo (online) utawezesha upokeaji wa maombi ya
leseni za madini katika ofisi yoyote kati ya ofisi 21
nchini. Aidha, mtandao huu utawezesha ofisi kuelewa
hatua iliyofikiwa katika utayarishaji wa leseni
zinazohusiana na maeneo husika.
13. Kufanya marekebisho ya vipengele vya Baada ya Mapendekezo ya Kamati kuwasilishwa
Sera na Sheria ya Madini. Serikalini, Wizara ya Nishati na Madini iliyachambua na
kuandaa rasimu ya marekebisho ya Sera ya Madini ya
mwaka 1997. Kazi hiyo imekamilika, kwa sasa Wizara
inaandaa rasimu ya waraka wa BLM kwa ajili ya
kuwasilisha Mapendekezo ya Kurekebisha Sera ya
Madini ya Mwaka, 2007.
14. Kufanya ukaguzi katika maeneo ya Kwa kipindi cha Januari hadi Juni, 2007: ukaguzi
uchimbaji madini ya mikoa ya Lindi, ulifanyika katika maeneo ya uchimbaji madini ya mikoa
Mtwara, Tanga, Pwani, Dar es Salaam ya Lindi, Mtwara, Tanga, Pwani, Dar es Salaam na
na Morogoro. Morogoro. Maeneo ya uchimbaji yaliyofanyiwa ukaguzi
katika mikoa hiyo ni ya wachimbaji wa kati na
wachimbaji wadogo. Jumla ya viwanja 580 katika mikoa
hiyo ilikaguliwa kama ifuatavyo:
Lindi (Lindi Mjini-34, Ruangwa – 58, Kilwa- 62); Mtwara
(Mtwara Mjini-51, Masasi-70, Newala-2); Tanga
(Korogwe-13, Mkinga-10, Tanga Mjini- 11, Lushoto- 5,
Handeni- 35, Kilindi- 54); Morogoro (Morogoro Mjini-6,
Morogoro Vijijini-10, Mvomero- 100, Kilosa- 24, Ulanga-
20); Dar es salaam (Temeke- 12, Ilala-1). Jumla ya
viwanja vilivyokaguliwa ni 580.
131
Baadhi ya upungufu ulioonekana wakati wa ukaguzi wa
migodi hiyo ni pamoja na:
Wafanyakazi kutokuwa na vifaa vya kujikinga.
Migodi kutokuwa na taratibu za uokoaji (mining
rescue plan & emergency preparedness).
Ukosefu wa maji salama ya kunywa kwa
wafanyakazi wa migodi na ukosefu wa vifaa vya
huduma ya kwanza.
Utunzaji na utumiaji wa baruti usiozingatia sheria
na kanuni za baruti.
Mashimo kutozungushiwa wigo kwa ajili ya
usalama.
Baadhi ya wamiliki wa leseni za madini kutotoa
taarifa zao za uzalishaji madini Serikalini kwa
mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 1998.
Wamiliki wa viwanja hivyo waliagizwa kurekebisha
kasoro zilizoonekana wakati wa ukaguzi.
15. Kujenga mazingira bora ya kuongeza Serikali imeamua kudurusu Sheria ya Usonara
thamani ya Madini. (Goldsmith and Silversmith Ordinance). Maandalizi
yanafanyika ili yawasilishwe kwa wadau kupata maoni
kabla ya kuundwa kuwa Sheria ya Usonara. Warsha ya
wadau inatarajiwa kufanyika mwezi Septemba, 2007
ambapo muswada wa Sheria ya Usonara utawasilishwa
Bungeni kwa mara ya kwanza Februari, 2008 . Katika
jitihada nyingine za Serikali, Wizara imeanzisha chuo
cha kukata madini na kusanifu vinyago vya mawe
kinachojulikana kama “Arusha Gemstones Carving
Centre” na tayari chuo hicho kinatumika kufundishia
wanafunzi juu ya elimu ya ukataji wa madini ya vito na
usonara.
132
WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kukamilisha Sera ya Sekta ya Sheria. Rasimu ya kwanza tayari imeandaliwa na kuwasilishwa
kwenye kikao cha Makatibu Wakuu ili wakijadili na
kutoa maelekezo yao kama wadau. Aidha Rasimu hii
imesambazwa kwa wadau wengine kwa lengo la
kupata maoni yao.
2. Kuimarisha uendeshaji wa kesi na Serikali imeajiri Mahakimu Wakazi 70 na mahakimu wa
kupunguza mlundikano wa kesi Mahakama za Mwanzo115. Vile vile hivi karibuni
mahakamani kwa kuandaa programu ulifanyika uteuzi wa majaji 21 wa Mahakama Kuu na
maalum kwa ajili ya upunguzaji wa wawili (2) wa Mahakama ya Rufani. Majaji hao
mlundikano wa kesi katika Mahakama wamepangiwa katika vituo vya mikoani na wameanza
(Case backlog Disposal Programme kufanya kazi.
and Resident Magistrate Courts).
Ongezeko la Majaji na Mahakimu limeongeza kasi ya
usikilizaji wa kesi kwa kuongeza idadi ya vikao vya
Mahakama kutoka 12 hadi 15 kwa mwaka, kwa
Mahakama ya Rufani, na kutoka 88 hadi 102 kwa
mwaka kwa Mahakama Kuu. Mahakama za Mwanzo
zitaendelea kufanya vikao vya Mahakama vya kila siku.
3. Kuboresha huduma za kisheria,
kuimarisha usimamizi na uendeshaji
wa mashauri nchini kwa kutekeleza
yafuatayo:
Mchakato wa kutenganisha shughuli za upelelezi na
(a) Kutenganisha shughuli za upelelezi
uendeshaji mashtaka ulianza mapema baada ya
na shughuli za uendeshaji wa
marekebisho ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano
mashauri ya jinai mahakamani.
wa Tanzania. Marekebisho hayo yaliifanya Ofisi ya
Mpango wa majaribio utaanza
Mkurugenzi wa Mashtaka kuwa na Mamlaka ya
katika mikoa ya Arusha, Dar-
Kikatiba. Kwa mujibu wa marekebisho hayo,
Es-Salaam, Mwanza, Ruvuma,
Mkurugenzi wa Mashtaka anatakiwa kusimamia
Shinyanga na Tanga. Jumla ya
shughuli zote za uendeshaji mashtaka katika Tanzania
mawakili 104 wataajiriwa,
Bara. Kwa sasa shughuli hizo zinaendeshwa na Jeshi
magari 6 na majengo 6
la Polisi kwa sehemu, ingawa idara nyingine nazo
yatanunuliwa.
huchangia kwa kiasi fulani.
Rasimu ya Sheria itakayoanzisha mfumo wa Kitaifa wa
Uendeshaji Mashtaka (National Prosecution Service
Act) imeandaliwa na hivi sasa ipo katika mchakato wa
kuiwezesha kuwasilishwa Bungeni. Sanjari na Rasimu
hiyo umeandaliwa Mwongozo utakaosimamia mfumo
wa uendeshaji mashtaka nchi nzima. Hata hivyo
inatarajiwa kwamba utekelezaji wa Mpango huo
133
utakuwa wa hatua kwa hatua na kwamba mikoa ya
Arusha, Dar es Salaam, Mwanza, Ruvuma, Shinyanga,
na Tanga imeteuliwa kuwa katika awamu ya kwanza,
yote ikiwa na jumla ya wilaya 24.
Ili kuwezesha programu hiyo kuanza katika mikoa sita
ya awamu ya kwanza, yanahitajika mambo yafuatayo:
ajira za wanasheria wenye shahada 150 na watumishi
wa kada nyingine 12, majengo ya ofisi 24 na magari 24
katika mikoa na wilaya.
(b)Kuendeleza na kutekeleza Mkakati Taratibu za kupata fedha kupitia programu ya
wa majaji na Mahakimu kusikiliza kuboresha sekta ya sheria nchini, kwa ajili ya
mashauri kwa haraka na kwa haki kutekeleza Mpango huo zimeanza kufanyiwa kazi.
na kumaliza mashauri kati ya 6 na 7 Mkakati umetekelezwa sambamba na mkakati namba
katika kila mashauri 10 mbili (2) hapo juu kupitia uteuzi wa majaji 2 wa
yanayoandikishwa mahakamani. Mahakama ya Rufani; 21 wa Mahakama Kuu na ajira
za Mahakimu Wakazi 70 na Mahakimu wa Mahakama
za Mwanzo 115. Aidha, Kamati za Kusukuma Kesi
ziliendelea kutumika.
(c)Kuendelea kutumia utaratibu wa Majaji na Mahakimu wa ngazi zote wanaendelea
kalenda binafsi katika kusikiliza kutumia utaratibu wa kalenda binafsi katika kusikiliza
kesi. kesi, katika Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu
Mkazi, Mahakama ya Wilaya na Mahakama za
Mwanzo.
(d)Kuzipatia mahakama vitendea kazi: Mahakama Kuu, Mahakama za Hakimu Mkazi,
vifaa vya ofisi, usafiri na majengo na Mahakama za Wilaya na Mahakama za Mwanzo
vifaa vya kunasa kumbukumbu za zinaendelea kupata vitendea kazi, kama vile - vifaa vya
mwenendo wa kesi mahakamani. ofisi na vyombo vya usafiri. Magari 52 ya ukaguzi wa
Mahakama za Mwanzo tayari yamenunuliwa na
kugawiwa yote kwa Mahakama za Wilaya. Shughuli za
ujenzi na ukarabati wa majengo ya mahakama
mbalimbali umekuwa ukiendelea. Ujenzi wa Mahakama
Kuu Bukoba na Mahakama ya Hakimu Mkazi Manyara
unaendelea ambapo taratibu za ujenzi wa jengo la
Mahakama Kuu Shinyanga ziko katika hatua za awali
kabisa. Aidha ukarabati wa jengo la Makao Makuu ya
muda ya Mahakama ya Rufani ulikamilka na limeanza
kutumika.
Utekelezaji wa Mkakati huu unaenda sanjari na upanuzi
wa ofisi za Mahakama ya Biashara ya Mwanza ambayo
uzinduzi wake unatarajiwa kufanyika mapema mwaka
2007/08.
134
(e)Mahakama ya Biashara kufungua Kwa ujumla ziko masjala 13 kwenye Mahakama Kuu –
masjala katika Kanda ya Mwanza. Songea, Mbeya, Iringa, Dodoma, Tabora, Mwanza, Dar
Mahakama ya Ardhi kufungua es Salaam, Tanga, Moshi, Arusha, Sumbawanga,
masjala 2 ndogo katika mikoa ya Bukoba na Mtwara. Huduma za masjala katika mikoa
Shinyanga na Mara. ya Shinyanga na Mara hazijaanzishwa. Huduma za
masjala katika mikoa hii kutategemea upatikanaji wa
fedha.
(f) Kuendesha programu ya ujenzi wa Ujenzi wa Mahakama katika ngazi zote umeanza na
majengo ya Mahakama za ngazi unaendelea. Maandalizi ya kuanzisha ujenzi wa Chuo
zote, Chuo cha Sheria (Law cha Sheria yameanza kupitia Programu ya Kuboresha
School) na Jengo la Makao Sekta ya Sheria ambapo wafadhali wameanza kuweka
Makuu ya Wizara ya Katiba na fedha kwenye mfuko wa pamoja wa Programu kwa ajili
Sheria chini ya Programu ya hiyo.
Kuboresha Sekta ya Sheria chini
ya Mradi wa Accountability,
Integrity, & Transparency Project
in Tanzania (ATIP).
4. Kuboresha masjala zote katika Sekta Utekelezaji wa shughuli hii umeanza kwa kuandaa
ya Sheria chini ya Programu ya hadidu za rejea ili kumpata mtaalamu mwenye uwezo
Kuboresha Sekta ya Sheria kwa wa kufunga mfumo maalum wa mawasiliano kwa
kufunga mfumo maalum wa masjala na uendeshaji wa kesi.
mawasiliano.
5. Kwa kupitia Programu ya Uboreshaji Ahadi hii ya Serikali imeanza kutekelezwa na
wa Mazingira ya Biashara Tanzania kuwezesha kuandaliwa kwa rasimu ya awali ya mapitio
(MKUMBITA – BEST) sheria zifuatazo ya sheria zote zinazohusu mfumo mzima wa utoaji wa
zitafanyiwa marekebisho: haki katika masuala ya madai, (The Report on the
(a) Sheria ya Mwenendo wa kesi za Review of Civil Justice in Tanzania). Rasimu hiyo
Madai; imeweza kuandaliwa kupitia mchakato ulioainishwa
(b) Sheria ya Mawakili. hapa chini:
(c) Sheria ya Madalali wa Mahakama
Tume ya Kurekebisha Sheria imekabidhiwa
jukumu la kuratibu mchakato wa mapitio ya mfumo
mzima unaohusu haki katika masuala ya madai
(The Review of Civil Justice System in Tanzania)
kwa ajili ya kuboresha mazingira ya biashara
Tanzania.
Tume imeunda kikundi-kazi (Civil Justice
Technical Working Group) ambacho
kimeunganisha wadau muhimu kutoka katika
sekta mbalimbali ili kuweza kufanya kazi ya kupitia
Sheria hizo kwa lengo la kuzifanyia marekebisho.
Wadau hao ni pamoja na wawakilishi kutoka:
135
Benki, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,
Chama cha Wanasheria Tanzania, Kitivo cha
Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
Mahakama Kuu, Mahakama ya Rufani na Wizara
ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji.
6. Kuendelea kutoa ushauri wa Kisheria Ushauri wa Kisheria umeendelea kutolewa kwa
kwa Serikali kuhusu masuala mbali Serikali na taasisi zake, katika mikataba ya
mbali ya Sheria za Kimataifa. Kimataifa; mikopo, ubinafsishaji na uwekezaji;
masuala ya Katiba na Haki za Binadamu; Madai
na Jinai.
Jumla ya Mashauri 1,113 yalipokelewa, kati ya
hayo mashauri 386 yametolewa uamuzi na
mashauri 727 yanaendelea kusikilizwa. Vile vile
jumla ya Mikataba 230 ya manunuzi, na migogoro
5 ya masuala ya upatanishi (arbitrations)
inayoihusu Serikali imeshughulikiwa. Aidha, kesi
za Katiba na Haki za Binadamu zimeendelea
kusimamiwa na kutolewa ushauri wa kisheria.
Jumla ya kesi za Katiba 36 zilizofunguliwa, 18 kati
ya hizo zimemalizika.
Katika kujenga uwezo wa wataalam wetu katika
kutoa ushauri makini kwa Serikali, baadhi ya
Mawakili wa Kitengo cha tafsiri na urekebu wa
sheria wamepatiwa mafunzo ya muda mfupi ya
uandishi wa sheria.
7. Kuimarisha zaidi kitengo cha tafsiri na Kitengo hicho kimeongezewa wataalam 3 kutoka ofisi
urekebu wa Sheria kwa kukiongezea ya Mkurugenzi wa Mashtaka.
idadi ya Wataalam wa fani hiyo.
8. Mahakama ya Wilaya ya Kahama Mahakama za Wilaya ya Kahama na Karagwe ni
itapewa usafiri ili iweze kuhudumia pia miongoni mwa Mahakama za Wilaya 52 ambazo
Wilaya ya Bukombe wakati taratibu zimepatiwa magari kwa ajili ya kurahisisha uendeshaji
zinafanyika kujenga Mahakama ya wa shughuli za Mahakama ikiwa ni pamoja na ukaguzi
Wilaya ya Bukombe. Aidha, wa Mahakama za Mwanzo.
Mahakama zote za Wilaya ambazo Magari pia yamenunuliwa kwa ajili ya Majaji wapya 21
hazina magari ikiwa ni pamoja na wa Mahakama Kuu na wawili (2) wa Mahakama ya
Karagwe zitapatiwa magari mapya. Rufani.
9. Mahakama ya Wilaya ya Ruangwa Kutokana na uhaba wa Mahakimu katika kituo cha
kupatiwa huduma za Hakimu wa Lindi, zoezi la Wilaya ya Ruangwa kutembelewa na
Wilaya kutoka Wilaya jirani wakati Hakimu Mkazi wa Lindi halikufanyika. Hii ni kutokana
taratibu za kuanzisha Mahakama ya na kuacha kazi Mahakimu 2 na mmoja kufariki dunia na
Wilaya zikiwa zinaendelea. kufanya kituo cha Lindi kubakiwa na mahakimu 3 tu.
Hata hivyo hivi karibuni Mahakama imeajiri Mahakimu
wapya 77 ambapo watatu (3) kati yao wamepelekwa
Mahakama ya Mkoa Lindi na wengine wamehamia
kutoka wilaya nyingine.
136
Kutokana na hatua hizo, Mahakama ya Wilaya ya
Ruangwa itaanza kutembelewa kwa ratiba
itakayopangwa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Lindi.
10. Mahakama ya Wilaya ya Misungwi Wakati jitihada za kuipatia Wilaya ya Misungwi huduma
kupatiwa Hakimu wa Wilaya katika za mahakama ya wilaya zikiwa zinaendelea wananchi
mwaka wa fedha 2007/08. wa Misungwi wameanza kupatiwa huduma hiyo kwa
kutembelewa na Hakimu Mkazi wa wilaya kutoka
Ngudu, Kwimba.
11. Sheria ya Uandikishaji Vizazi na Vifo Wakala wa Vizazi na Vifo Tanzania (RITA) imeandaa
ipitiwe upya na kuboreshwa. hadidu za rejea na kuzipeleka "BEST na Legal Sector
Reform Program (LSRP)” ili kuomba fedha kwa ajili ya
kufanya kazi hiyo. LSRP tayari wameonyesha nia ya
kusaidia fedha kwa ajili ya kazi hiyo ya kupitia na
kuboresha sheria ya Uandikishaji wa Vizazi na Vifo.
12. Hukumu zote zenye maamuzi Utaratibu wa maamuzi makubwa ya kisheria (hukumu)
makubwa ya kisheria kuchapishwa huchapwa kwa wakati kwenye ripoti za kesi na kwamba
kwa wakati kwenye ripoti za kesi (Law ripoti za kesi zitatolewa hivi karibuni baada ya
Reports). kukamilika.
13 Serikali itaangalia namna ya Bado utaratibu huu haujafanyiwa maandalizi ili uweze
kuwatumia wanasheria ambao kutumika.
hawajaajiriwa kuweza kuwasaidia
Majaji katika kufanya utafiti.
14. Mahakama zote za Wilaya ambazo Ununuzi wa magari kwa ajili ya ukaguzi wa Mahakama
hazina magari ikiwa ni pamoja na unafanywa kwa awamu katika awamu hii, magari
Karagwe zitapatiwa magari mapya. yaliyoagizwa yanajumuisha gari litakalopelekwa Wilaya
ya Karagwe.
15. Kuendelea na jukumu lake la uandishi Hadi sasa jumla ya Miswada 25 imeandaliwa, sheria
wa Miswada ya Sheria, Serikali ndogo 250 zimehakikiwa na kuchapishwa katika Gazeti
itaandaa Miswada 25 na kuandika la Serikali. Sheria moja (1) imetafsiriwa katika Kiswahili,
sheria ndogo 500; kutafsiri sheria 10 na sheria nyingine 18 zimefanyiwa marekebisho.
katika lugha ya Kiswahili; na
kurekebisha sheria 30.
Uimarishaji wa Tume ya Kurekebisha Tume ya Kurekebisha Sheria imeimarishwa kwa
Sheria. kupatiwa vitendea kazi kama vile Kompyuta, kuajiri
watumishi na kuwapatia wengine mafunzo. Jumla ya
magari matatu (3) yamenunuliwa.
16. Tume ya Kurekebisha Sheria Tume ya Kurekebisha Sheria imeendelea kufanya
itazifanyia utafiti sheria zilizopitwa na shughuli za utafiti wa Sheria kwa ufanisi mkubwa na
wakati na kukamilisha taarifa za kuiwezesha kuandaa ripoti mbalimbali.
maeneo yafuatayo:
(a) Ushindani wa haki katika Rasimu ya mwisho ya ripoti kuhusu Sheria ya
biashara (competition Law); Ushindani wa Haki katika Biashara (Fair Competition
Law) inafanyiwa marekebisho kwa sasa.
137
(b) Usimamizi wa haki za Ugunduzi Tume imeshafanya utafiti wa kina juu ya usimamizi wa
na Uhamishaji wa Teknolojia Haki za Ugunduzi na Uhamishaji wa Teknolojia na
(Industrial property and Transfer kuandaa ripoti. Rasimu ya mwisho ya ripoti hii
of Technology & Pantents inafanyiwa marekebisho kabla ya kuwasilishwa kwenye
Protection). kikao cha Makamishna na hatimaye Wizarani kwa
Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria.
(c) Kufanya mapitio ya Sheria Tume imefanya utafiti wa kina juu ya Sheria za Mila
za Mila (Customary Law). kwa nia ya kuziondoa zile zinazowakandamiza
wanawake. Rasimu ya awali ya ripoti kuhusiana na
Sheria hii imeandaliwa kwa kuzingatia taratibu zote za
tafiti.
(d) Kufanya utafiti wa kisheria Tume ya Kurekebisha Sheria haikuweza kuanza kazi
kuhusu Usimamizi wa jumla wa ya utafiti juu ya Usimamizi wa Maliasili kutokana na
Maliasili (Natural Resources); kupewa kazi nyingine na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu
wa Serikali. Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliitaka
Tume kufanya utafiti wa kina kuhusu kuanzishwa kwa
Mahakama za Kadhi na kufutwa kwa adhabu ya kifo,
adhabu ya viboko na adhabu ya muda mrefu, na kutoa
ripoti katika mwaka wa fedha 2006/2007. Badala yake
kazi hii imepangwa kufanyika katika mwaka wa fedha
2007/2008.
(e) Ulinzi wa Haki za Watu wenye Tume ya Kurekebisha Sheria imefanya utafiti wa kina
ulemavu (Disability Law) juu ya Sheria za kutetea haki za watu wenye ulemavu
na Rasimu ya awali ya marekebisho ya Sheria ya
watu wenye ulemavu imeandaliwa na inatarajiwa
kujadiliwa katika mkutano wa wadau siku za hivi
karibuni.
(f) Kufanya mapitio na utafiti wa Utafiti wa kina umefanyika juu ya Teknolojia ya
kuainisha Sheria itakayosimamia kutambua chembechembe za vinasaba (DNA) ikiwa ni
matumizi ya teknolojia ya pamoja na warsha ya kukusanya maoni ya wadau
Chembe za asili za urithi (DNA). ambayo yatajumuishwa kwenye ripoti ya zoezi hilo.
17. Kusimamia masuala ya haki za Utaratibu wa masuala ya Haki za Binadamu
Binadamu na Utawala Bora na Mambo unatekelezwa vizuri kwa kuisimamia Serikali katika
ya Katiba. chunguzi za Kimataifa za uvunjaji wa haki za binadamu.
Chunguzi moja inayohusu kuondoa adhabu ya Kifo
Taarifa ya utekelezaji wa Mkataba katika Sheria ya Kanuni za Adhabu Sura ya 16 ni moja
wa Kimataifa juu ya Haki za ya masuala yaliyofanyiwa kazi.
Kiuchumi; Kijamii na Kiutamaduni.
Kutoa tafsiri ya Katiba ya nchi kwa Tafsiri ya Katiba kwa lugha ya Kiingereza iliandaliwa
lugha ya Kiingereza na pia kwa madhumuni ya kutumika wakati wa Uchaguzi Mkuu
138
kutoa vitabu vidogo vya Katiba hiyo. wa Mwaka 2005. Rasimu hiyo itafanyiwa kazi zaidi ili
kupata Katiba rasmi iliyotafsiriwa kwa Kiingereza.
Kuimarisha utoaji wa haki kwa Tume ilikagua Magereza 35 na vituo vya Polisi 53
umma hususan Haki za katika wilaya 33 za Tanzania Bara ili kuona hali ya
Binadamu, jumla ya Wilaya 4 na Mahabusu na utekelezaji wa haki za binadamu na
Magereza 16 yatatembelewa na misingi ya utawala bora. Mikutano ya hadhara ilifanyika
Wizara. kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi. Idadi ya
malalamiko yaliyoshughulikiwa ni 3,006 sawa na
asilimia 43.1. Malalamiko mapya yaliyopokelewa katika
kipindi hicho ni 4,442 na ya zamani yalikuwa 5,860 na
kufanya jumla ya malalamiko kuwa 10,302. Kati ya
malalamiko yaliyopokelewa 195 yalitoka Zanzibar.
Kufungua matawi 2 ya Ofisi za Ofisi zimefunguliwa katika mikoa ya Lindi na Mwanza
Tume ya Haki za Binadamu na na zinafanya kazi.
Utawala Bora katika mikoa ya
Lindi na Mwanza.
18. Kuendelea kuratibu Programu ya Jumla ya watumishi 10 wa kada mbalimbali
Kuboresha Sekta ya Sheria (LSRP) wameajiriwa katika ofisi ya kuratibu Programu ya
kwa kufanya yafutayo: kuboresha Sheria kama ifuatavyo:
Kuajiri wataalamu zaidi. Mratibu wa Programu; Afisa Mkuu Utawala/Mhasibu;
Afisa Mkuu Uchambuzi wa Sera, Ufuatiliaji na
Tathmini; Afisa Mkuu Ugavi; Afisa Mwandamizi Habari
na Wasaidizi wanne (support staff).
Kuwapatia mafunzo wasimamizi 45 wa Utekelezaji wa mpango huu umeanza kwa kutumia
Programu na maofisa 120 kutoka fedha za Serikali katika maeneo ya Sector Wide
Taasisi na Asasi zinazotekeleza LSRP. Approach Programme (SWAP) na Change
Management na unategemewa kuendelea katika
maeneo mengine, kupitia wafadhili,
baada ya kukamilika kwa taratibu za basket fund kati ya
Serikali na Wahisani.
Katika mafunzo hayo wasimamizi 42 (link officers) wa
Programu na maofisa 64 toka Tasisi na Asasi
zinazotekeleza Programu hii wamepatiwa mafunzo ya
namna ya kuandaa mpango na bajeti kwa kufuata
utaratibu wa kuhusisha sekta mbali mbali (SWAP).
Kuandaa mfumo wa usimamizi wa Ofisi ya Uratibu wa Programu ya Kuboresha Sekta ya
Programu - Monitoring & Evaluation Sheria imeanza kuandaa Mfumo wa uratibu, usimamizi
(M&E). na tathmini (M & E) kwa ajili ya programu.
Aidha, Taasisi na wizara zote zinazotekeleza Programu
ya kuboresha sekta ya Sheria zimeandaa na
zinatekeleza mpango wa kazi wa mwaka mmoja.
139
19. Kuboresha utoaji huduma kwa wateja
na wananchi kwa ujumla kwa
kuwapeleka watumishi wa Kada
mbalimbali kwenye mafunzo na kuajiri
wengine zaidi:
Mahakimu 6 na mawakili 16 Mahakimu 2 na Mawakili wa Serikali 12 wanasoma
watahudhuria mafunzo ya muda shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu cha Dar es
mrefu katika viwango vya Salaam.
Stashahada ya Uzamili na
Mawakili 50 watapatiwa mafunzo
ya muda mfupi.
Mahakimu na watendaji 99 Idara ya Mahakama imedhamini watumishi/wanafunzi
watapata mafunzo katika diploma 117 kwa ajili ya Stashahada ya Sheria na
ya juu na cheti, na watumishi wa watumishi/wanafunzi 20 kwa ajili ya Cheti cha Sheria.
mahakama wa Kada nyingine 234 Watumishi wengine 87 wamehudhuria mafunzo ya
watapata mafunzo ya muda mrefu muda mfupi na mrefu kwa kada za Wapiga Chapa
na mfupi. (Typists), Wahudumu, Walinzi na Makarani.
"Induction training" itafanyika baada ya kutolewa kwa
Makatibu Muhtasi na Mawakili 30 fedha zilizotengwa kwa kazi hiyo.
waajiriwa wapya watapatiwa
”Induction course”.
Mawakili 6 na watumishi wengine 17 wapya
Kuajiri watumishi wapya 52 wameajiriwa. Idadi iliyobaki inasubiri taratibu za
hususan Mawakili wa Serikali 31 kupandisha vyeo. Watumishi wengine 64 wa kada
na watumishi wengine 21. nyingine Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
walipata mafunzo ya muda mfupi.
20. Kuboresha mazingira ya kazi na utoaji Jumla ya magari 75 yamenunuliwa na Mahakama kwa
haki kwa kufanya yafuatayo: ajili ya Majaji na matumizi ya ofisi za Mahakama za
Mikoa na Wilaya kwa ajili ya Ukaguzi.
Kuimarisha vyombo vya utoaji Hatua za kuwapatia mahakimu wa Mahakama za
haki nchini kwa kuzipatia vitendea Mwanzo vyombo vya usafiri zinachukuliwa kulingana
kazi vya kisasa na vyombo vya na upatikanaji wa fedha. Hali kadhalika ofisi mbalimbali
usafiri hususan kwa mahakimu wa za Wizara zinapatiwa vitendea kazi vya kisasa -
mahakama za Mwanzo. Kompyuta, Samani na shajala (stationeries).
Kuimarisha usimamizi na ukaguzi Ukaguzi wa Ofisi za Kanda za Mahakama na Ofisi ya
wa Ofisi za Kanda za Mahakama, Mwanasheria Mkuu wa Serikali unafanyika kila robo
na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa mwaka kwa kuwahusisha viongozi wa idara husika.
Serikali.
Kufuatilia utekelezaji wa Mpango Ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mpango na Bajeti
na Bajeti ya Wizara, ukusanyaji umefanyika na taarifa zake kuandaliwa kwa kila robo
wa maduhuli ya Serikali, na mwaka. Uzingatiaji wa taratibu za manunuzi katika ofisi
140
uzingatiaji wa taratibu za zote za Wizara umeimarishwa na unaendelea vizuri.
manunuzi katika ofisi za Kanda za
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Ofisi ya Wakala wa Ufilisi, Usajili na Udhamini (RITA)
Serikali na Mahakama za ngazi imekusanya maduhuli ya Shilingi 667,910,319.50
zote kwa lengo la kuongeza ikilinganishwa na lengo la shilingi 642,400,000 ziada
uwajibikaji kwa wananchi. ya asilimia 4 juu ya lengo.
21. Kuimarisha na Kuboresha utoaji wa
ushauri wa Kisheria katika mikataba ya
Serikali kwa kufanya yafuatayo:
(i) Kufanya maandalizi ya kutosha Ushauri wa Kisheria uliendelea kutolewa katika maeneo
ya pamoja na Sekta na Idara yafuatayo: - mikataba ya Kimataifa; Mikopo;
zote zinazohusika na Mikataba; Ubinafsishaji na uwekezaji; Masuala ya Katiba na Haki
za Binadamu; Madai na Jinai.
(ii) Kuwapatia Mawakili wa Serikali Aidha, maandalizi ya kutosha na yenye kuwahusisha
katika Ofisi ya Mwanasheria wataalam wa Idara husika na Mawakili wa Serikali
Mkuu wa Serikali na wale walio yamefanyika katika kuandaa Mikataba mbalimbali
katika Wizara na Idara za hususan iliyohusu Madini na Nishati kwa lengo la
Serikali elimu ya fani ya kulinda uwekezaji wa rasilimali baina ya Tanzania na
majadiliano katika maeneo nchi nyingine. Mabilioni ya shilingi yameweza
maalum; kuokolewa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
katika mashauri mbalimbali ya Madai. Kuhusu
mafunzo, Wakili wa Serikali mmoja (1) amehudhuria
mafunzo mafupi ya fani ya majadiliano katika maeneo
maalumu.
(iii) Kuongeza usimamizi wa hatua Mawakili wa Serikali wamekuwa wakipitia Mikataba
zote za majadiliano ya mikataba baina ya Serikali, kwa upande mmoja, na watu binafsi,
ili kubaini matatizo kabla ya Mashirika ya Kitaifa na Kimataifa au Mamlaka nyingine
Mkataba kusainiwa: ya nje na ndani ya nchi, kwa upande mwingine, ili
kuona kama inazingatia misingi ya Kisheria na
kushauri ipasavyo pale ambapo inaonekana
kutokukidhi matakwa ya kisheria. Katika hili Mikataba
ya Madini imepitiwa na ile ya Nishati bado
inashughulikiwa.
22. Kutekeleza Sheria ya Ofisi ya Sheria imeanza kutumika na kwa sasa Wizara
Mwanasheria Mkuu wa Serikali inakamilisha uandaaji wa daftari ya orodha ya
iliyopitishwa na Bunge mwaka 2005; mawakili. Muundo mpya umeandaliwa kwa mujibu wa
sheria na umepitishwa na Baraza Kuu la Wafanyakazi
ngazi ya Taifa. Kwa sasa muundo huo unasubiri
kupitishwa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi
wa Umma kabla ya kuwasilishwa kwenye Kamati ya
Rais.
23. Kuimarisha Ofisi ya Kabidhi Wasii Wakala imezidi kuimarika tangu ilipozinduliwa rasmi
Mkuu ambayo sasa ni Wakala wa tarehe 23/06/2006 ambapo imeweza kupata jengo la
141
Serikali tangu tarehe 23/6/2006. kupanga ili kupisha ujenzi ambao unaandaliwa na
imeweza kununua samani ambazo zitaboresha na
kupunguza tatizo la vitendea kazi. Jina jipya la ofisi ni
Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini, [Registration,
Insolvency and Trusteeship Agency [RITA)].
Aidha, Wakala imeendelea kusajili vizazi na vifo, ndoa
na talaka, kusimamia ufilisi, usajili na udhamini wa mali
isiyokuwa na mwenyewe na uasii wa watoto. Wakala
pia imeanzisha tovuti ambayo inaelimisha umma
kuhusu huduma zinazotolewa na Wakala.
24. Kutoa mafunzo kwa watumishi ya jinsi - Katika kutoa mafunzo ya elimu ya UKIMWI
ya kujikinga na janga la Ukimwi, Mahakama ya Biashara imeendesha na
kuepuka rushwa na kuzingatia inaendelea kuendesha semina mbalimbali elimishi
masuala ya jinsia na kuhifadhi kwa watumishi wake. Aidha katika masuala ya
mazingira katika mipango ya Wizara. jinsia Mahakama imewahusisha watumishi wa
jinsia zote katika utekelezaji wa shughuli zake za
kila siku.
- Katika kupambana na rushwa katika sehemu za
kazi, Mahakama ya Biashara imeboresha
mazingira kwa kutoa motisha na vitendea kazi kwa
watumishi wake.
- Kwa upande wa ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali semina 4 zinazohusu UKIMWI
zimeendeshwa kwa viongozi. Pia Kamati ya
kuratibu shughuli za ukimwi imeundwa kwa
kuteua wajumbe kutoka Idara zote za Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Mawakili na
watumishi wa Ofisi za Kanda, wamepatiwa
mafunzo ya kujikinga na maambukizi ya Ukimwi,
ambapo mikutano miwili imeendeshwa Ki-kanda
mjini Iringa na Dodoma. Mikutano mingine ya
namna hii inatarajiwa kuendeshwa katika Kanda
ya Arusha, Mwanza na Dar es Salaam.
- Vile vile semina kwa viongozi za kuepuka na
kupambana na rushwa kazini, kudumisha
nidhamu na maadili ya Uongozi kwa watumishi wa
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali
zimefanyika. Aidha, Watendaji Wakuu wote wa
Serikali walifanyiwa warsha Jijini Dar es Salaam
kuhusu majukumu ya Kamati za Maadili
zilizoundwa na Ofisi ya Rais ya Kitengo cha
142
Utawala Bora.
- Katika kampeni ya kuhifadhi mazingira Mahakama
ya Biashara imeunda kamati ya kushughulikia
utunzaji wa mazingira na masuala ya mazingira
yanazingatiwa kwenye mpango wa Wizara.
Kuziimarisha Kamati za Kusukuma Kamati za kusukuma kesi za ngazi zote (Kitaifa,
kesi (Case Flow Management Kikanda, Kimkoa, na Kiwilaya) zimeimarishwa kwa
Committee). kupatiwa fedha na vitendea kazi kwa kuziwezesha
kukutana mara moja kwa kila robo mwaka.
Kuongeza mzunguko wa Ukaguzi wa Mkakati wa ukaguzi wa ofisi za Kanda za Ofisi ya
Ofisi za Kanda za Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mara mbili kwa mwaka
Mwanasheria Mkuu wa Serikali. umetekelezwa na ushauri kutolewa ipasavyo. Mpango
na Bajeti ya Wizara ya 2006/07 imeendelea
kusimamiwa katika utekelezaji wake na taarifa za robo
mwaka za utekelezaji kuandaliwa na kuwasilishwa
Hazina. Ushauri kuhusu masuala ya Sera, Mipango na
Bajeti na uboreshaji wa Sekta ya Sheria na Utekelezaji
wa MKUKUTA umetolewa ipasavyo.
Kanda 3 zimetembelewa (follow up & supervision) kwa
ofisi za Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mahakama
za ngazi zote ili kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa
Mipango na bajeti, kuona hali halisi ya Ofisi na Majengo
ya Mahakama, kuongea na watumishi wote juu ya
matatizo na mafanikio yao na kushauri ipasavyo.
Kanda zilizotembelewa ni Tabora, Tanga na Dar es
Salaam. Taarifa imeandaliwa na kuwasilishwa kwa
uongozi wa Wizara. Kanda nyingine zitatembelewa
pindi za bajeti ya shughuli hiyo zikitolewa.
Taratibu zinaendelea kukamilishwa. Maandalizi ya
Kukamilisha taratibu za Mawakili
kuwaajiri Mawakili 104, kununua magari 6 na kununua
wa Serikali kuendesha kesi za
majengo ya ofisi 6 kwa mikoa ya Dar es Salaam,
jinai hadi ngazi ya Mahakama za
Arusha, Shinyanga-Bariadi, Mwanza, Tanga, Ruvuma-
Wilaya.
Songea na kununua vitendea kazi zinafanyika. Tayari
gari moja limenunuliwa. Juhudi zinafanyika kupata
fedha za kutekeleza majukumu haya chini ya Mkakati
wa Programu ya Kuboresha Sekta ya Sheria na kupitia
bajeti ya Serikali.
Wizara iliunda Kamati ya Wataalamu ambayo ilipitia
Kuendeleza Mpango wa
143
mabadiliko katika Sheria ya vifungu vyote muhimu na kutoa mapendekezo ya jinsi
Mwenendo wa Mashauri ya Madai ya kuviboresha. Aidha mapendekezo hayo sasa
na Sheria ya Mwenendo wa yanatafsiriwa katika vifungu vya sheria ili kuwezesha
Mashauri ya Jinai ili kuimarisha kutungwa kwa sheria ya marekebisho ya vifungu hivyo.
dhana ya upatikanaji wa haki kwa Mapendekezo ya Marekebisho ya kutungwa sheria ya
wakati chini ya Mradi wa BEST. Marekebisho ya mwenendo wa jinai eneo "Anti-Money
Laundering" yaliwasilishwa katika Bunge la Februari,
2007.
144
WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kukusanya Maduhuli ya Serikali ya Hadi Juni 2007 jumla ya TSh. 8,632,957,800 zilikuwa
jumla ya sh. 10,747,833,000 zimekusanywa sawa na asilimia 80 ya lengo.
yanayotokana na kodi ya pango la
ardhi na vyanzo vingine katika Jiji la
Dar es Salaam na vituo vya mikoani.
2. Kutoa miliki za ardhi yenye ukubwa wa Mashamba 6 ya ardhi yenye ukubwa wa hekta 18,233
kuanzia hekta tano na kuendelea, kwa ajili ya uwekezaji yametengwa na kupimwa na
ukanda wa Pwani (Fukwe, Visiwa hatimaye kuingizwa kwenye Hazina ya Ardhi (Land
vidogo) ardhi ya uwekezaji, viwanja Bank). Maeneo hayo yaliyoko katika Mikoa ya
kwa ajili ya Balozi na maeneo mengine Morogoro na Pwani yamekabidhiwa kwa Kituo cha
ambayo matumizi yake ni ya manufaa Uwekezaji Tanzania (TIC) ili yamilikishwe kwa
kwa Taifa. wawekezaji.
3. Kutayarisha na kusaini hati miliki 6,000 Hadi kufikia Mei, 2007 hati 9,096 ziliandaliwa, kati ya
za ardhi na nyaraka mbalimbali za hizo hati 6,599 zilitoka Halmashauri na 2,497
kisheria. ziliandaliwa Wizarani. Aidha, Nyaraka mbalimbali
zipatazo 21,921 zilisajiliwa. Hii ni asilimia 182.6 ya
lengo la kusajili nyaraka za kisheria 12,000.
4. Kufuta miliki za viwanja ambavyo Zoezi la kufuta miliki za viwanja liliendelea nchini kote
havijaendelezwa kwa mujibu wa sheria ambapo hadi kufikia Mwezi Juni, 2007 ufutaji wa miliki
katika maeneo mbalimbali nchini. 637 za Viwanja na Mashamba kutoka mikoa mbalimbali
nchini ulikuwa umependekezwa.
Kutoa elimu kwa umma kuhusu Katika kipindi cha Julai, 2006 hadi Juni, 2007 Wizara
matakwa ya Sera na Sheria za Ardhi imetoa elimu kwa umma kuhusu Sera, Sheria na
nchini. matumizi bora ya Ardhi kwa njia mbalimbali katika
Wilaya 23 na Vijiji 172. Elimu pia ilitolewa kwa njia ya
redio, televisheni na Magazeti. Aidha, nakala 2,092 za
vitabu vya Sheria ya Ardhi ya Vijiji, Kanuni ya Sheria ya
Ardhi na Mwongozo nakala 5,270 zilisambazwa.
5. Kuratibu ujenzi wa masjala 10 za ardhi Masjala za Ardhi za Wilaya 7 na Vijiji 14 ziko katika
katika ngazi za Wilaya na 80 katika hatua mbalimbali za ujenzi. Vyeti vya ardhi ya Vijiji 211
ngazi ya vijiji na kusajili vyeti vya ardhi Hati za Hakimiliki za Kimila 3,940 zimetolewa kwa
ya vijiji na hatimiliki za kimila katika wanavijiji. Hii inafanya idadi kamili ya Vyeti ambavyo
maeneo hayo. vimetolewa kuwa 402 na Hati za Hakimiliki za Kimila
kuwa 5,202.
6. (a)Kujenga hazina ya kumbukumbu za Mpaka sasa kumbukumbu za uthamini 821,973
Uthamini (Valuation Data Bank) zimeingizwa kwenye Kompyuta. Vile vile, uingizaji wa
itakayowezesha Uthamini wa takwimu kwa mkono bado unaendelea.
mali kufanyika kulingana na Kinachosubiriwa ni mfumo wa Interface ili kuwezesha
viwango vya bei ya soko. matumizi ya kumbukumbu hizi.
(b)Kuthamini nyumba na mali
mbalimbali na kuhakiki taarifa za Taarifa 5,519 za uthamini za Wizara na za wathamini
145
uthamini kutoka kwa Makampuni wa nje ya Wizara zimefanyika na kuiingizia Serikali
binafsi, Halmashauri za miji na Jumla ya Shilingi 232,579,237 sawa na asilimia 155.02
Wilaya kama zitakavyopokelewa. ya lengo.
7. (a) Kujenga mtandao wa mawasiliano Uanzishwaji wa mtandao unaounganisha Kanda za
ya mbali (Wide Area Network) na Msajili wa Hati za Dodoma, Mwanza, Mbeya, Moshi na
mfumo wa habari na kumbukumbu Makao Makuu ya Wizara ya Ardhi umekamilika. Aidha,
za ardhi za Wizara (MOLIS) na mtandao katika Manispaa za Ilala, Kinondoni na
kuboresha tovuti ya Wizara Temeke umekamilika kwa asilimia 100.
(www.ardhi.go.tz).
(b) Kujenga, mfumo wa kisasa wa Ujenzi umekamilika kwa asilimia 90 ambapo “Movable
Masjala ya ardhi (Computerized shelves” zimekwishafungwa na zinafanya kazi. Hivi
Movable Shelves). sasa Wizara inaingiza kumbukumbu zote zinazohusu
majalada ya ardhi kwenye kompyuta ili kurahisha
upatikanaji wake.
(c) Kuziwezesha ofisi za Halmashauri Serikali imeziwezesha Halmashauri za Miji ya Mwanza,
za miji na wilaya kuongeza Moshi, Arusha, Morogoro na Mbeya kutumia kompyuta
matumizi ya teknolojia ya habari na katika ukadiriaji wa kodi ya pango la Ardhi kwa
mawasiliano. kuwapatia mafunzo, kompyuta na vifaa vya ofisi kama
stationery. Kazi ya kuziunganisha katika mtandao
Manispaa za Ilala, Kinondoni na Temeke ili kurahisisha
mawasiliano kati ya Wizara na Manispaa hizo
imekamilika kwa asilimia 95.
8. Kuboresha kumbukumbu za ardhi Zoezi la kuimarisha kumbukumbu za walipa kodi kwa
zikiwemo orodha za viwanja kuhakiki wamiliki wa ardhi linaendelea.
vilivyopimwa, wamiliki na matumizi Halmashauri zipatazo 81 zimekwishaleta taarifa za
yake. kumbukumbu za viwanja vilivyopimwa, wamiliki na
matumizi ya viwanja hivyo. Kati ya hivyo, kumbukumbu
za Halmashauri 77 zimekwishaingizwa katika
kompyuta.
9. (a) Kuunda Mabaraza 7 ya Ardhi na Mabaraza ya Ardhi na Nyumba yameundwa katika
Nyumba katika wilaya zenye Wilaya 10 zenye migogoro mingi ya ardhi. Wilaya hizo
migogoro mingi ya ardhi na ni Same, Simanjiro, Karatu, Tarime, Geita, Chato,
nyumba ili kuwapunguzia wananchi Kilomero, Njombe, Rungwe na Mbinga.
gharama za kusafiri umbali mrefu
hadi Makao Makuu ya Mikoa.
(b) Kuyapatia vitendea kazi Mabaraza Vifaa vya Ofisi vimetolewa kwa mabaraza yote 23.
23 ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya
yanayoendelea kushughulikia
mashauri yaliyopokelewa na
kufungua mashauri mapya.
146
10. Kukamilisha kazi ya kupiga picha za Zoezi halijakamilika kutokana na mawingu kuendelea
anga na kutayarisha digital kutanda katika Jiji la Dar es Salaam na Kanda nzima ya
orthophotos kwa eneo lililobakia katika Mashariki.
Jiji la Dar es Salaam na kufanya kazi
kama hiyo katika Jiji la Mbeya na
Manispaa ya Morogoro kwa ajili ya
kuendeleza mradi wa kupima viwanja
na kudhibiti ujenzi holela.
Kupiga picha za anga katika Kanda ya Hali ya hewa haijaruhusu upigaji picha msimu wa
Mashariki inayojumuisha miji 128 kiangazi kutokana na mawingu kuendelea kutanda
iliyopo katika Mikoa ya Pwani, Tanga, katika kanda ya Mashariki. Kazi hii inatarajiwa
Kilimanjaro, Manyara, Arusha, Singida, kufanyika katika Mwaka ujao wa fedha.
Dodoma na Morogoro.
11. Kuendelea kuwasiliana na Shirika la Mkutano wa wadau ulifanyika ukihudhuriwa na ujumbe
Kimataifa linalohusika na Upimaji wa wa United Kingdom Hydrographic Organisation (UKHO)
ardhi ndani ya Maji (International kwa niaba ya IHO. Shirika hili ni msimamizi wa masuala
Hydrographic Organization – IHO) ili ya Upimaji majini kwa Bara la Afrika. Aidha, Wizara
kupata fedha kwa ajili ya kununua vifaa imehudhuria mkutano wa 17 wa UNCLOS (United
vya msingi vya upimaji wa ardhi ndani Nations Convention on the Laws of the Seas)
ya maji (hydrographic surveying) na uliofanyika tarehe 18 - 24 Juni, 2007 huko New York,
wataalam ili kupima na kutayarisha Marekani.
ramani za maeneo ya ardhini chini ya
Bahari ya Hindi na Maziwa Makuu.
12. (a) Kuongeza kasi ya kushughulikia Ukaguzi umeimarishwa kwa kuweka hatua ya kuchuja
kazi za upimaji zinazopokelewa kazi mara tu inapoingia Wizarani na zile zisizokidhi
kutoka kwenye Halmashauri za vigezo vilivyowekwa hurudishwa kwenye Halmashauri
miji, wilaya, na makampuni ya zilikotoka. Aidha, matumizi ya kompyuta
wapima banafsi. yameongezeka katika kukagua kazi hizo na hivyo
kuongeza ufanisi.
(b) Kuratibu na kusimamia upimaji wa Hadi kufikia Julai, 2006 Halmashauri 14 zilikamilisha
viwanja katika Halmashauri za miji marejesho yao yenye Jumla ya Shilingi
na wilaya zilizopatiwa fedha za 157,207,161.15. Halmashauri 18 bado hazijakamilisha
mkopo kwa ajili ya upimaji wa marejesho yao yenye jumla ya Shilingi 212,605,195.50.
viwanja mijini (Plot Development Hadi kufikia Juni, 2007 Halmashauri 32 zilikuwa
Revolving Fund) na kukusanya zimepatiwa mikopo inayofikia Shilingi 576,333,351.
marejesho.
(c) Kuziwezesha Halmashauri za Jiji Jiji la Mwanza limewezeshwa kupima viwanja 9,800
na Manispaa zenye mahitaji kwa miaka mitatu iliyopita. Manispaa ya Morogoro
makubwa ya viwanja kama Dar es 2,764 kati ya 4,000 vilivyotarajiwa kupimwa, Jiji la
Salaam, Mbeya, Mwanza na Mbeya limepima viwanja 2,350 kati ya 5,000
Morogoro kupima viwanja kwa vilivyotarajiwa na Jiji la Dar es Salaam viwanja 5,800
utaratibu wa wananchi kuchangia katika eneo la Kibada. Aidha, maandalizi ya kupima
147
gharama. viwanja zaidi yanaendelea. Maombi ya mikopo
yamepokelewa kutoka Halmashauri za Mji wa Kibaha,
Arusha na Moshi na yanachambuliwa ili kupitishwa.
(d) Kusimamia upimaji wa vijiji 3,000 Upimaji wa Vijiji ulianza mwishoni mwa Mwezi Oktoba,
katika mikoa yote ya Tanzania 2006 kwa Mikoa ya Pwani, Lindi, Iringa, Mbeya, Rukwa,
Bara. Kigoma, Kagera, Shinyanga na Tanga. Hadi katikati ya
Mwezi Juni, 2007 upimaji wa vijiji 2,800 umekamilika
sawa na asilimia 90.
13. Kutayarisha Sera na Sheria za upimaji Mtaalam Mwelekezi tayari amependekezwa na Wizara
wa ardhi ili upimaji wa ardhi na ndani inasubiri majibu kutoka Benki ya Dunia.
ya maji uendane na mabadiliko ya
teknolojia Duniani na Sera ya Taifa ya
Ardhi ya Mwaka 1995.
14. (a) Kufanya mashauriano kati ya Mazungumzo yalifanyika kati ya Tanzania na Serikali
Tanzania na nchi za Comoro na ya Msumbiji ambayo yaliwezesha kuandikwa barua ya
Msumbiji yatakayohusu kuweka pamoja kuwaita Comoros kwa ajili ya alama ya utatu
mpaka ndani ya Bahari ya Hindi. Baharini. Aidha, ukaguzi wa mpaka kati ya Tanzania na
Msumbiji ulifanyika katika eneo la kutoka Mto Ruvuma
hadi Ziwa Nyasa. Matokeo ya ukaguzi huo ni kwamba
alama zipo lakini zinahitaji ukarabati. Pia, kuna haja ya
kuongeza alama hizi ili zionekane kwa urahisi kwa
wananchi wanaoishi mpakani.
(b) Kuendelea na majadiliano ya Mazungumzo yamefanyika kati ya Serikali za Burundi,
kuhuisha na kutekeleza uimarishaji Uganda, Kenya na Tanzania kuhusu uimarishaji wa
wa mipaka kati ya Tanzania na mipaka yetu. Kuhusu mpaka kati ya Tanzania na
nchi za Malawi, Zambia, Burundi, Malawi, mkutano wa pamoja ulishauri Serikali hizi mbili
Rwanda, Uganda na Kenya. kutenga fedha za kuanzia miradi iliyobainishwa katika
upembuzi yakinifu uliofanyika katika bonde la mto
Songwe.
15. Kutafsiri mipaka ya ndani ya nchi Wakuu wa Wilaya zote Tanzania Bara wamepewa
hususan mipaka kati ya Wilaya na nakala za “Government Notice” (GN) za mipaka ya
Wilaya hasa kwenye maeneo yenye Wilaya zao.
migogoro. Pia, kusambaza
“Government Notice” (GN) za mipaka
ya Wilaya zote nchini ili kila Mkuu wa
Wilaya awe na Nyaraka hizo.
16. (a)Wizara kwa kushirikiana na Wataalam tayari wako mjini Mwanza kwa maandalizi ya
Halmashauri za miji na wilaya na “Master Plan” ya mji huo. Maandalizi kwa mpango wa
kwa kuzingatia dhana shirikishi namna hiyo yameanza kwa mji wa Mtwara na
zitaandaa mipango kabambe yanatarajiwa kukamilika mwaka ujao wa fedha
(Master plans), ikiwemo ya Jiji la 2007/2008. Kwa miji ya Dar es Salaam na Bukoba
DSM, Mwanza, na miji ya Mtwara utekelezaji unatarajiwa kufanyika katika mwaka wa
na Bukoba. fedha 2007/2008.
148
(b) Kuandaa mipango ya matumizi ya Miji ya Bunda, Chato, Dakawa (Mvomero) na Kibaigwa
ardhi (Interim Urban Land Use imeandaa Mipango ya Matumizi ya Ardhi. Aidha, kazi
Plans), katika miji mbalimbali hasa itaendelea kufanyika katika Mwaka wa fedha
kwa vijiji vilivyotangazwa kuwa miji 2007/2008. Miji ya Mbarali, Kyela, Kasulu na Kibondo
midogo. haijafanyiwa kazi kwa sababu ya uhaba wa wataalamu
na fedha zilizochangiwa katika punguzo la Bajeti la
Shilingi milioni 700 lililofanyika Mwaka 2006/2007.
17. (a) Kuandaa mipango ya kuendeleza Mipango hiyo imefanyika kwa eneo la Upanga. Aidha,
upya maeneo kongwe yaliyoko Maandalizi ya mipango ya namna hiyo
Jijini Dar es Salaam ambayo ni yamekwishaanza kwa maeneo ya Magomeni, Dar es
Upanga, Magomeni na Temeke. Salaam.
Maeneo mengine
yatakayoandaliwa mpango huo ni
pamoja na eneo la katikati ya mji
wa Lindi.
(b) Kuandaa na kutekeleza mpango wa Hadi kufikia Novemba, 2006 wananchi 50 kati ya 188
kuendeleza upya eneo la Kurasini waliopangwa kulipwa katika mwaka 2006/07
lililoko Jijini Dar es Salaam. wamelipwa fidia na wengine wataendelea kulipwa kadri
fedha zitakavyopatikana. Uthamini wa mali unaendelea.
18. Kuandaa Miswada ya Sheria kwa ajili Miswada yote imewasilishwa Bungeni na imepitishwa
ya kuhuisha au kutunga Sheria mpya na Bunge Mwezi Aprili, 2007. Uandaaji wa Kanuni
zinazohusu: - Sheria ya mipango miji unaendelea.
na vijiji sura Na. 378 ya mwaka 1956;
Sheria ya Mipango ya Matumizi ya
Ardhi Na. 3 ya mwaka 1984; na Sheria
ya Kusimamia taaluma ya mipangomiji.
19. Kuandaa michoro mbalimbali ya Wizara imeandaa aina 20 tofauti ya michoro ya nyumba
mifano ya nyumba yenye lengo la za mfano na kukamilisha uidhinishaji wake kwa
kupunguza gharama za ujenzi. Manispaa zote za Jiji la Dar es Salaam. Michoro hiyo
Michoro hiyo itaandaliwa katika miji ya pamoja na vifaa mbalimbali tayari vimekabidhiwa kwa
Arusha, Moshi, Bukoba, Iringa, Mtwara Manispaa hizo. Vifaa vilivyonunuliwa ni Kompyuta 1 na
na Musoma. „Printer‟ kubwa kwa kila Halmashauri. Kila Halmashauri
inatakiwa kuajiri mtaalam wa kuzalisha ramani hizo
pamoja na chumba maalum katika ofisi zake.
20. Kusimamia mfuko wa kutoa mikopo Usimamizi wa mfuko umekuwa mzuri katika kipindi
kwa ajili ya ujenzi na ununuzi wa husika na watumishi 677 waliidhinishiwa mikopo yenye
nyumba kwa watumishi wa Serikali thamani ya Shilingi 1,730,677,979.00. Hadi Mwezi Mei,
(Revolving Housing Loan Fund) ili 2007 marejesho yalifikia Shilingi 663,674,255.00.
uweze kuwafikia watumishi walio
wengi.
21. Kusimamia utekelezaji wa awamu ya Ukusanyaji wa taarifa juu ya maeneo yanayoweza
pili ya mradi wa kutambua maeneo kutumika katika uwekaji wa huduma muhimu za makazi
yaliyojengwa kiholela hasa pembezoni unafanyika katika maeneo ya Kimara, Mbezi, Kibamba
mwa Jiji la Dar es Salaam. Pia, na Kiluvya ambayo yako pembezoni mwa jiji la Dar es
149
utambuzi wa maeneo yaliyojengwa Salaam. Usajili wa mali umeanza katika eneo la
kiholela utafanyika katika miji mingine Kimara.
nchini, ikiwa ni pamoja na Jiji la
Mwanza na Manispaa ya Dodoma.
23. (a) Kuandaa na kusimamia mipango Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi Bora ya ardhi
shirikishi ya matumizi bora ya imeandaa na kukamilisha mipango shirikishi ya
ardhi ngazi ya wilaya na vijiji matumizi bora ya ardhi, ikiwemo maeneo wanayohamia
mbalimbali nchini hasa kwenye wafugaji kama ifuatavyo:- Chunya vijiji 15, Kisarawe
maeneo wanayotoka na vijiji 8, Rufiji vijiji 14, Kilwa vijiji 10, Lindi vijiji 10,
watakayohamishiwa wafugaji Nachingwea vijiji 10, Mkuranga vijiji 5. Aidha, Tume
nchini. kwa kushirikiana na Halmashauri za wilaya husika
imeandaa Mipango ya Matumizi Bora ya Ardhi ya
wilaya 13 ambazo ni Iringa vijijini, Kilolo, Kisarawe,
Lindi vijijini, Nachingwea, Chunya, Njombe, Makete,
Kilosa, Rufiji, Mafia, Kilwa na Mbarali.
(b) Kuandaa Mpango wa Taifa wa Tume ilikiteua Chuo Kikuu Kishiriki cha Ardhi na
Matumizi ya Ardhi. Usanifu wa Majengo (UCLAS) kuwa Mkandarasi wa
kuandaa Mpango wa Taifa wa Matumizi Bora ya Ardhi
mnamo Januari, 2007. Mnamo Februari, 2007
mkandarasi aliwasilisha taarifa ya awali (Inception
Report). Baada ya kuafiki taarifa hii mkandarasi alipitia
(review) taarifa za hali halisi kisekta (Sectoral Existing
Situation) na kuandaa rasimu ya kwanza inayoonyesha
hali halisi ya matumizi ya ardhi nchini na ramani zake
na kubainisha mtiririko na masuala yanayojitokeza.
Rasimu iliwasilishwa katika mkutano wa wadau tarehe
12 Juni, 2007. Hivi sasa kila sekta inapitia kwa makini
taarifa hii hususan sekta husika na kutoa maoni na
marekebisho na kuyawasilisha kwa mkandarasi. Maoni
haya, pamoja na maoni yaliyotolewa kwenye mkutano
yatazingatiwa na kujumuishwa na mkandarasi ili
kukamilisha Mpango wa Taifa wa Matumizi Bora ya
Ardhi.
(c)Kutekeleza Mkakati wa Kuhifadhi Vyanzo vya maji vya mto Ruaha Mkuu, Ruaha Mdogo
mazingira ya ardhi na vyanzo vya na Lukosi maji katika wilaya mbalimbali vimebainishwa
maji wenye lengo la kudhibiti na kuwekewa mikakati ya uhifadhi. Wavamizi wa
uharibifu wa mazingira vyanzo vya maji katika kijiji cha Kikondo wilayani
unaotokana na ufugaji kwenye Makete, wamehamishiwa vijiji vya Kinyika, Ipelele na
vyanzo vya maji, kilimo kwenye Mapanda. Vilevile wafugaji na wakulima katika vyanzo
miteremko ya milima; mabonde na vya maji wamehamishwa wilayani Mbarali na Mbeya
vyanzo vya maji. Kutafiti na vijijini na kupatiwa ardhi mbadala wilayani Chunya,
kubaini maeneo mbadala Kisarawe, Rufiji, Kilwa, Lindi vijijini na Nachingwea.
yanayofaa kuwahamishia wakulima Katika maeneo haya mipango shirikishi ya matumizi
150
na wafugaji. bora ya ardhi imeandaliwa kwa wilaya za Mbarali vijiji 9,
Mbeya vijijini vijiji 5, Makete vijiji 4, Chamwino vijiji 5,
(d)Kufanya utafiti na kuandaa mipango Iringa vijijini vijiji 7, Kilolo vijiji 3, Mufindi vijiji 5, Njombe
ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji 5 na Manyoni vijiji 5.
maeneo ya Manyoni, Dodoma
Vijijini, Singida, Shinyanga Vijijini, Mipango Shirikishi ya Matumizi Bora ya Ardhi ya vijiji
Ilemela, Musoma nk. ambayo kwa imeandaliwa na kuanza kutekelezwa kama ifuatavyo;
asili ni ya ufugaji, lakini wafugaji Kilombero vijiji 5, Kilosa vijiji 5, Ulanga vijiji 5, Mvomero
wanahama na kuingia kwenye vijiji 5, Liwale vijiji 9 na Morogoro vijijini vijiji 5.
vyanzo vya maji.
24. (a)Kuendesha semina za kuhamasisha Wananchi wameendelea kuhamasishwa kuhusu ujenzi
wananchi juu ya ujenzi wa nyumba wa Nyumba Bora za gharama nafuu katika Wilaya ya
bora na za gharama nafuu katika Namtumbo, Kijiji cha Msindo wamehamasishwa na
maeneo mbalimbali nchini na kutoa kuanzisha kikundi cha ujenzi (Grassroot Building
mafunzo ya vitendo na kuonyesha Brigade – GBB). Pia, wamepatiwa mafunzo ya vitendo
katika halmashauri za miji na wilaya ya ujenzi wa kutumia matofali yanayofungamana na
zinazohamasishwa. wameanza kujenga nyumba za waalimu kwa kutumia
ujuzi walioupata. Aidha, vikundi vya utengenezaji wa
matofali yanayofungamana vimeanzishwa katika
Manispaa ya Iringa eneo la Ipogoro kwenye mradi wa
National Housing Corporation (NHC) utakaotumia
matofali ya udongo saruji yanayofungamana.
Aidha, Semina za uhamasishaji ziliendeshwa katika
mikoa kama ifuatavyo; Morogoro (Morogoro Vijijini),
Tabora (vijiji vya Ilolangulu, Mbola, Ngokolo, Isila na
Mpenge - Tabora Vijijini), Pwani (Kisarawe -vijiji vya
Gwata na Mitengwe),Dar es Salaam, (Kinondoni katika
eneo la Mivumoni ambako imejengwa nyumba ya
mfano), Arusha (watendaji wa wilaya ya Karatu na kwa
Katibu Tawala wa Mkoa), Manyara (watendaji wa
Wilaya ya Simanjiro) Dodoma (Wakuu wote wa Wilaya
na kwa Katibu Tawala wa Mkoa) na Mara (Wilayani
Bunda).
(b)Kuendesha uhamasishaji na Magazeti na Vipindi vya redio na Televisheni vilitumika
usambazaji wa teknolojia za ujenzi katika uhamasishaji. Wizara ilishiriki katika maonyesho
wa nyumba bora na za gharama ya kitaifa ya Saba Saba na pia imeshiriki katika
nafuu kwa njia za Redio, Magazeti, maonyesho ya kitaalam yanayoandaliwa na Baraza la
na televisheni, pamoja na kushiriki Taifa la Ujenzi (National Construction Council) na yale
katika Maonyesho ya Kitaifa na yanayoandaliwa na Bodi ya Usajili wa Makandarasi
Kimataifa. (Contractors‟ Registration Board), Maonyesho kwa
Waheshimiwa Wabunge waliotembelea Wilaya ya
Kisarawe katika kufuatilia matumizi Bora ya Ardhi.
Aidha, Wizara ilishiriki kufanya maonyesho kwenye
151
Mkutano wa Kimataifa wa HAKIMILIKI (Intellectual
Property Day) yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi
Mmoja Mkoani Dar es Salaam.
25. (a) Kuongeza kasi ya kukusanya kodi Shirika lilipanga kukusanya kodi ya Tsh.
za pango la nyumba kutoka 19,073,808.000.00 kwa mwaka wa fedha 2006/2007.
kwenye nyumba zinazosimamiwa Hadi Mei, 2007 Shirika limekusanya Tsh.
na Shirika la Nyumba la Taifa. 17,527,037,406.65 sawa na asilimia 92 ya lengo.
Kurekebisha viwango vya kodi Shirika limefanya marekebisho ya viwango vya kodi za
za nyumba za Shirika la Taifa la nyumba zake kuanzia mwezi Februari 2007 ili liweze
Nyumba ili kuliwezesha kuongeza uwezo wake wa kufanya matengenezo,
kutekeleza majukumu yake kwa kujenga nyumba mpya, na kujiendesha kibiashara. Kodi
ufanisi. hiyo mpya itaongeza mapato kutoka TSh.
15,000,000,000 hadi 22,000,000,000 kwa Mwaka.
(b) Kukamilisha zoezi la kuuza nyumba Hadi kufikia Mei 2007, jumla ya nyumba ndogo ndogo
ndogondogo za Shirika zilizosalia, 4,838 kati ya nyumba 4,988 zilizokusudiwa kuuzwa
na kuzifanyia matengenezo zimelipiwa kikamilifu na kulipatia Shirika Sh.
nyumba zilizoko katika maeneo 7,383,936,065.00. Jumla ya nyumba 1,865
mbalimbali nchini. zilitengenezwa pamoja na majengo 406 kwa gharama
ya Tsh. 4,853,209,870.00
26. Kujenga nyumba 239 kwa ajili ya Ujenzi wa nyumba 23 eneo la Boko katika awamu ya III
kuuza na kupangisha katika Jiji la unaendelea na hadi sasa umefikia asilimia 99.
Dar es Salaam (Boko, Mbweni Makadirio ya gharama ya ujenzi ni Tsh.
JKT, Mbezi Beach, Msasani na 1,054,343,130.00. Matumizi hadi Mei 2007 ni Tsh.
Mwongozo) na Dodoma 1,019,198,875.00. Mradi unatarajiwa kukamilika ifikapo
(Mpwapwa Flats). mwishoni mwa Mwezi Juni, 2007. Awamu hii
ikikamilika mradi mzima utakuwa na nyumba 213.
Mradi wa ujenzi wa nyumba Boko, Ujenzi wa nyumba 15 kati ya nyumba 63 ulioanza
Dar es Salaam. Januari, 2006 unaendelea. Nyumba 10 kati ya 15
ujenzi umefikia asilimia 100, nyumba 1 aina ya
Mradi wa ujenzi wa Nyumba maisonettes imefikia asilimia 70, na nyumba 4 ujenzi
Mbweni JKT, Dar es Salaam. umefikia asilimia 70. Hadi Mei, 2007 Sh.
881,555,574.00 zilitumika.
Mradi wa ujenzi wa nyumba Mbezi Ujenzi wa nyumba 3 eneo la Mbezi Beach unaendelea.
Beach – Dar es Salaam. Kati ya nyumba hizi, nyumba 1 inajengwa kwa mtindo
wa Complete type na nyumba mbili ni shell type.
Gharama ya ujenzi ni Sh. 317,928,526.00. Ujenzi wa
nyumba 1 umekamilika na kwa sasa ujenzi wa nyumba
ya mtumishi (servant quarter) na kazi zingine za nje
kwa nyumba kubwa unaendelea. Ujenzi wa nyumba
zingine umefikia asilimia 80. Fedha Sh.
244,096,880.00 zimetumika. Nyumba hizi tatu
zikikamilika mradi utakuwa na nyumba 47.
152
Mradi wa ujenzi wa Nyumba za Ujenzi wa majengo mawili (2) ya ghorofa mjini Dodoma
kupangisha Dodoma (Mpwapwa unaendelea. Kila ghorofa litakuwa na nyumba 12 za
Block of Flats ). kuishi. Makadirio ya gharama ya ujenzi ni Shs.
1,088,071,746.00. Ujenzi umefikia asilimia 70.
Mradi wa ujenzi wa maduka Ipogoro, Mradi huu ni wa ujenzi wa maduka 72 katika eneo la
Iringa. Ipogoro katika manispaa ya Iringa. Ujenzi ulianza
Mwezi Desemba, 2006 kwa makadirio ya Sh.
334,657,932.00
Mradi wa ujenzi wa jengo la NHC Hadi Mei, 2007 Tshs. 101, 972,000.00 zilishatumika.
House.
Mradi huu ni wa ujenzi wa jengo la ghorofa 12
unaotekelezwa kwa mpango wa Turn- Key na Kampuni
ya SEM (Tanzania) Ltd. Makadirio ya ujenzi ni USD
28.8 Milioni. Ujenzi umefikia ghorofa 10 kati ya 12.
27. (a)Kuajiri watumishi 166 wenye Katika nusu ya kwanza ya 2006/07 Wahasibu 17 na
taaluma mbalimbali wakiwemo, wapima 2 waliajiriwa. Katika nusu ya pili wameajiriwa
Maafisa Ardhi, Wapima na Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba Wa
Wahasibu. Wilaya 7, Wasajili wasaidizi 6, Afisa Ardhi Msaidizi 1,
Wathamini 3, Katibu Mahsusi 3, Afisa Habari 1 na
Wasaidizi wa Kumbukumbu 4. Hii inafanya jumla ya
Ajira mpya kuwa 44.
(b)Kukarabati jengo la „Ardhi House‟ na Ukarabati ghorofa ya 7 na 6 umekamilika. Usanifu wa
kuanza ujenzi wa jengo la Upimaji jengo la Upimaji na Ramani umekamilika.
na Ramani.
(c)Kutoa mafunzo ya mfumo wa wazi Mafunzo ya OPRAS yamefanyika kwa wafanyakazi 80
wa upimaji kazi kwa watumishi wa ngazi ya kati na chini wa Idara ya Maendeleo ya
(OPRAS) hasa kwa watumishi wa Ardhi.
ngazi ya chini.
(d)Kumteua Mtaalam Mwelekezi kwa Mtaalam alipatikana na amekwishatoa taarifa yake na
ajili ya kutafiti na kuandaa taarifa ya kuiwasilisha Wizarani. Mafunzo kwa ajili ya waelimisha
hali ya maambukizi ya UKIMWI rika yamefanyika kuanzia Januari hadi Juni, 2007.
Wizarani na mapendekezo ya
mikakati ya kukabiliana na Janga
hili. Pia, kuongeza idadi ya
waelimisha rika kufikia 80 ikiwa ni
wastani wa watumishi 10 kwa
muelimisha rika mmoja.
28. Kusimamia mafunzo kwa wanafunzi 59 Usimamizi wa wanafunzi walioko katika Vyuo vya Ardhi
yanayotolewa na Chuo cha Ardhi cha Tabora na Morogoro unafanyika na hadi Mwezi Juni,
Morogoro (ARIMO) ambayo ni Diploma 2007, vyuo hivi vilikuwa na jumla ya wanafunzi 237 wa
153
na Cheti katika fani za Upimaji wa kozi za Cheti na Diploma. Chuo cha Ardhi Morogoro
Ardhi. Pia, kusimamia mafunzo kwa kina wanafunzi 100 wakati Chuo cha Ardhi Tabora kina
wanafunzi 88 yanayotolewa na Chuo wanafunzi 137.
cha Ardhi cha Tabora (ARITA) ambayo
ni Diploma na Cheti katika fani za
Urasimu Ramani na mafunzo ya Cheti
katika masomo ya Umiliki wa Ardhi na
Uthamini na Uchapaji Ramani.
154
WIZARA YA MIUNDOMBINU
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuendelea na utekelezaji wa Mradi
maalum wa ujenzi wa barabara kuu
zifuatazo kwa kiwango cha lami:-
Nangurukuru – Mbwemkulu(km.95). Jumla ya Km 47 za barabara zimejengwa katika
kiwango cha lami. Utekelezaji wa mradi huu kwa ujumla
umefikia asilimia 65. Ujenzi unaendelea.
Mbwemkulu – Mingoyo (km.95). Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 63. Tabaka
la lami halijaanza kuwekwa kutokana na mkandarasi
kutaka kutumia mawe ya kokoto zenye kiwango
kisichotakiwa. Kazi ya ujenzi huo inaendelea.
Dodoma – Manyoni (km.127). Hadi sasa Km 63 za tabaka la lami zimeshajengwa.
Utekelezaji wa mradi huu imefikia asilimia 58. Aidha,
ujenzi unaendelea.
Manyoni – Singida (km.119). Tayari Km 22 za barabara zimejengwa kwa kiwango
cha lami. Utekelezaji wa mradi huu kwa ujumla umefikia
asilimia 39. Aidha, ujenzi unaendelea.
2. Kuendelea na ukarabati wa barabara Mkandarasi amepatikana na mkataba wake ulisainiwa
ya Ilunde – Malagarasi. tarehe 21/11/2006. Kazi za ujenzi zinaendelea na
zimefikia asilimia 50.
3. Kuendelea na ukarabati kwa kiwango Ukarabati unaendelea ambapo kazi zilizo kamilika ni
cha lami sehemu ya barabara ya Km 23.6 za tuta, Km 18.1 la tabaka la mwanzo la
Mkuranga – Kibiti (km.45). msingi, Km 15.2 tabaka la mwisho la msingi, na Km 12
za tabaka la lami la kwanza limekamilika.
4. Kuendelea kufanya usanifu na Mkataba wa usanifu na uandaaji wa nyaraka za zabuni
kuandaa nyaraka za zabuni za ujenzi ulisainiwa mwezi Agosti, 2006. Kazi zinaendelea.
wa barabara ya Kigoma – Uvinza
(km.223) na Kaliua – Tabora (km.126).
5. Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Ujenzi kwa kiwango cha lami kwa kipande cha Km 80,
Nzega – Tinde – Isaka/ Tinde – Ilula madaraja 6, pamoja na makalvati yote yamekamilika.
(km.169) kwa kiwango cha lami. Mradi umekamilika kwa asilimia 96.
6. Kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kambi ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri
Kagoma – Lusahunga (km.154) kwa zimekamilika. Asilimia 80 ya mitanbo ipo eneo la kazi.
kiwango cha lami. Km 30 za barabara zimesafishwa, ujenzi wa tuta la
barabara na mifereji ya mvua unaendelea. Kokoto za
majaribio zinaendelea kutengenezwa. Ujenzi
unaendelea.
7. Kuendelea na ukarabati wa barabara Mkataba wa kazi ya ujenzi ulisainiwa tarehe
Shinyanga Border – Mwanza (km.10). 30/11/2006. Kazi zimeanza tarehe 05/03/2007, hadi
sasa kazi zimekamilika kwa asilimia 35.
155
8. Kufanya usanifu sehemu ya barabara Uchambuzi wa zabuni za Wahandisi Washauri
ya Nzega – Tabora. umekamilika mwezi Juni, 2007.
9. Kuendelea na Ujenzi wa barabara ya Ujenzi wa barabara ya Usagara- Bwanga unaendelea
Usagara – Bwanga – Kyamiorwa ambapo Km 47 zimewekewa tabaka la lami. Kazi
(km.120). Aidha, kuendelea na kazi ya imekamilika kwa asilimia 70.2.
ujenzi sehemu ya Kyamiorwa – Ujenzi wa sehemu ya Kyamihorwa – Buzirayombo
Buzirayombo (km.100). unaendelea ambapo Km 34 zimewekewa tabaka la
lami. Kazi imekamilika kwa asilimia 40.
10. Kuendelea na Ujenzi wa barabara ya Tuta la barabara Km 90, tabaka la msingi la kati Km 33,
Singida – Shelui (km.110) kwa na tabaka la msingi la juu Km 45 zimekamilika.
kiwango cha lami. Makalvati 117 yamekamilika. Asilimia 45 ya madaraja
yamekamilika. Tabaka la lami limekamilika kwa Km 5.8,
aidha ujenzi unaendelea.
11. Kufanya upembuzi yakinifu wa Mkataba wa ushauri ulisainiwa tarehe 02/02/2007.
barabara ya Sumbawanga – Matai – Mwezi Aprili, 2007 amewasilisha ripoti ya awali na
Kasanga – port/Matai – Kasesya. anaendelea na awamu ya kazi inayofuata.
12. Kuendelea na upembuzi yakinifu wa Mchakato wa kuwapata Wahandisi Washauri wa
barabara ya Sumbawanga – Mpanda – kufanya kazi za upembuzi yakinifu umekamilika. Kazi
Kanyani – Kigoma – Nyakanazi itaanza Julai, 2007.
(km.865).
13. Kuendelea na Ukarabati wa barabara Mkataba wa usanifu ulisainiwa Februari, 2007. Aidha,
ya Mwandiga – Manyovu (km.43). kazi ya ujenzi imekamilika kwa asilimia 15.
14. Kuendelea na ukarabati wa barabara Ujenzi wa barabara ulikamilika Desemba, 2006. Kazi za
ya Morogoro – Dodoma(km.256). kurekebisha sehemu na alama za barabara
zilizoharibiwa na mvua unaendelea.
15. Kukamilisha upembuzi yakinifu na Uchambuzi wa Zabuni za Wahandisi Washauri
usanifu wa barabara ya Dodoma – zilifunguliwa na unategemewa kukamilika mwezi Juni,
Mtera – Iringa (km.267). 2007.
16. Kukamilisha usanifu wa barabara ya Upembuzi yakinifu umekamilika na Mhandisi Mshauri
Minjingu – Babati – Dodoma. ameagizwa kuendelea na kazi ya Usanifu wa kina.
17. Kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha
lami barabara zifuatazo:-
Marangu – Tarakea – Rongai – Kwa kipande cha Marangu – Rombo Mkuu (Km 36)
Kamwanga. (km.100) uteuzi wa Mkandarasi umekamilika na mkataba
ulisainiwa tarehe 23/02/2007. Mkandarasi anaendelea
kupeleka vifaa.
Kipande cha Rombo Mkuu – Tarakea (Km 32)
Mkandarasi ameanza kazi za awali.
Kipande cha Tarakea – Kamwanga (Km 32) Km nane
(8) zimewekwa tabaka la lami la awali, Km 14 za
barabara zimekamilika kwa kuweka tabaka la juu na
Km 14 zimekamilika kwa kiwango cha tabaka la chini.
Ujenzi wa makalvati yote umekamilika. Hadi sasa kazi
156
zimekamilika kwa asilimia 60.
Rujewa – Madibira – Mafinga. Mkataba wa kazi za ujenzi unategemewa kusainiwa
mwezi Juni, 2007 baada ya kukamilisha majadiliano ya
kupata mkopo kutoka ADB.
Mbeya – Chunya – Makongolosi. Mradi umegawanywa sehemu tatu, ambapo mapitio ya
nyaraka za zabuni yamekamilika. Uchumbuzi wa
zabuni unaendelea na unatarajia kukamilika mwezi
Juni, 2007.
Msimba – Ikokoto – Mafinga. Usanifu umekamilika. Nyaraka za zabuni za ujenzi
zimepelekwa kwa mfadhili kwa ajili ya kuzipitia na kutoa
kibali.
Arusha – Namanga. Zabuni kwa ajili ya ujenzi zilitangazwa tarehe
30/10/2006, na kuwasilishwa tarehe 16/03/2007.
Uchambuzi wa zabuni unaendelea na unategemewa
kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2007.
18. Kuanza Kufanya ukarabati wa
barabara zifuatazo:-
Dsm – Mbagala (Kilwa Road Mkataba wa usanifu na usimamizi ulisainiwa mwezi
km.12). Agosti, 2006. Zabuni zimeitishwa mwezi Septemba,
2006 na zimepokelewa mwezi Desemba, 2006 ambapo
mkandarasi aliyeteuliwa alisaini mkataba tarehe 21
Desemba, 2006 nchini Japani. Kazi zimeanza rasmi
mwezi Februari, 2007.
Nelson Mandela (km.16.8). Mkataba wa Mhandisi Mshauri umesainiwa. Zabuni kwa
ajili ya ukarabati zilifunguliwa tarehe 21/02/2007 na
uchambuzi unaendelea.
Sam Nujoma (km. 4). Ujenzi unaendelea na umekamilika kwa asilimia 33.
19. Kuhimiza maandalizi ya ujenzi wa NSSF walileta maombi Wizarani ili Wizara iombe
daraja la Kigamboni chini ya Uongozi Hazina kuthibitisha mambo yafuatayo.
wa Shirika la Hifadhi ya jamii ili Kuithibitishia Serikali ya Uholanzi kuwa mradi huu ni
kuunganisha Kigamboni na Jiji la Dar wa kipaumbele (Letter of Priority) kwa mujibu wa
es Salaam. matakwa ya kupata msaada chini ya utaratibu wa
ORET.
Kutoa dhamana kwa NSSF kuweza kukopa katika
benki ya Uholanzi.
Kuthibitisha kuwepo kwa fedha za ujenzi wa
“Package” Na. 2 na gharama za fidia kwa usumbufu
utakaotokea kwa jamii.
157
Wizara ya Fedha iliafiki na kushauri mapendekezo haya
yapelekwe Baraza la Mawaziri kwa maamuzi. Wizara
imekwisha andaa Rasimu ya Waraka kama
ilivyopendekezwa na sasa yanasubiriwa maamuzi ya
Baraza la Mawaziri.
20. Kukamilisha usanifu na kuandaa Kazi ya usanifu na kuandaa nyaraka za zabuni
Nyaraka za zabuni za Ujenzi wa imekamilika. Majadiliano yanaendelea na kampuni ya
barabara ya Tanga – Horohoro (km.65) MCC toka Marekani kwa ajili ya kugharimia ujenzi.
kwa kiwango cha lami.
21. Kukamilisha Usanifu na kuandaa Mhandisi Mshauri anaendelea na kazi za usanifu na
nyaraka za zabuni za ujenzi wa kuandaa nyaraka za zabuni na anatarajiwa
barabara ya Tunduma – Sumbawanga kuzikamilisha mwezi Juni, 2007.
(km.231) kwa kiwango cha lami.
22. Kukamilisha ujenzi wa daraja jipya la Ujenzi umekamilika.
Mpiji.
23. Kufanya upembuzi yakinifu, usanifu na Kazi ya Upembuzi Yakinifu na Usanifu imekamilika kwa
ujenzi wa daraja la Mto Kilombero. kiwango cha asilimia 30.
24. Kukamilisha ujenzi wa daraja la Mto Kazi ya usanifu na uandaaji wa nyaraka za zabuni
Mwatisi katika mkoa wa Morogoro. umekamilika. Zabuni za ujenzi zitaitishwa baada ya
kupatikana fedha za ujenzi.
25. Kuendelea na usanifu wa ujenzi wa Mkandarasi ameanza kazi ya ujenzi wa mihimili ya
daraja jipya la Ruvu. kubeba nguzo za daraja jipya. Matayarisho ya ujenzi
wa tuta la barabara za maingiliano yameanza.
26. Kuendelea na ujenzi wa Daraja la Ujenzi wa mradi huu umekamilika kwa asilimia 25
Umoja. ambapo kazi zilizofanywa ni pamoja na:
Ujenzi wa nguzo 6 za daraja; Ujenzi wa nguzo za
msingi 5 uko katika hatua mbalimbali; Daraja la muda
(Bailey Bridge) limewekwa na Mkandarasi tarehe
24/09/2006 ili kuvusha mitambo na vifaa upande wa
Msumbiji; Usanifu wa kina ulikamilika na kuidhinishwa
tarehe 04/09/2006; Calvati 2 kwa upande wa Tanzania
zimekamilika; Kazi ya kujenga msingi wa barabara
kwa Tanzania na Msumbiji unaendelea.
27. Kuanzisha programu ya Taifa ya Mpango huu sasa unatekelezwa na TAMISEMI.
Usafiri Vijijini.
28. Kujenga mwamko wa kuzingatia Yafutayo yameanza kuzingatiwa:
mahitaji maalum ya watu wenye Kuwekwa kwenye sheria ya majengo (Codes,
ulemavu katika ujenzi wa majengo standards & specification).
yanayotumiwa na umma. Kuwekwa kwenye sera ya nyumba na majengo
suala la walemavu.
Kuna miradi kumi katika Tanzania ambayo imeanza
kutekelezwa kwa kuzingatia mahitaji maalum ya
walemavu.
158
29. Kuendelea kujenga nyumba za Nyumba 12 za bei nafuu zinajengwa kila mkoa, mpaka
watumishi wa Serikali kwa ajili ya sasa mikoa 16 zinajengwa nyumba 12 na mikoa miwili
kuwauzia. nyumba 4 kila mmoja.
Mradi wa ujenzi wa nyumba 200 mikoani kote Tanzania
bara uko katika hatua mbalimbali.
Mradi wa ujenzi wa nyumba 25 za bei nafuu Jijini Dar
es Salaam. Aidha, Wakala pia unajenga majengo
matatu ya ghorofa ya familia sita kila moja kwa ajili ya
kupangisha katika Jiji la Dar es Salaam.
30. Kujenga kwa kiwango cha lami Barabara hii ipo katika hatua mbalimbali za ujenzi kama
barabara ya Iringa – Dodoma – zilivyoelezwa katika na. 15 na 16 hapo juu.
Arusha.
31. Kukamilisha zabuni na kuanza ujenzi Taratibu za kumpata mkandarasi ziko katika hatua za
wa sehemu ya barabara ya Ndundu – mwisho.
Somanga (km.60).
32. Kuweka vivutio kwa sekta binafsi ili Serikali imechukua hatua zifuatazo:
ishiriki uwekezaji kwenye ujenzi wa Uanzishwaji wa „National Fibre Optic‟ kwa ajili ya
Miundombinu inayohitajika katika kurahisisha upelekaji wa huduma za mawasiliano
ukuaji wa Miji. hadi vijijini na kwa gharama nafuu.
Uanzishaji wa mfuko wa Maendeleo ya Huduma za
Mawasiliano (Universal Communication Access
Fund) utakaotumika kufidia gharama za huduma za
mawasiliano kwenye maeneo yasiyo na mvuto wa
kibiashara.
33. Kufanya upembuzi yakinifu wa
barabara ya:-
Bagamoyo – Saadani – Tanga. Zabuni ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya
upembuzi yakinifu ilitangazwa mwezi Novemba, 2006
na itawasilishwa tarehe 05/07/2007.
Musoma – Mugumu – Loliondo – Mkataba wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu
Mto wa Mbu. ulisainiwa mwezi Agosti, 2006. Kazi zimekamilika kwa
asilimia 75.
34. Kufanya upembuzi yakinifu na usanifu Uchambuzi wa Zabuni za kumpata Mhandisi Mshauri
wa barabara ya Bagamoyo – Msata. umekamilika na mkataba unategemewa kusainiwa
mwezi Juni, 2007.
35. Kuendelea na Ukarabati wa barabara Uchambuzi wa maombi ya Makandarasi wanaotaka
ya Same – Mkumbara –Korogwe kushiriki zabuni kwa ajili ya kazi ya ujenzi unatarajiwa
(km.165). kukamilika mwezi Juni, 2007.
36. Kuimarisha kivuko cha Pangani. Kivuko cha Pangani kimefanyiwa matengenezo
makubwa kwenye injini zake mwezi wa Desemba,
2006. Pia mtambo wake wa kuendeshea (Propulsion
Unit) umefanyiwa matengenezo mwezi Machi, 2007.
159
Kivuko hicho kimekuwa kikifanyiwa matengenezo ya
kinga (Preventive Maintenance) kulingana na ratiba ya
matengenezo“Maintenance. Matengenezo hayo yote
yameigharimu Wakala kiasi cha Tshs. 11,700,000/=.
TANROADS wamepeleka Benki ya Dunia zabuni ya
ununuzi wa kivuko kipya ili kupata „No Objection‟ ya
kutangaza tena zabuni hiyo baada ya mkandarasi wa
kwanza kushindwa kusaini mkataba.
37. Kufanya Usanifu wa kina wa sehemu Mhandisi Mshauri amepatikana kufanya usanifu na
ya Songea – Matemanga na Masasi – uandaaji wa nyaraka za zabuni katika sehemu ya
Mangaka katika barabara ya Mtwara – Songea – Tunduru (km 265), ambapo kazi ilianza
Masasi – Songea – Mbamba Bay. mwezi Januari, 2007.
Kampuni ya kihandisi kwa ajili ya kufanya usanifu wa
awali wa sehemu ya Masasi – Mangaka imekamilika.
Usanifu wa kina unaendelea na unatarajia kukamilika
Julai, 2007.
38. Kujenga Majengo manne ya ghorofa Ujenzi wa majengo saba katika mkoa wa Dar es
Dar es Salaam na mawili Salaam na majengo mawili mkoani Arusha umeanza,
Arusha. na jengo moja mkoani Dar es Salaam liko katika hatua
ya upembuzi yakinifu.
Kujenga nyumba za viongozi katika Nyumba za viongozi 91 Jijini Dar es Salaam na 38
mikoa mbalimbali zikiwemo mikoani yaani mbili kila mkoa isipokuwa Dar es Salaam
nyumba za Majaji. na Dodoma zipo katika hatua ya mwisho. Nyumba 42
katika wilaya mpya za Chato, Mkinga, Siha na
Nanyumbu zipo katika hatua ya mwisho. Aidha,
Nyumba 4 za Majaji Jijini Dar es Salaam zipo katika
hatua mbalimbali za ujenzi.
Kutafuta viwanja jijini Dar es Fedha zimetengwa kwa ajili ya kununua viwanja 2 Dar
Salaam kwa ajili ya ujenzi wa es Salaam, 1 Dodoma, 1 Arusha na 1 Mwanza. Aidha,
nyumba. fedha nyingine zimetengwa kwa ajili ya kupata na
kupima viwanja mikoani. Viwanja 400 vilivyo katika
mradi wa Bunju Dar es Salaam vimenunuliwa.
Kuhifadhi jengo moja la kihistoria Jengo hilo limetambuliwa na hatua za kutambua
mkoani Lindi. gharama za ukarabati zimeanza kuchukuliwa.
Kufanya matengenezo ya kawaida Matengenezo ya kawaida yaliyo katika hatua
ya nyumba pamoja na Ofisi za mbalimbali yanaendela.
Serikali.
39. Kufanya Mapitio ya Majukumu ya Kazi hiyo imekamilika na „Business Plan‟ ya mwaka
TEMESA kwa lengo la kuainisha 2006/07 imepitishwa mwezi November, 2006.
160
shughuli ambazo zitaendelea
kufanywa na wakala kulingana na
malengo mapya ya Wizara ya
Miundombinu.
40. Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Mfuko wa Maendeleo ya Sekta ya Ujenzi (CIDF).
kuendelea na jitihada za kuhakikisha Kwa sasa hatua zinazoendelea zinajumuisha ajira ya
mfuko wa maendeleo ya sekta ya Mtaalam wa mambo ya fedha ambaye atatayarisha
ujenzi (Construction Industry miongozo na nyaraka kwa ajili ya utoaji huduma na
Development Fund – CIDF) unaanza “Business Plan”. Hii itafuatiwa na kumwajiri Meneja wa
kufanya kazi na kuendeleza maandalizi Mfuko.
ya mazingira mazuri ya utekelezaji wa
miradi ya ujenzi kwa njia ya ubia kati Mazingira ya Utekelezaji Miradi kwa njia ya ubia kati
ya sekta ya Umma na sekta Binafsi ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP).
(PPPs). Katika mwaka huu wa fedha, miongozo ya kiufundi
ilikamilika. Miongozo hiyo inahusu namna ya kufanya
upembuzi yakinifu, usimamizi wa mikataba, utunzaji wa
mahesabu ya fedha na ukaguzi wake. Mwaka ujao wa
fedha Rasimu ya Sera ya Taifa ya Ubia kati ya Sekta ya
Umma na Sekta binafsi itaandaliwa.
41. Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB) Hadi tarehe 30/04/2007 Bodi ilikusanya jumla ya Shs
kukusanya jumla ya shilingi 77,123.9 milioni 83,917 ikiwa ni mapato yatokanayo na vyanzo
milioni ikiwa ni mapato yanayotokana vyake mbalimbali.
na vyanzo vyake mbalimbali.
42. Kusajili wahandisi 620 na Kampuni Wahandisi 543 wamesajiliwa na kampuni za ushauri wa
za Ushauri wa Kihandisi 20. kihandisi 10 zimesajiliwa.
Kusimamia utekelezaji wa mpango Jumla ya wahandisi wahitimu waliopo katika mpango
wa mafunzo ya vitendo kwa huu hadi sasa, ni 855.
wahandisi wahitimu wapatao 700.
Kufanya ukaguzi wa shughuli za Ukaguzi wa shughuli za kihandisi na wahandisi
kihandisi nchini ili hatimaye ulifanyika katika Migodi mikubwa yote nchini, na pia
shughuli zote za kihandisi ziwe katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro,
zinafanywa na wahandisi Dodoma, Rukwa, Kigoma, Mwanza, Shinyanga, Mara,
waliosajiliwa kwa kufuata maadili ya Tanga, Kilimanjaro, Manyara, Kagera, Tabora, Mbeya
utendaji kazi za kihandisi. na Iringa. Jumla ya Makampuni ya kihandisi 46
yalikaguliwa.
43. Kusajili wataalam wa usimamizi wa Katika kipindi cha 2006/2007 wataalamu wapatao 64
vifaa pamoja na Uboreshaji wa walisajiliwa.
kiwango cha sifa za kujiunga na
mafunzo.
Kupanua huduma za Bodi ya Taifa Bodi imeanza mchakato wa kurekebisha mitaala
ya Usimamizi wa Vifaa (NBMM) iliyoanza kutumika kuanzia 2004 kwa lengo la
kwa kufungua vituo vya kuboresha sifa za kujiunga na mafunzo ya NBMM.
kuendeshea mafunzo au mitihani Mtaala mpya unategemea kukamilika mwaka ujao wa
161
katika mikoa mingi zaidi badala ya fedha. Juhudi zilizofanywa na Bodi kufungua vituo vya
kutegemea huduma zitolewazo kuendeshea mitihani au mafunzo mikoani hazijaweza
sasa katika mikoa ya Mbeya, kukamilika vyema; hata hivyo kuna uwezekano
Arusha, Mwanza, Singida, Mtwara, mkubwa wa kufungua kituo Dodoma ambapo
Tanga, Kilimanjaro, Dar es Salaam maandalizi yanaendelea vizuri.
na Visiwa vya Zanzibar na Pemba.
44. Kukuza uwezo wa makandarasi wa Rasimu ya mkakati wa makusudi wa kuendeleza
ndani kufikia viwango vya kimataifa makandarasi wazalendo “Program for Deliberate
ili kujenga uwezo wa Taifa katika Development of Selected Contractors” unaandaliwa
kutekeleza miradi mikubwa na waraka “Cabinet Paper” ili Baraza la Mawaziri uweze
hivyo kuwezesha Makandarasi kuridhia mpango huo.
wenzao wadogo kupata miradi kwa
njia ya “Sub-Contracts”.
Kusajili, kuratibu na kutoa mafunzo Bodi imekamilisha vigezo vya usajili wa makandarasi
kwa makandarasi wa nguvu kazi ili wa nguvu kazi katika ujenzi wa barabara katika
kuwezesha Watanzania wenye madaraja matatu. Bodi imesajili makandarasi 99 katika
mtaji kidogo kushiriki katika kazi za fani hii. Aidha, Bodi imeendesha kozi tatu za mafunzo
ujenzi. kwa ajili ya makandarasi.
45. Bodi ya Wabunifu Majengo na
Wakadiriaji Majenzi (AQSRB):
Kusajili wataalam 35 na wale Wataalam 54 na wenye sifa 39 wamesajiliwa; Kampuni
wenye sifa za kati 75; Kusajili 23 za kitaalam zimesajiliwa; Wataalamu 100
kampuni za kitaalam 15 na kutahini wametahiniwa
watalaam watarajiwa 81.
Kuendeleza mpango wa mafunzo Wahitimu 60 wako katika mafunzo katika makampuni
maalum ya vitendo kwa ajili ya ya kitaalam ya ubunifu majengo na ukadiliaji majenzi na
kuwasaidia wahitimu 60 wa 18 wamehitimu mafunzo hayo.
taaluma husika ili waweze
kusajiliwa kwa mujibu wa Sheria.
Kuangalia upya mfumo wa mitihani Mfumo ya mitihani, na mitaala mipya katika fani za
na mfumo mzima wa usajili kwa ubunifu majengo na ukadiriaji majenzi imekamilika na
lengo la kuimarisha na kuvutia imeanza kutumika. Utafiti juu ya mfumo mzima wa
wataalam wengi zaidi kujisajili. usajili na maeneo mengine ya mfumo wa mitihani bado
inafanyiwa kazi.
46. Chuo cha ujenzi Morogoro (MWTI)
Kufundisha mafundi sanifu Hadi sasa chuo kimeshafundisha Mafundi sanifu
(Technicians) 120, madereva mahiri 40 (Technicians) 65, Madereva mahiri 12 na Mafundi
pamoja na kuendesha mafunzo ya stadi (artisans) 52 na madereva wa awali 64.
mafundi stadi mbalimbali (artisans) 65
na wanafunzi wa udereva wa awali
160.
162
47. Chuo cha Matumizi Stahili ya nguvu
kazi (Appropriate Technology Training
Institute – ATTI)
Kuimarisha kitengo cha “Labour Kitengo kimeanzishwa na Mratibu wa mradi
Based Technology Unit” (LBTU) ameteuliwa. Aidha, Vifaa vya ofisini na usafiri
ili kiweze kusimamia utekelezaji vimenunuliwa. Taratibu za kuajiri na kuwahamishia
wa mpango wa “Taking Labour Wahandisi kwenda katika kitengo hiki unaendelea.
Based Technology (LBT) to
scale”.
Kushiriki kwenye Maandalizi ya Maandalizi ya kumpata Mshauri Mwelekezi “Consultant”
Sera ya kitaifa ya Matumizi ya atakayepitia sera za sekta mbalimbali ili kubaini mahitaji
teknolojia ya nguvukazi katika muhimu ya uandaaji wa sera ya nguvu kazi
kazi mbalimbali za Miundombinu. yanaendelea.
Kukiendeleza kituo cha utunzaji Ukumbi wa kuanzisha kituo hiki upo tayari na vifaa vya
habari zihusuzo teknolojia ya ofisi vimenunuliwa.
nguvukazi.
Kuandaa mtaala mpya na Kazi ya kuboresha mtaala wa Chuo kwa ushirikiano na
kukiandikia chuo (NACTE) ili JICA imeanza.
kiweze kutoa mafunzo
yanayotambuliwa kitaifa na
kimataifa.
48. Kufanya ukarabati barabara ya Kibiti – Mkandarasi amepatikana na kuanza kazi tarehe 10
Utete. Novemba, 2006. Kazi ya kuchonga tuta imekamilika
kwa asilimia 10.
49. Kufanya upembuzi yakinifu katika Kiasi cha shilingi 240 milioni kimetengwa. Kazi itaanza
barabara ya Bomang‟ombe – baada ya kumpata Mhandisi Mshauri. Kwa sasa
Sanyajuu. taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri zinaendelea.
50. Kuendelea na ujenzi kwa kiwango cha Kazi zinaendelea na zipo katika hatua za mwisho za
lami kwa barabara ya Sangasanga kukamilika.
kuelekea chuo Kikuu cha Mzumbe.
51. Kufanya ukarabati katika barabara ya Kiasi cha shilingi milioni 57 kimetengwa kwa kazi za
Uru (Rau) - Mlimani ukarabati wa barabara hiyo kwa kiwango cha
changarawe. Kazi zilianza mwezi Machi, 2007 na
zinaendelea.
52. Kuanza ujenzi wa barabara ya Muuze Barabara itafanyiwa ukarabati chini ya ufadhili wa
– Kilyamatundu (km. 170) kwa kiwango DANIDA. Kiasi cha shilingi milioni 290 kwa mwaka huu
cha changarawe. kimetengwa kugharamia kazi hizo. Kwa sasa taratibu
za kumpata mkandarasi zinaendelea.
53. Kuendelea na ukarabati wa barabara Kazi zilianza mwezi April, 2007 na zinaendelea.
ya Magu – Ngudu – Jojiro ( km. 64)
54. Kufanya usanifu wa kina katika Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kwa
barabara ya Mikumi – Kilosa. barabara yenye urefu wa kilometa 150 kutoka Mikumi –
163
Kilosa hadi Dumila imekamilika mwezi Mei, 2007.
55. Kuzirekebisha sheria nane za sekta ili Mapendekezo ya mabadiliko ya Sheria Na. 20 ya 1979
ziendane na sera na mwelekeo wa ya Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) na Sheria Namba 9
uchumi wa soko. Sheria zilizoko katika ya mwaka 1981 ya Bodi ya Taifa ya Usimamizi wa
utaratibu wa kufanyiwa mapitio ya Vifaa (NBMM) yalijadiliwa na Kamati ya Makatibu
sheria ni sheria ya TAA, TMA, CRB, Wakuu (IMTC) tarehe 15/11/2006. Mapendekezo hayo
AQSRB, NBMM, ERB na NCC. sasa yanasubiri kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri
kabla ya kufikishwa Bungeni.
Mapitio ya sheria za sekta za TAA, AQSRB, na ERB
yanaendelea. Aidha, Rasimu ya Sera ya Hali ya Hewa
imekamilika na iliwasilishwa kwa Wadau wa Sekta kwa
utekelezaji zaidi.
56. Kuendelea na mikakati ya Mazingira ya sekta binafsi katika uwekezaji na utoaji wa
kuboresha viwanja vya ndege kwa huduma yanaendelea kuwekwa kwa kushirikisha sekta
kushirikisha sekta binafsi katika binafsi. Hadi sasa Mamlaka imependekeza viwanja
uwekezaji na utoaji huduma vitatu vya Julius Nyerere, Mwanza na Arusha ili kutoa
nyingine. huduma kwa kushirikiana na sekta binafsi. Mamlaka
imeshafanya hatua za awali za kutangaza miradi ya
uwekezaji kwa kiwanja cha ndege cha Julius Nyerere.
Kuendeleza kiwanja cha ndege cha TAA inaendelea kukikarabati kiwanja kinachotumika
Singida sasa ili kiweze kutoa huduma kwa mkoa wakati
mpango wa kujenga kiwanja kipya eneo la Manga
ukiendelea.
Kuanza ukarabati wa kiwanja cha Mamlaka imepanga kufanya ukarabati wa barabara ya
ndege cha Mafia kurukia na kutua ndege, kiunga chake na maegesho ya
ndege kwa kiwango cha changarawe kwa kujenga
tabaka la kwanza. Aidha, Mamlaka imekwisha
kamilisha mchakato wa manunuzi ambapo Mkandarasi
na Mhandisi Msimamizi wamekwisha patikana.
Mkandarasi alikabidhiwa eneo la kazi tarehe
16/05/2007 na kazi itachukua muda wa miezi saba.
57. Kuendelea kufanya matengenezo ya Mamlaka imeendelea na Mradi wa kukarabati reli katika
reli ya TAZARA kati ya Kitete-Mpanga. eneo la Km 561 na 500m, Mpanga – Kitete (Landslide
formation repair and rail alignment).
58. Shirika la Reli Tanzania (TRC)
kuendelea na utekelezaji wa mradi Kazi hii ilikamilika Juni, 2006.
wa kutandika nyaya (optic fibre) za
mawasiliano ya simu katika njia ya
reli kati ya Dodoma na Tabora.
Shirika la Reli kuendelea
kutekeleza mradi wa kutandika Fedha za kutekeleza mradi huu hazikupatikana na
164
upya reli za uzito wa ratili 80 badala hivyo kazi hiyo haikufanyika.
ya 56 ambapo jumla ya kilometa
26.5 katika sehemu zilizochakaa
zaidi kati ya Tabora na Kigoma
zitakarabatiwa
59. Kufanya utafiti kubaini mahitaji Utafiti uko katika hatua ya kutafuta mzabuni.
muhimu ya bandari zote katika Makampuni yaliyoonyesha nia ya kufanya utafiti (EOI)
Bahari na Maziwa nchini (Ports yamejitokeza na kibali cha benki ya Dunia kimepatikana
Master Plan Study). mwezi Novemba, 2006. Kazi ya kuitisha zabuni
inaendelea na utafiti umeanza mwezi Januari, 2007.
Kuendelea na uboreshaji wa Jumla ya Shilingi bilioni 40.9 zimetengwa kwa ajili ya
maeneo ya kazi ili kulinda ufanisi kununua vifaa mbalimbali na ukarabati katika bandari
na ubora wa rasilimali iliyopo za Dar es salaam, Tanga, Mtwara na bandari za
maziwa. Vifaa vilitarajiwa kuwasili mwezi Machi, 2007.
Kuinua uwezo wa bandari kwa Zabuni kwa ajili ya kazi za ukarabati na
kukarabati na kubadilisha vifaa na matengenezo zimetangazwa na kazi imeanza mwezi
maeneo ya kuhudumia meli na Machi, 2007. Mchakato wa ununuzi wa vifaa
mizigo unaendelea.
Ununuzi wa pantoni ya kupokelea Shirika la kuhudumia wakimbizi Duniani (UNHCR)
abiria na mizigo kutoka kwenye waliomba na kupewa kibali cha kununua na kuweka
meli (landing pantoon) katika pantoni, Kazi ya kununua na kuweka pantoni
bandari ya Kigoma. imekamilika mwezi Novemba, 2006.
Uchambuzi wa makadirio ya gharama za matengenezo
Kufanya ukarabati wa gati la unaendelea na kazi ilitarajiwa kuanza mwezi Machi,
Kasanga 2007.
60. Kampuni ya Meli ya Serikali ya China Kampuni kwa kushirikiana na Kampuni ya Meli ya
na Tanzania (SINOTASHIP) itaongeza Uchina (COSCO) inaendelea kutafuta meli inayofaa ili
meli moja ili kuongeza utendaji wa iweze kununuliwa. Vigezo vinavyozingatiwa ni pamoja
Kampuni kibiashara na kumudu na ukubwa, bei, na umri wa meli.
ushindani.
61. Serikali itaendelea na juhudi za Katika kipindi husika ajali za treni zilizotokea katika
kuhakikisha kuwa ajali za treni Shirika la Reli Tanzania (TRC) zilikuwa 56 , na
zinapungua. SUMATRA itabuni na zilipungua hadi kufikia 33 katika kipindi cha Julai-
kuandaa mpango wa usalama wa Septemba 2006. Aidha, ajali zilianza kuongezeka hadi
usafiri wa reli. kufikia ajali 49 katika kipindi cha Januari-Machi 2007.
Hali hiyo ilitokana na kukosekana kwa matengenezo ya
njia na uchakavu wa mabehewa.
Kwa upande wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na
Zambia (TAZARA) hali ilikuwa ya kuridhisha. Ajali
165
kubwa zilipungua kutoka ajali 20 hadi kufikia ajali 7
(saba) katika kipindi cha Januari-Machi, 2007. Hii
inatokana na juhudi mbalimbali zilizofanyika ikiwa ni
pamoja na kufanya matengenezo ya njia.
Kuandaa semina, warsha na SUMATRA ikishirikiana na wadau mbali mbali wa
kutumia redio, television, magazeti, huduma za mizigo bandarini inaendelea kuratibu
vipeperushi, na pia kwa shughuli za utoaji mizigo bandarini. Kwa hivi sasa
kushirikiana na wadau ili kuweza wastani wa Makontena 350 kwa siku hutolewa
kuboresha ufanisi wa utoaji mizigo bandarini ukilinganisha na awali ambapo wastani wa
bandarini. makontena 250 kwa siku yalikuwa yakitolewa.
Kuimarisha ukaguzi wa vyombo vya Katika kuimarisha ukaguzi wa vyombo vya usafiri
usafiri majini majini, mwezi Julai, 2006 na Januari, 2007 SUMATRA
ilitangaza zabuni kwa ajili ya kupata makampuni
yatakayofanya shughuli za ukaguzi wa vyombo vya
majini. Usaili wa makampuni yaliyojitokeza
umekamilika na uteuzi rasmi wa makampuni
yaliyoshinda utafanyika karibuni. Kwa yale maeneo
ambayo hayakupata mzabuni, SUMATRA kwa
kuwatumia wataalam wake itafanya ukaguzi husika.
Aidha, mwezi wa Julai, 2006, SUMATRA iliajiri maofisa
watatu (Flag and Port State control officers) katika vituo
vya Bukoba, Kigoma na Kyela.
Kuendelea na ujenzi wa kituo cha Ujenzi wa mnara wa kuongozea meli na ambao
kuongozea meli na kutafuta meli utasaidia katika suala zima la utafutaji na uokoaji
zilizopotea au kupata ajali katika (Maritime Rescue Coordinating Sub Centre – (MRCSC)
eneo la bandari ya Dar es Salaam kwa eneo la bahari ya Hindi kwa vyombo vinavyopata
kwa kutumia vifaa vya mawasiliano ajali au kupotea baharini unaendelea vizuri. Mnara huu
vya ubora wa kimataifa. unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba, 2007.
62. Kuendelea kufanya kaguzi katika Hili ni zoezi la kudumu na endelevu. Mamlaka imeweka
viwanja vyote vya ndege nchini ili ratiba ya kaguzi za kupangwa na kushtukiza kwa
kufikia viwango vya Kimataifa vya viwanja vya ndege, makampuni ya ndege na watoa
usalama wa anga. huduma katika usafiri wa anga nchini.
Kufunga mitambo na vifaa mbali Mradi wa kufunga nyaya za mawasiliano (optic fibre
mbali katika viwanja vya Dar es project) ili kurahisisha mawasiliano ya kuongoza ndege
Salaam, Zanzibar, Mwanza, uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere umekamilika.
Kilimanjaro, Songwe, Tabora na
Kigoma. Mtambo wa kuzalisha nguvu za umeme kwa kutumia
mionzi ya jua kwa ajili ya mtambo wa kuongozea ndege
NDB Delta Mike pamoja na benki ya betri umefungwa.
Zabuni imekwishatolewa kwa ufungaji wa „Doppler
166
VOR- DME katika uwanja wa ndege wa Kilimanjaro ili
kuongeza ufanisi kwa waongoza ndege.
Mitambo ya kuongoza ndege ya VOR/DME imefungwa
katika Uwanja wa ndege wa Zanzibar pamoja na
mtambo wa dharura wa umeme (standby generator
25KVA) ili kuimarisha usambazaji wa umeme. Aidha,
Meza ya waongoza ndege pamoja na radio zake mpya
pia imefungwa.
Jenereta la dharura la umeme (standby generator
25KVA) limefungwa ili kuimarisha usambazaji wa
umeme uwanja wa ndege wa Mwanza.
Katika Uwanja wa ndege wa Tabora uzio wa
kuimarisha usalama wa mitambo umekamilika ;
Mtambo wa kuzalisha nguvu za umeme kwa kutumia
mionzi ya jua (solar power) ili kuimarisha upatikanaji wa
umeme kwa mitambo ya kuongoza ndege pamoja na
Mitambo mipya ya kuongoza ndege (NDBs) imefungwa.
Aidha, mtambo mpya wa radio kwa mawasiliano wakati
wa tahadhari na dharura (121.500Mhz Distress radios)
umefungwa.
Zoezi la kufunga mitambo Uwanja wa ndege wa
Songwe linasubiri kukamilika kwa ujenzi wa uwanja.
Katika Uwanja wa ndege wa Kigoma mtambo mpya wa
radio kwa mawasiliano wakati wa tahadhari na dharura
(121.500Mhz Distress Radios) pamoja na „Antenna‟
mpya kwa ajili ya mitambo ya mawasiliano na ndege
kutoka kwenye mnara wa waongoza ndege
vimefungwa.
Kuweka mtambo maalum wa Mtambo huu unafungwa ili kufuatilia mienendo ya watu
kuona kwa njia ya televisheni na matukio mbalimbali na kuweka kumbukumbu.
(CCTV) katika kiwanja cha Mpaka sasa jengo la abiria Na. 2 (TB II) na kamera
ndege cha kimataifa cha zimekwisha fungwa. Jengo la Na. 1 (TBI) utandazaji wa
Mwalimu J.K.Nyerere nyaya kuunganisha maeneo yatakayofungwa kamera
yanaendelea.
63. Kukamilisha taratibu za kuhamisha Nyumba 3 za Nairobi, nyumba 1 ya Lusaka na nyumba
umiliki wa nyumba tano zilizoko 1 ya Harare zimekabidhiwa Wizara ya Mambo ya Nje
Johannesburg, Lusaka na Nairobi. na Ushirikiano wa Kimataifa.
Kukamilisha uuzaji wa mali Nyumba zote za Dar es Salaam zimeuzwa. Nyumba za
zisizohamishika zilizoko KIA na KIA, Harare na Lusaka bado zipo katika hatua
167
uuzaji wa nyumba zilizoko Dar es mbalimbali za uuzaji.
salaam, KIA, Harare na Lusaka.
64. Kuendelea kudumisha na kuboresha Wakala iliendelea kutimiza masharti yatolewayo na
usalama, aina na ubora wa huduma za Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) na Mamlaka za
Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA). Kimataifa ikiwemo ICAO. Katika utekelezaji huo
Wataalam mbalimbali wamepelekwa mafunzoni pamoja
na kuzingatia Matengenezo ya ndege kulingana na
ratiba na yale ya dharura kulingana na viwango vya
Kimataifa.
65. Kuhakikisha watoa huduma za Mpango huu unatekelezwa chini ya “Association”
takwimu (data) na mtandao iitwayo “Tanzania Internet Service Providers
(Internet Service Providers) Association - TISPA” iliyoanzishwa mwezi April, 2005.
wanajiunganisha kwenye mitambo Mitambo imewekwa Dar es Salaam na inafanya kazi
ya kuunganisha mawasiliano hayo ambapo jumla ya makampuni 12 ya watoa huduma za
kitaifa (Internet Exchange points - takwimu na intaneti yameunganishwa. Baadaye
IXPs) ili kupunguza gharama kwa mitambo ya IXPs itasimikwa katika mikoa ya Mwanza,
watumiaji kwa kutumia njia na Arusha, Zanzibar na Mbeya.
masafa ya kimataifa wakati wa
kufanya mawasiliano ndani ya nchi.
Kuwezesha nchi kuwa na mhimili Kamati maalum (Task Force) ya maandalizi ya
wa Teknolojia ya Habari na “National ICT Broadband Infrastructure Backborne
Mawasiliano ya kisasa na yenye Network” imeshaundwa, na imekutana na kutoa
uwezo mkubwa kwa kuendelea mapendekezo Serikalini kwa ajili ya hatua zaidi.
kushirikiana na Baraza la Watumiaji
wa Huduma za Mawasiliano
pamoja na jumuiya za watoa
huduma za mawasiliano ili
kuhakikisha kuwa viwango
vinavyotozwa vinakuwa vya bei
nafuu.
66. Kutekeleza ujenzi wa Njia kuu za Mkandarasi alishapatikana, na kwa sasa kazi za ujenzi
simu “Digital Microwave” kati ya inaendelea. Kazi hii inategemewa kukamilika mwishoni
Dar es Salaam na Dodoma na Dar mwa mwaka 2007.
es Salaam/Tanga/Arusha. Ujenzi
huu utapanua njia kutoka njia 1,890
za sasa kufikia njia 3,780.
Kukamilisha uboreshaji wa huduma Kazi ya kuondoa simu za kukoroga inaendelea kwa
kwa kuondoa mitambo 23 ya awamu. Mitambo hii kwa sasa imekwisha ondolewa
kukoroga (manual boards) iliyobaki Kondoa, Kiomboi, Ikwiriri, Utete, Kibiti, Kilwa Masoko,
nchini na kuweka mitambo ya Mafia, Namanyere, Malya, Misungwi, na Ngudu. Kazi
kisasa kwenye vituo vya Mtera, ya kuondoa mitambo 18 iliyobaki inatarajiwa kukamilika
Mvumi, Mwakaleli, Lwangwa, mwezi Julai, 2007.
Litembo, Liuli, Itigi, Misungwi,
168
Ngudu, Mallya, Malampaka,
Urambo, Sikonge, Ruangwa,
Nachingwea, Mikindani, Ndanda,
Makiungu, Liwale na Kaliua.
Kuweka mitambo ya kuwezesha Usambazaji (Rollout) wa huduma hii mikoani
kupata huduma bora za takwimu na unatekelezwa kwa awamu kwa kutumia teknolojia ya
mtandao katika makao makuu ya ADSL. Huduma hii ya TTCL Broadband kwa sasa
Mikoa na baadhi ya Wilaya. inapatikana katika miji mikuu yote ya mikoa na baadhi
ya wilaya.
Kuweka mtandao wa “optical fibre” Katika miji ya DSM, Mwanza, Dodoma, Arusha, na
katika jiji la Dar es Salaam ili Zanzibar kutawekwa mtandao wa „Optical Fibre‟
kuimarisha uunganishaji wa kwenda kwenye majengo makubwa, na kazi hii
majengo na wateja wakubwa ili imekwishaanza katika mikoa ya DSM na Arusha na
wapate huduma bora na za kisasa. inatarajiwa kukamilika mwezi Julai, 2007.
Kuweka mitambo mipya ya simu za Ujenzi wa kuweka mitambo ya kisasa yenye uwezo wa
msingi kati ya Tanga na Arusha na kutoa huduma ya sauti, „data na Internet‟ kwa miji ya
kuondoa mitambo michakavu Moshi, Morogoro, Tanga, Kigoma, Kagera, na Arusha
ambayo vipuri vyake havipatikani. imeshaanza na inatarajiwa kukamilika mwezi Julai,
2007.
Kuweka mitambo kati ya Dodoma Utekelezaji wa mradi huu upo katika hatua ya ujenzi wa
na Arusha kupitia Babati na hivyo mitambo na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Julai,
kuwezesha kupatikana njia 2007.
mbadala kwenda na kutoka Arusha.
Mkandarasi amekwishapatikana na utengenezaji
(manufacturing) wa mitambo umekamilika. Mitambo hii
inategemewa kuwasili nchini Desemba, 2006 na mara
itakapowasili ufungaji wa mitambo utaanza.
67. Kuhusisha utoaji wa huduma kwa Shirika la Posta tayari linatumia teknolojia ya kompyuta
kutumia teknolojia ya kompyuta katika kwa mawasiliano kwenye Ofisi zote Kuu za Posta nchi
mawasiliano katika ofisi zote kuu za nzima. Mtandao huo unatoa huduma za “internet” na
posta za mikoa na kuimarisha biashara “e-mail”. Ili kuimarisha biashara za ki-elektroniki (e-
za ki-elektroniki (e-business) business) Shirika limeanzisha huduma ya “internet
cafe” kwenye ofisi kuu za Posta kumi na moja kati ya
kumi na nne. Lengo ni kupanua huduma hii hadi makao
makuu ya Wilaya.
Kufungua posta ndogo katika Utekelezaji wa ufunguaji wa vituo vya posta ni kama
maeneo ya Kicheba (Tanga), ifuatavyo:
Bereko (Dodoma) na Posta kamili Kicheba (Tanga) – anatafutwa wakala mpya baada
katika maeneo ya Nyakato ya aliyekuwepo kufariki dunia na hivyo Shirika
(Mwanza) na Namanga (Arusha). kusitisha huduma.
169
Bereko (Dodoma) – Mkuu wa shule ya Bereko
amepewa jukumu la kuuza stempu (Stamp
Vendor) kwa niaba ya ofisi.
Nyakato (Mwanza) – ofisi kamili yenye kutoa
huduma zote muhimu za Posta imefunguliwa.
Namanga (Arusha) – Ofisi kamili imefunguliwa.
68. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania “Technical specifications” kwa ajili ya ununuzi wa rada
(TMA) inatarajia kununua rada ya ya kisasa umekamilika. Utaratibu wa kutangaza zabuni
kisasa ili kuboresha utoaji huduma za husika umeanza.
hali ya Hewa.
69. Chuo cha Mabaharia cha Dar es Kozi hizi mbili zimeshaanzishwa katika muhula wa
Salaam (DMI) kinatarajia kuimarisha masomo wa 2006/07.
utendaji wake kwa kuanzisha program
za mafunzo kwa maofisa wa meli ngazi
ya Nahodha (Class 2/1 Master
Mariner) na Mhandisi Mkuu (Class 1/2
– 2 Chief Engineer).
70. Kufanya mapitio na kuunganisha Rasimu imeandaliwa na kuwasilishwa Ofisi ya Rais,
Mipango Mkakati (Strategic Plans) ya Menejiment ya utumishi wa Umma mwezi Novemba,
zilizokuwa Wizara ya Ujenzi na Wizara 2006 kwa mapitio.
ya Mawasiliano na Uchukuzi iliyokuwa
imetayarishwa
71. Kuimarisha bandari ya Tanga ili kuibua Jumla ya Tshs 2.05 bilioni zimetengwa kwa ajili ya
uchumi wa nchi kwa kuchochea kasi ukarabati wa miundombinu na kununua vifaa
ya ukuaji wa uchumi. mbalimbali vya kuhudumia mizigo ikiwa ni pamoja na
cargo Lighter, Mooring Boat, Light Towing Tug na cargo
Pantoon.
Aidha, ukarabati na “Dredging” katika gati namba 1 na
2 utafanyika, pia maboya matatu ya kuongozea meli
yatafungwa. Taratibu za ununuzi wa vifaa zinaendelea
na kutegemewa kukamilika mwezi Juni, 2007.
72. Kuanza mchakato wa kuanzisha Bodi iliyoingia madarakani mnamo mwezi Februari,
“National Carrier” mpya baada ya 2007, imeshaanza mchakato wa kuanzisha “National
mkataba wa sasa kati ya „South Africa Carrier”. Ili kuweza kufanikisha hilo, bado inapitia
Airways‟ na Serikali kusitishwa. “Business Plan” ya ATCL. Hata hivyo tayari malipo ya
awali ya kukodishwa ndege tatu (3) za kisasa aina ya
Air Bus A.319‟s yameshafanyika. Ndege zote tatu
zitakuwa zimeingizwa nchini kati ya mwezi Septemba
na Novemba, 2007.
73. Ujenzi wa bandari ya nchi kavu (Dry Kutokana na ufinyu wa bajeti, fedha ya kuchangia
port) wa Shinyanga na Mwanza ili kwenye mradi huu hazikupatikana kutoka Serikali ya
kuunganisha bandari ya Dar es Tanzania ili kukidhi moja ya masharti iliyokubaliana na
Salaam na nchi jirani Serikali ya Ubelgiji.
170
74. Upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli ya Mshauri Mwelekezi (Consultant) wa kufanya upembuzi
Isaka-Kigali utafanyika katika mkakati yakinifu amepatikana na ameanza kazi mwezi Mei,
wa kuunganisha ukanda wa kati 2007.
(Central Corridor)
75. Kuendelea na miradi ya ukarabati wa Reli, mataruma na Vifaa vya kubadilisha Km 47 za reli
reli ya kati ikiwa ni pamoja na kufanya kati ya Itigi na Tabora vimeanza kuwasili Dar es
uchunguzi kwa lengo la kupanua geji Salaam mwezi Novemba, 2006. Utandikaji utaanza
ya reli hiyo ambayo ni mhimili mkubwa mara kazi ya kupokea vifaa hivyo itakapokamilika.
wa maendeleo ya Ukanda wa kati. Uchunguzi wa kupanua geji ya reli umewekwa katika
Mpango wa Uwekezaji wa Sekta ya Uchukuzi
(Transport Sector Investment Programme-TSIP).
171
WIZARA YA KAZI, AJIRA NA MAENDELEO YA VIJANA
Na AHADI UTEKELEZAJI
1. Kukamilisha maandalizi ya kuandaa Uandaaji wa Kanuni za Sheria ya Ajira na Mahusiano
kanuni za Sheria za Ajira na Kazini na Sheria ya Taasisi za Kazi, 2004
Mahusiano Kazini na Sheria ya Taasisi umeshakamilika na kuchapishwa katika Gazeti la
za Kazi zote za mwaka 2004, ili Serikali Na.42 la tarehe 16/02/2007 na hivyo
kuwezesha sheria hizo kuanza kufanya kuwezesha Sheria hizo kuanza kufanya kazi.
kazi katika robo ya kwanza ya
2006/07.
2. Kuunda Tume ya Usuluhishi na Utatuzi Tume ya Usuluhishi na Utatuzi wa Migogoro ya kikazi
wa Migogoro ya Kikazi (Commission imeshaundwa na kuanza kufanya kazi rasmi tangu
for Mediation and Arbitration) na tarehe 4/5/2007 katika kanda 11 ambazo ni: Dar es
kuiwezesha kuanza kufanya kazi Salalam (Kibaha, Temeke na Ilala); Dodoma (Singida);
katika robo ya kwanza ya mwaka wa Morogoro (wilaya zote); Moshi (wilaya zote); Tanga
fedha 2006/07. (wilaya zote); Arusha (Manyara); Mwanza (Kagera,
Shinyanga na Mara); Tabora (Kigoma na Kahama);
Iringa (Mufindi); Songea (Njombe) na Mbeya (Rukwa).
3. Kutoa elimu kwa umma juu ya dhana Mafunzo juu ya Sheria za Kazi yametolewa kwenye
nzima ya masuala ya kazi na Hifadhi Wizara na Asasi mbalimbali kama ifuatavyo:
ya Jamii, mchango wa sekta hizi katika
kuondoa umaskini na sheria mpya za (i) Wizara sita ambazo ni Afya na Ustawi wa Jamii,
kazi katika mfumo wa utatu kwa lengo Usalama wa Raia, Ardhi na Maendeleo ya Makazi,
la kudumisha mahusiano mema kazini. Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa na Viwanda, Biashara
na Masoko;
(ii) Mashirika sita ambayo ni Benki Kuu, Shirika la
Posta, Kampuni ya Usafiri DSM, COASCO,
Chuo Kikuu DSM na Kampuni ya Ndege;
(iii) Asasi nne ambazo ni Mahakama Kuu ya Tanzania,
DAWASCO, TUCTA, Bodi ya Pamba Tanzania;
(iv) Mamlaka tatu ambazo ni Viwanja vya Ndege,
Usalama wa Anga na Usimamizi wa Bandari.
Mafunzo mengi ya sheria za kazi yanafanyika kwa
ushirikiano wa UTATU. Juhudi zinafanyika kwa
ushirikiano baina ya Wizara na vyama husika vya
wafanyakazi na waajiri kuona kuwa wafanyakazi na
waajiri wanahusishwa katika mafunzo hayo ya UTATU.
4. Kushirikiana na Idara ya Mahakama Taratibu za kuanzisha Divisheni ya Mahakama ya Kazi
kuanzisha Divisheni ya Mahakama ya zinaendelea ambapo Jaji wa Mahakama hiyo na Msajili
Kazi katika Mahakama Kuu ya wamekwishateuliwa. Mahakama hiyo imezinduliwa
172
Tanzania. tarehe 12/6/2007. Aidha, Kanuni za Mahakama hiyo
ziko kwenye hatua ya mwisho kwa kuchapishwa.
5. Kusimamia uundaji wa Bodi za kisekta Bodi za Kisekta za Vima vya Chini vya Mishahara
za vima vya chini vya mishahara kwa zimekwishaundwa katika sekta nane;
kuzingatia Sheria ya Ajira na Sekta ya huduma za majumbani; Sekta ya huduma za
Mahusiano Kazini na Sheria ya Taasisi Biashara na Viwanda; Sekta ya Madini; Sekta ya
za Kazi zote za mwaka 2004. huduma za Afya; Sekta ya huduma za Majini, Bahari na
Maziwa; Sekta ya huduma za Ulinzi Binafsi; Sekta ya
Kilimo na Sekta ya Usafiri na huduma za Mawasiliano.
Bodi hizo zimezinduliwa rasmi tarehe 18/4/2007 na
hatua za awali za mchakato mzima wa kuandaa kima
cha chini cha mshahara katika kila sekta
umekwishaanza na kazi hiyo itakamilika katika kipindi
cha miezi mitatu.
6. Kuendeleza juhudi za kutoa elimu juu Mwongozo wa Utatu juu ya Mapambano dhidi ya
ya mapambano dhidi ya UKIMWI kwa UKIMWI katika sehemu za kazi (Tripartite Code of
Waajiri na Wafanyakazi katika maeneo Conduct of HIV/AIDS at work places in Tanzania
ya kazi nchini. Mainland) umekwishaandaliwa na kupitishwa na
Kanseli ya masuala ya Kazi, Uchumi na Kijamii
(LESCO). Aidha wafanyakazi na waajiri kupitia vyama
vyao wameshirikishwa katika makongamano
mbalimbali yanayohusu masuala ya UKIMWI.
7. Kuendelea kupokea na kushughulikia Jumla ya madai 563 ya malipo ya fidia kwa watumishi
rufaa, mikataba ya hiari na madai ya wa Umma walioumia/kupata madhara wakiwa kazini
malipo ya fidia kwa wafanyakazi yamepokelewa na kiasi cha TShs.21,000,000/=
walioumia au kupata maradhi kazini. zimelipwa hadi kufikia mwezi Juni, 2007. Halikadhalika
jumla ya madai 1,412 yalipokelewa kutoka Sekta
Binafsi, na kati ya hayo madai 898 yamelipwa. Aidha
jumla ya Migogoro ya kikazi 268 imepokelewa na
kushughulikiwa hadi kufikia mwezi Mei, 2007.
Rufaa 1016 zilipokelewa kutoka kwa wafanyakazi na
waajiri katika Sekta Binafsi, na kati ya hizo rufaa 431
zimetolewa uamuzi. Rufaa 66 zilipokelewa kutoka kwa
wafanyakazi na waajiri kutoka katika Sekta ya Umma
na kati ya hizo rufaa 62 zimetolewa uamuzi.
8. Kuratibu ufanisi wa kazi za Mabaraza Uratibu wa ufanisi wa kazi za Mabaraza ya Usuluhishi
ya Usuluhishi. unaendelea kufanyika na unaandaliwa mkakati maalum
kwa ajili ya kuharakisha utolewaji maamuzi katika
mabaraza hayo.
9. Kuratibu na kusimamia Sheria na Sera Mikutano mbalimbali ya wadau ilifanyika kati ya Januari
zinazopambana na Ajira mbaya ya na Mei, 2007 kutathmini suala zima la Ajira ya Watoto
mtoto. ikiwa ni pamoja na kuzishirikisha Halmashauri za
Wilaya na Wadau kwa ujumla katika kuweka mipango
173
na mikakati ya kupambana na utumikishwaji wa watoto.
10. Kukamilisha taratibu za kutunga Sheria Nyaraka za Baraza la Mawaziri zinazohusu kutungwa
ya Hifadhi ya Jamii nchini. kwa Sheria ya fidia kwa Wafanyakazi na sheria ya
Hifadhi ya Jamii zimekwishajadiliwa katika ngazi ya
Makatibu Wakuu (IMTC) kwa sasa zinasubiri kujadiliwa
katika ngazi ya Baraza la Mawaziri.
11. Kufanya ukarabati wa Ofisi za Kazi za Ukarabati wa Ofisi ya Kazi ya Arusha umekamilika.
Morogoro, Dodoma, Mtwara, Arusha, Ukarabati wa majengo ya ofisi za kazi Dar es Salaam,
Dar es Salaam, Kilimanjaro, Kigoma Morogoro, Same na Kigoma unaendelea. Aidha,
na kufanya maandalizi ya ukarabati maandalizi ya ukarabati wa majengo ya ofisi za kazi
kwa Ofisi za Kazi za Shinyanga, Mara, Shinyanga, Mara, Kagera, Rukwa, Tabora, Singida na
Kagera, Rukwa, Tabora, Singida na Lindi yanaendelea.
Lindi.
12. Kukamilisha na kuanza kutekeleza Rasimu ya Mkakati wa Taifa wa Kukuza Ajira
Mpango wa Taifa wa kukuza Ajira imekamilika, kuwasilishwa na kupitishwa na Sekretarieti
nchini na kusimamia shughuli za ya Baraza la Mawaziri na inasubiri kujadiliwa na Kamati
kukuza ajira katika sekta rasmi na ya Makatibu Wakuu (IMTC). Ili baada ya sera ya Taifa
sekta isiyo rasmi. ya Ajira kupitishwa na Baraza la Mawaziri, Mkakati huo
utatekelezwa.
Mpango wa Taifa wa kukuza ajira (National
Employment Creation Programme) umekamilika na
kujadiliwa na wadau wa sekta ya Ajira tayari kwa hatua
za utekelezaji katika mwaka wa fedha wa 2007/08 –
2009/2010. Sekta mbalimblai zikiongozwa na
Wizara/Idara na Wakala wa Serikali, Serikali za Mikoa
pamoja na Halmashauri za Manispaa/Wilaya zote
zitahusika na utekelezaji wa Mpango huu.
Jumla ya Tshs.67,200,000/= zimetolewa kwa
Halmashauri za Wilaya 16 za Tanzania Bara (kila moja
Tshs.4,200,000/=) kwa ajili ya utekelezaji wa mpango
wa mafunzo kwa wananchi kujiajiri kwa lengo la
kuondoa umaskini.
13. Kuendelea kukusanya mawazo na Viashiria muhimu “Key indicators” vya Utafiti wa watu
mbinu za kukuza ajira katika sekta wenye uwezo wa kufanya kazi “Intergrated Labour
mbalimbali na kupima kasi ya ukuaji Force Survey” 2005/06 vinavyotoa mwelekeo na
wa ajira na Nguvu kazi nchini kwa mwenendo wa hali ya ajira vimekamilika na vinaweza
kushirikiana na Ofisi ya Takwimu ya kutumika katika mipango mbalimbali ya kisera. Ripoti
Taifa. kamili inatarajiwa kuzinduliwa mwezi Julai, 2007.
Kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu
umeandaliwa mkakati wa ukusanyaji wa Takwimu mpya
za ajira kwa kupitia tafiti mbalimbali za Kaya za kila
mwaka zilizopangwa kwenye Mkakati wa Kukuza
174
Uchumi na kupunguza umaskini Tanzania (MKUKUTA);
ambapo kwa mara ya kwanza masuala ya ajira
yameingizwa katika utafiti wa mapato na matumizi ya
kaya binafsi “Household Budget Survey” 2006/07.
Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu
(National Bureau of Statistics) inakamilisha utaratibu
endelevu wa kukusanya taarifa na takwimu za hali na
mipango ya ukuaji wa Ajira nchini kupitia mpango wa
takwimu wa Wizara (Sectoral Statistical Master Plan).
14. Kuanzishwa kwa vituo vya ajira katika Ukarabati wa jengo la Wizara katika jiji la Mwanza
miji ya Mwanza, Arusha na Mbeya ili umekamilika na Kituo kimefunguliwa na kuanza
kupanua wigo wa huduma za ajira kwa shughuli zake kuanzia tarehe 21/04/2007. Kituo hiki
wananchi nchini. kitatoa huduma katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa
ikiwemo Mkoa wa Kagera, Shinyanga, Mara na
Mwanza. Juhudi za kuanzisha vituo katika majiji ya
Arusha na Mbeya zinaendelea.
15. Kukamilisha taratibu za upatikanaji wa Utaratibu umekamilika na fedha zimewasilishwa kwa
mitaji kupitia mabenki kutokana na CRDB Bank na National Micro-Finance Bank (NMB)
fedha za wastani wa shilingi billioni kwa ajili ya kuwakopesha walengwa. Benki hizi
moja kwa kila Mkoa zilitolewa na zimeshatoa mikopo kwa SACCOS, Vikundi vya
Serikali. wajasiriamali mbalimbali katika Mikoa/Halmashauri za
Tanzania Bara.
Jumla ya Tshs.17,802,129,660/= zimeshatolewa hadi
kufikia mwezi Mei, 2007. Wizara kwa kushirikiana na
Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji, Ofisi za
Serikali za Mikoa, Halmashauri za Manispaa/Wilaya,
Benki Kuu ya Tanzania, CRDB na NMB zimeendelea
kutoa elimu na taarifa kuhusu utaratibu wa wananchi
kupata mitaji kupitia benki na Taasisi zilizoidhinishwa
kutoa mikopo kwa wananchi.
Halmashauri zimeelimishwa juu ya majukumu ya
uwezeshaji na kutoa mafunzo ya kuwaelimisha
wajasiriamali. Wizara imesambaza mwongozo kuhusu
utaratibu wa utekelezaji wa Mpango wa Uwezeshaji
kwa Halmashauri zote na jinsi ya kutoa mikopo kwa
wananchi. Utaratibu unaandaliwa kuhusu mfumo bora
wa ukusanyaji wa takwimu, kuhifadhi na kutoa taarifa
kwa mamlaka husika kuhusu mwenendo wa utekelezaji
wa mpango.
16. Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara Kikao cha utatu kimekuwa kikiendelea kupitia maombi
katika makampuni mbalimbali ili yote ya vibali na kutoa maamuzi ya kukagua wageni
kuhakiki ajira kwa wageni na ambao wanatiliwa shaka. Kikao hiki hufanyika mara
175
kujiridhisha kuwa sheria za nchi tatu kwa mwezi na kinahusisha wadau kutoka TUCTA,
zinafuatwa. ATE, Idara ya Uhamiaji na Wizara ya Kazi, Ajira na
Maendeleo ya Vijana.
17. Kuanzisha kitengo cha “Cross border Kitengo bado hakijaanza rasmi japokuwa kwa sasa kina
placement services” kwa ajili ya maofisa wawili wanaoshughulikia kuanzishwa kwa
kuwatafutia Watanzania nafasi za kazi kitengo hiki. Kwa sasa maofisa hawa wakisaidiana na
nje ya nchi na kusaidia Watanzania wafanyakazi wengine tayari wameshakamilisha rasimu
waishio nje ya nchi kupata nafasi za ya kuanzishwa kwa kitengo hiki pamoja na mpango wa
kazi. kazi kwa mwaka ujao wa fedha.
18. Kuratibu maonesho ya biashara ya Maonesho ya Nane ya Nguvu Kazi/Juakali kwa Nchi za
sekta isiyo rasmi (nguvu kazi) kwa nchi Jumuiya ya Afrika Mashariki yalifanyika Dar es Salaam
za Afrika Mashariki yatakayofanyika tarehe 3 – 13 Desemba, 2006. Jumla ya Wajasiriamali
Dar es Salaam Novemba, 2006 kwa ilikuwa 577; Kenya (127), Uganda (75), Tanzania (343)
kushirikiana na Wizara ya Viwanda, na Rwanda (32).
Biashara na Masoko pamoja na
Taasisi za Sekta Isiyo Rasmi. Maandalizi ya Ushiriki wa Wajasiriamali wa Tanzania
kwenda kwenye maonesho ya Tisa Jijini Nairobi, Kenya
mwezi Novemba, 2007 yanaendelea.
19. Kutoa taarifa kupitia vyombo Serikali imekuwa ikitoa taarifa mbalimbali kuhusu
mbalimbali vya habari na mawasiliano utekelezaji wa mpango wa uwezeshaji kupitia vyombo
ili kuwawezesha wananchi kujua vya habari (TV, Radio na Magazeti).
namna ya kupata mitaji na mafunzo ya
kujiajiri na kuondokana na umaskini. Aidha, Wizara imekuwa ikiwasiliana na Halmashauri za
Wilaya mbalimbali vijijini kutoa taarifa kuhusu mpango
wa Serikali kuendesha mafunzo kwa wananchi
kuwawezesha kujiajiri, kuboresha miradi yao kwa lengo
la kuondoa umaskini. Kipaumbele ni kwa wananchi
walioko vijijini. Wizara inahusika na kuwasilisha fedha
za mafunzo, Halmashauri zinahusika na kuibua
washiriki kulingana na mahitaji yao ya mafunzo na pia
kulingana na malengo ya Halmashauri kwa wakati
husika.
20. Kuratibu na kuendeleza uanzishwaji Hivi sasa makampuni yanayotoa huduma hizi yanakuja
wa wakala binafsi wa huduma za ajira wizarani kujiandikisha kabla ya kuanza kutoa huduma.
nchini.
21. Kukamilisha hatua ya pili ya Rasimu ya Sera ya Taifa ya Ajira ya mwaka 2007
marekebisho ya Sheria za Kazi na imekamilika na kuwasilishwa kwa Kamati ya Makatibu
Ajira. Wakuu (IMTC) na kujadiliwa. Kamati imetoa hoja
muhimu za nyongeza na mapendekezo ya maeneo ya
kufanyiwa marekebisho na kuwasilishwa kwa
majadiliano zaidi kabla ya kuwasilishwa kwenye kikao
cha Baraza la Mawaziri.
Wizara imeandaa mapendekezo ya utaratibu wa
mchakato wa kukamilisha Rasimu ya Mswada wa
176
Sheria ya Huduma za Ajira nchini (Draft National
Employment Promotion Services Bill, 2007) kwa mfumo
wa kushirikisha wadau.
Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Katiba na
Sheria/Kamisheni ya kurekebisha Sheria (Law Reform
Commission) itawashirikisha wadau wa Sekta ya Ajira
na Kazi kuijadili na kukamilisha rasimu husika na
baadaye kuwasilisha kwenye Mamlaka za Serikali na
hatimaye Bungeni kwa kujadiliwa na kupitishwa.
22. Kuratibu mpango wa kukuza ajira kwa Kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Chakula na
kuainisha Vyama vya Ushirika vya Ushirika, Wizara iliandaa ujumbe wa Mwenge wa
Akiba na Mikopo (SACCOS) za vijana mwaka 2006 kuhusu uanzishaji na Uimarishaji wa
katika Wilaya zote kwa kushirikiana na SACCOS kama njia mojawapo ya kukuza ajira na
Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kupunguza umaskini kwa watanzania. Ujumbe huu
ulitolewa katika wilaya zote 136 za Tanzania na
Watanzania wengi wamehamasika na kuanzisha
SACCOS katika sehemu mbalimbali nchini. Aidha
wataalam wa Wizara wameendelea kuhamasisha
vijana kuanzisha SACCOS kwa kutumia fursa
zinazojitokeza.
23. Kuandaa Warsha za Wadau kwa ajili Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani
ya Mashirika na Taasisi za Serikali na (ILO) iliendesha Warsha za wadau zilizolenga kupata
NGOs zenye lengo la kuhamasisha mawazo na michango kutoka kwa vijana wajasiriamali
ukuzaji wa ajira kwa vijana katika na wadau wa maendeleo ya vijana ili kuandaa na
Mikoa yote. kutekeleza mkakati wa Taifa wa kukuza ajira. Jumla ya
warsha tatu zilifanyika Dar es Salaam, Tanga na Iringa
na kuwajumuisha vijana 300 kutoka Mikoa ya Dar es
Salaam, Tanga, Kilimanjaro, Arusha, Iringa, Mbeya na
Ruvuma. Vijana walitoa michango mizuri ambayo
imejumuishwa katika mkakati wa Taifa wa kukuza ajira
nchini.
24. Kuchapisha na kusambaza kwa vijana Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana iliyofanyiwa
na wadau wengine Sera ya Maendeleo mapitio, tayari imepitishwa na Baraza la Mawaziri. Hivi
ya Vijana iliyofanyiwa mapitio baada ya sasa imepelekwa Baraza la Kiswahili la Taifa kufanyiwa
kupitishwa na Baraza la Mawaziri. Tafsiri na baada ya zoezi hili itachapishwa na
Aidha programu ya Utekelezaji wa kuzinduliwa rasmi ambapo usambazaji wake na
Sera hiyo itaandaliwa na kuanza utekelezaji utaanza mara moja.
kutekelezwa ili kukuza ajira kwa vijana
kote nchini na kupambana na
umaskini.
25. Kushirikiana na vyuo vikuu kuhakikisha Wizara iliendelea kuhamasisha vijana wanaotarajia
vijana wote wanaomaliza Vyuo Vikuu kuhitimu na wale waliohitimu katika vyuo vikuu
wanaandikishwa katika vituo vya Ajira kujiandikisha katika vituo vya ajira kwa kushirikiana na
kama nguvu kazi iliyo tayari kwa ajira. vyuo vikuu na taasisi mbalimbali zinazojihusisha na
177
suala la ajira kwa vijana ili waweze kupata ajira pale
nafasi zinapopatikana.
26. Kuimarisha uzalishaji katika vikundi Wizara imeendelea kuwahamasisha vijana kuanzisha
vya vijana na “vijiwe” kwa kuwapatia na kujiunga katika vikundi vya kuzalisha mali kote
mafunzo katika nyanja za ukuzaji nchini kupitia mbio za Mwenge wa Uhuru, Halmashauri
biashara na Masoko, Ufundi na za Wilaya na mikutano/warsha mbalimbali
Uongozi na utawala wa Miradi. inayoendeshwa na Wizara. Aidha kwa mwaka wa
fedha 2006/2007 Wizara kwa kushirikiana na Mkoa wa
Mwanza imeainisha/imetambua “vijiwe” vya vijana 169
vyenye washiriki 1945 katika jiji la Mwanza kwa lengo la
kuvibadilisha na kuwa vikundi vya kuzalisha mali. Kwa
upande wa mafunzo ya ujasiriamali jumla ya vijana 80
kutoka mikoa ya Dodoma, Iringa, Singida, Tanga,
Mbeya na Morogoro wamepata mafunzo haya chini ya
uratibu wa Kituo cha Vijana Ilonga yaliyofanyika mwezi
Machi, 2007 Dodoma na mwezi Mei, 2007 Morogoro.
27. Kuendelea kuratibu shughuli za Mfuko Jumla ya Tshs.500,000,000/= zilitengwa kwa ajili ya
wa Maendeleo ya Vijana kwa kuweka kuwakopesha vijana kupitia mfuko wa vijana. Aidha
utaratibu mzuri zaidi utakaohakikisha maofisa wa Idara walikwenda wilayani Kwimba Jijini
fedha zinazotolewa zinawafikia Mwanza na Manispaa ya Arusha kuratibu utekelezaji
walengwa. Aidha wakopaji mzima wa utoaji wa mikopo na urejeshaji wa fedha za
wanapatiwa mafunzo kabla ya kupewa mfuko. Wizara inaendelea kuzihamasisha halmashauri
mikopo na kuwajengea uwezo vijana ili za wilaya kutenga asilimia 5% ya mapato yake kwa ajili
waweze kurejesha mikopo kwa wakati. ya mfuko wa maendeleo ya vijana.
Wilaya 26 mpaka sasa zimerejesha jumla ya
Tshs.75,602,469.28. Wilaya 15 zimekopeshwa mara
mbili jumla ya Tshs.86, 513,390.80 na Wilaya tatu
zimekopeshwa mara tatu jumla ya shilingi 38,
932,902/=.
28. Kukusanya takwimu za vijana Serikali imeendelea kukusanya takwimu zinazohusu
zinazohusu shughuli zao katika Wilaya shughuli za vijana nchini na hadi sasa tayari imepokea
43 zilizobaki na kuandaa orodha ya taarifa na takwimu hizo kutoka wilaya 27 kati ya wilaya
vikundi vya vijana (Youth Mapping) 46 zilizokuwa zimesalia awali na hivyo kufanya zoezi
zima la “youth mapping” kukamilika katika wilaya 103.
Zoezi hili lenye lengo la kutambua vijana nchini waliko
na shughuli wanazofanya kwa lengo la kuwafikia
kiurahisi linaendelea.
29. Kuendeleza ukarabati wa vituo vya Jumla ya Shilingi 151,966,538.30 zimetolewa kwa ajili
Mafunzo kwa vijana vya Ilonga, ya zoezi la ukarabati wa vituo vya vijana vya Ilonga,
Sasanda na Marangu na pia Sasanda na Marangu. Utaratibu wa kumpata
kuendelea kuimarisha Kituo cha Mkandarasi umefanyika na kazi hiyo itaanza mara tu
Mtandao wa mawasiliano (Tovuti ya taratibu nyingine zitakapokamilika. Aidha, wizara
Vijana) Ilonga na kuhamasisha vijana imeandaa muhtasari na miongozo ya kufundishia katika
178
wengi zaidi kukitumia. vituo vya vijana nchini katika masomo ya ujasiriamali,
uongozi, utunzaji wa hesabu za fedha na stoo,
uanzishaji na uendeshaji wa miradi.
30. Kuandaa na kutekeleza mpango wa Semina ya mafunzo ya UKIMWI imeendeshwa kwa
malezi unaojumuisha vijana na waelimisha rika 25 kutoka mikoa ya Pwani na Dar es
viongozi wa NGOs za vijana katika Salaam. Aidha, imeendeshwa semina ya shughuli za
kutoa ushauri nasaha, stadi za Maisha, ushauri nasaha na maongozi kwa viongozi 20 kutoka
Afya ya Uzazi na vita dhidi ya UKIMWI. Idara ya Vijana, NGOs na vituo vya mafunzo ya vijana
vya Ilonga, Sasanda na Marangu.
Kwa kushirikiana na Asasi ya vijana ya UVIKITWE,
elimu kuhusu maambukizi ya UKIMWI imetolewa na
kuwanufaisha jumla ya vijana 100 kutoka Wilaya ya
Kinondoni.
Kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya kudhibiti dawa
za kulevya, Wizara imeendesha warsha ya kutoa elimu
ya ufahamu kuhusu dawa za kulevya na athari zake
kijamii, kiuchumi na kiafya kwa wadau kutoka katika
NGOs na Taasisi za kiserikali zinazoshughulika na
vijana nje ya shule. Washiriki 30 kutoka mkoa wa
Pwani na Dar es Salaam walifaidika na mafunzo hayo.
Viongozi wa vikundi vya vijana kutoka Mkoa wa
Morogoro walipatiwa mafunzo kuhusu stadi za maisha
kupitia semina iliyofanyika Ilonga – Kilosa ambapo
vijana 30 walihudhuria.
31. Kuwahamasisha vijana kushiriki Serikali kwa kushirikiana na UNDP iliandaa na
kwenye shughuli za kujitolea Duniani kuendesha kambi za kazi za vijana nne ambazo
na kuendesha kambi za kujitolea za zilifanyika Sasanda wilayani Mbozi, Madale katika
vijana kwa kushirikiana na UNDP ikiwa manispaa ya Kinondoni, Ilonga Wilayani Kilosa na
ni utekelezaji wa kuinua moyo wa Marangu – Moshi vijijini. Kambi hizi ziliwahusisha
kujitolea kwa vijana nchi nzima. vijana takriban 150 na wananchi wa maeneo husika
walihamasika na kushiriki katika kazi mbalimbali za
maendeleo zikiwa ujenzi wa shule, hifadhi ya mazingira
n.k. Aidha sherehe za siku ya kujitolea Duniani
zilifanyika wilayani Mwanga – Mkoani Kilimanjaro
ambapo wananchi wa Wilaya ya Mwanga na vijana
kutoka mataifa mengine walijitolea kufanya shughuli za
usafi na ujenzi wa uwanja wa mpira wa Cleopa D.
Msuya – Mjini Mwanga kwa wiki nzima.
32. Kuhamasisha uanzishwaji wa vituo vya Vituo vya vijana vimeanzishwa katika wilaya 19 ambazo
Maendeleo ya vijana katika ngazi za Wizara kwa kushirikiana na Shirika la kuhudumia
wilaya kote nchini (Youth Development watoto Duniani (UNICEF) zinaendesha mpango wa
Centres). vijana nje ya shule (Out of School Youth Programme)
179
lakini katika Wilaya nyingine bado zoezi hili
halijafanyika kutokana na ufinyu wa bajeti.
33. Kuratibu Mbio za Mwenge wa Uhuru Wizara iliratibu mbio za Mwenge zilizozinduliwa rasmi
na Wiki ya Vijana na kuhamasisha kila tarehe 30/05/2006 mjini Morogoro, katika Mikoa ya
halmashauri ya wilaya kuadhimisha Morogoro, Mwanza, Tanga, Kilimanjaro, Dar es
wiki ya vijana ambayo hufanyika kila Salaam, Zanzibar na Ruvuma.
mwaka tarehe 8 - 14 Oktoba.
Kilele cha Mbio za Mwenge kilifanyika kwa ufanisi
Mkoani Ruvuma na wiki ya vijana kitaifa iliadhimishwa
tangu tarehe 8 – 14 Oktoba, 2007. Halmashauri zote
za wilaya zilihamasishwa kuadhimisha wiki hiyo ya
vijana. Katika Mbio za Mwenge za mwaka 2006 jumla
ya miradi 1679 yenye thamani ya
Tshs.73,929,512,030/= ilizinduliwa. Aidha vijana
kutoka Mikoa mbalimbali walishiriki katika wiki ya vijana
na maonyesho pamoja na warsha iliyoendeshwa kwa
siku saba na kuzungumzia pia masuala ya UKIMWI,
ushauri nasaha, dawa za kulevya na matumizi ya ARV.
Kwa mwaka huu mbio za Mwenge wa Uhuru
zimezinduliwa rasmi tarehe 30/05/2007 mjini Magharibi
– Zanzibar na matayarisho yote ya shughuli
yamefanyika; kilele kitafanyika mkoani Arusha tarehe
14/10/2007.
34. Kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Muundo wa Utumishi “Scheme of Service” kwa maofisa
(TAMISEMI) ili kuajiri Maafisa Vijana vijana umeshaandaliwa na kuwasilishwa Ofisi ya Waziri
katika Halmashauri zote ili kuwafikia Mkuu (TAMISEMI) kama mojawapo ya hatua za
vijana. mchakato wa kuwaajiri maofisa vijana katika kila
Halmashauri ya Wilaya. Baadhi ya Halmashauri za
Wilaya nchini zimeshatangaza nafasi za ajira ya Afisa
vijana kwa mfano Halmashauri ya Mji wa Shinyanga.
35. Kuratibu uanzishwaji wa Baraza la Kwa kuwa uanzishwaji wa Baraza umetamkwa ndani ya
Taifa la Vijana kisheria, pamoja na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana, uundaji wake
kuanzishwa kwa vikundi vya vijana na ulitegemea ukamilishaji wa Sera ya Taifa ya Maendeleo
kuvisajili katika ngazi ya kata na vijiji ya Vijana. Tayari Sera imepitishwa na Baraza la
ikiwa ni maandalizi ya kuunda baraza Mawaziri na hivyo kutoa mwanya kwa Wizara kuanza
la vijana kuanzia ngazi ya kijiji. mchakato wa kuunda Baraza la vijana kwa kuzingatia
vipengele muhimu vilivyorekebishwa katika sera kama
vile umri. Hivi sasa Idara inaendelea na taratibu za
kuandaa sheria itakayoanzisha Baraza la Vijana ikiwa
ni pamoja na kuhamasisha vijana kuanzisha vikundi
kisheria.
36. Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri
Kusimamia na kuratibu shughuli za Vyama viwili vya Wafanyakazi ambavyo ni “Tanzania
Vyama vya Wafanyakazi na Waajiri Pilot Association” (TPA) na “Tanzania Agro-Forestry
kwa mujibu wa sheria mpya ya kazi. Workers Union” (TAWU) vilisajiliwa. Idadi ya Vyama
180
vya Wafanyakazi na Waajri vilivyosajiliwa mpaka sasa
imefikia 21. Aidha, ombi moja la usajili wa chama cha
waajiri katika sekta za viwanda, kilimo, madini na
biashara lilipokelewa na linashughulikiwa.
37. Kufanya kaguzi za vyama pamoja na Kaguzi 19 za kumbukumbu za wanachama kwa vyama
matawi yake yaliyopo nchini kote ili vilivyo katika Mikoa ya Kagera, Mara, Rukwa na Mbeya
kuhakikisha kuwepo kwa ufanisi. zilifanyika.
Ushauri juu ya utekelezaji wa majukumu hususan
katika uundaji wa Matawi mapya ya Vyama, utunzaji wa
kumbukumbu za wanachama, matumizi mazuri ya
fedha za Vyama, na usuluhishi wa migongano ya
kichama, kupitia majadiliano (dialogue) umetolewa.
38. Kutoa ushauri na kuelimisha vyama juu Ushauri kwa vyama na wanachama, hususan
ya utekelezaji wa Sheria Mpya za Kazi migongano inayotokana na kunyang‟anyana
pamoja na majukumu yake kwa mujibu wanachama, uundaji wa vyama vipya na migogoro kati
wa kanuni na katiba za vyama hivyo ili ya vyama na ile ya kiuongozi umetolewa kwa vyama 9
kupunguza migogoro. (TASU, WAMEUTA, COTWU (T) DOWUTA, TEWUTA,
RAAWU, TUICO, TUGHE na TUPSE).
Aidha, ushauri umeendelea kutolewa kwa mfanyakazi
mmoja mmoja kuhusiana na hoja mbalimbali
zilizotolewa juu ya uhuru wa kujiundia vyama vya
wafanyakazi. Mkutano kuhusu matumizi ya sheria mpya
za kazi ulifanywa kwa kuwashirikisha wadau husika.
39. Kushirikiana na ILO, kufanya mafunzo Maandalizi ya mafunzo yamekamilika na mafunzo
ya kuboresha uwezo wa majadiliano yatafanyika robo ya kwanza ya mwaka 2007/08.
kwa viongozi wa vyama vya
wafanyakazi.
40. Kukamilisha mchakato wa kushirikisha Mchakato wa kushirikisha sekta binafsi
sekta binafsi katika utoaji wa huduma umeshakamilika. Sekta Binafsi inashirikishwa katika
kwa Umma utoaji wa Huduma kwa Umma Wizarani kupitia shughuli
za ulinzi na uhudumu (hasa kutoa huduma ya usafi na
matengenezo madogo madogo ya vifaa vya Ofisi).
41. Kuendeleza mkakati wa kuongeza Kwa mwaka 2006/2007 jumla ya watumishi arobaini
idadi ya watumishi kwa kuajiri (40) wa kada mbalimbali wameajiriwa.
watumishi wapya na kuboresha
mazingira ya kazi ili kuleta ufanisi na
ubora unaotakiwa.
42. Kuzindua mkataba wa Huduma kwa Mkataba wa Huduma kwa Wateja (Clients Service
wateja (Clients Service Charter) Charter) kwa Utumishi wa Umma umezinduliwa tarehe
23/06/2007.
43. Kuratibu na kusimamia shughuli za Wizara inaendelea kushiriki kikamilifu katika shughuli
michezo kwa wafanyakazi wa Wizara za michezo ya wizara na Idara za Serikali. Wizara pia
ikiwa ni pamoja na kuhakikisha Wizara inashirikisha wafanyakazi kwenye michezo ya Mei Mosi
181
inashiriki michezo ya Wizara na Idara inayofanyika kila mwaka. Aidha watumishi 10
za Serikali (SHIMIWI). walishiriki kwenye Mei Mosi 2007 mkoani Mwanza.
Wafanyakazi pia hushiriki katika michezo ya
BONANZA inayoshirikisha watumishi wa umma kutoka
Wizara/Taasisi mbalimbali za umma katika Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
44. Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF)
Kukusanya mapato yanayofikia shilingi Shirika lilikusanya kiasi cha shilingi milioni 168,122.4
billioni 208.8 kutoka katika vyanzo kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali mpaka mwezi
vyake mbalimbali vya mapato na Machi, 2007 na kutumia kiasi hicho hicho kulipia mafao
kutumia kiasi hicho hicho cha fedha. ya wanachama, kuwekeza kwenye vitega uchumi
mbalimbali, gharama za uendeshaji na miradi ya
maendeleo. Hii ni asilimia 104 ya lengo la kukusanya
shilingi milioni 162,058.3 katika kipindi hicho. Shirika
lilitarajia kukusanya Shilingi 214,757.5 mpaka kufikia
mwishoni mwa mwezi Juni, 2007.
45. Kuendelea kuweka kompyuta katika Uwekaji wa kompyuta katika Ofisi mbalimbali na
ofisi za Mikoa na Wilaya na kisha kuziunganisha unaendelea. Wataalam wa kuweka
kuziunganisha katika mtandao wa mifumo ya kompyuta na mawasiliano kupitia mtandao
shirika (“Internet communication”). wa kompyuta kwa shughuli zote za Shirika
wanaendelea na kazi hiyo ili kuboresha huduma
ambapo Ofisi 21 za mikoa na 2 za wilaya
zimekwishaunganishwa kwenye mfumo wa kompyuta
wa Shirika katika kipindi hiki.
46. Kuendelea kuboresha uwekaji wa Shirika linaendelea kuboresha uwekaji wa
kumbukumbu mbalimbali za kumbukumbu mbalimbali za wananchama, vituo vya
wanachama kwa kujenga vituo vitatu kutunzia kumbukumbu katika mikoa ya Mtwara na
vya kuweka kumbukumbu katika Mikoa Morogoro, Iringa, Mwanza umekamilika. Vituo vingine
ya Mbeya, Shinyanga na Mara. vidogo viko kwenye maandalizi navyo ni Mbeya na
Musoma.
47. Kuendelea na ujenzi wa majengo ya Ujenzi wa jengo la Ofisi katika Jiji la Mwanza
ofisi na vitega uchumi katika jiji la umeshakamilika. Ujenzi wa Ofisi katika mkoa wa
Mwanza, Manispaa ya Bukoba na ofisi Kagera, wilaya ya Mbozi na Njombe umesogezwa
ya Wilaya ya Mbozi. mpaka kipindi cha mwaka wa fedha ujao.
48. Kukamilisha ujenzi wa jengo la Mafuta Ujenzi wa jengo la Benjamin Mkapa Pension Tower
House (Benjamin Mkapa Pension (Mafuta House) unaendelea vizuri na uko katika hatua
Tower). za mwisho kukamilika.
49. Kuanzisha Miradi Mipya ya ujenzi wa Jengo la Bunge limekamilika na kukabidhiwa kwa
jengo la Ubalozi wa Tanzania Jijini Serikali. Ujenzi wa nyumba za watumishi wa Serikali
Nairobi Nchini Kenya, Ujenzi wa Kijitonyama umeshakamilika ujenzi umegharimu kiasi
nyumba za Jeshi la Wananchi wa cha Shilingi bilioni 13.8.
Tanzania (JWTZ) na ujenzi wa nyumba
za Jeshi la Polisi, Nyumba za Mamlaka Shirika limeanza ujenzi wa nyumba za Jeshi la
ya Mapato Tanzania (TRA), Wananchi. Aidha mazungumzo ya ujenzi wa nyumba
Uendelezaji wa kiwanja cha Ex-AISCO za Polisi na Magereza yanaendelea.
182
kilichopo Jijini Dar es Salaam na
Ujenzi wa majengo kwa ajili ya
Wafanyabiashara ndogondogo
(Industrial Parks).
50. Kukamilisha taratibu za maandalizi ya Mapendekezo ya ujenzi wa daraja la Kigamboni
ujenzi wa daraja la Kigamboni ambapo yamekamilishwa na kuwasilishwa Serikalini kwa
ujenzi wake utaanza katika mwaka wa maamuzi.
fedha wa 2007/2008
51. Kuanza ujenzi wa mabweni ya Mabweni ya Wanafunzi yataanza kujengwa katika
wanafunzi wa Chuo Kiukuu kishiriki mwaka wa fedha wa 2007/08.
cha Waalimu Chang‟ombe (DUCE)
Jijini Dar es Salaam.
52. Kufanya kaguzi 3800 za kawaida za Kaguzi 3,432 za kawaida zilifanyika.
usalama na afya viwandani na sehemu
zingine za kazi.
53. Kufanya kaguzi 3,680 muhimu za Kaguzi 3,005 maalum za kisheria zilifanyika. Kati ya
kisheria za Usalama na Afya Mahali pa hizo 239 ya mitambo ya mvuke, 780 ya vyombo vya
Kazi. upepo na 1,986 ya vyombo vya umeme.
54. Kukamilisha uandaaji wa Sera ya Taifa Maandalizi ya Sera ya Taifa ya Usalama na Afya
ya Afya na Usalama Mahala pa Kazi. Mahali pa Kazi yamekamilika na iko katika hatua ya
kupelekwa katika kikao cha Makatibu Wakuu.
55. Kuimarisha Ofisi mbili za Kanda za Ukarabati wa Ofisi ya Kanda ya Kaskazini
Kaskazini na Ziwa zinazohusiana na umeshakamilika. Maandalizi ya ukarabati wa Ofisi ya
Usalama na Afya Mahali pa Kazi. Kanda ya Ziwa yamekamilika na kazi imeanza Juni,
2007.
56. Kuendelea kutoa mafunzo ya afya na Mafunzo ya Afya na Usalama yanaendelea kutolewa.
usalama mahali pa kazi wa kutumia Mafunzo ya Kamati za Usalama na Afya yametolewa
njia mbalimbali zikiwemo redio, katika sehemu za kazi sita (6) na vipindi vya TV vitatu
televisheni, magazeti na vipeperushi ili vimerushwa.
kuwafikia walengwa kwa wingi zaidi,
hususan namna ya kuunda na
kuendesha kamati za afya na usalama
mahala pa kazi.
57. Kuendelea kukamilisha ukarabati wa Ukarabati wa makao makuu sehemu ya maabara na
jengo la Ofisi sehemu ya Maabara na maktaba unakaribia kumalizika, kilichobaki ni ufungaji
Maktaba. wa viyoyozi na samani.
58. Kuendelea kuboresha shindano la Afya Shindano la Afya na Usalama Kazini limeendelea
na Usalama mahali pa kazi katika kuboreshwa. Mwaka huu washiriki wameshirikishwa
sehemu za kazi na waajiri wanaofanya katika sekta tatu, ambazo ni Sekta ya Ujenzi, Madini na
vizuri kupewa tuzo katika jitihada za Kilimo na Misitu.
kuboresha afya na usalama mahali pa
kazi.
59. Kuwahamasisha wafanya biashara Mafunzo ya wahamasishaji wa warsha hizo
wadogowadogo na wa kati ili waweza yameshafanyika na uchambuzi wa sekta ya kuanzia
kuboresha mazingira ya kazi kwa umekamilika.
183
kuendesha warsha katika mikoa sita ya
Tanzania Bara.
60. Kuajiri Wakaguzi zaidi ili kuimarisha Tayari OSHA imepata kibali cha kuajiri watumishi 46.
kanda zote nchini. Kati ya hao Wakaguzi ni 25.
61. Kutoa mafunzo 80 ya kuboresha Mafunzo 75 kati ya 80 yametolewa sawa na asilimia
ufanisi na tija yatakayonufaisha 95.75 ya lengo lililopangwa. Aidha, Washiriki 1085 kati
Watanzania kwa watu 1100 kutoka ya 1100 waliotegemewa wamepata mafunzo sawa na
taasisi za umma na binafsi. asilimia 98.64 ya lengo lililokusudiwa.
62. Kutoa huduma za uelekezi kwa wateja Huduma za uelekezi zimetolewa kwa wateja 28. Hii ni
30. sawa na asilimia 93 ya lengo lililopangwa.
63. Kufanya tafiti 8 katika maeneo Tafiti 6 kati ya 8 zilizopangwa zimefanyika. Hii ni sawa
yanayolenga kuboresha tija pamoja na na asilimia 75 ya lengo lililopangwa.
kuchangia katika juhudi za kukuza
uchumi na kupunguza umaskini.
64. Kuamua mashauri yatakayowasilishwa Divisheni ya Mahakama ya Kazi inataratibu mbili za
kwa mara ya kwanza mbele ya usikilizaji wa mashauri kwa sasa. Utaratibu wa kwanza,
Mahakama pamoja na kukaza hukumu ni ule wa zamani wa kusikiliza mashauri yatokayo kwa
na kumalizia mashauri yaliyopo. Kamishna wa Kazi na Waziri wa Kazi. Kwa utaratibu
Pia itapokea, itasikiliza na kuamua huu imeendelea kusikiliza na kuyatolea maamuzi
rufaa marejeo na rejea kutoka mashauri 468 yaliyofikishwa mbele ya Mahakama.
Kamisheni ya usuluhishi na utatuzi wa
migogoro (CMA). 1. Mashauri yaliyokuwepo yalikuwa 252.
2. Mashauri mapya yaliyopokelewa ni 216
3. Jumla ya mashauri yaliyopo ni 468
4. Mashauri hayo yamegawanywa kama ifuatavyo:
Migogoro ya uchunguzi 338
Migogoro ya kikazi 3
Mikataba ya hiari 19
Marejeo 108
5. Jumla ya mashauri yaliyotolewa maamuzi ni 116
6. Mashauri yaliyokaziwa hukumu ni 7.
Katika utaratibu wa pili, Divisheni ya Mahakama ya Kazi
imepokea mashauri mawili yaliyofikishwa Mahakamani
kwa utaratibu wa Sheria mpya za Kazi. Kati ya
Mashauri hayo shauri moja ni rufaa kutoka Kamisheni
ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) na shauri jingine
limeletwa moja kwa moja Mahakamani na tayari
limeshatolewa uamuzi.
65. Kukarabati Jengo la Mahakama na Divisheni ya Mahakama ya Kazi ya Mahakama Kuu
kuhamia. haikuweza kukarabati jengo lake lililoko Kinondoni Dar
es Salaam kwa sababu ya zuio lililotolewa na Divisheni
ya Mahakama ya Ardhi katika shauri lililofunguliwa na
aliyekuwa mpangaji wa jengo hilo akidai kurudishiwa
fedha alizotumia kukarabati jengo hilo wakati akiingia
184
kwenye jengo hilo miaka mitano iliyopita. Wakala wa
Majengo Tanzania (TBA) wamekataa kumrudishia
gharama hizo kwa sababu anadaiwa kodi ya pango
inayozidi gharama za ukarabati alioufanya mpangaji
huyo. Divisheni ya Mahakama ya Ardhi bado haijatoa
uamuzi wa suala hili.
66. Kuboresha huduma za Mahakama kwa Divisheni ya Mahakama ya Kazi imeweka vifaa vya
kuweka na kutumia vifaa vya kisasa kisasa vya kutendea kazi katika kila ofisi ikiwa ni
vya kimahakama, usajili, ukatibu na pamoja na kompyuta, “laptops” na kadhalika. Divisheni
kiutawala. pia imeweka samani mpya katika kila ofisi zake na
ilianza kuweka mtambo wa kusajili, kupanga na
kusikiliza mashauri kwa mtandao wa kompyuta kwa
kutumia mtaalamu wa Mahakama ya Kazi ya Denmark.
Lakini wakati wa ku-“install software” kati ya mtaalamu
huyo akiwa Denmark na mtaalamu wa Divisheni ya
Mahakama ya Kazi aliyekuwa Dar es Salaam,
iligundulika kwamba utaalamu huo pamoja na mtambo
wenyewe ulikuwa ukimtegemea sana mwenye mtambo
huo aliyeko Denmark. Hivyo suala zima la
“sustainability” lilijitokeza. Divisheni ya Mahakama ya
Kazi ilipendekeza na wafadhili walikubali kwamba kazi
hiyo sasa ifanywe na wataalamu walioko nchini.
Divisheni ya Mahakama ya Kazi hivi sasa iko kwenye
mchakato wa kumtafuta mtaalamu atakaye “design” na
ku-“install” mtambo huo.
67. Kuboresha utendaji wa Mahakama Divisheni ya Mahakama ya Kazi imeendelea
kwa kuwaendeleza na kuwa na kuwasomesha watumishi wake karibu wote waliokuwa
watumishi wenye sifa ile kuleta ufanisi hawana sifa ili wapate sifa. Watumishi wawili, Katibu
zaidi. Muhtasi na dereva mmoja wamefanya mtihani wa
kidato cha nne. Watumishi wawili dereva na mhudumu
wamefanya mtihani wa kidato cha pili na ili kuboresha
utendaji wa watumishi, Divisheni ya Mahakama ya Kazi
imewapeleka watumishi wake karibu wote, isipokuwa
wahudumu, madereva na walinzi kwenye masomo
mafupi ya mwezi mmoja mmoja nje ya nchi kama vile
Swaziland, Afrika ya Kusini, Nairobi – Kenya, Zambia
na Arusha hapa nchini. Pia watumishi wa ngazi ya
chini waliotajwa hapo juu wamepelekwa kwenye
mafunzo yanayotolewa na NIP Morogoro.
68. Kufikisha huduma za Mahakama kwa Divisheni ya Mahakama ya Kazi imeendelea kusogeza
wahitaji kwa kufungua Ofisi za Kanda, huduma zake karibu na wananchi. Mahakama
kutumia “circuit/mobile courts” na njia imeendesha kesi zake katika Kanda zake za Dar es
za kisasa za mawasiliano pamoja na Salaam, Arusha, Mbeya, Dodoma na kwa njia ya
kuwapatia watumishi wa Mahakama Circuit/Mobile Courts kwenye Mikoa ya Tanga,
vitendea kazi. Morogoro na Mwanza. Watumishi wameendelea
185
kupatiwa vitendea kazi na huduma mbalimbali
zimeendelea kutolewa kwa watumishi.
69. Kuendesha Semina na mafunzo Divisheni ya Mahakama ya Kazi imeendesha semina
mbalimbali ili kuongeza uelewa kwa moja ya watumishi na familia zao (mke na mume) na
wafanyakazi na wadau juu ya janga la kuwahamasisha kupima kwa hiari. Watumishi ishirini
UKIMWI, uwajibikaji kazini, kuzuia na na saba na familia zao walipima kati ya watu themanini
kuepusha rushwa na kujenga maadili waliohudhuria semina hiyo.
mema ya wafanyakazi na wadau.
70. Kuwaelimisha wadau na kutoa taarifa Divisheni ya Mahakama ya Kazi ilianzishwa tarehe 20
mbalimbali kwenye vyombo vya habari Desemba, 2006 na ilizinduliwa rasmi na Mhe. Jaji Mkuu
juu ya haki za wadau katika tarehe 12 Juni, 2007. Wadau wote walifahamishwa na
Mahakama ya Kazi. kualikwa. Divisheni ya Mahakama ya Kazi imeendelea
na utaratibu wake wa kutoa taarifa mbalimbali za kuitwa
shaurini kwenye magazeti, kubandikwa kwenye mbao
za matangazo katika ofisi zake na kusambaza samasi
kwa wadau kwa kutumia watumishi waliopo na kwa njia
ya posta na EMS.
186
WIZARA YA MAJI
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuimarisha mtandao wa vituo vya Serikali ilikarabati jumla ya vituo 53 katika Mabonde ya
kukusanya takwimu na taarifa Pangani (14), Rufiji (5), Ziwa Victoria (4), Wami/Ruvu
mbalimbali za raslimali za maji. (29) na Ziwa Nyasa (1). Aidha, vituo vya hali ya hewa
10 vilikarabatiwa katika Mabonde ya Ziwa Victoria (4)
na Wami/Ruvu (6) na kituo kipya kimoja cha kupima
mvua kilijengwa katika Bonde la Wami/Ruvu kupitia
mradi wa Uboreshaji wa Huduma ya Maji katika Jiji la
Dar es Salaam.
2. Ununuzi wa vifaa vya kiufundi ili Serikali iliendelea kuimarisha Ofisi za Mabonde ya Maji
kuimarisha na kupanua mtandao wa kwa kuzipatia vifaa vya kuchunguza mwenendo wa maji
kufuatilia wingi na ubora wa rasilimali chini ya ardhi. Kwa kutumia vifaa hivyo jumla ya
za maji. maeneo 850 yalionekana kuwa yanafaa kwa ajili ya
kuchimba visima vya maji.
3. Kuimarisha Ofisi za Mabonde kwa Serikali iliendelea kuziimarisha Ofisi za Mabonde ya
kuzipatia wataalam, nyenzo na Maji kwa kuzipatia wataalam mbalimbali wa kada za
vitendea kazi. Wahaidrolojia Daraja la II (21), Maafisa Maendeleo
Jamii Daraja la II (11) na Mafundi Sanifu (Haidrolojia)
(11) ambao wanatarajiwa kuajiriwa. Mgawanyo wa
watumishi ni kama ufuatavyo:
Wahaidrolojia Daraja la II – Makao Makuu Dar es
Salaam (2), Bonde la Pangani (2), Bonde la
Wami/Ruvu (2), Bonde la Rufiji (2), Bonde la Mto
Ruvuma (2), Bonde la Ziwa Nyasa (2), Bonde la
Kati (3), Bonde la Ziwa Rukwa (2), Bonde la Ziwa
Tanganyika (3) na Bonde la Ziwa Victoria (1).
Maafisa Maendeleo Jamii Daraja la II – Bonde la
Pangani (2), Bonde la Wami/Ruvu (1), Bonde la
Rufiji (2), Bonde la Mto Ruvuma (1), Bonde la
Ziwa Nyasa (1), Bonde la Kati (1), Bonde la Ziwa
Rukwa (1), Bonde la Ziwa Tanganyika (1) na
Bonde la Ziwa Victoria (1).
Mafundi Sanifu (Haidrolojia) Daraja la II – Bonde la
Mto Ruvuma (3), Bonde la Ziwa Nyasa (3), Bonde
la Kati (3), Bonde la Ziwa Rukwa (3).
4. Kujenga Ofisi mpya ya Bonde la Ziwa Maandalizi ya kujenga ofisi mpya ya Bonde la Ziwa
Nyasa katika mji wa Tukuyu na Nyasa yamekamilika baada ya kupatiwa eneo la ujenzi
kukamilisha ukarabati wa Ofisi ya katika mji wa Tukuyu.
Bonde la Mto Ruvuma katika mji wa
Mtwara. Ujenzi wa jengo la ofisi ya Bonde la Mto Ruvuma
umekamilika, kazi iliyobaki ili majengo ya ofisi kuanza
187
kutumika baada ya kuwekewa samani. Kazi hii
itafanyika katika mwaka ujao wa fedha.
5. Kuchunguza upatikanaji wa maji chini Jumla ya maeneo 1,500 yamefanyiwa utafiti wa maji
ya ardhi ili kubaini maeneo 1,500 ya chini ya ardhi nchini ili kubaini maeneo yanayofaa
kuchimba visima virefu. kuchimba visima vya maji. Katika uchunguzi huo jumla
ya maeneo 850 yalionekana kuwa yanafaa kwa ajili ya
kuchimba visima vya maji. Maeneo hayo yapo katika
mikoa ya Arusha (124), Dodoma (52), Iringa (19),
Kagera (6), Kilimanjaro (97), Lindi (39), Manyara (34),
Mara (6), Mbeya (5), Mtwara (48), Mwanza (40), Pwani
(2), Rukwa (51), Ruvuma (18), Shinyanga (168),
Singida (29), Tabora (74) na Tanga (38).
6. Kusimamia na kuratibu uchimbaji wa Serikali iliendelea kusimamia uchimbaji wa visima kwa
visima vya maji kwa kuimarisha lengo la kuhakikisha taratibu zilizowekwa zinafuatwa.
usimamizi na udhibiti kupitia Ofisi za Serikali ilisimamia uchimbaji visima 161 katika maeneo
Mabonde. yafuatayo: Arusha (1), Dodoma (6), Lindi (38),
Kilimanjaro (12), Manyara (6), Mtwara (47), Singida (6),
Shinyanga (9), Tabora (3) na Tanga (2).
7. Kuanzisha Kamisheni itakayoratibu Tanzania iliendelea na mchakato wa kuridhia Mkataba
matumizi endelevu ya rasilimali za maji wa Makubaliano ya Uanzishaji wa Kamisheni ya Bonde
katika bonde la Mto Zambezi. la Mto Zambezi (ZAMCOM), ambao ulisainiwa tarehe
13 Julai 2004 huko Kasane, Botswana. Aidha, nchi
zilizomo kwenye Bonde la Mto Zambezi zilianza
kutayarisha Mkakati wa Usimamizi Shirikishi wa
Rasilimali za Maji (Strategy for Integrated Water
Resources Management) chini ya mradi unaosimamiwa
na SADC katika bonde hilo.
Takwimu za sekta mbalimbali zinazohusiana na
rasilimali za maji katika bonde hilo zilikusanywa ili
zitumike katika kupanga matumizi ya uwiano kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali. Mradi huo
utawezesha nchi zote zilizopo kwenye bonde la Mto
Zambezi kubadilishana taarifa na takwimu kupitia
mtandao utakaoanzishwa.
8. Kutekeleza mkakati wa kuhifadhi Katika jitihada za kulinda vyanzo vya maji dhidi ya
mazingira na vyanzo vya maji ili uchafuzi unaotokana na majitaka ya viwandani na
kudhibiti uchafuzi na uharibifu wa majumbani, jumla ya viwanda 90 vilikaguliwa katika
vyanzo hivyo mabonde yafuatayo:- Mto Pangani 16, Mto Rufiji 14,
Wami/Ruvu 19 na Ziwa Victoria 41. Vilevile, ukaguzi
wa miundombinu ya majitaka kwenye Jiji la Arusha,
Mbeya na Mwanza na Manispaa 5 za Moshi, Dodoma,
Morogoro, Tanga na Iringa umefanyika. Katika ukaguzi
huo, jumla ya sampuli 195 za majitaka zilichunguzwa
kimaabara na matokeo yameonyesha kuwa viwango
188
vya majitaka yanayorejeshwa kwenye vyanzo vya maji
vinakubalika.
Hata hivyo ukaguzi huo ulibainisha kuwepo kwa
matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na uchakavu wa
miundombinu iliyopo. Mamlaka zinazomiliki
miundombinu ya majitaka na viwanda zimeagizwa
kufanya marekebisho ili kuondoa kasoro hizo. Lengo ni
kuhakikisha kuwa majitaka yanasafishwa kwa viwango
vilivyokubaliwa kisheria kabla ya kurejeshwa katika
vyanzo vya maji.
9. Kuziimarisha maabara za maji nchini Serikali iliendelea kuziimarisha maabara za maji kwa
kwa kuzipatia usafiri, vifaa na madawa. kutekeleza yafuatayo:
Maabara za Tanga, Arusha, Singida, Mbeya,
Sumbawanga, Kigoma, Songea na Mtwara
zimepatiwa madawa kwa ajili ya kuratibu ubora wa
maji katika vyanzo vilivyoko kwenye maeneo yao.
Watumishi 2 walihudhuria mafunzo ya Statistical
Method Validation for Test Laboratory – Afrika ya
Kusini.
Maabara ya Maji ya Mwanza ilipatiwa vifaa ambavyo
ni Autoclave, Incubator na Refrigerator kwa ajili ya
kuchunguza ubora wa maji yanayotumika kusindika
minofu ya samaki.
10. Kujenga, kupanua na kukarabati miradi Jumla ya miradi 33 ilikarabatiwa kwa viwango
ya maji vijijini, kuchimba visima virefu mbalimbali katika maeneo ya Kwimba, Monduli, Meatu,
na vifupi, kujenga mabwawa hususani, Bariadi, Iringa Vijijini, Tarime, Lushoto, Rondo,
katika Wilaya kame na kuendeleza Karagwe, Muheza, Njombe Vijijini, Muheza,
teknolojia ya uvunaji wa maji ya mvua. Mugango/Kiabakari, Maswa, Njombe Mjini, Magu,
Nzega, Lindi Vijijini, Mbalizi, Korogwe, Makonde,
Wanging‟ombe, Chalinze, Makete, Mwanga,
Sengerema, Chunya, Kongwa, Masasi, Mwanza
(Mkurugenzi wa Jiji), Same, Tunduru na Sikonge.
Aidha, miradi 5 ya maji vijijini ilipanuliwa katika maeneo
ya Madibira, Lesingita, Bunda mjini, Nyamuswa na
Kilwa Masoko.
Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya Ujerumani
iliendelea na ujenzi wa miradi ya maji katika maeneo ya
Lyamungo Kiranya, Lyamungo Sinde, Lyamungo Kati,
Mrama, Tella, Usari, Urori na Kimashuku katika Wilaya
ya Hai na Kifuni, Umbwe Onana, Umbwe Sita, Kindi
Kati, Sambarai, Mkomongo, Kombo, Manushi Ndoo na
Manushi Sinde katika wilaya ya Moshi Vijijini.
189
Ujenzi wa miradi ya maji katika mikoa ya Lindi na
Mtwara uliotekelezwa kwa ushirikiano na Serikali ya
Japan na ulikamilika. Wananchi wapatao 200,000
wananufaika na huduma ya maji. Aidha, serikali kwa
kushirikiana na Serikali ya Uholanzi ilichimba visima
144 kupitia mradi wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini
katika mkoa wa Shinyanga. Mradi huo ulikamilika
mwezi Desemba, 2006.
Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya
Afrika (AfDB), iliendelea na utekelezaji wa mradi wa
maji katika wilaya ya Monduli kwa kuchimba visima 25,
kujenga mabwawa 16 na matangi 29, na kulaza
mabomba yenye urefu wa kilomita 131. Vilevile,
uhamasishaji wa uvunaji wa maji ya mvua ulitekelezwa
katika wilaya ya Masasi, kwa kufundisha mafundi
binafsi 37 kutoka katika Kata 37 za wilaya hiyo. Ujenzi
wa matangi 2 ya mfano umekamilika katika maeneo ya
Shule ya Msingi ya Mangaka (1) wilayani Nanyumbu na
katika zahanati ya kijiji cha Nanyindwa (1) wilayani
Masasi.
Ujenzi wa mabwawa
Serikali ilipanga kujenga mabwawa 21 na kuendelea na
ujenzi wa bwawa la Mugumu. Hadi sasa ujenzi wa
mabwawa mapya 9 umefikia hatua mbalimbali za
utekelezaji. Mabwawa hayo yanajengwa katika maeneo
yafuatayo: Ugunga (Urambo), Moita na Ingamuriak
(Monduli), Nyashitanda (Misungwi), Habiya (Bariadi),
Nyambele na Kinyambwiga (Bunda), Matwiga (Chunya)
na Iguluba (Iringa Vijijini). Aidha, mikataba ya ujenzi wa
mabwawa 3 mapya katika maeneo ya Amasatwa
(Kiteto), Emboret (Simanjiro) na Katoro (Geita)
imesainiwa na wakandarasi wapo katika hatua za
kupeleka vifaa vya ujenzi kwenye maeneo hayo.
Tathmini ya zabuni za ujenzi wa mabwawa mengine
mapya 9 katika maeneo ya Masuguru (Bagamoyo),
Seke Ididi (Kishapu), Nyambori (Tarime), Sasajila
(Dodoma Vijijini), Mwanjoro (Meatu), Wegero (Musoma
Vijijini), Ingondin (Longido), Mnazi Mmoja (Monduli) na
Bulenya (Igunga) imekamilika na wakandarasi
wameteuliwa na taratibu za kusaini mikataba
zinaendelea.
190
Uchimbaji wa Visima
Hadi Juni, 2007 visima virefu 429 vilichimbwa na kati ya
hivyo, visima 364 vilifanikiwa kupata maji na vina
uwezo wa kutoa maji mita za ujazo milioni 32 .
11. Kusanifu miradi ya maji kwa ajili ya miji Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Kiarabu ya
ya Muleba, Urambo, Chunya, Maendeleo ya Afrika (BADEA) imekamilisha upembuzi
Ruangwa na kijiji cha Nyakagomba yakinifu wa mradi wa kuvipatia huduma ya maji vijiji 46
(Geita) na Awamu ya pili ya mradi wa ambapo vijiji 42 viko wilayani Bagamoyo na 4 katika
maji wa Chalinze. wilaya ya Morogoro vijijini. Uchunguzi huo ni moja ya
hatua za utekelezaji wa mradi wa maji wa Chalinze
Awamu ya Pili.
12. Kukarabati miradi ya maji ya Same, Hadi kufikia Juni, 2007, jumla ya miradi 33 ilikarabatiwa
Gonja Maore, Kilulu, kwa viwango mbalimbali katika maeneo ya Kwimba,
Kiponzero/Kihanga, Monduli, Meatu, Bariadi, Iringa Vijijini, Tarime, Lushoto,
Mugango/Kiabakari, Gabimori, Hedaru, Rondo, Karagwe, Muheza, Njombe Vijijini, Muheza,
Makonde, Maswa, Lushoto, Rombo Mugango/Kiabakari, Maswa, Njombe Mjini, Magu,
vijijini, Njombe-Wakichi Kibena, Nzega, Lindi Vijijini, Mbalizi, Korogwe, Makonde,
Karagwe, Muheza - Wanging‟ombe, Chalinze, Makete, Mwanga,
Ubembe/Kwemhosi, Bariadi, Mwanza Sengerema, Chunya, Kongwa, Masasi, Mwanza
vijijini, Mbinga vijijini na Iringa Vijijini. (Mkurugenzi wa Jiji), Same, Tunduru na Sikonge.
Miradi mingine ni ya Kayenze -
Ilemela, Nassa, Sikonge, Kitomanga,
Iwindi, Chato, Tunduma, Makete,
Dindimo, Nyang‟hanga/Kabila,
Masonga, Singa-Kibosho,
Elerai/Longido, Kwanyange-Mwanga,
Sumve/Mantare, Korogwe mjini na
Njombe vijijini. Miradi mingine
itakayokarabatiwa ni ya Usangi,
Nzega vijijini, Mgwashi-Handeni,
Kamachumu, Ileje vijijini, Rondo,
Litumbakuhama/Kingirikiti-Mbinga,
Njombe mjini, Maswa, Mwanga mjini,
Kongwa,
Galula/Mbuyuni/Mbagala/Songwe,
Magu, Ngudu, Igunga, Nderema -
Handeni, Same mjini, Namanyere,
Tukuyu, Magubike, Biharamulo, Kilwa
Masoko na Sengerema.
13. Kuziwezesha Halmashauri za Wilaya Hadi kufikia Juni, 2007 ujenzi wa matangi 2 ya mfano
za Lindi Vijijini na Babati kujenga umekamilika katika maeneo ya Shule ya Msingi ya
matangi ya mifano ya kuvuna maji ya Mangaka (1) wilayani Nanyumbu na katika zahanati ya
mvua kwenye mapaa ya nyumba kijiji cha Nanyindwa (1) wilayani Masasi.
katika taasisi za umma.
191
14. Kupanua miradi ya maji ya Madibira, Miradi 5 ya maji vijijini ilipanuliwa katika maeneo ya
Chiuwe, Pangani, Ilula, Igombe, Malya, Madibira, Lesingita, Bunda mjini, Nyamuswa na Kilwa
Kilwa Masoko, Mwisanga/Ntomoko, Masoko. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na Serikali ya
Mundarara, Mji wa Bunda na Ujerumani iliendelea na upanuzi wa miradi ya maji
Nyamuswa. katika maeneo ya Lyamungo Kiranya, Lyamungo
Sinde, Lyamungo Kati, Mrama, Tella, Usari, Urori na
Kimashuku katika Wilaya ya Hai na Kifuni, Umbwe
Onana, Umbwe Sita, Kindi Kati, Sambarai, Mkomongo,
Kombo, Manushi Ndoo na Manushi Sinde katika wilaya
ya Moshi Vijijini.
15. Kutekeleza Programu ya Taifa ya Maji Kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika
na Usafi wa Mazingira Vijijini. Serikali kwa kutumia Vigezo vya kugawa fedha kwa kila
Halmashauri kwa kuzingatia idadi ya watu ambao bado
hawajapata huduma ya maji na aina ya tekinolojia
inayotumika katika miradi ya maji katika kila Wilaya
ilipeleka fedha kwenye halmashauri kutekeleza miradi
ya maji ya mafanikio ya haraka (quick wins).
Pia, Serikali iliendelea na utekelezaji wa mradi wa Maji
na Usafi wa Mazingira Vijijini kwa mkopo kutoka Benki
ya Dunia. Mradi huo unatekelezwa katika wilaya 14 za
Rufiji, Morogoro Vijijini, Mvomero, Kilosa, Kongwa,
Mpwapwa, Kondoa, Manyoni, Singida Vijijini, Iramba,
Igunga, Kiteto, Kilindi na Handeni, ambapo utekelezaji
umefikia wastani wa asilimia 85. Katika wilaya mbili za
Rufiji na Mpwapwa utekelezaji umekamilika. Aidha,
chini ya mradi huo, upembuzi yakinifu ulifanyika kubaini
vyanzo vya maji na viwango vya mahitaji ya maji katika
miji midogo tisa (9) ya Utete, Ikwiriri, Kibiti, Mvomero,
Turiani, Kilosa, Gairo kwa msaada wa serikali ya
Ufaransa. ,
16. Kuimarisha skimu kubwa Sita (6) za Serikali iliendelea kuendesha skimu kubwa za maji za
maji vijijini za Maswa, Handeni, Makonde, Chalinze, Wanging‟ombe
Maswa,Mugango/Kiabakari/Butiama, na Mugango/Kiabakari kwa kulipia umeme, madawa na
Chalinze, Makonde, Handeni Trunk mishahara ya watumishi. Kwa mwaka 2006/2007, jumla
Main (HTM) na Wanging‟ombe. ya shilingi 572,456,170 zimelipwa kwa ajili ya kulipia
umeme, fidia kwa wananchi walioathirika na ujenzi wa
miradi ya maji ya Chalinze na Makondeko, ununuzi wa
vipuri vya mitambo na kulipia mafao ya vibarua.
17. Kukamilisha ujenzi wa bwawa la Ujenzi wa tuta la bwawa umefikia kimo cha mita 3 na
Mugumu katika Wilaya ya Serengeti. Ujenzi wa bwawa hilo utakamilika katika mwaka wa
fedha 2007/2008.
18. Kukarabati mifumo ya majisafi katika Serikali kwa kushirikiana na Washiriki wa Maendeleo
miji ya Babati, Lindi, Mtwara na ikiwa ni pamoja na Jumuiya ya Nchi za Ulaya (EU) na
192
Sumbawanga. Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW), Benki ya
Kiarabu kwa Maendeleo ya Afrika (BADEA), iliendelea
kuboresha huduma za maji mijini kwa kukarabati na
kupanua mifumo ya majisafi na majitaka. Kazi
zilizotekelezwa kama ifuatavyo:-
Kujenga mtambo wa kusafisha maji, matangi na
mabomba ya kusambaza maji na kuchunguza
mfumo wa majitaka katika makazi yasiyo rasmi
katika Jiji la Mwanza.
Kujenga vyanzo vya maji, matangi na kupanua
mifumo ya usambazaji wa maji safi na majitaka
katika maeneo ya kati ya Jiji la Mbeya.
Kusanifu mradi wa majisafi katika Manispaa ya
Iringa.
Kujenga mfumo wa usambazaji wa majisafi na
ujenzi wa mfumo wa majitaka katika Manispaa
ya Songea.
Kuchimba visima virefu 3 vya maji na kuanza
usanifu wa mfumo wa majitaka mjini Singida.
19. Kuchunguza, kusanifu na kuandaa Kwa kushirikiana na Jumuiya ya nchi za Ulaya (EU)
mpango wa muda mrefu wa kukarabati kupitia Mfuko wa ACP - EU Water Facility, Benki ya
na kupanua mifumo ya majisafi na Maendeleo ya Ujerumani (KfW), na Serikali ya
ujenzi wa mifumo ya uondoaji wa Ufaransa kupitia shirika la Maendeleo la AFD, serikali
majitaka (Urban upgrading program) ilifanya uchunguzi kwa lengo la kuandaa mpango wa
katika miji saba ya Babati, Lindi, muda mrefu wa kukarabati na kupanua mifumo ya
Mtwara, Sumbawanga, Bukoba, majisafi na ujenzi wa mifumo ya uondoaji wa majitaka
Musoma na Kigoma. (Urban Upgrading Program) katika miji saba ya Babati,
Lindi, Mtwara, Sumbawanga, Bukoba, Musoma na
Kigoma. Pia, Serikali ikishirikiana na Serikali ya Uswisi
kupitia Shirika la SECO ilianza maandalizi ya
utekelezaji wa mradi wa kuboresha huduma za majisafi
na usafi wa mazingira katika miji ya Dodoma na Tabora
kwa kumteua Mshauri Mwelekezi (consultant).
20. Kuchimba na kuendeleza visima virefu Uchunguzi wa kubaini kuwa maji yapo umefanyika kwa
vinne ili kuboresha huduma za majisafi kuchimba visima vitatu vya majaribio. Maji
katika mji wa Singida. yamepatikana mengi. Usanifu na Utayarishaji wa
vitabu vya zabuni kwa ajili ya kuchimba visima vya
uzalishaji umekamilika. Taratibu za kumpata
Mkandarasi zinaendelea kwa kuomba kibali BADEA.
21. Kukarabati miradi ya majisafi kwenye Fedha za ukarabati zilipelekwa katika miji ya Mtwara
miji ya Sumbawanga, Lindi, Mtwara, (50mil), Musoma (50mil.) na Lindi (88mil). Kazi za
Kigoma, Musoma na Tabora. ukarabati wa mifumo ya maji safi zinaendelea. Katika
miji ya Sumbawanga na Kigoma, fedha za ukarabati
hazikutolewa na Hazina, hivyo kazi ya ukarabati
193
haikufanyika. Hata hivyo kazi ndogondogo zinafanywa
kwa kutumia fedha za Mamlaka.
22. Kupanua mifumo ya majisafi katika miji Utekelezaji unaendelea katika miji ya Dodoma, Singida
ya Iringa, Mwanza, Dodoma, Singida na Bukoba. Aidha, miji ya Mwanza na Iringa inaendelea
na Bukoba. kutekeleza upanuzi wa miundombinu kwa kutumia
fedha kutoka KFW na EU.
23. Kuendelea na ujenzi wa mradi wa Serikali iliendelea na ujenzi wa mradi mkubwa wa kutoa
kutoa maji Ziwa Victoria kwenda Miji ya maji Ziwa Victoria kwenda miji ya Kahama na
Kahama na Shinyanga. Shinyanga. Mradi huo ambao unagharamiwa na
Serikali yetu, utavipatia maji vijiji 54 vilivyoko umbali
usiozidi kilometa tano kutoka kwenye bomba kuu katika
mikoa ya Mwanza na Shinyanga. Ujenzi wa mradi huo
unaendelea kutekelezwa kwa kutumia Kandarasi 5
kama ifuatavyo:-
Kandarasi Na. 1 inahusu ujenzi wa chanzo cha maji
ziwani na ulazaji wa mabomba makubwa ya kipenyo
cha mm 900 ya urefu wa kilomita 9.6 kutoka kijiji cha
Ihelele hadi mlima Mabale; ujenzi wa chujio la
kusafishia maji; ujenzi wa tangi kubwa la kuhifadhia
maji lenye uwezo wa mita za ujazo 35,000; kufunga
pampu za kusukuma maji yasiyosafishwa na
yaliyosafishwa na upanuzi wa kituo cha umeme cha
Bulyanhulu na kujenga njia ya umeme ya msongo
wa megavolti 33 hadi Ikangala.
Kandarasi Na. 2 inahusu ulazaji wa mabomba ya
kipenyo cha mm 1,200 ya urefu wa kilomita 27.7
kutoka mlima Mabale hadi kijiji cha Mwawile; ulazaji
wa mabomba ya kipenyo cha mm 300 kwa urefu wa
kilomita 22 kutoka kijiji cha Mwawile hadi Tarafa ya
Mwamashimba; na ulazaji wa mabomba ya kipenyo
cha mm 1,100 ya urefu kilomita 18.3 kutoka kijiji cha
Mwawile hadi Solwa.
Kandarasi Na. 3 inahusu kazi za ulazaji wa
mabomba ya kipenyo cha mm 750 kwa urefu wa
kilomita 62.1 kutoka Solwa hadi mji wa Kahama
ikiwa ni pamoja na ujenzi wa tangi lenye mita za
ujazo 18,000 na upanuzi wa mfumo wa usambazaji
wa maji safi katika mji huo.
Kandarasi Na. 4 inahusu kazi ya ulazaji wa
mabomba ya kipenyo cha mm 700 yenye urefu wa
kilomita 64.4 kutoka Solwa hadi Manispaa ya
Shinyanga; na ujenzi wa tangi lenye mita za ujazo
18,000, upanuzi na ukarabati wa mfumo wa
usambazaji wa maji safi katika Manispaa hiyo.
Kandarasi Na. 5 inahusu kuvuta umeme kwa ajili
194
ya kuendesha mitambo imeanza kwa kulaza
nyaya za umeme kutoka Ikangala hadi kijiji cha
Nyamtukuza.
Hadi kufikia mwezi Juni, 2007, utekelezaji wa mradi huo
ulifikia asilimia 88.
24. Kuanza taratibu za awali za ujenzi wa Kumekuwa na tatizo la kupungua kwa wingi wa maji
bwawa la Kidunda kwa ajili ya katika Mto Ruvu ambao ni chanzo kikuu cha maji kwa
kuboresha huduma za majisafi katika ajili ya Jiji la Dar es Salaam na Miji ya Kibaha na
Jiji la Dar es Salaam na Miji ya Bagamoyo hususan wakati wa kiangazi na hivyo
Bagamoyo na Kibaha. kuathiri uzalishaji wa maji katika mitambo ya Ruvu Juu
na Ruvu Chini. Katika jitihada za kukabiliana na tatizo
hilo, Serikali iliendelea kuchunguza vyanzo vipya vya
maji juu na chini ya ardhi. Matokeo ya uchunguzi
yamependekeza kujengwa bwawa katika mto Ruvu
maeneo ya Kidunda Wilayani Morogoro. Maandalizi ya
awali ya ujenzi ya bwawa hilo yanaendelea ikiwemo
uchunguzi wa athari za kimazingira zinazoweza
kusababishwa na ujenzi huo na uchunguzi wa hali ya
miamba katika eneo la ujenzi.
25. Kutoa mafunzo kwa watumishi 335 Watumishi 250 walipatiwa mafunzo ya muda mrefu na
kwa muda mfupi na mrefu ndani na nje mfupi.
ya nchi.
26. Kuwathibitisha kazini watumishi Watumishi 220 waliajiriwa kwa ajili ya sekta ya maji,
wanaomaliza muda wao wa majaribio kati ya hao 98, ni Wahandisi walioajiriwa kwa mkataba
kazini. kwa lengo la kuzijengea uwezo Halmashauri, na
Sekretarieti za Mikoa katika kutekeleza Programu
Ndogo ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini. Aidha,
watumishi 16 walithibitishwa kazini, watumishi 598
walipandishwa vyeo.
27. Kutathimni kwa pamoja na wahisani Mwezi Septemba, 2006 Serikali kwa kushirikiana na
wa sekta ya Maji katika nyanja za Washiriki wa Maendeleo (Development Partners),
utoaji huduma, uwekezaji na maeneo ilifanya tathmini ya pamoja ya sekta ya maji. Tathmini
ya ushirikiano na sekta nyingine. hiyo iliangalia mwenendo wa sekta ya maji ili kubaini
matatizo yanayoikabili, changamoto zilizopo na mbinu
za kuiwezesha kufikia malengo ya MKUKUTA na yale
ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapindizi (CCM)
ya mwaka 2005, pamoja na Malengo ya Milenia.
Mapitio hayo yalibaini mambo makuu manne
yanayotakiwa kutekelezwa kama ifuatavyo:
Kuimarisha uhusiano kati ya Serikali, Washirika wa
Maendeleo na asasi nyingine zisizo za kiserikali
kwa kuweka utaratibu wa kujadili mara kwa mara
kwa pamoja na kwa uwazi matatizo na changamoto
zinazoikabili sekta ya maji na kupendekeza njia
195
sahihi za kutatua matatizo hayo.
Serikali kuanza kuandaa mipango na bajeti kwa
kuhusisha sekta nzima (Sector Wide Approach to
Planning – SWAP) kuanzia mwaka wa fedha wa
2007/2008 badala ya kuangalia mradi mmoja
mmoja kama ilivyokuwa hapo awali.
Kuainisha vigezo sahihi na vilivyo wazi vya kupima
maendeleo ya sekta ya maji na kubaini mafanikio
na matatizo mwaka hadi mwaka.
Kuipatia sekta ya maji fedha kwa kiwango cha
kutosha ili kuwezesha uwekezaji katika ujenzi na
uboreshaji wa miundombinu na kuijengea uwezo
wa kutekeleza majukumu yake.
28. Kutathmini hali halisi ya UKIMWI Suala la UKIMWI limeendelea kupewa kipaumbele na
pamoja na madhara yake katika Serikali na ni moja ya ajenda katika matukio muhimu ya
Wizara. sekta ya maji. Mwaka 2006/2007, Wizara iliendelea
kutekeleza mkakati wa kupambana na janga la UKIMWI
kwa kuwapatia mafunzo ya kujikinga na maambukizi
watumishi 787 na kuwahamasisha kupima afya zao
mapema ili waweze kupatiwa msaada kwa wale
watakaobainika kwamba wameathirika. Hadi Juni, 2007
watumishi wawili (2) wamejitokeza na wameanza
kupatiwa huduma kwa kuzingatia Waraka wa Utumishi
wa Umma Na.2 wa mwaka 2006.
196
WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kusambaza Sera ya Mifugo kwa Kufuatia Serikali kupitisha Sera ya Taifa ya Mifugo
wadau baada ya kupitishwa. mnamo mwezi Desemba, 2006, Wizara imechapisha na
kusambaza nakala kwa wadau. Aidha, tafsiri ya Sera hii
katika lugha ya Kiswahili imekamilika na itachapishwa
hivi karibuni.
2. Kuandaa Mkakati wa kutekeleza Sera Maandalizi ya kutayarisha Mkakati wa kutekeleza Sera
ya Taifa ya Mifugo baada ya ya Taifa ya Mifugo yanaendelea. Hatua za kumpata
kupitishwa. Mtaalamu mwelekezi zinaendelea.
3. Kurekebisha sheria za mifugo Rasimu ya sheria mpya ya Ustawi wa Wanyama
zifuatazo: Ulinzi kwa Wanyama (Animal Welfare Act) imekamilishwa na marekebisho
Wafugwao (The animal protection ya sheria ya Ngozi yamefanyika. Mapendekezo
Ordinance) Sura ya 153 ya mwaka yamewasilishwa Sekretariati ya Baraza la Mawaziri na
1930 na Kuzuia wanyama wazururao yamepangwa kujadiliwa Julai, 2007.
(The Animal Pounds Ordinance) Sura
ya 154 ya mwaka 1930; Kudhibiti Rasimu ya sheria ya Maeneo ya Malisho na Sheria ya
Ndorobo (The Tsetse fly Control Vyakula vya Wanyama (Grazing Land and Animal Feed
Ordinance) Sura ya 100 ya mwaka Resources Act), imekamilishwa na itapelekwa kwa
1943; Ngozi Na. 30 Sura ya 120 ya wadau ili kupata maoni yao.
mwaka 1965; na Sheria ya Mbolea na
vyakula vya Mifugo (The Fertilizer and Rasimu ya kwanza ya sheria ya kuanzishwa Taasisi ya
animal Foodstuff Ordinance) Sura ya Utafiti wa Mifugo (National Livestock Research Institute
467 ya mwaka 1962. Pia, kuandaa Act), sheria ya kuanzishwa Maabara Kuu ya Mifugo
sheria mpya zifuatazo:- Sheria ya (Central Veterinary Laboratory Act) na sheria ya
kuanzishwa Taasisi ya Utafiti wa Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji (Livestock Identification,
Mifugo (The National Livestock Registration and Traceability Act) zinaendelea
Research Institute); Sheria ya kuboreshwa na wataalamu.
kuanzishwa Maabara kuu ya Mifugo
(The Central Veterinary Laboratory);
na Sheria ya Uendelezaji wa Maeneo
ya Malisho.
4. Kuimarisha kitengo cha takwimu kwa Kitengo cha takwimu kimeimarishwa kwa kukipatia
kukipatia vifaa zaidi, kutoa mafunzo na vifaa zaidi, kutoa mafunzo na kukipatia watumishi
kukiunganisha na vituo vingine vya watatu (3). Aidha, watumishi wa kitengo hicho
Wizara. wamepatiwa mafunzo.
5. Kuimarisha mashamba ya uzalishaji Mashamba ya uzalishaji mitamba ya Nangaramo,
mitamba ya Nangaramo, Ngerengere, Ngerengere, Sao Hill, Mabuki na Kitulo yameimarishwa.
Sao Hill, Mabuki na Kitulo kwa Jumla ya ng‟ombe wazazi 60 aina ya “boran”
kuyanunulia ng‟ombe wazazi 310, walinunuliwa na kufanya jumla ya ng‟ombe
kuyapatia vitendea kazi na pembejeo walionunuliwa kufikia 230 mwaka 2006/07 na
za mifugo. kugawanywa kama ifuatavyo: Mabuki (85), Nangaramo
(85) na Sao Hill (60). Lengo la kununua ng‟ombe 310
halikufikiwa kutokana na kupanda kwa bei ya ng‟ombe.
197
6. Kushirikiana na Wadau wengine Wizara kwa kushirikia na shirika lisilokuwa la kiserikali
kusambaza ng‟ombe 200 ili kuongeza la „Heifer Project Tanzania‟ lilisambaza ng‟ombe 178
idadi ya ng‟ombe wa maziwa katika kipindi cha Julai – Desemba, 2006 katika mikoa ya
Mikoa ya Kusini ya Lindi, Mtwara na Lindi, Mtwara na Ruvuma.
Ruvuma.
7. Kushirikiana na mkoa wa Rukwa Serikali imeshatangaza umilikishaji wa shamba la
kukamilisha umilikishaji wa shamba la ng‟ombe wa maziwa la Malonje kwa wananchi. Taratibu
ng‟ombe wa maziwa la Malonje kwa za umilikishaji zinaendelea.
wananchi.
8. Kushirikiana na Bodi ya Maziwa Kwa kushirikiana na Bodi ya Maziwa Wizara
kuratibu uzalishaji na usindikaji wa imeendelea kuratibu uzalishaji, usindikaji na
maziwa nchini na kuandaa Wiki ya uhamasishaji wa matumizi ya maziwa nchini kupitia
Uhamasishaji Unywaji wa Maziwa machapisho mbalimbali. Wiki ya Uhamasishaji Unywaji
ikiwa ni pamoja na kuhamasisha Maziwa ilifanyika Kitaifa Jijini Mbeya kuanzia tarehe 1-4
unywaji wa maziwa, hususani mwezi Juni, 2007.
mashuleni.
9. Kuandaa na kutekeleza Mpango Mpango Mkakati wa kuboresha na kuendeleza
Mkakati wa kuboresha na kuendeleza uzalishaji katika ranchi za NARCO umekamilika na
uzalishaji katika ranchi za NARCO. kusambazwa kwa wadau (TIC, Hazina, MPEE na
PSRC) ili kupata maoni yao.
10. Kuhamasisha uzalishaji wa nyama na Mkutano wa wadau kuhusu kuhamasisha uzalishaji wa
biashara ya mifugo pamoja na nyama bora inayokidhi viwango vya kimataifa
uundwaji wa vyama vya ulifanyika. Aidha, u hamasishaji wa kuunda vyama vya
wafanyabiashara ya mifugo ili wafanya biashara ya mifugo na nyama umefanyika
kuwawezesha kutafuta masoko ya katika mikoa 11 ya Arusha, Manyara, Shinyanga,
ndani na nje. Dodoma, Singida, Mwanza, Mbeya, Iringa, Pwani,
Tanga na Dar es salaam ambayo imeshaunda kamati
za kimkoa zinazohamasisha wilaya kuanzisha vyama
vya wafanyabiashara.
11. Kuimarisha kitengo cha Utambuzi, Kitengo cha Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji wa Mifugo
Usajili na Ufuatiliaji kwa kutoa mafunzo kimeimarishwa kwa kupatiwa vitendea kazi na
na vitendea kazi ili kiweze kuandaa watumishi wake kufanya ziara ya mafunzo nchini
mfumo wa kutambua, kusajili na Zimbabwe, Namibia na Botswana. Serikali iko katika
kufuatilia mifugo na mazao yake. hatua za mwisho za kuanzisha Mfumo wa Utambuzi,
Aidha, kuanzisha Rejista ya Taifa ya Usajili na Ufuatiliaji wa Mifugo na Mazao yake.
kumbukumbu za mifugo kwa ng‟ombe Watalaamu wa mifugo 250, wafugaji 300,
wa maziwa na nyama katika wafanyabiashara ya mifugo 80 na wenye viwanda vya
mashamba makubwa 10 ya Serikali na kusindika mazao ya mifugo watano (5) walielimishwa
watu binafsi ya Mabuki, Kongwa, na kuhamasishwa kuhusu mfumo huo.
Kitulo, Mpwapwa, Nangaramo,
Ngerengere, Ruvu, Sao Hill, Kibebe Mashamba 35 ya serikali na watu binafsi yamefanyiwa
Farm na Sumbawanga Agricultural and tathmini kwa kukusanya takwimu za kutambua mifugo
Animal Feeds Industries. iliyopo kwa lengo la kuisajili katika Rijesta ya Taifa ya
Kumbukumbu za Mifugo.
198
Serikali imezindua uanzishaji wa Ofisi na shughuli za
Ofisi ya Kanda ya Afrika ya Shirika la Kulinda
Wanyama Duniani (World Society for Protection of
Animal – WSPA) Jijini Dar-es-Salaam ambayo imetoa
ajira kwa Watanzania watano (5). Ofisi inaratibu
shughuli za shirika na kusaidia Asasi zisizo za Kiserikali
kama TSPCA, ASPA na Dar Animal Haven kuendeleza
ustawi wa wanyama nchini.
12. Kuimarisha vituo vyote vya uhamilishaji Kituo cha NAIC kimeimarishwa kwa kununua
na kununua mtambo mpya wa microscope na kukarabati mtambo wa kutengeneza
kutengeneza “liquid nitrogen” kwa ajili hewa baridi ya Nitrojeni (LN2) itumikayo kuhifadhia
ya Kituo cha Mwanza. Pia, kuzalisha mbegu za uhamilishaji. Jumla ya dozi 58,500 za mbegu
dozi 48,950 za mbegu bora za zimezalishwa. Aidha, ng‟ombe 20,720 wamehamilishwa
uhamilishaji na kuhamilisha ng‟ombe na kufanya ng‟ombe waliohamilishwa kuanzia mwezi
48,500. Julai, 2006 hadi sasa kufikia 50,500. Lengo lilikuwa
kuzalisha dozi 48,950 na kuhamilisha ng‟ombe 48,500.
13. Kuanzisha matumizi ya teknolojia ya Maandalizi ya kumpata mshauri mwelekezi wa
upandikizaji wa mayai yaliyorutubishwa kuanzisha na kuendeleza teknolojia hii katika shamba
(Multiple Ovulation and Embryo la Uzalishaji mifugo la Sao Hill yanaendelea.
Transfer) katika shamba la mifugo la
Sao Hill.
14. Kutoa mafunzo kwa wachinjaji, Mafunzo yametolewa kwa wachinjaji, wachunaji na
wachunaji, wakataji nyama (butchers), wataalam wenigne 267 na kufanya idadi yao kufikia 441
wawambaji na wakaguzi wa ngozi 400 mwaka 2006/2007 katika mikoa ya Dar es Salaam,
ili kuboresha ubora na ukusanyaji wa Mwanza, Mbeya, Shinyanga, Dodoma na Arusha
ngozi katika maeneo ya vijijini. kupitia mradi wa ngozi wa CFC.
15. Kukarabati minada ya Buhigwe Ujenzi wa uzio kuzunguka mnada wa Meserani
(Kasulu), Kasesya (Sumbawanga (Arusha) na mnada wa Lumecha (Ruvuma) umefikia
Vijijini), Lumecha, Mlowa, Mbuyuni asilimia 50. Taratibu za kujenga na kukarabati minada
(Chunya), Meserani na vituo vya ya Buhigwe (Kigoma), Kasesya (Rukwa) na Mbuyuni
kupakilia mifugo katika minada hiyo. (Mbeya) zinaendelea. Aidha, mnada wa Kizota
Aidha, kuboresha mnada wa Kizota (Dodoma) unaboreshwa kwa kujenga bucha, maeneo
(Manispaa ya Dodoma) ili kufikia hadhi ya kupumzikia wateja na ya mfano ya kuchomea
ya kituo cha biashara ya mifugo. nyama ili uwe na hadhi ya kituo cha biashara ya
mifugo.
16. Kuanzisha mfumo wa kukusanya na Kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda, Biashara na
kusambaza taarifa za masoko ya Masoko Wizara imeanzisha mfumo wa utoaji wa taarifa
mifugo. za masoko ya mifugo (Livestock Information Network
Knowledge System - LINKS) katika minada 14 ya Pugu
(Ilala), Mhunze (Kishapu), Meserani (Monduli),
Weruweru (Hai), Ulemo (Singida), Korogwe,
Lugodalutali (Mufindi), Mkongeni (Mvomero), Kizota
(Dodoma Manispaa), Igunga (Igunga), Nasa (Magu),
Kiabakari (Tarime), Kiliamatundu (Sumbawanga Vijijini)
199
na Mbuyuni (Chunya) ambayo hutoa taarifa za bei na
aina ya mifugo iliyouzwa kwa madaraja kwa kutumia
ujumbe wa simu.
17. Kubaini maeneo yenye maziwa mengi Tathmini kubaini maeneo yenye maziwa mengi ili
na kuanzisha mfumo wa kukusanya, kuweza kuanzisha mfumo wa kukusanya, kuhifadhi na
kuhifadhi na kusindika maziwa. Aidha, kusindika maziwa imefanyika katika mikoa 11 ya
kuhamasisha uundaji wa vikundi vya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Dar es Salaam, Pwani,
wasindikaji na mazao yake. Morogoro, Iringa, Mbeya, Mwanza, Kagera na Mara.
18. Kuhamasisha uwekezaji zaidi katika Tathmini ya hali halisi ya viwanda vya kusindika nyama
viwanda vya kusindika nyama ili katika mikoa ya Arusha, Mbeya, Dar es Salaam na
kukidhi mahitaji ya soko. Shinyanga imefanyika. Aidha, Serikali imeridhia
kubinafsisha Kiwanda cha nyama cha Shinyanga kwa
Kampuni ya Triple “S” Beef Limited. Pia, Serikali
imeridhia kuuza asilimia 51 ya mali za machinjio ya
Dodoma kwa Kampuni ya National Investment
Company Limited (NICO).
19. Kujenga mabwawa mawili (2) katika Serikali ilichangia jumla ya Shilingi milioni 130 kwa ajili
Wilaya za Mwanga (1) na Kishapu (1). ya uchimbaji na ukarabati wa malambo 13 katika
Aidha, kuchangia ujenzi wa malambo Wilaya 8 za Lindi (2), Nachingwea (2), Kilwa (2),
20 katika maeneo ya Kiwawa na Longido (2), Maswa (2), Misungwi (1), Bariadi (1) na
Marendegu (Lindi), Maurowa na Chunya (1). Pia, mabwawa ya Kishapu na Mwanga
Ngereyani (Longido), Mbondo na yalichangiwa jumla ya Shilingi milioni 160 na ujenzi
Matekwe (Nachingwea), Mchakama na unaendelea.
Mtandago (Kilwa), Zavuza na Chogo
(Handeni), Mwamabiti (Shinyanga
Vijijini), Magaji (Chunya), Mwamboka
(Misungwi), Tubugwe (Kongwa),
Kinamweri (Bariadi), Kambala
(Mvomero), Manyoni (1), Urambo (1)
na Maswa (2).
20. Kuainisha maeneo yanayofaa kwa Hekta takriban 1,894,700 zimeainishwa kwa ajili ya
ufugaji, kuhamasisha matumizi ufugaji na kati ya hizo, hekta 706,783 zimetengwa
endelevu ya ardhi kwa ajili ya malisho katika vijiji 135 vya Halmashauri za Wilaya za Chunya
na kutoa mafunzo kwa wataalamu (hekta 448,977), Kisarawe (hekta 28,579), Lindi Vijijini
katika Halmashauri 10 za Wilaya za (hekta 76,800), Kilwa (hekta 10,733), Nachingwea
Bagamoyo, Bukombe, Handeni, (hekta 41,577), Makete (823), Mbarali (28,101),
Kishapu, Manyoni, Mvomero, Morogoro (9,871), Chamwino (9,176) na Rufiji (hekta
Nachingwea, Namtumbo, Nkasi na 52,146).
Urambo kuhusu matumizi bora ya
ardhi. Aidha, kuhamasisha uendelezaji Mafunzo yametolewa kwa wafugaji 102 na wataalamu
wa njia za asili za hifadhi ya malisho, 50 wa Mikoa 5 ya Kanda ya Ziwa kwa lengo la
matumizi bora ya mabaki ya mazao ya kuhamasisha uendelezaji wa njia za asili za hifadhi ya
kilimo, hususan wakati wa kiangazi na malisho na matumizi bora ya mabaki ya mazao ya
kufuatilia hali ya malisho katika kilimo.
maeneo ya malisho ili kutoa tahadhari
200
kwa wafugaji.
21. Kuimarisha mashamba ya malisho ya Mashamba ya kuzalisha mbegu bora za malisho ya
Vikuge na Langwira na kuanzisha Langwira (Mbeya) na Vikuge (Pwani) yaliendelea
mashamba mapya ya Kizota na kuimarishwa na mashamba mapya 6 ya taasisi za
Kongwa (Dodoma) Sao Hill (Iringa), Serikali yalianzishwa huko Tanga (Mivumoni na
Mivumoni na Buhuri (Tanga), West Buhuri), Dodoma (Kizota na Kongwa), Mwanza
Kilimanjaro na Mabuki (Mwanza) kwa (Mabuki) na Iringa (Sao Hill) kwa lengo la kuongeza
lengo la kuzalisha tani 25 za mbegu za uwezo wa uzalishaji mbegu bora za malisho. Pia,
malisho na marobota ya hei 150,000. mashamba 6 binafsi yameanzishwa. Tani 26 za mbegu
Aidha, kugharamia upimaji wa bora za malisho na marobota 216,000 ya hei
mashamba ya Vikuge na Langwira na yalizalishwa katika mashamba ya Serikali pamoja na
mashamba mapya yatakayo anzishwa. taasisi.
22. Kuhamasisha Halmashauri na Sekta Serikali imehamasisha watu binafsi kuanzisha
Binafsi kuanzisha mashamba ya mashamba ya kuzalisha mbegu za malisho. Zaidi ya
mbegu za malisho na hei ili kuwa na ekari 1,346 za watu binafsi zimepandwa malisho. Kazi
uhakika wa malisho, hususan wakati ya kuhamasisha inaendelea. Hadi sasa, mashamba
wa kiangazi. mapya sita yameanzishwa na Sekta binafsi imezalisha
tani 15 za mbegu na marobota 90,000.
23. Kudhibiti ubora wa vyakula vya mifugo Sheria ya vyakula vya mifugo inapitiwa upya ili kudhibiti
vinavyozalishwa na sekta binafsi ubora wa vyakula vya mifugo. Tani 606,566 za vyakula
ambayo inatarajiwa kuzalisha tani vya mifugo zilizalishwa. Uzalishaji huo ni sawa na
574,400. asilimia 93.3 ya mahitaji ya takriban tani 650,000 kwa
mwaka.
24. Kufuatilia maambukizi ya Sotoka katika Serikali imeendelea kufuatilia ugonjwa wa Sotoka
Kanda ya Ziwa na Kanda ya Kaskazini katika Kanda za Ziwa na Kaskazini ambapo sampuli za
na kuwasilisha Shirika la Afya ya damu 2,842 za ng‟ombe, 1,186 za mbuzi na kondoo na
Wanyama Duniani (OIE) maombi ya 18 za wanyama pori zilipimwa na kuthibitisha kwamba
nchi yetu kutambuliwa kuwa huru na nchi yetu haina maambukizi ya ugonjwa huo. Maombi
maambukizi ya Sotoka. ya kutambuliwa na Shirika la Afya ya Wanyama
Ulimwenguni (OIE) kuwa huru na virusi vya ugonjwa wa
Sotoka yamekubaliwa baada ya kuridhiwa na Baraza la
OIE na kutoa Cheti kwa nchi yetu cha kutokuwa na
virusi vya ugonjwa wa Sotoka mwezi Mei, 2007.
25. Kununua dozi milioni 5 za chanjo ya Serikali imenunua dozi milioni 3.2 za chanjo ya Homa
CBPP ili kuendeleza mpango wa „Roll ya Mapafu ya ng‟ombe (CBPP) kwa ajili ya kuendelea
Back Vaccination Plan‟ na mpango wa “Roll Back Vaccination Plan” ambapo
utakaotekelezwa na Halmashauri za jumla ya ng‟ombe milioni 2.5 wamechanjwa dhidi ya
Wilaya na Manispaa katika mikoa yote ugonjwa huo. Zoezi la uchanjaji linaendelea.
nchini isipokuwa Mkoa wa Kilimanjaro
ambao hauna ugonjwa ambapo jumla
ya ng‟ombe milioni 6 watachanjwa.
26. Kushirikiana na sekta binafsi na Sekta binafsi imeendelea kuhamasishwa kuagiza na
wafugaji kudhibiti ugonjwa wa Miguu kusambaza dawa ya chanjo ya Ugonjwa wa Miguu na
na Midomo. Aidha, kukamilisha ujenzi Midomo (FMD) ambapo jumla ya dozi 240,000
wa maabara ya ugonjwa wa Miguu na zilinunuliwa na kutumika katika mikoa ya Mwanza,
201
Midomo, Temeke. Iringa, Arusha, Morogoro, Dar es Salaam na Pwani.
Ujenzi wa Maabara ya ugonjwa wa Miguu na Midomo,
Temeke umekamilika.
27. Kushirikiana na Halmashauri na Ugonjwa wa Homa ya Nguruwe umedhibitiwa na
wafugaji kudhibiti ugonjwa wa Homa hakuna matukio mapya yaliyoripotiwa nchini. Aidha,
ya Nguruwe ambao bado hauna kinga elimu ya tahadhari ya kujikinga imeendelea kutolewa
ikiwa ni pamoja na kuzuia usafirishaji kutokana na taarifa ya kuwepo kwa ugonjwa huo nchini
holela wa nguruwe na mazao yake. Kenya.
28. Kutoa ruzuku ya shilingi milioni 500 Serikali ilitoa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ruzuku ya
kwa ajili ya ununuzi na usambazaji wa dawa za kuogeshea mifugo. Kampuni 8 ziliingia
madawa ya kuogeshea mifugo. mkataba wa kuagiza na kusambaza lita 126,000 za
dawa hizo katika mikoa 18 nchini ya Mwanza, Arusha,
Tanga, Kigoma, Rukwa, Tabora, Kilimanjaro, Kagera,
Manyara, Dodoma, Iringa, Mara, Morogoro, Lindi,
Shinyanga, Pwani, Singida na Mbeya. Aidha, dozi
120,000 za chanjo ya Ndigana Kali zilitolewa na FAO
ambazo zilitumika kuchanja ng‟ombe 117,184 katika
mikoa 12 nchini.
29. Kushirikiana na Halmashauri na Mafunzo yalitolewa kwa jumla ya wataalamu 15 kutoka
wananchi kufuatilia na kudhibiti Halmashauri za Wilaya 15 za Iringa (V), Karatu,
Mbung‟o na Nagana na kutoa mafunzo Kibaha, Kiteto, Kyela, Mbeya (V), Mbulu, Mvomero,
kwa wataalamu 50 katika mikoa yote Newala, Ngorongoro, Simanjiro, Singida (V), Temeke,
yenye tatizo la mbung‟o na nagana. Tunduru na Uyui walipatiwa mafunzo ya kudhibiti
mbung‟o na ugonjwa wa Nagana.
30. Kununua dozi 100,000 za chanjo ya Jumla ya dozi 100,000 za chanjo ya Kichaa cha Mbwa
kichaa cha mbwa na kusambazwa zimenunuliwa na kusambazwa katika wilaya 39 zenye
katika wilaya 90. Aidha, kuhamasisha ukubwa wa tatizo na zilizotoa taarifa za matukio ya
Halmashauri kutunga sheria ndogo ugonjwa huo. Aidha, maelekezo kuhusu udhibiti wa
ndogo za kuzuia uzururaji wa mbwa na Kichaa cha Mbwa na mbwa wanaozurura yametolewa
paka ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa kwa wilaya zote nchini.
huo.
31. Kuimarisha vituo vya ukaguzi wa Serikali imeendelea kuimarisha vituo vya ukaguzi wa
mifugo na mazao yake vya Madaba mifugo na mazao yake ambapo kituo cha Marendego
(Songea Vijijini), Sirari (Tarime), Holili (Kilwa) kimeimarishwa kwa kupatiwa mtumishi,
(Rombo), Ruvu Darajani (Kibaha) na kununuliwa vifaa vya kufanyia chanjo, usafiri wa pikipiki,
Kasanga (Sumbawanga Vijijini) pamoja ujenzi wa josho na nyumba ya mtumishi ili kutoa
na vituo vya bandarini vya Pangani na huduma kwa mifugo inayohamia mikoa ya kusini. Aidha,
Bagamoyo na viwanja vya ndege kituo cha Kwala (Pwani) kimeimarishwa na kimeanza
Kilimanjaro na Dar es Salaam kwa kutoa huduma za ukaguzi wa mifugo inayosafirishwa
kukarabati, kuvipatia vitendea kazi na kwenda nje ya nchi.
vifaa vya mawasiliano. Pia kuimarisha
vituo vya Karantini vya Kwala na
Mparange (Rufiji), Kirumi (Musoma
Vijijini) na Manjenga/Ihefu (Mbarali)
kwa ajili ya kudhibiti magonjwa ya
202
mifugo na uharibifu wa mazingira.
Aidha, kutoa mafunzo kwa wataalamu
60 katika vituo hivyo.
32. Kushirikiana na Halmashauri na wadau Ukaguzi umefanywa katika machinjio na mabanda ya
wengine kufanya ukaguzi wa ngozi katika mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya na
machinjio, mabanda ya ngozi, maghala Rukwa. Mafunzo yalifanyika kipindi cha Julai –
ya kuhifadhia ngozi, madawa ya Desemba, 2006 ambapo wakaguzi 80 wa nyama na
mifugo na pembejeo nyingine. Pia, ngozi kutoka Halmashauri 16 katika mikoa 6 walipatiwa
kutoa mafunzo kwa wakaguzi wa mafunzo kupitia mradi wa kuboresha zao la ngozi wa
nyama na ngozi 150 wa Halmashauri CFC.
mbalimbali.
33. Kuimarisha Baraza la Veternari ili Baraza la Veterinari lilisajili madaktari wa mifugo 18 na
liweze kusimamia utekelezaji wa kufanya idadi ya waliosajiliwa mwaka 2006/07 kufikia
miongozo, kusajili madaktari wapya, 36. Aidha wataalamu wasaidizi 89 waliorodheshwa na
kuandikisha, kuorodhesha na kujenga kuandikishwa na kufanya idadi ifikie 217.
uwezo wa wataalamu wasaidizi 300 wa
afya ya mifugo; kusajili na kukagua Vituo 22 vya huduma ya afya ya mifugo vimesajiliwa na
vituo 140; kutoa mafunzo ya kitaaluma kufanya vituo vilivyosajiliwa kufikia 37 mwaka huu wa
kwa wajumbe 9, watendaji 65 wa fedha, Pia vituo 43 vimekaguliwa na watoa huduma 135
Baraza la Taaluma ya Veterinari na wamekaguliwa katika Halmashauri za Jiji la Mbeya na
wakaguzi 77 na kuhamasisha Tanga na Manispaa za Arusha, Kinondoni, Morogoro
Halmashauri kuhusu ushirikishwaji wa na Wilaya ya Handeni.
sekta binafsi katika kutoa huduma za
mifugo. Wakaguzi 57 walipatiwa mafunzo kuhusu utekelezaji
wa kanuni za ukaguzi wa maadili chini ya Sheria ya
Veternari.
Mitaala ya kufundishia taaluma ya Veterinari Chuo
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Vyuo vya Mafunzo ya
Mifugo vya Madaba, Morogoro, Mpwapwa na Tengeru
imefanyiwa mapitio na kutolewa ushauri kwa kuzingatia
kanuni za Sheria ya Veternari.
34. Kufanya utafiti wa ng‟ombe wa nyama Taasisi ya Utafiti wa Mifugo – Mpwapwa imeendelea na
aina ya Mpwapwa pamoja na utafiti na uzalishaji wa ng‟ombe aina ya Mpwapwa
kuongeza idadi yao ili waweze ambapo idadi ya ng‟ombe hao imeongezeka kutoka
kusambazwa kwa wingi kwa wafugaji 979 hadi 1,060 na hivyo kukidhi mahitaji ya kuwa koo
nchini. kamili (stable breed). Pia, madume 50 yamesambazwa
kwa ajili ya utafiti na kuboresha uzalishaji katika
mazingira ya vijijini.
35. Kufanya utafiti wa ng‟ombe wa maziwa Utafiti wa ng‟ombe wa maziwa kwa ajili ya kuongeza
kwa kuzalisha na kusambaza kiwango cha kuzaa (calving rate) na kupunguza muda
teknolojia zitakazolenga kuongeza wa mzao (calving interval ) unaendelea katika vituo vya
kiwango cha kuzaa (calving rate) utafiti wa mifugo vya Tanga, Uyole na Mpwapwa
kutoka wastani wa asilimia 40 hadi 70, ambapo matokeo ya awali katika kundi la ng‟ombe wa
kupunguza muda wa mzao (calving maziwa nchini yanaonyesha kuwa kiwango cha kuzaa
203
interval) kutoka wastani wa miezi 24 kimeongezeka kutoka asilimia 40 na kufikia asilimia 55
hadi miezi 15. na muda wa mzao kutoka miezi 24 hadi 20. Vile vile,
vifo vya ndama vimepungua kutoka asilimia 40 hadi 30.
Aidha, uzalishaji wa maziwa kutoka ng‟ombe wa asili
umeongezeka kutoka wastani wa lita 0.5 hadi lita 2.5
vyote vikiwa na uhusiano wa karibu na lishe ya
wanyama na kiwango cha damu chotara.
36. Kufanya utafiti wa mbuzi na kondoo Utafiti wa mbuzi na kondoo umeendelea katika vituo
kwa kuzalisha na kusambaza vya utafiti vya Tanga, West Kilimanjaro, Kongwa,
teknolojia zitakazolenga kupunguza Naliendele na Mpwapwa. Tathmini ya utunzaji bora wa
vifo vya vitoto vya mbuzi na kondoo mbuzi chotara 526 waliozaliwa katika wilaya za
kutoka wastani wa asilimia 50 hadi 20 Kondoa, Muheza, na Handeni ulionyesha kuwa vifo vya
na kuongeza uzito wa mbuzi na mbuzi watoto vimepungua kutoka asilimia 50 hadi 30
kondoo kutoka kilo 25 hadi kilo 45 kwa na uzito kuongezeka kutoka kilo 25 hadi 30 kwa umri
umri wa miaka 2. wa miaka 2 ikiwa ni matokeo ya kuboresha mabanda
na lishe.
37. Kuendeleza utafiti wa kuku unaolenga Utafiti wa kutathmini ubora wa kuku chotara katika
katika kutathmini ubora wa kuku mazingira ya vijijini umefanywa katika vijiji 30 vya
chotara wanaoweza kukua haraka na Wilaya za Bagamoyo, Korogwe, Muheza, Pangani na
kuzalisha mayai kwa wingi katika Tanga mjini. Utafiti huo umeonyesha kuwa kuku
mazingira ya wafugaji wadogo. chotara wakilishwa vyakula vya ziada wanataga
wastani wa mayai 60 hadi 70 kwa mwaka ukilinganisha
na mayai 40 yanayotagwa na kuku wa asili
wanaofugwa kwenye mazingira hayo. Aidha, tathmini
ya aina 5 za kuku wa asili (Kuchi, Bukini, Kinyavu,
Kawaida na Kishingo) katika mazingira yaliyoboreshwa
imeanza katika vituo vya utafiti wa mifugo vya Tanga na
Mpwapwa ili kuangalia uhimili wa magonjwa na
uzalishaji wao wa nyama na mayai.
38. Kuendeleza utafiti wa nguruwe Utafiti unaolenga kuboresha nguruwe wa asili na
unaolenga kuboresha nguruwe wa asili chotara na mbinu za kuboresha uzalishaji umefanyika
katika maeneo mengine ya mikoa ya katika kaya 75 za Sumbawanga Vijijini. Tathmini
Mbeya, Iringa na Rukwa. imeonyesha kuwa katika mazingira ya wafugaji
nguruwe wa asili huzaa wastani wa watoto 7 kwa mzao
na kati yao ni 4 tu wanaofikia umri wa kuachishwa
kunyonya. Aidha, uzito wakati wa kuachishwa
kunyonya huwa ni wastani wa kilo 10.8 katika mazingira
ya vijijini.
39. Kuendeleza utafiti wa malisho ya Utafiti wa malisho ya mifugo unaendelea kufanyika
mifugo katika mikoa yenye mifugo katika vituo 5 vya utafiti kwa kusia mbegu bora za
mingi na maeneo kame ya Arusha, nyasi, mikunde na miti malisho kwa lengo la kuongeza
Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Manyara, uwingi na ubora wa malisho. Aidha, hifadhi ya malisho
Mara, Mbeya, Morogoro, Mwanza, (forage conservation) ilijaribiwa ili kukidhi mahitaji
Pwani, Rukwa, Shinyanga, Singida, hususani wakati wa kiangazi. Jumla ya hekta 117 za
Tabora na Tanga. malisho zilihusika katika Mikoa ya Dodoma, Mbeya,
204
Tabora na Tanga. Tathmini ya viinilishe vya
mchanganyiko na ongezeko la uzalishaji inaendelea.
40. Kuendelea kufanya utafiti wa maradhi Serikali imeendelea kufanya utafiti wa magonjwa ya
ya mifugo katika Maabara Kuu ya mifugo katika Maabara Kuu ya Mifugo Temeke na
Mifugo Temeke na Taasisi ya Utafiti Taasisi ya Utafiti wa Ndorobo na Malale (Tsetse and
wa Ndorobo na Malale (Tsetse and Trypanosomosis Research Institute – TTRI), Tanga
Trypanosomosis Research Institute – yakiwemo Homa ya Mafua Makali ya Ndege na Homa
TTRI), Tanga. ya Bonde la Ufa. Aidha, sampuli za ndege 3,438
zilifanyiwa uchunguzi katika maabara hiyo kwa
kushirikiana na OVI - Afrika Kusini na Chuo Kikuu cha
Minnesota Marekani na kudhihirisha kuwa ugonjwa wa
Homa ya Mafua Makali ya Ndege haujaingia nchini.
41. Kuendelea na utafiti wa chanjo ya Utafiti na uzalishaji wa chanjo ya Mdondo wa Kuku
Ugonjwa wa Mdondo wa Kuku pamoja unaendelea ambapo dozi 7,328,800 zimezalishwa na
na kuzalisha na kusambaza dozi kusambazwa nchini kupitia Vituo vya Kanda vya
milioni 12 za chanjo hiyo. Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo (VIC‟s) na kufanya
jumla ya dozi zilizozalishwa mwaka 2006/07 kufikia
14,496,000.
42. Kuimarisha Taasisi ya Mbung‟o na Taasisi ya Utafiti wa Mbung‟o na Nagana imefanyiwa
Nagana kwa kukarabati majengo na ukarabati wa majengo. Aidha, uchunguzi wa
kununua vitendea kazi. Aidha, mtawanyiko wa mbung‟o katika mikoa ya Kagera,
itakamilisha ramani inayoonyesha Tabora, Kigoma na Mwanza umefanyika na kazi ya
mtawanyiko wa mbung‟o nchini na kuandaa ramani ya kuonyesha mtawanyiko huo
itahamasisha wafugaji kutumia mitego inafanyika. Pia, wafugaji wamehamasishwa kutumia
inayohamishika ili kuweza kunasa mitego inayohamishika ili kuweza kunasa mbung‟o kwa
mbung‟o kwa wingi. wingi.
43. Kutayarisha na kusambaza mwongozo Rasimu ya mwongozo wa utoaji wa huduma za ugani
wa utoaji wa huduma za ugani na imeandaliwa na itapelekwa kwa wadau ili kupata maoni
kuratibu utoaji wa huduma hizo katika yao. Kukamilishwa kwa mwongozo huu kutasaidia
Halmashauri na sekta binafsi. kuratibu utoaji wa huduma za ugani katika Halmashauri
na sekta binafsi.
44. Kushirikiana na Halmashauri na wadau Wafugaji 20,440 walipatiwa mafunzo juu ya ufugaji
wengine kuwaelimisha wafugaji 20,000 bora, usindikaji, malisho, masoko na udhibiti wa
juu ya umuhimu wa ufugaji bora ikiwa magonjwa ya mifugo kupitia Vyuo vya Mafunzo ya
ni pamoja na matumizi na hifadhi bora Mifugo, Vituo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) na
ya mabaki yatokanayo na mazao ya Vituo vya Mafunzo kwa Wakulima (FTC).
Kilimo ili kuongeza chakula cha mifugo
wakati wa kiangazi.
45. Kushirikiana na Halmashauri Wataalam tisa wa mifugo kutoka Halmashauri nane za
kuanzisha mashamba darasa 10 katika Chamwino, Kongwa, Meatu, Misungwi, Morogoro
Mikoa ya Arusha, Dodoma, Morogoro, Vijijini, Mvomero, Ngorongoro na Nyamagana walipata
Mwanza na Shinyanga na kuimarisha mafunzo kwa ajili ya kuanzisha mashamba darasa
mengine 10 katika wilaya za Bukoba katika Halmashauri zao. Jumla ya mashamba darasa
Vijijini (2), Karagwe (2), Tanga Vijijini tisa kuhusu ufugaji bora wa kuku, mbuzi wanyama na
(1), Pangani (3) na Handeni (2). unenepeshaji wa ng‟ombe yameanzishwa katika Wilaya
205
hizo.
46. Kuandaa na kusambaza vipeperushi Nakala za vijitabu 13,200, vipeperushi 152,100, na
24,000 vya ufugaji bora, kuandaa na mabango 30,700 ya mada mbalimbali kuhusu uzalishaji
kurusha hewani vipindi 64 vya redio na bora wa mifugo, usindikaji, malisho, masoko na udhibiti
televisheni kuhusu ufugaji bora. Aidha, wa magonjwa ya mifugo viliandaliwa na kusambazwa
kushirikiana na TALMETA na kwa wadau. Jumla ya vipindi 52 vya redio na 12 vya
Halmashauri kukamilisha uundaji wa televisheni kuhusu ufugaji bora, uboreshaji zao la
vikundi vya wafanyabiashara ya mifugo ngozi, uendelezaji wa malisho na masoko; na udhibiti
katika mikoa ya Manyara, Singida na wa Mafua Makali ya Ndege, Homa ya Bonde la Ufa na
Tabora. Kichaa cha Mbwa vilitayarishwa na kurushwa hewani.
Uhamasishaji wa kuunda vyama vya wafanya biashara
ya mifugo na nyama umefanyika katika mikoa 11 ya
Arusha, Manyara, Shinyanga, Dodoma, Singida,
Mwanza, Mbeya, Iringa, Pwani, Tanga na Dar es
salaam ambayo imeshaunda kamati za kimkoa
zinazohamasisha wilaya kuanzisha vyama vya
wafanyabiashara.
47. Kuongeza idadi ya wanafunzi katika Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo vimeongeza usajili wa
Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo kutoka wanafunzi kutoka 748 katika kipindi cha mwaka
748 waliopo kwa sasa hadi 800 kwa 2005/2006 hadi 765 mwaka 2006/2007. Kati yao
lengo la kutumia kikamilifu uwezo wa wanafunzi 190 wanafadhiliwa na Serikali na 575
vyuo hivyo. Aidha, kugharamia wanajigharamia.
mafunzo kwa wataalamu 250 katika
ngazi ya astashahada (80) na
stashahada (170).
48. Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa Serikali imeendelea kusimamia utekelezaji wa mitaala
mitaala na mitihani katika vyuo vya na kuhakiki mitihani ya pamoja ya vyuo na kuweka
mafunzo ya mifugo. Pia, kuanzisha mihtasari katika mfumo wa moduli. Pia, ukaguzi wa
kozi ya ufugaji kibiashara ili kuboresha utendaji kazi ulifanyika katika vyuo vya Tengeru,
mbinu za ufugaji wa kibiashara. Mpwapwa, Morogoro, Madaba, Temeke na Buhuri.
49. Kukarabati majengo, miundombinu na Mazingira ya vyuo vya mifugo yameboreshwa kwa
kununua vifaa kwa ajili ya vyuo 6 vya kukarabati majengo, kuimarisha miundombinu,
mafunzo ya mifugo na kuendelea kununua vifaa vya kufundishia na vifaa vingine vya
kugharamia mafunzo ya uzamili kwa ofisi.
watumishi wake 6.
50. Kuajiri watumishi 113 ili kuimarisha Wizara imeajiri watumishi wanane na kukamilisha
utendaji na kutoa motisha kwa taratibu za kuajiri watumishi wengine 99, kuthibitisha
watumishi ikiwa ni pamoja na kazini 20 na kupandisha vyeo 179.
kuwapatia vitendea kazi na mafunzo.
51. Kutoa elimu kwa watumishi wake na Elimu kwa watumishi na wadau wa Sekta ya Mifugo
wadau wa Sekta ya Mifugo kuhusu kuhusu taratibu, kanuni, na maadili ya utendaji katika
taratibu, kanuni, na maadili ya utendaji utumishi wa umma imeendelea kutolewa. Aidha,
katika utumishi wa umma. Aidha, utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Kupambana na
kuendelea kutekeleza Mkakati wa Rushwa umeimarishwa.
206
Taifa wa Kupambana na Rushwa.
52. Kuendelea kuimarisha mahusiano ya Dawati la Jinsia limeimarishwa kwa kuundiwa Kamati
jinsia katika vitengo vyake na kutoa yenye wajumbe kutoka kila idara. Pia, mafunzo
mafunzo yahusuyo masuala ya jinsia yametolewa kwa Mratibu wa dawati hilo.
na kuandaa viashiria muhimu vya
kuweza kufuatilia na kupima mafanikio
ya jinsia ndani ya Wizara.
53. Kushirikiana na Tume ya Taifa ya Mpango Mkakati wa kudhibiti UKIMWI sehemu ya kazi
Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) kufanya umetekelezwa kwa kuunda Kamati ya UKIMWI (TAC)
tathmini ya athari za UKIMWI kijamii na na Sekretarieti yake. Aidha, dawati la kudhibiti UKIMWI
kiuchumi katika Wizara na Taasisi limeimarishwa kwa kupatiwa vitendea kazi na
zake na kuchukua hatua za kuzuia linandelea kuhamasisha vita dhidi ya UKIMWI ambapo
athari hizo. Aidha, kutoa mafunzo kwa Jumla ya makasha 411 ya kondom yalinununuliwa na
watumishi wa ngazi zote kwa lengo la kusambazwa. Aidha, watumishi wamehudhuria semina
kupambana na kupunguza athari na makongamano mbalimbali kuhusu UKIMWI.
zitokanazo na ugonjwa hatari wa Mtumishi mmoja wa Wizara alihudhuria mafunzo ya
UKIMWI. Vile vile, kuboresha mkakati muda mfupi nchini Afrika Kusini.
wake wa kupambana na kuenea kwa
UKIMWI.
54. Kukiimarisha kitengo cha habari, Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano kimeendelea
mawasiliano na elimu kwa kutoa kuimarishwa kwa kuwapatia watumishi husika mafunzo
mafunzo kwa watumishi na kukipatia stahili pamoja na kukipatia vitendea kazi na samani.
vifaa na vitendea kazi muhimu ili
kiweze kutekeleza majukumu yake
kwa ufanisi.
55. Kushirikiana na wadau wa sekta Rasimu ya Mkakati wa Mawasiliano wa Wizara ipo
kukamilisha maandalizi ya Mkakati wa katika hatua za kukamilishwa.
Mawasiliano wa Wizara.
207
WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI NA MICHEZO
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuanzisha Tovuti ya Habari kwa umma Ujenzi wa Tovuti umekamilishwa na kampuni ya
itakayotumiwa na wananchi kuelezea Infocom Technologies Ltd. Tovuti ilianza kwa majaribio
kero zao za maisha na kutoa maoni tarehe 22 Juni, 2007.
mbalimbali yatakayosaidia Serikali
katika utekelezaji wa mipango yake. Maafisa Habari wawili wamepelekwa Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam kusomea masomo ya juu ya kompyuta
yatakayowawezesha kuendesha Tovuti hiyo baada ya
mkandarasi kuondoka.
2. Kupendekeza Serikalini muswada wa Maoni ya wadau kuhusu muswada huo
uhuru wa habari kuhusu upatikanaji wa yameshakusanywa. Mchakato umeanza kuandaa
haki ya wananchi ya kupata na kutoa Waraka wa Baraza la Mawaziri kwa hatua za kutunga
habari. Sheria ya Habari.
3. Kupendekeza Serikalini uanzishwaji Mapendekezo ya chombo hicho kitakachojulikana kama
wa Chombo kitakachoratibu kisheria Bodi ya Viwango vya Vyombo vya Habari (Media
viwango vya elimu na taaluma ya Standards Board) yatakuwa ni sehemu ya Sheria ya
habari. Habari inayopendekezwa kutungwa.
4. Kuanzisha mtandao kati ya Idara ya Mkutano wa kwanza baina ya Maafisa Habari na
Habari na Vitengo vya Habari Maafisa Mawasiliano ulifanyika tarehe 25 Agosti, 2006
Serikalini. na kubainisha vipaumbele katika kuitetea na kuitangaza
Serikali.
Mkutano wa pili ulifanyika Mbeya, Oktoba 30 hadi
Novemba 2, 2006 na kuhusisha Maafisa Habari na
Mawasiliano 70. Katika mkutano huo, mkakati wa
pamoja wa kuitangaza Serikali uliandaliwa.
Mtandao wa Mawasiliano ya intaneti unaanzishwa chini
ya Mradi wa Tovuti ya Habari kwa Umma. Kazi ya
Kufunga mitambo katika ofisi za Maafisa Habari na
Mawasiliano wa Wizara itaanza Julai, 2007.
5. Kufungua Ofisi za Habari katika Mikoa Serikali imeamua kuwa Ofisi za Habari Mikoani ziwe
ya Kigoma, Mbeya, Mtwara, Mwanza sehemu ya Sekretarieti ya Mikoa kama sehemu ya
na Rukwa na kuimarisha zilizopo kwa mpango wa Serikali wa kuimarisha Sekretarieti hizo.
vifaa na mafunzo. Wizara itashirikiana kwa karibu na TAMISEMI katika
zoezi la kuajiri na kuwaendeleza kitaaluma maafisa wa
Habari Mikoani.
6. Kuimarisha Vitengo vya Habari katika Orodha ya vifaa vya kompyuta kwa ajili ya maofisa
Wizara na Idara zinazojitegemea. wasiokuwa navyo imeandaliwa na baadhi vimeanza
kununuliwa chini ya Mradi wa Habari kwa Umma
unaotekelezwa na Idara ya Habari.
Aidha, mafunzo yameanza kutolewa kwa Maafisa
Mawasiliano wa Wizara. Awamu ya kwanza ya
208
mafunzo hayo ilifanyika Mbeya Oktoba/ Novemba,
2006.
7. Kueneza usikivu na kuonekana kwa Mitambo imeagizwa na mkandarasi ameteuliwa
vipindi vya RTD na TVT nchi nzima. kufunga mitambo ya FM katika Mikoa ya Kigoma,
Mtwara, Mbeya, Mwanza na Arusha. Ujenzi unatarajiwa
kukamilika mwezi Julai, 2007.
8. Kuongeza muda wa kurusha Radio Tanzania (PRT) inatangaza saa 24 kuanzia Julai,
matangazo ya RTD na TVT kufikia saa 2006 katika Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.
24. Televisheni ya Taifa nayo ilianza kutangaza saa 24
kuanzia Julai, 2006.
9. Kuanzisha gazeti la Kiswahili la Gazeti hilo lilizinduliwa mwezi 21 Desemba, 2006.
Serikali. Linajulikana kama Habari Leo.
10. Kukarabati Maktaba ya Taifa ya Mchakato wa kumpata mkandarasi umekamilika na
Kumbukumbu ya Picha iliyopo Dar es imeteuliwa kampuni ya „MF1 Office Solutions Ltd‟ ya
Salaam. Dar es Salaam kwa gharama ya sh. 369,052,710.00.
Mkataba tayari umeidhinishwa na Ofisi ya Mwanasheria
Mkuu wa Serikali. Utekelezaji wa mchakato huo
unaendelea.
11. Kuendesha mafunzo ya mbinu za Warsha ya mafunzo ya mbinu za Utawala na
utawala na uendeshaji wa shughuli za Uendeshaji wa shughuli za Utamaduni kwa Maofisa
utamaduni kwa Maofisa Utamaduni wa Utamaduni Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji
Wilaya, Miji, Manispaa na Majiji. haikufanyika kutokana na ufinyu wa bajeti.
12. Kutathmini mradi wa “TUSEME” kwa Tathimini ya Mradi wa “TUSEME” ilifanyika mwezi
wasichana wa Shule za Msingi na za Februari, 2007 katika Shule za Sekondari za Arusha,
Sekondari. Machame, Lindi, Msalato, Kilakala, Korogwe,
Bagamoyo na Mwenge. Tathimini imewasaidia
wanafunzi hasa wa kike kueleza waziwazi matatizo
yanayowasibu katika shule hizo na kuyatafutia
ufumbuzi wao wenyewe.
13. Kufanya utafiti wa mila na lugha za Utafiti umefanyika katika Mikoa ya Mara, Arusha na
asili kwa makabila ya nchi yetu ili Ruvuma. Katika utafiti huo imeonekana kwamba yapo
kukuza msamiati wa Lugha ya maneno mengi katika lugha za asili katika fani
Kiswahili. mbalimbali hususani, kilimo, uvuvi, ufugaji, n.k. ambayo
yanaweza kuingizwa katika lugha ya Kiswahili badala
ya kutumia maneno ya lugha za kigeni.
14. Kuendesha warsha 2, semina 1 na Warsha moja ya Kiswahili Sanifu ilifanyika Morogoro
mkutano 1 ili kuimarisha matumizi ya mwezi Septemba, 2006 iliyohusisha washiriki 50
Kiswahili sanifu na fasaha kwa wakiwemo Waandishi wa Habari, Watangazaji wa
Wizara, Idara za Serikali na Mashirika Radio na watumishi kutoka Idara ya Maendeleo ya
ya Umma. Utamaduni.
15. Kuandaa na kuendesha Mkutano Mkuu Mkutano ulifanyika Dodoma tarehe 11 - 16 Novemba,
wa Nne wa Sekta ya Utamaduni, 2006. Ulihusisha Maofisa Utamaduni kutoka Wilaya,
utakaofanyika Novemba, 2006. Mikoa, Taasisi za Utamaduni na wadau wengine wa
Utamaduni.
209
16. Kuratibu na kusimamia uendeshaji wa Tamasha la Utamaduni liliadhimishwa pamoja na siku
Tamasha la Utamaduni Kitaifa ya Utamaduni Duniani. Jumla ya vikundi 18 vya
litakalofanyika mwezi Mei, 2007. Utamaduni vilishiriki katika maonyesho ya Utamaduni
na shughuli za Sanaa. Shughuli hii ilifanyika Dar es
Salaam tarehe 21 Mei, 2007.
17. Kuanza kujenga Jumba la Utamaduni Kiwanja chenye ukubwa wa ekari 100 kimepatikana
la Taifa hapa jijini Dar es Salaam. katika Kijiji cha Kiromo Wilaya ya Bagamoyo.
Mkutano wa wadau kuhusiana na dhana nzima ya
Jumba la Utamaduni katika muktadha wa Tanzania
umefanyika. Aidha, mbunifu Majengo „Architect‟
ameshapatikana ambaye ndiye atasimamia kazi ya
kuandaa michoro na ujenzi.
Mawazo ya awali ni kuwa Jumba litakuwa na sehemu
kuu zifuatazo:-
Maonyesho ya Sanaa; Maigizo; Kituo cha Habari za
Utamaduni; Utunzaji wa Kumbukumbu za Utamaduni
wa Historia ya nchi yetu.
18. Kuendesha mafunzo ya Stashahada Chuo cha Sanaa Bagamoyo kiliendesha mafunzo ya
kwa Washiriki 100 na Mafunzo ya Stashahada kwa wanafunzi 95 na Mafunzo ya muda
muda mfupi kwa Wasanii 120 ambao mfupi kwa Wasanii 120 walio kazini
wako kazini katika Chuo cha Sanaa,
Bagamoyo.
19. Kuendesha Tamasha la 25 la Tamasha la 25 la Kimataifa la Chuo cha Sanaa
Kimataifa la Chuo cha Sanaa Bagamoyo lilifanyika mwezi Septemba, 2006 kwa
Bagamoyo litakalofanyika mwezi mafanikio makubwa.
Septemba 2007.
20. Kukarabati Jengo la Maonyesho ya Chuo cha Sanaa Bagamoyo kimeanza kufanya
Sanaa na kujenga Bweni la Wanafunzi ukarabati wa majengo ya Ukumbi wa Maonyesho
Chuo cha Sanaa Bagamoyo. yaliyoungua. Ujenzi wa bweni la wanafunzi
haukufanyika kutokana na ufinyu wa bajeti.
21. Kutoa elimu kwa kutumia Sanaa na Mpango wa uraghibishi kuhusu kujikinga na
Vipeperushi katika sehemu za maambukizi mapya ya VVU na UKIMWI umefanyika.
burudani nchini kuhusu namna ya Jumla ya vipeperushi 1,000 vimesambazwa katika
kupunguza maambukizi mapya ya maeneo ya burudani.
VVU/UKIMWI.
Utafiti umefanyika katika Mikoa ya Kigoma, Singida na
Tabora na kubaini kwamba kuna mila na desturi nzuri
zinazoweza kusaidia katika jitihada za kupambana na
kuenea kwa maambukizi ya ukimwi.
210
22. Kuendelea na kazi ya ujenzi wa Ujenzi wa Ukumbi wa Wazi wa Maonyesho (Open Air
Ukumbi wa Wazi kwa maonyesho ya Theatre) umekamilika kwa asilimia 60. Lengo ni
Sanaa awamu ya pili Ilala - BASATA kukamilisha ujenzi wa Ukumbi huo mwezi Septemba,
2007.
23. Kuandaa Warsha ya Wataalamu wa Warsha ya Wataalamu wa Kiswahili ilifanyika Kibaha
Lugha wa BAKITA na BAKIZA. mwezi Mei, 2007. Lengo la mafunzo lilikuwa kuwapa
mbinu zaidi za kufanya kazi zao ambazo wamekuwa
wakifanya kwa uzoefu.
24. Kuchapisha kitabu cha kufundishia Warsha iliyowajumuisha walimu wa Kiswahili kwa
Kiswahili kwa wageni nchini. wageni ilifanyika kwa lengo la kufanya maandalizi ya
msingi ya kuandika kitabu cha kufundishia wageni
Kiswahili Hatua ya kwanza. Kazi iliyofanyika ni
kuainisha mada za kitabu na uteuzi wa wataalamu wa
kuandaa Muswada wa kitabu hicho.
25. Kuandaa warsha ya kusanifisha istilahi Kufanya utafiti na kukusanya istilahi 1,800 katika
za kidiplomasia za mchanganyiko na uwanja wa Diplomasia na Uhusiano wa Kimataifa kwa
kuandaa mwongozo wa usafirishaji. lengo la kuzisanifu na kuandaa Kamusi kwa ajili ya
mikutano ya UA na kwingineko.
26. Kuchapisha kitabu cha makosa katika Ilifanyika warsha ya kuwaandaa Walimu wa Kiswahili
matumizi ya Kiswahili sanifu. kwa wageni. Kazi iliyofanyika ni kuainisha mada za
kitabu na uteuzi wa Wataalamu wa kuandaa Muswada
wa kitabu chenyewe.
27. Kuandaa semina kwa Vyombo vya Vipindi 52 vya “Lugha ya Taifa” vilitangazwa katika
Habari ili kudhibiti matumizi ya lugha redio. Aidha, vipindi 52 vya “kumepambazuka” na
ya Kiswahili yasiyokuwa sahihi. vipindi 52 vya “ulimwengu” wa Kiswahili vilitangazwa
katika Televisheni. Mafunzo hayo yalielimisha na
kuhamasisha matumizi fasaha ya Kiswahili.
28. Kuandaa Warsha kwa Wafasiri na Semina ya mafunzo kwa Wafasiri na Wakalimani 15
Wakalimani. ilifanyika. Lengo la mafunzo haya ilikuwa kuwapatia
wataalam mbinu zaidi za kufanya kazi ya Ukalimani na
tafsiri kwa umakini na ufanisi zaidi.
29. Kuandaa Mwongozo wa Waandishi wa Kazi hii haijafanyika kutokana na ufinyu wa bajeti.
Vitabu vya Kiswahili.
30. Kukarabati Banda la Maonyesho la Kazi imeanza na kukamilika.
BAKITA katika Uwanja wa Maonyesho
ya Kimataifa ya Biashara wa Mwalimu
J.K. Nyerere, Dar es Salaam.
31. Kuendelea kusimamia ukamilishaji wa Uwanja Mpya wa Michezo unaendelea kujengwa
Uwanja wa Kisasa unaojengwa jijini utakabidhiwa Serikalini mara utakapomalizika. Awamu
Dar es Salaam hadi hapo ya Pili ya ujenzi itahusisha utaratibu wa jenga, endesha
utakapokabidhiwa kwa Serikali mwezi na kabidhi {Build Operate and Transfer - (BoT)}.
Februari, 2008; na kukamilisha awamu
ya pili ya ukarabati wa Uwanja wa
211
zamani wa Taifa.
32. Kuandaa na kusimamia mjadala wa Mwongozo wa kuendesha mjadala huo umetayarishwa.
kitaifa utakaowashirikisha Watanzania Aidha, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) linaendelea
wote, hasa wadau wa michezo, ili kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wa
kupata mawazo yao kuhusu hatma ya Michezo kote nchini ambayo yatasaidia wakati wa
michezo nchini mwetu. majadiliano hayo.
33. Kuiandaa Timu ya Taifa inayojumuisha Timu ya Taifa katika Michezo ya 9 ya Mataifa ya Afrika
michezo mbali mbali kwa ajili ya 2007 huko Algeria ilishiriki kama ilivyopngwa. Timu
michezo ya Mataifa ya Afrika ilijumuisha Michezo ya Ngumi, Riadha, Judo, Mpira wa
yatakayofanyika Algiers-Algeria, Meza, na Michezo kwa watu wenye ulemavu wa
mwaka 2007. viungo.
34. Kuendelea kutoa mafunzo ya utaalamu Mafunzo ya Stashahada ya miezi 18 ya Ualimu na
wa Ualimu, Uamuzi, Uongozi bora na Uamuzi kwa michezo ya mpira wa miguu, mpira wa
huduma ya Kinga na Tiba, ili kuinua mikono, mpira wa kikapu, mpira wa wavu, netiboli na
viwango vya fani hizo katika Vyama na riadha yanaendelea katika Chuo cha Malya. Wanachuo
Vilabu vya Michezo. 36 wanaendelea na mafunzo hayo.
35. Kuboresha mazingira ya kufundishia Chumba kimoja cha darasa kimejengwa ikiwa ni
na kujifunza katika Chuo cha nyongeza ya Madarasa ya kujifunzia katika Chuo cha
Maendeleo ya Michezo Malya na vituo Michezo Malya.
vya Kanda vya Arusha na Songea.
Chumba cha Kompyuta na Maktaba vinaendelea
kujengwa katika Chuo cha Maendeleo ya Michezo
Malya. Majiko mapya mawili ya kupikia yamefungwa
na yanatumika.
Vituo vya Michezo vya Kanda Arusha na Songea vilitoa
mafunzo mbalimbali ya michezo. Washiriki 501
walihudhuria mafunzo hayo, Arusha 296 na Songea
205.
36. Kuwawezesha watu wenye ulemavu Timu ya wachezaji 24 ya watu wenye ulemavu ya
kushiriki mashindano ya kitaifa na Olimpiki Maalumu inaendelea na Maandalizi kwa
kimataifa, kwa kuiandaa timu ya Michezo ya Dunia itakayofanyika China mwaka 2007.
Olimpiki Maalumu itakayoshiriki
michezo ya Dunia itakayofanyika
China mwaka 2007.
37. Wizara ya Habari, Utamaduni na Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na
Michezo itashirikiana na Wizara ya Mafunzo ya Ufundi pamoja na TAMISEMI
Elimu na Mafunzo ya Ufundi zimekubaliana kuimarisha somo la Elimu ya Michezo
kuimarisha somo la Elimu kwa Shuleni, Vyuoni pamoja na kurejesha michezo Shuleni
Michezo shuleni kwa kutoa mafunzo ya na Vyuoni. Waraka wa Utekelezaji wa Baraza la
ualimu wa michezo. Mawaziri umeshaandaliwa.
38. Kuandaa na kuendesha kongamano Wizara imeandaa utaratibu wa kuwa na kongamano na
kwa vyama vya michezo na watu mbali viongozi wa vyama vya michezo ngazi ya Taifa kila
mbali kuhusu uanzishaji wa michezo baada ya miezi mitatu. Mikutano mitatu imefanyika.
ya kulipwa na kukusanya maoni Suala kuhusu michezo ya kulipwa lilipewa msukumo
212
kuhusu maendeleo ya michezo kwa mkubwa.
jumla.
39. Kuhamasisha kwa njia ya mikutano, Uhamasishaji umefanyika na vikundi 27 vya wanawake
semina na makongamano ili kuongeza vya michezo viliundwa na watu wenye ulemavu
ushiriki na uundaji wa vikundi zaidi vya wanaendelea kujitokeza katika michezo mbali mbali.
michezo kwa wanawake na watu
wenye ulemavu.
40. Kuwawezesha watumishi kuunda Mchakato umeshaanza kwa kulifikisha suala la
Ushirika wa Kuweka na Kukopa. kuanzisha SACCOS kwa watumishi katika Baraza la
Wafanyakazi lililofanyika Dodoma tarehe 1 – 2 Machi,
2007. Baraza la Wafanyakazi lilipitisha azimio la
kuanzishwa kwa SACCOS.
Mawasiliano yanaendelea baina yetu na Wizara ya
Kilimo, Chakula na Ushirika katika ukamilishaji wa
hatua za uanzishaji wa SACCOS kwa wafanyakazi.
213
WIZARA YA ULINZI NA JKT
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuendelea na kuimarisha mafunzo Jumla ya maafisa na askari 169 walihudhuria kozi
ndani na nje ya nchi kwa wanajeshi katika nchi 21 tofauti, na matokeo yake ni mazuri.
wetu. Aidha, mwezi Februari, 2007 kulifanyika zoezi la kivita
liitwalo JUHUDI. Zoezi hilo lilifanywa na 27 KJ Mkoani
Mara.
2. Kuendeleza na kuimarisha mazoezi ya Serikali imeendelea kuchukua hatua kuhakikisha Jeshi
medani na mazoezi ya ulinzi na amani. linapata uwezo wa kuwapatia wanajeshi wake
mafunzo na mazoezi ya elimu ya Kijeshi hususani
kuhusu matumizi ya teknolojia mpya ya kijeshi, mbinu
za kisasa za kivita na utendaji katika majukumu yake
mapya. Katika mwaka 2006/2007 wanajeshi wetu
wamewezeshwa kufanya mafunzo na mazoezi kuanzia
ngazi ya mtu binafsi (Individual training) hadi mazoezi
ya pamoja na makundi (collective formation training
exercises).
Ushiriki wa jeshi letu katika majukumu ya kimataifa,
ikiwa ni pamoja na ulinzi na uangalizi wa amani katika
nchi zenye migogoro duniani, ni njia mojawapo ya
kuwapatia wanajeshi wetu elimu zaidi ya kijeshi.
Ushiriki wa wanajeshi wetu katika majukumu haya
umewapatia ujuzi na kutekeleza majukumu yao katika
mazingira mbalimbali. Aidha, umetoa fursa kwa
wanajeshi wetu kujipatia uzoefu wa kujifunza kutoka
kwa wanajeshi wa nchi nyingine.
3. Kuendeleza na kuimarisha upatikanaji Jenereta mbili zimeshanunuliwa kwa ajili ya matumizi
wa vifaa na nyenzo bora za kufanyia kwenye kambi za JKT.
kazi.
4. Kuendeleza mipango ya ujenzi wa Wizara imepata mkopo wa fedha toka Shirika la Akiba
makambi mbali mbali ikiwemo ya Wafanyakazi (NSSF) shs. bilioni 21.0 kwa lengo la
kukamilisha ujenzi wa nyumba kwa ajili kujenga nyumba za makazi 270 maeneo ya Dar es
ya makazi, maghala na mifumo ya maji Salaam na Arusha kwa mwaka wa fedha 2006/07.
safi na maji taka na umeme. Ukarabati wa mifumo ya maji safi na maji taka
umekamilika katika kambi za Mirambo (Tabora) na
Lugalo (Dar es Salaam). Aidha, kwa kutumia fedha za
matumizi ya kawaida wizara iliendelea kufanya
ukarabati wa majengo mbali mbali na miundombinu
katika kambi mbalimbali zikiwemo za JKT.
5. Kupatikana kwa vyombo vya usafiri Magari yaliyonunuliwa kuanzia Julai, 2006 hadi Juni,
hasa magari. 2007 ni kama ifuatavyo:-
Nissani Patrol Pick up kumi na tatu (13); Nissan
Civilian Minbus mbili (2); Nissan Patrol station wagon
214
sita (6); Toyota Land cruiser S/wagon moja (1); Toyota
Hiace 15 seater moja (1); IVECO Trucks (6 Ton) 72.
Magari ya msaada yaliyopokelewa Julai, 2006 – Juni,
2007.
Kutoka China: Hyundai Tucson 32; Mitsubish Rosa
Minbus moja (1); IVECO Jeep nane (8)
Kutoka UAE:
Land Rover 110 P/up kumi (10); Land Rover
Ambulance mbili (2), Bedford Lorry mbili (2).
6. Kuwapatia wanajeshi na vijana wa JKT Hatua zilizochukuliwa ni kununua sare za jeshi na vifaa
sare za kutosha kulingana na stahili vyake kukidhi mahitaji ya askari wapya pamoja na
kwa wakati. mavazi ya kubadili kwa wanajeshi waliopo kulingana na
uwezo kifedha. Kipaumbele kinatolewa kwa combat
dress, boots, mavazi ya baridi na vitambaa vya
kushonea sare za matumizi ya kila siku katika majeshi
yetu.
7. Kuwapatia vijana wa JKT, wanajeshi Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa inaendelea
pamoja na familia zao huduma za tiba. kuwapatia wanajeshi na vijana wa Jeshi la Kujenga
Taifa (JKT) huduma na mahitaji muhimu katika viwango
vinavyoridhisha. Ikiwemo chakula, sare, vifaa vya
malazi, mabwalo na huduma bora za tiba na juhudi za
kuzuia maambukizi mapya ya ugonjwa wa UKIMWI.
8. Kuwapatia wanajeshi na vijana wa JKT Ili kukabili tatizo la upandaji bei za vyakula na
huduma ya chakula. kusababisha kushuka kwa ubora wa huduma
inayotolewa Serikali imeongeza kiwango kutoka Tshs.
60,000/= hadi Tshs. 75,000/= kwa mtu kwa mwezi
kuanzia nusu ya pili ya mwaka 2006/2007.
Inategemewa kuwa badiliko hilo litaleta unafuu, ingawa
kiwango hicho bado hakijafikia gharama halisi
kulingana na bei za chakula katika soko.
9. Kulipia kikamilifu huduma za maji na Huduma za maji na umeme zimekuwa zikilipwa kwa
umeme. wakati kwa mamlaka husika kwa kutumia fedha
zinazopatikana kwa kila mwezi.
10. Kuendelea na upimaji wa maeneo ya Maeneo yaliyopimwa ni pamoja na; Tanganyika
JWTZ na JKT na kuyapatia hatimiliki Packers (977 KJ); Mwenge Band Coy; Dodoma
pamoja na kulipa fidia kwa wananchi Makutopora JKT; Lindi- Singino Radar; Ngerengere;
waliochukuliwa maeneo kwa ajili ya Mtwara – Umoja Camp; Mwanza Nyegezi (MTC);
shughuli za JWTZ na JKT. Shinyanga – Meatu; Songea (37 KJ); KTC – Dar es
Salaam; Ubungo Kibangu (671 KJ), Lake Duluti Estate-
Ltd (eneo la ziada la CSC Tengeru) na Singino Kilwa.
11. Kuwapatia wanajeshi na watumishi wa Kero ya makato ya baiskeli na mafriji imeondolewa kwa
Umma stahili zao za kisheria kwa kuwafidia wahusika vifaa walivyokuwa wanadai kabla
wakati na kikamilifu zikiwemo ya mwaka 2001. Kuhusu kero ya mikopo ya magari
mishahara na likizo. Hii ni pamoja na kwa maafisa wa JWTZ, Serikali imesimamisha makato
kuendelea na udhibiti wa kero ya mikopo hiyo na kusamehe 25% ya mkopo kwa
215
zilizokwisha kuondolewa jeshini hasa wanajeshi wanaoendelea na makato ya mikopo.
zinazohusu madeni binafsi kwa
wapiganaji. Mishahara na malipo mengine vikosini imeboreshwa
hususan ongezeko la kima cha mishahara. Sehemu
kubwa ya madai binafsi ya wanajeshi na watumishi wa
Umma ya miaka ya nyuma yamelipwa. Usimamizi wa
utoaji wa huduma bora za mikopo na vinywaji vya
motisha kwa wanajeshi umetekelezwa kwa kusimamia
makato ya mikopo bila kuathiri wakopaji/au
wakopeshaji.
Jitihada kubwa zimefanyika kuwalipa wanajeshi na
watumishi wa Umma stahili zao za kisheria kikamilifu
ikiwa ni pamoja na kulipa mishahara na likizo kwa
wakati. Madeni yaliyokuwa yanadaiwa huko nyuma
katika mwaka 2004/2005 yamelipwa.
12. Kuendeleza juhudi za kupambana na Majeshi yetu yameendelea na juhudi za kupambana na
janga la Ukimwi. janga la UKIMWI kwa njia mbali mbali:-
Zimeundwa kamati maalum za kudhibiti Ukimwi (JWTZ
na JKT); JKT lilipeleka ujumbe wa maafisa wa ngazi
ya juu kwenda nchini Uganda kujifunza jinsi nchi hiyo
ilivyofanikiwa katika kudhibiti Ukimwi; katika mikutano
ya kila siku na amri za kila siku, suala la UKIMWI
hujadiliwa na kupewa uzito unaostahili; yameendeshwa
mafunzo kwa wajumbe wa kamati za ushauri za vikosi
pamoja na kuundwa kamati za vikosi, zimeanzishwa
huduma za ushauri nasaha na upimaji kwa hiari katika
vikosi, Hospitali za JWTZ na JKT zimekuwa ni vituo vya
kutoa dawa za kurefusha maisha kwa waathirika wa
ugonjwa wa Ukimwi.
13. Kuendeleza ushirikiano wa kijeshi kati JWTZ limeendelea kudumisha mahusiano mazuri
ya nchi jirani na rafiki katika nyanja kimataifa katika nyanja ya Ulinzi. Kwa kupitia
zinazohusu mafunzo ya pamoja, ushirikiano huo Tanzania imepata misaada mbali mbali
taaluma mbali mbali na kutekeleza ya kijeshi kama ifuatavyo:-
makubaliano yaliyofikiwa katika
ushirikiano wa kiulinzi ndani ya Mafunzo
ushirikiano wa Afrika Mashariki na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imetoa nafasi za
Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa kozi za kijeshi kwa maafisa na askari wa JWTZ nchini
Afrika. China.
Misaada ya Vifa na Zana za Kijeshi
JWTZ limepata msaada uliowezesha kununua vifaa vya
kijeshi kama meli za kijeshi, ukarabati wa rada na
ndege.
Ziara za Viongozi wa Majeshi. Katika kudumisha
mahusiano kati ya nchi hizi mbili, kumekuwepo na ziara
216
za kirafiki kwa viongozi wa juu, ambapo Waziri wa
Ulinzi na JKT ametembelea nchini China mwezi Mei,
2007 na viongozi wa ngazi za juu wa Jeshi la Watu wa
China pia walifanya ziara za kikazi nchini mwaka 2006
na 2007.
Ujerumani
Tanzania iliendelea kupata misaada toka Serikali ya
Ujerumani kama ifuatavyo:-
Ujenzi na ukarabati wa Hospitali ya Kijeshi ya Lugalo,
Hospitali ya Kanda ya Arusha, Mwanza na Mbeya.
Ujenzi wa Hospitali ya Bububu Kanda ya Zanzibar
umekamilika na ilikabidhiwa rasmi mwezi Machi 2007.
Vile vile Ujerumani wamekamilisha ukarabati wa
karakana kuu ya Jeshi iliyopo 501 KJ.
Nafasi mbali mbali za kozi za kijeshi na kitaalam katika
fani mbali mbali nchini Ujerumani zikiwemo uhandisi
makenika na tiba zilitolewa.
Canada
Serikali ya Canada iliendelea kutoa nafasi za kozi kama
vile kozi za ulinzi wa amani, lugha ya Kifaranza na
“Junior Command and Staff Course.” Jeshi la Canada
linatarajia kuendesha kozi maalum kwa wanasheria
wetu wa jeshi ili hatimaye waweze kufanya
marekebisho ya sheria zetu za kijeshi.
Marekani
Kufuatia uamuzi wa kurejesha mafunzo kwa Tanzania,
Marekani imetoa nafasi kwa baadhi ya kozi na semina
zinazofadhiliwa na nchi hiyo.
India
Iliendelea kutoa nafasi za mafunzo ya kijeshi kwa
maafisa.
Uingereza
Imeendelea kutoa nafasi mbali mbali za kozi na semina
zinazoendeshwa nchini Uingereza.
Ushirikiano na nchi zenye JKT
Ushirikiano na nchi zenye JKT za Zambia na Guyana
unaendelea kuimarika. Aidha Wizara ya Ulinzi ya
Msumbiji ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha
217
utaratibu wa kusaini mkataba wa ushirikiano katika
sekta ya ulinzi ili waweze kusaidiwa kuanzisha shughuli
za JKT.
Ushirikiano na Nchi za EAC
JWTZ linaendelea na utekelezaji wa mkataba wa
ushirikiano na Nchi za Afrika Mashariki katika sekta ya
ulinzi. Mpango wa utekelezaji wa mkataba huo
ulipitishwa na Mawaziri wa Ulinzi:-
Mafunzo ya Kijeshi
Nafasi katika vyuo zilitolewa na kutumiwa kama
ilivyopangwa. Ubadilishanaji wa Wanafunzi na
Wakufunzi umetekelezwa kama ipasavyo. Mzunguko
wa mazoezi matatu ya vituo vya uamrishaji kama
utangulizi wa Field Training Exrcises umekamilika. Nchi
za EAC hivi sasa zinafanya maandalizi ya zoezi la
medani litakalofanyika mwaka 2008.
Ushirikiano Kiufundi
Vifaa vya mawasiliano salama vimenunuliwa na
kufungwa kwa ajili ya Wakuu wa Majeshi. Taasisi za
kiufundi za kijeshi zimetolewa kwa matumizi ya nchi za
EAC. Rasimu ya Mwongozo (Roadmap) wa matumizi
ya taasisi za kiufundi imeandaliwa na itapitishwa katika
vikao vya sekta ya ulinzi. Rasimu ya sera ya utafiti na
maendeleo kijeshi imeandaliwa.
Ziara na Ubadilishanaji wa Taarifa
Ziara za viongozi zinafanyika mara kwa mara. Aidha,
michezo na utamaduni inafanyika kila mwaka kwa
mzunguko wa kila nchi kuwa mwenyeji wa michezo
hiyo. Tanzania ilikuwa mwenyeji wa wiki ya tatu ya
michezo na utamaduni wa kijeshi kuanzia tarehe 20 –
30 Mei, 2007 ambapo Tanzania ilikuwa mshindi wa
kwanza wa jumla wa michezo yote. Mzunguko wa pili
unatarajiwa kuanza mwaka 2008 ambapo nchi za
Rwanda na Burundi pia zitashiriki. Wakuu wa Usalama
wanakutana mara kwa mara kwa ajili ya kubadilishana
habari.
Ushirikiano na Nchi za SADC
Tanzania hivi sasa ni Mwenyekiti wa “SADC Organ”.
JWTZ limeendelea kuratibu na kufuatilia utekelezaji wa
makubaliano ya ki-ulinzi ya Jumuiya hiyo na kushiriki
218
katika vikao kwenye ngazi ya Mawaziri na Wakuu wa
Majeshi na Wataalam. Pamoja na utaratibu wa kikanda
majeshi ya nchi za SADC yamekuwa yakishirikiana kwa
karibu katika kutoa nafasi za mafunzo katika vyuo vya
kijeshi ili kubadilishana ujuzi na kuimarisha utendaji wa
majeshi hayo.
Wakuu wa Majeshi na viongozi wa Majeshi wamekuwa
wakitembeleana kudumisha mahusiano. Makao
Makuu ya Jeshi yanaendelea na mpango wa
kukamilisha mikakati ya kuunda kikosi ambacho
kitakuwa chini ya Brigedi ya SADC itakayoundwa katika
Jeshi la pamoja la Afrika. Pamoja na majukumu
mengine katika nyanja ya ulinzi Tanzania kama
mwenyekiti wa “Organ” ina jukumu la kufanikisha
uzinduzi wa SADCBRIG ambao unatarajiwa kufanyika
tarehe 17 Agosti, 2007 Lusaka nchini Zambia.
Tanzania inalo jukumu la kusimamia na kuratibu
msaada wa kikanda wa SADC nchini DRC baada ya
nchi hiyo kuwa katika migogoro ya kivita vya ndani hata
baada ya uchaguzi mkuu wa kidemokrasia uliofanyika
mwaka 2006.
Operesheni za Kulinda Amani
Tanzania inashiriki katika Operesheni za Umoja wa
Mataifa za kulinda amani katika nchi mbali mbali za
Afrika na Asia ambazo zilikumbwa na vita vya wenyewe
kwa wenyewe.
Kipindi cha mwaka 2006 – 2007 JWTZ lilipeleka
maafisa katika opereshini za kimataifa za kulinda amani
katika nchi za Ethiopia na Eritrea, Lebanon, Ivory
Coast, Sudan (UNMIS) kama waangalizi katika Jeshi la
Umoja wa Mataifa la kulinda Amani (UN MILOBs) na
wanadhimu.
14. Kuendeleza tafiti na uboreshaji katika Viwanda vinavyomilikiwa na JWTZ, (TATC--Nyumbu
uzalishaji wa bidhaa mbali mbali toka Project na Mzinga Corporation – Mazao KJ),
viwanda na mashirika yetu kwa vinaboreshwa ili kuweza kufanya tafiti na uzalishaji wa
matumizi ya majeshi yetu. bidhaa bora kwa matumizi ya Majeshi yetu.
15. Kuendelea kutoa mafunzo ya JKT kwa Mafunzo kwa vijana yameendelea kutolewa tangu
vijana wa Kitanzania yanayohusu yaliporejeshwa tena mwaka 2001. Lengo ni kufikia
Ulinzi na Ujenzi wa nchi, uimarishaji idadi ya vijana 15,000 kwa mwaka ifikapo mwaka 2010.
wa Umoja wa Kitaifa na kuwajenga Hadi hivi sasa imefikiwa idadi ya vijana 4,000 kwa
vijana katika uzalendo wa hali ya juu. mwaka 2006/2007.
219
16. Kuendelea kutoa mafunzo ya Mgambo Kanda zote nne za ulinzi zimeendesha mafunzo ya
kwa Umma wa Kitanzania kwa mgambo ya awali, “refresher” na uongozi mdogo katika
madhumuni ya kuimarisha ulinzi wa kipindi cha mwaka 2006/2007, vikosi vya JWTZ
umma. viliendelea kutoa wakufunzi wa kutosha. Mafanikio ya
kiasi cha asilimia 97% yamefikiwa kwa nchi nzima.
Mafunzo ya Awali
Mwongozo wa mafunzo ya mgambo wa mwaka 2007 ni
mwendelezo wa mafunzo ya mwaka 2006. Kila mkoa
uliagizwa kuwafundisha wanamgambo 1,000 kwa
mwaka ambapo jumla ya wanamgambo 11,600
walipata mafunzo.
Mafunzo ya Kujikumbusha (Refresher)
Maendeleo ya mafunzo ya kujikumbusha (refresher)
yaliendeshwa katika mikoa kumi ya Tanzania Bara.
Mikoa ambayo haikuendesha, sababu kubwa ilikuwa ni
kutojitokeza kwa wanamgambo pale ambapo mafunzo
yalipotangazwa.
Mafunzo ya Uongozi Mdogo
Katika mwaka 2006/2007 JWTZ liliazimia kuanzisha
tena mafunzo ya uongozi wa Mgambo yaliyokuwa
yamesimamishwa mwaka 1992 kwa sababu mbali
mbali za kiutawala. Jumla ya viongozi wa Mgambo 619
wamepatikana katika kipindi hiki. Mafanikio katika kila
mkoa ni kama ifuatavyo:-
Kagera (34); Mwanza (28); Kigoma (28); Tabora (28);
Shinyanga (29); Mara (29); Dar es Salaam (37);
Dodoma (29); Lindi (26); Morogoro (28); Pwani
(28); Mtwara (28); Manyara (25); Kilimanjaro (29);
Tanga (30); Singida (31); Arusha (34); Iringa
(30);Mbeya (3); Rukwa (29); Ruvuma (29); Jumla
(619).
Ushiriki wa Vikosi vya Mgambo katika Mazoezi ya
Kivita. Katika mwaka 2006/2007 Wanamgambo nchini
wameshirikishwa katika mazoezi mbali mbali ya kivita
kwa ngazi ya Kombania na Kikosi katika Kanda za
Ulinzi kama ifuatavyo:-
Kanda ya Magharibi ilishirikisha kikosi kimoja cha
askari wa miguu cha Mgambo katika zoezi la kivita
lililojulikana kama Ulinzi wa Umma mwaka 2006.
Mwaka 2006 kanda ya Mashariki ilishirikisha
kombania moja ya Mgambo katika zoezi lililoitwa
220
ZOEZI PIMA UWEZO.
(Uundaji wa Kombania za Mgambo)
Mikoa yote nchini imeagizwa kuunda Kombania za
Mgambo kuanzia ngazi za uongozi wa Tarafa. Kila
Wilaya nchini inatarajiwa kuwa na angalau kikosi
kimoja cha Wanamgambo hai wasiopungua 516
wanaofahamika kwa Makamanda wa Mgambo wa
Wilaya (DC) ifikapo mwezi Julai, 2008. Mafanikio
katika utekelezaji yameanza kuonekana, Vikosi 170
nchini vimeundwa na hatua ya kuviimarisha
inaendelea.
17. Kuendelea na utekelezaji wa Awamu Ujenzi umekamilika wa mtambo chotara wa (Hybrid)
ya Tatu ya Mradi wa Mtandao wa masafa ya “C” na “K”. Hii ni kuashiria utayari wa kutoa
Mawasiliano ya Pekee (ITN). huduma zozote za ki-mawasiliano zinazohitajika.
Ubadilishaji wa mitambo iliyochakaa unaendelea
vituoni. JKT imeaanzisha mtandao wa mawasiliano ya
ndani.
18. Kuboresha Utumishi wa Umma kama Jukumu hilo limekuwa likitekelezwa katika ngazi ya
ilivyoelekezwa katika “Public Service wizara. Aidha, kwa upande wa JWTZ, maafisa, askari
Reform Programme”. na watumishi wa Umma wamepelekwa katika vyuo
mbali mbali hapa nchini kwa lengo la kuboresha
utendaji.
221
WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuratibu utekelezaji wa Programu ya Semina za uhamasishaji zimefanyika kwa Wabunge,
Maendeleo ya Sekta ya Kilimo. Wakuu wa Mikoa, Makatibu tawala wa Mikoa,
Wakurugenzi wa Maendeleo wa Wilaya na Halmashauri
Kuu ya Taifa ya CCM.
Mipango kazi na Bajeti (Annual workplans and Budget)
zimeandaliwa na kujadiliwa na kupitishwa na “ASDP
Basket fund steering Committee”.
Akaunti ya Programu (ASDP Basket Fund Holding A/C)
imefunguliwa ili wahisani waweze kuweka fedha. Aidha,
wafadhili wanne wamekwishaingiza fedha zao (Japan
USD 752,445.44 na Irish Aid USD 1,534,925.00),
Jumuiya ya Ulaya (Euro 7,100,000) na Benki ya Dunia
(USD 8,053,046). IFAD bado wako kwenye hatua ya
kukamilisha taratibu zao kisheria
Kikao cha kuhamasisha ushiriki na nafasi ya sekta
binafsi katika utekelezaji wa ASDP kimefanyika.
2. Kuzijengea uwezo Halmashauri za Timu za wawezeshaji za Wilaya (District Facilitation
Wilaya wa kuandaa Mipango ya Team) katika Halmashauri zote zimepatiwa mafunzo ya
Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya namna ya kuandaa na kutekeleza Mipango ya
DADPs. Maendeleo ya Wilaya zao. Wataalamu wa wizara za
sekta wamekamilisha zoezi la kutoa maelekezo na
ufafanuzi zaidi kwa timu za wawezeshaji wa wilaya
zilizokuwa zikitoa mafunzo kwa timu za wawezeshaji
wa kata.
3. Kuandaa utaratibu wa kuratibu, Kamati inayoangalia masuala ya takwimu, utoaji wa
kufuatilia, na kutathmini utekelezaji wa taarifa na tathmini na ufuatiliaji imeundwa na
ASDP. inaendelea na kazi.
Mfumo wa ufuatiliaji na tathmini (M&E Framework)
unaendelea kuandaliwa kwa kuanza kuangalia na
kupitia mfumo wa utoaji wa taarifa za Halmashauri kwa
kutumia Plan Rep, Mfumo wa Serikali kuu wa kutoa
taarifa. Aidha, rasimu ya viashiria muhimu (Key
performance indicators) vimetayarishwa pamoja na
mchakato wa kupata mtaalam muelekezi
atakayetayarisha M&E System unaendelea.
4. Kuhakikisha upatikanaji wa pembejeo Mikopo ya pembejeo za kilimo na mifugo iliyotolewa na
za kilimo. pembejeo zilizonunuliwa ni kama ifuatavyo: Mikopo 88
222
ya mbolea mbalimbali tani 2,337.25, mikopo 14 ya
mbegu mbalimbali tani 49.5, madawa ya mimea ya
unga tani 4,363.62 na ya maji lita 2,569. Aidha,
madawa ya mifugo lita 1,557, vifungashi robota 10 na
plau 2,280. Matrekta makubwa 81 yamekopeshwa,
power tillers 51 na matrekta machakavu 5
yamekarabatiwa.
5. Kurutubisha udongo kulisha taifa. Utekelezaji wa usambazaji wa pembejeo umeendelea
katika vituo vikuu 24 vilivyoteuliwa kusambazia
pembejeo zenye ruzuku katika mikoa 21 ya Tanzania
bara. Vituo hivyo ni vya Iringa, Makambako, Mbeya,
Songea, Tunduru, Sumbawanga, Mpanda, Bukoba,
Mwanza, Musoma, Shinyanga, Tabora na Kigoma.
Vituo vingine ni Dodoma, Singida, Arusha, Babati,
Moshi, Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Tanga, Lindi
na Mtwara. Hadi kufikia tarehe 24 Mei 2007, jumla ya
tani 112,670.42 za mbolea na tani 1,355.63 za mbegu
bora zimesambazwa. Kati ya pembejeo hizo, tani
76,906.24 za mbolea zimeuzwa na zitafidiwa kiasi cha
sh. 12,201,512,860. Aidha, tani 628.70 za mbegu bora
zimeuzwa na zitafidiwa kiasi cha sh. 521,919,965.
6. Kupanua Kilimo cha Umwagiliaji. Upanuzi umeanza katika kanda 7 za umwagiliaji za
Mbeya, Mwanza, Kilimanjaro Morogoro, Manyara,
Mtwara na Tabora ili kuwezesha eneo linalomwagiliwa
kufikia Hekta 274,388 kutoka Hekta 264,388 za mwaka
2005/06.
Usanifu wa skimu 63 utakaowezesha uendelezaji wa
hekta 1,000,000 zilizopangwa kuendelezwa kwa kilimo
cha umwagiliaji hadi mwaka 2009/2010 umeendelea na
kufikia hatua mbali mbali. Kati ya skimu hizi, jumla ya
skimu 16 usanifu wake umekamilishwa.
Ili kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji
katika skimu 12, taratibu za zabuni za ujenzi kwa
skimu 4 zimefikia hatua za mwisho. Hizi ni skimu za
Uturo, Gwiri, Kimani na Luanyo Katika Wilaya ya
Mbarali Mkoani Mbeya. Ujenzi wa banio Skimu ya
Mwiruzi (Kibondo) umefikia 50% na mfereji mkuu
umejengwa km 2.
Ukarabati umeendelea katika skimu 8 ambazo ni
Mgololo Mufindi), Mto wa Mbu (Monduli), Sakalilo
(Sumbawanga), Rwangenyi (Tarime), Mang‟ola
(Karatu), Mwiruzi (Kibondo), Msoga (Bagamoyo) na
223
Msanjesi (Namtumbo) na uko katika hatua mbalimbali.
Usanifu wa Bwawa la Ulyanyama (Sikonge)
umekamilika, taratibu za zabuni ya ujenzi zinaendelea.
Pia usanifu wa mabwawa mengine matatu (3)
umekamilishwa. Aidha uanzishwaji na uimarishaji wa
skimu za umwagiliaji katika maeneo ya mwambao wa
Ziwa Nyasa na Ziwa Viktoria umeeendelezwa. Katika
maeneo ya mwambao wa Ziwa Viktoria, utoaji wa vifaa
vya umwagiliaji kwa wakulima wadogo wadogo
umefanyika baada ya kutoa pampu 155 za umwagiliaji,
vifaa kwa ajili ya kilimo cha matone (Drip Kits) 380,
pampu za upepo 12 na matanki 380 kwa vikundi vya
umwagiliaji 162. Hii ni katika Wilaya za Ilemela,
Nyamagana, Magu (Mwanza) Maswa, Tarime (Mara)
na Bukoba. Ukarabati wa skimu 4 kutoka katika
mwambao wa Ziwa Nyasa umeendelezwa na ujenzi wa
banio umekamilika kwenye Skimu za Kibande, Mkalati
na Ngingama.
Kazi za usimamizi, uendeshaji na ukarabati wa
miundombinu ya umwagiliaji iliyochakaa imekamilika
kwa Skimu ya Gichameda (200 ha) kanda ya Manyara
na ukarabati unaendelea katika Kanda zingine 7 za
Mwanza, Morogoro, Tabora, Mtwara, Kilimanjaro na
Mbeya.
7. Kuimarisha huduma za ugani. Mbinu shirikishi jamii ya Shamba Darasa zilitumika
kulenga kutoa mafunzo kwa wataalamu 262 wa ngazi
ya wilaya katika Halmashauri zote nchini. Aidha,
mafunzo ya aina hii yalilenga kutolewa kwa wakulima
200. Hadi kipindi hiki, wataalamu 147 kutoka Wilaya za
Mikoa ya Singida, Dodoma, Tanga, Pwani, Mbeya,
Rukwa, Iringa, Lindi, Mtwara na Ruvuma
wamefundishwa. Mikoa mingine ni Morogoro, Arusha,
Manyara, Mara, Kagera, Kigoma, Tabora, Mwanza na
Shinyanga. Wataalamu hawa watasimamia uenezaji
wa mbinu shirikishi ya Shamba Darasa kwa wakulima.
Pia wakulima 100 kutoka wilaya za Mbeya, Rungwe,
Morogoro, Mvomero, Babati, Arusha, Mbinga,
Namtumbo, Kongwa na Dodoma Vijijini nao wamepata
mafunzo ili wasaidiane na maafisa kilimo kuanzisha
Mashamba Darasa na watakuwa wahamasishaji kwa
wakulima wengine.
Ili kukabiliana na upungufu wa Wataalamu wa Ugani,
uchambuzi wa kina wa mahitaji ya wataalamu pamoja
224
na vifaa/vitendea kazi umefanywa kwa kushirikiana na
OWM -TAMISEMI. Wataalamu wa Ugani
wanaohitajika katika ngazi ya kata na kijiji ni 15,082,
waliopo ni 3,379 na upungufu ni 11,703. Utaratibu wa
kuajiri Wataalamu wa Ugani 2,500 unaendelea kwa
kushirikiana na Wizara za TAMISEMI, Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Fedha.
8. Kupanua matumizi ya Zana bora za Mafunzo ya matumizi ya zana za Kilimo Hifadhi
Kilimo. yamefanywa kwa wataalamu 23 kutoka Wizara ya
Kilimo Chakula na Ushirika na Mashirika yasiyo ya
Kiserikali ya RECODA, WADEC na CPAR-TZ,
mtaalamu kutoka Mradi wa Kilimo Hifadhi wa Babati na
Mkuu wa Kituo cha Mradi wa Matrekta Morogoro.
Mafunzo hayo yalitolewa kwa mfumo wa Shamba
Darasa na wakulima 3,675 walijifunza kwa vitendo
matumizi ya zana hizo.
Mafunzo juu ya matumizi ya zana bora za kilimo za
kukokotwa na wanyamakazi yamefanyika kwa
wakulima wafundishaji 40 kwa wiki tatu wilayani
Mpwapwa kwa kushirikiana na Asasi isiyo ya Kiserikali
(NGO) ya LVIA.
Zana bora za Kilimo Hifadhi zimesambazwa kwa
vikundi vya mafunzo vya wakulima. Zana hizo ni
pamoja na “ripper” 75 na “knife rollers” 30 ambazo
zimesambazwa katika Wilaya 20 za Mbeya, Kilosa,
Mvomero, Babati, Mbulu, Kiteto, Hanang, Karatu,
Arumeru, Dodoma (M). Dodoma (V), Mpwapwa,
Singida (V), Singida (M), Ileje, Kyela, Mufindi, Njombe,
Sumbawanga (V), na Sumbawanga (M). Aidha
mashamba darasa 200 ya mafunzo ya matumizi ya
zana za Kilimo Hifadhi yameandaliwa katika wilaya hizo
na pembejeo zikiwemo mbolea tani 24.1, mbegu za
mahindi tani 1.3, mbegu za mazao funika (cover crops)
tani 1.3, dawa za kuua wadudu lita 97 na za magugu
lita 79 kwa ajili ya mashamba ya mfano
zimesambazwa.
Vituo vya maksai 12 vya Sikonge FDC (Sikonge), Konje
(Handeni), Inonelwa (Misungwi) Kifunda (Rungwe),
Kipalapala (Tabora Mjini), Malagarasi (Kigoma),
Katumba (Sumbawanga), Kibakwe (Mpwapwa), Milama
(Mvomero), Ngimu (Singida), Gairo (Kilosa) na Ngana
(Kyela) vimeendelea kufanyiwa ukarabati kwa
225
kushirikiana na Halmashauri za Wilaya. Vituo hivyo
vimepatiwa zana mbalimbali zikiwemo plau, majembe
ya palizi, majembe ya matuta na “ripper” kwa ajili ya
kutoa mafunzo na kufanya maonesho kwa wakulima.
9. Kuanzisha mifuko ya utafiti wa Kanda Warsha za uzinduzi wa mfuko zilizoshirikisha wadau
(Zonal Agricultural Research and walioko kwenye ngazi ya kanda zilifanyika kwenye
Development Fund – ZARDEFs). kanda zote. Wadau waliwachagua kwa kura wajumbe
wa Kamati za Kanda kwa ajili ya kusimamia mfuko wa
ZARDEF (Zonal Steering Committee – ZSC). Kamati
hizi zitasimamia shughuli zote za Utafiti na Maendeleo
kwenye kanda. Kamati hizi za Usimamizi, kila moja ina
wajumbe 10 ambao asilimia 50 ni wakulima
wawakilishi. Wajumbe wengine ni wawakilishi wa
wajasiriamali wa shughuli za Kilimo na wawakilishi wa
taasisi zinazohusika na maendeleo ya Kilimo. Vile vile
katika warsha hizo kamati za kiufundi (ZARDEF
Technical Committee) zilichaguliwa. Wajumbe
waliochaguliwa katika kamati hizo mbili watapewa
mafunzo ya kuwawezesha kutekeleza majukumu yao.
Kwa kuanzia, kanda za Kati, Ziwa na Kaskazini
zitahusishwa katika mafunzo haya mwishoni mwa
mwaka wa fedha 2006/2007.
10. Kueneza dhana ya usimamizi wa utafiti Uhamasishaji wa CORDEMA umefanyika kwa
kulingana na mahitaji ya wateja (Client wadau wa Kilimo kwenye kanda zote za Utafiti na
Oriented Research and Development Mafunzo. Mafunzo kamili yatafanyika baada ya Kamati
Management Approach (CORDEMA)). za Uongozi (Zonal Steering Committee – ZSC) kuanza
kazi zake. Mafunzo ya CORDEMA yatahusisha wadau
wote; na ni ya wiki sita zilizogawa kwenye mafunzo ya
wiki mbilimbili (3 phase training programe). Mafunzo
haya yataanza katika kipindi cha fedha cha mwaka
2007/2008.
11. Kudhibiti visumbufu vya mimea na Ukaguzi wa mazao yanayoingia na yanayotoka nchini
mazao. ulifanyika katika bandari za DSM, Tanga, Kigoma na
Mtwara. Aidha, ulihusisha viwanja vya ndege vya DSM
na Kilimanjaro; vituo vya mpakani vya Namanga, Sirari,
Horohoro, Murongo, Mutukula, Tunduma na Holili.
Jumla ya tani 259,831.57 za mazao mbalimbali ya
kilimo zilisafirishwa nje ya nchi na tani 630,209.54 za
mazao yaliyoingia nchini yalikaguliwa na kupasishwa.
Katika kipindi hiki, vyeti vya usafi wa mazao 3,874 na
vibali 257 vya kuingiza mazao nchini vilitolewa, na
jumla ya shilingi 512,839,927.40 zilikusanywa.
Udhibiti uingizaji kiholela madawa ya kilimo umefanyika
ambapo viuatilifu 49 vya aina mbalimbali vimesajiliwa
na TPRI.
226
Udhibiti wa nzi wa maembe (Bactrocera invadens)
umefanyika kwa kusambaza mabango 2,700 na
vipeperushi 4,800 vinavyoelezea namna ya kumtambua
na kumdhibiti nzi mharibifu wa maembe. Kwa
kushirikiana na FAO/IFAD nakala 100 za kitabu kipya
(Mwaka 2006) kiitwacho “A Field Guide to the
Management of Economically Important Tephritid Fruit
Flies in Africa” kinachoelezea kuwatambua na
kuwadhibiti nzi waharibifu wa matunda kimechapishwa
na kusambazwa kwa wakaguzi wa vituo vyote vya
mipakani nchini ili kuwaongezea utaalamu wa
kutambua na kudhibiti nzi waharibifu wa matunda.
Aidha, wataalamu 19 wa kilimo wa wilaya kutoka
Wilaya zote za Mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara na
mabwana shamba 74 na wakulima 800 wamepatiwa
mafunzo juu ya kumdhibiti na kumtambua inzi mharibifu
wa embe. Mafunzo kama haya yalifanyika huko vikindu
wilayani Mkuranga kwa wakulima 19 wanaolima
maembe kibiashara (Association of Mango Growers –
AMAGRO). Katika jitihada za kupambana na tatizo hili
Wizara imeagiza lita 60 za kiuatilifu kijulikanacho kama
“Methyl euginol” kwa lengo la kumdhibiti nzi huyu
mharibifu katika mashamba ya wakulima. Dawa hii
ilichelewa kufika katika muda uliopangwa kwa sababu
ya kuharibika kabla ya kuingia nchini. Dawa hii sasa
itawasili nchini tarehe 30/07/07.
Migomba 40,644 yenye ugonjwa wa mnyauko wa
migomba unaotishia zao la migomba katika Mkoa wa
Kagera imeng‟olewa ili kuzuia ugonjwa huo usienee.
Aidha vimeundwa vikundi vya wakulima katika vijiji
vyote vinavyohofiwa kupata ugonjwa huo ili kufuatilia
kwa karibu tatizo hilo.
Mipango ya kutoa mafunzo ya IPM imefanywa na
utekelezaji umefanyika kwa watalaamu 28 wa Mikoa ya
Kigoma na Kagera. Aidha, mafunzo mengine kwa
watalaamu wa Afya ya Mimea ya Wilaya (DPPOs)
yalifanyika katika wilaya 26 zilizo chini ya mradi wa
PADEP.
Katika jitihada za kudhibiti viwavijeshi, mitego 70
ilifanyiwa ukarabati katika Mikoa ya Mtwara, Lindi,
Morogoro, Iringa, Mbeya, Dodoma, Singida, Shinyanga,
Tanga na Kilimanjaro. Jumla ya lita 29,983 za viuatilifu
227
na mabomba 4,429 ya kunyunyizia viuatilifu
yamesambazwa katika Mikoa ya Mtwara, Lindi, Mbeya,
Iringa, Ruvuma, Dodoma, Morogoro, Tanga,
Kilimanjaro, Arusha na Manyara. Aidha mafunzo
yalitolewa kwa mabwana shamba 871 wakulima 232 na
wahudumu wa mitego 34 katika mikoa ya Morogoro,
Lindi, Mtwara, Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara.
Panya walidhibitiwa katika vijiji 622 vya Wilaya 27 za
Mvomero, Morogoro vijijini, Morogoro mjini, Ulanga,
Kilombero, Bagamoyo, Mkuranga, Kibaha mjini,
Kisarawe, Rufiji, Mheza, Handeni,Korogwe na
Pangani. Wilaya zingine ni Kilindi, Lindi vijijini, Liwale,
Nachingwea, Ruangwa, Kilwa, Moshi vijijini,Hai,
Monduli, Kinondoni,Temeke, Nzega na Masasi. Jumla
ya kilo 3,606.11 za sumu ya panya zilitumika katika
udhibiti huo na wakulima 67,670 walipatiwa mafunzo
juu ya udhibiti panya katika wilaya zao.
Nzige wekundu walidhibitiwa katika maeneo ya mazalio
yao ambayo ni mbuga za Wembere, Malagarasi,
Iku/Katavi, Ziwa Rukwa na Bahi. Nzige hawa walikuwa
kwenye eneo lenye jumla ya hekta 16,580. Jumla ya
lita 7,895 za viuatilifu zilitumika katika kudhibiti nzige
hawa .
Udhibiti wa ndege waharibifu umefanyika katika Mikoa
ya Morogoro, Singida Shinyanga, Mwanza, Dodoma
na Kilimanjaro ambapo zaidi ya ndege milioni 100
waliangamizwa na lita 4,420 zilitumika.
Wasingedhibitiwa ndege hawa wangeweza kuleta
uharibifu wa tani 1,002 za nafaka kwa siku.
Ili kudhibiti magugumaji, mbawakavu wanaendelea
kuzalishwa na kusambazwa Ziwa Viktoria pamoja na
mabwawa yenye magugumaji. Jumla ya mbawakavu
milioni 4.5 walizalishwa katika vituo vya Kyakairabwa,
Kyaka, Chato, Nyegezi na Nyahiti na walisambazwa.
Kwa kuwa wadudu aina ya mbawakavu wameonekana
kushindwa kudhibiti magugumaji katika mito ya ukanda
wa ziwa (hasa mto Kagera na Mara) uchunguzi
unaohusiana na ubora wa maji, virutubisho katika maji
na hali ya hewa unafanyika ukilinganishwa na mito ya
Pangani na Sigi ambako mbawakavu wameonyesha
mafanikio ya kudhibiti gugumaji katika mito hiyo. Aidha
228
kwa kushirikiana na nchi za Kenya na Uganda mipango
inafanywa ya kutafuta wadudu maadui aina nyingine
ambao wataweza kudhibiti gugumaji katika mito.
12. Kutoa mafunzo ya Kilimo kwa Wakulima walipata mafunzo ya nyanja mbalimbali
wataalam na wakulima. katika vyuo saba, ambapo KATC Moshi ilifundisha
wanawake 117 na wanaume 176, Igurusi ilifundisha
wanawake 16 na wanaume 24, Ilonga ilifundisha
wanawake 13 na wanaume 37, Mlingano ilifundisha
wanawake 148 na wanaume 55, Mtwara ilifundisha
wanawake 58 na wanaume 63, Ukiriguru ilifundisha
wanawake 292 na wanaume 287, na Uyole ilifundisha
wanawake 42 na wanaume 216. Jumla ya wakulima
waliofundishwa ni 1,544.
Aidha, mafunzo kwa maafisa ugani 50 hayakuweza
kutolewa kwa sababu fedha iliyotengwa haikuweza
kutoka hadi sasa.
13. Kutoa mafunzo ya usindikaji wa mazao Tathmini ya mahitaji ya mafunzo katika hifadhi,
ya Kilimo. usindikaji na matumizi ya mazao hayo ilifanyika katika
mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa, Ruvuma na Mtwara.
Aidha program ya mafunzo iliandaliwa na mafunzo
kufanyika katika mikoa ya Iringa, Mbeya, Rukwa na
Ruvuma. Jumla ya wataalamu 123 wa kilimo katika
ngazi ya Mkoa na Halmashauri walipatiwa mafunzo.
14. Kuandaa mpango kabambe wa Mkutano kwa ajili ya kuandaa Mpango Kabambe wa
matumizi bora ya ardhi ya Kilimo Matumizi Bora ya Ardhi ya Kilimo umefanyika mjini
(Agricultural Land Use Masterplan). Morogoro. Mkutano umeshirikisha wadau mbalimbali
wa kilimo kutoka baadhi ya Wizara na Taasisi za
Serikali, na pia Taasisi zisizo za Serikali kama vile
Wizara ya Kilimo, Mifugo, Maliasili, TAMISEMI,
Mazingira, Ardhi, na baadhi ya Taasisi kama; – SUA,
IRA, UCLAS, NEMC, NLUPC, TIC n.k. Lengo la
mkutano lilikuwa kupata maoni ya wadau kuhusu
mambo muhimu ya kuzingatiwa kwenye mchakato wa
maandalizi ya “Agricultural Land Use Master Plan”, na
majukumu (nafasi) ya kila mdau katika utekelezaji wa
mpango huo.
Wadau kwa pamoja wameona umuhimu wa kuwa na
Mpango Kabambe wa Matumizi Bora ya Ardhi ya Kilimo
kwa kuwa mpango huo utasaidia kuelekeza matumizi
endelevu/ kuilinda, kurahisisha uwekezaji na kuchangia
katika kuondoa migogoro ya ardhi ya Kilimo.
15. Kuongeza uzalishaji wa mazao makuu Ekari 400 zimelimwa kwa ajili ya kuzalisha vipando
ya chakula na biashara nchini. bora milioni kumi na sita (16,000,000) vya zao la
muhogo vyenye ukinzani dhidi ya magonjwa na
229
wadudu. Kazi ilifanyika kwa kushirikiana na Idara ya
Magereza. Magereza yaliyohusika ni Namajani
(Masasi), Lilungu (Mtwara), Nachingwea, Korogwe,
Kigongoni (Bagamoyo), Tabora B (Serengeti),
Kasungamile (Sengerema), Kibondo, Urambo na
Kanegele (Bukombe).
Bustani sita za Serikali kwa ajili ya kuzalisha vipando
bora vya mazao ya bustani ziliendelea kutunzwa.
Bustani hizo pia ni kwa ajili ya kutoa mafunzo ya
teknolojia bora za uzalishaji mazao kwa wakulima.
Vituo hivyo pia hutumika katika kuhifadhi aina mpya na
bora za vipando vya matunda, viungo na mboga. Jumla
ya miche 48,400 ya aina mbalimbali ya mazao
ilizalishwa katika vituo hivyo. Usambazaji wa miche,
uliendelea kwa kasi ndogo kwa upande wa kituo cha
Songa kutokana na kutokuwa na mvua za uhakika.
Mipango ya kuendeleza zao la chai kwa Wilaya za
Mufindi, Bukoba, Muleba, Korogwe, Muheza, Kilolo,
Njombe na Rungwe imeingizwa kwenye mipango ya
Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya (DADPs) kwa ajili ya
kutekelezwa.
Wakulima 50 na wataalamu 10 Wilaya za Morogoro na
Muheza walipata mafunzo ya kilimo bora cha vanilla.
Machipukizi 70 ya migomba iliyozalishwa kwa chupa
(tissue culture banana) yalipandwa katika maonyesho
ya viwanja vya Nanenane mjini Dodoma. Aidha, bustani
za serikali ziliendelea kutunzwa na kuzalisha jumla ya
miche 16,000 ya michungwa iliyobebeshwa katika
bustani za Songa na Kizugu. Miche hiyo itasambazwa
kwa wakulima msimu wa mvua. Bustani za Mpiji,
Bugaga, Inyala na Jaegetal pia ziliendelea kuzalisha
aina mbalimbali za miche ya matunda na viungo.
Jumla ya kilo 500 za mahindi aina ya Situka
yanayostahimili ukame kutoka Selian zilipelekwa
Gereza la Kigongoni wilayani Bagamoyo kwa ajili ya
kuzalisha mbegu zaidi.
Kilo 2,300 za mbegu bora za soya toka kituo cha utafiti
cha Uyole zilipelekwa Ileje, Songea na Naliendele kwa
ajili ya kuzalisha mbegu zaidi.
230
Warsha ya kuendeleza uzalishaji na matumizi ya zao la
soya kwa mwaka 2006/2007 ilifanyika. Warsha iliweka
mikakati ya kuliweka zao hilo katika kuinua uchumi na
kuboresha afya ya watumiaji. Wajumbe walikuwa ni
wasindikaji wa vyakula vya binadamu na mifugo,
watafiti na wataalamu wa kilimo ngazi ya mkoa na
wilaya wa Mikoa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini na
Kanda ya Kusini. Wengine ni Taasisi za TFNC, TIRDO,
COSTECH, SIDO, TBS na Wizara za Mifugo na
Viwanda, Biashara na Masoko.
Ziara ya mafunzo juu ya kilimo cha zao la soya nchini
Zimbabwe ilifanyika. Mapendekezo ni kwa Tanzania
kuangalia uwezekano wa kuagiza teknolojia ya
matumizi ya virutubisho aina ya “rhizobium inoculant”
kuongeza uzalishaji wa soya kwa eneo na kuiga
utaratibu wa namna ya kuunda chama cha wazalishaji
wa soya (soya bean association) kama ilivyo
Zimbabwe.
Jumla ya machipukizi 22,970 ya migomba bora
yamesambazwa, yaliyotokana na migomba ya msimu
wa 2005/2006 ya Mwanza (Ilemela 5,630 na
Nyamagana- 5,440) na Mara (Tarime-11,900).
Miche bora 350 ya miembe ilipelekwa Dodoma
(Chalinze na Makang‟wa); miche 450 Mkuranga na 500
iliyozalishwa kwa ushirikiano na AMAGRO ilipandwa
Kibaha, Mkuranga na Kinondoni. Wakulima 100
walipewa mafunzo ya kilimo bora cha miembe.
16. Kuhimiza Kilimo nishati na mazao Taasisi na asasi mbalimbali zinazozalisha mbegu za
mapya. jatropha ziliainishwa kwa lengo la kuzifanya ziwe
wazalishaji wa mbegu ambazo zitasambazwa kwa
wakulima wengine wa kilimo cha mbono (jatrofa) nchini.
Taasisi hizo ni pamoja na JKT waliopewa tani nne (4)
za mbegu za jatrofa. Miche 650 ya jatrofa imepandwa
viwanja vya nanenane vya Dodoma na Morogoro kwa
ajili ya maonyesho.
Halmashauri nane (Sumbawanga, Mpanda, Nkasi,
Same, Mkuranga, Ilala na Bunda) zimepatiwa jumla ya
tani 1.5 za mbegu za jatrofa kwa ajili ya vikundi vya
wakulima wa maeneo yao.
231
Makampuni 21 ya ndani na nje yameanza kuwekeza
katika uzalishaji na usindikaji wa mazao ya nishati
mbadala. Baadhi yake ni SEKAB/BAFF, FELISA,
PROKON, AMMA na KAKUTE. Makampuni haya
yamekwisha panda zaidi ya hekta 5,000; na
yanaendesha kilimo cha mkataba. Aidha, wakulima na
taasisi zilizoainishwa ni vituo vya mfano vya
kuendeleza kilimo na matumizi ya mazao ya nishati
mbadala.
Jumla ya washiriki 15 kutoka Jeshi la Kujenga Taifa
(JKT) walipata mafunzo ya uzalishaji na matumizi ya
zao la jatropha mjini Arusha. Mafunzo hayo yalifanyika
kwa kushirikiana na Kampuni ya Kusambaza Teknolojia
(KAKUTE) inayoendeleza zao hilo nchini Tanzania.
Jumla ya kilo 450 za kutosha ekari 225 na zenye
thamani ya shilingi milioni 1.057 zilinunuliwa toka
KAKUTE na kusambazwa katika mashamba ya JKT ya
Oljoro, Maramba, Mgambo, Chita, Ruvu, Itende na
Mlale. Mashamba hayo yatakuwa chanzo cha mbegu
za jatropha na kutoa mafunzo kwa wadau juu ya
uzalishaji na matumizi ya zao hilo. Wizara inashirikiana
na Wizara za Nishati na Madini, Mipango, Uchumi na
Uwezeshaji na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na
Taasisi za Serikali na zisizo za Serikali katika
maandalizi ya sera ya kuendeleza uzalishaji na
matumizi ya mazao ya nishati mbadala.
17. Kuzijengea uwezo Halmashauri kuibua Mwongozo kwa ajili ya mafunzo ya utekelezaji wa
miradi inayolenga kutatua matatizo ya DADPs katika nyanja za usalama wa chakula
upungufu wa Chakula kupitia DADPs. umeandaliwa. Mwongozo huu utatumika kwa ajili ya
kutoa mafunzo kwa wawezeshaji wa ngazi za wilaya.
18. Kuimarisha uwezo wa kuratibu hali ya Jumla ya wataalamu 147 kutoka ngazi ya mkoa na
uzalishaji wa mazao ya Chakula nchini. wilaya zote walipatiwa mafunzo juu ya ukusanyaji wa
takwimu za uzalishaji wa mazao na taarifa za hali ya
chakula nchini.
19. Kupanua mtandao wa kupima kiasi cha Jumla ya wapima mvua 85 kutoka mikoa ya Dodoma,
mvua kutoka vituo 500 vya sasa hadi Singida, Shinyanga na Tanga wamepatiwa mafunzo ya
vituo 600. ufuatiliaji wa hali ya mvua na mazao mashambani.
Aidha vitendea kazi, makoti 100 na “gum boots” 100
vilisambazwa.
20. Kusambaza teknolojia mbalimbali Uboreshaji wa miongozo ya teknolojia za usindikaji
zitakazosaidia kupunguza upotevu wa umefanyika. Miongozo ya Utayarishaji na matumizi ya
mazao ya Chakula baada ya mavuno. mazao ya mtama, muhogo mboga na matunda
iliandaliwa jumla ya nakala. 750 zimechapishwa.
21. Kununua jumla ya tani 80,000 za Jumla ya tani 122,058 za akiba ya mahindi
mahindi na mtama tani 1,500. zimenunuliwa. Kati ya hizo, tani 92,097.51
232
zimenunuliwa kutoka kwa wakulima wa hapa nchini na
tani 30,000 zimenunuliwa kutoka kwa wafanyabiashara
walioagiza nje ya nchi. Hivyo, kuna akiba ya mahindi
yenye jumla ya tani 128,667.97. Aidha, tani 2,831.32
za mtama zimenunuliwa kutoka kwa wakulima wa hapa
nchini.
22. Kuweka mkakati wa kuvutia Kwa kushirikiana na Wizara na Idara nyingine za
wawekezaji na kuongeza upatikanaji Serikali wizara imeanza kutekeleza mikakati ya kuvutia
wa mikopo katika kilimo. wawekezaji katika sekta ya kilimo. Mikakati hiyo ni
pamoja na:
Kuondoa kodi zote zinazohusiana na uagizaji na
usambazaji wa pembejeo za kilimo kama vile
matrekta, mbolea na madawa.
Kuondoa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa
mazao yote ya kilimo ambayo hayajasindikwa.
Kupunguza kodi ya ardhi kutoka shilingi 600 hadi 200
kwa ekari.
Serikali kupitia TIC imeanzisha hifadhi ya ardhi ya
uwekezaji (landbank). Aidha, Serikali imepunguza
urasimu wa upatikanaji wa Hatimiliki kwa kuanzisha
kitengo maalum cha Ardhi katika ofisi za TIC.
Wawekezaji hutumia Hatimiliki hizo kupata mikopo
benki.
Serikali imeondoa kodi ya mauzo ya nje (export
taxes) kwa mazao yote ya kilimo ili kuvutia uwekezaji
na uuzaji wa mazao nje ya nchi.
23. Kuratibu utekelezaji wa Programu Utekelezaji umeanza kwa kuratibu chaguzi za viongozi
Kabambe wa Mageuzi na wa vyama vya ushirika nchini. Hadi Mei 30, 2007
Modenaizesheni ya Ushirika nchini. zimekamilika chaguzi za viongozi wa vyama vya
ushirika vya msingi katika mikoa ya Tanzania Bara
(ukiondoa vyama vya msingi vichache ambavyo
vilikuwa havijakamilisha taratibu). Aidha, chaguzi za
viongozi kwenye vyama vikuu zimekamilika kwa
asilimia 90. Mikoa ambayo chaguzi hizo hazijafanyika
ni Pwani na Morogoro. Vyama vikuu ambako chaguzi
zimekamilishwa karibuni ni; WETCU NA ICU (Tabora);
MBOCU, MICU, KYECU, RUCU na ISAYULA (Mbeya);
TANECU na MAMCU (Mtwara); ILULU (Lindi);
SONAMCU (Ruvuma) na CETCU – Singida. Lengo la
chaguzi hizo lilikuwa ni kupata viongozi waadilifu na
wenye upeo katika masuala ya uongozi na pia
kuwezesha vyama hivyo kufanya maboresho
yaliyokusudiwa.
Kuratibu Mikutano ya wadau wa Programu Kabambe ya
233
Mageuzi na Modenaizesheni ya Ushirika nchini ambayo
imechambua mipango ya kuboresha TFC na SCCULT
na kupanga mikakati ya utekelezaji wake.
Wizara imeandaa miongozo ya: Uhasibu na
Menejimenti ya fedha za SACCOS, Mifumo ya
Menejimenti ya Taarifa ili kuviwezesha vyama
kujiendesha kibiashara na kwa kuzingatia Sheria,
taratibu na maslahi ya wanachama wake.
Rasimu ya Waraka wa Baraza la Mawaziri kuhusu
utaratibu wa uanzishaji wa Benki ya Ushirika ya Taifa
inaandaliwa kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo
Serikalini.
Mafunzo ya awali yametolewa kwa wajumbe wa Bodi
za Vyama Vikuu vya Ushirika 7 vinavyohusika na uuzaji
wa mazao ya Pamba, Kahawa na Tumbaku kwa Mikoa
ya Tabora, Shinyanga, Mwanza, Mara na Kagera.
Kutoa udhamini wa mafunzo mbalimbali ambapo
Maafisa 146 wa Ushirika wamepata udhamini kama
ifuatavyo: Masters Degree (3), Post graduate Diploma
(11), Advanced Diploma (43), Ordinary Diploma (18) na
Professional Cooperative Financial Management (7),
Computer (2), Waendesha Mashitaka- Cooperative
Procecutors (14), na kozi nyingine fupi (5).
24. Kufufua, kuimarisha na kuendeleza Wizara imeshiriki katika utatuzi wa migogoro katika
Ushirika nchini. Vyama vya Ushirika ambapo miongoni mwa migogoro
iliyosuluhishwa ni mgogoro wa mali kati ya KCU na
KDCU uliokuwa umekwamisha shughuli za uwekezaji
katika miradi yao. Usuluhishi uliviwezesha vyama hivyo
kufikia makubaliano ya kugawana mali husika. Vilevile
Wizara iliendelea kufuatilia kesi mahakamani
zinazohusu viongozi, wanachama au wabia wa vyama
vya ushirika wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhirifu
katika vyama wanavyoviongoza.
Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imefanya
uhamasishaji mkubwa kwa wananchi ili wajiunge
pamoja na kuanzisha vyama vya ushirika. Jumla ya
SACCOS mpya 1,441 na vyama vya ushirika wa mazao
– AMCOS 43 vimeanzishwa nchini kati ya mwezi Mei,
2006 hadi Mei, 2007.
234
Mafunzo yametolewa kwa SACCOS 25 za mikoa ya
Pwani, Dar es salaam na Arusha kuhusu uboreshaji
(modernisation) wa SACCOS hizo ikiwa ni pamoja na
kubadili mifumo ya uendeshaji. Wajumbe wa Bodi na
watendaji 20 wa SACCOS 5 za Mkoa wa Dodoma
walipelekwa kwenye ziara ya mafunzo Pwani na Dar es
salaam kujifunza kwenye SACCOS zilizobadili mifumo
na kuajiri watendaji na zinatoa huduma/bidhaa
mbalimbali ikiwa ni pamoja na bima na huduma ya
ATM.
25. Kuimarisha uwezo wa Wizara wa kutoa Watumishi wapya 279 wa kada mbalimbali wameajiriwa
huduma kwa wadau wa Sekta ya hadi sasa. Watumishi walioajiriwa wameanza kuongeza
Kilimo. nguvu kazi katika utoaji huduma baada ya kupangiwa
vituo na kuanza kuteleza majukumu yaliyopo.
Mafunzo yametolewa kwa watumishi 13 ili kuweza
kukidhi mahitaji ya miundo yao ya Utumishi. Mafunzo
hayo yametolewa katika Chuo cha Utumishi wa umma.
Aidha, mafunzo ya muda mfupi yametolewa kwa
Wahudumu, Makarani wa Masijala na Makatibu
Muhtasi 35. Pia yalitolewa mafunzo elekezi kwa
waajiriwa wapya 279 ambayo yalitolewa kwa muda wa
wiki moja Makao Makuu ya Wizara.
Watumishi 973 walipandishwa vyeo katika zoezi la
mlundikano baada ya kupata kibali kutoka Ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Kero za muda
mrefu za kutopandishwa vyeo watumishi zimepungua
kwa kiwango kikubwa na hivyo kuongeza morali ya
watumishi kufanya kazi zilizopangwa.
Watumishi 475 wa Kanda za Nyanda za Juu Kusini,
Mashariki na Kusini wamepata mafunzo ya jinsi ya
kujikinga na maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
Watumishi waliopata mafunzo hayo wameonekana
kuelewa mbinu mbalimbali za kujikinga na maambukizi
na wengi wamehamasika na kujitokeza kupima virusi
vya UKIMWI.
26. Kuandaa maeneo mengine kwa Kazi ya kusavei (topographical survey) na kusanifu
wakulima waliovamia shamba la miundombinu mbalimbali iliyoainishwa imekamilika kwa
umwagiliaji la Mbarali. skimu zote zilizoandaliwa ambazo ni Gwiri (ha 500),
Luanyo (ha 500), Uturo (ha 700) na Kimani (ha 1,000).
Kazi ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji kwa
kutumia mkandarasi imeanza mwezi Mei, 2007 kwenye
skimu mbili za Uturo na Kimani.
235
27. Kufanya mapitio ya Sera, sheria na Wizara kwa kuwahusisha wadau mbalimbali kwenye
kanuni za Sekta ya Kilimo. sekta ya Kilimo, Ardhi na Sheria imekamilisha taarifa na
rasimu ya awali ya mapendekezo ya mfumo wa
kisheria unaofaa kwa ajili ya kulinda na kuendeleza
ardhi ya kilimo. Mapendekezo ya Sheria hiyo
yatawezesha maandalizi ya Muswada wa Sheria
ambao utazingatia mahitaji ya kisekta. Wizara
inaendelea na mchakato wa kukusanya maoni ya
wadau na kupata kibali cha Serikali cha kutunga Sheria
hiyo ya kutambua, kulinda na kuendeleza ardhi ya
kilimo.
Wizara iliandaa vikao mbalimbali vya wadau ili kupata
maoni na mapendekezo ya kuwezesha kufanya
marekebisho katika Sheria za Bodi za mazao ili
ziendane na mabadiliko ya kisekta. Kupitia vikao hivyo,
Wizara imepata maoni na mapendekezo ya
marekebisho ya Kisheria na inaendelea na kukamilisha
mchakato wa kuandaa rasimu ya marekebisho kwa kila
sheria na kanuni za Bodi za Mazao.
Wizara imekamilisha rasimu za mapendekezo ya
marekebisho ya Sheria ya Usalama wa Chakula (Food
Security Act of 1991) na Sheria ya Hifadhi ya Mimea
(Plant Protection Act 1997).
Kuhusu maandalizi ya kanuni za Sheria za sekta ya
kilimo, Wizara imekamilisha na kupitisha Kanuni za
Sheria ya Mbegu (Seeds Regulations) ambazo zilianza
kufanya kazi mwezi Februari, 2007.
Kwa kuwahusisha wadau, Wizara imeweza kukusanya
maoni na taarifa mbalimbali na kukamilisha rasimu ya
awali ya taarifa ya mchakato wa kutunga Sheria ya
Kulinda Nasaba za Mimea kwa ajili ya Kilimo na
Chakula (Plant Genetic Resource for food and
Agriculture). Sheria itakayotungwa itakuwa na
madhumuni ya kutambua na kulinda nasaba zote za
mimea kwa mujibu wa mkataba wa kimataifa wa
kulinda nasaba za mimea wa mwaka 2001 ambao
Tanzania ni mwanachama.
236
WIZARA YA VIWANDA, BIASHARA NA MASOKO
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuendelea kutekeleza MKUKUTA. Wizara imeendelea kutoa Ruzuku kwa Mashirika na
Taasisi zilizo chini yake kwa lengo la kutekeleza
majukumu mbalimbali ya taasisi hizo yanayolenga
kukuza uchumi na kupunguza umaskini. Hata hivyo,
fedha zinazotolewa ni kidogo kulingana na kiasi
kilichopangwa kwenye mpango wa kazi (Action Plan)
wa Taasisi mbalimbali. Tatizo hili linatokana na
mabadiliko katika makusanyo ya mapato ya Serikali.
2. Ifikapo mwaka 2010 kiwango cha Serikali inaendelea kubuni mikakati itakayosaidia
ukuaji wa sekta ya Viwanda kitafikia kuimarisha sekta ya viwanda hapa nchini ili ukuaji wa
asilimia 15 kwa mwaka. sekta uonekane mwaka hadi mwaka na hatimaye
kufikia kiwango cha uchumi kilichokusudiwa. Takwimu
zinaonyesha kuwa sekta ya viwanda imeendelea kukua
kutoka asilimia 1.6 mwaka 1995 hadi asilimia 9 mwaka
2005. Hata hivyo, kutokana na matatizo ya uhaba wa
umeme yaliyojitokeza mwaka 2006 ambao ni nyenzo ya
msingi katika uzalishaji viwandani na katika kuvutia
wawekezaji wa ndani na nje kuanzisha viwanda vipya
ni dhahiri kwamba ukuaji wa viwanda katika mwaka
2006 umeathirika. Mikakati inayotekelezwa na Serikali
inayolenga kusaidia kuimarisha sekta ya viwanda ni
pamoja na:-
Kutatua matatizo ya upatikanaji umeme ikiwemo
kutafuta vyanzo vingine vya kuzalisha umeme
hapa nchini hususan kuzalisha umeme kwa
kutumia makaa ya mawe.
Kuimarisha Miundombinu inayojumuisha
barabara, reli, mawasiliano n.k ili kurahisisha
usafirishaji wa malighafi zinazohitajika viwandani
na kusambaza bidhaa zinazozalishwa kufikia
walaji.
Kuimarisha sekta ya Kilimo ili kuhakikisha
upatikanaji wa malighafi za kutosha kwa viwanda.
Kuhamasisha na kuhimiza uanzishwaji wa viwanda
vya kusindika mazao ya kilimo, misitu na maliasili.
Kuwawezesha wananchi kukuza kipato chao na
hatimaye waweze kuwa soko kuu la bidha
237
zinazozalishwa na viwanda ili kukuza soko la
ndani.
Kuhakikisha upatikanaji wa mikopo ya muda mrefu
kwa wawekezaji katika viwanda.
Kuweka vivutio (incentive packages) kwa sekta za
viwanda zenye mwelekeo wa kuchangia kwa
kiwango kikubwa katika maendeleo ya viwanda, hii
ikiwa ni pamoja na sekta ya ngozi, nguo, usindikaji
wa matunda na kujenga miundombinu ya EPZ na
kuhamasisha uwekezaji ndani ya EPZ.
Kuhamasisha na kuhimiza uanzishwaji wa viwanda
vidogo kwa kutekeleza Sera ya Viwanda Vidogo na
Biashara ndogo.
Kuvutia wawekezaji kutoka nje kuja kuwekeza
katika sekta ya Viwanda.
Kuhimiza uzalishaji wa vida bora kwa kutoa
mafunzo ya ubora wa vida, ufungashaji wa vida na
utafutaji masoko hususan kwa wazalishaji wadogo
(SMEs).
3. Kuandaa mikakati itakayouwezesha Mikakati hiyo imeandaliwa katika ripoti ya marejeo ya
uchumi wa Taifa kuhimili ushindani na Sera ya Biashara kwa nchi yetu na nchi za Afrika
kulifanya Taifa letu liwe na uwezo Mashariki (Trade Policy Review for Tanzania and EAC)
madhubuti wa kushiriki na kufaidika iliyowasilishwa Makao Makuu ya Shirika la Biashara la
katika mfumo wa biashara kwenye Dunia (WTO) Geneva, Uswisi tarehe 25-27/10/2006.
masoko ya Kitaifa, Kikanda na
Kimataifa katika mazingira ya
utandawazi.
4. Kupanua ajira kwa kuendeleza SIDO imeendelea kutoa huduma zinazolenga kuwapa
ujasiriamali katika viwanda vidogo na wananchi ufahamu wa ujasiriamali, kuwawezesha
biashara ndogo. kutambua mahitaji ya soko, kuwawezesha kupata
teknolojia zifaazo na utoaji wa mikopo pale ambapo
haja ilijitokeza. Huduma katika maeneo yote haya,
yanawawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika
kuanzisha viwanda vidogo na biashara ndogo na hivyo
kujiajiri wenyewe na kutoa ajira kwa watu wengine pia.
5. Kuanzisha viwanda mama, kwa Mchakato wa kupata wawekezaji katika mradi wa
kutafuta wabia wa kuwekeza katika makaa ya mawe Mchuchuma na mradi wa chuma
mradi wa makaa ya mawe ya Liganga unaendelea. Serikali imefikia hatua ya
Mchuchuma, mradi wa chuma wa kubainisha wawekezaji watakaofaa kuendeleza mradi
Liganga na tafiti za miradi mingine wa machimbo ya mkaa na uzalishaji wa umeme.
238
kama vile soda-ash iliyo katika Ukanda Wawekezaji waliojitokeza ni wafuatao;-
wa Maendeleo wa Mtwara. MMI Steel Mills Ltd (Tanzania); Athi River Steel Plant
Ltd (Kenya); BSG Resources (Israel); Sub – Sahara
Resources NL (Australia); ISPAT Mittal ya India; Lugala
Mining Ltd/Pangea Proprietary (Pty) Ltd (Afrika Kusini);
China CAMCE Engineering Company Ltd (China);
SIEMENS/Grinaker LTA/Cinergy Global Power (Africa
Kusini).
6. Kuendelea na utekelezaji wa programu Utafiti wa mashine za mkono (manual) za kukamua
inayolenga katika kuimarisha usindikaji mafuta kutoka aina zote za mbegu umekamillika.
wa mazao ya kilimo, mifugo na Teknolojia ya mashine za kukatakata majani ya kula
maliasili; wanyama imekomaa. Utafiti wa mashine za kusindika
maziwa na bidhaa zake unaendelea. Aidha SIDO
imeendeleza mafunzo kwa wasindikaji wa vyakula
mbali mbali na mpaka sasa mafunzo yamewafikia watu
5,000. Mazungumzo yamefanyika pia kati ya Wizara,
SIDO na Jumuiya ya Madola ili kuendeleza mafunzo ya
usindikaji.
7. Kuendelea kuhamasisha uanzishaji wa Mamlaka ya EPZ (EPZ Authority) imeendelea na zoezi
maeneo ya uzalishaji kwa ajili ya uuzaji la kuhamasisha uwekezaji katika maeneo ya EPZ kwa
nje (EPZ) pamoja na uwekezaji katika kutembelea na kutoa Mada katika nchi za Marekani,
viwanda ndani ya maeneo hayo. Urusi, Japan, China, Korea na Falme za Kiarabu.
Wawekezaji wawili wamepewa leseni za kuzalisha chini
ya EPZ (EPZ Operator‟s License). Wawekezaji hawa ni
Unnat Fruits Processing Ltd na CAMI Apparel Ltd.
Aidha, Kampuni ya Unnat Fruits Processing Ltd ilipewa
vile vile leseni ya ujenzi wa miundombinu ya EPZ (EPZ
Developer‟s License).
8. Kuandaa taarifa kuhusu fursa za Wizara inaendelea kukusanya taarifa za rasilimali
uwekezaji katika miradi ya maendeleo zilizopo katika mikoa mbalimbali zitakazosaidia
ya viwanda (project profiles) na kubainisha fursa za uwekezaji na kuandaa taarifa za
kubainisha fursa za mitaji kwa miradi (project profiles).
wawekezaji.
9. Kuendelea kuvutia na kuhamasisha Kwa kushirikiana na ubalozi wa Tanzania nchini China,
wawekezaji wa nje na wa ndani na Wizara iliandaa ziara ya wawekezaji kutoka taasisi ya
kuwekeza katika sekta mbalimbali za “China Textile Planning Institute of Construction”
viwanda. wakiambatana na Mkurugenzi wa MIZUDA group of
companies, mojawapo ya kampuni kubwa ya
kutengeneza nguo nchini China kwa nia ya
kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya nguo nchini.
Aidha, Wizara ilipokea wawekezaji kutoka kampuni ya
RITES Limited wenye nia ya kuwekeza katika miradi ya
Soda-ash ya Lake Natron, Kampuni kutoka Ukraine
yenye nia ya kuwekeza katika uzalishaji wa nyaya za
239
umeme. Wengine ni kutoka Kuwait wenye nia ya
kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza bidhaa
zitokanazo na petroli.
Wizara imeendelea kutembelea mikoa mbalimbali kwa
lengo la kubainisha fursa za uwekezaji katika sekta ya
Viwanda ikiwemo mikoa ya kusini yenye uzalishaji
mkubwa wa korosho, miradi ya chumvi na gesi asilia.
Mheshimiwa Rais, Waziri wa Viwanda, Biashara na
Masoko na wafanyabiashara wamefanya ziara katika
nchi za Marekani, Japan, Korea, China, UAE n.k kwa
lengo la kushawishi wawekezaji wa nchi hizo kuwekeza
nchini. Wawekezaji hao wameonyesha nia kubwa ya
kuwekeza hapa nchini.
10. Kuendelea kutekeleza mkakati wa Mfuko wa kuendeleza sekta ya ngozi na bidhaa za
kuimarisha sekta ya ngozi na viwanda ngozi ulianzishwa kwa jina la “Livestock Development
vya ngozi; Fund”, ili kupata fedha za kutekeleza mkakati wa
kufufua na kuendeleza sekta ya ngozi na viwanda vya
ngozi. Hadi sasa mfuko huu umekusanya zaidi ya
shilingi bilioni 5. Utekelezaji wa mkakati husika bado
unasuasua kutokana na kutokukamilika kwa taratibu za
kiserikali za kuteua msimamizi wa mfuko ili kupata
ridhaa ya Bunge kuweza kutumia fedha za mfuko huo.
Suala hili linashughulikiwa ili kukamilisha taratibu hizo.
Shughuli nyingine ni kukamilisha GN ya Motisha kwa
wasindikaji wa ngozi ili kuhamasisha usindikaji na
uuzaji nje ngozi zilizosindikwa badala ya ngozi ghafi.
Aidha, wakulima chini ya CAMARTEC, Wakulima 123
wamepewa mafunzo kuhusu matumizi na utengenezaji
wa lijamu za punda na mijeledi ya ng‟ombe.
11. Kuwezesha na kuhamasisha Jitihada mbalimbali zimefanyika katika kufanikisha
uanzishaji wa viwanda vya kusindika uhamasishaji wa usindikaji wa mazao ya kilimo. Katika
mazao ya kilimo, mifugo na maliasili. jitihada za kusindika matunda nchini, kampuni ya Unnat
Fruit Processing Ltd inakamilisha ujenzi wa kiwanda
cha kusindika matunda (machungwa na mananasi)
huko Kingorwila Morogoro chini ya mpango wa EPZ.
Kiwanda hicho kitasindika tani 25,000 za matunda kwa
mwaka na kuuza nje ya nchi tani 2,500 za juisi.
Matunda yatatoka katika vijiji vya Mikuyuni na Matombo
mkoani Morogoro, Muheza mkoani Tanga na Chalinze
mkoani Pwani. Kwa upande wa mazao ya mifugo
Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko ilianzisha
mkakati wa kuendeleza sekta ya ngozi. Aidha mfuko wa
240
kuendeleza sekta ya ngozi umeanzishwa ili kuweka
motisha kwa wasindikaji wa ngozi.
12. Kutekeleza mkakati wa kuhifadhi Wizara kama mojawapo wa wadau wakuu wa kuhifadhi
Mazingira ya Ardhi na Vyanzo vya Maji na kutunza mazingira, hususan katika jukumu la
na kufuatilia utekelezaji wa tamko la kuoanisha uhamasishaji na uendelezaji wa viwanda na
serikali la kupiga marufuku mazingira endelevu (industrial development and
utengenezaji wa mifuko laini ya environmental sustainability), imefanya shughuli
plastiki; zifuatazo:
i. Semina (Mwezi Julai, 2006) kwa baadhi ya wakuu
(Chief Executive Officers) katika sekta ya viwanda
iliyolenga kuwahamasisha kutumia teknolojia bora
(Cleaner Production Technologies), kutoa elimu na
ufafanuzi juu ya utekelezaji wa Sheria mpya ya
mazingira ya mwaka 2004, njia bora za urejerezaji
na utupaji wa maji-taka na taka ngumu zitokanazo
na shughuli za uzalishaji viwandani (Recycling
Techiniques and Disposal).
ii. Mwezi Novemba, 2006 ilifanyika semina ya
kuhamasisha na kutoa elimu kwa viwanda
vinavyotumia kuni kama nishati, kutumia nishati
mbadala kama vile makaa ya mawe, gesi, majiko
sanifu na mabaki ya mimea. Aidha, walihimizwa
kupanda miti kwa ajili ya mahitaji yao.
iii. Mikutano imefanyika ikihusisha viwanda
vinavyotengeneza bidhaa na mifuko ya plastiki kwa
lengo la kuwahamasisha kutumia technolojia ya
kisasa zaidi ambayo itasaidia kuzalisha
bidhaa/mifuko inayooza (bio-degradable bags).
iv. Kutembelea viwanda kila mara malalamiko ya
uchafuzi wa mazingira unaotokana na shughuli za
viwanda yanapojitokeza na kuwahamasisha
watendaji wakuu kuchukua hatua za haraka dhidi
ya uchafuzi huo pale unapodhihirika.
v. Wajasiriamali mafundi mchundo 23
wamefundishwa jinsi ya kutengeneza, kutumia na
kubiasharisha teknolojia za kilimo cha hifadhi ardhi
na maji kutoka Singida vijijini, Iramba (Singida),
Babati, Mbulu, Hanang na Simanjiro (Manyara),
Karatu, Ngorongoro, Arumeru (Arusha) na Maswa
(Shinyanga).
241
13. Kuweka utaratibu wa kudumu wa Rasimu ya utaratibu wa kusimamia biashara ya chuma
upatikanaji wa biashara ya chuma chakavu imeandaliwa na kuwasilishwa katika kikao cha
chakavu; wadau tarehe 5/7/2006. Maoni ya wadau yameingizwa
kuboresha rasimu ya utaratibu husika. Kikao kingine
cha wadau kitaitishwa kupata muafaka juu ya utaratibu
huo kabla ya kuwasilishwa Serikalini kwa uamuzi.
14. Kuimarisha taasisi za utafiti na Taasisi husika zinaendelea kuimarishwa kwa kupatiwa
maendeleo ya viwanda hususan, fedha za kuendeshea shughuli zake kutoka katika bajeti
CAMARTEC, TEMDO, TIRDO; ya MKUKUTA. Mapato mengine hutokana na huduma
za utafiti na ushauri wa kitaalam zitolewazo katika
taasisi hizo.
15. Kushirikiana na Sekta Binafsi katika Katika kuendeleza ushirikiano katika utatuzi wa
kubuni mikakati ya kuendeleza sekta matatizo ya sekta ya viwanda nchini, Wizara imefanya
ya viwanda kwa lengo la kukuza vikao vilivyohusisha wadau wa sekta kujadili biashara
mchango wa sekta hiyo katika ya chuma chakavu, mkakati wa sekta ya ngozi, mkakati
maendeleo ya uchumi wa Taifa wa mazingira na kuandaa kongamano lililofanyika siku
ya viwanda Afrika tarehe 20 Novemba, 2006 kujadili
mafanikio na matatizo ya sekta ya viwanda.
16. Kuendelea kushirikiana na Wizara na Serikali inaendelea kuhamasisha taasisi za kifedha
Taasisi nyingine pamoja na Sekta kusaidia kwa kutoa mikopo ya muda wa kati na mrefu
Binafsi katika kubainisha na kutafuta kwa wawekezaji. Pia Wizara kwa kushirikiana na taasisi
ufumbuzi wa matatizo mbalimbali ikiwa zingine inajiandaa kutoa mapendekezo ya kuanzishwa
ni pamoja na matatizo ya upatikanaji kwa Benki ya Uwekezaji itakayolenga kutoa mikopo
wa mikopo ya muda mrefu kwa kwa wawekezaji hususan wanaoanzisha viwanda
wawekezaji kwani suala hili limekuwa likiungwa mkono na wadau
wengi.
17. Kuhamasisha wawekezaji kuwekeza Baadhi ya viwanda vimehamasishwa na kukubali
katika teknolojia mpya za kisasa ili kuwekeza katika teknolojia inayoviwezesha kutumia
kuzalisha bidhaa bora zinazoweza gesi asilia. Aidha, juhudi za kuhamasisha uwekezaji
kuhimili ushindani. kuwekeza katika teknolojia ya uzalishaji wa umeme
kwa kutumia makaa ya mawe ya Mchuchuma
zinaendelea. Teknolojia nyingine ni pamoja na Chuma
cha Liganga ili kuzalisha vipuri na bidhaa za chuma
kwa matumizi ya viwandani, uzalishaji wa mbolea kwa
kutumia gesi na madini ya Phosphate, soda-ash kwa
ajili ya kuzalisha Caustic soda na nyingine kwa ajili ya
kuongeza thamani kwenye mazao ya kilimo, madini na
maliasili.
18. Kuendelea na juhudi za kuimarisha EAC
ushirikiano wa kiuchumi na nchi Kenya, Uganda na Tanzania tayari zimeanza
nyingine za ki-Afrika kupitia EAC na kutekeleza mpango wa ushirikiano wa umoja wa ushuru
SADC ili kufungua masoko ya bidhaa wa forodha. Tayari nchi wanachama zinafaidika katika
za Tanzania katika nchi hizo. mpango huu ambao ulianza tangu tarehe 1 Januari,
2005. Tanzania imeshafunguliwa masoko ya bidhaa
zake zote kwa nchi za Kenya na Uganda. Wakati
242
Tanzania imefungua masoko yake kwa bidhaa zote
zinazotoka Uganda na baadhi ya bidhaa za kutoka
Kenya. Ifikapo mwaka 2010, Tanzania itakuwa
imefungua masoko kwa bidhaa zote kutoka Kenya pia.
SADC
Katika harakati za kufungua milango ya masoko,
Tanzania imejitahidi kupunguza viwango mbalimbali
vya ushuru ili kwenda sanjari na mpango wa SADC wa
kufikia soko huru huria mwaka 2008. Katika harakati
hizo takwimu zinaonyesha kuwa ifikapo 2008, Tanzania
tutakuwa tumepunguza kiasi cha asilimia 83 kulingana
na asilimia 85 ambayo ilikubaliwa na nchi wanachama,
kwamba ifikapo 2008 kila nchi mwanachama wa SADC
awe amepunguza ushuru kwa kiasi cha asilimia 85 kwa
bidhaa nyingi ili kuweza kufungua milango kwa masoko
ya nchi wanachama. Asilimia 15 iwe kwa “sensitive
products” ambazo ndizo kitovu cha uchumi kwa nchi
mbalimbali.
19. Kuandaa mikakati itakayouwezesha Wizara imeshiriki katika mikakati ya biashara ya nje
uchumi wa Taifa kuhimili ushindani na kwa kuandaa mapitio ya sera ya Biashara ambayo
kuweza kushiriki kikamilifu na kufaidika ilifayika Geneva Septemba, 2006.
na mfumo wa biashara katika Wizara imekuza na kuendeleza ushirikiano wa
mazingira ya utandawazi kama kibiashara na nchi mbalimbali za Mashariki ya Mbali na
ilivyoelekezwa kwenye Ilani ya Mashariki ya Kati ambazo zimeonyesha nia ya kufanya
Uchaguzi. biashara ya kununua bidhaa zetu.
20. Kituo cha Biashara cha Tanzania Kituo cha Biashara London kinaratibu safari za
kilichopo London kitaendelea wafanyabiashara kutoka Tanzania wanaokwenda Bara
kushirikiana na Makampuni Binafsi, la Ulaya kutafuta masoko ya bidhaa zinazotengenezwa
Mashirika na Mamlaka mbalimbali ili nchini. Pia huandaa semina mbalimbali pamoja na
kuongeza ufanisi wa mauzo ya bidhaa makongamano kuhusu ukuzaji wa biashara kati ya nchi
na mazao ya asili kwa lengo la hizo na Tanzania. Kutokana na jitihada hizo kumekuwa
kuliongezea Taifa mapato ya fedha za na ongezeko la mauzo ya bidhaa zinazouzwa Ulaya
kigeni na kuendeleza mkakati wa kama vile chai, kahawa, madini, viungo, sukari, bidhaa
kuitangaza Tanzania kiutalii katika zinazozalishwa na tumbaku, nguo, samaki na pamba.
vyombo vya habari nchini Uingereza. Kila mwaka wakati wa maonyesho huja Tanzania
kushiriki maonyesho na kuchukua sampuli za bidhaa
kwa ajili ya kuziingiza kwenye mtandao ili kuzitangaza
katika soko la nje.
21. BET kuboresha Maonesho ya Biashara Kwa kushirikiana na BET, Wizara itatenga maeneo
ya Kimataifa ya Dar es Salaam maalum kwa ajili ya washiriki wanaotaka kuonjesha
ambayo sasa yanatambulika na bidhaa zao kwa walaji watarajiwa (test sales) na wale
Chama Kinachosimamia Maonesho wanaotaka kuonyesha tu bidhaa zao. BET itaendelea
Duniani (Union des Foires kuboresha huduma katika uwanja wa Maonyesho wa
Internationale - UFI) Mwalimu Nyerere, hasa upatikanaji wa maji, umeme,
243
mawasiliano na huduma za mtandao. Kadhalika
itaendelea kuchukua hatua za kuboresha huduma za
usafi na mandhari ya uwanja kwa ujumla ikiwa ni
pamoja na kupanda miti.
Ili kuboresha usimamizi wa shughuli za Maonyesho
BET itashirikisha sekta binafsi katika Kamati za
Kupanga, Kuratibu na Kusimamia maonyesho.
Katika kuchangia ukuzaji wa mauzo nje ya nchi, BET
iliendelea kuandaa na kushiriki katika maonyesho ya
Biashara ya Kitaifa na Kimataifa. Mwaka 2006/2007
BET ilishiriki maonyesho ya Biashara ya Kimataifa
katika nchi za Kenya, Rwanda, Zimbabwe, Malawi,
China, Dubai na Marekani (New York). Kadhalika BET
iliandaa maonyesho ya kitaifa (Dar es Salaam
International Trade Fair) na yale ya Uhuru Shopping
Festival.
22. Bodi ya Biashara ya Nje itaendelea BET iliendesha mafunzo katika nyanja zilizotajwa katika
kutoa mafunzo kwa wajasiriamali maeneo yafuatayo na idadi katika mabano. Morogoro
wapatao 100, kuhusu ubora wa (124) kwa wafanyabiashara wa kawaida, Wilaya ya
bidhaa, utaalamu wa kuuza nje kwa Mvomero na Morogoro Vijijini (92) kwa Wakulima wa
ujumla na jinsi ya kuzitumia fursa za Iliki, Mdalasini na Pili pili manga. Mkoa wa mwanza
upendeleo zinazopatikana katika (116), Mkoa wa Arusha (130), Mkoa wa Kigoma kwa
masoko kadhaa. Wavuvi wa Samaki (97), Mkoa wa Mbeya (121), Mkoa
wa Rukwa (143), Mkoa wa Singida (70), Wilaya ya
Bagamoyo kwa Wazalishaji wa Vikundi (130). Hii ni
mbali na mafunzo yanayoendeshwa na BET kwa
kushirikiana na Taasisi za nje ambapo silabasi ya
mafunzo hayo inagusia pia vipengele vilivyopo katika
mada hii. Na kazi hiyo bado inaendelea.
23. Kuendeleza kampeni ya “NUNUA Kampeni hii iliendelezwa kwa kushirikiana na Chama
BIDHAA ZA TANZANIA JENGA cha Wenye Viwanda (Confederation of Tanzania
TANZANIA”. BET kuendelea kufikisha Industries – CTI) hasa katika Maonesho ya Biashara ya
huduma za kutoa habari za biashara Dar es Salaam yaliyofanyika Julai, 2006. Pamoja na
kupitia “Tele-Centres” katika Mikoa ya wito katika Semina zilizofanyika, pia kulikuwepo na
Morogoro na Mbeya. vipeperushi (banners) katika eneo lote la viwanja vya
maonyesho.
Kuhusu “Tele Centres” katika Mikoa ya Morogoro na
Mbeya, jitihada zinafanyika kupata majengo ya kudumu
yatakayotumika kwa shughuli hiyo.
24. BET itaimarisha na kuongeza BET imeimarisha ofisi ya Zanzibar kwa kuipa vitendea
wafanyakazi na vitendea kazi kwa kazi kama vile Kompyuta, printa, „scanner‟, viyoyozi,
upande wa Zanzibari. meza, viti, vitabu na Majarida. Pia jitihada zinafanyika
244
kutafuta ofisi yake ya kudumu ili iweze kuajiri rasmi.
Kwa hivi sasa, BET inatumia ofisi za kuazima zilizoko
katika ofisi ya jengo la Wizara ya Viwanda, Biashara na
Masoko na Utalii.
25. Kuiunda upya BET kuwa Mamlaka ya Mchakato wa kuunda upya BET kuwa Mamlaka ya
Maendeleo ya Biashara (Tanzania Maendeleo ya Biashara (Tanzania Trade Development
Trade Development Authority) yenye Authority), umeanza kwa kuwashirikisha wadau
jukumu la kuendeleza biashara na mbalimbali katika kujadili rasimu ya mapendekezo ya
wafanyabiashara. uundaji mamlaka hiyo. Mapendekezo yanajadiliwa
katika ngazi mbalimbali wakiwemo wafanyakazi wa
BET, Bodi ya Wakurugenzi na Wizara. Waraka wa
Baraza la Mawaziri kuhusu mabadiliko haya
umeandaliwa.
26. Kuendelea kutekeleza Sera ya Taifa ya Lengo kuu la Sera ya Taifa ya Biashara (2003) ni
Biashara. kuiwezesha Tanzania kubaini njia na mbinu za
kuelekea katika uchumi imara unaotegemea biashara
ya kimataifa kuondoa umaskini. Sera inatoa fursa kwa
Serikali kubuni mikakati ya kutekeleza azma hii kwa
kuzingatia maslahi ya Kitaifa na makubaliano yetu ya
Kimataifa. Moja ya mbinu zinazotumika ni kushirikiana
na Wizara pamoja na Washirika wetu wa Maendeleo
wa nje (Development Partners) kujenga uwezo wa
kitaifa wa kushiriki katika majadiliano ya biashara ya
kimataifa kwa kutoa mafunzo kwa wadau mbalimbali
wakiwemo watumishi wa Serikali, Taasisi pamoja na
Asasi zisizokuwa za kiserikali kwa njia ya semina,
warsha na mafunzo ya muda mrefu vyuo vikuu. Kwa
mara ya kwanza mwezi wa Oktoba, 2006 Nchi za Afrika
ya Mashariki ziliwasilisha kwa pamoja Sera zao za
biashara kwenye Shirika la Kimataifa kwa ajili ya
mapitio (Trade Policy Review) kama masharti ya
uanachama wetu katika shirika hilo yanavyohitaji.
Wizara inaendelea kuratibu utekelezaji wa mikakati na
programu mbalimbali zinazolenga kukuza biashara
kama vile Mpango Shirikishi wa Kukuza Biashara
(Intergrated Framework - IF) uliobuniwa na WTO na
kufadhiliwa na wafadhili mbalimbali, Mkakati wa
Kuboresha Mazingira ya Biashara Tanzania (Business
Environment Strategy for Tanzania – BEST) pamoja na
utekelezaji wa mapendekezo ya Uchambuzi wa
Mchango wa Sekta ya Kiuchumi katika Kukuza Mauzo
Nje (Diagnostic Intergrated Framework – DTIS).
27. Kuainisha na kuandaa mkakati wa Wizara imeboresha mahusiano kati ya Balozi zetu
utekelezaji wa fursa zitokanazo na Geneva na makao makuu ya Wizara, hii imerahisisha
makubaliano ya WTO; Wizara kupokea na kutoa taarifa mbalimbali
245
zinazohusu WTO. Aidha, wataalam wawili wa Biashara
wameongezwa katika Ubalozi wa Tanzania huko
Geneva.
28. Kuimarisha Mamlaka ya EPZ pamoja Zoezi la kuajiri watumishi wa Mamlaka ya EPZ
na BET ili kuongeza juhudi za linaendelea. Kufuatana na ufinyu wa Bajeti, zoezi la
kuongeza mauzo ya nje; kuimarisha Mamlaka ya EPZ kifedha bado
halijafanikiwa.
29. Kuendelea kufanya mashauriano na Rasimu ya waraka wa BLM imeshawasilishwa
wadau kuhusu programu ya kuainisha Serikalini. Baada ya kukubalika na Serikali wadau
matatizo yanayokwamisha biashara watafanya mashauriano juu ya utekelezaji wake kabla
(Diagnostic Trade Integration Study - ya utekelezaji halisi.
DTIS);
30. Kwa kushirikiana na DANIDA kufadhili Watumishi 26 walifadhiliwa na DANIDA kuchukua
watumishi 26 wa Wizara, Idara za mafunzo ya Shahada ya Uzamili ya Biashara ya
Serikali, Sekta Binafsi na Asasi Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
nyingine kuchukua mafunzo ya Walianza mafunzo Agosti, 2006.
Shahada ya Uzamili ya Biashara ya
Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam.
31. Kuendeleza shughuli za vituo vya Wizara imekuwa ikishirikiana na vituo hivyo kwa
kupokelea na kutolea taarifa kuwapatia watumishi mafunzo ya kitaalam kila nafasi
mbalimbali zilizoanzishwa na mpango inapopatikana hapa nchini na nje ya nchi. Hadi sasa
wa pamoja (UNCTAD/WTO/ITC) wa watumishi 15 wameshanufaika na mpango huo.
kujenga uwezo wa kitaalamu katika
muasuala ya biashara.
32. Kuendelea na majadiliano ya EPAs Tanzania inaendelea na majadiliano ya EPA ikiwa
baina ya nchi zinazoendelea na katika kundi la SADC – EPA. Kundi hili linajumuisha
Jumuiya ya Ulaya; nchi za Botswana, Namibia, Lesotho, Swaziland,
Angola na Msumbiji.
Majadiliano kati ya SADC –EPA na EU hayajapiga
hatua kubwa, pamoja na kwamba majadiliano hayo
yalitakiwa yawe yamekamilika Juni, 2007 na kutoka
Julai-Desemba, 2007 ni wakati wa kutiliana saini
makubaliano yaliyoafikiwa.
33. Kuendelea kuboresha mazingira ya Sheria ya Usajili wa Shughuli za Biashara ilipitishwa na
biashara nchini ikiwa ni pamoja na Bunge mwezi Februari, 2007. Sheria hii inalenga katika
kukamilisha utaratibu wa uandikishaji kupunguza gharama za kufanya biashara kwa
wa biashara badala ya utaratibu wa kuanzisha mfumo rahisi wa kusajili shughuli za
utoaji wa leseni. biashara na kuondokana na mfumo wa zamani wa
kutumia leseni kama vyanzo vya mapato. Sheria hii
itawezesha wafanyabiashara walio katika sekta isiyo
rasmi kuingia kwenye sekta iliyo rasmi. Maandalizi ya
Kanuni za kutekeleza Sheria hii yameanza.
246
34. Kuendeleza mkakati wa kurasimisha Kanuni za kutekeleza Sheria ya Usajili wa Shughuli za
biashara; Biashara zinaandaliwa. Mkakati wa kurasimisha
biashara utaendelezwa baada ya kukamilika kwa
Kanuni hizo ikiwa ni pamoja na kuunganisha ofisi za
usajili wa leseni mikoani katika mtandao wa kompyuta.
35. Kamati ya Kitaifa ya kusimamia Awali Kamati kwa kushirikiana na baadhi ya wadau
utekelezaji wa mpango wa AGOA imeandaa rasimu ya “AGOA National Strategy Paper”
itaimarishwa kwa madhumuni ya kutoa ambayo baadaye itahusisha wadau wote na kuijadili ili
ushauri katika masuala ya utekelezaji iwe dira ya utekelezaji wa mpango mzima wa AGOA.
na uenezaji wa taarifa za masoko kwa
Sekta Binafsi ili waweze kuuza zaidi
kupitia mpango wa AGOA;
36. Kuendelea na jitihada za kuwezesha Wakulima, wasindikaji na wafanyabiashara
mazao ya wakulima kuuzwa kwa bei wamewezeshwa kushiriki katika maonesho mbalimbali
ya kuridhisha kulingana na mahitaji ya kama yale ya Nane Nane na Siku ya Viwanda Afrika ili
ubora wa soko la ndani na nje. kujifunza aina ya ubora, usindikaji na ufungashaji
unaotakiwa ili kuwawezesha kuuza bidhaa zao katika
masoko ya uhakika na hivyo kujipatia bei nzuri za
mazao yao.
Taarifa za bei ya mazao makuu ya chakula ilikusanywa
na kusambazwa kwa wadau mara tatu kila wiki.
Kanuni za kutekeleza Utaratibu wa Stakabadhi za
Mazao zilikamilishwa. Utaratibu wa Stakabadhi za
Mazao utawawezesha wakulima kuweka mazao yao
katika maghala na kuyauza wanapopata bei nzuri.
37. Kuendeleza usindikaji wa mazao Semina, Warsha na mikutano mbalimbali imefanyika
yanayozalishwa hapa nchini ili kwa lengo la Kuhamasisha na kuelimisha wakulima juu
kuongeza thamani na nafasi za ajira. ya umuhimu wa kusindika mazao yao ili kuongeza
muda wa kutumika kwa mazao yenyewe, kuimarisha
uzalishaji na kuongeza ajira. Aidha kwa kupitia
Programu ya ACCESS inayofadhiliwa na Canada,
SIDO ilishirikiana na TBS, BET na Wizara ya Kilimo
kuelimisha wadau kuhusu mbinu za kuweza kuyafikia
masoko ya nje.
38. Kuhakikisha upatikanaji wa masoko Wafanyabiashara wanaosafirisha bidhaa mbalimbali nje
kwa bidhaa zisizokuwa za kilimo. ya nchi walipewa leseni za kusafirisha bidhaa hizo
kwa wakati, baadhi ya bidhaa hizo ni pamoja na mifugo,
mazao ya biashara kama korosho, maua, kahawa n.k.
Muswada wa kurahisisha na kuboresha shughuli za
usajili wa shughuli za biashara umeshapitishwa kwenye
BLM kinachosubiriwa ni taratibu za kuupeleka Bungeni
na hatimaye kupitishwa na kuwa Sheria.
247
39. Kukamilisha Sera na Mkakati wa Sera ya Masoko ya Mazao ya Kilimo imekamilishwa.
Masoko ya Mazao ya Kilimo nchini. Waraka wa Baraza la Mawaziri umeandaliwa na
kuwasilishwa. Mkakati wa utekelezaji wa sera hiyo
utaandaliwa baada ya Sera hiyo kupitishwa na Baraza
la Mawaziri.
40. Kuimarisha na kuendeleza mfumo wa Mafunzo kwa wakusanyaji wa taarifa za masoko ya
ukusanyaji, uchambuzi na usambazaji mazao yameandaliwa na yamefanyika mwezi
wa taarifa za masoko. Desemba, 2006. Taratibu za kukusanya, kuchambua
na kusambaza taarifa za masoko kutoka katika Ofisi za
Dar es Salaam zinakamilishwa kwa kuimarisha
vitendea kazi.
Mtandao wa “Internet” umewekwa na baadhi ya wadau
usambaziwa taarifa hizo kwa njia ya “Internet”.
Takwimu za bei zimeingizwa katika Programu maalumu
ya kutunzia taarifa za masoko ya Mazao (FAO
AgriMarket).
41. Kuwezesha mchakato wa ujenzi wa Taratibu (Hadidu za Rejea) za kuwezesha ujenzi wa
masoko ya kimataifa ya mazao ya masoko ya kimataifa zimeandaliwa. Mshauri mwelekezi
kilimo na bidhaa zake pamoja na kwa ajili ya kufanya uchambuzi yakinifu atateuliwa
kufanya tathmini ya uboreshaji wa baada ya fedha kupatikana.
miundombinu ya masoko;
42. Kufanya tathmini ya uboreshaji wa Kazi ya kuendeleza miundombinu ya masoko
miundombinu ya masoko inaendelea kutekelezwa chini ya Programu ya
Kuendeleza Mifumo ya Masoko ya Mazao (AMSDP) na
Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo (ASDP).
Aidha, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tanzania Social
Action Fund – TASAF) unajihusisha na uendelezaji wa
miundombinu.
Jumla ya wilaya 20 zimeshiriki katika uendelezaji wa
miundombinu ya masoko chini ya AMSDP na mchakato
wa kuendeleza masoko katika miji ya Makambako na
Segera unaendelea chini ya ASDP. Katika kipindi cha
2007/08, Wizara itafanya tathmini ya miundombinu
iliyoendelezwa na inayoendelea kutekelezwa.
43. Kukamilisha Kitabu cha Orodha ya Kitabu hiki kwa sasa kipo katika hatua za mwisho
Wanunuzi na Wasindikaji wa mazao; baada ya kufanyika kwa warsha ya wadau wa mazao
ya kilimo ambao walichangia maoni mbalimbali ya
kukiboresha zaidi. Hatua itakayofuata ni kukisambaza
kwa wadau hao.
44. Kuelimisha wadau kuhusu maendeleo Kamati ya kitaifa yenye wadau mbalimbali toka
ya masoko ya mazao na bidhaa ndani Serikalini, Sekta Binafsi, Taasisi za Elimu na Utafiti na
ya nchi na katika Jumuiya za Taasisi zisizo za kiserikali zimehusishwa katika
Ushirikiano wa Kibiashara (EAC, majadiliano ya kutafuta masoko nafuu. Ushiriki wa
248
SADC, EU) na nchi nyingine. Wizara kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa na
Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma (Public
Service Week) pia vimetoa fursa kwa wadau mbalimbali
hususan wafanyabiashara na wananchi kujua fursa hizi
za masoko. Vilevile, Wizara inachapisha vipeperushi
vinavyotoa taarifa za fursa hizo za masoko. Mbali na
fursa hizo, Wizara ina mipango ya kufanya Semina za
Kikanda, kutumia vyombo vya habari ikiwa ni pamoja
na televisheni, radio, magazeti na tovuti kwa
kushirikiana na Kitengo cha Habari Wizarani.
45. Kuimarisha uwezo wa Halmashauri na Mafunzo kwa wakusanyaji wa taarifa za masoko ya
Manispaa kukusanya na kusambaza mazao yameandaliwa na kufanyika mwanzoni mwa
taarifa za masoko. mwezi Desemba, 2006.
46. Kuratibu na kusimamia Programu ya Programu ya Kuendeleza Mifumo ya Masoko ya Mazao
Kuendeleza Mifumo ya Masoko ya ya Kilimo iliendelea kutekeleza majukumu yake kama
Mazao ya Kilimo kwa kushirikiana na ilivyopangwa. Majukumu hayo ni pamoja na kuwezesha
Ofisi ya Waziri Mkuu na wadau ukamilishaji wa Sera ya Masoko ya Mazao ya Kilimo,
wengine; kuwaunganisha wazalishaji, wasindikaji na
wafanyabiashara na masoko (market linkages),
kuwaunganisha wazalishaji, wasindikaji na
wafanyabiashara na vyanzo vya fedha (financial
support services) na uimarishaji wa miundombinu ya
masoko ya mazao.
47. Kuendelea kutekeleza Mradi wa Kanuni za Matumizi ya Mfumo wa Stakabadhi za
Kuendeleza na Kuboresha Biashara ya Mazao zimekamilishwa. Jitihada zinazoendelea kwa
Pamba na Kahawa hususan sasa ni mikakati ya kuelimisha umma juu ya taratibu,
utekelezaji wa Mfumo wa Stakabadhi. kanuni na sheria za mfumo huu ambao kwa kiasi
kikubwa utachangia katika kuwapatia bei nzuri
wazalishaji.
48. Kuendeleza soko la ndani kwa kukuza Semina, warsha na mikutano imefanyika yenye lengo la
matumizi ya mazao na bidhaa mbali kuhamasisha na kuelimisha wazalishaji, wasindikaji
mbali zinazozalishwa nchini. kuhusu kuboresha bidhaa zao ili kujipatia soko la
uhakika ndani ya nchi. Aidha, Kamati kwa ajili ya
kuhamasisha matumizi ya bidhaa zinazozalishwa nchini
imeundwa.
49. Kuhamasisha uanzishaji na uimarishaji Wizara kwa kushirikiana na IFAD imeandaa mradi wa
wa viwanda vidogo na biashara ndogo. Uendelezaji wa Viwanda vidogo na Biashara Ndogo
Vijijini.
Mradi wa MUVI {Muunganisho wa Ujasiriamali Vijijini
(Rural SMEs Support Programme)} ambao
unasimamiwa na IFAD upo katika hatua za mwisho za
maandalizi na unategemea kuanza katika kipindi cha
mwaka 2007/2008. Lengo la mradi huu ni kuimarisha
ujasiriamali vijijini. Mradi utajihusisha katika usindikaji
249
wa mazao ya kilimo na unatarajia kutekelezwa katika
mikoa ya Ruvuma, Manyara, Iringa, Mwanza, Pwani na
Tanga.
50. Kuendelea kuimarisha utoaji wa Mradi wa “Gender Mainstreaming” umeendelea kujenga
huduma zinazolenga kuchochea uwezo wa asasi na kutoa mafunzo juu ya upatikanaji
uanzishaji na uimarishaji wa viwanda wa masoko na kutoa mafunzo kwa wajasiriamali na
vidogo na biashara ndogo. kwa wakufunzi. Hadi kufikia Mei, 2007 programu hii
ilikuwa imewafikia wajasiriamali 1,195.
Wizara kwa kushirikiana na Shirika la Kazi Duniani
(ILO) na Serikali ya Irish iliandaa Maadhimisho ya
Mwanamke Mjasiriamali Tanzania mwezi Novemba,
2006 kwa lengo la kuwawezesha wanawake wasio na
wenye ulemavu na wale wanaoishi na VVU kushiriki
katika shughuli za ujasiriamali. Katika mwezi huo wa
Novemba, 2006 zilifanyika warsha katika mikoa ya
Pwani, Dar es Salaam, Morogoro, Mbeya na Tanga
ambapo kila warsha ilikuwa na washiriki wasiopungua
50.
Mfuko wa kujenga Ushindani (SCF) umekuwa
ukichangia katika uboreshaji wa bidhaa na huduma na
kuwezesha biashara kufikia kiwango cha kimataifa na
kuuza nje. Mfuko huu unalenga usindikaji wa vyakula
na mazao ya kilimo, uchimbaji madini mdogo,
uboreshaji wa ufungashaji wa bidhaa na kushiriki katika
maonesho ya biashara kwa manufaa. Hadi kufikia Mei,
2007 vikundi 250 vilikuwa vimewasilisha maombi yake
na kati ya hivyo, vikundi 42 vilikuwa vimesaidiwa kwa
mfumo wa „matching grant‟.
51. Kujenga uwezo wa wajasiriamali Uhamasishaji wa wanaviwanda wadogo kushiriki katika
kuzalisha kwa tija kwa kutafuta na kuzalisha na kuuza mashine na vifaa vitokanavyo na
kusambaza teknolojia teknolojia zilizobuniwa na kutengenezwa na taasisi za
zilizotengenezwa na kujaribiwa na utafiti za hapa nchini umeedelea vizuri. Mashine na
taasisi mbalimbali za hapa nchini. zana katika maeneo yafuatayo sasa zinazalishwa na
kusambazwa kwa wahitaji katika sehemu mbalimbali za
nchi kupitia juhudi hizi; ubanguaji wa korosho, usindikaji
wa mihogo, ukamuaji wa mafuta ya mawese, uhifadhi
wa malimbichi kwa kutumia matenki ya barafu,
uoteshaji uyoga, usindikaji wa chumvi, uvunaji wa maji
ya mvua na kupura mtama. Bidhaa hizi zimewezekana
kutengenezwa kwa ushirikiano mkubwa wa taasisi za
TIRDO, TEMDO, CAMARTEC na TATC (Nyumbu).
Aidha ulianzishwa mpango wa kulea wabunifu kwa njia
ya viatamizi au „incubators‟. Kwa sasa programu hii
250
inaendelezwa na SIDO, Chuo Kikuu cha Dar-es-
Salaam na pia mashirika ya TIRDO, TEMDO na
CAMARTEC.
52. Kuwawezesha wajasiriamali kuanzisha Wananchi wamehamasishwa na kupewa mafunzo ya
miradi ya usindikaji wa vyakula na usindikaji wa vyakula, mikopo ya zana na mitaji kwa
kutoa huduma za ushauri wa kiufundi. miradi ya wasindikaji. Mafunzo yanayolenga
kuainishwa viwango vya ubora wa bidhaa pamoja na
vifungashio yameendeshwa kwa kushirikiana na Shirika
la Viwango nchini (TBS) ili kuhakikisha kuwa uzalishaji
unafanywa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa
na hivyo kukidhi mahitaji ya soko.
53. Kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa, Uhamasishaji ulifanywa vya kutosha, Halmashauri za
SIDO kutafuta maeneo na kuratibu Wilaya ziliitikia vizuri, jumla ya maeneo 192
ujenzi wa miundombinu na majengo yaliainishwa na kutengwa kwa ajili ya matumizi ya
kwa matumizi ya wajasiriamali wazalishaji na wafanyabiashara wadogo. Mahitaji ya
wadogo. raslimali kwa maana ya fedha ni makubwa, utekelezaji
hadi sasa umefanywa kwa Serikali kuchangia ujenzi wa
soko la Songea mjini, Masoko ya Mchikichini (Ilala),
Kawe (Kinondoni) na Rangitatu (Temeke) ambayo
ujenzi wake umekamilika na sasa yanatumika.
54. Kuhamasisha zaidi huduma Jumla ya wahunzi 150 wamewezeshwa kupata
zitakazoweka msisitizo katika kusaidia mafunzo ya kuongeza ujuzi wao na kushiriki katika
maendeleo ya shughuli za uzalishaji na maonesho ya Kanda ya Ziwa mjini Kahama, nane nane
biashara vijijini hasa kujenga na mjini Arusha na Kanda ya Mashariki mjini Morogoro.
kuimarisha uwezo wa wahunzi na
makundi mengine. CAMARTEC imetoa mafunzo kwa wajasiriamali
mafundi katika utengenezaji na utunzaji wa zana za
kilimo kutoka Wilaya za Singida vijijini, Iramba
(Singida), Babati, Mbulu, Hanang na Simanjiro
(Manyara), Karatu, Ngorongoro, Arumeru (Arusha) na
Maswa (Shinyanga).
55. Kuendelea kutoa huduma za kiatamizi Huduma za kiatamizi tayari zinatolewa Mkoa wa Dar es
pamoja na huduma kwa wachimbaji salaam, tayari wajasiriamali 12 wamekwishafaidika, kati
wadogo wa madini katika maeneo ya hao wanane (8) bado wapo katika hatua mbali mbali
mbalimbali ya nchi za utengenezaji wa vida mpya, watatu (3) bidhaa zao
ziko tayari kuzalishwa kibiashara na mmoja (1)
amekwishafuzu na kuanzisha mradi wake kwa
mafaniko nje ya mpango wa kiatamizi. Mitambo na
bidhaa zinazohusika ni pamoja na: „Popcorn making
machine, Food warmer, Fruit/Honey yogurt, Test tubes,
Biogas incubator, Bamboo products‟ na vida mbalimbali
kutokana na Mihogo (Keki, „Donuts‟ n.k). Utoaji wa
huduma kama hii utaanza kutolewa mkoani Mbeya na
Mwanza katika mwaka wa fedha wa 2007/08. Aidha,
maandalizi ya majengo kwenye mitaa ya viwanda
251
vidogo inayomilikiwa na SIDO kwa ajili ya uanzishaji wa
huduma ya kiatamizi yanaendelea.
56. Kuhamasisha uzalishaji wa bidhaa za Kutokana na Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Ngozi
ngozi kwa kutoa mafunzo na huduma na Viwanda vya Ngozi, mpango wa kazi (Action Plan)
kwa wazalishaji. umeandaliwa na utahusisha vituo vya mafunzo kwa
vijana wa DSM na Morogoro (Leather Training Centres)
kupatiwa ujuzi wa kutengeneza bidhaa za ngozi ili
kujiajiri kwa kuanzisha viwanda vidogo.
Aidha, Mfuko wa Maendeleo ya Mifugo (Livestock
Development Fund) kwa sasa una takriban shilingi
bilioni 4. Pamoja na shughuli zingine, Mfuko huu
utaanza kutumika mwaka wa fedha 2007/2008.
57. Kuendesha kozi za ujasiriamali na Mafunzo ya aina mbalimbali yamekuwa yakitolewa ama
uongozi wa biashara na kutoa mafunzo kutoa ufahamu na ujuzi wa namna nzuri ya kuzalisha
kwa wasindikaji wa vyakula na na kufanya biashara au kutoa ujuzi maalumu wa
matunda. kuwawezesha wajasiriamali kuongeza thamani za
bidhaa zao. Hadi sasa wajasiriamali wapatao 5,000
wamenufaika na programu hii.
58. SIDO kutumia mbinu ya kuwaendeleza Maandalizi ya zoezi la kuwahamasisha na
wazalishaji wadogo kwa kuwatumia kuwashawishi wazalishaji na wafanyabiashara wazoefu
wazalishaji na wafanyabiashara kushiriki katika utaratibu huu bado linaendelea.
waliofanikiwa (mentorship program). Utekelezaji halisi utaanza baada ya kuwapata na
kuweka utaratibu mzuri wa kuwaunganisha.
59. Kuendelea kuilea mifuko ya mitaji Mfuko wa kuwaendeleza wafanyabishara wadogo
iliyopo na kuhakikisha kuwa mitaji (NEDF) ulioanzishwa na Serikali na SIDO kupewa kazi
inatolewa na kutumika kwa ufanisi. ya kuratibu utoaji mikopo umeendelea kuimarishwa
ambapo kwa mwaka 2005/06 na 2006/07 mfuko
ulitunishwa kwa shillingi billioni moja kila mwaka. Aidha,
katika mwaka 2007/08 mfuko utatunishwa. Usimamizi
wa mfuko huu umeedelea kuimarishwa na ufanisi
kuongezeka, wastani wa marejesho ni zaidi ya asilimia
80.
60. SIDO kuendelea kutoa mitaji kwa Pamoja na mfuko wa NEDF uliotajwa hapo juu, SIDO
wajasiriamali wadogo na kutafuta imeendelea kusimamia fedha za mikopo kutoka
vyanzo mbalimbali vya fedha kwa ajili sehemu mbalimbali, mfuko wa „Regional Revolving
ya mitaji ya wajasiriamali. Fund‟ (RRF) wenye mtaji wa Sh. 1.5 billioni, mfuko wa
Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB) wenye
mtaji wa Sh. 500 milioni na mifuko mingine midogo.
Ufanisi wa mifuko yote ni mzuri, wastani wa marejesho
umefikia asilimia 83.
61. Kuendelea na juhudi za kuwawezesha Shirika la TIRDO lilitoa huduma kwa wajasiriamali ili
wajasiriamali kushiriki katika masoko kuwawezesha kuimarisha miradi yao na kuongeza
ya ndani na nje ya nchi na pia uwezo wao wa kuyafikia masoko ya nje. Huduma
kongamano la Kitaifa
252
litakalowakutanisha wadau mbali mbali zilizotolewa ni pamoja na:-
wa sekta litaandaliwa.
Mfumo wa Ufuatiliaji (Traceability)
Kwenye mfumo huu nia ni kufuatilia bidhaa kufuatana
na kumbukumbu na ubora wa kutoka kwa mlaji kurudi
hadi kwa mzalishaji ili kukidhi matakwa ya walaji
kimataifa. Mazao ambayo yameangaliwa ni pamoja na
kahawa, chai na korosho. Aidha, mafunzo yalitolewa
kwa washika dau 47.
Mfumo wa kutengeneza chaki
Kikundi kilichopo Kipunguni B, Dar es Salaam (Tuamke
Women Group) wajasiriamali 40 wamefundishwa jinsi
ya kutengeneza chaki. Kisarawe wamefundishwa watu
35.
Uchomeleaji wa chuma cha pua ili kutengeneza
vifaa vya kubebea chakula (Stainless steel
welding)
Mikoa iliyonufaika na mpango huu ni pamoja na Dar-es-
Salaam, Tabora na Iringa.
Kutengeneza vifaa vya chuma ya udongo (Metal
casting)
Sampuli 11 kutoka Songea na Moshi zimefanyiwa
uchunguzi kwenye maabara kwa nia ya kuona ubora
wa vifaa vinavyotengenezwa huko na kutoa ushauri wa
kitaalamu.
Vikausha vyakula kwa kutumia Nishati ya Jua
Vikausha samaki (hasa dagaa) vimetengenezwa na
mafunzo ya matumizi ya vifaa hivyo yalitolewa Dar-es-
Salaam, Pwani na Mwanza. Aidha, mafunzo yalitolewa
kuhusu namna ya kukausha mboga za majani na
matunda.
Mafunzo ya uzalishaji uyoga
Mafunzo yalifanyika huko Kilimanjaro na DSM kuhusu
kuzalisha uyoga. Aidha, mbegu za uyoga zilizalishwa
na kusambazwa nchini kote.
Kutengeneza unga wa Muhogo na Wanga
Wajasiriamali 150 kwenye Wilaya za Newala, Tunduru
na Ruangwa walipata mafunzo na kupelekewa mashine
tatu za kutengeneza unga wa muhogo na tatu za
253
kutengeneza wanga.
Kurejea taka za plastiki
Vikundi viwili Dar es Salaam vimepatiwa mafunzo
kuhusu jinsi ya kurejea takataka za plastiki (plastic
recycling) kwa nia ya kujua jinsi ya kukusanya,
kuzitenga kwenye vikundi vya plastiki za aina moja na
kuvifanyia usafi.
Kutengeneza matembe ya kukaushia Tumbaku.
Jumla ya watu 21 wilayani Mbinga wamehamasishwa
jinsi ya kutengeneza matembe bora yatumiayo kuni
kidogo ili kukausha tumbaku.
62. Utafiti na Maendeleo
Taasisi za utafiti yaani CAMARTEC, CAMARTEC imefanya utafiti na majaribio ya pampu
TEMDO na TIRDO, kuendelea kulenga ya maji iendeshwayo kwa nguvu za upepo (Vertical
katika kubuni teknolojia Sail Wing Windmill) kwa ajili ya kilimo cha
zitakazokwamua matatizo yanayokabili umwagiliaji, mifugo, na matumizi ya familia wilayani
sekta ya kilimo na viwanda hususan, Ngorongoro.
viwanda vidogo na vya kati ambavyo
havina uwezo wa kufanya utafiti Utafiti na majaribio juu ya mashine ya kukatakata
vyenyewe. malisho ya wanyama kwa kutumia injini itumiayo
mafuta ya diezeli unaendelea.
Utafiti katika mashine za kukoboa na kusaga nafaka
na za kuvuta maji umekamilika.
Kuanzia Septemba, 2006 CAMARTEC imeanza
kufanya utafiti wa kutengeneza sehemu zitakazotumika
katika kuunda trekta dogo la kulima chini ya mradi wa
PANTIL kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Sokoine,
(SUA).
Katika juhudi za kujikwamua kutoka katika tatizo la
nishati, CARMATEC inafanya tathmini ya utumiaji wa
kinyesi cha binadamu katika uzalishaji wa umeme.
Kitaalamu teknolojia hiyo inaitwa “Bio-latrine” na tayari
imeshaanza katika nchi jirani ya Rwanda. Aidha
Wizara itaandaa Mpango wa Utekelezaji (Business
Action Plan) ya teknolojia mbalimbali ikiwemo ya
Biolatrine kwa lengo la kufanikisha usambazaji wake.
TIRDO imekamilisha utafiti wa sumu aina ya
“Ochratoxin A (OTA)” kwenye zao la kahawa kwa
kushirikiana na taasisi nyingine za nje kwa kufadhiliwa
254
na Jumuiya ya Ulaya (EU). Utafiti umeonyesha kuwepo
kwa ukungu (fungus) yenye kutoa sumu ya “Ochratoxin
A” kwenye kahawa mikoani Kilimanjaro na Arusha.
Udhibiti wa ukungu huo kwa kutumia bacteria na
“yeast” zipatikanazo kwenye kahawa kwenye maeneo
hayo imetayarishwa (bio-control). Hii itatumika pamoja
na uzalishaji bora (Good Manufacturing Practices and
HACCP).
63. Kushughulikia utafiti wa teknolojia ya Utaratibu wa kuunda tovuti ya Wizara umeanza na
mawasiliano kamati imeundwa ikijumuisha wawakilishi kutoka kila
Idara kushughulikia taarifa zitakazowekwa kwenye
tovuti hiyo ili kurahisisha mawasiliano kati ya Wizara na
Wadau wa sekta ya viwanda, biashara na masoko.
Wataalamu wa TIRDO wamefanya tathmini ya kiwango
cha matumizi ya teknolojia ya mawasiliano na habari
kwenye viwanda kwa kuanzia kwenye miji ya Dar es
Salaam, Arusha na Mwanza. Hatua itakayofuatwa ni
kuviwezesha kitaaluma viwanda kutumia Internet kama
njia ya kujitangaza na kupata masoko mapya kwa
kuwawekea tovuti (Websites) na kuwajengea mitandao
(Local Area Networks) na mawasiliano ya barua pepe
(E-mail).
64. Kuendelea kuzitengea Taasisi hizi Kiasi cha shilingi milioni 202.25 zimetengwa kwa ajili ya
fedha za bajeti kupitia MKUKUTA na CAMARTEC, shilingi milioni 433.5 zimetengwa kwa ajili
kutafuta wafadhili kwa lengo la ya TIRDO na shilingi milioni 163 zimetengwa kwa ajili
kuziwezesha kuendelea na shughuli ya TEMDO.
zao.
65. Taasisi kuongeza nguvu katika Taasisi za TIRDO, CAMARTEC, SIDO, TEMDO,
kutangaza teknolojia ilizobuni na BRELA na TBS zimehamasishwa kushiriki katika
kutengeneza ili kupata soko na maonyesho mbalimbali ikiwa ni pamoja na maonesho
kujipatia fedha na kuzingatia kubuni ya DITF, na Siku ya Viwanda Afrika ili kutangaza
teknolojia kulingana na mahitaji ya teknolojia walizobuni. Aidha taasisi hizo zimeanzisha
soko (demand driven) badala ya mfumo wa ushirikiano katika kuendeleza teknolojia
kuzitengeneza ndipo watafute soko wanazozalisha hii ikiwa ni pamoja na kufanya
maonyesho ya pamoja.
Usimamiaji wa Sheria za Udhibiti
Ubora:
Kulenga kukamilisha ununuzi wa vifaa Hatua za awali za ununuzi wa vifaa vya kituo
muhimu vya Kituo cha Ufungashaji ili zimechukuliwa kwa kushirikiana na “Crown Agents”
kuongeza ubora wa ufungashaji wa ambao wametangaza tenda ya kimataifa.
bidhaa zinazozalishwa hapa nchini na
kuhakiki vifungashio kwa bidhaa
zinazotoka nje ya nchi.
255
67. Kuanza utekelezaji wa kiwango cha Utekelezaji wa mita za teksi utafanyika mwaka ujao wa
mita za teksi na kukamilisha ujenzi wa fedha 2007/08 mara baada ya uchaguzi wa chama cha
maabara ya kemikali madereva teksi wa Dar es Salaam kufanyika.
68. Kuendelea na hatua za kuthibitisha Maabara ya Ugezi (Metrology) imeishatathiminiwa
maabara za shirika na mifumo ya (assessed against ISO 17025) na Shirika la
utendaji wa Shirika la Viwango la Kuthathimini Maabara la Afrika ya Kusini (South Africa
Kimataifa (ISO certification) pamoja na National Accreditation System – SANAS) na kufanikiwa
kuhakikisha kuwa maabara zake kupita hatua zote za tathimini hiyo. Maabara hii
zinaboreshwa ili kuweza kutoa huduma imekubaliwa kupata cheti cha Umahiri wa Utendaji Kazi
nzuri zaidi kwa wananchi zake (Accreditation Certificate) terehe 15 Desemba,
2006.
Aidha maabara za Chakula (Food Microbiology) na
Nguo/Ngozi (Male Latex Condom Testing) zimefanyiwa
tathimini ya Umahiri wake (Initial Assessment) tarehe
11 – 14 Desemba, 2006.
Maabara ya Kemikali imefanyiwa uchanganuaji wa
awali kabla ya kutathiminiwa (Pre-assessment).
69. Kuendelea kutoa mafunzo kwa Tume ya Ushindani (Fair Competition Commission)
wataalam wake, kuelimisha umma na imeendelea kuajiri watendaji na tarehe 2 Mei, 2007
utekelezaji wa Sheria ya Ushindani ya imefikia idadi ya watumishi 30, kiwango cha chini
Mwaka 2003 ambacho kinaiwezesha Tume kusimamia shughuli za
uchumi wa soko kwa mujibu wa Sheria ya Ushindani.
Tume imeanza kutoa huduma kwa Baraza la Kushauri
Mlaji ili hatimaye kuwe na asasi au umoja wa kitaifa
unaojitegemea wa kutetea maslahi ya mlaji nchini.
Aidha, Tume kwa kushirikiana na vyombo vingine vya
Dola imeanza kudhibiti bidhaa feki (counterfeits)
zinazoingizwa nchini kwa kuzikamata na kuziharibu kila
zinapopatikana.
70. Kuhakiki vipimo vinavyotumika kwenye Ofisi ya Vipimo katika mikoa yote nchini zinaendelea na
biashara; jukumu hili kwa kufanya uhakiki na ukaguzi wa vipimo
katika maeneo ya biashara.
71. Kutangaza majukumu ya Wakala wa Jukumu hili linafanywa na maafisa vipimo wakati wa
Vipimo ili wadau waweze kuelewa zoezi la uhakiki wa vipimo katika ngazi za mitaa, vijiji
huduma zinazotolewa na kata. Kabla ya kuwahudumia wananchi, maafisa
hao huwaeleza kwanza madhumuni ya kuhakiki vipimo
vyao na faida ya matumizi ya vipimo sahihi.
- Baadhi ya mikoa imefanikiwa kutumia ziara za wakuu
wa Mikoa na Wilaya katika kuelezea wananchi
umuhimu wa kutumia vipimo sahihi. Mfano wa mikoa
hiyo ni Tanga, Arusha, Mbeya, Iringa na Mara.
- Mkoa wa Arusha ulipata ufadhili toka AMSDP
256
(Agricultural Marketing Systems Development
Programme) na kuweza kuendesha semina kuhusu
matumizi ya vipimo sahihi kwa ngazi za wilaya
(Arumeru, Karatu na Monduli).
- Wakala iliweza kushiriki Maonesho ya Sabasaba na
Nanenane na kutumia fursa hiyo kuonesha huduma
za wakala na kuelezea wananchi umuhimu wa
matumizi ya vipimo sahihi.
- Vipindi vya redio na televisheni (TV) vimeanza
kurushwa hewani kuanzia mwezi Januari, 2007.
72. Kushirikiana na taasisi nyingine, Wakala inashirikiana kwa karibu na Serikali za Mitaa,
hususan Wizara ya Kilimo, Chakula na Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Idara ya
Ushirika na Ofisi ya Waziri Mkuu, Masoko (Katika Wizara ya Viwanda), Ofisi za Wakuu
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa wa Mikoa na wilaya na NGO kama DAIPESA, AMSDP
ili kuhakikisha wauzaji wa mazao ya na TCCIA.
kilimo wanatumia vipimo sahihi.
73. Kuhakikisha mianya yote ya wizi na Jukumu hili linatekelezwa kwa kuhakiki na kufanya
udanganyifu wa kutumia vipimo ukaguzi wa kawaida (routine) na ule wa kushtukiza
visivyokuwa sahihi na rasmi katika (suprise inspections) na wahalifu wote huchukuliwa
biashara inazibwa. hatua za kisheria.
Tumefanikiwa kuanza kupima matenki makubwa ya
mafuta (bulk storage tanks) na hivyo kulisaidia taifa
katika juhudi za kuondoa udanganyifu mkubwa
unaofanyika katika biashara ya mafuta nchini.
74. Wakala wa Usajili (BRELA) Kuanza Lengo ni kupanua wigo na kuboresha huduma za usajili
kutekeleza mpango wa awamu ya tatu wa makampuni ya ndani na nje ya nchi, Majina ya
wa mwaka 2006/07-2008/09. Biashara, Alama za Biashara, Utoaji wa Hataza
(Patents) na utoaji wa leseni za Viwanda. Utekelezaji
unahusisha kupitia Sheria zinazosimamiwa na BRELA
na kubainisha maeneo yanayohitaji marekebisho na
kuondoa vipengele ambavyo sio vya lazima ili
kurahisisha utoaji huduma haraka.
Kuboresha na kusimamia sheria. Wakala imeanza kutekeleza sheria mpya ya
Makampuni (New Company) Act No. 12 of 2002.
Kuelimisha na kuhamasisha wadau Sheria ya Usajili wa Majina ya Biashara (Business Cap
wake kwa kutangaza huduma zake 213) na Sheria ya Leseni za Viwanda (National
kupitia radio na televisheni. Industries Act No. 10 of 1967) zinategemewa kupitiwa
upya kuondoa masharti yasiyo ya lazima na kuongeza
ufanisi katika usimamizi wa sheria na tija.
257
Sheria ya Miliki Ubunifu inaandaliwa upya kwa lengo
la kuirekebisha ili iende sambamba na hali halisi ya
kiuchumi, kijamii na kimaendeleo. Hatua hizi
zitatekelezwa na BRELA ikishirikiana na wahisani
chini ya mpango wa BEST (Business Environment
Strengthening Tanzania).
Kujenga uwezo wa ndani. Kazi kubwa ni kuboresha mazingira ya utendaji kazi
ili kuongeza tija na usimamizi bora wa vitendea kazi
na rasilimali za Serikali.
Kujenga na kutumia mbinu za Kurahisisha taratibu za kutoa huduma na
kisasa za utekelezaji. kuchapisha vipeperushi vitakavyoelezea utaratibu
wa kutoa huduma kwa kiswahili na kiingereza na
kwa lugha rahisi.
Kutoa elimu ya utawala bora kwa viongozi na
wafanyakazi.
Kutoa elimu ya juu ya madhara ya rushwa sehemu
za kazi na kwa nchi kwa ujumla.
Kupanua wigo ili kupeleka huduma Mkakati wa utekelezaji ni kuwa Wakala imeazimia
karibu na wananchi. kupeleka huduma mikoani na kwenye kanda na kutoa
huduma kikamilifu kwa kutumia Ofisi za Biashara za
Mikoa kwa wakati. Mradi huu muhimu unafadhiliwa na
wafadhili kwa kupitia BEST kabla ya kufungua ofisi za
kanda.
75. Kuboresha na kuzingatia mkataba wa BRELA imeshaandaa Mkataba wa Huduma kwa Mteja
huduma kwa wateja. ambao ni makubaliano ya kijamii baina ya Wakala
kama mtoa huduma na wateja wakiwa wapokea
huduma. Mkataba huu unategemewa kuzinduliwa hivi
karibuni.
76. Kupunguza kero za wadau kwa Ili kuondoa matatizo yanayojitokeza wakati wa
kuanzisha mtandao wa kuratibu kuwahudumia wateja, Wakala imeanzisha taratibu za
matatizo yanayojitokeza wakati wa kupeleka matangazo kwenye magazeti ili wateja watoe
kuwahudumia; maoni yao kuhusu huduma zetu “Mnatuonaje”. Aidha,
lipo sanduku la maoni makao makuu ya Wakala ili
wateja waweze kutoa maoni yao na wakala iweze
kuyafanyia kazi na hivyo kupunguza kero za wateja.
77. Kuendelea kujijengea uwezo wa MKUMBITA unasaidia Wakala kwa kujijengea uwezo
utendaji kazi na ufanisi wa utekelezaji kwa njia zifuatazo:-
kwa msaada wa MKUMBITA Kutoa mafunzo mbalimbali kwa wafanyakazi wa
Wakala; kutoa vitendea kazi kwa Wakala
258
Kufanya “Computation” ya BRELA kwa nia ya
kurahisisha upatikanaji wa huduma bora na haraka.
Kupeleka huduma karibu na wanachi kwa
kuwezesha kuwepo kwa mtandao na kufungua ofisi
za kanda.
Kusaidia kupitia sheria mbalimbali kwa nia ya
kuziboresha.
78. Kukusanya mirabaha kupitia kwa Wakala 16 wameanza zoezi la kukadiria na kukusanya
Wakala katika kila mkoa wa Tanzania mirabaha nchini kote. Jumla ya sh. 8,862,500
na kuweza kuwagawia wasanii husika ziligawiwa tarehe 25 Agosti, 2006. Wakala hao sasa
wamekusanya sh. 65, 001,90o.
79. Kuendesha semina na elimu kwa Semina ziliendeshwa katika Mikoa ya Tabora na Dar es
umma katika mikoa kwa njia ya Salaam. Pia, elimu kwa umma ilitolewa kwenye
vyombo vya habari; na vyombo vya habari kupitia radio na televisheni.
80. Kuingia mikataba na Vyama vya Mikataba na vyama vya nje vya Perfoming Rights
Hakimiliki vya nchi mbalimbali vya Society (PRS) cha Uingereza na ONDA (Algeria)
kulinda Hakimiliki kwa lengo la itakamilika hivi karibuni.
kukusanya mirabaha kwa niaba ya
COSOTA pale ambapo kazi za wasanii
na watunzi wa Tanzania zimetumiwa
nchini kwao.
81. Kuendeleza warsha za utawala bora Wizara iliendesha warsha za utawala bora na elimu ya
na huduma kwa mteja kwa watumishi Huduma kwa Mteja kwa watumishi na viongozi ili
wake na watumishi wa Wakala wa kuboresha huduma na kuondoa mianya ya rushwa.
Vipimo ikiwa ni mwendelezo wa Aidha, Wizara imeandaa Mkataba wa Huduma kwa
utekelezaji wa Mkakati wa Wizara wa Mteja ambao umeainisha masuala mbalimbali juu ya
Vita dhidi ya Rushwa. utoaji huduma zinazotolewa na Wizara ili kuruhusu
maoni na kuboresha huduma zaidi kwa wananchi.
Mafunzo ya Sheria ya Fedha na Manunuzi
yameendelea kutolewa kwa viongozi wa Wizara na
wajumbe wa Kamati ya Bodi ya Zabuni ya Wizara na
Maafisa Ugavi ili kuwawezesha kutoa maamuzi sahihi
katika masuala ya manunuzi na fedha.
82. Kuendeleza juhudi za kupambana na Katika kuendeleza juhudi za kupambana na kudhibiti
kupunguza athari zitokanazo na maambukizi mapya kwa watumishi wake Wizara imetoa
ugonjwa wa UKIMWI pia kudhibiti mafunzo ya uelimishaji na uhamasishaji wa kupima
maambukizi mapya kwa kushirikiana virusi vya UKIMWI kwa watumishi na wadau wa sekta
na Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI ya Viwanda, Biashara na Masoko na kutoa msaada
(TACAIDS). usio wa kimatibabu kwa watumishi walioathirika na
ugonjwa huo na kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa
mipango ya shughuli za UKIMWI sehemu za kazi
wizarani na kwenye taasisi.
83. Kupitia na kuboresha Mkakati wake wa Katika kuendeleza juhudi za kupambana na kuthibiti
kupambana na UKIMWI, ikiwa ni maambukizi mapya kwa watumishi wake Wizara
259
pamoja na kufanya tathmini ya hali imepitia na kuboresha Mkakati wake wa kupambana na
halisi ya maambukizi kwa watumishi UKIMWI na kuendesha zoezi la tathimni ya hali halisi
wake. ya UKIMWI kama ilivyopanga kwenye wizara na taasisi
zilizo chini yake kwa lengo la kujua hali ya watumishi na
kuweza kupanga mikakati ya kuwaendeleza ili
waendelee kutoa michango yao katika sekta.
84. Kuendesha semina za uhamasishaji Mafunzo hayo hayakuweza kufanyika kwa sababu ya
kuhusu masuala ya jinsia ili ufinyu wa bajeti. Mara bajeti ya Wizara itakapopatikana
wafanyakazi waweze kuwa na uelewa ya kutosha mafunzo haya yataendeshwa.
wa jinsi ya kuyahusisha katika kazi zao
za kila siku.
260
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. (a) Kutoa ruzuku ya maendeleo ya Vyumba vya madarasa 2,303 vimejengwa kwa kutumia
Shilingi 3,010,000,000 kwa ajili Ruzuku ya Maendeleo ya shilingi 7,845,300,000. Hili ni
ya ujenzi wa vyumba vya ongezeko la vyumba 1,443 zaidi ya lengo la kujenga
madarasa 860. vyumba 860.
(b) Kuendelea kutoa ruzuku ya Shilingi Bilioni 52 za Ruzuku ya Uendeshaji zimetolewa
uendeshaji kwa ajili ya ununuzi kwa Halmashauri zote nchini. Kati ya fedha hizo
wa vitabu vya kiada vya shilingi 20,800,000,000 zimetolewa kwa lengo la
kufundishia na kujifunzia ili kununua vitabu. Aidha, zoezi la ufuatiliaji wa ununuzi,
kufikia uwiano wa kitabu kimoja matumizi na uhifadhi wa vifaa vya kufundishia na
kwa mwanafunzi mmoja(1:1) kujifunzia umefanyika kote nchini. Mpaka sasa uwiano
wa kitabu kwa mwanafunzi ni wastani wa kitabu kimoja
kwa wanafunzi watatu (1:3) kama ilivyokuwa mwaka
2006.
(c) Kuandikisha watoto wa darasa Jumla ya wanafunzi 1,407,812 wameandikishwa darasa
la kwanza 1,166,737 wenye la kwanza ambao ni wanafunzi 241,075 zaidi ya lengo
umri wa miaka 7 na waliobaki la kuandikisha wanafunzi 1,166,737 mwaka 2007.
wa miaka 8 na 9 wa mwaka
2005 na 2006.
(d) Kujenga Nyumba za Walimu Nyumba za walimu 2,183 zimejengwa hususan maeneo
500 hasa vijijini ya vijijini kwa ruzuku ya maendeleo ya shilingi
7,858,800,000. Hili ni ongezeko la nyumba 1,683 zaidi
ya lengo.
(e) Kuajiri walimu wapya 7,337 ili Walimu wapya 6,565 wameajiriwa, sawa na asilimia
kukabiliana na ongezeko la 89.5% ya lengo na kufanya uwiano wa mwalimu kwa
uandikishaji. wanafunzi kuwa 1:55.
(f) Kusimamia utekelezaji wa Wizara imesimamia utekelezaji wa Elimu ya Msingi kwa
Mpango wa Elimu ya Msingi Walioikosa (MEMKWA) pamoja na kuendesha mafunzo
kwa Walioikosa (MEMKWA). kwa walimu wa MEMKWA na ununuzi wa vitabu
180,000 kwa Shilingi 251,826,000. Aidha, Wizara
imeendesha uhakiki wa vituo vya MEMKWA katika
Halmashauri 56 nchini
(g) Kujenga majiko 27 katika Kwa kushirikiana na Halmashauri na mashirika
shule za Wilaya ya Mpwapwa mbalimbali kupitia mradi wa lishe shuleni yamejengwa
na kujenga matangi manne ya majiko 27 katika Wilaya ya Mpwapwa na Kondoa.
maji katika shule za Mkoa wa
Singida zilizo kwenye Mpango
wa Lishe Shuleni.
(h) Kufuatilia na kutathmini ushiriki Ufuatiliaji na tathmini vimefanyika. Aidha, uhamasishaji
wa viongozi wa wilaya, Kamati wa jamii umefanyika katika shule 622 za mradi wa
za shule na jamii katika kuleta shule zinazomjali mtoto.
mazingira ya kumjali mtoto
katika shule za mradi.
261
(i) Kuinua kiwango cha kufaulu Kiwango cha kufaulu katika mtihani wa kumaliza darasa
kufikia 90% la VII kimepanda kutoka asilimia 61.8 mwaka 2005 hadi
asilimia 70.48 mwaka 2006. Kwa darasa la IV kiwango
cha kufaulu kimeshuka kutoka asilimia 87.8 mwaka
2005 hadi asilimia 86 mwaka 2006.
(j) Kuandikisha watoto wa shule za Jumla ya wanafunzi 795,011 wameandikishwa katika
awali 1,321,124. elimu ya awali mwaka 2007. Hii ni sawa na asilimia 60
ya lengo la kuandikisha watoto 1,321,124.
2. (a) Kujenga madarasa mapya Jumla ya madarasa mapya 1631 kati ya 1637
1,637 kwenye shule za yaliyotarajiwa yalijengwa katika shule za wananchi
sekondari za ngazi ya kawaida zenye kidato cha I-IV. Aidha, madarasa 128
zinazojengwa kwa nguvu za yamejengwa katika shule zenye kidato cha V-VI
wananchi na mengine 128
katika shule za ngazi ya juu
zilizopo.
(b) Kujenga nyumba za walimu Ruzuku ya kuchangia ujenzi wa nyumba za walimu
1,000 kwa gharama ya Shilingi 1,000 ilitolewa katika shule za Serikali hasa zilizoko
9,000,000,000 kwenye shule za vijijini.
sekondari.
(c) Kuchangia ujenzi wa maabara Shule 40 zimepelekewa fedha za ujenzi wa maabara.
40 kwa gharama ya Shilingi
560,000,000/=
(d) Kujenga vyoo katika shule 60, Shule 30 zilipelekewa fedha shilingi Milioni 9 kila moja
mabweni 5 na maktaba 30. kwa ajili ya ujenzi wa maktaba, pia shule 47 kati ya
shule 60 zilipelekewa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo.
Aidha, shule 24 zikiwemo za wasichana tano
zimepatiwa fedha jumla ya shilingi Milioni 22 kila moja
kwa ajili ya ujenzi wa mabweni (Hostel).
(e) Kukarabati shule 30 kati ya Ruzuku ilitolewa kwa ajili ya ukarabati wa shule 16 kati
shule 100 za zamani. ya shule 30 zilizotarajiwa.
(f) Kukarabati miundombinu Shule tatu (3) kati ya Sita (6) zenye wanafunzi wenye
kwenye shule sita (6) za ulemavu ambazo ni Njombe, Pugu na Jangwani
wanafunzi wenye mahitaji zimeshapatiwa fedha za MMES kwa ajili ya ukarabati.
maalumu.
(g) Kugharamia elimu ya Sekondari Wanafunzi 33,865 wa kidato cha I-IV wanaotoka katika
kwa wanafunzi 45,873 familia zenye kipato duni na wasichana 147 waliokuwa
wanaotoka katika familia zenye wakigharimiwa na Mradi wa „Girls Secondary
kipato duni wakiwemo 33,934 Education Support‟ (GSES) uliokwisha mwaka 2003
wanaoendelea kulipiwa. waligharimiwa elimu ya sekondari.
(h) Kuwajengea uwezo wa Wakuu wa shule 450 walipatiwa mafunzo ya
kimenejimenti wakuu wa shule, manejimenti na uongozi kwa siku tano (5) ADEM-
Bodi za shule, kamati za Bagamoyo.
uendeshaji za shule, maafisa
walioko Makao Makuu ya
Wizara.
262
(i) Kuendesha mafunzo kwa Waratibu 105 wa Elimu ya Sekondari ngazi ya Wilaya
viongozi wa ngazi ya Mkoa na walipatiwa mafunzo ya Menejimenti ya uongozi.
Wilaya ili kuwashirikisha
kikamilifu katika ufuatiliaji wa
Mpango wa Maendeleo ya
Elimu ya Sekondari katika
maeneo yao.
(j) Kuteua Mratibu wa Elimu ya Waratibu 105 wameshateuliwa na wameanza kazi
Sekondari kila Wilaya Januari 2007 baada ya kupatiwa mafunzo mafupi.
atakayesimamia matumizi ya
fedha za MMES pamoja na
kazi nyingine.
(k) Kugharimia walimu 200 Jumla ya walimu 150 kati ya 200 wanaosoma chuo
mafunzo ya shahada ya kikuu huria waligharimiwa vitabu na fedha za utafiti.
kwanza katika Chuo Kikuu
Huria.
3. (a) Kuandaa miundombinu na Mitambo ya kisasa ya Kompyuta imefungwa katika
Mtandao wa TEHAMA na vyuo 32 vya Ualimu vya Serikali na kuunganisha vyuo
kugharimia na kuandaa nane (8) kwenye mtandao wa internet kwa njia ya
muhtasari wa kufundishia Setelite (VSAT System).
TEHAMA kwenye Vyuo vya
Ualimu.
(b) Kuchagua wanachuo wa Walimu Tarajali Daraja la III A 7,200
kujiunga na Mafunzo ya ualimu walichaguliwa kujiunga na mafunzo ya Ualimu
tarajali Daraja A 7,200, katika Vyuo vya Ualimu 18.
Stashahada 4,000, Mafunzo
Maalum ya mwezi mmoja Wanachuo 4,390 waliomaliza kidato cha sita
3,500 na Mafunzo kazini 1,350. wenye sifa stahili walichaguliwa kujiunga na
mafunzo ya Stashahada ya ualimu.
Mafunzo maalumu ya muda mfupi yalitolewa kwa
vijana 5,546 waliohitimu kidato cha sita ili
waweze kufundisha katika shule za sekondari
kwa leseni.
(c) Kuendeleza walimu 26,000 wa Walimu wa Daraja C na B 21,519 walifanya mitihani ya
Daraja C na B kwa utaratibu Baraza la Mitihani la Tanzania ngazi ya Daraja III A.
wa moduli kufikia Daraja A Kati ya hao 20,021 walifaulu. Hii ni asilimia 92.10 ya
ifikapo mwaka 2007. walimu walioandikishwa kwa kozi hiyo.
(d) Kugharamia wakufunzi 314 Jumla ya wakufunzi 645 wanaosoma Chuo Kikuu Huria
wanaosoma Chuo Kikuu Huria. walilipiwa ada.
(e) Kufuatilia uandaaji wa Serikali ilisaidia kugharamia maandalizi ya awali ya
muhtasari wa Teknolojia ya muhtasari wa kufundisha TEHAMA katika Vyuo vya
Habari na Mawasiliano Ualimu ambao upo katika hatua za awali. Kwa sasa
263
(TEHAMA) kwa ajili ya vyuo wataalamu wanaendelea kufanyia kazi.
vya ualimu.
(f) Kuwa na Mkakati wa Wadau wa elimu walifanya ziara ya kutembelea vyuo
Maendeleo na Uongozi wa vya ualimu 32 ili kukusanya taarifa, takwimu na kuona
Elimu ya Ualimu (Teachers hali halisi ya maandalizi ya Mkakati wa Maendeleo na
Development and Menejimenti ya Walimu katika vyuo. Aidha, rasimu ya
Management Strategy-TDMS). Mkakati huo imekamilika.
(g) Kufuatilia na kutathmini (Rapid Ufuatiliaji wa programu ya walimu wa shule zinazomjali
Needs Assessment – RNA) mtoto katika wilaya zote sita ulifanyika. Aidha, mpango
program ya walimu wa Shule huu utasambazwa katika shule 10 za mfano.
za Msingi
Zinazomjali Mtoto (Child
Friendly Schools) katika wilaya
sita za majaribio, Ngara,
Musoma (V), Kisarawe,
Masasi, Songea (V) na
Makete.
(h) Kupatiwa mafunzo ya Mafunzo kwa walimu 41,650 wa shule za msingi
ufundishaji na ujifunzaji wa njia kuhusu ufundishaji na ujifunzaji yalitolewa.
shirikishi walimu wa shule za
msingi wa Daraja “A” 41,975.
4. (a) Kukagua jumla ya asasi 20,112 Jumla ya asasi 13,695 sawa na asilimia 68 ya lengo la
zikiwemo shule za awali 4,411, kukagua 20,112 zilikaguliwa. Asasi hizi ni: Shule za
msingi 7,164, vituo vya EWW Awali 2,250, Shule za Msingi 3,242, Vituo vya Elimu
7,164, vituo vya ufundi stadi maalumu 36, Vituo vya Ufundi Stadi 14, Vituo vya
162, vituo vya elimu maalum EWW 2,552, Shule za sekondari 452 na Vyuo vya
129, shule za sekondari 1,032 Ualimu 45.
na vyuo vya ualimu 50.
(b) Kutoa nakala 1,000 za Nakala 500 za Mwongozo wa Mafunzo ya Awali ya
Mwongozo wa Mafunzo ya ukaguzi wa shule na nakala 1500 za Kiongozi cha
Awali ya ukaguzi wa shule na Mkaguzi wa Shule zilitolewa.
nakala 1,000 za Kiongozi cha
Mkaguzi wa shule.
(c) Kuendesha Mtihani wa Taifa Mtihani wa Taifa Kidato cha pili mwaka 2006
Kidato cha II Mwaka 2006. uliendeshwa katika Kanda zote nane (8). Jumla ya
vituo 1,790 vilisajili watahiniwa 220,617, ambapo jumla
ya watahiniwa 209,967 walifanya mtihani huo.
(d) Kuboresha mazingira ya kazi Jumla ya ofisi 20 zilikarabatiwa. Aidha samani kwa ajili
kwa wakaguzi wa shule kwa ya ofisi za wakaguzi pamoja na Kompyuta zilitolewa
Kununua samani na vifaa vya Katika Wilaya 20.
ofisi, kukarabati ofisi za Kanda
na Wilaya.
264
(e) Kutoa mafunzo juu ya mtaala Mafunzo kuhusu mtaala uliorekebishwa mwaka 2005
mpya kwa wakaguzi wa shule yalifanyika kwa wakaguzi 1,064 kama yalivyopangwa.
1,064.
(f) Kununua magari matano (5) Jumla ya magari 16 yalinunuliwa na kusambazwa
kwa ajili ya ofisi za ukaguzi katika Kanda saba (7) na Wilaya tisa (9).
wilayani.
5. (a) Kufuatilia utekelezaji wa Ufuatiliaji wa utekelezaji wa Waraka wa Elimu Na. 3 wa
Waraka wa Elimu Na. 3 wa Mwaka 2006 ulifanywa na Walezi wa Elimu ya Watu
Mwaka 2006, unaoelekeza Wazima katika mikoa yote 21.
kuhusu utekelezaji wa Mkakati
wa Elimu ya Watu Wazima na
Elimu nje ya Mfumo Rasmi.
(b) Kununua vifaa vya kufundishia Ununuzi wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia
na kujifunzia Wanafunzi wenye Wanafunzi Wenye Ulemavu ulifanyika.
Ulemavu wa Akili, Wasiiona,
Wenye Uoni Hafifu, Wenye
Otizim, Viziwi, Viziwi Wasioona,
Ulemavu wa Viungo na Albino.
(c) Kuchapa aina 13 za vitabu vya Jumla ya aina 13 za Vitabu vya Kiada zenye nakala
kiada zenye nakala 600 kila 600 kila moja kwa Shule za Msingi, aina nane (8) zenye
moja kwa shule za msingi, aina nakala 400 kila moja kwa Shule za Sekondari na aina
nane (8) zenye nakala 400 kila mbili (2) zenye nakala 400 kila moja kwa Vyuo vya
moja kwa shule za sekondari Ualimu zilichapwa.
na aina mbili (2) zenye nakala
400 kila moja kwa vyuo vya
Ualimu.
(d) Kuchapa mwongozo wa Jumla ya nakala 1,000 za mwongozo wa mwezeshaji
Mwezeshaji na Kuendesha wa Mafunzo ya Elimu Jumuishi ulichapwa. Aidha,
Mafunzo ya Elimu Jumuishi Mafunzo ya Elimu Jumuishi kwa walimu 432 katika
kwa walimu 1,200 katika Halmashauri 18 yalitolewa.
Halmashauri 50.
(e) Kuendesha mafunzo ya muda Mafunzo ya muda mfupi kwa wataalamu wa elimu
mfupi kwa wataalam wa Elimu Maalumu kwa Wasioona na wenye Uono Hafifu 50,
Maalumu kwa Wasiiona na wenye ulemavu wa Akili na wenye Otizim 50 na Viziwi
Wenye Uono Hafifu 50, Wenye pia Viziwi Wasioona 50 yalitolewa.
Ulemavu wa Akili na Wenye
Otizim 50 na Viziwi na Viziwi
Wasioona 50.
265
6. (a) Kusajili jumla ya shule zisizo Shule 160 zilisajiliwa: Awali saba (7), Msingi mbili (2),
za Serikali 150. Awali na Msingi 63, Sekondari 82 na Vyuo vya Ualimu
sita (6).
(b) Kushughulikia maombi 100 ya Maombi 164 yalithibitishwa Mwenye Shule na Meneja:
kuthibitisha Meneja na Wenye Awali mbili (2), Msingi moja (1), Awali na Msingi 59,
Shule Zisizo za Serikali. Sekondari 96 na Vyuo vya Ualimu tano (5) na Chuo
cha Kidini moja (1).
(c) Kuchambua maombi ya vibali Shule za Sekondari 1,084 za Serikali zilizojengwa kwa
vya kuanzisha Shule za nguvu za wananchi zilisajiliwa.
Sekondari zilizojengwa kwa
nguvu za Wananchi.
(d) Kuchambua maombi ya leseni Leseni 6,319 zilitolewa: Shahada ya Uzamili 44,
za kufundisha. Shahada ya Kwanza 152, Stashahada 26, Vyeti 22,
Kidato cha Sita 44, na Mafunzo ya muda mfupi 6,031.
(e) Kuendesha mafunzo kuhusu Mafunzo kuhusu taratibu za usajili wa shule
taratibu za usajili wa Shule na yaliendeshwa katika Halmashauri (4) nne.
Walimu kwa Watendaji 200
kutoka Halmashauri (7) Saba.
(f) Kukusanya takwimu za Walimu Jumla ya taarifa za walimu walio kazini kutoka
walio kazini kutoka Halmashauri 33 zimekusanywa.
Halmashauri 60.
(g) Kuratibu utafiti kuhusu ubora Uratibu wa uendeshaji wa utafiti wa awali kuhusu ubora
wa Elimu kwa nchi 15 za Kusini wa elimu katika nchi 15 za Kusini mwa Afrika –
mwa Afrika „Southern Africa “Southern Africa Consortium for Monitoring Education
Consortium for Monitoring Quality” (SACMEQ III) umefanyika.
Education Quality‟ (SACMEQ
III).
7. (a) Kuandaa na kutangaza vipindi Jumla ya vipindi 52 vya BORESHA ELIMU
mbalimbali 536 vikiwepo 52 viliandaliwa na kutangazwa na RTD kwa lengo la
vya BORESHA ELIMU, 52 vya kuhamasisha jamii juu ya utekelezaji wa MMEM na
ufundishaji na 432 vya MMES.
masomo mbalimbali ya shule
za msingi.
Vipindi 52 vya ufundishaji kuhusu mbinu shirikishi
viliandaliwa na kutangazwa na RTD.
Vipindi 432 vya masomo ya Kiingereza, Maarifa ya
Jamii, Kiswahili na Sayansi kwa madarasa V, VI na VII
pamoja na Historia, Jiografia na Uraia Darasa la III na
IV viliandaliwa na kutangazwa na RTD.
(b) Kuendesha semina kwa Walimu Walimu 164, Wakaguzi wa Shule 120 wa Kanda ya
1,260 na Wakaguzi wa Shule Mashariki, Kaskazini Magharibi na Magharibi na
756 kutoka kanda sita (6) za Magharibi walielimishwa kuhusu utumiaji wa mwongozo
266
elimu kuhusu utumiaji wa Wa mkakati wa Ujanishaji shule na kufundishia Elimu
mwongozo wa elimu ya ya Mazingira.
mazingira pamoja na kuhariri
Mwongozo wa kufundisha Elimu ya Mazingira kwa
nakala 200,000 za kufundishia
Shule za Msingi ulihaririwa na nakala 150,000
elimu ya mazingira.
zilichapwa.
(c) Kuchapisha nakala 9,000 za Jumla ya nakala 10,000 za Mwongozo wa Ushauri
Mwongozo wa Ushauri Nasaha Nasaha zimechapwa.
na unasihi na kutoa mafunzo ya
ushauri nasaha na unasihi kwa
walimu 1,000 wa shule za
sekondari na vyuo vya ualimu.
(d) Kutafsiri Mwongozo wa Ushauri
Mwongozo wa Ushauri Nasaha ulitafsiriwa kutoka lugha
Nasaha na Unasihi kutoka
ya Kiingereza kwenda Kiswahili.
Kiingereza kuwa Kiswahili.
(e) Kuchapisha na kusambaza Andiko la Elimu Rika Dhidi ya UKIMWI kwa shule za
maandiko ya mafunzo ya sekondari limekamilika.
kujikinga na UKIMWI katika
Nakala 86,400 za vitabu vya Uelimishaji Rika, UKIMWI
shule na vyuo vya ualimu.
na Magonjwa ya Zinaa zimenunuliwa na kusambazwa.
Kuchapa na kusambaza nakala 58,000 za vitabu vya
kujikinga na UKIMWI katika shule za Msingi na
Sekondari.
(f) Kuendesha mafunzo ya elimu Walimu wa shule za msingi 200 wamepatiwa mafunzo
ya familia kwa walimu 777 wa juu ya namna ya kufundisha mada za UKIMWI.
masomo chukuzi ya elimu ya
familia na wakuu wa shule za
sekondari 250 kutoka kanda ya
nyanda za juu kusini.
8. (a) Kufanya utafiti juu ya
maendeleo ya taaluma na Utafiti kuhusu mwenendo wa mdondoko wa wanafunzi
uongozi kwa baadhi ya shule katika shule za Msingi na Sekondari umefanyika.
za msingi zilizoteuliwa nchini Aidha, pendekezo la utafiti (research proposal) wa
Tanzania, kutafiti mwenendo maendeleo ya taaluma ya uongozi kwa baadhi ya shule
wa mdondoko (drop-out) wa za Msingi limeandaliwa.
wanafunzi wa shule za msingi
na sekondari kuanzia mwaka
1995 hadi 2005 na kufanya
utafiti wa athari za ada katika
utoaji wa elimu ya sekondari.
267
(b) Kufanya ufuatiliaji na tathmini Ufuatiliaji na tathmini juu ya matumizi ya fedha na utoaji
katika shule na vyuo vya wa huduma za elimu na mafunzo umefanyika katika
ualimu kuhusu matumizi ya shule 380 za Sekondari.
fedha na utoaji wa huduma za
elimu na mafunzo ya ufundi.
(c) Kuboresha rasimu ya mapitio Zana za ukusanyaji maoni ya wadau na kuingiza
ya Sera ya Elimu na Mafunzo masuala mtambuka ili kuboresha rasimu ya Sera ya
ya mwaka 1995 ili kuingiza Elimu na Mafunzo zimeandaliwa.
masuala ya Mafunzo ya
Ufundi.
(d) Kukamilisha andiko la pili la Andiko la pili la Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya
Mpango wa Maendeleo ya Msingi (MMEM II) 2007-2011 limekemilika. Aidha,
Elimu ya Msingi (MMEM II) na nakala 5000 za Vitabu vya Basic Education Statistics in
kuchapa kitabu cha Takwimu Tanzania (BEST) 2007 vimechapwa.
za Elimu ya Msingi Tanzania
2007 (Basic Education
Statistics in Tanzania 2007).
(e) Kusimamia ukarabati wa shule Jumla ya majengo katika shule 20 za sekondari, ofisi za
za sekondari 20, Vyuo vya makao makuu, ofisi tatu (3) za kanda za Mpango wa
Ualimu 10, ofisi za makao matengenezo zilikarabatiwa kama ilivyokusudiwa, pia
makuu na Wakala wa vyuo tisa (9) vya Ualimu kati ya 10 vilivyokusudiwa
Maendeleo ya Uongozi wa vilikarabatiwa.
Elimu (ADEM) na ofisi za
Kanda tatu (3) za Mpango wa
Matengenezo (Physical
Planning and Maintenance
Zones).
(f) Kutoa Ithibati 80 kwa vitabu Jumla ya vitabu 80 vilivyokusudiwa pamoja na vifaa
vya kielimu na zana za vingine vya kufundishia na kujifunzia vilitolewa ithibati.
kufundishia shuleni na vyuoni.
(g) Kuimarisha hifadhi na Mtandao wa Kompyuta imeunganishwa katika Idara
mpangilio kwa taarifa za zote za Makao Makuu.
kompyuta (Database) na
kumbukumbu za Wizara.
(h) Kuendesha mafunzo ya Walimu 72 kutoka shule 36 za sekondari walipewa
matengenezo na dhana ya mafunzo ya matengenezo na utunzaji majengo na
utunzaji wa majengo na Mazingira.
mazingira kwa Wakuu wa
Shule na Vyuo vya Ualimu
268
katika kanda 8 za elimu.
9. (a) Kuratibu utoaji wa habari katika Utoaji wa taarifa za elimu kwa vyombo vya habari
vyombo vya habari na kupiga uliandaliwa na kuratibiwa ipasavyo, pia utunzaji wa
picha za video na mnato katika kumbukumbu za matukio ya elimu katika picha za video
matukio mbalimbali ili kuweka na mnato ulifanyika kama ilivyopangwa.
kumbukumbu za Wizara.
(b) Kutayarisha matangazo 40 ya Matangazo 40 ya redio na televisheni yalitayarishwa ili
redio na televisheni ili kuifahamisha jamii kuhusu mikakati, changamoto na
kufahamisha na kuhamasisha mafanikio; pamoja na kuhamasisha jamii kushiriki
jamii kuhusu mikakati na katika kutekeleza mipango ya elimu.
mafanikio ya Wizara katika
kutekeleza mipango ya elimu.
(c) Kuandaa na kusambaza Jumla ya nakala 330,000 za jarida la “Ed-SDP
nakala 330,000 za jarida la Newsletter” zilichapwa na kusambazwa katika kanda
EdSDP la kitaifa na katika nane (8) za elimu ili kuwaelimisha wadau na
kanda nane (8) za elimu nchini kuwahamasisha kushiriki katika utekelezaji wa mipango
kwa ajili ya kuhamasisha jamii ya elimu.
na wadau wa elimu kushiriki
katika kutekeleza mpango wa
elimu nchini.
(d) Kuandaa vipindi 50 vya redio na Vipindi 50 vya redio na televisheni ili kuelezea Sera ya
televisheni kwa kushirikiana na Elimu ya mwaka 1995 na utekelezaji wa programu za
vyombo vya habari vya redio na MMES na MMEM viliandaliwa.
televisheni kuelezea kuhusu
kazi za Wizara, Sera na
utekelezaji wa miradi ya elimu
kama MMEM, MMES,
MEMKWA na Elimu nje ya
mfumo rasmi (Non-Formal).
(e) Kuandaa vipeperushi na Jumla ya nakala 50,000 za kalenda, vipeperushi
kalenda 50,000 za MMEM na 20,000 mabango 10,000 na shajara 50,000 zenye
MMES. taarifa na takwimu
za utendaji wa programu za MMES na MMEM
zilichapwa na kusambazwa.
10. (a) Kuajiri watumishi 7,024 Jumla ya walimu 7,872 wa sekondari na vyuo vya
wakiwemo walimu 6,755 na ualimu pamoja na watumishi wengine wasio walimu
watumishi wasio walimu 269. 170 waliajiriwa.
269
(b) Kugharimia mafunzo ya muda Viongozi na Watumishi wa Wizara 360 walihudhuria
mrefu na mfupi ndani na nje ya mafunzo ya muda mfupi ya huduma kwa mteja.
nchi kwa watumishi 150.
(c) Kuthibitisha kazini watumishi Jumla ya watumishi 127 walithibitishwa kazini.
220 wasio walimu.
(d) Kupandisha madaraja Watumishi 545 walipandishwa madaraja.
watumishi 1,347 wasio walimu.
(e) Kuendelea kushirikisha Sekta Wizara imeshirikisha sekta binafsi katika utoaji huduma
Binafsi katika kutoa huduma za za ulinzi, usafi na mapokezi Makao Makuu.
usafi, ulinzi na mapokezi.
(f) Kutekeleza Mpango wa Mwaka Utekelezaji wa OPRAS kwa ajili ya walimu mashuleni
wa Thathmini ya Utendaji Kazi kwa majaribio ulianza Januari, 2007. Aidha, utaratibu
wa Watumishi kwa utaratibu huu utaanza kutumika rasmi Julai, 2007.
mpya unaolenga kuweka
malengo na matokeo katika
utendaji kazi (Open
Performance Review and
Appraisal System (OPRAS) kwa
watumishi wa Wizara.
(g) Kupitia muundo wa Utumishi Uchambuzi wa Muundo unaendelea.
wa Walimu kwa kushirikiana na
Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma.
11. (a) Kutoa mafunzo ya Stashahada Wanachuo 97 wamepata mafunzo ya Stashahada ya
ya Uongozi wa Elimu kwa Uongozi na Uendeshaji wa Elimu Kati ya 100
viongozi 150 wa idara walioandikishwa na 148 kati ya 150 wanaendelea na
mbalimbali za Elimu mafunzo.
yanayowahusu Walimu Wakuu
wa shule za Msingi, Waratibu
Elimu Kata, Maafisa wa Elimu
ngazi ya Wilaya, Walimu wa
Shule za awali, Msingi,
Sekondari, Wafanyakazi katika
Mashirika yasiyo ya Kiserikali
(NGOs) na Mameneja na
Wamiliki wa shule Zisizo za
Serikali.
(b) Kuendesha mafunzo ya Mafunzo ya awali ya uongozi wa elimu kwa wakuu wa
Uongozi na Menejimenti ya shule wapya 450 wa shule za sekondari katika vituo
mwezi mmoja kwa wakuu wa vya Kanda vya elimu yametolewa.
shule wapya na wasaidizi wa
shule za sekondari za serikali
120 na zisizo za serikali 100
kutoka kanda zote.
270
(c) Kutoa mafunzo ya Uongozi na Mafunzo ya Uongozi na Uendeshaji wa Elimu kwa
Uendeshaji wa elimu kwa Waratibu wa Elimu Kata 746 kati ya 2,300 yamefanyika
Waratibu wa Elimu kata, 2,300 kutoka katika Wilaya za Mpwapwa, Singida vijijini,
kutoka Wilaya za Mpwapwa, Singida Manispaa, Nachingwea, Mtwara vijijini, Mtwara
Nachingwea, Mbinga, Urambo, Mikindani, Mbinga, Urambo, Nzega, Kasulu, Shinyanga
Kasulu, Sumbawanga (M), Vijijini, Shinyanga Manispaa, Kishapu, Sumbawanga
Sumbawanga (V), Njombe, Vijijini, Sumbawanga Manispaa, Mbeya Vijijini, Mbeya
Kilombero, Same, Monduli, Jiji, Njombe, Iringa Vijijini, Iringa Manispaa, Kilolo,
Karagwe, Singida (M), Singida Kilombero, Rufiji, Same, Lushoto, Monduli, Arumeru,
(V), Dodoma (V), Ilala, Karagwe, Musoma Vijijini, Musoma Manispaa, Tarime
Mkuranga, Kilosa, Mwanga, na Geita.
Lushoto, Arumeru, Babati,
Geita, Tarime, Bukoba (M),
Bukoba (V), Iringa (M), Iringa
(V), Mbeya (J), Mbeya (V),
Mtwara Mikindani, Songea,(M),
Songea (V) na Lindi (M).
(d) Kutoa mafunzo ya mwezi Mafunzo ya Uongozi wa Elimu ngazi ya cheti kwa
mmoja ya Cheti cha Uongozi Walimu Wakuu wa Shule za Msingi 127 kati ya 1,000
na Uendeshaji Elimu kwa waliokusudiwa yalitolewa.
Walimu Wakuu wa Shule za
Msingi 1,000 katika kanda zote
za kielimu kupitia Vyuo vya
Ualimu.
(e) Kuendesha mafunzo ya Mafunzo ya OPRAS kwa viongozi wa kielimu 700
OPRAS kwa Maafisa Elimu ambao ni Maafisa Elimu Mkoa na Wilaya, Wakuu wa
Mkoa na Wilaya, Wakuu wa Shule za Sekondari, Wakaguzi wa Shule (W) na
Shule za Sekondari, Wakaguzi Makatibu wa Idara ya Utumishi wa Walimu yametolewa.
wa Shule (W), na Makatibu wa
Idara ya Utumishi wa Walimu.
Mafunzo hayo yataendeshwa
katika kanda ya Nyanda za
Juu, Magharibi, Ziwa na Kanda
ya Kaskazini.
(f) Kutoa mafunzo ya mwezi Mafunzo ya uongozi kwa Maafisa Elimu vifaa na
mmoja ya Uongozi na Takwimu na Maafisa Elimu Taaluma 116 katika ngazi
Uendeshaji wa Elimu kwa ya Wilaya kutoka Mikoa ya Tabora, Pwani, Morogoro,
maafisa Elimu wa Wilaya Mara, na Manyara yametolewa.
Taaluma, Vifaa na Takwimu 40
kwa mikoa ya Tabora na
Pwani.
271
(g) Kutoa mafunzo ya wiki mbili ya Mafunzo elekezi ya wiki mbili kwa uongozi wa elimu
Uongozi wa Elimu kwa kwa wajumbe wa bodi za Shule za Sekondari 2,500,
wajumbe wa Bodi za Shule za kutoka katika kanda nne (4) yalifanyika.
Sekondari kutoka kanda zote
za Elimu.
(h) Kutoa mafunzo ya wiki mbili ya Mafunzo kwa Timu za Menejimenti za shule za
Uendeshaji kwa Timu za sekondari yameendeshwa katika mikoa ya: Pwani,
Menejimenti za Shule za Singida, Rukwa, Lindi na Kigoma. Washirki 1,351
Sekondari 1,400 kutoka kanda wamehudhuria mafunzo hayo.
zote za kielimu.
(i) Kuendesha tafiti za kielimu kwa Tafiti nne (4) za uongozi na uboreshaji wa taasisi za
kushirikiana na nchi za Malawi, elimu zinaendelea kwa ushirikiano na Malawi, Uganda
Zambia, Msumbiji na Afrika ya na Afrika ya Kusini.
Kusini. Tafiti hizo zinahusu
uboreshaji wa Uongozi,
Kutathmini mahitaji ya
Mafunzo, Tabia za Viongozi na
Mifano Bora ya Uongozi katika
Shule za Msingi.
12. (a) Kuendesha mafunzo ya Jumla ya walengwa 182 (Me 119 na Ke 63) walipewa
stashahada ya juu kwa mafunzo ya Stashahada ya juu kwa mwaka wa kwanza
walengwa 124 na stashahada na wa pili, na pia walengwa 261 (Me 151 na Ke 110)
ya kawaida ya Elimu ya Watu walipewa mafunzo ya kawaida mwaka wa kwanza na
Wazima kwa walengwa 260. wa pili.
(b) Kutoa elimu ya Sekondari kwa Walengwa 16,801 (Me 7,596 na Ke 9,205) wa masomo
walioikosa kwa njia ya masafa ya ana kwa ana na Elimu masafa wameandikishwa na
au posta kwa walengwa wanaendelea na masomo.
30,000 katika mikoa yote
Tanzania bara.
(c) Kuchapa moduli za masomo ya Nakala 500 za “Studies in Adult Education”(SAED) Na
Uraia, Kiingereza, Kiswahili, 63 na 500 za “Journal of Adult Education” Na 15
Historia, Jiografia, Hisabati na zilichapwa na kusambazwa.
Baiolojia za elimu kwa masafa,
hatua ya pili Kuandaa na
kuchapisha majarida ya
“Studies in Adult Education
(SAED) Na. 63 “Journal of
Adult Education Tanzania
(JAET) Na. 15, na “Alumni
News letter” kwa ajili ya
kufahamisha jamii kazi za
Taasisi ya Elimu ya Watu
Wazima.
(d) Kuongeza idadi ya wanafunzi Wanachuo 190 (Me 137 na Ke 53) wanaendelea
wa Cheti cha Sheria kutoka kusoma Mafunzo ya cheti cha sheria.
272
168 hadi kufikia 200.
(e) Kuendelea kutoa mafunzo ya Jumla ya wafanyakazi 112 wamepata mafunzo
kuendeleza wafanyakazi wa mbalimbali kama ifuatavyo: Shahada ya uzamili
Wizara katika mafunzo ya wafanyakazi 3, Stashahada ya juu wafanyakazi 3,
Shahada ya Udaktari wa Stashahada ya kompyuta na uongozi 2, Masomo ya
Falsafa 1, Shahada ya Uzamili sekondari 21 na Mafunzo ya muda mfupi wafanyakazi
4, Elimu ya sekondari kwa 85.
watumishi 40 ambao hawana
elimu hiyo na mafunzo ya
muda mfupi kwa watumishi 60.
(f) Kufanya ukarabati wa chumba Viwanja vya ujenzi wa ofisi katika mikoa ya Dodoma na
cha Studio Makao Makuu na Manyara vimenunuliwa.
kuanza kujenga kituo cha
masomo eneo la Kisota Dar es
Salaam na kununua nyumba
mbili kwa ajili ya ofisi za mikoa
ya Mwanza na Shinyanga
ambapo hakuna majengo ya
Taasisi.
(g) Kuimarisha shughuli za TEWW Mtandao wa internet umefungwa makao makuu ya
kwa kuweka mtandao wa TEWW na watumishi 35 wameajiriwa.
“internet” katika vituo 21 vya
Elimu ya Watu Wazima mikoa
yote, kuajiri watumishi 72 wa
kada mbalimbali na kuomba
kibali cha ajira mpya 14 na
mbadala 8 kwa wafanyakazi
wa kada za utaalamu.
(h) Kuimarisha uendeshaji na Magari 5 yamenunuliwa kwa Mikoa ya Arusha,
usimamizi wa Elimu Masafa Dodoma, Ruvuma, Dar-es-salaam na Makao Makuu.
kwa kununua magari 5 kwa ajili
ya Kanda ya Ziwa, Mashariki,
Magharibi, Kaskazini Magharibi
na Kusini.
13. (a) Kuendesha mikutano ya paneli Mikutano ya Panel za masomo kumi (10) imefanyika
za masomo 10 kwa Shule za katika elimu ya Msingi, Sekondari na Ualimu.
Msingi na za Sekondari.
(b) Kufaragua (Improvise) zana za Zana za kufundishia na kujifunzia Elimu ya Awali
kufundishia na kujifunzia kwa zimeandaliwa.
ajili ya Shule za Elimu ya Awali.
(c) Kuandaa Mitaala na Mihtasari Mtaala na Mihtasari 27 ya ualimu ngazi ya Cheti na
ya Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada imeandaliwa. Aidha, Mwongozo wa Mtaala
Stashahada ili iendane na wa Ualimu ngazi ya cheti umeandaliwa.
Mitaala iliyorekebishwa.
273
(d) Kuandaa Miongozo ya Miongozo ya uandishi wa moduli 24 za kufundishia
kufundishia masomo ya masomo ya Sekondari kidato cha I hadi IV kulingana
sekondari ya kidato cha I-IV na mtaala mpya imeandaliwa.
kulingana na mtaala mpya.
(e) Kufuatilia utekelezaji wa Mitaala Ufuatiliaji umefanyika juu ya utekelezaji wa Mtaala wa
ya Elimu ya Msingi na Elimu ya Msingi katika kanda zote za elimu ili kupata
Sekondari. taarifa kwa ajili ya uboreshaji.
(f) Kuandaa vipindi sita (6) vya Maandalizi ya kazi hii bado yanaendelea mafunzo ya
radio na televisheni vya namna ya kutumia vifaa vya kurekodia yamefanyika.
kufundisha masomo ya Elimu
ya Msingi vya Hisabati na
Kiingereza darasa la III na IV
(g) Kuchapisha na kusambaza Mwongozo wa Taifa wa Ukuzaji Mitaala unaendelea
kwa wadau wa elimu kuboreshwa ili uweze kuchapwa na kusambazwa kwa
Mwongozo wa Taifa wa wadau wa elimu.
Ukuzaji Mitaala.
(h) Kurekebisha vitabu 12 vya Vitabu 24 vya MEMKWA vya mwaka wa tatu kwa kundi
MEMKWA vya mwaka wa tatu. rika la kwanza na la pili vimerekebishwa.
(i) Kutoa mafunzo kwa Mafunzo kwa wawezeshaji 30 yamefanyika kwa ajili ya
wawezeshaji kwa ajili ya upanuzi wa shughuli za MEMKWA katika Wilaya ya
upanuzi wa shughuli za Makete.
MEMKWA katika Wilaya ya
Makete.
(j) Kutoa mafunzo kwa wakuza Mafunzo kwa wakuza mitaala 25 na wafanyakazi
mitaala 15 na wafanyakazi wawezeshaji 10 wa TET yametolewa kikamilifu.
waendeshaji 10 wa Taasisi ya
Elimu Tanzania katika maeneo
yao ya kitaalamu.
(k) Kuendesha Semina tatu (3) za Jumla ya semina tatu (3) za kitaalamu ziliendeshwa
mafunzo ya kitaalamu kwa kwa wafanyakazi 85 wa TET kuhusu utumiaji wa
wafanyakazi wa TET kuhusu TEHAMA.
utumiaji wa Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano
(TEHAMA).
(l) Kuendesha mafunzo yahusuyo Mafunzo yanayohusu mitaala iliyoboreshwa kwa
Mitaala iliyorekebishwa kwa walimu wa shule za msingi pamoja na wakaguzi wa
walimu wa shule za msingi na shule yamefanyika.
sekondari, wakufunzi wa vyuo
Vya Ualimu na Wakaguzi wa
Shule
(m) Kuandika mihtasari ya Historia, Mihtasari ya Masomo ya Uraia na jiografia pamoja na
Uraia na Jiografia kwa ajili ya vitabu vya masomo hayo kwa darasa la III kwa shule za
shule za msingi na Fizikia na msingi na mihtasari ya fizikia na Kemia kwa shule za
Kemia kwa ajili ya shule za sekondari imerekebishwa.
sekondari.
274
(n) Kudurusu mihtasari ya Andiko la kufanya utafiti ili kupata maoni ya wadau
masomo ya sekondari ya kuhusu mihtasari ya masomo ya sekondari kidato cha 5
kidato cha 5 hadi 6. na 6 limeandaliwa.
(o) Kuaandaa mwongozo wa Mwongozo wa kuboresha masomo ya michepuo
kurekebisha masomo ya umeandikwa.
michepuo ili kuainisha masomo
ya ufundi Kilimo, Biashara,
Sayansi Kimu na Mafunzo ya
Ufundi Stadi yanayotolewa na
VETA.
14. (a) Kuimarisha na kuboresha Machapisho 7,226 yaliongezeka kati ya hayo: Vitabu
huduma katika mikoa 18 yenye vilivyonunuliwa ni 4,300; vilivyopatikana kwa mujibu wa
maktaba kwa kuongeza Sheria 164; vilivyopatikana kwa misaada ni 2,762; jumla
machapisho 40,000. ya magazeti na majarida ni 6,618. Kati ya hayo,
magazeti ni 5,864 na majarida 754 ; Idadi ya Vitabu
vyote ni 810,060 na Idadi ya magazeti na Majarida yote
ni 496,570.
(b) Kutoa makala 2 za orodha ya Toleo la mwaka 1999 hadi 2001 limekamilika na toleo la
vitabu na machapisho mengine 2002 linaendelea kutayarishwa.
yanayochapishwa nchini
(Tanzania National
Bibliography-TNB).
(c) Kuendeleza ujenzi wa awamu Hatua ya kwanza na ya pili ya ujenzi wa sehemu ya
ya tatu ya Maktaba ya Mkoa chini na gorofa ya kwanza ya maktaba ya Dodoma
wa Dodoma kwa kujenga imekamilika na huduma imeanza kutolewa. Hatua ya
Ukumbi wa mikutano na tatu inakamilishwa kwa ununuzi wa samani za shilingi
ununuzi wa samani. milioni 18 na kuandaa michoro kwa ajili ya ujenzi wa
ukumbi wa mikutano.
(d) Kuendeleza ujenzi wa Chuo Awamu ya kwanza ya ujenzi wa madarasa na ofisi za
cha Ukutubi na Uhifadhi utawala umefikia asilimia 97.
Nyaraka Bagamoyo kwa
kujenga mabweni, jiko na
ununuzi wa samani na vifaa.
(e) Kukarabati majengo ya Maktaba ya wilaya ya Njombe, Kagera na Singida
maktaba za mikoa ya Ruvuma, zimefanyiwa ukarabati.
Mtwara na Kagera.
(f) Kuboresha Maktaba za Shule Elimu ilitolewa kuhusu matumizi ya Maktaba kwa shule
za sekondari 21 na Vyuo vya za sekondari na Msingi 3,105 na Taasisi 90
Ualimu 10 nchini kwa kutoa zilitembelewa. Aidha, kitengo cha "Multimedia"
mafunzo ya ukutubi kwa kiliendesha vipindi vya hadithi, kazi za mikono, usanii,
watumishi husika na uandishi, uchoraji, utumiaji wa kompyuta na maandalizi
kuimarisha huduma za watoto ya vipindi vya maonesho katika televisheni.
nchini.
275
(g) Kuanzisha Maktaba mpya Uongozi wa Mkoa wa Singida umekabidhi kwa Bodi hati
katika mikoa ya Singida, Pwani miliki ya kiwanja Na. 174 kilichoko Singida mjini. Aidha,
na Manyara. vyumba vitatu (3) vilivyotengwa kwa ajili ya kuanza
huduma za maktaba ya muda ya Mkoa vimekarabatiwa
na mkutubi ameteuliwa. Mkoa wa Pwani Kiwanja
kimepatikana. Bodi inafuatilia hati miliki. Katika Mkoa wa
Manyara uongozi unafanya mawasiliano na
wahusika/watawala wa mkoa huo kuhusu uanzishaji wa
maktaba.
(h) Kununua magari matatu (3) Chuo cha ukutubi Bagamoyo kimepata gari. Aidha,
kwa ajili ya Bodi, Chuo cha Bodi inaendelea kufanya juhudi ya kutafuta fedha ili
Ukutubi na Wasioona. kupata gari la kusambaza vitabu mashuleni na vyuoni
(Mobile Library Service).
(i) Kupanua na kuongeza uwezo Watumishi wa Bodi 19 waliokuwa mafunzoni
na ujuzi wa wafanyakazi wa wanaendelea na masomo.
maktaba za umma kwa kutoa
mafunzo katika ngazi za cheti,
stashahada, shahada, shahada
ya uzamili na mafunzo ya
Muda mfupi.
15. (a) Kufanya utafiti tathmini, usanifu Karatasi 27 za Maswali ya Mtihani wa Kumaliza
na kuinua ubora wa Mitihani Elimu ya Msingi 2006 kwa masomo ya Kiswahili,
mbalimbali ya Kitaifa. Kiingereza, Maarifa ya Jamii, Hisabati na Sayansi
zilirekebishwa na kuhakikiwa.
Mafunzo ya ndani (In-House Training) kwa waajiriwa
wapya 15 juu ya utunzi na urekebishaji bora wa
Maswali ya Mtihani Kitaifa yaliendeshwa.
(b) Kuendesha mitihani ya Mitihani katika ngazi mbalimbali iliendeshwa ikiwemo
Kumaliza Elimu ya Msingi, Mitihani ya kumaliza Elimu ya Msingi Septemba, 2006,
Maarifa, Kidato cha nne (4) na Kidato cha nne (4), Ualimu daraja III A na mtihani wa
sita (6), Ualimu Daraja A na maarifa Oktoba, 2006, kidato cha sita (6) na
Stashahada ya Ualimu. Stashahada ya Ualimu Februari, 2007, Ufundi Mei,
2007.
(c.) Kuendesha mitihani ya Cheti Watahiniwa 663 walifanya mitihani ya Ufundi, kati yao
cha Ufundi Sanifu na 313 walifaulu sawa na asilimia 47.2.
Stashahada ya Juu ya
Uhandisi kwa niaba ya Baraza
la Taifa la Elimu ya Ufundi
(NACTE).
(d) Kusimamia mitihani ya nje Usimamiaji wa mitihani itolewayo na Bodi za nje ya nchi
inayofanywa na watahiniwa uliendelea. Baraza lilisimamia mitihani ya nje kwa niaba
binafsi hapa nchini. ya Taasisi za Uingereza.
276
(e) Kukamilisha ujenzi wa Kituo Ujenzi wa kituo cha usahihishaji Mitihani cha Mbezi
cha Kusahihishia Mitihani cha Wani unaendelea.
Mbezi Wani.
(f) Kutoa mafunzo yenye lengo la Mafunzo yametolewa kwa wafanyakazi wote kwa lengo
kupunguza maambukizi ya la kupunguza maambukizi ya virusi vya UKIMWI.
virusi vya UKIMWI, kifua kikuu,
malaria, ukoma na kisukari.
16. (a) Kukamilisha ukarabati kwa Mkataba wa ununuzi wa vifaa kwa ajili ya vyuo vya
kufunga vifaa katika vyuo vya ufundi stadi vya Mara, Kagera, Songea, Mikumi, Arusha
ufundi stadi vya Mara, Kagera, na Dakawa umesainiwa.
Dakawa, Mikumi, Songea,
Oljoro na Kigoma.
(b) Kuendelea na ukarabati na Makandarasi kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa vyuo
upanuzi wa vyuo vya ufundi vya Ufundi Stadi vya Shinyanga, Mpanda, Tabora,
stadi vya Shinyanga, Mpanda, Ulyankulu, Singida na ujenzi wa Chuo kipya cha Hoteli
Tabora Ulyankulu na Dakawa. Arusha kwa kushirikiana na ADB wamepatikana na
ujenzi umeanza.
(c) Kuanza ujenzi wa vyuo vipya Mchakato wa kuwapata makandarasi kwa ajili ya ujenzi
vya Arusha, Singida, Pwani, wa vyuo vipya vya ufundi stadi vya Lindi, Manyara,
Manyara, Lindi na kituo cha Pwani na Dar es Salaam kwa kushirikiana na Serikali ya
Habari Teknolojia na Korea ya Kusini umeanza.
mawasiliano (ICT) Dar es
Salaam.
(d) Kuhamasisha na kuvisaidia Vyuo vya Asasi zisizo za Serikali vimesaidiwa kikanda
vyuo vya Ufundi Stadi vya kama ifuatavyo :
Asasi Zisizo za Serikali, watu Dsm - (42,249,000/=) ;
binafsi na taasisi za kidini ili Ziwa - (41,990,000/=) ;
viweze kukuza na kuboresha Magharibi - (1,828,000/=) ;
mafunzo yanayotolewa. Kusini Mashariki –(40,280,000/=) ;
Mashariki - (62,113,000/=) ;
Nyanda za Juu - (41,021,000/=) ;
Kaskazini - (90,788,000/=) ;
Kusini Magharibi - (10,665,000/=) ;
Kati - (59,928,000/=)
Jumla kuu 400,862,000/=.
(e) Kuandaa mkakati wa Mkakati wa utekelezaji wa mpango wa uanzishaji wa
utekelezaji wa Mpango wa vyuo vya Ufundi Stadi kila Wilaya umeandaliwa. Aidha,
Uanzishaji wa Vyuo vya Ufundi kamati maalumu yenye kushirikisha wajumbe 11
Stadi kila Wilaya. kutoka wizara na taasisi mbalimbali imeundwa na
Imeshakutana mara mbili kujali namna ya kufanya kazi
hiyo.
(f) Kuboresha viwango vya Mitaala ya mafunzo imeboreshwa ki-sekta. Mtaala wa
mafunzo yanayotolewa kwa sekta ya Hoteli na Utalii umekamilika na sasa
kutoa mitaala inayolingana na unafanyiwa majaribio (piloting).
mahitaji ya soko la ajira, chini
277
ya utaratibu wa mafunzo ya
CBET kulingana na mahitaji ya
mfumo wa mafunzo hayo.
(g) Kujiunga na kazi ya ualimu wa Mafunzo ya taaluma (technical skills upgrading) kwa
ufundi. walimu wa Ufundi Stadi 140 yametolewa.
(h) Kukuza na kuboresha mafunzo Mafunzo kwa ajili ya sekta isiyo rasmi yamekuzwa
yanayotolewa kwa sekta isiyo kupitia kozi fupi fupi kwa wanafunzi 18,788 ambapo
rasmi ikiwa ni pamoja na sekta asilimia 27 ni wasichana.
ya kilimo ili kutoa fursa kwa
walengwa kujipatia stadi na
kukuza ajira na kuboresha
Kilimo.
(i) Kupanua utekelezaji wa Kitabu cha maelekezo (INTEP) kimefanyiwa
utaratibu mpya “Integrated marekebisho kwa lengo la kupanua na kuboresha
Training for Entrepreneural utekelezaji.
Promotion” (INTEP) unaolenga
sekta isiyo rasmi kwa kubaini
fursa za kiuchumi zilizopo
katika jamii na kutoa mafunzo
kulingana na fursa hizo.
278
WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
NA. AHADI UTEKELEZAJI
1. Kutoa mafunzo ya rejea kuhusu Jumla ya watumishi 301 wa Maendeleo ya Jamii kutoka
uandishi wa miradi (Project write ups) kwenye Halmashauri za Wilaya za Mikoa ya Tanga,
kwa watumishi wa Maendeleo ya Lindi, Mtwara, Mbeya, Rukwa, Ruvuma, Iringa,
Jamii kutoka kwenye Halmashauri Dodoma, Morogoro, Singida, Manyara, Kilimanjaro,
Arusha na Pwani wamepatiwa mafunzo hayo.
2. Kununua pikipiki 15 ambazo Jumla ya pikipiki 10 zimenunuliwa na kugawiwa katika
zitagawiwa katika Halmashauri 15 kwa Halmashauri 10 zifuatazo: Handeni, Rombo, Uyui,
ajili ya matumizi ya Maafisa Maendeleo Muheza, Iringa, Songea, Morogoro, Singida (V),
ya Jamii. Shinyanga na Ikwiriri.
3. Kuandaa mitaala ya Maendeleo ya Mitaala ya Stashahada imeandaliwa na imekamilika.
Jamii katika ngazi ya Stashahada Aidha, mitaala ya Astashahada imedurusiwa.
katika Vyuo vya Rungemba, Misungwi
na Buhare kwa mwaka 2007/08.
4. Kuboresha mazingira ya Chuo cha Ujenzi wa jengo la Mihadhara umeanza na unaendelea.
Tengeru kwa kukamilisha ujenzi wa Michoro ya awali ya Usanifu wa jengo la Maktaba
jengo la maktaba, Mihadhara na imekamilika. Matengenezo ya Ofisi na ujenzi
matengenezo ya Ofisi. haukufanyika kutokana na ufinyu wa bajeti.
5. Kuweka vifaa vya kisasa vya Vifaa zikiwemo kompyuta na „satellite dish‟
mawasiliano, kukuza matumizi ya vimenunuliwa na kufungwa Chuoni Tengeru. Tovuti ya
Teknolojia katika Chuo cha Tengeru. Chuo tayari imezinduliwa na inafanya kazi.
6. Kutoa mafunzo ya kompyuta kwa Mtumishi mmoja tu amepata mafunzo hayo kutokana
watumishi 20 wa Chuo cha Tengeru. na ufinyu wa bajeti.
7. Kutoa mafunzo kwa wanachuo 810 Jumla ya wananchuo 1,235 wamepatiwa mafunzo.
wanawake kwa wanaume katika Chuo Aidha, mafunzo yanaendelea kutolewa katika Vyuo
cha Tengeru katika ngazi ya vyote vinne (4) vya Maendeleo ya Jamii.
Stashahada ya Juu na wanachuo 600
katika ngazi ya cheti kwa Vyuo vya
Maendeleo ya Jamii, Missungwi,
Buhare na Rungemba.
8. Kufanya ukarabati mkubwa katika Kiasi cha shilingi 180,000,000 zimepelekwa Buhare na
Chuo cha Buhare ambapo Chuo cha kazi ya ukarabati wa nyumba za walimu, ujenzi wa
Rungemba kitafanyiwa ukarabati maktaba mpya na ukumbi wa chakula inaendelea.
mdogo. Aidha, kiasi cha Shilingi 54, 000,000 zimepelekwa
Rungemba na kazi inaendelea. Ukarabati wa nyumba
4 za walimu ulitekelezwa na utamalizika mwanzoni
mwa Julai, 2007. Aidha Chuo cha Buhangija pia
kilipata jumla ya shilingi 35,668,500 kwa ajili ya
ukarabati wa majengo yake.
9. Kutoa mafunzo ya stadi za kazi mbali Jumla ya wananchi 27,907 wakiwemo wanawake
mbali katika vyuo 58 vya Maendeleo 13,054 na wanaume 14,853, wamepatiwa mafunzo ya
ya Wananchi kwa makundi ya stadi mbali mbali za kazi.
wanawake, vijana, wazee na
279
walemavu.
10. Kuimarisha majengo na miundombinu Fedha zilizopatikana Shilingi 118,571,000 zimetumwa
katika vyuo vinne (4) vya Chala, kwenye Vyuo vya Chilala, Munguri na Malampaka.
Chilala, Kiwanda na Malya.
11. Kuweka mitambo ya umeme Chuo cha Chisalu kimepatiwa Shilingi 35,000,000/=
unaotokana na nguvu za jua (Solar kwa ajili ya kazi ya kuweka mitambo ya umeme
Power) katika Chuo cha Chilala, utokanao na nguvu za jua. Aidha Chuo cha Ulembwe
Muhukuru na Ulembwe na kuwezesha kimepewa shilingi milioni 35 na Mhukuru kimepewa
upimaji wa maeneo kwenye vyuo shilingi milioni 29 kwa kazi hiyo hiyo. Chuo cha Chilala
thelathini. kimefanyiwa ukarabati wa majengo kwanza, upimaji wa
maeneo ya Vyuo unaendelea kama ifuatavyo:
Handeni - (600,000/-);
Masasi - (1,104,000/-);
Mamtukuna - (2,100,000/-);
Nzega - (600,000/-);
Ifakara - (1,448,000/-);
Bariadi - (391,800/-);
Muhukuru - (1,500,000/-);
Rubondo - (1,100,000/-);
Mlale - ( 3,883,000/-);
Ulembwe - (2,064,000/-);
Malampaka - (945,000/-);
Ilula - (1,448,000/-);
Nandembo - (2,500,000/-);
Kibondo - (818,000/-).
12. Kununua pikipiki 10 kwa ajili ya Vyuo Pikipiki 8 zimenunuliwa na zitapelekwa katika Vyuo vya
vya Chala, Chilala, Chisalu, Kiwanda, Chilala, Chisalu, Msaginya, Sofi, Muhukuru, Mlale,
Nzega, Malampaka, Mlale, Msaginya, Kiwanda na Chala.
Msingi, Muhukuru na Sofi.
13. Kudurusu Mkakati wa Kuwakinga Kazi ya kudurusu Mkakati wa Kuwakinga Wanawake na
Wanawake na Watoto Dhidi ya Watoto Dhidi ya UKIMWI imekamilika na utasambazwa
UKIMWI na Magonjwa ya Zinaa na kwa wadau.
kuusambaza Mkakati huo kwenye
Halmashauri.
14. Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka Maafisa Maendeleo ya Jamii 301 kutoka mikoa ya
Mikoa ya Iringa, Mbeya, Ruvuma, Iringa, Lindi, Mtwara, Mbeya, Rukwa, Ruvuma,
Singida na Tabora watapatiwa Dodoma, Morogoro, Kilimanjaro, Arusha na Pwani
mafunzo ya Mbinu Shirikishi walipatiwa mafunzo ya mbinu shirikishi jamii (Mapping)
yatakayowezesha kuandaa mipango ya kupambana na UKIMWI.
ya kukabiliana na janga la UKIMWI.
15. Kuhamasisha wanawake waanzishe Mafunzo ya Uhamasishaji na Uanzishaji wa Vyama vya
vyama vya wanawake vya ushirika vya Ushirika vya Kuweka na Kukopa yaliendeshwa kwa
kuweka na kukopa (SACCOS). wanawake na Maafisa Maendeleo ya Jamii ngazi ya
Wilaya na Kata. Jumla ya washiriki 30 na wanawake
280
wajasiriamali 40 walihudhuria mafunzo hayo.
16. Kukamilisha mchakato wa kuanzisha Benki imesajiliwa na kupatiwa jina la „Benki ya
Benki ya Wanawake. Wanawake Tanzania Ltd‟, Kanuni za Makampuni
imeandaliwa na kutiwa saini. Aidha, Benki imefungua
akaunti ya ASCROW Na.011103028717 katika Benki
ya Biashara ya Taifa (NBC) Ltd, tawi la Corporate,
Mkakati wa upatikanaji wa hisa umeandaliwa.
17. Kutoa mafunzo kwa Maafisa wa Mafunzo haya yalifanyika kwa Maafisia wa Serikali
Serikali wanaosimamia utekelezaji wa wapatao 100 kutoka mikoa ya Tabora, Singida,
sheria na upatikanaji wa haki katika Dodoma, Kilimanjaro, Kigoma, Pwani, Dar es Salaam
jamii. na Morogoro.
18. Kuelimisha Maafisa Maendeleo ya Mafunzo haya yamefanyika mwezi Juni, 2007.
Jamii ngazi ya Kata kuhusu utunzaji
wa taarifa na takwimu za wanawake na
wanaume waliodhurika na vitendo vya
ukatili.
19. Kuelimisha jamii kuhusu Sheria za Mafunzo haya kwa jamii yalifanyika kwa Maafisa wa
Makosa ya Kujamiiana (1998), Sheria Serikali wapatao 100 kutoka mikoa ya Tabora, Singida,
ya Ardhi na Sheria ya Ardhi Vijijini Dodoma, Kilimanjaro, Kigoma, Pwani, Dar es Salaam
(1999). na Morogoro.
20. Kutoa mafunzo ya ujasiriamali na Wanawake wajasiriamali wapatao 200 walipatiwa
ushauri nasaha kwa wanawake 200 mafunzo ya ujasiriamali na ushauri nasaha katika
waliobainishwa na mitandao yao kipindi cha Januari-Machi, 2007. Wanawake hawa
ambao watatoa mafunzo kwa wengine. walitoka Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA),
Wanawake waishio na virusi vya UKIMWI na
Walemavu wengine. Mafunzo haya yalifanyika Dar es
Salaam.
21. Kuandaa mpango utakaohakikisha Mkakati wa Taifa wa kuwasaidia watoto yatima na
watoto wanaondolewa mitaani na waishio katika mazingira magumu zaidi wakiwemo
wanapatiwa elimu kama haki yao ya watoto wa mitaani umeandaliwa na kuwasilishwa katika
msingi na kuwaunganisha na familia sekretariati ya Baraza la Mawaziri. Vilevile kumefanyika
zao. utafiti kuhusu jukumu la familia na jamii katika
kupunguza ongezeko la watoto wa mitaani na
wanaoishi katika mazingira magumu zaidi katika mikoa
ya Iringa, Dodoma na Mwanza. Haya yote yatasaidia
kuwahusisha wadau mbalimbali kuweza kuwasaidia
watoto hao waweze kuunganishwa na familia zao.
22. Kuandaa Mkakati wa Taifa wa Elimu Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa
ya Malezi ya Watoto Wachanga chini masuala ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya
ya Umri wa Miaka Minane (8). Mtoto imeandaaa mafunzo ya kuratibu utekelezaji wa
shughuli zinazofanywa na taasisi za Serikali na zisizo
za kiserikali ili kuboresha taasisi za Serikali na zisizo za
kiserikali katika utoaji wa malezi ya awali ya watoto.
Aidha, hivi sasa mchakato wa kuandaa Mkakati wa
Taifa wa Elimu ya Malezi ya Watoto Wachanga chini ya
281
umri wa miaka minne 8 unaandaliwa na wataalamu
washauri.
23. Kuelimisha familia na jamii kuhusu Kitini cha Jamii cha Elimu ya Idadi ya Watu na Maisha
malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya Familia kimeshaandaliwa. Kitini hicho kitaanza
ya mtoto ili kuongeza uelewa kuhusu kutumika kufundishia Jamii/Familia katika mwaka wa
elimu ya Idadi ya watu na familia kwa fedha 2007/2008.
kupitia Maafisa Maendeleo ya Jamii
katika Halmashauri na vyombo vya
Habari.
24. Kuandaa zana za habari, elimu na Zana zitaandaliwa baada ya kuchapishwa kwa Kitini
ushawishi kwa lengo la kutoa mafunzo katika mwaka wa fedha 2007/2008.
kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii 260
katika ngazi za Kata.
25. Kuelimisha jamii na familia kuhusu haki Mafunzo ya haki za mtoto kulingana na mikataba ya
za msingi za watoto kulingana na kimataifa ya haki na ustawi wa mtoto yalitolewa kwa
mikataba ya kimataifa ya haki na Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka ngazi ya Wilaya,
ustawi wa mtoto. pamoja na Wakuu wa Vyuo vya Maendeleo ya
Wananchi katika mikoa yote isipokuwa mikoa ya Lindi,
Mtwara, Kigoma, Tabora na Shinyanga.
26. Kwa kushirikiana na Shirika la Umoja Wizara kwa kushirikiana na UNICEF imewezesha
wa Mataifa la Kuhudumia Watoto Mtandao wa Harakati za Watoto (TMC) kuendeleza
(UNICEF) Wizara itaendelea shughuli zake na kuwa na vikao vya wadau
kuwezesha mtandao wa harakati za vinavyotakiwa mara kwa mara. TMC inapata misaada
Watoto. (Tanzania Movement for and kutoka UNICEF ambapo Wizara inasaidia kutoa
with Children). utalaam.
27. Kushirikisha watoto katika kutoa Rasimu ya „Kitabu cha Mbiu – Shawishi na Mbinu
mawazo yao na kusikika katika Shirikishi’ kwa watoto kimeandaliwa katika mwaka huu
masuala yanayohusu maslahi na wa fedha. Kitabu hicho kitasaidia kuwapatia watoto
ustawi wao na kuanzisha Mabaraza ya ujuzi na uelewa kushiriki katika masuala mbalimbali ya
Watoto katika ngazi ya Mkoa na kitaifa. Hadi sasa mikoa 19 imeunda mabaraza ya
Wilaya. watoto.
28. Kuyawezesha Mashirika yasiyo ya Idara ilipata nafasi ya kuhudhuria Warsha ya Mafunzo
Kiserikali kuyawezesha kushiriki kwa Vyama vya Kiraia (CSOs) na kutoa mada kuhusu
kikamilifu katika kuleta maendeleo ya jukumu lao katika utekelezaji wa MKUKUTA. Warsha
Kijamii na Kiuchumi katika utekelezaji hii ilifanyika mkoani Kilimanjaro tarehe 24-2/06/2006 na
wa MKUKUTA na malengo ya Milenia. Morogoro tarehe 1 – 2/06/2006. Warsha hii
ilihudhuriwa na wajumbe 100. Wizara iliwaelimisha kwa
kina kuhusu jukumu la NGOs katika utekelezaji wa
MKUKUTA.
29 Kutafsiri Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Utekelezaji wa ahadi hii ulipangwa kufanyika katika
Kiserikali (NGOs) Na. 24/2002 katika robo ya 3 na 4 ya mwaka wa fedha 2006/07. Hata
lugha ya Kiswahili kuwawezesha hivyo kazi hii haikufanyika kutokana na mtiririko wa
wadau wengi kuielewa. fedha kutoka Hazina kutokuwa mzuri. Kazi hii sasa
inatarajiwa kufanyika katika kipindi cha mwaka wa
fedha 2007/2008.
282
30. Kuimarisha mifumo ya mawasiliano Wizara imepokea jumla ya taarifa za NGOs 250 kati ya
miongoni mwa Wadau wa Sekta ya hizi taarifa za kazi za mwaka ni 150 na taarifa za fedha
Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na za NGOs ni 100. Taarifa hizo zimechambuliwa na
kuendelea kuimarisha Benki ya kufanyiwa tathmini pamoja na kuziingiza kwenye Benki
Takwimu za Mashirika Yasiyo ya ya Takwimu ya Wizara. Taarifa hizi pia
Kiserikali. zimesambazwa kwa wateja kulingana na mahitaji yao.
31. Kuwezesha kuwepo kwa mkakati wa Mkakati wa mawasiliano utaweza kuwepo na kufanya
Mawasiliano, Kitabu cha Orodha kazi mara baada ya Baraza la Taifa la NGOs
(NGOs Directory), Kitabu cha Taarifa kukamilisha Kanuni za Maadili ya NGOs.
ya mwaka ya Sekta ya Mashirika
Yasiyo ya Kiserikali na kuboresha Kitabu cha Orodha ya NGOs (NGO‟s Directory)
taarifa ya sekta hii katika Tovuti ya hakikuandaliwa na kuchapishwa, lakini Benki ya
Taifa. Takwimu ya NGOs inazo taarifa zote za NGOs
zilizosajiliwa chini ya Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka
2002, taarifa za kazi za NGOs za mwaka na taarifa za
fedha.
32. Kuendelea kuweka kumbukumbu Mfumo wa computer (Gender Sensitive Monitoring and
muhimu katika tovuti ya Wizara ili Evaluation System) unafanyiwa majaribio na wakufunzi
taarifa zinazohusu Wanawake na wa “University Computing Centre” wanaendelea
Watoto, Maendeleo ya Jamii na Jinsia kurekebisha upungufu uliyojitokeza. Uingizaji wa
ziweze kusambazwa kwa wadau kumbukumbu utaanza mara baada ya mfumo kuanza
mbalimbali. kufanya kazi kikamilifu, mfumo huo umeanza kutumika
rasmi mwezi Januari, 2007.
33. Kuanzisha mchakato wa kudurusu Ilionekana kuwa Sera ya Maendeleo ya Wanawake na
Sera ya Maendeleo ya Wanawake na Jinsia ya mwaka 2000 bado inahitajika. Hivyo Wizara
Jinsia ya Mwaka 2000. Wizara pia iliandaa Mkakati wa Maendeleo ya Jinsia (2005) ili uwe
itaandaa programu ya sekta ya mwongozo kwa sekta zingine zinazotekeleza sera hii.
Maendeleo ya Jamii itakayo tekeleza Aidha, programu ya kuboresha sekta ya Maendeleo ya
sera hii na sera zingine. Jamii imeandaliwa.
34. Kutoa mafunzo kwa watumishi wake ili Wizara imewapeleka katika mafunzo watumishi wake
waweze kupata elimu na maarifa ya kama ifuatavyo:
kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Uongozi: Maafisa 26, London, Uingereza. Wakuu
wa Vyuo na Maafisa Waandamizi wa Wizara 50
walipatiwa mafunzo Morogoro mwezi Julai.
Ugavi: Mafunzo ya muda mfupi Afisa mmoja
Marekani na mmoja Singapore, Maafisa Ugavi
watatu walipata mafunzo ya muda mfupi ya
masuala ya Ugavi yaliyoendeshwa na NBMM:
Mafunzo ya muda mrefu: Maafisa Maghala wawili
wanaendelea na masomo ya Stashahada ya Juu,
TIA.
Makatibu Muhtasi saba (7) na Msaidizi wa
Kumbukumbu watatu (3) wanaendelea na mafunzo
283
katika Chuo cha Utumishi wa Umma.
Maafisa Habari wawili walihudhuria mafunzo ya
namna ya kuandaa vipindi vya redio na
televisheni.
Ofisa Maendeleo ya Jamii mmoja anaendelea na
masomo ya Shahada ya Uzamili ya masuala ya
Jinsia, mmoja anaendelea na masomo ya
Shahada ya Uzamili ya MBA ambapo
mwanasheria mmoja anaendelea na Stashahada
ya Uzamili ya Sheria na mwingine LLM.
Maafisa 24 wanaendelea na mafunzo ya Shahada
ya Kwanza katika Chuo Kikuu Huria.
Wahasibu Wasaidizi watano wanaendelea na
mafunzo ya Stashahada ya Juu ya Uhasibu katika
TIA na mmoja anaendelea na Shahada ya Kwanza
ya Biashara katika Chuo Kikuu cha Nyegezi.
Maafisa watatu (3) wamehitimu mafunzo ya Msc
(Community Economic Development) katika Chuo
Kikuu Huria.
284
WIZARA YA MIPANGO, UCHUMI NA UWEZESHAJI
NA AHADI UTEKELEZAJI
1. Kuelimisha na kuhamasisha wananchi Serikali imeendelea kuelimisha na kuhamasisha
kuhusu MKUKUTA na kuandaa taarifa wananchi kuhusu MKUKUTA kupitia vipeperushi na
ya utekelezaji wa MKUKUTA kipindi cha redio (RTD) kiitwacho “TUJIKOMBOE”.
(MKUKUTA Implementation Progress
Report) na Taarifa ya Hali ya Umaskini Taarifa ya kwanza ya utekelezaji wa MKUKUTA
(Poverty Status Report). (2005/06) na Taarifa ya Hali ya Umaskini 2006
imeshaandaliwa na kuchapishwa. Aidha taarifa hizo
zinapatikana kwenye tovuti ya Mfumo wa kufuatilia
Umaskini nchini http://www.tanzania
monitoring.go.tz.
2. Kufanya tathmini (survey) ya Hali ya Zoezi la ukusanyaji wa takwimu za utafiti wa Mapato
Matumizi na Kipato katika kaya binafsi, na Matumizi ya Kaya Binafsi kwa mwaka 2006/07
na tathimni ya Hali ya Ajira, na (Household Budget Survey) linaendelea Tanzania Bara
uchambuzi utakaotoa hali halisi ya na linatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba,
maendeleo katika sekta mbalimbali. 2007. Sampuli ya maeneo pamoja na vijiji ni jumla ya
448 na kila kijiji na eneo la mjini kaya 24 zitahusika.
Inatarajiwa kuwa kaya zisizozidi 10,752 zitahusika na
utafiti huu.
Katika utekelezaji wa Mfumo wa Ufuatiliaji wa
MKUKUTA, Utafiti wa Watu Wenye Uwezo wa Kufanya
kazi, 2005/06 (Integrated Labour Force Survey)
umekamilika na uchambuzi wa zoezi hili utakamilika
kabla ya mwezi Agosti, 2007. Aidha, utafiti wa Ajira na
Mapato wa mwaka 2002 umekamilika na matokeo
yanaonyesha kuwa kasi ya ongezeko la ajira kwenye
sekta binafsi ni kubwa kuliko sekta ya Umma.
3. Kuziwezesha sekta mbalimbali Tathmini ya gharama za kutekeleza MKUKUTA
kuainisha gharama za MKUKUTA, (MKUKUTA costing exercise) kwa sekta za elimu, afya,
kuandaa mfumo wa hifadhi za jamii, maji, barabara, ardhi, kazi/ajira na maendeleo ya vijana
kuandaa namna ya kupata taarifa za na madini imefanyika na zoezi linategemewa kuendelea
watu wenye hali tete, kuendesha wiki kufanyika katika sekta za Biashara na Utalii.
ya Sera za Kuondoa Umaskini,
kushiriki kwenye mijadala mbalimbali Mafunzo ya mfumo wa kuweka na kutunza
ya kitaifa na kimataifa inayohusu kumbukumbu za takwimu uitwao ‟Tanzania Social-
umaskini, na kuandaa midahalo ya Economic Data Base‟ (TSED) yamefanyika kwa sekta
kisekta katika Serikali za Mitaa. zote za Wizara, Idara na Wakala wa Serikali. Aidha,
maoni ya Wananchi juu ya sera mbalimbali za Serikali
yamekusanywa na ripoti inaendelea kuandaliwa (Views
of the People Report 2007).
285
4. Kuendelea na ujenzi wa Eneo Maalum Ujenzi wa Eneo Maalum la Uwekezaji “Benjamin
la Uwekezaji lililopo Mabibo (The William Mkapa Special Economic Zone” (BWM – SEZ)
Benjamin William Mkapa Special lililopo Mabibo unaendelea.
Economic Zone – BWM SEZ).
5. Kuunda Mamlaka ya Kusimamia Mamlaka ya kusimamia maeneo maalum ya uwekezaji
Maeneo Maalum ya Uwekezaji (SEZs (SEZs Authority) imeshaundwa.
Authority).
6. Maandalizi ya ujenzi wa Kituo cha Upembuzi yakinifu umeshakamilika kwa ajili ya kuanza
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ujenzi wa Kituo Maalum cha Teknolojia ya Habari na
katika eneo maalum la uwekezaji Mawasiliano (ICT - SEZ) katika eneo la Chuo Kikuu cha
lililoko eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Dar es Salaam. Ujenzi unategemewa kuanza katika
Salaam. mwaka wa fedha 2007/2008.
7. Kuutangaza mpango wa Tanzania Zoezi la kuutangaza Mpango wa Tanzania Mini-Tiger
Mini-Tiger 2020 kwa kuchapisha vitabu Plan 2020 kwa kuchapisha vitabu na kuvisambaza
na kuvisambaza. linaendelea.
8. Kulitangaza Eneo Maalum la Matayarisho ya matangazo na vipeperushi muhimu
uwekezaji rasilimali linalojengwa yamekamilika kwa kushirikiana na Japan Development
Mabibo. Institute (JDI) kwa ajili ya kulitangaza Eneo hili Maalum
la Uwekezaji “The Benjamin William Mkapa Special
Economic Zone (BWM- SEZ)”.
9. Kuratibu utekelezaji wa mradi wa Mradi wa Biashara ndogo ndogo na za kati unaendelea
Biashara Ndogo ndogo na za Kati na kuratibiwa ukiwa chini ya jina jipya la Mradi wa
kuboresha mazingira ya biashara kuendeleza Ushindani katika Sekta Binafsi (Private
ikiwemo mapitio ya sheria na kanuni Sector Competitiveness Project) umetekeleza
za biashara ndogo ndogo na za kati. yafuatayo:
Mkataba wa Makubaliano baina ya Benki ya
Dunia, Washirika wa Maendeleo na Serikali kwa
ajili ya kipengele cha Mpango wa Kuboresha
Mazingira Bora umeshaandaliwa na unasubiri
kutiwa saini na pande husika kwa utekelezaji.
Katika kipengele cha kuongeza ushindani wa
Taasisi za Kibiashara, maafisa wa mradi
wanaendelea kuajiriwa na utekelezaji wa sehemu
nne za mradi umeanza kutekelezwa chini ya
Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (Tanzania Private
Sector Foundation-TPSF).
Utekelezaji wa Kipengele cha kufanikisha
upatikanaji wa Huduma za Kifedha ulio chini ya
Mfuko wa Kuendeleza Sekta ya Fedha (Financial
Sector Deepening Trust-FSDT) .
10. Kufanya utafiti wa kubaini fursa za Kituo cha Uwekezaji kupitia wataalam wa ESRF
kukuza uchumi na uwezo wa wameshakamilisha taarifa ya tafiti za kubaini fursa za
286
kuharakisha ukuaji wa uchumi kwa kukuza uchumi (Study on Growth and Impact of
lengo la kuhimiza uwekezaji. Investment in Tanzania).
11. Kuwasaidia wawekezaji wadogo Kituo cha Uwekezaji (TIC) kiliendesha semina katika
wadogo na wa kati (SMEs) ili kuandaa Mikoa ya Ruvuma na Mara kwa lengo la
miradi inayouzika kwa lengo la kupata kuwahamasisha wawekezaji kuwekeza katika fursa
mikopo kutoka kwenye mabenki. zilizopo ndani ya mikoa yao ili kuinua uchumi wa Taifa
hatimaye kupunguza umaskini. Sambamba na
kuendesha semina Kituo kimeshirikiana na mikoa hiyo
kuandaa „Regional Profiles‟ kwa lengo la kuainisha
rasilimali zilizopo
12. Kutangaza miradi ya SMEs kwa lengo TIC kwa kushirikiana na viongozi wa Kitaifa waliandaa
la kuwavutia wabia wa ndani na nje ujumbe wa Watanzania wenye miradi inayofaa
kuwekeza kwenda nchi mbalimbali kwa lengo la
kutangaza fursa za uwekezaji na kunadi miradi ya
watanzania kwa lengo la kuwavutia wageni kuja
kuwekeza nchini. Nchi zilizotembelewa ni pamoja na
Marekani, China, Japani na Korea ya Kusini, Oman,
Umoja wa Nchi za Kiarabu (UAE), Canada, Thailand,
Get documents about "