Embed
Email

Ndugu zetu_ Wazee wetu_ Assalaam Alaaykum_ UMOJA_ UHURU ...

Document Sample

Shared by: gegeshandong
Categories
Tags
Stats
views:
0
posted:
12/7/2011
language:
pages:
23
Ndugu zetu, Wazee wetu,







Assalaam Alaaykum,







UMOJA, UHURU, UADILIFU







Waraka Maalum Kwa Wakristo Zanzibar



Tunaleta hapa huu “Waraka maalumu kwa Wakiristo Zanzibar”. Waraka huu

umepatikana na Waislamu, Zanzibar katika nusu ya pili ya mwezi wa June, 2009.

Waraka huu unaonesha dhaahir shaahir mbinu zao dhidi ya Waislamu,

Wazanzibari. Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala Inshaallah

awashinde na kila uwovu wao, Yaa Rabbi kula ajae na shari, waijua yake siri, ivunjé

yake dhamiri asiweze kusimama; Aamyn, Yaa Rabbi Aamyn. Tutajaribu kueleza juu

ya waraka huu kwa khati za Italic kama ifuatavyo humu. Tulioyakoleza kwa khati

nyekundu ndio tunaona khatari yake zaidi na kutaka tuyafahamu zaidi na tujikinge

nayo. Muhimu, tafadhali tuusome waraka huu tupate kufahamu mbinu zao na

chuki zao dhidi ya Waislamu, Wazanzibari; ili tutahadhari nao. Muhimu tusisahau

Qauli ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Ta’aala alipotueleza juu ya uovu wa

hawa wenye kuwapiga vita Waislamu, Wazanzibari kwa jina la Ukiristo.







‫“يآأيها ّلذين آمنوا ال تتخذوا بطانة من دونكم اليألونكم خباال، ودوا ماعنتم، قد بدت البغضآء من أفواههم، وماتخفى‬

‫ا‬

.)111 : ‫صدورهم أكبر، قد بينا لكم الآليات ان كنتم تعقلون”. (آل عمران‬



Enyi mlioamini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha

kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao

katika midomo yao. Na yanayo fichwa na vifua vyao ni makubwa zaidi.

Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini”.



(Al-‘Imraan : 118).







Lakinibasi, kuyafahamu ni ndivyo; bali kuyaondoa ni waajibu wa kila mmoja wetu

kwa kadiri ya uwezo wake. Hapana shaka ndugu zetu walioko kwenye madaraka

na uongozi na sisi, waongozwa kushirikiana nao na kwa hikma na busara, wao ndio

wenye wajibu zaidi wa kuchukuwa khatuwa za kuyaondoa maovu hayo, tena

hufuatia wenye vyombo vya khabari na mashekhe wanye kuwaidhi.







Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala atujaalie kila la

kheri na baraka; Aamyn.







Wa Billahi Tawfiiq







Umoja wa Wazalendo







Zanzibar



June 24, 2009









WARAKA MAALUM KWA WAKRISTO ZANZIBAR







Wapendwa katika Bwana



Ndugu Wakristo umefika wakati tumeonelea kuwa ipo haja ya kuwaelezeni

machache ili kuona maendeleo yetu na mafanikio tuliokwisha yapata hapa Zanzibar,

yanaendelezwa na hayarudi nyuma kwa namna yoyote. Hapana shaka kuwa

munaelewa kuwa idadi yetu hadi sasa bado ni ndogo sana na wengi wetu tungali

katika kiwango na hadhi ya wahamiaji na sio Wazanzibari kama wanavyosema

wenyewe.







Wanatwambia, “….yanaendelezwa na hayarudi nyuma kwa namna yoyote”. Qauli

yao hii inadhihirisha vipi walivyo azimia kuendeleza mbinu zao ovu dhidi ya Uislamu hapa

kwetu, Zanzibar.







MAFANIKIO YETU

Kabla kugusia yale ambayo tunahisi ndio lengo la waraka huu hapana budi

kuwatajieni mambo machache ambayo tumefanikiwa kuyapata hadi sasa. Pamoja

na jitihada zetu za muda mrefu bado tunapaswa tumsifu Bwana kwa msaada

wake mkubwa kwetu dhidi ya maadui zetu. Tunaamini kuwa kupitia nguvu za

Roho Mtakatifu, Bwana atatupa ushindi na mafanikio makuu zaidi ya haya na

atawafumba macho maadui zetu wazidi kulala ili mipango yetu yote ya

kuibadilisha Zanzibar kidemografia ifanikiwe katika kipindi kifupi kijacho.

Mafanikio yetu yameenea katika kila upande - katika uchumi, siasa, huduma za

serikali, umiliki wa ardhi, ujenzi, elimu, n.k. Ili kupata picha kamili ni vyema

tuorodheshe kwa ufupi mafanikio hayo:







“Pamoja na jitihada zetu za muda mrefu bado tunapaswa tumsifu Bwana kwa

msaada wake mkubwa kwetu dhidi ya maadui zetu”. Wameanza kwa kusema,

“Pamoja na jitihada zetu za muda mrefu”, hii ni ithbati ya hali kwamba mbinu zao

dhidi ya Uislamu “ni za muda mrefu”, wakaendelea kueleza, “dhidi ya maadui zetu”,

yaani sisi Waislamu ndio “maadui wao”. Hivi kuwa wao Wakiristo wanatufanya sisi ni

“maadui zao”, hufaa tujiulize lipi la uadui tuliloufanyia Ukiristo sisi Wazanzibari, tangu

taarikh ya miaka, bali karne nyuma? Ingelikuwa vyema kama wangalitueleza uadui

tulioufanyia Ukiristo au Wakiristo sisi Wazanzibari. Hauko, wala hawawezi kutaja hata

moja; tunawataka wataje kama uko. Lakini ihsani nyingi tumeufanyia Ukiristo hio

miaka mingi iliopita, ni Ufalme wa Zanzibar uliowapa Wamishinari hapa Zanzibar nyumba

ya kuendeshea ibada zao na kuwapa waongozi wa njia kuelekea barani Afrika kwa kuondokea

hapa Zanzibar. Hapana shaka maneno haya hayakubaliwi na ndugu zetu Wakiristo wa

Kizanzibari ambao tumeishi miaka na miaka kwa masikilizano na mapenzi, kwa la furaha na

kwa la msiba; daima tuko pamoja. Tumeishi katika ustahamilivu mkubwa wa imani

mbalimbli, bali hata mila mbalimbali, hapakuwepo yeyote kumbughudhi mwengine; sote

tukiishi kuwa ni Wazanzibari. Hakika ni kwamba hawa wenye maneno na mbinu hizi za

ufisadi sio Wakiristo wa kweli, hawa ni mishinari wenye kufanyakazi begakwabega na

wakoloni tangu karne na karne katika misingi ya siasa yao ya “WAGAWE ILI

UWATAWALE”. Wanafanya hivi si kwa maslaha ya Ukiristo, wanafanya hivi kwa maslaha

yao ya kutoamini dini “secularism”, na kuitumia imani kuwa ni njia ya chumo la kujaza

mifuko yao. Wamishinari hawa na wakoloni karne na karne mbinu zao ni fitna za kuwagawa

Umma ili waendeleze maslaha yao. Huwagawa Umma kwa kutumia dini, ukabila bali hata

rangi, kipato au madaraka.







1. Nafasi yetu kwa upande wa elimu imekua ya kuridhisha kupitia nafasi za

serikali. Hivi sasa ni rahisi na limekua jambo la kawaida katika kila matangazo ya

wito wa masomo kusikia majina ya Wakristo. Kati ya vijana saba hadi kumi, ni

lazima upate vijana wawili hadi watatu kutoka katika makanisa yetu. Qauli yao

kuwa “kupitia nafasi za serikali”, hapana shaka, hivi ni kwa kuwa Tanganyika wao ndio

dola, wao ndio sirikali, wao ndio wenye kupanga na kupangua kukhusu ilimu. Kati ya

vijana 7 hadi 10, ni lazima upate vijana wawili hadi watatu kutoka katika

makanisa yetu. Ikiwa wao Wakiristo walioko Zanzibar, ambao haidhaniwi kuwa wanafika

10% ya Wazanzibari; wanapata baina ya 20% hadi 30% ya fursa za masomo; itafahamika

vyema mbinu wanazozitekeleza (wao Wakiristo) katika kuwazuilia fursa za masomo

Wazanzibari, Waislamu; hilo ni miongoni mwa maazimio yao makuu. Waislamu,

Wazanzibari wasipate ilimu ya maana; walazimishwe kuishi katika ujinga.







2. Sambamba na matangazo ya elimu vijana wetu wamekuwa wanapata nafasi

nyingi za ajira katika Serikali ya Zanzibar. Hali ya kutoelewana kisiasa baina ya

Wazanzibari imetoa mwanya kwetu kuingiza vijana wa Kikristo wenye asili ya

bara kwa wingi kwani wamekuwa wanaaminika zaidi kuliko vijana wa Zanzibar.

Tuizingatie hii qauli yao, “vijana wetu wamekuwa wanapata nafasi nyingi za ajira

katika Serikali ya Zanzibar”. Hali hii si ajabu, kwa sababu wao Tanganyika ndio wenye

sauti na amri ya kuajiri, tangu huko bara na hapa visiwani. Inasemwa na wengi kwamba

hapo BoT, (Bank of Tanzania) (Bank of Tanganyika), hata mpika chai, licha ya dereva;

anajiriwa kutoka bara, Mzanzibari hafai. “Hali ya kutoelewana kisiasa baina ya

Wazanzibari imetoa mwanya kwetu kuingiza vijana wa Kikristo wenye asili ya

bara kwa wingi kwani wamekuwa wanaaminika zaidi kuliko vijana wa

Zanzibar”. Naam, hii ndio faida khasa ya wao kupanga na kutekeleza hali ya kutoaminiana

na kuvutana Wazanzibari, lakinibasi, hilo lishapitwa na wakati. Alhamdulillahi, leo

Wazanzibari wakiwa kwenye Umoja wao wa Wazalendo wote qauli yao ni moja juu ya kila la

Nchi yao, kwa maslaha ya Nchi yao, hawana tena siasa za kichama, siasa zenye kutumika

kwa kujenga mfarakano baina yao. Wajuwe na watambue hawa mabwana wenye kujiita

wakiristo kwamba uwaminifu wa vijana wa Kizanzibari kwa jumla ni wa daraja ya juu

kabisa, wachache ulimwenguni wa mfano wao. Hali hii si ajabu hata kidogo, kwani haya ndio

malezi ya wazee na wazee wa wazee wetu, uwaminifu, mapenzi, kusaidiana, kushirikiana,

kushauriana na ustahamilivu wa kidini ndio sifa ya Wazanzibari tangu karne na karne.

Suala la kuajriwa zaidi vijana wa Kikiristo kuliko vijana wa Kiislamu, Kizanzibari; katika

nchi yao wenyewe, Zanzibar; ni miongoni mwa mbinu zao Wakiristo katika kuongeza idadi

ya Wakiristo hapa visiwani ili wajaze makanisa yao. Wanafanya hivyo ili waweze kudai

misaada kutoka huko Uzunguni, kutoka makanisani na/au watubinafsi, hivyo wapate fedha

hizo wajaze mifuko yao kwa kisingizio cha kueneza Ukiristo. Vilevile katika hivi kuwapatia

zaidi ajira vijana wa bara wanaowajaza hapa nchini mwetu bila ya kitambulisho chochote cha

uingiaji nchini, ni katika kuiandalia (CCM) “Catholic Christian Movement”, “Chama Cha

Mwalimu”, kuandaa wapigakura kwa makusudio ya kuendelea madarakani katika kuitawala

Zanzibar na kuendeleza mbinu zao dhidi ya Waislamu, Wazanzibari. Ndugu zetu

Wazanzibari mulioko kwenye uongozi, katika vyama na/au Sirikalini, na Wazanzibari sote

kwa jumla, haya ndivyo yalivyo; tafadhalini tukumbuke hii Qauli ya Mola wetu Mlezi,

Subhaanahu wa Taáala anayotutaka tuokoe nafsi zetu na ahali zetu kutokana na adhabu kali

ya Moto:







‫“يآأ ّها اّذين آمنوا قوا أنفسكم وأهليكم نارا وقودها ال ّاس والحجارة عليها مالئكة غالظ شداد ال يعصون اهلل مآأمرهم‬

‫ن‬ ‫ي ل‬

.)6 : ‫ويفعلون مايؤمرون”. (التحريم‬



" Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu wenu, na Moto ambao kuni zake ni

watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu hawamuasi

Mwenyezi Mungu kwa amri zake; na wanatenda wanayo amrishwa (yote)”. (At-

tahriim : 6)..







3. Hali tulioieleza juu imetuwezesha kuwa na Wakirsto wengi katika nafasi za

juu serikalini na katika chama tawala. Tunarejea tena kufahamishana sisi Wazanzibari,

Waislamu; yote haya wanajifanyia, au wanafanyiwa wao Wakiristo kwa sababu wao ndio

wenyewe dola, na wao ndio wenyewe khasa chama, bali wao ndio khasa wenye khatamu za

uongozi wa Tanganyika, Tanganyika ambayo ndio yenye kuitawala Zanzibar baada ya

kuivamia na kuimeza siku ile ya Januari 11, 1964. Kutokana na hali hii, ilivyo ni hivi;

Tanganyika inatawaliwa na Kanisa, Zanzibar inatawaliwa na Tanganyika, kwahivyobasi,

Zanzibar inatawaliwa na Kanisa. Wazanzibari CCM sio yao, Wazanzibari, Waislamu;

si wanachama wa “Chama Cha Mwalimu, “Chama Cha Msalaba””, chama hichi wenyewe

khasa ni wao wenyekujiita wakiristo.. Hali hii ni lazima iendelezwe katika ngazi zote

kwani imekuwa ikitusaidia hasa katika kiwango cha masheha na kamati zao

kwani huku ndiko kunako mambo mengi ya kila siku. Hizi ndizo mbinu zao ovu

kuwatendea Waislamu, Wazanzibari. Kwa hivi kuwa mbinu zote hizi zinafanywa kwa

kushirikiana makanisa na utawala Tanganyika; kwa vile wao Tanganyika ndio dola na ndio

nchi, sisi Wazanzibari, “Zanzibar si Nchi”, ndio kilasiku tunazidi kuangamizwa, sisi na

vizazi vyetu. Njia pekee ya kuondoa maafa haya ni “Zanzibar kurejea kuwa Nchi, Dola

Huru Kaamili; kama ilivyokuwa Zanzibar yetu siku ile ya Disemba kumi, 1963

ilipopata uhuru wake na kujiunga na Umoja wa Mataifa (UN), taarikh kumi na

sita, Disemba hiohio ya 1963”. Kila jambo la kheri linahitajia Umoja, mashauriano na

mashirikiano, lakini hili la ukombozi wa Nchi yetu linahitaji zaidi Umoja, ushirikiano na

mashauriano. Kwahivyobasi, ni wajibu wetu sote kuwacha mfarakano na kujenga

mshikamano, ili tukomboe Nchi yetu, Zanzibar irejee katika kheri na neema zake na itokane

na idhalaali, Aamyn.







4. Tumepata fursa ya kutumia Taasisi za serikali kwa uendeshaji wa ibada zetu

hali hii imefanya tuzidi kukubaliwa na Waislamu na kuvumiliwa na inaweza

kutupa nafasi ya kuwavuta katika NENO LA BWANA. Tunarejea tena qauli yetu

ileile kama tulivyojaaliwa kueleza hapo juu, yaani kwa sababu tumevamiwa na tukafanywa

kuwa “Zanzibar si Nchi”, ndio ikawa tunafikishiwa yote haya ya idhlaali na mbinu za

uangamizi, wetu sisi na khasa vizazi vyetu.







5. Kwa upande wa mashamba (vijijini) tumepata wasaa mzuri wa kununua ardhi

toka kwa Waislamu ambao hadi sasa bado hawajashtuka. Ardhi hizi

zimetuwezesha kujenga makanisa kadhaa mabayo hapo awali hayakuwepo. Jee,

tunasemaje sisi Wazanzibari, Waislamu; wenye kuuza ardhi zetu, bali hata mava zetu

kilasiku? Haya ndio makusudio yao mabwana kwa kuzivamia ardhi zetu. Tusisahau kwamba

kwa kuwauzia ardhi zetu, mbali ya khasara kubwa ya kuuza ardhi, tuna adhabu ya Mola

wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala kwamba ardhi zetu ndizo zinazojengwa makanisa ndani

yake. Tunauza Akhera yetu kwa khasara ya duniani, tunakhasirika duniani na Akhera..

Khasara ilioje hii! Yaa Rabbi tunusuru waja wako!! Ya Rabbi tunusuru waja wako!!

Mweyezi Mungu Mtukufu amrehemu Dr. Omar Ali Juma; aliyaona haya mapema na

akatahadharisha, lakini hayakupata sikio la kheri. Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu

wa Taáala amlipiea kwa kila aliemdhulumu na iwe ni upungufu wa makosa yake, Aamyn.







6. Idadi ya skuli na vituo vyetu (ambavyo licha ya picha ya juu kuwa

haviendeshwi kwa misingi ya Kikristo lakini kiukweli ni vituo vya kimisionari)

vimeongezeka kwa hali ya kuridhisha. Skuli hizi nikuanzia kwa watoto wadogo

hadi vituo kama hichi kilichopo Mji Mkongwe (Stone Town Youth Centre) na

zinafanya kazi vizuri katika kupandikiza mila za Kikristo. Haya ndio maneno yao

wenyewe, hivi vituo vyao japo hujaribu kudanganya kuwa haviendeshwi kwa msingi wa

Kikiristo, lakini kiukweli ni vituo vya kimishinari. Vituo hivi ni kuanzia skuli za watoto

wadogo mpaka hiki cha “Stone Town Youth Centre”. Vyote hivi ni kwa makusudio ya

kueneza ukiristo dhidi ya Uislamu, Wazanzibari. Lakinibasi, kama tulivyo tangulia kusema,

vitimbi vyao hivi ni vya tangu kale na kale; wala havijaleta lolote kuongeza huo ukiristo

wanaodai kuuwania. Na vipi isiwe hivyo, Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa

Taáala ametueleza hayo bayana kabisa. Wamokutoa mali yao tangu karne na karne, na

wataendelea kutoa, lakini hali itabakia ileile, khasara na majuto. Mwenyezi Mungu Mtukufu,

Subhaanahu wa Taáala hawi pamoja na mwenye kufisidi, wala mwenye kumsaidia mwenye

kufisidi. Fisadi yeyote yule, daima hufisidi nafsi yake.







ّ ‫م‬ ‫د‬ ‫ن ل‬

، ‫" إ ّ اّذين كفروا ينفقون أموالهم ليص ّوا عن سبيل اهلل ، فسينفقونها ث ّ تكون عليهم حسرة ثم يغلبون‬



‫ن‬ ‫ل‬

.) 66 : ‫و اّذين كفروا إلي جه ّم يحشرون" . (األنفال‬



“Hakika wale walio kufuru hutoa mali yao ili kuzuia Njia ya Mwenyezi Mungu.

Basi watayatoa, kisha yatakuwa juu yao majuto, na kisha watashindwa. Na wale

walio kufuru watakusanywa kwenye Jahannam



(Al Anfaal : 36).







Hii ni Qauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala, haiendi pogo hata

mara moja, ni iwe tu; kun-faya-kun, bila kizuizi. Lakinibasi, ni wajibu wetu kujitahidi

kutekeleza na kuhifadhi Dini yetu kwa ajili ya dunia yetu na Akhera yetu.







7. Sera ziliopo hivi sasa kwa upande wa uingiaji na utokaji Zanzibar imetusaidia

sana katika uingiaji wetu (Wakristo) kutoka Bara na hivyo kusaidia kufuta ile

imani ya kuwa Zanzibar ni kisiwa cha Waislamu na eti Wazanzibari kwa zaidi ya

aslimia 99 ni Waislamu. Hii sera ya uingiaji na utokaji Zanzibar, yaani bila ya

vitambulisho sio tu imesaidia kuendeleza hujma dhidi ya Uislamu, Wazanzibari; kwa kupitia

mishinari, bali zaidi imeleta wimbi kubwa la uharamia na ujambazi nchini Zanzibar.

Zanzibar imegeuzwa chaka la watoro, watu wanaingia vile wanavyotaka, hufanya ujambazi

wao, huuwa, huiba; kisha hupanda vyombo na kutoweka. Inafaa tukumbushane kwamba kila

aliesaidia kuleta hali hii, hali ya uovu kabisa, basi anafungu lake la ghadhabu ya Mwenyezi

Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala:







‫“ من يشفع شفاعة حسنة يكن ّه نصيب ّنها، ومن يشفع شفاعة س ّئة يكن ّه كفل منها، وكان اهلل على ك ّ شىء‬

‫ل‬ ‫ل‬ ‫ي‬ ‫م‬ ‫ل‬

.)18 : ‫ّقيتا”. (النساء‬

‫م‬







“Atakayeombea maombezi mema (atakayesaidia maombezi mema hata yakatokea)

atapata sehemu katika hayo. Na atakayeombea maombezi mabaya atakuwa na

sehemu katika mabaya hayo, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye ujuzi wa kila kitu”.

(Annissai : 85).







Maafa ya kuachiliwa watu kuingia Zanzibar bila kitambulisho, kila Mzanzibari anayafahamu

na analipa thamani yake kwa kila njia na kila hali. Kwahivyobasi, ni waajibu wa kila mmoja

kufanya kila analoweza kuhakikisha kwamba kuingia Zanzibar – sawa na nchi yoyote ile

ulimwenguni - ni kwa kutumia vitambulisho vyenye kukubalika kikanuni. Wajibu huu ni

juu ya ndugu zetu Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi, tunawaomba walitilie hima suala

hili mpaka litekelezwe.







8. Ujaji wa Wakristo kwa wingi kutoka bara umewezesha kuongezeka kwa idadi

ya mabaa na klabu za pombe. Hivi sasa ni jambo la kawaida kuona magari ya aina

mbalimbali yanayomilikiwa na eti Waislamu yanabeba kreti za pombe kali.

Maneno yao yanathibitisha maelezo yetu kwamba hawa si “Wakiristo wa kweli”, hawa ni

wamishinari ambao tangu karne na karne ni wenye kufanyakazi na wakoloni begakwabega

katika kuupiga vita Uislamu nyuma ya pazia la Ukiristo. Kama wanavyosema, ujaji wa

Wakristo wa namna hii umeongeza idadi ya mabaa na klabu za pombe, bali pia umeongeza

idadi ya nyumba za uchafu. Haya ndio makusudio yao khasa, ujaji wao kwa wingi

haujaongeza idadi ya waumini wao; makanisa yao bado ni matupu, na yataendelea kuwa

matupu. Kuupiga vita Uislamu, Wazanzibari; kwao ni muhimu zaidi kuliko

kuujenga Ukiristo. Inafaa wafahamu kwamba mbinu zao hizi ovu hazitaleta matunda, kwa

sababu Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala ameahidi kuihifadhi Dini yake:







.)1 : ‫“ يريدون ليطفئوا نوراهلل بأفواههم واهلل متم نوره ولو كره الكافرون”. )ال ّف‬

‫ص‬ ّ



“Wanataka kuizima nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao. Na Mwenyezi

Mungu atakamilisha nuru yake ijapo kuwa makafiri watachukia”. (Ass’af : 8 ).







Juhudi zao za kuupiga vita Uislamu ni za tangu karne na karne, lakini Alhamdulillah; kama

alivyoahidi Subhaanahu wa Taáala haiwaongezei wenye kujaribu kuupigavita Uislamu

isipokuwa khasara na ghamu. Dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala

kilasiku inazidi kukua na kushamiri, na Inshaallah itaendelea hivyo daima dawamu. Kwa

kuvamiwa Nchi yetu na kumezwa chini ya huu wenyekuitwa muungano, tukawekwa katika

hali mbaya kabisa ya kiuchimi, ndio tumefika baadhi yetu kuingia katika upungufu wa imani

kufika kushiriki katika maasi haya ya ulevi. Kwa kitendo chetu hiki ndio hawa mabwana

wanafika kutuita, “eti Waislamu”; yaani Uislamu wetu wanaubeza.







9. Kujiingiza kwetu katika Taasisi za dola katika ngazi za mitaa kumetuwezesha

kupata nafasi ya kutangaza Ukristo kwa njia ya mihadhara. Hapana shaka kujiingiza

kwao huku kunapata kuungwamkono na kusaidiwa na baadhi yetu sisi wenyekuitwa “eti

Waislamu”. Tafadhali naturejelee hayo maneno ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taála

hapo juu, kukhusu malipo ya mwenye kusaidia katika kitendo, au hata maneno; ikiwa kwa

wema au kwa uovu. Malipo ni kulingana na kitendo au maneno. Yaa Rabbi tujaalie wenye

kusaidia katika kheri.







Wakati huo huo kudhibiti mihadhara ya wazi ya Waislamu kwa kutumia madai ya

kashafa na kutatanisha maelewano mazuri baina ya watu wa dini tafauti. Hii ndio

sera na mwendo wao, hawana ukweli, nifaaq ndio mwendo wao. Mbinu zao ni kutumia

uwongo katika kutaka kuwazuilia Waislamu, Wazanzibari kuendeleza Dini ya Mwenyezi

Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala kama alivyoamrisha. Hivi ndivyo walivyo tangu

karne na karne, tangu siku za Mitume a.s.w., kwa hii inadi yao Mwenyezi Mungu Mtukufu

akawapiga mihuri ya upotofu.







10. Tumefanikiwa kupata viwanja vingi katika maeneo ya Mjini ambayo yangali

mapya. Maeneo haya ni kama Tomondo, Mombasa, Mwanakwerekwe, n.k. ambayo

tayari tumeshajenga makanisa yetu ingawaje kwa sasa hayajawa na waumini

wengi wa kuyatumia na bado yanaonekana ni matupu. Vingi ya viwanja hivi

wamevipata kwa kuvinunua kutoka kwetu sisi Waislamu, Wazanzibari; miongoni mwa

viwanja hivi pia ni “eka”, mali yalionyangánywa na kugaiwa vipande vipande. Haramu hii

ya unyangányi ya mali ya watu imeongezeka haramu kwa hivi kutumiwa ardhi hizi

kujengwa makanisa, si kwa kuabudiwa; kwani hao wakuabudu hawapo, bali kwa kuleta

idhlaali kwa Waislamu, Wazanzibari na utekelezaji wa mbinu zao za kujaribu kuupigavita

Uislamu.

Ndugu wapendwa katika bwana,



Mafanikio hayo yasitufanye tuka lewa na kusahau jukumu la kanisa la kuona kuwa

utawala wa Bwana unashuka Zanzibar haraka iwezekanavyo. Kosa lolote

tutakalofanya hivi sasa litaweza kuturudisha hatua kadhaa na huenda nafasi hii

tulionayo hivi sasa tusiipate kwa karne mpya ijayo. Mambo ya kufanya

yanayotukabili ili kuimarisha nafasi yetu na kuona yale tuliokwisha yapata

hayatutoki na kuyafanyia dira kwa karne ijayo ni haya yafuatayo:







Tusahau tafauti zetu dhidi ya adui



Ingawaje tupo madhehebu nyingi lakini tunawajibika kuelewa kuwa Waislamu na

Uislamu wao ni adui yetu namba moja ambaye hatutofaulu kupambana nae mmoja

mmoja. Uislamu hapa Zanzibar ni dini iliofungamana na mila na utamaduni hivyo

kila itakapowezekana tusahau tafauti zetu ndogo ndogo na hata kubwa kukabiliana

nao, vyenginevyo tutarudi kama wakati wa Karume. Wanabainisha tena fahamu yao

potofu kwamba “Waislamu na Uislamu wao ni adui yetu namba moja”. Kama

tulivyotangulia kuelezana, sisi Waislamu, Wazanzibari hatuna uadui na Wakiristo, tumeishi

pamoja kwa furaha, amani na mapenzi kwa miaka na miaka.







Tuhakikishe tunapata ardhi



Hii ni mbinu kongwe katika usambazaji wa Ukristo. Wazee wetu walipoleta

Ukristo Zanzibar na katika Afrika jitihada waliyofanya ni kupata ardhi kubwa kwa

ajili ya ujenzi wa maeneo yetu majengo ya hospitali shule zahanati vituo vya

chekechea makanisa n.k. Tunahitaji ardhi kubwa ili kuziweka huduma hizo

mahala pamoja kwa ajili ya kueneza injili ya bwana na Muokozi wetu. Wazanzibari,

hii ndio mbinu yao; wazipate ardhi zetu kwa kuenezea hizo mbinu zao potofu, mbinu za

ufisadi dhidi ya ubinaadamu, mbinu wenyekuziita ukiristo, na hakika sio Ukiristo wa kweli.

Katika hali hii, inafaa tuchukue kila hadhari kuhakikisha kuwa hatuuzi ardhi zetu,

khasa kwa waliokuwa si katika sisi, yaani Waislamu, Wazanzibari. Ugawaji wa eka

umesaidia pakubwa katika wao kuzipata ardhi zetu na kuendeleza ujenzi wa makanisa nchini

mwetu. Tena tunarejelea Qauli ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala tulioitaja hapo

juu kukhusu kusaidia katika wema na katika uovu; na wewe utapata sehemu yako, ikiwa ni

kheri au ni shari. Tutahadhari na kuuza ardhi zetu. Tuhakikishe hatuuzi ardhi zetu

kwa hali yoyote ile. Kuuza ardhi sio kuondoa umasikini, bali ni kuzidisha

umasikini na ufukara na ni kujenga idhlaali kwa nafsi zetu na kwa vizazi vyetu.







Tununue nyumba na viwanja kwa ujenzi wa makanisa



Inaonesha Waislamu wenye siasa kali na baadhi ya watendaji kwenye sirikali

wameanza kushtuka na ongezeko kubwa la makanisa katika kisiwa cha Unguja.

Kuna dalili kuwa tunaweza kupata ugumu katika kupata viwanja kwa ajili ya

makanisa. Njia tunayoweza kuitumia kwa muda huu ni kununuwa viwanja vitupu

au nyumba za Waislamu kwa bei kubwa itayowashawishi kuviuza na baadae

tutaweza kuvijenga au kugeuza nyumba hizo kuwa makanisa. Tuone jinsi

wanavyopanga kila njia ovu za kutufisidi na kujaribu kuifisidi Dini yetu. Hivi wao

kubainisha uovu na mbinu zao, ni fursa kwetu sisi kuchukuwa kila hadhari kujikinga na

uovu wao huu. Neno “Waislamu wenye siasa kali” tushalizowea, kila Muislamu mwenye

kutekeleza wajibu wa Dini yake, ndio hupangwa kila jina la uovu. Kwao wao sote sisi tuwe

“Waislamu kanzu” hio ndio haja yao, hapo tena ndipo watupe jina walipendalo, “eti

waislamu”. Madhali hawawezi kutubatiza, na Inshaallah hawataweza, laa sisi wala vizazi

vyetu, basi tuwe “Waislamu kanzu” itatosha kwao; Inshaallah hatutakuwa hivyo.

Alhamdulillahi, hao wanaowaleta hapa Zanzibar kialsiku wanazidi kurejea kwenye Dini yao,

yaani Uislamu; yaani wanasilimu. Haqi lazima idhihiri, haqi haikubali kukaliwa juu, lazima

ikae juu.







Tujenga shule na hospitali kwa wingi



Hizi ni taasisi pekee ambazo tunaweza kuzitumia kueneza neno la Bwana kwa

Waislamu walio wengi hapa Zanzibar. Kwa kutumia umasikini unaowakabili

wengi ya Wazanzibari na uchache wa huduma hizo tunaweza kujitangaza vizuri,

tujitahidi kutoa huduma nzuri kuweka vifaa vya kisasa kuweka bei ndogo kuweka

upendo ili vituo vya Waislamu au hata vile vya serikali visiweze kuvikaribia vyetu.

Shule ni sehemu muhimu ya kupandikiza mafundisho yetu, zaidi kwa watoto

wadogo (Nursery). Mbinu za kutumia huduma hizi kwa uenezaji wa wenyekuitwa

ukiristo ni za kale, na Inshaallah kama wanavyosema wao wenyewe, Waislamu

Alhamdulillahi ndio wengi hapa Zanzibar, itaendelea hivihivi na miongoni mwao Inshaallah

watazidi kupata uwongozi na warejee kwenye Dini yao ya asli - Uislamu, wote wanazaliwa

Waislamu, ni wao ndio huwabatiza na kuwatia kwenye Ukiristo. Suala la wao kutumia

“umasikini unaowakabili wengi ya Wazanzibari na uchache wa huduma hizo”,

kama tulivyotangulia kufahamishana, huu umasikini wametutia wao watawala wetu,

Dodoma; ili waweza kutuendesha wanavyotaka, tangu kisiasa, kidini na katika nyanja

nyenginezo. Umasikini huu umekuja kwa kuivamia Nchi yetu na kuimeza kwa kisingizio cha

huu wenyekuitwa muungano. Kutokana na hali hii ndio hii leo Wazanzibari wakawa

kwa hali yoyote ile wanawania kurejea Dola yao ya Zanzibar na itokane na huu

ukoloni wa Tanganyika, ukoloni wa Kanisa; leo kabla ya kesho. Suala la kuzitumia

hizi skuli za chekechea kwa kupotosha imani ya wenetu, hili ni jambo la khatari sana na ni

wajibu wetu kuchukua kila hadhari. Kubwa la kufanya sisi ni kutowapeleka wanetu kwenye

hizi skuli zao za chekechea, hizo ni vidonge vya sumu vilivyozongereshwa sukari. Tuviepuke

kama tunavyoweza, tuviepuke kwa kujenga skuli zetu za chekechea na kuwapeleka wenetu

humo.







Tunadai muda zaidi katika Vyombo vya habari (Tv na Redio)

Kwa muda mrefu sasa uislamu na waislamu wamehodhi vombo hivi vya habari

mbali na kuwa siku ya ijumaa ambayo yote humilikiwa na vipindi vya kiislamu

vyombo hivyo hutenga siku nyengine kadhaa kwa vipindi vya kiislamu na hata

kuthubutu kutia adhana kila wakati wa sala hali hii inaudhi na inatoa picha ya

wazi ya serikali kupendelea uislam ingawaje inadai kuwa haina dini. Wakati wa

kusherehekea miaka 25 ya TVZ tulizungumzia suala hili lakini inaonekana

halikupata mtu wa kulifanyia kazi. Sasa tuhakikishe kuwa ukristo unapata muda

zaidi katika vyombo hivyo au uislam nao upunguziwe nafasi. Kuzidi chuki zao,

dharau na ihana; wanasahau kuwa Zanzibar ni nchi ya Waislamu, kwa hivyo kutumia

vyombo vyao, khasa idhaa kwa kutumikia Dini yao ni waajibu juu yao. Kuudhika kwao kwa

kutiwa adhana katika idhaa yetu, halina msingi; bali tu ni dalili ya chuki zao juu ya Uislamu,

khaasa na juu ya Wazanzibari kwa jumla. Tizama jinsi ya chuki na uovu wao, “wao

wapate muda zaidi na Waislamu wapunguziwe”, hii ndio sera ya hasidi, weye ukose,

yeye apate. Lakini kwa mipango ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala, hasidi daima

haendelei, hasidi yake ni khasara na idhlaali.







Tuongeze mihadhara ya wazi



Wakati Waislam wamezuiliwa kufanya mihadhara ya wazi, sisi tujitahidi

kuhakikisha kuwa mihadhara yetu inaongezeka kwa kiwango kikubwa. Kwa

kuwa Waislamu hawahudhurii mihadhara hiyo, lazima tuone wakristo wa Mjini na

Mashamba wanahamasishwa na kupatiwa nyenzo ili kuhudhuria. Vipaza sauti

vitumike kuhakikisha kuwa neno la bwana linafika kila pahala. Mihadhara ifanyike

karibu na nyumba, misikiti na kwenye viwanja vya wazi. Ndio hayo! Hii ndio sera yao,

Waislamu wazuiliwe, wao wapewe na waongezewe.







Tuendelee kutumia shule na sehemu za Umma



Ili kuwafanya waislamu watuzoee na kuondosha chuki yao kwetu ni lazima

kuendelea kutumia mashule na sehemu za Umma zilizo wazi kwa mambo yetu ya

ibada kwa kipindi kirefu hali hii inaweza kuwafanya washindwe kuona tafauti kati

yetu na wao. Kila ukiusoma waraka wao huu ndivyo unavyozidi kutambua kuwa hawa

“wenyekujiita wakiristo”, sio Wakiristo wa kweli; Ukiristo wa kweli haunadi uadui na

Uislamu. Hii leo, Bwana Pope; mara nyingi amesikika kusema juu ya kuondoa mvutano

baina ya dini, bali baina ya mataifa. Kama wao hawa ni waumini wa kweli wa Ukiristo

wengelifuata mwenendo wa Bwana Pope. Lakini kamaitavyokuwa, sisi ni waajibu wetu

kuchukuwa kila hadhari kujilinda na mbinu za mabwana hawa wenye fikra na mipango ya

kujenga chuki na khasama baina ya waumini wa dini tafauti. Hadhari ni waajibu, hivyo

ndivyo alivyotuamrisha Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala katika hii Aya

tuliotangulia kuitaja humu. Kwa hivi kuwa nia na dhamiri yao mabwana hawa si njema juu

ya Uislamu, Wazanzibari; ndio inatufanya na sisi kulazimika zaidi kujihami dhidi ya mbinu

zao ovu kwa uwezo wetu. Hivi kujihami kwetu dhidi ya mbinu zao ovu ndiko wanakosingizia

kuwa ni “chuki”. Tunawahakikishia kuwa sisi Waislamu, Wazanzibari; hatuna chuki na

Ukiristo hata kidogo, lakini tuna waajibu wa kufuata maamrisho ya Mola wetu Mlezi,

Subhaanahu wa Taáala na Sunna za Mtume wetu Mpenzi s.a.w. Miongoni mwa maamrisho

hayo ni kuihami na kuihifadhi Dini yetu tukufu kwa kila hali. Hapa tena ni waajibu

kuzinduana na ndugu zetu walioko kwenye madaraka juu ya mbinu hizi na kuwaomba

kuchukuwa hadhari katika utumizi wa hizi sehemu walizozitaja hawa mabwana kupanga

kuzitumia ili kuepusha athari ya sisi kusaidia katika utekelezaji wa njama zao ovu dhidi ya

Uislamu, Wazanzibari. Tusisahau kuwa mwenye kusaidia katika la kheri, nae hupata sehemu

ya kheri hio; na mwenye kusaidia katika shari nae hupata sehemu ya shari hio. Yote hayo

tutayakuta kwenye vitabu vyetu hio Kesho, na hii leo, hapahapa ulimwenguni tutapata

malipo yetu, qabla ya hio Kesho..







Tufanye suala la uhamiaji Zanzibar kuwa jepesi



Uzoefu unaonesha kuwa ni jambo gumu kuwabatiza Wazanzibari waislamu. Hali

hii inafanya ongezeko la wakristo kuwa dogo au halipo kabisa ukitoa wale

wanaozaliwa katika familia za kikristo. Alhamdulillahi, kweli wanaitambua; lakini

wamo wanagombana nayo. Inshaallah daima dawamu, Waislamu, Wazanzibari hawata

nasarishwa, daima wataendelea katika Dini yao tukufu. Inshaallah na uwongofu utawafikia

na wao warejee kwenye Dini yao ya kuzaliwa. Binaadamu huzaliwa ni Muislamu, ni wazee

wake ndio wenye kumtoa katika Uislamu na kumtia kwenye upotoful.







Njia pekee ya kuhakikisha ongezeko la makanisa na Taasisi zetu ni kuongezeka kwa

wakristo. Jambo hili litawezekana kwa kuingiza Wakristo wengi kutoka Tanzania

Bara au wapagani ambao tutaweza kuwabatiza kwa kutumia udugu wetu wa

kikabila au asili ya Bara. Tunaposoma maelezo yao haya tunafahamu bila taabu kwamba

haja yao ni kuongezeka makanisa na taasisi zao. Kuongezeka Wakiristo sio haja

yao khasa, kuongezeka Wakiristo kwao wao ni ngazi tu ya kufikia haja yao khasa,

yaani kuongezeka makanisa na taasisi zao. Hii hakika wanaoshindwa kuificha, vitendo

na mwenendo wao pia unathibitisha hakika hii. Huu ujenzi wa makanisa na taasisi nyengine

ni mtaji wa kujipatia chumo binafsi hao viongozi wa hizi harakati za hawa “wenyekujiita

wakiristo” kutoka wafadhili wao huko Ulaya na kwengineko. Na kwa kuwa makanisa haya

lazima waonekane wenye kuyatumia, ndivyo hivi kupanga hata kuleta na kuhamisha watu

kutoka huku na huku. Ni vyema wawalete, Inshaallah itakuwa ndio njia ya wao

kurejea kwenye Dini yao ya asili; Uislamu; kheri hutoka kwenye tumbo la shari.







Kwa kuwatumia ndugu zetu waliomo serikalini (SMZ au SMT) tuhakikishe kuwa

suala la uhamiaji linabakia wazi na rahisi na linaendelea kwa kila hali. Lugaha nzuri

na ndivyo khasa, yaani “kwa kuwatumia”. Hawa mabwana “wenyekujiita wakiristo”,

mipango yao ni mbinu za uovu, kwahivyobasi; ili kutekeleza mbinu zao hizo, ndio wakawa

wanapanga “kuwatumilia” hao wanaowaita “ndugu zao” waliomo sirikalini dhidi ya

Waislamu, Wazanzibari - “adui zao namba moja”. Tena, tunawaomba ndugu zetu,

Wazanzibari, khasa waliomo kwenye madaraka, tuzidi kuchukuwa hadhari na kujikinga na

mbinu zao hizi. Suala la uhamiaji na uingiaji nchini bila ya vitambulisho, kilasiku tunaona

maafa yake, tangu ujambazi na mengi mengineo. Na zaidi ni hili la kuwa ni mbinu ya

kupangwa khasa kwa kuongezeka makanisa nchini mwetu.







Tuzuie jaribio lolote la kadi za uraia au vitambulisho



Wakristo tunapaswa kuelewa kuwa iwapo serikali ya Zanzibar itaamua kufanya cho

chote ili kuwa na vitambulisho au kadi za uraia kwa wazanzibari pekee basi jambo

hilo litaathiri sana mipango yetu ya muda mrefu kwa Zanzibar. “Mipango yao ya

muda mrefu itaathirika”, hii ndio qauli yao. Iwapo sirikali ya Zanzibar italeta

vitambulisho vya Wazanzibari, basi mipango yao ya muda mrefu hawa mabwana

wenyekujiita wakiristo itaathirika. Hii ni ilani ya wazi kabisa kwamba kuondolewa

vitambulisho vya Wazanzibari na kuletwa vya Watanzania, wenye kunufaika khasa ni hawa

mabwana wenyekujiita wakiristo. Ikiwa Wazanzibari fikra zetu ni kwamba hivi vitambulisho

ni kwa maslaha ya chama cha kisiasa dhidi ya chama cha kisiasa, basi ndivyo hivi

tunavyoelezwa wazi kabisa kwamba vitambulisho ni mpango wa Wakiristo dhidi ya

Waislamu, Wazanzibari. Kwahivyobasi, vitu viwili ni muhimu kwa Kanisa, (1)

Uhamiaji, (2) Vitambulisho. Vitu viwili hivi ni dharura vibakie katika maslaha yao wao

hawa wenyekujiita wakiristo, ili waendeleze vita vyao dhidi ya Waislamu, Wazanzibari.

Tena, tunawaomba ndugu zetu waliomo kwenye madaraka wayazingatie haya kwa

hikma na busara na kutambuwa dhamana zao na kuhisabika kwao katika

dhamana zao, mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala na

mbele ya Umma wa Kizanzibari.







Jitihada zozote za kuiimarisha Zanzibar kama Zanzibar na nje ya Utanzania ni

lazima tuelewe kuwa Uislamu utapata nguvu na kuwa tishio kwa hapa Zanzibar

na hata Bara. Kutokana na imani na siasa yao hii, ndipo pale Januari 11, 1964 makanisa

wakimtumia Nyerere akaleta majeshi yake na kuivamia Dola Huru ya Zanzibar. Dola

ambayo ilipata uhuru wake taarikh 10 Disemba, 1963; na kujiunga na Umoja wa Mataifa

taarikh 16 Disemba hiohio 1963. Baada ya siku thalathini na tatu tu, yaani hio Januari 11,

1964 ndipo makanisa kwa kumtumia Nyerere wakaivamia Zanzibar. Mavamizi haya lengo

lake kuu ni kuimeza kikamilifu Dola Huru ya Zanzibar, ndipo hapo siku ile ya April 26, 1964

ilipomezwa Zanzibar kwa kisingizio cha huu wenyekuitwa muungano kwa kubuniwa zile

“Articles of Union, 1964” na hapo tena ndipo ilipofanywa “Zanzibar si Nchi”.







Iwapo tutawajibika kuunga mkono ni kadi za Uraia na vitambulisho vya

Watanzania kwa Ujumla na sio Zanzibar peke yake. “Zanzibar si Nchi” ndivyo

alivyotwambia Mhishimiwa Waziri Mkuu wa Tanganyika, Bwana Pinda; kwahivyobasi,

madhali hatuna nchi na bado Zanzibar ni koloni la Tanganyika, vitambulisho, kadi ya uraia,

na hio passpoti, vyote hivi tutaazimwa na bwana mtawala Tanganyika. Kabla ya Zanzibar

kupata uhuru wake siku ile ya Diemba 10, 1963, Wazanzibari wakipewa passpoti za

“Zanzibar Protectorate” yaani “Himaya ya Zanzibar”. Wakati huo juu ya kutawaliwa na

Muingereza lakini tulibakia kuwa Dola, lakinibasi; bwana mkoloni Tanganyika yeye

ameimeza nchi yetu na kuitia chini ya ukoloni wake, kisha akatwambia “Zanzibar si Nchi”;

mkoloni Muingereza hakufika kuimeza nchi yetu na kufika kutwambia kuwa “Zanzibar si

Nchi”. Hapa ndipo inaposemwa “kheri ya ukoloni mweupe kuliko ukoloni mweusi”.

Naam! Halina shaka hili! Hivi ndivyo walivyosema wanafunzi wa Chuo Kikuu cha

Dar-es-Salaam, mnamo miaka ya sitini; mara tu baada ya Tanganyika kupata

uhuru. Qauli hii ilimchoma na kumuudhi sana Mwalimu Nyerere, hivyo akaamrisha

kufungwa Chuo hiki kwa muda. Kweli ni chungu!







Tujipenyeze Vyamani na kushika nafasi muhimu



Lazima tuelewe kuwa chama cho chote cha siasa kinalenga kukamata serikali ili

kiweze kutekeleza yale yanayoaminika kuwa ni mazuri kwa chama hicho.

Tunapozungumzia vyama vya siasa kwa Zanzibar tunahusisha zaidi kwenye CCM

na CUF. Watu wetu wamefaulu kuingia kwa wingi katika chama tawala na katika

jumuia zake. Ikiwa inavyosemwa ni hakika, kwamba “CCM”, maana yake khasa ni

“Catholic Christian Movement” au “Chama Cha Msalaba”; basi si ajabu hata kidogo kuwa

“watu wetu wamefaulu kuingia kwa wingi katika chama tawala (CCM) na katika

jumuia zake”. Hali kuwa hivyo si ajabu, ingalikuwa ajabu lau kama hali haingalikuwa

hivyo. Baada ya maneno yaliowazi kabisa kama haya, sawa na pale tulipoambiwa kuwa

“Zanzibar si Nchi”, ni kweli sisi Wazanzibari tuendelee kudhania kwamba CCM ni chama

cha Wazanzibari? Ni kweli baada ya chama hikihiki CCM kutueleza dhaahiri shaahiri,

kwamba “Zanzibar si Nchi”, bado sisi tuendelee kudhania kwamba CCM ni chama cha

Wazanzibari? Tutakuwa tunajidhulumu nafsi zetu kwa kuzidanganya.







Tupenyeze wenzetu serikalini



Sambamba na suala tulilolielekeza juu hatuna budi kusomesha vijana wetu na

kuhakikisha kuwa tunatumia kila njia na ushawishi ili kuwaingiza serikalini na hasa

katika sehemu muhimu. Hii itarahisisha kuungwa mkono mipango yetu na

kupunguzwa vikwazo kwa mikakati yetu. Hapana shaka hii ni mbinu yenye kutekeleza

makusudio bila ya wasiwasi. Hali hii ndivyo ilivyo hivi sasa hapa kwetu, nyingi ya nafasi

muhimu za juu zimo mikononi mwa mabwana watawala, Tanganyika, Kanisa. Waswahili

wa Tanganyika na Waswahili wa Zanzibar, bali na Waswahili wa Kenya na

Waswahili wa Uganda sote tumetiwa kikaango kimoja tunakaangwa kwa matufa

yetu wenyewe. Kwa mabwana hawa wenyekujiita wakiristo, kosa letu sisi Waswahili,

Waislamu ni Uislamu wetu. Hivyo ndivyo ikavamiwa Uganda kuwaondosha watawala wa

jadi, kina Kabaka na machifu wao, na kuvamiwa kuondoshwa Sirikali ya utawala wa kina Idi

Amin; yote hayo ni vita dhidi ya Uislamu, Waswahili.







Tuunge mkono sera za utalii

Hadi sasa wengi wa watalii wanaoingia Zanzibar hutokea nchi za Kikristo. Desturi

za watalii hupingana na zile za Kizanzibari na hata za Kiislamu. Watalii

wanasaidia kuongezeka kwa mabaa na vivazi ambavyo waislamu wanataka

visivaliwe hasa na wanawake. Waingereza wanasema, “when the drink is in, the

truth comes out”; maana ya maneno haya ni kama hivi, “ulevi ukijaa (kichwani),

ukweli hutoka nje”. Ulevi wa hawa mabwana wenyekujiita wakiristo, si pombe, bali ni

haya wenyekuyaita “mafanikio yao”. Haya mafanikio yao yamewalevya na kufika hadi hivi

wao kubwabwaja vile wanavyopenda bila ya wasiwasi wowote ule. Tena Waingereza

wanasema, “power corrupts, obsulute power corrupts obusulutely”, maana ya maneno

haya ni kama hivi, “nguvu za madaraka zinafisidi, na nguvu za madaraka yasio na

kizuizi, hufisidi bila ya kizuizi”. Hawa mabwana wenyekujiita wakiristo, baada ya

kupewa madaraka, kuvamiwa nchi yetu na kutiwa chini ya ukoloni wao; wamelewa kwa

utamu wa madaraka, hivyo ndio hivi wao kuzama katika kuleta kila upotofu na ufisadi;

kinyume kabisa na “Ukiristo wa kweli”. Kwa kitendo chao hiki, badala ya kuutendea vyema

Ukiristo; wamekuwa wanautia aibu na fedheha Ukiristo wa kweli, Ukiristo ambao unaamini

juu ya kuishi kwa salama, amani na mapenzi na waumini wote.







Tujenge mabaa na kuongeza pombe



Waislamu wengi huchukia pombe na huweza kuhama iwapo duka la pombe au baa

ipo karibu nao. Waislamu hatari ni wale wanaosoma na kupata muda wa

kujishughulisha na dini yao. Pombe ni kitu ambacho humtoa Muislamu katika

Uislamu wa vitendo na kumkaribisha na Ukristo. Jee, haya ndio maamrisho ya Ukiristo,

yaani kupanga kufisidi waumini wengine? Mzee Pope haidhaniwi hata kidogo kama

atakubaliana na mbinu fisadi kama hizi? Ukiristo wa kweli ni ule wenye kujenga mapenzi

baina ya waumini. Pombe sio humtoa Muislamu katika Uislamu wa vitendo, bali pia humtoa

Mkiristo katika Ukiristo wa kweli, bali humtoa hata mpagani katika utu wake. Kutokana na

uovu huu ndivyo pale pombe kukatazwa na kila imani. Jee, ni kweli kwamba pombe

humkaribisha mtu na Ukiristo? Haya mapya kabisa! Inavyojuulikana ni kwamba pombe, na

kila ulevi, bali maasi humtoa mtu katika ubinaadamu wake na kumtia katika siubinaadamu.

Pombe haingaliitwa mama wa maasi lau kama si yenye kupelekea kwenye kila maasi. Jee,

Ukiristo wa kweli ndivyo unavyoamrisha kwamba binaadamu ajitie katika kila aina ya maasi,

au katika maasi? Hatudhani kuwa ni hivyo.







Tuwafuate Wakristo waliosilimu ili warudie Ukristo



Watu wa aina hii wanakuwa bado hawajatulia na mara nyingi huwemo katika

matatizo.. Pana haja ya kuwalenga watu hawa ili kuwarudisha kabla hawajatulia au

kupata elimu nzuri. Matatizo yao ndipo mahala pa kuanzia ili Bwana awateremshie

roho ya utulivu. Uzima wa Ukristo ni kuwa na wafuasi wengi kadiri

iwezekanavyo. Jee, ndugu zetu, mnaamini kwamba hawa si Wakiristo wa kweli? Hawa

basi ni wenyekujiita wakiristo, sio Wakiristo. Hivyo ni kweli kwamba Ukiristo wa kweli ni

kumpangia binaadamu hilaki na kufisidika tu? “Wawarudishe kabla hawajatulia na

kupata elimu nzuri”. Ikiwa mbinu hizi si ufisadi tuziite nini? Ni ufisadi wa hali ya juu

kabisa. “Uzima wa Ukristo ni kuwa na wafuasi wengi kadiri iwezekanavyoo”, “uzima wa

jengo” haupimwi kwa ukubwa wake, bali hujuulikana kwa misingi yake, nguzo zake,

matumizi yake na watumizi wake.







Tuwafuate wanawake kwa misaada



Jumuiya zisizo za kiserikali zinaungwamkono duniani kote na hasa zile za

wanawake na watoto tujiweke pamoja ili tuweze kuwavutia wanawake kwa jina la

kuwasaidia. Enyi mabwana wenyekujiita wakiristo, hivyo kweli hamna hata mara moja nia

ya matengenezo kwa ajii ya Ukiristo, licha ya ubinaadamu; bali basi kwa kufisidi na

kujionesha? “….. kuwavutia wanawake kwa jina la kuwasaidia”.







.)126 : ‫" ....... و ما يمكرون إال بأنفسهم و ما يشعرون ". (الألنعام‬



“….. Na wala hawafanyii vitimbi isipo kuwa nafsi zao, nao hawatambui”.



(Al Anaám : 123).







Vitimbi vyenu viovu, haviwaleteeni lolote isipokuwa kufisidi nafsi zenu. Waswahili

wanasema, “mchimba kisima huingia mwenyewe”, na “muomba chumvi huombea

chunguche”; na, “upandacho ndicho uvunacho”. Ajabu ya mabwana hawa na hao wakuu

wao, karne na karne sasa wamo katika vitimbi vya ufisadi wao; karne zote hizi hawana lolote

walilolipata, lakini bado hawajatanabahi, bado wamo kwenye upotofu wao. Lakini hayo si

ajabu hata kidogo, hivyo ndivyo alivyoahidi Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala

kwamba madhaalimu hawatopata uwongofu.







.)85 : ‫“.......... إن اهلل ال يهدى القوم الظالمين“ . (القصص‬



“…….Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu”.



(Al-Qas’as’ : 50).







Kwa vile hawa mabwana ni madhaalimu, basi kwanza dhulma yao huwafikia nafsi zao, yaani

wao ni wenye kudhulumu nafsi zao kabla ya zile wanazopanga kudhulumu na kufisidi.

Muhimu la sisi kutanabahi hapa ni kwamba ikiwa hawa hawana uwongofu, vipi itakuwa

watowe uwongofu. Ni kanuni yenye kutambulika na kukubalika, hata kiakili tu, kwamba; “

asiekuwa na kitu hatoi kitu”. Hili liko dhaahiri kabisa, hao wenye kughurika na

kuwafuata wao, ukiwatazama utagunduwa kuwa hawana lolote la uongofu katika maisha yao

ya hapa duniani, licha ya kesho Akher, na hivyo ndio wengi wao hawakawii kutambua na

kurejea kwenye Uislamu – Alhamdulillahi.







Tuongeze vituo vya mafunzo ya kikristo



Kituo cha vijana cha mji mkongwe (Stone Town Youth Centre) kimekuwa

kikifanya kazi yake vizuri kwani hadi sasa lengo lake la ndani bali (bado)

halijaeleweka na vijana wanaohudhuria hapo kwa shughuli mbali mbali, jitihada

zifanyike ili kuwa na vituo vya aina hii katika maeneo mengine. Lengo kuu liwe ni

vijana na wanawake bila ya kuonesha dalili za kidini. Mola wetu Mlezi, Subhaanahu

wa Taáala anatupenda sana waja wake, mapenzi ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa

Taáala ni kuliko ya mama kwa mwanawe. Uovu ni wetu sisi jinsi tunavyokuwa hatuthamini

hata kidogo haya mapenzi ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala juu yetu. Miongoni

mwa mapenzi hayo, ni hivi daima kutubainishia na kutufichulia vitimbi viovu vya hawa

mabwana wenyekujiita wakiristo. Tunaona jinsi vinavyobainika vitimbi vyao viovu. Kama

tulivyotangulia kusema, sumu yao daima huizongeresha kwa vidonge vya sukari. Ndugu

zetu wenye kutumia vituo vyao hivi, khasa hicho cha (Stone Town Youth Centre), hii ndio

qauli yao. Tunaendelea kuwaomba ndugu zetu waliomo kwenye madaraka watuvue na wavue

nafsi zao na uovu huu, khasa kwa vile wao ndio wenye uwezo huo kikanuni. Inshaallah

wapate tawfiiq wafanye hivyo, Aamyn.







Tuwaowe wanawake wao kwa kusilimu kimajina



Jitihada za makusudi zifanyike ili kila itakapowezekana kuwaoa wanawake wa

Kiislamu ili tuweze kuwabatiza baadae, njia nzuri iwapo patakuwa na ugumu ni

kusilimu kiuongo ili kuruhusiwa kuwaoa wanawake wao. Wao hawa mabwana

wanasema, ”watuowe ili watubatize”. Alhamdulillahi hivi kutambuwa na kubaini

kwamba hawana la “nguvu za hoja” kuwatia watu katika huu upotofu wao, hivyo ndio

wanamalizikia kwa “hoja za nguvu” na “hoja za udanganyifu”. Yote haya si mapya, tangu

siku za Mitume a.s.w. wao hushindwa na “nguvu za hoja”, na ndipo walipokuwa

wakimalizikia kwa kutumia “hoja za nguvu”. Kwa kutumia “hoja za nguvu”, ndipo wakawa

katika mbinu za kutaka kuwauwa Mitume a..s.w. waliopelekewa na kuwatesa Waislamu.

Hali zao, uovu wao, vitimbi vyao, tangu karne na karne ndio vilevile, hapana kilichobadilika.

Wanaendelea kuishi katika giza la upotofu kwa kuukataa mwangaza wa uwongofu.

Wataendelea hivihivi mpaka wataposema yaalaiti ningelikuwa udongo:



‫م‬ ‫ن‬

.. ) 85 : ) ّ ‫"....... ياليتنى كنت ترابا ". ( الّباْ (ع‬







“…… Laiti ningeli kuwa udongo”. (Annbaaa : 50).

Tunamuomba Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala atunusuru kuwa miongoni mwa

qaumu hio, Aamyn.







Tuanzishe NGOS na sisi tuwe viongozi



Kwa hivi sasa wafadhili wengi wameonesha hamu ya kuzisaidia ngos moja kwa

moja badala ya serikali ni lazima tujitahidi kuunda jumuiya zetu ambazo

zitawashirikisha waislam lakini uongozi wa juu ni lazima uwe mikononi mwetu.

Hii itatuwezesha kuona sera zetu na malengo yetu yanatekelezwa kwa kivuli hicho.

Vitimbi vyao Inshaallah vitawarejea wenyewe. Hapana shaka hawa wenye kuleta hizi

waziitazo “Non Governmental Organizations”(NGOs) ni hawahawa mabwana wasiotutakia

kheri Waislamu, Wazanzibari. Ni tangu karne na karne, wakoloni washirika wake wakuu ni

hao mishinari. Msiba mkubwa ni hivi sisi kuwafanya mabwana hawa ndio wenzutu, kitendo

ambacho Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala ametukataza na kutuhadharisha uovu wa

mabwana hawa, lakini wapi; sisi ndio kilasiku tunazidi kuwakumbatia na kuwafanya ndio

wenzetu, bali hata kuwafanya ni wasiri wetu. Ole wetu!! Tumo tunajitia katika hilaki

kwa mikono yetu wenyewe, Ole wetu!! Yaa Rabbi tunusuru.







Tujenge ukaribu na viongozi ili kuwadhibiti waislam



Mambo yetu mengi yamekuwa yanakwenda vizuri katika maeneo mbali mbali

baada ya wenzetu kuwemo katika kamati za masheha na matawi ya vyama na

kamati za maendeleo za maeneo mbalimbali. Hali hii ni lazima iongezeke ili

udhibiti wa shughuli za waislam uwe mzuri zaidi na wakati huo huo kuona kuwa

mambo yetu yanakwenda yakiwa na baraka ya vyombo vya dola na vyama vya

siasa. “Tujenge ukaribu na viongozi ili kuwadhibiti waislam”. Daima dhamiri zao

sio njema, yote walioeleza humu katika hizo mbinu zao yamo katika njia za uvunjaji na

ufisadi, sio ujengaji na utengenezaji. Hawapangi lolote la maendeleo yao, na wanapopanga,

basi wanapanga kwa hisabu ya kufisidi binaadamu. Wanasema “wajenge ukaribu na

viongozi”, viongozi wanaokusudia hapa ni ndugu zetu, Waislamu, Wazanzibari waliomo

kwenye madaraka. Wajenge ukaribu huo kwa nia ya kuwafisidi Waislamu, Wazanzibari; sio

kwa nia ya kuutengenezea Ukiristo. Ndugu zetu mliomo kwenye madaraka, hivi ndivyo

vitimbi vyao hao mabwana wenyekujiita wakiristo, kilasiku uovu wao unazidi kudhihiri. Ni

juu yetu tuzidi hadhari na tuzidi kupanga ili tuweze kufanikiwa na kujihami dhidi ya ufisadi

wa kila fisadi.







Tuwachonganishe mashehe wenye msimamo mkali



Mashehe wenye msimamo mkali wamekuwa ni tatizo kwa ukristo kwani wana

wafuwasi wengi na wamekuwa wakisema wazi na kushutumu maendeleo yetu.

Mashehe hao ni lazima wachonganishwe na serikali ili hali ikiruhusu wazuiliwe

kuendesha shughuli zao. Wakati tukifanya hivyo hatuna budi kuwaunga mkono

mashehe wote ambo wamekuwa wakitusaidia kwa njia mbali mbali. Huu ndio

mwenendo wao, si ajabu hata kidogo. Fitna ndio mtaji na turufu yao, uwongo ndio nyenzo ya

fitna zao. Kama wanavyosema, wakati wakiwemo katika fitna zao; wakati huohuo wafanye

waweze kuwanunua wale wanaokuwa tayari “kuuza Akhera yao kwa dunia yao”,

Akhera ya daima kwa dunia yenye kupita. Muhimu tuwakumbushe hawa mabwana

wenyekujiita “wakiristo”, kwamba fitna ni mbaya kuliko kuuwa:



.)212 : ‫“........ و الفتنة أكبر من القتل .......”. ( البقرة‬







“………… Na fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa………..”.



(Al Baqra : 217).







Na Mola wetu Mlezi Subhaanahu wa Taáala, ametwambia kwamba mwenye kuwafitinisha

Waumini kisha asitubie, basi malipo yake ni kudumu maisha milele katika moto ya

Wahannamu.







.”‫“ إ ّا اّذين فتنوا المؤمنين و المؤمنات ث ّ لم يتوبوا فلهم عذاب جه ّم و لهم عذاب الحريق‬

‫ن‬ ‫م‬ ‫ن ل‬



.)15 : ‫(البروج‬







“Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha

hawakutubia, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya

kuungua”. (Al Buruuj :10).







Basi hawa mabwana wenyekujiita wakiristo, wajuwe na watambuwe kwamba hayo ndio

malipo ya wenye kutia fitna baina ya viumbe; makaazi yao ya milele ni katika Jahannamu.

Adhabu hii itawakuta vilevile wale wenye kushirikiana na kusaidiana nao katika kuwafitini

viumbe. Ajabu yao hawa mabwana wenyekujiita wakristo, kwani ni dhana yao kwamba

watawapata binaadamu wawafuate hali ya kuwa wamo katika upotofu kiwango hiki?

Ametwambia Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala:







‫“ من يشفع شفاعة حسنة يكن ّه نصيب ّنها، ومن يشفع شفاعة س ّئة يكن ّه كفل منها، وكان اهلل على ك ّ شىء‬

‫ل‬ ‫ل‬ ‫ي‬ ‫م‬ ‫ل‬

.)18:‫ّقيتا”. (النساء‬

‫م‬

“Atakayeombea maombezi mema (atakayesaidia maombezi mema hata yakatokea)

atapata sehemu katika hayo. Na atakayeombea maombezi mabaya atakuwa na

sehemu katika mabaya hayo, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye ujuzi wa kila kitu”.

(Annissai : 85).







Ikiwa Ukiristo ni dini ya mapenzi na maendeleo, tunawaasa watende mema kwa ajili ya dini

na waache njama na vitimbi dhidi ya binaadamu.







Tulenge kuifuta tabligh



Pamoja na kuwa tabligh sio hatari moja kwa moja kwa ukristo lakini bado inastahili

kupigwa vita kwa sababu ni aina pekee ya mihadhara ya waislamu inayoruhusiwa

humu Zanzibar. Tabligh inaweza kuwazindua baadhi ya waislam ambao ni vyema

kubaki bila ya kuzinduliwa. Haya ndio maneno yao, “tabligh haina khatari na ukiristo,

lakini juu ya hivyo inastahili kupigwa vita”. Kwa nini? Kwa sababu inaweza kuwazindua

Waislamu, na ni vyema kubaki bila ya kuzinduliwa. Ajabu ya mabwana hawa, sifahamu ni

maadili yepi wanayoyafuata; Uislamu unabainisha kwamba, “Hawi muumini wa kweli

mmoja wenu mpaka ampendelee nduguye lile analojipendelea nafsi yake”. Sasa hawa

mabwana wenyekujiita wakiristo, ikiwa wao hawawapendelei kheri binaadamu wenziwao,

vipi wanatarajia kupata mapenzi ya binaadamu wenziwao? Vipi wanatarajia wapate

mapenzi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala? Hivyo ni kweli haya ndio

mafunzo ya Ukiristo? Hapana shaka haya sio. La hakika zaidi ni kwamba hawa sio Wakiristo

wa kweli. Waswahili wanasema, “Chema chajiuza, kibaya chajitembeza”.







Tudai turudishiwe taasisi zetu



Serikali ya Zanzibar bado inaonekana kuwa ngumu kurudisha katika milki ya

makanisa ardhi na taasisi zetu. Dalili za huko nyuma zilionekana nzuri kwani

tulifanikiwa kupata hospitali yetu ya Welezo na eneo la kiungani hata hivyo

panakuwepo ugumu wa kurudishiwa shule zetu. Kwa kuwatumia wenzetu

waliomo serikalini na baraza la wawakilishi lazima tuzidishe harakati na madai ya

taasisi zote zilizobaki. Wao wanadai kurejeshewa taasisi zao, tunawakumbusha kwamba

Waislamu wameporwa Chuo chao Kikuu Cha Ufundi, (MIOME), wamenyangánywa jumuia

yao iliokuwa na manufaa makubwa, “East African Muslim Welfare Society” (EAMWS), si

kwa Waislamu tu; bali kwa Afrika Mashariki, bali kwa Afrika nzima. Isitoshe, Waislamu

daima dawamu wananyimwa fursa za masomo ya juu, wananyimwa fursa ya kazi za

dhamana, Jeshini, Polisi, Vikosi vya Usalama, Magereza, Ubalozini na mwingi

mwenginemo. Wananchi katika nchi yao ambao kwa hio hisabu yao wao mabwana wenye

khatamu za nchi, basi Waislamu Tanganyika hawapungui 65% na Zanzibar hawapungui

98%, hii leo baada ya mavamizi ya 1964 na kumezwa Dola Huru ya Zanzibar. Mzee

Kambona baada ya kuona maji yanazidi unga, yaani dhulma ya Nyerere juu ya Waislamu,

alimnasihi asiwabane sana Waislamu. Kambona haiwi kafanya hivyo isipokuwa zaidi ni kwa

manufaa ya hao wakiristo. Lakini wapi, Mwalimu hakuacha mbinyo wake juu ya Waumini

mpaka akafika mbele ya haqi.







Tulete waumini kutoka mashamba kuanza makanisa



Hivi sasa pameibuka wasi wasi kuhusiana na wingi wa makanisa ambayo

hayajapata waumini wa kuyajaza. Ili kuficha dosari hii na hoja kadhaa utaratibu

uliopo hivi sasa chini ya baadhi ya makanisa ni lazima uungwe mkono. Wakristo

wahamiaji wengi hufikia mashamba hivyo pawekwe na utaratibu wa kuwaleta mjini

ili kujaza makanisa. Almuradi mumo mbioni tu, leo wa shamba wapelekwe mjini, kesho wa

mjini wapelekwe shamba, leo wa bara wapelekwe visiwani, kesho wa visiwani wapelekwe

bara. Leo wa Machui wapelekeni Mahonda, kesho wa Mahonda wapelekeni Kama. Mabwana

wakubwa! Wengi wa hawa munaowasema “wakiristo”, ni wenye kutafuta riziki, dini kwao

ni hadithi tu, huko mashamba ndiko kwenye mbio zao za kujipatia riziki, riziki wajisaidie

nafsi zao na watu wao waioko huko mabara. Zanzibar wamekuja kutafuta riziki, kama

walivyokuwa wakifanya miaka na miaka, tafadhalini waacheni waishi kwa amani na

mafahamiano na wenyeji wao, wacheni kuwajengea fitna na bughdha na wanyeji wao kwa

maslaha yenu binafsi, wala si kwa huo ukiristo mnaojinasibu nao.









NENO LA MWISHO



Wapendwa katika Bwana.



Miongozo hii ni mikubwa na inaweza kuwatisha baadhi ya waumini wa kikristo

hasa wale ambao bado hawajampokea Roho Mtakatifu vizuri. Hata hivyo kwa

uwezo wa Bwana Mungu wetu ni mpango rahisi. Suala la muhimu ni haya

kufahamika na kila mkiristo apendae kumtumikia Bwana. Pia hatuna budi

kuishukuru awamu ya nne ya serikali ya mapinduzi ambao imefungua milango

kwa ukristo na kushuhudia ongezeko la makanisa.







Bwana awe nasi!







Nasi tunasema, “Enyi Wapendwa katika Bwana”, Enyi Wakiristo wa kweli, tafadhalini

inukeni muutakase Ukiristo na aibu kama hii unaopakwa. Aibu ya kunasibishwa na kila uovu

na njama dhidi ya binaadamu. Aibu ya kuitia Sirikali ya Zanzibar katika ushirika wa njama

hizi za uovu dhidi ya Waislamu, Wazanzibari.







Kukumbushana ni Waajibu kwa Waumini



Ametutaka Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala tukumbushane; kwani

kukumbushana kunawafaa Waumini, Inshaallah tuwe wenye kunufaika.









. 88 .”



“Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini”.



(Adhaariyaat : 55).







Kwa vile sisi ni Waumini ni wajibu wetu kukumbushana. Kwanza tunawaomba

ndugu zetu waliomo kwenye madarka na uongozi watumie wakati wao thamini

wausome huu waraka wa hawa jamaa wenyekujiita wakiristo. Wakishausoma, kwa

kituo; tunawaomba wazingatie vyema yaliomo kwenye waraka huu na wazingatie

wajibu wa dhamana yao, kuwa vile wao ndio viongozi wa huu Umma wa

Waislamu, Wazanzibari. Katika huko kuzingatia tunawaomba wazingatie yaliomo

kwenye Quráni Tukufu, khasa Aya tatu hizi. Tunawaombea viongozi wetu na

Sirikali yetu ya Zanzibar kwa jumla kila kheri na baraka na mafanikio katika

utumishi waliochukuwa dhamana ya kuutekeleza. Tunapenda kuzidi

kuwahakikishia kwamba Umma wa Zanzibar chini ya umoja wao, Umoja wa

Wazalendo, daima uko pamoja nao kwa kila hali kwa maslaha Nchi yetu na vizazi

vyetu.







‫ي ا‬

‫" يآأ ّها ّلذين آمنوا ال تتخذوا بطانة من دونكم اليألونكم خباال، ودوا ماعنتم، قد بدت البغضآء من أفواههم، وماتخفى‬

.)111 : ‫صدورهم أكبر، قد بينا لكم الآليات ان كنتم تعقلون”. (آل عمران‬



Enyi mlioamini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha

kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao

katika midomo yao. Na yanayo fichwa na vifua vyao ni makubwa zaidi.

Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini”.



(Al-‘Imraan : 118).







‫“ يآأ ّها اّذين آمنوا قوا أنفسكم وأهليكم نارا وقودها الناس والحجارة عليها مالئكة غالظ شداد ال يعصون اهلل مآأمرهم‬

‫ي ل‬

.)6 : ‫ويفعلون مايؤمرون”. (التحريم‬



" Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu wenu, na Moto ambao kuni zake ni

watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu hawamuasi

Mwenyezi Mungu kwa amri zake; na wanatenda wanayo amrishwa (yote)”. (At-

tahriim : 6)..







‫“ من يشفع شفاعة حسنة يكن ّه نصيب ّنها، ومن يشفع شفاعة س ّئة يكن ّه كفل منها، وكان اهلل على ك ّ شىء‬

‫ل‬ ‫ل‬ ‫ي‬ ‫م‬ ‫ل‬

.)18:‫ّقيتا”. (النساء‬

‫م‬



“Atakayeombea maombezi mema (atakayesaidia maombezi mema hata yakatokea)

atapata sehemu katika hayo. Na atakayeombea maombezi mabaya atakuwa na

sehemu katika mabaya hayo, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye ujuzi wa kila kitu”.

(Annissai : 85).







Tunamuomba Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala atujaalie kila kheri na

baraka na atuepushe na kila shari, na atuzidishie tawfiiq, uwezo na uwongozo

katika huu utumishi wa Dini yetu tukufu na wa’tani wetu ghali, Lillahi Taáala,

atuepushe na ria, atuepusehe na taájub, na atuepushe na kibri; Aamyn, Yaa Rabbi,

Aamyn.







Wa Billahi Tawfiiq







Umoja wa Wazalendo







Zanzibar



July 10, 2009



Related docs
Other docs by gegeshandong
A_E_KY-4PSE30WUSeries-Rev1012A
Views: 0  |  Downloads: 0
688_xls
Views: 0  |  Downloads: 0
2-1 辫措康
Views: 0  |  Downloads: 0
VINPR Lit Order Form New Jan 09
Views: 0  |  Downloads: 0
WRECKED - Torino Film Festival
Views: 0  |  Downloads: 0
project2btestcases
Views: 0  |  Downloads: 0
Fund Account transfer form9.2011
Views: 0  |  Downloads: 0
By registering with docstoc.com you agree to our
privacy policy

You are almost ready to download!

You are almost ready to download!