Ndugu zetu, Wazee wetu,
Assalaam Alaaykum,
UMOJA, UHURU, UADILIFU
Waraka Maalum Kwa Wakristo Zanzibar
Tunaleta hapa huu “Waraka maalumu kwa Wakiristo Zanzibar”. Waraka huu
umepatikana na Waislamu, Zanzibar katika nusu ya pili ya mwezi wa June, 2009.
Waraka huu unaonesha dhaahir shaahir mbinu zao dhidi ya Waislamu,
Wazanzibari. Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala Inshaallah
awashinde na kila uwovu wao, Yaa Rabbi kula ajae na shari, waijua yake siri, ivunjé
yake dhamiri asiweze kusimama; Aamyn, Yaa Rabbi Aamyn. Tutajaribu kueleza juu
ya waraka huu kwa khati za Italic kama ifuatavyo humu. Tulioyakoleza kwa khati
nyekundu ndio tunaona khatari yake zaidi na kutaka tuyafahamu zaidi na tujikinge
nayo. Muhimu, tafadhali tuusome waraka huu tupate kufahamu mbinu zao na
chuki zao dhidi ya Waislamu, Wazanzibari; ili tutahadhari nao. Muhimu tusisahau
Qauli ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Ta’aala alipotueleza juu ya uovu wa
hawa wenye kuwapiga vita Waislamu, Wazanzibari kwa jina la Ukiristo.
“يآأيها ّلذين آمنوا ال تتخذوا بطانة من دونكم اليألونكم خباال، ودوا ماعنتم، قد بدت البغضآء من أفواههم، وماتخفى
ا
.)111 : صدورهم أكبر، قد بينا لكم الآليات ان كنتم تعقلون”. (آل عمران
Enyi mlioamini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha
kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao
katika midomo yao. Na yanayo fichwa na vifua vyao ni makubwa zaidi.
Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini”.
(Al-‘Imraan : 118).
Lakinibasi, kuyafahamu ni ndivyo; bali kuyaondoa ni waajibu wa kila mmoja wetu
kwa kadiri ya uwezo wake. Hapana shaka ndugu zetu walioko kwenye madaraka
na uongozi na sisi, waongozwa kushirikiana nao na kwa hikma na busara, wao ndio
wenye wajibu zaidi wa kuchukuwa khatuwa za kuyaondoa maovu hayo, tena
hufuatia wenye vyombo vya khabari na mashekhe wanye kuwaidhi.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala atujaalie kila la
kheri na baraka; Aamyn.
Wa Billahi Tawfiiq
Umoja wa Wazalendo
Zanzibar
June 24, 2009
WARAKA MAALUM KWA WAKRISTO ZANZIBAR
Wapendwa katika Bwana
Ndugu Wakristo umefika wakati tumeonelea kuwa ipo haja ya kuwaelezeni
machache ili kuona maendeleo yetu na mafanikio tuliokwisha yapata hapa Zanzibar,
yanaendelezwa na hayarudi nyuma kwa namna yoyote. Hapana shaka kuwa
munaelewa kuwa idadi yetu hadi sasa bado ni ndogo sana na wengi wetu tungali
katika kiwango na hadhi ya wahamiaji na sio Wazanzibari kama wanavyosema
wenyewe.
Wanatwambia, “….yanaendelezwa na hayarudi nyuma kwa namna yoyote”. Qauli
yao hii inadhihirisha vipi walivyo azimia kuendeleza mbinu zao ovu dhidi ya Uislamu hapa
kwetu, Zanzibar.
MAFANIKIO YETU
Kabla kugusia yale ambayo tunahisi ndio lengo la waraka huu hapana budi
kuwatajieni mambo machache ambayo tumefanikiwa kuyapata hadi sasa. Pamoja
na jitihada zetu za muda mrefu bado tunapaswa tumsifu Bwana kwa msaada
wake mkubwa kwetu dhidi ya maadui zetu. Tunaamini kuwa kupitia nguvu za
Roho Mtakatifu, Bwana atatupa ushindi na mafanikio makuu zaidi ya haya na
atawafumba macho maadui zetu wazidi kulala ili mipango yetu yote ya
kuibadilisha Zanzibar kidemografia ifanikiwe katika kipindi kifupi kijacho.
Mafanikio yetu yameenea katika kila upande - katika uchumi, siasa, huduma za
serikali, umiliki wa ardhi, ujenzi, elimu, n.k. Ili kupata picha kamili ni vyema
tuorodheshe kwa ufupi mafanikio hayo:
“Pamoja na jitihada zetu za muda mrefu bado tunapaswa tumsifu Bwana kwa
msaada wake mkubwa kwetu dhidi ya maadui zetu”. Wameanza kwa kusema,
“Pamoja na jitihada zetu za muda mrefu”, hii ni ithbati ya hali kwamba mbinu zao
dhidi ya Uislamu “ni za muda mrefu”, wakaendelea kueleza, “dhidi ya maadui zetu”,
yaani sisi Waislamu ndio “maadui wao”. Hivi kuwa wao Wakiristo wanatufanya sisi ni
“maadui zao”, hufaa tujiulize lipi la uadui tuliloufanyia Ukiristo sisi Wazanzibari, tangu
taarikh ya miaka, bali karne nyuma? Ingelikuwa vyema kama wangalitueleza uadui
tulioufanyia Ukiristo au Wakiristo sisi Wazanzibari. Hauko, wala hawawezi kutaja hata
moja; tunawataka wataje kama uko. Lakini ihsani nyingi tumeufanyia Ukiristo hio
miaka mingi iliopita, ni Ufalme wa Zanzibar uliowapa Wamishinari hapa Zanzibar nyumba
ya kuendeshea ibada zao na kuwapa waongozi wa njia kuelekea barani Afrika kwa kuondokea
hapa Zanzibar. Hapana shaka maneno haya hayakubaliwi na ndugu zetu Wakiristo wa
Kizanzibari ambao tumeishi miaka na miaka kwa masikilizano na mapenzi, kwa la furaha na
kwa la msiba; daima tuko pamoja. Tumeishi katika ustahamilivu mkubwa wa imani
mbalimbli, bali hata mila mbalimbali, hapakuwepo yeyote kumbughudhi mwengine; sote
tukiishi kuwa ni Wazanzibari. Hakika ni kwamba hawa wenye maneno na mbinu hizi za
ufisadi sio Wakiristo wa kweli, hawa ni mishinari wenye kufanyakazi begakwabega na
wakoloni tangu karne na karne katika misingi ya siasa yao ya “WAGAWE ILI
UWATAWALE”. Wanafanya hivi si kwa maslaha ya Ukiristo, wanafanya hivi kwa maslaha
yao ya kutoamini dini “secularism”, na kuitumia imani kuwa ni njia ya chumo la kujaza
mifuko yao. Wamishinari hawa na wakoloni karne na karne mbinu zao ni fitna za kuwagawa
Umma ili waendeleze maslaha yao. Huwagawa Umma kwa kutumia dini, ukabila bali hata
rangi, kipato au madaraka.
1. Nafasi yetu kwa upande wa elimu imekua ya kuridhisha kupitia nafasi za
serikali. Hivi sasa ni rahisi na limekua jambo la kawaida katika kila matangazo ya
wito wa masomo kusikia majina ya Wakristo. Kati ya vijana saba hadi kumi, ni
lazima upate vijana wawili hadi watatu kutoka katika makanisa yetu. Qauli yao
kuwa “kupitia nafasi za serikali”, hapana shaka, hivi ni kwa kuwa Tanganyika wao ndio
dola, wao ndio sirikali, wao ndio wenye kupanga na kupangua kukhusu ilimu. Kati ya
vijana 7 hadi 10, ni lazima upate vijana wawili hadi watatu kutoka katika
makanisa yetu. Ikiwa wao Wakiristo walioko Zanzibar, ambao haidhaniwi kuwa wanafika
10% ya Wazanzibari; wanapata baina ya 20% hadi 30% ya fursa za masomo; itafahamika
vyema mbinu wanazozitekeleza (wao Wakiristo) katika kuwazuilia fursa za masomo
Wazanzibari, Waislamu; hilo ni miongoni mwa maazimio yao makuu. Waislamu,
Wazanzibari wasipate ilimu ya maana; walazimishwe kuishi katika ujinga.
2. Sambamba na matangazo ya elimu vijana wetu wamekuwa wanapata nafasi
nyingi za ajira katika Serikali ya Zanzibar. Hali ya kutoelewana kisiasa baina ya
Wazanzibari imetoa mwanya kwetu kuingiza vijana wa Kikristo wenye asili ya
bara kwa wingi kwani wamekuwa wanaaminika zaidi kuliko vijana wa Zanzibar.
Tuizingatie hii qauli yao, “vijana wetu wamekuwa wanapata nafasi nyingi za ajira
katika Serikali ya Zanzibar”. Hali hii si ajabu, kwa sababu wao Tanganyika ndio wenye
sauti na amri ya kuajiri, tangu huko bara na hapa visiwani. Inasemwa na wengi kwamba
hapo BoT, (Bank of Tanzania) (Bank of Tanganyika), hata mpika chai, licha ya dereva;
anajiriwa kutoka bara, Mzanzibari hafai. “Hali ya kutoelewana kisiasa baina ya
Wazanzibari imetoa mwanya kwetu kuingiza vijana wa Kikristo wenye asili ya
bara kwa wingi kwani wamekuwa wanaaminika zaidi kuliko vijana wa
Zanzibar”. Naam, hii ndio faida khasa ya wao kupanga na kutekeleza hali ya kutoaminiana
na kuvutana Wazanzibari, lakinibasi, hilo lishapitwa na wakati. Alhamdulillahi, leo
Wazanzibari wakiwa kwenye Umoja wao wa Wazalendo wote qauli yao ni moja juu ya kila la
Nchi yao, kwa maslaha ya Nchi yao, hawana tena siasa za kichama, siasa zenye kutumika
kwa kujenga mfarakano baina yao. Wajuwe na watambue hawa mabwana wenye kujiita
wakiristo kwamba uwaminifu wa vijana wa Kizanzibari kwa jumla ni wa daraja ya juu
kabisa, wachache ulimwenguni wa mfano wao. Hali hii si ajabu hata kidogo, kwani haya ndio
malezi ya wazee na wazee wa wazee wetu, uwaminifu, mapenzi, kusaidiana, kushirikiana,
kushauriana na ustahamilivu wa kidini ndio sifa ya Wazanzibari tangu karne na karne.
Suala la kuajriwa zaidi vijana wa Kikiristo kuliko vijana wa Kiislamu, Kizanzibari; katika
nchi yao wenyewe, Zanzibar; ni miongoni mwa mbinu zao Wakiristo katika kuongeza idadi
ya Wakiristo hapa visiwani ili wajaze makanisa yao. Wanafanya hivyo ili waweze kudai
misaada kutoka huko Uzunguni, kutoka makanisani na/au watubinafsi, hivyo wapate fedha
hizo wajaze mifuko yao kwa kisingizio cha kueneza Ukiristo. Vilevile katika hivi kuwapatia
zaidi ajira vijana wa bara wanaowajaza hapa nchini mwetu bila ya kitambulisho chochote cha
uingiaji nchini, ni katika kuiandalia (CCM) “Catholic Christian Movement”, “Chama Cha
Mwalimu”, kuandaa wapigakura kwa makusudio ya kuendelea madarakani katika kuitawala
Zanzibar na kuendeleza mbinu zao dhidi ya Waislamu, Wazanzibari. Ndugu zetu
Wazanzibari mulioko kwenye uongozi, katika vyama na/au Sirikalini, na Wazanzibari sote
kwa jumla, haya ndivyo yalivyo; tafadhalini tukumbuke hii Qauli ya Mola wetu Mlezi,
Subhaanahu wa Taáala anayotutaka tuokoe nafsi zetu na ahali zetu kutokana na adhabu kali
ya Moto:
“يآأ ّها اّذين آمنوا قوا أنفسكم وأهليكم نارا وقودها ال ّاس والحجارة عليها مالئكة غالظ شداد ال يعصون اهلل مآأمرهم
ن ي ل
.)6 : ويفعلون مايؤمرون”. (التحريم
" Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu wenu, na Moto ambao kuni zake ni
watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu hawamuasi
Mwenyezi Mungu kwa amri zake; na wanatenda wanayo amrishwa (yote)”. (At-
tahriim : 6)..
3. Hali tulioieleza juu imetuwezesha kuwa na Wakirsto wengi katika nafasi za
juu serikalini na katika chama tawala. Tunarejea tena kufahamishana sisi Wazanzibari,
Waislamu; yote haya wanajifanyia, au wanafanyiwa wao Wakiristo kwa sababu wao ndio
wenyewe dola, na wao ndio wenyewe khasa chama, bali wao ndio khasa wenye khatamu za
uongozi wa Tanganyika, Tanganyika ambayo ndio yenye kuitawala Zanzibar baada ya
kuivamia na kuimeza siku ile ya Januari 11, 1964. Kutokana na hali hii, ilivyo ni hivi;
Tanganyika inatawaliwa na Kanisa, Zanzibar inatawaliwa na Tanganyika, kwahivyobasi,
Zanzibar inatawaliwa na Kanisa. Wazanzibari CCM sio yao, Wazanzibari, Waislamu;
si wanachama wa “Chama Cha Mwalimu, “Chama Cha Msalaba””, chama hichi wenyewe
khasa ni wao wenyekujiita wakiristo.. Hali hii ni lazima iendelezwe katika ngazi zote
kwani imekuwa ikitusaidia hasa katika kiwango cha masheha na kamati zao
kwani huku ndiko kunako mambo mengi ya kila siku. Hizi ndizo mbinu zao ovu
kuwatendea Waislamu, Wazanzibari. Kwa hivi kuwa mbinu zote hizi zinafanywa kwa
kushirikiana makanisa na utawala Tanganyika; kwa vile wao Tanganyika ndio dola na ndio
nchi, sisi Wazanzibari, “Zanzibar si Nchi”, ndio kilasiku tunazidi kuangamizwa, sisi na
vizazi vyetu. Njia pekee ya kuondoa maafa haya ni “Zanzibar kurejea kuwa Nchi, Dola
Huru Kaamili; kama ilivyokuwa Zanzibar yetu siku ile ya Disemba kumi, 1963
ilipopata uhuru wake na kujiunga na Umoja wa Mataifa (UN), taarikh kumi na
sita, Disemba hiohio ya 1963”. Kila jambo la kheri linahitajia Umoja, mashauriano na
mashirikiano, lakini hili la ukombozi wa Nchi yetu linahitaji zaidi Umoja, ushirikiano na
mashauriano. Kwahivyobasi, ni wajibu wetu sote kuwacha mfarakano na kujenga
mshikamano, ili tukomboe Nchi yetu, Zanzibar irejee katika kheri na neema zake na itokane
na idhalaali, Aamyn.
4. Tumepata fursa ya kutumia Taasisi za serikali kwa uendeshaji wa ibada zetu
hali hii imefanya tuzidi kukubaliwa na Waislamu na kuvumiliwa na inaweza
kutupa nafasi ya kuwavuta katika NENO LA BWANA. Tunarejea tena qauli yetu
ileile kama tulivyojaaliwa kueleza hapo juu, yaani kwa sababu tumevamiwa na tukafanywa
kuwa “Zanzibar si Nchi”, ndio ikawa tunafikishiwa yote haya ya idhlaali na mbinu za
uangamizi, wetu sisi na khasa vizazi vyetu.
5. Kwa upande wa mashamba (vijijini) tumepata wasaa mzuri wa kununua ardhi
toka kwa Waislamu ambao hadi sasa bado hawajashtuka. Ardhi hizi
zimetuwezesha kujenga makanisa kadhaa mabayo hapo awali hayakuwepo. Jee,
tunasemaje sisi Wazanzibari, Waislamu; wenye kuuza ardhi zetu, bali hata mava zetu
kilasiku? Haya ndio makusudio yao mabwana kwa kuzivamia ardhi zetu. Tusisahau kwamba
kwa kuwauzia ardhi zetu, mbali ya khasara kubwa ya kuuza ardhi, tuna adhabu ya Mola
wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala kwamba ardhi zetu ndizo zinazojengwa makanisa ndani
yake. Tunauza Akhera yetu kwa khasara ya duniani, tunakhasirika duniani na Akhera..
Khasara ilioje hii! Yaa Rabbi tunusuru waja wako!! Ya Rabbi tunusuru waja wako!!
Mweyezi Mungu Mtukufu amrehemu Dr. Omar Ali Juma; aliyaona haya mapema na
akatahadharisha, lakini hayakupata sikio la kheri. Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu
wa Taáala amlipiea kwa kila aliemdhulumu na iwe ni upungufu wa makosa yake, Aamyn.
6. Idadi ya skuli na vituo vyetu (ambavyo licha ya picha ya juu kuwa
haviendeshwi kwa misingi ya Kikristo lakini kiukweli ni vituo vya kimisionari)
vimeongezeka kwa hali ya kuridhisha. Skuli hizi nikuanzia kwa watoto wadogo
hadi vituo kama hichi kilichopo Mji Mkongwe (Stone Town Youth Centre) na
zinafanya kazi vizuri katika kupandikiza mila za Kikristo. Haya ndio maneno yao
wenyewe, hivi vituo vyao japo hujaribu kudanganya kuwa haviendeshwi kwa msingi wa
Kikiristo, lakini kiukweli ni vituo vya kimishinari. Vituo hivi ni kuanzia skuli za watoto
wadogo mpaka hiki cha “Stone Town Youth Centre”. Vyote hivi ni kwa makusudio ya
kueneza ukiristo dhidi ya Uislamu, Wazanzibari. Lakinibasi, kama tulivyo tangulia kusema,
vitimbi vyao hivi ni vya tangu kale na kale; wala havijaleta lolote kuongeza huo ukiristo
wanaodai kuuwania. Na vipi isiwe hivyo, Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa
Taáala ametueleza hayo bayana kabisa. Wamokutoa mali yao tangu karne na karne, na
wataendelea kutoa, lakini hali itabakia ileile, khasara na majuto. Mwenyezi Mungu Mtukufu,
Subhaanahu wa Taáala hawi pamoja na mwenye kufisidi, wala mwenye kumsaidia mwenye
kufisidi. Fisadi yeyote yule, daima hufisidi nafsi yake.
ّ م د ن ل
، " إ ّ اّذين كفروا ينفقون أموالهم ليص ّوا عن سبيل اهلل ، فسينفقونها ث ّ تكون عليهم حسرة ثم يغلبون
ن ل
.) 66 : و اّذين كفروا إلي جه ّم يحشرون" . (األنفال
“Hakika wale walio kufuru hutoa mali yao ili kuzuia Njia ya Mwenyezi Mungu.
Basi watayatoa, kisha yatakuwa juu yao majuto, na kisha watashindwa. Na wale
walio kufuru watakusanywa kwenye Jahannam
(Al Anfaal : 36).
Hii ni Qauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala, haiendi pogo hata
mara moja, ni iwe tu; kun-faya-kun, bila kizuizi. Lakinibasi, ni wajibu wetu kujitahidi
kutekeleza na kuhifadhi Dini yetu kwa ajili ya dunia yetu na Akhera yetu.
7. Sera ziliopo hivi sasa kwa upande wa uingiaji na utokaji Zanzibar imetusaidia
sana katika uingiaji wetu (Wakristo) kutoka Bara na hivyo kusaidia kufuta ile
imani ya kuwa Zanzibar ni kisiwa cha Waislamu na eti Wazanzibari kwa zaidi ya
aslimia 99 ni Waislamu. Hii sera ya uingiaji na utokaji Zanzibar, yaani bila ya
vitambulisho sio tu imesaidia kuendeleza hujma dhidi ya Uislamu, Wazanzibari; kwa kupitia
mishinari, bali zaidi imeleta wimbi kubwa la uharamia na ujambazi nchini Zanzibar.
Zanzibar imegeuzwa chaka la watoro, watu wanaingia vile wanavyotaka, hufanya ujambazi
wao, huuwa, huiba; kisha hupanda vyombo na kutoweka. Inafaa tukumbushane kwamba kila
aliesaidia kuleta hali hii, hali ya uovu kabisa, basi anafungu lake la ghadhabu ya Mwenyezi
Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala:
“ من يشفع شفاعة حسنة يكن ّه نصيب ّنها، ومن يشفع شفاعة س ّئة يكن ّه كفل منها، وكان اهلل على ك ّ شىء
ل ل ي م ل
.)18 : ّقيتا”. (النساء
م
“Atakayeombea maombezi mema (atakayesaidia maombezi mema hata yakatokea)
atapata sehemu katika hayo. Na atakayeombea maombezi mabaya atakuwa na
sehemu katika mabaya hayo, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye ujuzi wa kila kitu”.
(Annissai : 85).
Maafa ya kuachiliwa watu kuingia Zanzibar bila kitambulisho, kila Mzanzibari anayafahamu
na analipa thamani yake kwa kila njia na kila hali. Kwahivyobasi, ni waajibu wa kila mmoja
kufanya kila analoweza kuhakikisha kwamba kuingia Zanzibar – sawa na nchi yoyote ile
ulimwenguni - ni kwa kutumia vitambulisho vyenye kukubalika kikanuni. Wajibu huu ni
juu ya ndugu zetu Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi, tunawaomba walitilie hima suala
hili mpaka litekelezwe.
8. Ujaji wa Wakristo kwa wingi kutoka bara umewezesha kuongezeka kwa idadi
ya mabaa na klabu za pombe. Hivi sasa ni jambo la kawaida kuona magari ya aina
mbalimbali yanayomilikiwa na eti Waislamu yanabeba kreti za pombe kali.
Maneno yao yanathibitisha maelezo yetu kwamba hawa si “Wakiristo wa kweli”, hawa ni
wamishinari ambao tangu karne na karne ni wenye kufanyakazi na wakoloni begakwabega
katika kuupiga vita Uislamu nyuma ya pazia la Ukiristo. Kama wanavyosema, ujaji wa
Wakristo wa namna hii umeongeza idadi ya mabaa na klabu za pombe, bali pia umeongeza
idadi ya nyumba za uchafu. Haya ndio makusudio yao khasa, ujaji wao kwa wingi
haujaongeza idadi ya waumini wao; makanisa yao bado ni matupu, na yataendelea kuwa
matupu. Kuupiga vita Uislamu, Wazanzibari; kwao ni muhimu zaidi kuliko
kuujenga Ukiristo. Inafaa wafahamu kwamba mbinu zao hizi ovu hazitaleta matunda, kwa
sababu Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala ameahidi kuihifadhi Dini yake:
.)1 : “ يريدون ليطفئوا نوراهلل بأفواههم واهلل متم نوره ولو كره الكافرون”. )ال ّف
ص ّ
“Wanataka kuizima nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao. Na Mwenyezi
Mungu atakamilisha nuru yake ijapo kuwa makafiri watachukia”. (Ass’af : 8 ).
Juhudi zao za kuupiga vita Uislamu ni za tangu karne na karne, lakini Alhamdulillah; kama
alivyoahidi Subhaanahu wa Taáala haiwaongezei wenye kujaribu kuupigavita Uislamu
isipokuwa khasara na ghamu. Dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala
kilasiku inazidi kukua na kushamiri, na Inshaallah itaendelea hivyo daima dawamu. Kwa
kuvamiwa Nchi yetu na kumezwa chini ya huu wenyekuitwa muungano, tukawekwa katika
hali mbaya kabisa ya kiuchimi, ndio tumefika baadhi yetu kuingia katika upungufu wa imani
kufika kushiriki katika maasi haya ya ulevi. Kwa kitendo chetu hiki ndio hawa mabwana
wanafika kutuita, “eti Waislamu”; yaani Uislamu wetu wanaubeza.
9. Kujiingiza kwetu katika Taasisi za dola katika ngazi za mitaa kumetuwezesha
kupata nafasi ya kutangaza Ukristo kwa njia ya mihadhara. Hapana shaka kujiingiza
kwao huku kunapata kuungwamkono na kusaidiwa na baadhi yetu sisi wenyekuitwa “eti
Waislamu”. Tafadhali naturejelee hayo maneno ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taála
hapo juu, kukhusu malipo ya mwenye kusaidia katika kitendo, au hata maneno; ikiwa kwa
wema au kwa uovu. Malipo ni kulingana na kitendo au maneno. Yaa Rabbi tujaalie wenye
kusaidia katika kheri.
Wakati huo huo kudhibiti mihadhara ya wazi ya Waislamu kwa kutumia madai ya
kashafa na kutatanisha maelewano mazuri baina ya watu wa dini tafauti. Hii ndio
sera na mwendo wao, hawana ukweli, nifaaq ndio mwendo wao. Mbinu zao ni kutumia
uwongo katika kutaka kuwazuilia Waislamu, Wazanzibari kuendeleza Dini ya Mwenyezi
Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala kama alivyoamrisha. Hivi ndivyo walivyo tangu
karne na karne, tangu siku za Mitume a.s.w., kwa hii inadi yao Mwenyezi Mungu Mtukufu
akawapiga mihuri ya upotofu.
10. Tumefanikiwa kupata viwanja vingi katika maeneo ya Mjini ambayo yangali
mapya. Maeneo haya ni kama Tomondo, Mombasa, Mwanakwerekwe, n.k. ambayo
tayari tumeshajenga makanisa yetu ingawaje kwa sasa hayajawa na waumini
wengi wa kuyatumia na bado yanaonekana ni matupu. Vingi ya viwanja hivi
wamevipata kwa kuvinunua kutoka kwetu sisi Waislamu, Wazanzibari; miongoni mwa
viwanja hivi pia ni “eka”, mali yalionyangánywa na kugaiwa vipande vipande. Haramu hii
ya unyangányi ya mali ya watu imeongezeka haramu kwa hivi kutumiwa ardhi hizi
kujengwa makanisa, si kwa kuabudiwa; kwani hao wakuabudu hawapo, bali kwa kuleta
idhlaali kwa Waislamu, Wazanzibari na utekelezaji wa mbinu zao za kujaribu kuupigavita
Uislamu.
Ndugu wapendwa katika bwana,
Mafanikio hayo yasitufanye tuka lewa na kusahau jukumu la kanisa la kuona kuwa
utawala wa Bwana unashuka Zanzibar haraka iwezekanavyo. Kosa lolote
tutakalofanya hivi sasa litaweza kuturudisha hatua kadhaa na huenda nafasi hii
tulionayo hivi sasa tusiipate kwa karne mpya ijayo. Mambo ya kufanya
yanayotukabili ili kuimarisha nafasi yetu na kuona yale tuliokwisha yapata
hayatutoki na kuyafanyia dira kwa karne ijayo ni haya yafuatayo:
Tusahau tafauti zetu dhidi ya adui
Ingawaje tupo madhehebu nyingi lakini tunawajibika kuelewa kuwa Waislamu na
Uislamu wao ni adui yetu namba moja ambaye hatutofaulu kupambana nae mmoja
mmoja. Uislamu hapa Zanzibar ni dini iliofungamana na mila na utamaduni hivyo
kila itakapowezekana tusahau tafauti zetu ndogo ndogo na hata kubwa kukabiliana
nao, vyenginevyo tutarudi kama wakati wa Karume. Wanabainisha tena fahamu yao
potofu kwamba “Waislamu na Uislamu wao ni adui yetu namba moja”. Kama
tulivyotangulia kuelezana, sisi Waislamu, Wazanzibari hatuna uadui na Wakiristo, tumeishi
pamoja kwa furaha, amani na mapenzi kwa miaka na miaka.
Tuhakikishe tunapata ardhi
Hii ni mbinu kongwe katika usambazaji wa Ukristo. Wazee wetu walipoleta
Ukristo Zanzibar na katika Afrika jitihada waliyofanya ni kupata ardhi kubwa kwa
ajili ya ujenzi wa maeneo yetu majengo ya hospitali shule zahanati vituo vya
chekechea makanisa n.k. Tunahitaji ardhi kubwa ili kuziweka huduma hizo
mahala pamoja kwa ajili ya kueneza injili ya bwana na Muokozi wetu. Wazanzibari,
hii ndio mbinu yao; wazipate ardhi zetu kwa kuenezea hizo mbinu zao potofu, mbinu za
ufisadi dhidi ya ubinaadamu, mbinu wenyekuziita ukiristo, na hakika sio Ukiristo wa kweli.
Katika hali hii, inafaa tuchukue kila hadhari kuhakikisha kuwa hatuuzi ardhi zetu,
khasa kwa waliokuwa si katika sisi, yaani Waislamu, Wazanzibari. Ugawaji wa eka
umesaidia pakubwa katika wao kuzipata ardhi zetu na kuendeleza ujenzi wa makanisa nchini
mwetu. Tena tunarejelea Qauli ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala tulioitaja hapo
juu kukhusu kusaidia katika wema na katika uovu; na wewe utapata sehemu yako, ikiwa ni
kheri au ni shari. Tutahadhari na kuuza ardhi zetu. Tuhakikishe hatuuzi ardhi zetu
kwa hali yoyote ile. Kuuza ardhi sio kuondoa umasikini, bali ni kuzidisha
umasikini na ufukara na ni kujenga idhlaali kwa nafsi zetu na kwa vizazi vyetu.
Tununue nyumba na viwanja kwa ujenzi wa makanisa
Inaonesha Waislamu wenye siasa kali na baadhi ya watendaji kwenye sirikali
wameanza kushtuka na ongezeko kubwa la makanisa katika kisiwa cha Unguja.
Kuna dalili kuwa tunaweza kupata ugumu katika kupata viwanja kwa ajili ya
makanisa. Njia tunayoweza kuitumia kwa muda huu ni kununuwa viwanja vitupu
au nyumba za Waislamu kwa bei kubwa itayowashawishi kuviuza na baadae
tutaweza kuvijenga au kugeuza nyumba hizo kuwa makanisa. Tuone jinsi
wanavyopanga kila njia ovu za kutufisidi na kujaribu kuifisidi Dini yetu. Hivi wao
kubainisha uovu na mbinu zao, ni fursa kwetu sisi kuchukuwa kila hadhari kujikinga na
uovu wao huu. Neno “Waislamu wenye siasa kali” tushalizowea, kila Muislamu mwenye
kutekeleza wajibu wa Dini yake, ndio hupangwa kila jina la uovu. Kwao wao sote sisi tuwe
“Waislamu kanzu” hio ndio haja yao, hapo tena ndipo watupe jina walipendalo, “eti
waislamu”. Madhali hawawezi kutubatiza, na Inshaallah hawataweza, laa sisi wala vizazi
vyetu, basi tuwe “Waislamu kanzu” itatosha kwao; Inshaallah hatutakuwa hivyo.
Alhamdulillahi, hao wanaowaleta hapa Zanzibar kialsiku wanazidi kurejea kwenye Dini yao,
yaani Uislamu; yaani wanasilimu. Haqi lazima idhihiri, haqi haikubali kukaliwa juu, lazima
ikae juu.
Tujenga shule na hospitali kwa wingi
Hizi ni taasisi pekee ambazo tunaweza kuzitumia kueneza neno la Bwana kwa
Waislamu walio wengi hapa Zanzibar. Kwa kutumia umasikini unaowakabili
wengi ya Wazanzibari na uchache wa huduma hizo tunaweza kujitangaza vizuri,
tujitahidi kutoa huduma nzuri kuweka vifaa vya kisasa kuweka bei ndogo kuweka
upendo ili vituo vya Waislamu au hata vile vya serikali visiweze kuvikaribia vyetu.
Shule ni sehemu muhimu ya kupandikiza mafundisho yetu, zaidi kwa watoto
wadogo (Nursery). Mbinu za kutumia huduma hizi kwa uenezaji wa wenyekuitwa
ukiristo ni za kale, na Inshaallah kama wanavyosema wao wenyewe, Waislamu
Alhamdulillahi ndio wengi hapa Zanzibar, itaendelea hivihivi na miongoni mwao Inshaallah
watazidi kupata uwongozi na warejee kwenye Dini yao ya asli - Uislamu, wote wanazaliwa
Waislamu, ni wao ndio huwabatiza na kuwatia kwenye Ukiristo. Suala la wao kutumia
“umasikini unaowakabili wengi ya Wazanzibari na uchache wa huduma hizo”,
kama tulivyotangulia kufahamishana, huu umasikini wametutia wao watawala wetu,
Dodoma; ili waweza kutuendesha wanavyotaka, tangu kisiasa, kidini na katika nyanja
nyenginezo. Umasikini huu umekuja kwa kuivamia Nchi yetu na kuimeza kwa kisingizio cha
huu wenyekuitwa muungano. Kutokana na hali hii ndio hii leo Wazanzibari wakawa
kwa hali yoyote ile wanawania kurejea Dola yao ya Zanzibar na itokane na huu
ukoloni wa Tanganyika, ukoloni wa Kanisa; leo kabla ya kesho. Suala la kuzitumia
hizi skuli za chekechea kwa kupotosha imani ya wenetu, hili ni jambo la khatari sana na ni
wajibu wetu kuchukua kila hadhari. Kubwa la kufanya sisi ni kutowapeleka wanetu kwenye
hizi skuli zao za chekechea, hizo ni vidonge vya sumu vilivyozongereshwa sukari. Tuviepuke
kama tunavyoweza, tuviepuke kwa kujenga skuli zetu za chekechea na kuwapeleka wenetu
humo.
Tunadai muda zaidi katika Vyombo vya habari (Tv na Redio)
Kwa muda mrefu sasa uislamu na waislamu wamehodhi vombo hivi vya habari
mbali na kuwa siku ya ijumaa ambayo yote humilikiwa na vipindi vya kiislamu
vyombo hivyo hutenga siku nyengine kadhaa kwa vipindi vya kiislamu na hata
kuthubutu kutia adhana kila wakati wa sala hali hii inaudhi na inatoa picha ya
wazi ya serikali kupendelea uislam ingawaje inadai kuwa haina dini. Wakati wa
kusherehekea miaka 25 ya TVZ tulizungumzia suala hili lakini inaonekana
halikupata mtu wa kulifanyia kazi. Sasa tuhakikishe kuwa ukristo unapata muda
zaidi katika vyombo hivyo au uislam nao upunguziwe nafasi. Kuzidi chuki zao,
dharau na ihana; wanasahau kuwa Zanzibar ni nchi ya Waislamu, kwa hivyo kutumia
vyombo vyao, khasa idhaa kwa kutumikia Dini yao ni waajibu juu yao. Kuudhika kwao kwa
kutiwa adhana katika idhaa yetu, halina msingi; bali tu ni dalili ya chuki zao juu ya Uislamu,
khaasa na juu ya Wazanzibari kwa jumla. Tizama jinsi ya chuki na uovu wao, “wao
wapate muda zaidi na Waislamu wapunguziwe”, hii ndio sera ya hasidi, weye ukose,
yeye apate. Lakini kwa mipango ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala, hasidi daima
haendelei, hasidi yake ni khasara na idhlaali.
Tuongeze mihadhara ya wazi
Wakati Waislam wamezuiliwa kufanya mihadhara ya wazi, sisi tujitahidi
kuhakikisha kuwa mihadhara yetu inaongezeka kwa kiwango kikubwa. Kwa
kuwa Waislamu hawahudhurii mihadhara hiyo, lazima tuone wakristo wa Mjini na
Mashamba wanahamasishwa na kupatiwa nyenzo ili kuhudhuria. Vipaza sauti
vitumike kuhakikisha kuwa neno la bwana linafika kila pahala. Mihadhara ifanyike
karibu na nyumba, misikiti na kwenye viwanja vya wazi. Ndio hayo! Hii ndio sera yao,
Waislamu wazuiliwe, wao wapewe na waongezewe.
Tuendelee kutumia shule na sehemu za Umma
Ili kuwafanya waislamu watuzoee na kuondosha chuki yao kwetu ni lazima
kuendelea kutumia mashule na sehemu za Umma zilizo wazi kwa mambo yetu ya
ibada kwa kipindi kirefu hali hii inaweza kuwafanya washindwe kuona tafauti kati
yetu na wao. Kila ukiusoma waraka wao huu ndivyo unavyozidi kutambua kuwa hawa
“wenyekujiita wakiristo”, sio Wakiristo wa kweli; Ukiristo wa kweli haunadi uadui na
Uislamu. Hii leo, Bwana Pope; mara nyingi amesikika kusema juu ya kuondoa mvutano
baina ya dini, bali baina ya mataifa. Kama wao hawa ni waumini wa kweli wa Ukiristo
wengelifuata mwenendo wa Bwana Pope. Lakini kamaitavyokuwa, sisi ni waajibu wetu
kuchukuwa kila hadhari kujilinda na mbinu za mabwana hawa wenye fikra na mipango ya
kujenga chuki na khasama baina ya waumini wa dini tafauti. Hadhari ni waajibu, hivyo
ndivyo alivyotuamrisha Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala katika hii Aya
tuliotangulia kuitaja humu. Kwa hivi kuwa nia na dhamiri yao mabwana hawa si njema juu
ya Uislamu, Wazanzibari; ndio inatufanya na sisi kulazimika zaidi kujihami dhidi ya mbinu
zao ovu kwa uwezo wetu. Hivi kujihami kwetu dhidi ya mbinu zao ovu ndiko wanakosingizia
kuwa ni “chuki”. Tunawahakikishia kuwa sisi Waislamu, Wazanzibari; hatuna chuki na
Ukiristo hata kidogo, lakini tuna waajibu wa kufuata maamrisho ya Mola wetu Mlezi,
Subhaanahu wa Taáala na Sunna za Mtume wetu Mpenzi s.a.w. Miongoni mwa maamrisho
hayo ni kuihami na kuihifadhi Dini yetu tukufu kwa kila hali. Hapa tena ni waajibu
kuzinduana na ndugu zetu walioko kwenye madaraka juu ya mbinu hizi na kuwaomba
kuchukuwa hadhari katika utumizi wa hizi sehemu walizozitaja hawa mabwana kupanga
kuzitumia ili kuepusha athari ya sisi kusaidia katika utekelezaji wa njama zao ovu dhidi ya
Uislamu, Wazanzibari. Tusisahau kuwa mwenye kusaidia katika la kheri, nae hupata sehemu
ya kheri hio; na mwenye kusaidia katika shari nae hupata sehemu ya shari hio. Yote hayo
tutayakuta kwenye vitabu vyetu hio Kesho, na hii leo, hapahapa ulimwenguni tutapata
malipo yetu, qabla ya hio Kesho..
Tufanye suala la uhamiaji Zanzibar kuwa jepesi
Uzoefu unaonesha kuwa ni jambo gumu kuwabatiza Wazanzibari waislamu. Hali
hii inafanya ongezeko la wakristo kuwa dogo au halipo kabisa ukitoa wale
wanaozaliwa katika familia za kikristo. Alhamdulillahi, kweli wanaitambua; lakini
wamo wanagombana nayo. Inshaallah daima dawamu, Waislamu, Wazanzibari hawata
nasarishwa, daima wataendelea katika Dini yao tukufu. Inshaallah na uwongofu utawafikia
na wao warejee kwenye Dini yao ya kuzaliwa. Binaadamu huzaliwa ni Muislamu, ni wazee
wake ndio wenye kumtoa katika Uislamu na kumtia kwenye upotoful.
Njia pekee ya kuhakikisha ongezeko la makanisa na Taasisi zetu ni kuongezeka kwa
wakristo. Jambo hili litawezekana kwa kuingiza Wakristo wengi kutoka Tanzania
Bara au wapagani ambao tutaweza kuwabatiza kwa kutumia udugu wetu wa
kikabila au asili ya Bara. Tunaposoma maelezo yao haya tunafahamu bila taabu kwamba
haja yao ni kuongezeka makanisa na taasisi zao. Kuongezeka Wakiristo sio haja
yao khasa, kuongezeka Wakiristo kwao wao ni ngazi tu ya kufikia haja yao khasa,
yaani kuongezeka makanisa na taasisi zao. Hii hakika wanaoshindwa kuificha, vitendo
na mwenendo wao pia unathibitisha hakika hii. Huu ujenzi wa makanisa na taasisi nyengine
ni mtaji wa kujipatia chumo binafsi hao viongozi wa hizi harakati za hawa “wenyekujiita
wakiristo” kutoka wafadhili wao huko Ulaya na kwengineko. Na kwa kuwa makanisa haya
lazima waonekane wenye kuyatumia, ndivyo hivi kupanga hata kuleta na kuhamisha watu
kutoka huku na huku. Ni vyema wawalete, Inshaallah itakuwa ndio njia ya wao
kurejea kwenye Dini yao ya asili; Uislamu; kheri hutoka kwenye tumbo la shari.
Kwa kuwatumia ndugu zetu waliomo serikalini (SMZ au SMT) tuhakikishe kuwa
suala la uhamiaji linabakia wazi na rahisi na linaendelea kwa kila hali. Lugaha nzuri
na ndivyo khasa, yaani “kwa kuwatumia”. Hawa mabwana “wenyekujiita wakiristo”,
mipango yao ni mbinu za uovu, kwahivyobasi; ili kutekeleza mbinu zao hizo, ndio wakawa
wanapanga “kuwatumilia” hao wanaowaita “ndugu zao” waliomo sirikalini dhidi ya
Waislamu, Wazanzibari - “adui zao namba moja”. Tena, tunawaomba ndugu zetu,
Wazanzibari, khasa waliomo kwenye madaraka, tuzidi kuchukuwa hadhari na kujikinga na
mbinu zao hizi. Suala la uhamiaji na uingiaji nchini bila ya vitambulisho, kilasiku tunaona
maafa yake, tangu ujambazi na mengi mengineo. Na zaidi ni hili la kuwa ni mbinu ya
kupangwa khasa kwa kuongezeka makanisa nchini mwetu.
Tuzuie jaribio lolote la kadi za uraia au vitambulisho
Wakristo tunapaswa kuelewa kuwa iwapo serikali ya Zanzibar itaamua kufanya cho
chote ili kuwa na vitambulisho au kadi za uraia kwa wazanzibari pekee basi jambo
hilo litaathiri sana mipango yetu ya muda mrefu kwa Zanzibar. “Mipango yao ya
muda mrefu itaathirika”, hii ndio qauli yao. Iwapo sirikali ya Zanzibar italeta
vitambulisho vya Wazanzibari, basi mipango yao ya muda mrefu hawa mabwana
wenyekujiita wakiristo itaathirika. Hii ni ilani ya wazi kabisa kwamba kuondolewa
vitambulisho vya Wazanzibari na kuletwa vya Watanzania, wenye kunufaika khasa ni hawa
mabwana wenyekujiita wakiristo. Ikiwa Wazanzibari fikra zetu ni kwamba hivi vitambulisho
ni kwa maslaha ya chama cha kisiasa dhidi ya chama cha kisiasa, basi ndivyo hivi
tunavyoelezwa wazi kabisa kwamba vitambulisho ni mpango wa Wakiristo dhidi ya
Waislamu, Wazanzibari. Kwahivyobasi, vitu viwili ni muhimu kwa Kanisa, (1)
Uhamiaji, (2) Vitambulisho. Vitu viwili hivi ni dharura vibakie katika maslaha yao wao
hawa wenyekujiita wakiristo, ili waendeleze vita vyao dhidi ya Waislamu, Wazanzibari.
Tena, tunawaomba ndugu zetu waliomo kwenye madaraka wayazingatie haya kwa
hikma na busara na kutambuwa dhamana zao na kuhisabika kwao katika
dhamana zao, mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala na
mbele ya Umma wa Kizanzibari.
Jitihada zozote za kuiimarisha Zanzibar kama Zanzibar na nje ya Utanzania ni
lazima tuelewe kuwa Uislamu utapata nguvu na kuwa tishio kwa hapa Zanzibar
na hata Bara. Kutokana na imani na siasa yao hii, ndipo pale Januari 11, 1964 makanisa
wakimtumia Nyerere akaleta majeshi yake na kuivamia Dola Huru ya Zanzibar. Dola
ambayo ilipata uhuru wake taarikh 10 Disemba, 1963; na kujiunga na Umoja wa Mataifa
taarikh 16 Disemba hiohio 1963. Baada ya siku thalathini na tatu tu, yaani hio Januari 11,
1964 ndipo makanisa kwa kumtumia Nyerere wakaivamia Zanzibar. Mavamizi haya lengo
lake kuu ni kuimeza kikamilifu Dola Huru ya Zanzibar, ndipo hapo siku ile ya April 26, 1964
ilipomezwa Zanzibar kwa kisingizio cha huu wenyekuitwa muungano kwa kubuniwa zile
“Articles of Union, 1964” na hapo tena ndipo ilipofanywa “Zanzibar si Nchi”.
Iwapo tutawajibika kuunga mkono ni kadi za Uraia na vitambulisho vya
Watanzania kwa Ujumla na sio Zanzibar peke yake. “Zanzibar si Nchi” ndivyo
alivyotwambia Mhishimiwa Waziri Mkuu wa Tanganyika, Bwana Pinda; kwahivyobasi,
madhali hatuna nchi na bado Zanzibar ni koloni la Tanganyika, vitambulisho, kadi ya uraia,
na hio passpoti, vyote hivi tutaazimwa na bwana mtawala Tanganyika. Kabla ya Zanzibar
kupata uhuru wake siku ile ya Diemba 10, 1963, Wazanzibari wakipewa passpoti za
“Zanzibar Protectorate” yaani “Himaya ya Zanzibar”. Wakati huo juu ya kutawaliwa na
Muingereza lakini tulibakia kuwa Dola, lakinibasi; bwana mkoloni Tanganyika yeye
ameimeza nchi yetu na kuitia chini ya ukoloni wake, kisha akatwambia “Zanzibar si Nchi”;
mkoloni Muingereza hakufika kuimeza nchi yetu na kufika kutwambia kuwa “Zanzibar si
Nchi”. Hapa ndipo inaposemwa “kheri ya ukoloni mweupe kuliko ukoloni mweusi”.
Naam! Halina shaka hili! Hivi ndivyo walivyosema wanafunzi wa Chuo Kikuu cha
Dar-es-Salaam, mnamo miaka ya sitini; mara tu baada ya Tanganyika kupata
uhuru. Qauli hii ilimchoma na kumuudhi sana Mwalimu Nyerere, hivyo akaamrisha
kufungwa Chuo hiki kwa muda. Kweli ni chungu!
Tujipenyeze Vyamani na kushika nafasi muhimu
Lazima tuelewe kuwa chama cho chote cha siasa kinalenga kukamata serikali ili
kiweze kutekeleza yale yanayoaminika kuwa ni mazuri kwa chama hicho.
Tunapozungumzia vyama vya siasa kwa Zanzibar tunahusisha zaidi kwenye CCM
na CUF. Watu wetu wamefaulu kuingia kwa wingi katika chama tawala na katika
jumuia zake. Ikiwa inavyosemwa ni hakika, kwamba “CCM”, maana yake khasa ni
“Catholic Christian Movement” au “Chama Cha Msalaba”; basi si ajabu hata kidogo kuwa
“watu wetu wamefaulu kuingia kwa wingi katika chama tawala (CCM) na katika
jumuia zake”. Hali kuwa hivyo si ajabu, ingalikuwa ajabu lau kama hali haingalikuwa
hivyo. Baada ya maneno yaliowazi kabisa kama haya, sawa na pale tulipoambiwa kuwa
“Zanzibar si Nchi”, ni kweli sisi Wazanzibari tuendelee kudhania kwamba CCM ni chama
cha Wazanzibari? Ni kweli baada ya chama hikihiki CCM kutueleza dhaahiri shaahiri,
kwamba “Zanzibar si Nchi”, bado sisi tuendelee kudhania kwamba CCM ni chama cha
Wazanzibari? Tutakuwa tunajidhulumu nafsi zetu kwa kuzidanganya.
Tupenyeze wenzetu serikalini
Sambamba na suala tulilolielekeza juu hatuna budi kusomesha vijana wetu na
kuhakikisha kuwa tunatumia kila njia na ushawishi ili kuwaingiza serikalini na hasa
katika sehemu muhimu. Hii itarahisisha kuungwa mkono mipango yetu na
kupunguzwa vikwazo kwa mikakati yetu. Hapana shaka hii ni mbinu yenye kutekeleza
makusudio bila ya wasiwasi. Hali hii ndivyo ilivyo hivi sasa hapa kwetu, nyingi ya nafasi
muhimu za juu zimo mikononi mwa mabwana watawala, Tanganyika, Kanisa. Waswahili
wa Tanganyika na Waswahili wa Zanzibar, bali na Waswahili wa Kenya na
Waswahili wa Uganda sote tumetiwa kikaango kimoja tunakaangwa kwa matufa
yetu wenyewe. Kwa mabwana hawa wenyekujiita wakiristo, kosa letu sisi Waswahili,
Waislamu ni Uislamu wetu. Hivyo ndivyo ikavamiwa Uganda kuwaondosha watawala wa
jadi, kina Kabaka na machifu wao, na kuvamiwa kuondoshwa Sirikali ya utawala wa kina Idi
Amin; yote hayo ni vita dhidi ya Uislamu, Waswahili.
Tuunge mkono sera za utalii
Hadi sasa wengi wa watalii wanaoingia Zanzibar hutokea nchi za Kikristo. Desturi
za watalii hupingana na zile za Kizanzibari na hata za Kiislamu. Watalii
wanasaidia kuongezeka kwa mabaa na vivazi ambavyo waislamu wanataka
visivaliwe hasa na wanawake. Waingereza wanasema, “when the drink is in, the
truth comes out”; maana ya maneno haya ni kama hivi, “ulevi ukijaa (kichwani),
ukweli hutoka nje”. Ulevi wa hawa mabwana wenyekujiita wakiristo, si pombe, bali ni
haya wenyekuyaita “mafanikio yao”. Haya mafanikio yao yamewalevya na kufika hadi hivi
wao kubwabwaja vile wanavyopenda bila ya wasiwasi wowote ule. Tena Waingereza
wanasema, “power corrupts, obsulute power corrupts obusulutely”, maana ya maneno
haya ni kama hivi, “nguvu za madaraka zinafisidi, na nguvu za madaraka yasio na
kizuizi, hufisidi bila ya kizuizi”. Hawa mabwana wenyekujiita wakiristo, baada ya
kupewa madaraka, kuvamiwa nchi yetu na kutiwa chini ya ukoloni wao; wamelewa kwa
utamu wa madaraka, hivyo ndio hivi wao kuzama katika kuleta kila upotofu na ufisadi;
kinyume kabisa na “Ukiristo wa kweli”. Kwa kitendo chao hiki, badala ya kuutendea vyema
Ukiristo; wamekuwa wanautia aibu na fedheha Ukiristo wa kweli, Ukiristo ambao unaamini
juu ya kuishi kwa salama, amani na mapenzi na waumini wote.
Tujenge mabaa na kuongeza pombe
Waislamu wengi huchukia pombe na huweza kuhama iwapo duka la pombe au baa
ipo karibu nao. Waislamu hatari ni wale wanaosoma na kupata muda wa
kujishughulisha na dini yao. Pombe ni kitu ambacho humtoa Muislamu katika
Uislamu wa vitendo na kumkaribisha na Ukristo. Jee, haya ndio maamrisho ya Ukiristo,
yaani kupanga kufisidi waumini wengine? Mzee Pope haidhaniwi hata kidogo kama
atakubaliana na mbinu fisadi kama hizi? Ukiristo wa kweli ni ule wenye kujenga mapenzi
baina ya waumini. Pombe sio humtoa Muislamu katika Uislamu wa vitendo, bali pia humtoa
Mkiristo katika Ukiristo wa kweli, bali humtoa hata mpagani katika utu wake. Kutokana na
uovu huu ndivyo pale pombe kukatazwa na kila imani. Jee, ni kweli kwamba pombe
humkaribisha mtu na Ukiristo? Haya mapya kabisa! Inavyojuulikana ni kwamba pombe, na
kila ulevi, bali maasi humtoa mtu katika ubinaadamu wake na kumtia katika siubinaadamu.
Pombe haingaliitwa mama wa maasi lau kama si yenye kupelekea kwenye kila maasi. Jee,
Ukiristo wa kweli ndivyo unavyoamrisha kwamba binaadamu ajitie katika kila aina ya maasi,
au katika maasi? Hatudhani kuwa ni hivyo.
Tuwafuate Wakristo waliosilimu ili warudie Ukristo
Watu wa aina hii wanakuwa bado hawajatulia na mara nyingi huwemo katika
matatizo.. Pana haja ya kuwalenga watu hawa ili kuwarudisha kabla hawajatulia au
kupata elimu nzuri. Matatizo yao ndipo mahala pa kuanzia ili Bwana awateremshie
roho ya utulivu. Uzima wa Ukristo ni kuwa na wafuasi wengi kadiri
iwezekanavyo. Jee, ndugu zetu, mnaamini kwamba hawa si Wakiristo wa kweli? Hawa
basi ni wenyekujiita wakiristo, sio Wakiristo. Hivyo ni kweli kwamba Ukiristo wa kweli ni
kumpangia binaadamu hilaki na kufisidika tu? “Wawarudishe kabla hawajatulia na
kupata elimu nzuri”. Ikiwa mbinu hizi si ufisadi tuziite nini? Ni ufisadi wa hali ya juu
kabisa. “Uzima wa Ukristo ni kuwa na wafuasi wengi kadiri iwezekanavyoo”, “uzima wa
jengo” haupimwi kwa ukubwa wake, bali hujuulikana kwa misingi yake, nguzo zake,
matumizi yake na watumizi wake.
Tuwafuate wanawake kwa misaada
Jumuiya zisizo za kiserikali zinaungwamkono duniani kote na hasa zile za
wanawake na watoto tujiweke pamoja ili tuweze kuwavutia wanawake kwa jina la
kuwasaidia. Enyi mabwana wenyekujiita wakiristo, hivyo kweli hamna hata mara moja nia
ya matengenezo kwa ajii ya Ukiristo, licha ya ubinaadamu; bali basi kwa kufisidi na
kujionesha? “….. kuwavutia wanawake kwa jina la kuwasaidia”.
.)126 : " ....... و ما يمكرون إال بأنفسهم و ما يشعرون ". (الألنعام
“….. Na wala hawafanyii vitimbi isipo kuwa nafsi zao, nao hawatambui”.
(Al Anaám : 123).
Vitimbi vyenu viovu, haviwaleteeni lolote isipokuwa kufisidi nafsi zenu. Waswahili
wanasema, “mchimba kisima huingia mwenyewe”, na “muomba chumvi huombea
chunguche”; na, “upandacho ndicho uvunacho”. Ajabu ya mabwana hawa na hao wakuu
wao, karne na karne sasa wamo katika vitimbi vya ufisadi wao; karne zote hizi hawana lolote
walilolipata, lakini bado hawajatanabahi, bado wamo kwenye upotofu wao. Lakini hayo si
ajabu hata kidogo, hivyo ndivyo alivyoahidi Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala
kwamba madhaalimu hawatopata uwongofu.
.)85 : “.......... إن اهلل ال يهدى القوم الظالمين“ . (القصص
“…….Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu”.
(Al-Qas’as’ : 50).
Kwa vile hawa mabwana ni madhaalimu, basi kwanza dhulma yao huwafikia nafsi zao, yaani
wao ni wenye kudhulumu nafsi zao kabla ya zile wanazopanga kudhulumu na kufisidi.
Muhimu la sisi kutanabahi hapa ni kwamba ikiwa hawa hawana uwongofu, vipi itakuwa
watowe uwongofu. Ni kanuni yenye kutambulika na kukubalika, hata kiakili tu, kwamba; “
asiekuwa na kitu hatoi kitu”. Hili liko dhaahiri kabisa, hao wenye kughurika na
kuwafuata wao, ukiwatazama utagunduwa kuwa hawana lolote la uongofu katika maisha yao
ya hapa duniani, licha ya kesho Akher, na hivyo ndio wengi wao hawakawii kutambua na
kurejea kwenye Uislamu – Alhamdulillahi.
Tuongeze vituo vya mafunzo ya kikristo
Kituo cha vijana cha mji mkongwe (Stone Town Youth Centre) kimekuwa
kikifanya kazi yake vizuri kwani hadi sasa lengo lake la ndani bali (bado)
halijaeleweka na vijana wanaohudhuria hapo kwa shughuli mbali mbali, jitihada
zifanyike ili kuwa na vituo vya aina hii katika maeneo mengine. Lengo kuu liwe ni
vijana na wanawake bila ya kuonesha dalili za kidini. Mola wetu Mlezi, Subhaanahu
wa Taáala anatupenda sana waja wake, mapenzi ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa
Taáala ni kuliko ya mama kwa mwanawe. Uovu ni wetu sisi jinsi tunavyokuwa hatuthamini
hata kidogo haya mapenzi ya Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala juu yetu. Miongoni
mwa mapenzi hayo, ni hivi daima kutubainishia na kutufichulia vitimbi viovu vya hawa
mabwana wenyekujiita wakiristo. Tunaona jinsi vinavyobainika vitimbi vyao viovu. Kama
tulivyotangulia kusema, sumu yao daima huizongeresha kwa vidonge vya sukari. Ndugu
zetu wenye kutumia vituo vyao hivi, khasa hicho cha (Stone Town Youth Centre), hii ndio
qauli yao. Tunaendelea kuwaomba ndugu zetu waliomo kwenye madaraka watuvue na wavue
nafsi zao na uovu huu, khasa kwa vile wao ndio wenye uwezo huo kikanuni. Inshaallah
wapate tawfiiq wafanye hivyo, Aamyn.
Tuwaowe wanawake wao kwa kusilimu kimajina
Jitihada za makusudi zifanyike ili kila itakapowezekana kuwaoa wanawake wa
Kiislamu ili tuweze kuwabatiza baadae, njia nzuri iwapo patakuwa na ugumu ni
kusilimu kiuongo ili kuruhusiwa kuwaoa wanawake wao. Wao hawa mabwana
wanasema, ”watuowe ili watubatize”. Alhamdulillahi hivi kutambuwa na kubaini
kwamba hawana la “nguvu za hoja” kuwatia watu katika huu upotofu wao, hivyo ndio
wanamalizikia kwa “hoja za nguvu” na “hoja za udanganyifu”. Yote haya si mapya, tangu
siku za Mitume a.s.w. wao hushindwa na “nguvu za hoja”, na ndipo walipokuwa
wakimalizikia kwa kutumia “hoja za nguvu”. Kwa kutumia “hoja za nguvu”, ndipo wakawa
katika mbinu za kutaka kuwauwa Mitume a..s.w. waliopelekewa na kuwatesa Waislamu.
Hali zao, uovu wao, vitimbi vyao, tangu karne na karne ndio vilevile, hapana kilichobadilika.
Wanaendelea kuishi katika giza la upotofu kwa kuukataa mwangaza wa uwongofu.
Wataendelea hivihivi mpaka wataposema yaalaiti ningelikuwa udongo:
م ن
.. ) 85 : ) ّ "....... ياليتنى كنت ترابا ". ( الّباْ (ع
“…… Laiti ningeli kuwa udongo”. (Annbaaa : 50).
Tunamuomba Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala atunusuru kuwa miongoni mwa
qaumu hio, Aamyn.
Tuanzishe NGOS na sisi tuwe viongozi
Kwa hivi sasa wafadhili wengi wameonesha hamu ya kuzisaidia ngos moja kwa
moja badala ya serikali ni lazima tujitahidi kuunda jumuiya zetu ambazo
zitawashirikisha waislam lakini uongozi wa juu ni lazima uwe mikononi mwetu.
Hii itatuwezesha kuona sera zetu na malengo yetu yanatekelezwa kwa kivuli hicho.
Vitimbi vyao Inshaallah vitawarejea wenyewe. Hapana shaka hawa wenye kuleta hizi
waziitazo “Non Governmental Organizations”(NGOs) ni hawahawa mabwana wasiotutakia
kheri Waislamu, Wazanzibari. Ni tangu karne na karne, wakoloni washirika wake wakuu ni
hao mishinari. Msiba mkubwa ni hivi sisi kuwafanya mabwana hawa ndio wenzutu, kitendo
ambacho Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala ametukataza na kutuhadharisha uovu wa
mabwana hawa, lakini wapi; sisi ndio kilasiku tunazidi kuwakumbatia na kuwafanya ndio
wenzetu, bali hata kuwafanya ni wasiri wetu. Ole wetu!! Tumo tunajitia katika hilaki
kwa mikono yetu wenyewe, Ole wetu!! Yaa Rabbi tunusuru.
Tujenge ukaribu na viongozi ili kuwadhibiti waislam
Mambo yetu mengi yamekuwa yanakwenda vizuri katika maeneo mbali mbali
baada ya wenzetu kuwemo katika kamati za masheha na matawi ya vyama na
kamati za maendeleo za maeneo mbalimbali. Hali hii ni lazima iongezeke ili
udhibiti wa shughuli za waislam uwe mzuri zaidi na wakati huo huo kuona kuwa
mambo yetu yanakwenda yakiwa na baraka ya vyombo vya dola na vyama vya
siasa. “Tujenge ukaribu na viongozi ili kuwadhibiti waislam”. Daima dhamiri zao
sio njema, yote walioeleza humu katika hizo mbinu zao yamo katika njia za uvunjaji na
ufisadi, sio ujengaji na utengenezaji. Hawapangi lolote la maendeleo yao, na wanapopanga,
basi wanapanga kwa hisabu ya kufisidi binaadamu. Wanasema “wajenge ukaribu na
viongozi”, viongozi wanaokusudia hapa ni ndugu zetu, Waislamu, Wazanzibari waliomo
kwenye madaraka. Wajenge ukaribu huo kwa nia ya kuwafisidi Waislamu, Wazanzibari; sio
kwa nia ya kuutengenezea Ukiristo. Ndugu zetu mliomo kwenye madaraka, hivi ndivyo
vitimbi vyao hao mabwana wenyekujiita wakiristo, kilasiku uovu wao unazidi kudhihiri. Ni
juu yetu tuzidi hadhari na tuzidi kupanga ili tuweze kufanikiwa na kujihami dhidi ya ufisadi
wa kila fisadi.
Tuwachonganishe mashehe wenye msimamo mkali
Mashehe wenye msimamo mkali wamekuwa ni tatizo kwa ukristo kwani wana
wafuwasi wengi na wamekuwa wakisema wazi na kushutumu maendeleo yetu.
Mashehe hao ni lazima wachonganishwe na serikali ili hali ikiruhusu wazuiliwe
kuendesha shughuli zao. Wakati tukifanya hivyo hatuna budi kuwaunga mkono
mashehe wote ambo wamekuwa wakitusaidia kwa njia mbali mbali. Huu ndio
mwenendo wao, si ajabu hata kidogo. Fitna ndio mtaji na turufu yao, uwongo ndio nyenzo ya
fitna zao. Kama wanavyosema, wakati wakiwemo katika fitna zao; wakati huohuo wafanye
waweze kuwanunua wale wanaokuwa tayari “kuuza Akhera yao kwa dunia yao”,
Akhera ya daima kwa dunia yenye kupita. Muhimu tuwakumbushe hawa mabwana
wenyekujiita “wakiristo”, kwamba fitna ni mbaya kuliko kuuwa:
.)212 : “........ و الفتنة أكبر من القتل .......”. ( البقرة
“………… Na fitina ni mbaya zaidi kuliko kuuwa………..”.
(Al Baqra : 217).
Na Mola wetu Mlezi Subhaanahu wa Taáala, ametwambia kwamba mwenye kuwafitinisha
Waumini kisha asitubie, basi malipo yake ni kudumu maisha milele katika moto ya
Wahannamu.
.”“ إ ّا اّذين فتنوا المؤمنين و المؤمنات ث ّ لم يتوبوا فلهم عذاب جه ّم و لهم عذاب الحريق
ن م ن ل
.)15 : (البروج
“Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha
hawakutubia, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya
kuungua”. (Al Buruuj :10).
Basi hawa mabwana wenyekujiita wakiristo, wajuwe na watambuwe kwamba hayo ndio
malipo ya wenye kutia fitna baina ya viumbe; makaazi yao ya milele ni katika Jahannamu.
Adhabu hii itawakuta vilevile wale wenye kushirikiana na kusaidiana nao katika kuwafitini
viumbe. Ajabu yao hawa mabwana wenyekujiita wakristo, kwani ni dhana yao kwamba
watawapata binaadamu wawafuate hali ya kuwa wamo katika upotofu kiwango hiki?
Ametwambia Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala:
“ من يشفع شفاعة حسنة يكن ّه نصيب ّنها، ومن يشفع شفاعة س ّئة يكن ّه كفل منها، وكان اهلل على ك ّ شىء
ل ل ي م ل
.)18:ّقيتا”. (النساء
م
“Atakayeombea maombezi mema (atakayesaidia maombezi mema hata yakatokea)
atapata sehemu katika hayo. Na atakayeombea maombezi mabaya atakuwa na
sehemu katika mabaya hayo, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye ujuzi wa kila kitu”.
(Annissai : 85).
Ikiwa Ukiristo ni dini ya mapenzi na maendeleo, tunawaasa watende mema kwa ajili ya dini
na waache njama na vitimbi dhidi ya binaadamu.
Tulenge kuifuta tabligh
Pamoja na kuwa tabligh sio hatari moja kwa moja kwa ukristo lakini bado inastahili
kupigwa vita kwa sababu ni aina pekee ya mihadhara ya waislamu inayoruhusiwa
humu Zanzibar. Tabligh inaweza kuwazindua baadhi ya waislam ambao ni vyema
kubaki bila ya kuzinduliwa. Haya ndio maneno yao, “tabligh haina khatari na ukiristo,
lakini juu ya hivyo inastahili kupigwa vita”. Kwa nini? Kwa sababu inaweza kuwazindua
Waislamu, na ni vyema kubaki bila ya kuzinduliwa. Ajabu ya mabwana hawa, sifahamu ni
maadili yepi wanayoyafuata; Uislamu unabainisha kwamba, “Hawi muumini wa kweli
mmoja wenu mpaka ampendelee nduguye lile analojipendelea nafsi yake”. Sasa hawa
mabwana wenyekujiita wakiristo, ikiwa wao hawawapendelei kheri binaadamu wenziwao,
vipi wanatarajia kupata mapenzi ya binaadamu wenziwao? Vipi wanatarajia wapate
mapenzi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Subhaanahu wa Taáala? Hivyo ni kweli haya ndio
mafunzo ya Ukiristo? Hapana shaka haya sio. La hakika zaidi ni kwamba hawa sio Wakiristo
wa kweli. Waswahili wanasema, “Chema chajiuza, kibaya chajitembeza”.
Tudai turudishiwe taasisi zetu
Serikali ya Zanzibar bado inaonekana kuwa ngumu kurudisha katika milki ya
makanisa ardhi na taasisi zetu. Dalili za huko nyuma zilionekana nzuri kwani
tulifanikiwa kupata hospitali yetu ya Welezo na eneo la kiungani hata hivyo
panakuwepo ugumu wa kurudishiwa shule zetu. Kwa kuwatumia wenzetu
waliomo serikalini na baraza la wawakilishi lazima tuzidishe harakati na madai ya
taasisi zote zilizobaki. Wao wanadai kurejeshewa taasisi zao, tunawakumbusha kwamba
Waislamu wameporwa Chuo chao Kikuu Cha Ufundi, (MIOME), wamenyangánywa jumuia
yao iliokuwa na manufaa makubwa, “East African Muslim Welfare Society” (EAMWS), si
kwa Waislamu tu; bali kwa Afrika Mashariki, bali kwa Afrika nzima. Isitoshe, Waislamu
daima dawamu wananyimwa fursa za masomo ya juu, wananyimwa fursa ya kazi za
dhamana, Jeshini, Polisi, Vikosi vya Usalama, Magereza, Ubalozini na mwingi
mwenginemo. Wananchi katika nchi yao ambao kwa hio hisabu yao wao mabwana wenye
khatamu za nchi, basi Waislamu Tanganyika hawapungui 65% na Zanzibar hawapungui
98%, hii leo baada ya mavamizi ya 1964 na kumezwa Dola Huru ya Zanzibar. Mzee
Kambona baada ya kuona maji yanazidi unga, yaani dhulma ya Nyerere juu ya Waislamu,
alimnasihi asiwabane sana Waislamu. Kambona haiwi kafanya hivyo isipokuwa zaidi ni kwa
manufaa ya hao wakiristo. Lakini wapi, Mwalimu hakuacha mbinyo wake juu ya Waumini
mpaka akafika mbele ya haqi.
Tulete waumini kutoka mashamba kuanza makanisa
Hivi sasa pameibuka wasi wasi kuhusiana na wingi wa makanisa ambayo
hayajapata waumini wa kuyajaza. Ili kuficha dosari hii na hoja kadhaa utaratibu
uliopo hivi sasa chini ya baadhi ya makanisa ni lazima uungwe mkono. Wakristo
wahamiaji wengi hufikia mashamba hivyo pawekwe na utaratibu wa kuwaleta mjini
ili kujaza makanisa. Almuradi mumo mbioni tu, leo wa shamba wapelekwe mjini, kesho wa
mjini wapelekwe shamba, leo wa bara wapelekwe visiwani, kesho wa visiwani wapelekwe
bara. Leo wa Machui wapelekeni Mahonda, kesho wa Mahonda wapelekeni Kama. Mabwana
wakubwa! Wengi wa hawa munaowasema “wakiristo”, ni wenye kutafuta riziki, dini kwao
ni hadithi tu, huko mashamba ndiko kwenye mbio zao za kujipatia riziki, riziki wajisaidie
nafsi zao na watu wao waioko huko mabara. Zanzibar wamekuja kutafuta riziki, kama
walivyokuwa wakifanya miaka na miaka, tafadhalini waacheni waishi kwa amani na
mafahamiano na wenyeji wao, wacheni kuwajengea fitna na bughdha na wanyeji wao kwa
maslaha yenu binafsi, wala si kwa huo ukiristo mnaojinasibu nao.
NENO LA MWISHO
Wapendwa katika Bwana.
Miongozo hii ni mikubwa na inaweza kuwatisha baadhi ya waumini wa kikristo
hasa wale ambao bado hawajampokea Roho Mtakatifu vizuri. Hata hivyo kwa
uwezo wa Bwana Mungu wetu ni mpango rahisi. Suala la muhimu ni haya
kufahamika na kila mkiristo apendae kumtumikia Bwana. Pia hatuna budi
kuishukuru awamu ya nne ya serikali ya mapinduzi ambao imefungua milango
kwa ukristo na kushuhudia ongezeko la makanisa.
Bwana awe nasi!
Nasi tunasema, “Enyi Wapendwa katika Bwana”, Enyi Wakiristo wa kweli, tafadhalini
inukeni muutakase Ukiristo na aibu kama hii unaopakwa. Aibu ya kunasibishwa na kila uovu
na njama dhidi ya binaadamu. Aibu ya kuitia Sirikali ya Zanzibar katika ushirika wa njama
hizi za uovu dhidi ya Waislamu, Wazanzibari.
Kukumbushana ni Waajibu kwa Waumini
Ametutaka Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala tukumbushane; kwani
kukumbushana kunawafaa Waumini, Inshaallah tuwe wenye kunufaika.
. 88 .”
“Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini”.
(Adhaariyaat : 55).
Kwa vile sisi ni Waumini ni wajibu wetu kukumbushana. Kwanza tunawaomba
ndugu zetu waliomo kwenye madarka na uongozi watumie wakati wao thamini
wausome huu waraka wa hawa jamaa wenyekujiita wakiristo. Wakishausoma, kwa
kituo; tunawaomba wazingatie vyema yaliomo kwenye waraka huu na wazingatie
wajibu wa dhamana yao, kuwa vile wao ndio viongozi wa huu Umma wa
Waislamu, Wazanzibari. Katika huko kuzingatia tunawaomba wazingatie yaliomo
kwenye Quráni Tukufu, khasa Aya tatu hizi. Tunawaombea viongozi wetu na
Sirikali yetu ya Zanzibar kwa jumla kila kheri na baraka na mafanikio katika
utumishi waliochukuwa dhamana ya kuutekeleza. Tunapenda kuzidi
kuwahakikishia kwamba Umma wa Zanzibar chini ya umoja wao, Umoja wa
Wazalendo, daima uko pamoja nao kwa kila hali kwa maslaha Nchi yetu na vizazi
vyetu.
ي ا
" يآأ ّها ّلذين آمنوا ال تتخذوا بطانة من دونكم اليألونكم خباال، ودوا ماعنتم، قد بدت البغضآء من أفواههم، وماتخفى
.)111 : صدورهم أكبر، قد بينا لكم الآليات ان كنتم تعقلون”. (آل عمران
Enyi mlioamini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha
kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao
katika midomo yao. Na yanayo fichwa na vifua vyao ni makubwa zaidi.
Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini”.
(Al-‘Imraan : 118).
“ يآأ ّها اّذين آمنوا قوا أنفسكم وأهليكم نارا وقودها الناس والحجارة عليها مالئكة غالظ شداد ال يعصون اهلل مآأمرهم
ي ل
.)6 : ويفعلون مايؤمرون”. (التحريم
" Enyi mlioamini! Jiokoeni nafsi zenu na watu wenu, na Moto ambao kuni zake ni
watu na mawe. Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu hawamuasi
Mwenyezi Mungu kwa amri zake; na wanatenda wanayo amrishwa (yote)”. (At-
tahriim : 6)..
“ من يشفع شفاعة حسنة يكن ّه نصيب ّنها، ومن يشفع شفاعة س ّئة يكن ّه كفل منها، وكان اهلل على ك ّ شىء
ل ل ي م ل
.)18:ّقيتا”. (النساء
م
“Atakayeombea maombezi mema (atakayesaidia maombezi mema hata yakatokea)
atapata sehemu katika hayo. Na atakayeombea maombezi mabaya atakuwa na
sehemu katika mabaya hayo, na Mwenyezi Mungu ni Mwenye ujuzi wa kila kitu”.
(Annissai : 85).
Tunamuomba Mola wetu Mlezi, Subhaanahu wa Taáala atujaalie kila kheri na
baraka na atuepushe na kila shari, na atuzidishie tawfiiq, uwezo na uwongozo
katika huu utumishi wa Dini yetu tukufu na wa’tani wetu ghali, Lillahi Taáala,
atuepushe na ria, atuepusehe na taájub, na atuepushe na kibri; Aamyn, Yaa Rabbi,
Aamyn.
Wa Billahi Tawfiiq
Umoja wa Wazalendo
Zanzibar
July 10, 2009